Sunday, 19 January 2020

Picha : UNDER THE SAME SUN YAZINDUA MRADI WA 'HAKI YETU' KULINDA WATU WENYE UALBINO



Shirika la Under The Same Sun kwa kushirikiana na mashirika wenza GNRC NA CEFA wamezindua mradi wa “HAKI YETU” awamu ya pili, ambao umelenga kupunguza ama kutokomeza kabisa matukio ya kikatili ambayo wamekuwa wakifanyiwa watu wenye ualbino.


Uzinduzi wa mradi huo umefanyika leo Januari 19, 2020 kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga, na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na viongozi wa dini, ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akimwakilisha mkuu wa mkoa Zainab Telack.

Mboneko amesema Serikali inaahidi kutoa ushirikiano wa kutosha ili mradi huo ufanikiwe kwa asilimia 100, pamoja na kutoa elimu ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino, kuwaimarishia ulinzi na usalama, kuwapatia hifadhi na elimu katika shule ya Buhangija Jumuishi, pamoja na kufanya msako kwa wale wote wanaotekeleza mauaji na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Amesema bado kuna maeneo mengi katika jamii hayajafikiwa na elimu juu ya uelewa kwa watu wenye ulbino, kwa kutambua hao ni sawa na binadamu wengine, ambacho kinachowatofautisha ni rangi, huku akiahidi Serikali pamoja na wadau watashirikiana kwa pamoja kusambaza elimu hiyo ambayo itapunguza ama kutokomeza matukio ya ukatili na ubaguzi kwa watu wenye ualbino.

“Serikali kwa kushirikiana na wadau itaendelea kutoa elimu ya kupinga ukatili wa mauaji ya watu wenye ualbino, kuimarisha ulinzi na usalama, kuwapa hifadhi, kufanya msako kwa wale wote wanaotekeleza mauaji dhidi yao ama kupanga njama, pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria,”amesema Mboneko.

“Kutokana na jitihada hizi za kupinga matukio ya ukatili kwa watu wenye ualbino, katika mkoa wetu kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni hakuna tukio lolote lililotolewa taarifa linalohusu mauaji ya watu wenye ualbino, hivyo natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Shinyanga wasiwafanye ukatili watu hawa pamoja na kuwabagua,

“Natoa rai pia kwa wazazi na walezi kutowaficha watoto wenye ualbino, bali wawa patie haki zao kama walivyo watoto wengine, ikiwamo kuwapeleka shule, pamoja na kuwapenda,” ameeleza.

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya ameziagiza halmashauri zote sita za mkoa wa Shinyanga kuhakikisha zinatenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa mahitaji maalum ya watu wenye ualbino, pamoja na maofisa maendeleo kuwapatia elimu ya ujasiriamali na kuwaunga kwenye vikundi na kuwapa mikopo, ili wapate kufanya shughuli za kuwaingizia kipato.

Naye meneja mradi wa ‘HAKI YETU’ kutoka Shirika la Under The Same Sun Wakyo Musongo, amesema mradi huo unatekelezwa katika mikoa mitano kwa kushirikiana na mashirika matatu ambayo ni Under The Same Sun, GNRC NA CEFA, mikoa ambayo ni Simiyu, Kigoma, Mwanza, Geita pamoja na Shinyanga.

Amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Oktoba mwaka 2019, na sasa wameuzindua katika awamu ya pili mkoani Shinyanga ambapo utakoma Juni mwaka 2021, na utatekelezwa katika halmashauri ya Ushetu pamoja na halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambapo watakuwa wakitoa elimu ya kupinga matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino.

Aidha amesema katika utekelezaji wa mradi huo awamu ya pili kupitia warsha, maonyesho ya sanaa sehemu za wazi, semina, na vyombo mbalimbali vya habari, wanatarajia kufikia watendaji wa serikali 450, viongozi wa dini 400, wanafunzi 30,000, walimu 500, wenye ualbino 250, wananchi 26,000 pamoja na kupitia vyombo vya habari matarajio yao ni kufikia watu 4,000,000.


TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizundua mradi wa 'HAKI YETU' kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack. Mradi huo umelenga kupunguza ama kutokomeza kabisa matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi wa 'HAKI YETU' ambao umelenga kupunguza matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino.

Mkurugenzi wa Shirika la Under The Same Sun Berthasia Ladislaus, akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi wao wa 'HAKI YETU' ambao umelenga kupunguza matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino, wenye kauli mbiu isemayo Maisha yangu usalama wangu.

Meneja Mradi kutoka Shirika la Under The Same Sun Wakyo Musongo akielezea mradi wa HAKI YETU namna utakavyo fanya kazi mkoani Shinyanga katika kupunguza ama kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ualbino.

Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt. Rashidi Mfaume akizungumza kwenye uzinduzi huo wa mradi wa HAKI YETU kwa niaba ya katibu tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela. 

Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU kutoka Shirika la Under The Same Sun.

Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU kutoka Shirika la Under The Same Sun.

Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU.

Watoto wenye ualbino wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU .

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.

Mtoto mwenye ulbino akifuatilia uzinduzi wa mradi kwa kutumia kifaa maalumu cha kuongeza kuona kutokana na kusumbuliwa na tatizo la uoni hafifu.

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.

Viongozi wa dini wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi.

Mdau wa maendeleo kutoka Shirika la CHIDEP Mathias Chidama akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi wa 'HAKI YETU'.

Mdau wa maendeleo kutoka Shirika la Tawlae Eliasenya Nnko, akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU.

Kikundi cha Dar Creator kikitoa burudani kwenye uzinduzi wa mradi wa HAKI YETU.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko katikati mwenye nguo nyekundu akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi kutoka Shirika la Under The Same Sun, pamoja na watoto wenye ualbino.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:

SERIKALI YASEMA ITATUMIA HEKIMA KUWASAIDIA WANANCHI WALIOSHINDWA KUSAJILI LAINI ZA SIMU KISA NIDA

Na Happiness Tesha, Mwananchi 
 Serikali ya Tanzania imesema itatumia hekima kuwasaidia wananchi walioshindwa kusajili laini za simu kwa sababu ya kukosa kitambulisho cha Taifa na namba licha ya kuanza mchakato wa kupata kitambulisho hicho.

Imesema wananchi hao taarifa zao zipo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), huenda wamekosa kitambulisho au namba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Januari 19, 2020 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye katika mkutano wa ndani wa CCM mkoani Kigoma.

"Serikali itaona jinsi ya kutumia hekima kwa wananchi ambao taarifa zao zipo katika ofisi za Nida kuona namna ya kufanya lakini kwa wengine ambao hawajajaza fomu laini zao zitazimwa,” amesema Nditiye.

Amesema ambao laini zao zitazimwa ni wale waliosajili laini chache na kuacha nyingine licha ya kuwa na kitambulisho hicho.

Amebainisha kuwa usajili wa laini za simu ni endelevu licha ya baadhi ya wananchi kupuuza.

Kesho Jumatatu Januari 20, 2020 laini zote za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole zitazimwa. Ili uweze kusajili laini ni lazima uwe na kitambulisho cha Taifa au namba ya kitambulisho hicho.
Share:

SIMBA WAIADHIBU ALLIANCE FC... WAMEITANDIKA 4G KIRUMBA MWANZA

FULL TIME | Game imekwisha Kirumba Mwanza, Simba wanatoa adhabu kwa Allliance na kuchukua pointi tatu muhimu.

FT: Alliance FC 1-4 Simba SC.
Share:

MTU MFUPI ZAIDI DUNIANI AFARIKI DUNIA

Khagendra Thapa Magar enzi za uhai wake
Mtu mfupi zaidi duniani ambaye anaweza kutembea kama ilivyothibitishwa na kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness amefariki hospitalini Nepal akiwa na umri wa miaka 27.

