Monday, 20 January 2020
Sunday, 19 January 2020
WAKULIMA GEITA WAIOMBA KAMPUNI YA PETROBENA KUNUNUA TUMBAKU
Picha ya pamoja Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, Dk Titus Kamani akiwa na wajumbe wa mkutano wa MBCU pamoja na viongozi waandamizi wa kampuni ya uzambaziji pembejeo za kilimo ya Petrobena
Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, Dk Titus Kamani akizungumza na wanachama wa chama kikuu cha Ushirika Mbogwe na Bukombe (MBCU)
Baadhi ya wanachama wa chama kikuuu cha ushirika (MBCU) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, Dk Titus Kamani.
Mkuu wa wilaya ya Mbogwe Matha Julius Mkupas akiwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa MBCU
Na Salvatory Ntandu - Malunde 1 blog Mbogwe
Wakulima wa zao la Tumbaku katika wilaya za Mbogwe na Bukombe mkoani Geita wameiomba kampuni ya usambazaji wa Pembejeo za kilimo ya Petrobena kuanza ununuzi wa zao hilo kwenye AMCOS tatu ambazo zilikosa wanunuzi wa zao hilo baada ya kampuni ya Tanzania Leaf Tobacco Company Limited (TLTC) kusitsha ununuzi wa zao hilo katika msimu uliopita.
Ombi hilo limetolewa jana na Catherin Agostino mkulima wa Tumbaku kutoka Wilaya ya Bukombe katika Mkutano mkuu wa Chama kikuuu cha Ushirika Mbogwe na Bukombe (MBCU) kilichofanyika jana wilayani Mbogwe na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wa AMCOS 35 zilizopo katika Ushirika huo.
“Tangu Kampuni ya TLTC imesitisha ununuzi wa Tumbaku wakulima wengi wamekata tamaa ya kuendelea na kilimo hiki kutokana na kukosa mnunuzi tunaiomba kampuni ya Petrobena kukubali kununua mazao yetu ili tuweze kuendeleza familia zetu”,alisema Agostino.
Aliongeza kuwa kama wameweza kusambaza Pembejeo kwa wakulima wote hapa nchini kwa wakati na kuondoa urasimu uliokuwepo hapo awali wa kuchelewa kwa pembejeo na kusababisha wakulima kushindwa kulima kwa tija na kujikuta wameingia katika madeni makubwa ambayo hayawezi kulipika kwa haraka.
“Taarifa tulizonazo sisi wakulima wa Mbogwe na Bukombe ni kuwa kampuni ya PETROBENA msimu wa kilimo wa 2019/20 imefunga mkataba na AMCOS ya ngokolo iliyopo katika chama kikuu cha ushirika kahama (KACU) kwaajili ya kununua tumbaku hivyo tunaimbani ombi letu watalifanyia kazi”,alisema Agostino.
Akitolea Ufafanuzi suala hilo Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, Dk Titus Kamani alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano imehakikisha kero za wakulima zinapatiwa ufumbuzi ikiwemo suala la masoko ya mazao kwa kutafuta kampuni mbalimbali za ununuzi ambapo kwa mwaka huu vyama vyote vilivyokuwa vinalima tumbaku zimepata wanunuzi.
“Mbogwe na Bukombe mmepata wanunuzi katika zao la Tumbaku na Pamba changamoto iliyojitokeza mwaka huu ni kwamba baadhi ya taasisi za kifedha zimegoma kutoa mikopo kwa kampuni ya Grand Tobacco limite ambayo mmefunga nayo mkataba na AMCOS zetu sisi kama serikali tutalifanyika kazi na mtapata majibu kwa haraka”,alisema Dk Kamani.
Pia Dk. Kamani aliwataka pia viongozi wa vyama vikuu na AMCOS kuhakikisha wanatenga fedha kwaaajili ya kununulia pembejeo katika msimu ujao wa kilimo wa 2020/21 ili kuondokana na mikopo kutoka katika taasisi za kifedha ambayoimekuwa na riba kubwa isiyokuwa na tija kwa Wakulima.