Khagendra Thapa Magar, kutoka wilaya ya Baglung alikuwa na urefu wa sentimita 67.08cm sawa na futi mbili na nchi 4..

Nduguye aliambia chombo cha habari cha AFP kwamba alifariki siku ya Ijumaa baada ya kuugua homa ya mapafu.

Kitabu cha rekodi za Guiness kilituma risala za rambi rambi kwa bawana Magar kikisema kwamba hakuwacha udogo wake kumzuia kupata maisha bora duniani.

Bwana Magar alitambulika kuwa mtu mfupi zaidi duniani wakati wa sherehe za kuadhimisha mwaka wake wa 18 wa kuzaliwa mwaka 2010.

Katika sherehe iliowaleta pamoja maafisa wakuu kutoka maeneo tofauti alisema:. Sijichukulii kuwa mtu mdogo.

''Mimi ni mtu mkubwa , natumai kwamba taji hili litanifanya kuthibitisha hilo ili niweze kupata nyumba nzuri na familia yangu'' , alisema wakati huo.

Kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness kina orodha mbili za watu wafupi - wanaotembea na wasio tembea.

Raia wa Ufilipino Junrey Balawing ambaye hawezi kutembea ama hata kusimama bila usaidizi ndio mtu mfupi zaidi duniani asiyeweza kutembea. Akiwa na urefu wa sentimita 59.93.

Bwana Magar alipoteza taji lake akiwa mtu mfupi zaidi duniani kwa raia wa Nepal Chandra Bahadur Dangi ambaye alikuwa na urefu wa sentimita 54.6.

Hatahivyo, alihifadhi taji lake kufuatia kifo cha bwana Dangi 2015.

Bwana Magara kwa mara ya kwanza alionekana na muuzaji mmoja wakati alipokuwa na umri wa miaka 14 na kuchukuliwa katika maonyesho ya eneo hilo ambapo watoto walilazimika kulipa fedha ili kupigwa picha naye.

Baada ya kutambulika na kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness 2010, alisafiri maeneo mbalimbali duniani na kuonyeshwa katika vipindi vya runinga Ulaya na Marekani . Pia ndiye aliyekuwa sura rasmi ya kampeni za italii huko Nepal .

Craig Glenday, Muhariri wa kitabu cha rekodi za Guiness alisema kwamba alijawa na majonzi aliposikia habari za kifo cha bwana Magar.

''Alikuwa na tabasamu nzuri ambayo ilimvutia kila mtu aliyekutana naye'', alisema.

Rekodi ya mtu mfupi zaidi duniani anayetembea hivi sasa inashikiliwa na Edward Hernandez wa Colombia ambaye ana urefu wa sentimita 70.21.
Chanzo - BBC
Share:

Nafasi Mpya 650 za Kazi TANAPA...Mwisho wa Kutuma Maombi ni Tarehe 31 Mwezi huu

Nafasi Mpya  650 za Kazi TANAPA...Mwisho wa Kutuma Maombi ni Tarehe 31 Mwezi huu
__________________________

1. Conservation Assistant II- Wildlife Management-tourism 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Holder of Ordinary Diploma either in Wildlife Management, Conservation Science, Wildlife Tourism or equivalent qualifications from a recognized institution. 
 
_______________________________

2.Conservation Officer II- Geographical Information Systems 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Bachelor of Science Degree in Geo–informatics or Geomatics majoring in GIS or equivalent qualification from a recognised institution. 

_______________________________

3. Conservation Officer II- Information Communication Technology 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Bachelor Degree either in Computer Science, Information Technology, Computer Engineering or equivalent qualifications from a recognized institution.

_______________________________

4. Conservation Ranger III- Wildlife Management-driving - 15 Post 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Certificate of Secondary Education Examination (CSEE) with Certificate of Vehicle Driving from a recognized institution and valid Driving License Class E, D and C. A holder of Basic or Technician Certificate in Wildlife related fields or One-year National Service Certificate will be an added advantage.

_______________________________

5. Conservation Assistant II – Clinical Service 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Diploma in Clinical Medicine or equivalent qualification from a recognized institution and must be a holder of valid licence of registration by the Medical Council of Tanganyika (MCT).

_______________________________

6. Conservation Assistant II- Animal Health 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Ordinary Diploma in Animal Health and Production or equivalent qualification from a recognized Institution.

_______________________________

7. Conservation Ranger III-Wildlife Management- Law Enforcement  – 589 Post  

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Certificate of Secondary Education Examination (CSEE) with Basic or Technician Certificate in Wildlife Management or One-year National Service Certificate.

_______________________________

8. Conservation Ranger III- Plant Operation  – 2 Post  

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Certificate of Secondary Education Examination (CSEE) with Class “F” Plant Operators Licence.

_______________________________

9. Conservation Assistant II-Wildlife Management-Ecology- 4 Post  

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Diploma either in Wildlife Management, Conservation Science or equivalent qualification from a recognized institution.

_______________________________

10. Conservation Ranger III- Boat Operator

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Certificate of Secondary Education Examination (CSEE) with Basic Certificate in Marine Operations. A holder of Basic or Technician Certificate in Wildlife Management or One-year National Service Certificate will be an added advantage.

_______________________________

11.Conservation Ranger III- Nursing  – 4 Post  

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Certificate in Nursing. Must be licensed and Enrolled Nurse (EN) by the Tanzania Nurses and Midwives Council (TNMC).


_______________________________

12. Conservation Ranger III- Artisan - 6 Post  

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Certificate of Secondary Education Examination (CSEE) with Trade Test Grade III or Relevant CBET Level in Motor Vehicles Mechanics or Auto mobile or any other relevant fields from a recognized training Institution.


_______________________________

13. Conservation Officer II-Wildlife Management - 32 Post 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Bachelor Degree in either of the following fields; Wildlife Management, Conservation Science, Wildlife Ecology or equivalent qualification from a recognized institution.

_______________________________

14. Conservation Officer II-veterinary  – 2 Post 

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Bachelor of Science Degree in Veterinary Medicine or equivalent qualification from a recognized institution and must be registered by the Veterinary Council of Tanzania.

_______________________________

15. Conservation Officer II- Civil Engineering

QUALIFICATION AND EXPERIENCE
Bachelor Degree in Civil Engineering from a recognized Institution and must be registered by the Engineers Registration Board (ERB) as a “Graduate Engineer.”

_______________________________





Share:

RC SHIGELLA AWAAGIZA MA DC KUFANYA UZINDUZI WA VIFURISHI VYA BIMA YA AFYA KWENYE WILAYA ZAO


MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati akizundua kampeni ya uhamasishaji wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga kulia ni Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa NHIF Anna Makinda akizungumza wakati wa uzinduzi huo
MKURUGENZI wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga akizungumza wakati wa uzinduzi huo

MWENYEKITI wa Chama cha Bodaboda Tanzania Michael Haule akizungumza wakati wa uzinduzi huo
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa uzinduzi huo
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa NHIF Anna Makinda kushoto akipokea cheti kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kwa kutambua mchango wake kutokana na uhamasishaji ambao wanaufanya wakati wa uzinduzi huo
Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga kushoto akipokea cheti kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kwa kutambua mchango wake kutokana na uhamasishaji ambao wanaufanya
Msanii Mrisho Mpoto maarufu Mjomba akichangia fedha wakati wa uzinduzi huo
WATUMISHI wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakicheza wakati wa uzinduzi huo kushoto ni Meneja wa Mfuko huo Mkoani Tanga Ally Mwakababu katika ni Isaya Shekifu ambaye ni Meneja wa NHIF Mkoa wa Arusha na kulia ni Meneja wa NHIF Mkoa wa Kilimanjaro
 Sehemu ya wananchi wakiwa kwenye uzinduzi huo uliofanyika kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga



MKUU wa Mkoa wa Tanga Martin Shigella amezindua rasmi kampeni ya uhamasishaji wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga huku akitoa maelekezo kwa Wakuu wa wilaya za mkoa huo na Meneja wa NHIF Mkoa huo Ally Mwakababu kuhakikisha wanafanya uzinduzi kwenye ngazi ya wilaya.