Dk. Kamani aliwataka viongozi wa AMCOS zote zilizaopo katika mkoa wa Geita kuhakikisha wanajiunga na chama kikuu cha ushirika Mbogwe na Bukombe (MBCU) ili wawezekusaidiwa kwa ukaribu na serikali kupita viongozi wao pindi wanapopata matatizo sambamba na kupata huduma zingine ikiwepo mikopo ya pembejeo za kilimo.
KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA YATOA PONGEZI KWA BRELA

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Lugha Bashungwa (Mb) akizungumza jambo mara baada ya kutolewa Mafunzo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na BRELA.
Na Robertha Makinda -Dodoma
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imetoa elimu ya Majukumu yao kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira katika ukumbi wa Bunge leo tarehe 18/01/2020.
Mafunzo hayo yaliandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na BRELA. Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa kuhusiana na kazi na shughuli zinazofanywa na Wakala katika kutoa huduma kwa jamii bila kusahau changamoto mbalimbali zinazoikabili BRELA ili Kamati iweze kushauri.
Katika mawasilisho yaliyotolewa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Brela Bi. Roy Mhando alieleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na wakala ambazo ni kusimamia Sheria ya Makampuni Sura ya 212, sheria ya majina ya biashara sura ya 213, sheria ya alama za biashara na huduma, Sheria ya Usajili wa Hataza, Sheria ya Leseni za Viwanda, Sheria ya Leseni za Biashara. Ameileza Kamati kuwa Wakala inafanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha inatimiza majukumu yake kwa ufasaha na kuwafikia wateja wake kwa kutoa elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Kanali mstaafu Masoud Ally Khamis (Mb) amempongeza Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala kwa kazi nzuri anayoifanya na kuitaka Wakala kuendelea kutoa Elimu ili wadau wa biashara wajue huduma mbalimbali wanazotoa hasa katika maeneo ya pembezoni ambapo wadau wa biashara hawajui umuhimu wa kurasimisha biashara zao pia hawana uelewa wa matumizi ya Tehama.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Lugha Bashungwa (Mb) amewashukuru Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kwa maoni na mawazo yao waliyoyatoa ambayo kwa kiasi kikubwa yamekuwa ya kuongeza ufanisi kiutendaji katika kuwahudumia wananchi pia ametoa maelekezo kwa BRELA kuwa waweke mkakati wa mawasiliano wenye lengo la kutangaza huduma zinazotolewa na Wakala kupita vyombo mbalimbali vya habari hasa kupitia redio za kijamii.
Mbunge wa Sumve Mhe. Richard Ndasa ameipongeza BRELA katika suala zima la kuwahudumia wateja kwani wamewawezesha wananchi wengi kupata huduma kwa urahisi kwani hivyo ndivyo inavyotakiwa katika kufikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025.
Mbunge wa Ndanda Mhe. Cecil Mwambe amewashauri BRELA wawemakini kwenye kazi za kila siku ili kuondoa malalamiko na changamoto wanazopata wateja hii itasaidia kuongeza idadi ya wateja na pato la Taifa kwa ujumla.
Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Hawa Mwaifunga ameiomba BRELA wafike katika wilaya na Mikoa mbalimbali hapa nchi kwani huko kuna wadau wengi wanaohitaji kujua faida za kurasimisha biashara zao.
Mbunge wa Monduli Julius Kalanga Laizer ameipongeza BRELA kwa kuandaa mfumo wao ambao wanaendelea kuuhuisha na akapendekeza ni vema taasisi zingine za biashara kuunganishwa pamoja.Pia, amewapongeza watumishi wa BRELA kupitia kitengo cha TEHAMA wanaotoa msaada kwa wateja katika matumizi ya mtandao wa BRELA kwani wamekuwa wakisaidia sana wananchi pale wanapopata changamoto.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Kanali mstaafu Masoud Ally Khamis (Mb) alihitimisha kikao kwa kuwashukuru wajumbe wa kamati hiyo na kuwahimiza kuendelea kuishauri vema Serikali ili kuweza kufikia adhima ya Uchumi wa Kati unaongozwa na Viwanda ifikapo 2025.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Lugha Bashungwa (Mb) akizungumza jambo mara baada ya kutolewa Mafunzo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na BRELA. Lengo la mafunzo hayo ikiwa ni kuwajengea uelewa kuhusiana na kazi na shughuli zinazofanywa na Wakala katika kutoa huduma kwa jamii bila kusahau changamoto mbalimbali zinazoikabili BRELA ili Kamati iweze kushauri.Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Bunge Januari 18 ,2020.