Shigella aliyasema hayo kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga wakati wa uzinduzi huo ambapo aliipongeza NHIF kwa uamuzi wa kuja na vifurushi ikiwemo kufanya uzinduzi kwa kila mkoa ambao ni ubunifu mkubwa sana wanaoufanya na utawasaidia watanzania wengi kujiunga na mfuko huo.

Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza pia bodi ya NHIF kwa kuwa na ushirikiana mkubwa wa kufanya shughuli zao kwa ufanisi mkubwa unaowezesha mfuko huo kupiga hatua kubwa za kimaendeleo ikiwemo kutoa huduma nzuri kwa watanzania.

“Mimi nakufahamu vizuri sana Mwenyekiti wa Bodi kwa kazi nzuri ambazo unafanya kila mahala unapokabidhiwa hakujawahi kulegalega wala kurudi nyuma kunasonga mbele tena kwa kasi kubwa na mafanio hongera mama kwa kazi nzuri lakini pia niipongeze bodi ya NHIF”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa aliipongeza bodi ya mfuko huo kwa kazi nzuri ambao wamekuwa wakiifanya hata wanapokwenda mikoani kufuatilia maendeleo ya mfuko huo wamekuwa na ushirikiano mkubwa ambao umekuwa na tija kubwa kwa maendeleo.

“Lakini nipongeza Menejimenti chini ya Mkurugenzi wao Benard Konga wamekuwa wakifanya kazi kubwa katika kutimiza majukumu yao kwa kujituma ndio maana taarifa niliyoipata ni kwamba katika mifuko inayoenda vizuri na wanachama wanapata huduma kwa wakati na gharama zinazotokana na wanachjama kupata huduma za afya zinalipwa kwa wakati ni pamoja na NHIF”Alisema

Hata hivyo aliwaagiza wamiliki wa viwanda kuhakikisha wanawaingiza kwenye mpango wa huduma ya bima za afya vibarua wanaofanya shughuli za uzalishaji katika viwanda ili waweze kuwa na uhakika wa matibabu wao na familia zao.

Alisema kwamba miongoni mwa kundi lililo sahaulika ni vibarua toka viwandani ambao kwa sasa wanafikiria waingizwe kwenye mpango huo ili wakati wanapougua waweze kuwa na uhakika wa matibabu

Mkuu huyo wa mkoa alisema kundi hilo linafanyakazi kubwa ya uzalishaji lakini lipo kwenye mazingira magumu ya kazi zao huku hawajui hatma ya afya zao pamoja na familia zinazowategemea kutokana na kutokuwepo kwenye mfumo huo ambao unawawezesha kupata matibabu kwa njia ya Bima ya Afya.

“Jambo lililoanzishwa na NHIF la vifurushi vya bima ya afya ni jema sasa …nawaagiza MaDC na wamiliki wa viwanda wekeni utaratibu mzuri kwa vibarua wote wanapatiwa huduma hii ili kuwanusuru na afya zao”Alisema Shigella.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa NHIF Anna Makinda alisema ni mfumo bora ulioanzishwa na mfuko huo ambao unaweza kuyasaidia makundi mengi ambayo yalikosa fursa ya kupata huduma hiyo ya afya.

Makinda alisema awali mfuko huo uliwajali watumishi wa umma pekee huku asilimia kubwa ya watanzania ambao si watumishi hawakuwa na nafasi ya kujiunga na mfuko huo jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa afya zao.

“Yapo makundi kama bodaboda,machinga,na sacos mbalimbali ambazo hazikunufaika na huduma hii lakini kupitia mfumo huu wa vifurushi naamini kila mmoja anaweza kujiunga na kunufaika ili kwajengea uhakika wa matibabu yao”Alisema.

Mbali na hayo pia alisema tayari walishakubaliana na benki ya NMB ili kutoa mwanya kwa wananchi walio na kipato cha chini waweze kulipa kidogokidogo ili waweze kujiunga na huduma hiyo.

Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga alisema kwamba watanzania asilimia 34 ndio wapo kwenye mfumo wa bima ya afya bado safari ni ndefu kuhakikisha kila mtanzania anaingia kwenye bima ya Afya.

Alisema pia mfuko mwaka hadi mwaka mapato yamezidi kuongezeka na kuanzia mwaka 2014/2015 hadi kufikia sasa yameongezeka asilimia 33 hivi sasa wanakusanya Bilioni 502 kutoka kwa wanachama wao.

Alisema mchango wao kwenye sekta ya afya umeongezeka ambapo kwa mwaka wanalipa mpaka bilioni 441 ambazo wanatuma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.
Share:

Dr Bashiru Awaonya Wana CCM......"Mwenyekiti wala Katibu Mkuu Hawana Wagombea Wao"

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally ameweka bayana kuwa wanachama wote wanaotarajia kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi Mkuu wana haki sawa, na hakuna mwanachama wa Mwenyekiti wala Katibu Mkuu kama ambavyo baadhi ya wanachama wanavyoanza kuwalaghai wajumbe wa vikao kuwa wametumwa na Mwenyekiti na Katibu Mkuu kugombea.

Amesema kuwa ni vema, kila mmoja ajiandae kueleze sifa zake na kwa nini anadhani anafaa kuliko mwingine na sio kutumia sababu za kilaghai za kutumwa na Mwenyekiti, Katibu Mkuu ama Wazee, kwani anafahamu kuwa Mwenyekiti hana Mgombea yeyote, na  yeye (Katibu Mkuu) hana Mgombea kwa kuwa wagombea wote ni wakwao na wanahaki sawa.

Ameyasema hayo jana tarehe 18 Januari, 2020 katika Mkutano Mkuu wa Jimbo la Kigoma Kaskazini wa kupokea  taarifa ya kazi ya Mbunge wa jimbo hilo Ndg. Peter Serukamba.

“Wapo watarajiwa wanataka kugombea udiwani, ubunge, ni haki yao, na zipo kanuni na mila zetu, na mojawapo ni wewe kusema sifa zako sio kusema uongo, kusema nimetumwa na Katibu Mkuu kugombea hapa ni uongo, sema sifa zako, kusema nimetumwa na Mwenyekiti (Rais) ni uongo, nimetumwa na wazee, ni uongo, umewafanyaje wazee wakutume, sema sifa zako, una agenda gani, una sifa gani, una uwezo gani, unauzoefu gani, una mipango gani, na unaweza nini sio kusema uongo..”

Amesisitiza kuwa, watu ambao hawana sifa wanajiuza kwa kusema uongo, Mwenyekiti (Mhe. Rais Magufuli) hana Mgombea, wagombea wote ni wa kwake na Mwenyekiti hawezi kuwa na mgombea mmoja, hata yeye wakati anagombea hakusema ametumwa na yeyote ila sifa zake zilimuuza kwa wapiga kura.

Aidha, Katibu Mkuu kabla ya mkutano huo ametembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo mradi wa ujenzi wa barabara ya Chankele - Mwamgongo, upanuzi wa Kituo cha Afya cha Bitale na Kituo cha Utafiti wa mbegu za michikichi cha Kihinga

Ziara hii imeongozwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kigoma Ndg. Amandus Nzamba, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa Ndg. Kirumbe Ng’enda, Mkuu wa Mkoa huo Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga, wabunge ni Ndg. Daniel Nsanzugwako, Hasna Mwilima na Peter Serukamba.