Mbunge wa Monduli Mhe. Julius Kalanga Laizer akifafanua jambo wakati wa Mafunzo hayo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na BRELA

Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Hawa Mwaifunga akizungumza jambo huku akiiomba BRELA kufika katika Mikoa na Wilaya mbalimbali hapa nchini kuhakikisha Wadau wengi Wanajiunga na kurasimisha biashara zao.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Kanali mstaafu Masoud Ally Khamis (Mb) akihitimisha Mafunzo hayo huku akimpongeza Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala kwa kazi nzuri anayoifanya na kuitaka Wakala kuendelea kutoa Elimu ili wadau wa biashara wajue huduma mbalimbali wanazotoa hasa katika maeneo ya pembezoni ambapo wadau wa biashara hawajui umuhimu wa kurasimisha biashara zao pia hawana uelewa wa matumizi ya Tehama.


Kaimu Mtendaji Mkuu wa Brela Bi. Roy Mhando (aliyesimama) akitoa mawasilisho yake wakati wa Mafunzo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira iliyoandaliwa na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na BRELA.

Mbunge wa Ndanda Mhe. Cecil Mwambe (kushoto) akitoa ushauri kwa BRELA kuhusiana na kuaondoa malalamiko na changamoto wanazozipata wateja wao kuhakikisha wanazifanyia kazi na hatimae kusaidia kuongeza Idadi ya wateja na pato la Taifa kwa ujumla ,kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Hawa Mwaifunga

Baadhi ya Wafanyakazi wa BRELA wakiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu
wa pili kutoka kushoto Kabla ya kuingia Kwenye semina ya Kamati ya Bunge Wizarani ya Viwanda, Biashara na Mazingira.
Pichani kulia ni Mbunge wa Sumve Mhe. Richard Ndasa akiipongeza BRELAkatika suala zima la kuwahudumia wateja,huku Wananchi wengi wakiwezeshwa kupata huduma kwa urahisi,kushoto ni Mbunge wa jimbo la Igalula Mhe.Musa Ntimizi.
--
Picha : UNDER THE SAME SUN YAZINDUA MRADI WA 'HAKI YETU' KULINDA WATU WENYE UALBINO
Shirika la Under The Same Sun kwa kushirikiana na mashirika wenza GNRC NA CEFA wamezindua mradi wa “HAKI YETU” awamu ya pili, ambao umelenga kupunguza ama kutokomeza kabisa matukio ya kikatili ambayo wamekuwa wakifanyiwa watu wenye ualbino.
Uzinduzi wa mradi huo umefanyika leo Januari 19, 2020 kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na viongozi wa dini, ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akimwakilisha mkuu wa mkoa Zainab Telack.
Mboneko amesema Serikali inaahidi kutoa ushirikiano wa kutosha ili mradi huo ufanikiwe kwa asilimia 100, pamoja na kutoa elimu ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino, kuwaimarishia ulinzi na usalama, kuwapatia hifadhi na elimu katika shule ya Buhangija Jumuishi, pamoja na kufanya msako kwa wale wote wanaotekeleza mauaji na kuwachukulia hatua kali za kisheria.
Amesema bado kuna maeneo mengi katika jamii hayajafikiwa na elimu juu ya uelewa kwa watu wenye ulbino, kwa kutambua hao ni sawa na binadamu wengine, ambacho kinachowatofautisha ni rangi, huku akiahidi Serikali pamoja na wadau watashirikiana kwa pamoja kusambaza elimu hiyo ambayo itapunguza ama kutokomeza matukio ya ukatili na ubaguzi kwa watu wenye ualbino.