Share:

Waziri Mkuu Azuia Vibali Vya Sukari Nje ya Nchi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda Bw. Juma Hassan Reli ahakikishe anazuia utoaji wa vibali vya kuingiza sukari kutoka nje hadi sukari inayozalishwa na kiwanda cha sukari cha Zanzibar kilichopo Mahonda iishe.

Amesema haiwezekani kiwanda hicho cha pekee kinachozalisha tani 6,000 za sukari kwa mwaka kikakosa wateja wakati mahitaji ya sukari Zanzibar ni tani 36,000 kwa mwaka.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Jumamosi, Januari 18, 2020) wakati apotembelea kiwanda cha kuzalisha sukari cha Zanzibar kilichopo katika eneo la Mahonda wilaya ya Kaskazini ‘A’ mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema ni vizuri wizara ikahahakikisha sukari inayozalishwa na kiwanda hicho inapewa kipaumbele cha kwanza kwa kununuliwa kwa sababu wanauhakika na ubora wake kwa kuwa wameshuhudia uzalishaji wake kuanzia hatua ya awali miwa ikiwa shambani.

“Wizara ya Viwanda lazima mbadilike na muweke utaratibu mzuri wa kusimamia uingizwaji wa sukari kutoka nje. Haiwezekani sukari inayozalishwa ndani ikakosa soko kutokana na uingizwaji wa sukari kutoka nje. Hatuwezi kumfurahisha mtu mmoja huku wengi wakiumia.”

Waziri Mkuu amesema Serikali imeamua kukuza uchumi kwa kupitia sekta ya viwanda hivyo ni lazima viwanda vya ndani vikalindwa. “Viwanda vinasaidia katika kuondoa tatizo la ajira, vinawapa wakulima soko la uhakika la mazao yao pamoja na Serikali kupata kodi ya uhakika.”

Amesema kitendo cha wizara hiyo kushindwa kuratibu vizuri suala la uingizwaji wa sukari kutoka nje ya nchi kutakwamisha uwekezaji jambo ambalo ni sawa na kuihujumu Serikali kwa kuwa itasababisha wananchi kupoteza ajira pamoja na Serikali kukosa mapato.

Waziri Mkuu amesema “haiwezekani sukari inayotengezwa na kiwanda hicho ambayo ubora wake umethibitishwa na Shirika la Viwango Zanzibar ikakosa soko hii haiwezekani tukashindwa kununua tani 6,000 huku mahitaji yetu ni tani 36,000.”

Amesema sera ya nchi inasisitiza umuhimu wa kulinda wazalishaji wa ndani ambao bidhaa zao zimethibitishwa na mamlaka husika. Hivyo, ni lazima kuwalinda wawekezaji kwa kuhakikisha wanapata masoko ya uhakika pamoja na kuhamasisha wananchi kutumia bidhaa hizo.

Awali, Mkurugenzi Mkaazi wa kiwanda cha Sukari Zanzibar, Bw. Rahim Bhaloo alisema kiwanda chao kinazalisha tani 6,000 kwa mwaka huku kikiwa na uwezo wa kuzalisha tani zaidi ya 20,000 kwa mwaka ila tatizo ni soko pamoja na ardhi ya kutosha kulima miwa.

Alisema kutokana na uhaba wa soko sukari waliyozalisha katika msimu wa mwaka 2010/2020 wameuza tani 2,800 tu na kiasi cha tani 3,200 bado kipo kiwandani hapo, hivyo ameiomba Serikali iwasaidie kwa kuwatafutia masoko pamoja na ardhi ili waweze kuongeza uzalishaji.