“Serikali kwa kushirikiana na wadau itaendelea kutoa elimu ya kupinga ukatili wa mauaji ya watu wenye ualbino, kuimarisha ulinzi na usalama, kuwapa hifadhi, kufanya msako kwa wale wote wanaotekeleza mauaji dhidi yao ama kupanga njama, pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria,”amesema Mboneko.
“Kutokana na jitihada hizi za kupinga matukio ya ukatili kwa watu wenye ualbino, katika mkoa wetu kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni hakuna tukio lolote lililotolewa taarifa linalohusu mauaji ya watu wenye ualbino, hivyo natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga wasiwafanye ukatili watu hawa pamoja na kuwabagua,
“Natoa rai pia kwa wazazi na walezi kutowaficha watoto wenye ualbino, bali wawa patie haki zao kama walivyo watoto wengine, ikiwamo kuwapeleka shule, pamoja na kuwapenda,” ameeleza.
Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya ameziagiza halmashauri zote sita za mkoa wa Shinyanga kuhakikisha zinatenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa mahitaji maalum ya watu wenye ualbino, pamoja na maofisa maendeleo kuwapatia elimu ya ujasiriamali na kuwaunga kwenye vikundi na kuwapa mikopo, ili wapate kufanya shughuli za kuwaingizia kipato.
Naye meneja mradi wa ‘HAKI YETU’ kutoka Shirika la Under The Same Sun Wakyo Musongo, amesema mradi huo unatekelezwa katika mikoa mitano kwa kushirikiana na mashirika matatu ambayo ni Under The Same Sun, GNRC NA CEFA, mikoa ambayo ni Simiyu, Kigoma, Mwanza, Geita pamoja na Shinyanga.
Amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Oktoba mwaka 2019, na sasa wameuzindua katika awamu ya pili mkoani Shinyanga ambapo utakoma Juni mwaka 2021, na utatekelezwa katika halmashauri ya Ushetu pamoja na halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambapo watakuwa wakitoa elimu ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino.
Aidha amesema katika utekelezaji wa mradi huo awamu ya pili kupitia warsha, maonyesho ya sanaa sehemu za wazi, semina, na vyombo mbalimbali vya habari, wanatarajia kufikia watendaji wa serikali 450, viongozi wa dini 400, wanafunzi 30,000, walimu 500, wenye ualbino 250, wananchi 26,000 pamoja na kupitia vyombo vya habari matarajio yao ni kufikia watu 4,000,000.
TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizundua mradi wa 'HAKI YETU' kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack. Mradi huo umelenga kupunguza ama kutokomeza kabisa matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi wa 'HAKI YETU' ambao umelenga kupunguza matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino.
Mkurugenzi wa Shirika la Under The Same Sun Berthasia Ladislaus, akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi wao wa 'HAKI YETU' ambao umelenga kupunguza matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino, wenye kauli mbiu isemayo Maisha yangu usalama wangu.
Meneja Mradi kutoka Shirika la Under The Same Sun Wakyo Musongo akielezea mradi wa HAKI YETU namna utakavyo fanya kazi mkoani Shinyanga katika kupunguza ama kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino.
Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashidi Mfaume akizungumza kwenye uzinduzi huo wa mradi wa HAKI YETU kwa niaba ya katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela.
Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU kutoka Shirika la Under The Same Sun.
Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU kutoka Shirika la Under The Same Sun.
Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU.
Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU .
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.
Mtoto mwenye ulbino akifuatilia uzinduzi wa mradi kwa kutumia kifaa maalumu cha kuongeza kuona kutokana na kusumbuliwa na tatizo la uoni hafifu.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.
Viongozi wa dini wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.
Mdau wa maendeleo kutoka Shirika la CHIDEP Mathias Chidama akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi wa 'HAKI YETU'.
Mdau wa maendeleo kutoka Shirika la Tawlae Eliasenya Nnko, akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU.
Kikundi cha Dar Creator kikitoa burudani kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko katikati mwenye nguo nyekundu akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi kutoka Shirika la Under The Same Sun, pamoja na watoto wenye ualbino.
Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog



