Mkurugenzi huyo aliiomba Serika iwe inazuia utoaji wa vibali vya uagizaji wa sukari kutoka nje hususani kipindi cha uzalishaji ili waweze kuuza sukari yao na itakapoisha ndio vibali hivyo vianze kutolewa. Kiwanda kimeajiri wafanyakazi 300, pia wakulima wa nje zaidi ya 800 wanauza miwa yao kiwandai hapo.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Viwanda Zanzibar, Bw. Juma Hassan Reli amemhakikishia Waziri Mkuu kwamba sukari yote iliyopo kiwandani hapo itakuwa imeshanunuliwa ifikapo Februari mwaka huu. Pia maelekezo yote aliyoyatoa kuhusu utoaji wa vibali vya uagizaji wa sukari watayafanyia kazi.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili January 19















Share:

Saturday, 18 January 2020

CONSERVATION ASSISTANT II- ANIMAL HEALTH – 1 POST

POST CONSERVATION ASSISTANT II- ANIMAL HEALTH – 1 POST POST CATEGORY(S) FARMING AND AGRIBUSINESS EMPLOYER TANZANIA NATIONAL PARKS (TANAPA) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-17 2020-01-31 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES (i)Participating in examination and assessment of animal health to determine the nature of diseases or injuries; (ii)Collaborating with neighboring District Veterinary Department in offering Veterinary services to local communities;… Read More »

The post CONSERVATION ASSISTANT II- ANIMAL HEALTH – 1 POST appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

CONSERVATION RANGER III- NURSING – 4 POST

POST CONSERVATION RANGER III- NURSING – 4 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER TANZANIA NATIONAL PARKS (TANAPA) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-17 2020-01-31 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES (i)Administrating prescribed medications and treatments to patients; (ii)Preparing equipment and assist medical practitioner during treatment and examination of patient; (iii)Clarifying procedures and treatments to patient to gain cooperation, understanding and… Read More »

The post CONSERVATION RANGER III- NURSING – 4 POST appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mataifa yaliyopoteza raia kwenye ndege ya Ukraine yaidai fidia Iran

Mataifa yaliyopoteza raia katika ajali ya ndege ya Ukraine iliyodunguliwa na Iran yameitaka Tehran iwajibike kikamilifu, uchunguzi wa kimataifa uanzishwe na familia za wahanga zilipwe fidia.

Mawaziri wa mambo ya nje wa Canada, Uingereza, Ukraine, Sweden, Uholanzi na Afghanistan wamekutana jijini London katika ubolozi wa Canada.

Mawaziri hao baada ya mkutano wao walitoa taarifa ya pamoja wakiitaka Iran ifanye uchunguzi wa kimataifa utakao kuwa huru na wazi hasa kwa mataifa yanayoomboleza.

Waziri wa mambo ya nje wa Canada Francois-Philippe Champagne amesema wamekutana  kutafuta uwajibikaji na haki kwa wahanga wa mkasa huo na kuongeza kuwa familia za wahanga hao zinataka majibu, jamii ya kimataifa inataka majibu na dunia nzima pia inasubiri majibu na kwamba hawatapumzika hadi watakapoyapata.

Watu wote 176 waliokuwa ndani ya  ndege ya abiria ya Ukraine walipoteza maisha yao wakati ndege yao ilipodunguliwa na kombora muda mfupi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Imam Khomeini mjini Tehran tarehe 8 mwezi huu.


Share:

CONSERVATION RANGER III- WILDLIFE MANAGEMENT-DRIVING – 15 POST

POST CONSERVATION RANGER III- WILDLIFE MANAGEMENT-DRIVING – 15 POST POST CATEGORY(S) HR & ADMINISTRATION EMPLOYER TANZANIA NATIONAL PARKS (TANAPA) APPLICATION TIMELINE: 2020-01-17 2020-01-31 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES (i)Driving assigned motor vehicles, ensuring security and safety of the vehicle, passengers and goods on and off the road; (ii)Accounting for fuels, oil and spares parts as per stipulated… Read More »

The post CONSERVATION RANGER III- WILDLIFE MANAGEMENT-DRIVING – 15 POST appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger