Friday, 17 May 2019

Picha : AGAPE YAKUTANA NA WATENDAJI WA SERIKALI KISHAPU KUJADILI SAUTI YA MWANAMKE NA MTOTO




Shirika lisilo la kiserikali AGAPE AIDS CONTROL PROGRAM Mkoani Shinyanga, limekutanisha watendaji wa Serikali kutoka halmashauri ya wilaya ya Kishapu pamoja na mkoa, kwa ajili ya kujadili namna ya kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.


Kikao hicho kimefanyika leo Mei 17,2019 katika ukumbi wa mikutano wa Hotel ya Liga Shinyanga Mjini, kwa kukutanisha Maofisa Maendeleo ya jamii wilaya ya Kishapu, watendaji wa Kata, maofisa ustawi wa jamii, mahakimu, wanasheria, dawati la Jinsia, pamoja na baadhi ya madiwani.

Akizungumza kwenye kikao hicho wakati akiwasilisha mradi wa Sauti ya Mwanamke na Watoto, Ofisa mradi kutoka Shirikala Agape Felex Ngaiza, amesema wamekutanisha watendaji hao wa serikali pamoja na baadhi ya madiwani kutoka kata tatu mahali ambapo mradi huo unatekelezwa, ili kuunganisha nguvu ya pamoja kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Amesema watendaji hao wa serikali ni wa muhimu sana katika kuendeleza mapambano ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto, hali ambayo imewafanya kukaa nao kikao ili kuwaelezea namna mradi unavyofanya kazi pamoja na kutatua changamoto zake.

Amesema mradi huo utatekelezwa katika kata tatu za halmashauri ya wilaya ya Kishapu ambazo ni Itilima, Bunambiu na Kishapu, ambapo utatekelezwa kwa majaribio ndani ya miezi sita kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, na ukileta matokeo chanya utadumu ndani ya miaka mitano.

“Mradi huu wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto ni wa miezi sita tu, ambao uzinduzi wake ulifanyika Aprili 9 mwaka huu, na umelenga kutokomeza masuala ya matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, kwa kutolewa taarifa za matukio hayo na kuweza kuchukuliwa hatua za kisheria,”amesema Ngaiza.

“Matarajio ya mradi huu ni kuongeza uelewa wa kisheria kwa wanawake na watoto dhidi ya matukio ya kikatili ambayo hufanyiwa, utoaji wa taarifa nyingi za mtukio ya ukatili, pamoja na hatua za kisheria zipate kuchukuliwa dhidi ya watu ambao hufanya vitendo hivyo vya ukatili,”ameongeza.

Katika hatua nyingine Ngaiza ametaja changamoto ambazo wanakumbana nazo katika utekelezaji wa mradi huo, kuwa uongozi wa vijiji kukaa na kesi za matukio ya ukatili wa kinjsia kwa muda mrefu bila kuzipeleka kwenye mamlaka husika, na nyingine kuzifanyia suluhu bila ya kuwa na uwezo nazo, pamoja na ukosefu wa bajeti ya kuhudumia wahanga wanaofanyiwa ukatili.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa  Shirika la Agape, Amani Peter, amewataka watendaji hao wa serikali kuwa na ushirikiano mzuri na wananchi pale wanapopewa taarifa za matukio ya ukatili ,pamoja na kuwa wasiri ili kutoka haribu ushahidi dhidi ya kesi hizo, ambapo mara nyingi watuhumiwa wamekuwa wakikimbia kusiko julikana hasa wa matukio ya ubakaji na upigaji mimba wanafunzi pamoja na wananchi kuogopa kutengwa.

Nao baadhi ya washiriki wa kikao hicho walilipongeza Shirika hilo kwa kuwakutanisha pamoja, na kutoa maadhimio kuwa elimu iendelee kutolewa kwa wananchi juu ya kuachana na matukio hayo ya ukatili kwa wanawake na watoto hasa kwa kuendekeza tabia ya mfumo dume.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI

Kaimu mkurugenzi wa Shirika la Agape Peter Amani akielezea namna walivyoanzisha mradi huo wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto, ambao umelenga kutokomeza masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika Kata tatu za Bunambiu, Itilima na Kishapu. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Afisa mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto kutoka Shirika la Agape Felex Ngaiza, akielezea mradi namna utakavyokuwa unatekelezwa katika Kata hizo Tatu za Kishapu, ambapo utadumu kwa muda wa miezi sita.

Afisa Maendeleo ya Jamii halmashauri ya wilaya ya Kishapu Joseph Swalala akichangia mada kwenye kikao hicho na kushauri jamii iendelee kupewa elimu juu ya kupinga matukio hayo ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Afisa Ustawi wa Jamii mkoa wa Shinyanga Lidya Kwesigabo akichangia mada kwenye kikao hicho na kuomba pia kuwepo kwa usiri hasa kwa watu ambao wamekuwa wakitoa taarifa za matukio hayo ya ukatili, ili kulinda usalama wake pamoja na kutovuja kwa taarifa za mtuhumiwa kukata kukamatwa na matokeo yake wanakimbia.

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Itilima wilayani Kishapu Athumani Kitundu, akichagia mada kwenye kikao hicho na kuomba pia jamii ipewe elimu ya kutosha kuachana na masuala ya mfumo dume, pamoja na kutoa ushahidi Mahakamani ili watuhumiwa wapate kuchukuliwa hatua za kisheria ili kukomesha matukio hayo ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Mtendaji wa Kata ya Kishapu Nunya Chege akichangia mada kwenye kikao hicho ameilalamikia Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo imekuwa ikwazo kwao katika utendaji kazi wa kuzia matuki ya ukatili dhidi ya watoto hasa kwenye upewaji wa mimba na ndoa za utotoni kwa kushindwa kuwa tia hatiani watuhumiwa.

Askali kutoka dawati la jinsia Polisi wilaya ya Shinyanga Joseph Christopher naye akichangia mada kwenye kikao hicho na kuwataka wananchi wawe wanatoa ushirikiano kwa Jeshi la polisi juu ya matukio ya ukatili ili yapate kushughulikiwa na kubainisha usiri kwa jeshi hilo hua upo pamoja na kuwahikishia usalama wao watoa taarifa wote.

AfisaMaendeleo ya Jamii halmashauri ya wilaya ya Kishapu Neema Godwin Mwaifuge naye akichangia mada kwenye kikao hicho.

Kaimu Ofisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Shinyanga Octavian Kiwone akiongoza majadiliano kwenye kikao hicho.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha Shirika la Agape cha kujadili namna ya kuunganisha nguvu ya pamoja na watendaji wa Serikali na baadhi ya madiwani juu ya kupambana na tatizo la kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika Kata tatu za Bunambiu,Itilima na Kishapu.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha Shirika la Agape cha kujadili namna ya kuunganisha nguvu ya pamoja na watendaji wa serikali na baadhi ya madiwani juu ya kupambana na tatizo la kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika Kata tatu za Bunambiu,Itilima na Kishapu.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha Shirika la Agape cha kujadili namna ya kuunganisha nguvu ya pamoja na watendaji wa Serikali na baadhi ya madiwani juu ya kupambana na tatizo la kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika Kata tatu za Bunambiu,Itilima na Kishapu.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha Shirika la Agape cha kujadili namna ya kuunganisha nguvu ya pamoja na watendaji wa Serikali na baadhi ya madiwani juu ya kupambana na tatizo la kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika kata tatu za Bunambiu,Itilima na Kishapu.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha Shirika la Agape cha kujadili namna ya kuunganisha nguvu ya pamoja na watendaji wa Serikali na baadhi ya madiwani juu ya kupambana na tatizo la kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika Kata tatu za Bunambiu,Itilima na Kishapu.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha Shirika la Agape cha kujadili namna ya kuunganisha nguvu ya pamoja na watendaji wa Serikali na Baadhi ya Madiwani juu ya kupambana na tatizo la kutokomeza matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto wilayani Kishapu katika Kata tatu za Bunambiu,Itilima na Kishapu.

Picha zote na Marco Maduhu-Malunde 1 Blog


Share:

Picha : STEPHEN MASELE ARUDI TANZANIA BAADA YA MKUTANO WA BUNGE LA AFRIKA (PAP) KUFUNGWA


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mhe. Stephen Masele ambaye ni Mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini ameonekana akijiandaa kusafiri kurudi nchini Tanzania baada ya Mkutano wa Bunge la Afrika uliokuwa unaendelea jijini Johannesburg,Afrika Kusini tangu Mei 6,2019, kufungwa leo Ijumaa Mei 17,2019.


Mhe. Masele alikuwa anahudhuria mkutano wa bunge la Afrika na baada ya kukamilisha majukumu yaliyompeleka sasa amerejea nyumbani Tanzania.

Soma pia : Picha : MKUTANO WA PILI WA BUNGE LA AFRIKA (PAP) WAFUNGWA
Walinzi wakiwa wamebeba mizigo ya Mhe. Stephen Masele.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mhe. Stephen  Masele akiondoka katika Hotel ya Gallagher hoteli iliyopo jijini Johannesburg,Afrika Kusini baada ya mkutano wa Bunge la Afrika kufungwa leo Mei 17,2019.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mhe. Stephen Masele.

Share:

Waziri Mkuu Afungua Semina Ya Wanahisa Wa Benki Ya CRDB .....Autaka Uongozi Wa Benki Ya CRDB Uzidi Kuzingatia Misingi Ya Utawala Bora

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameutaka uongozi wa Benki ya CRDB uzidikuzingatia misingi ya utawala borana kuongeza juhudi katika utoaji wa huduma ili benki hiyo iendeleekuwa mfano wa mafanikio kwa taasisi zinazomilikiwa nakuendeshwa na wazalendo.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Mei 17, 2019) wakati akifungua semina ya wanahisa wa benki ya CRDB katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) jijini Arusha. Semina hiyo inahudhuriwa na wanahisa 1,500.

Amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imeendelea kuimarisha misingi ya utawala bora ili kuleta matokeochanya, hivyo ni vema kwa uongozi wa benki hiyo ukaizingatia. 

“Serikali imeendelea kuhakikisha kwamba katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali kunakuwepo na uwazi, uwajibikaji, ushirikishaji wa watu, ufanisi, tija, uadilifu, usawa, kuzingatia taratibu za kisheria, kanuni na miongozo inayotolewa na Viongozi wakuu wa kitaifa.”

Waziri Mkuu amesema Serikali imeendelea kusisitiza misingi hiyo ya utawala bora ili kujiridhisha kuwa taasisi mbalimbali zikiwemo za kifedha zinaongozwa kwa kufuata misingi hiyo.

“Serikali imeendelea kusisitiza uwazi katikakuendesha shughuli za umma na makampuni yanayomilikiwa nawananchi bila usiri na kificho. Lengo ni kuwapa wananchi uwezo wakupima utendaji na uzingatiaji wa kanuni, taratibu na sheria.”

Waziri Mkuu amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi wa jinsia zote na makundi yote wanahusishwa katika kupanga nakufanya maamuzi ya mambo yanayowahusu ili kuwawezesha kujiletea maendeleo.
“Nyote ni mashahidi kuwa Serikali imeendelea kuhimiza utendaji unaozalisha matokeo  yanayokidhi lengo na matarajio ya watu na kuhakikisha taasisi za kifedha zinatimiza ndoto za wananchi katika kupata huduma nzuri ikiwemo upatikanaji wa mikopo na elimu ya matumizi bora ya fedha.”

Hivyo, Waziri Mkuu amesema ni vema benki hiyo kupitia kitengo chake cha elimu ihakikishe inatoa elimu kwa umma juu ya matumizi mazuri ya fedha zikiwemo za mikopo ili wananchi waweze kuitumia vizuri na kujiongezea tija.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Abdulmajid Msekela alisema zaidi ya asilimia 80 ya hisa za benki hiyo zinamilikiwa na Watanzania ikiwemo Serikali, hivyo uongozi wa benki hiyo una jukumu kubwa la kuhakikisha wanatoa huduma bora.

Alisema wamejipanga kuboresha huduma zao ili wanahisa waweze kujivunia uwekezaji wao walioufanya kwenye benki hiyo. “Tupo tayari kuhakikisha benki ya CRDB inasonga mbele zaidi ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma kwa wateja.”

Mkurugenzi huyo alisema kuwa mbali na kuboresha huduma kwa wateja, pia wataongeza ufanisi katika utoaji wa huduma na hatimaye waweze kutoa gawio kubwa kwa wanahisa wao. Benki ya CRDB inaongoza kwa kupata faida kubwa.

Kwa upande wake,Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kicheere ambaye alimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango katika semina hiyo, alitumia fursa hiyo kuwashauri wananchi wajenge tabia ya kuwekeza kwenye hisa. Alisema mwamko wa  Watanzania katika kuwekeza kwenye hisa bado ni mdogo.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kupewa vifaa na zana bora za kisasa.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussen Mwinyi, amesema katika mwaka ujao wa fedha 2019/20, watalipa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) vifaa na zana bora za kisasa.

Alisema sambamba na hilo, watatoa mafunzo kwa wanajeshi ili kuliongezea jeshi hilo uwezo na weledi wa kiutendaji, kiulinzi na kivita.

Akiwasilisha hotuba ya wizara hiyo bungeni jana, Dk. Mwinyi alisema pia wamepanga kuboresha mazingira ya kazi, kuimarisha upatikanaji wa huduma stahiki na mahitaji ya msingi kwa wanajeshi na watumishi wa umma.

Pia, kuwapatia vijana wa Tanzania mafunzo ya ukakamavu, umoja wa kitaifa, uzalendo na stadi za kazi.

Aidha waziri huyo alieleza kuwa wizara itaendeleza tafiti na uhaulishwaji wa teknolojia kwa kuimarisha na kuanzisha viwanda kwa madhumuni ya kuzalisha bidhaa na huduma kwa matumizi ya kijeshi na kiraia.

Pia kuimarisha ushirikiano wa jumuiya za kimataifa, kikanda na nchi moja moja katika nyanja za kijeshi na kiulinzi.

Nyingine ni kufanya upimaji, uthamini na ulipaji fidia ya ardhi katika maeneo yaliyotwaliwa kwa matumizi ya jeshi.

Dk. Mwinyi aliongeza kuwa wataendelea kushirikiana na mamlaka za kiraia katika kukabiliana na majanga na dharura pale inapohitajika.

“Kulipa stahili mbalimbali za maafisa, askari, vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa na watumishi wa umma.

“Kukamilisha sera ya ulinzi wa taifa, mwongozo wa viwanda jeshini na mpango wa maendeleo wa miaka 10, yaani 2018/29-2027/28 wa kuliimarisha Shirika la Nyumbu,” alisema.

Dk. Mwinyi pia alizungumzia hali ya usalama wa mipaka ya Tanzania kuwa ipo shwari licha ya kuwapo tishio kutoka kwenye vikundi vya kigaidi katika baadhi ya nchi jirani.


Share:

Taarifa Mbalimbali Za Uhalifu Kutoka Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mbeya

KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WANNE KWA TUHUMA ZA WIZI NA KUGHUSHI NYARAKA MBALIMBALI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wanne [04] ambao ni:-
1.     PILI OMARI [30] Mkazi wa Mbezi – Dar es Salaam
2.     HAMIS NGOWI [40] Mkazi wa Dar es salaama na
3.     OMARY MOHAMED [41] Mwalimu na Mkazi wa Nzovwe
4.     MARTHA KASMIRI [34] Mkazi wa Dar es salaam - Mbezi kwa tuhuma ya wizi katika Benki.

Mnamo tarehe 13.05.2019 saa 14:00 mchana huko katika Benki ya Posta tawi la Mwanjelwa iliyopo Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi kwa kushirikiana na maafisa wa benki hiyo waliwakamata PILI OMARI [30] na MARTHA KASMIRI [34] wote wakazi wa Dar es salaam - Mbezi wakiwa na nyaraka ‘salary slip’ zenye majina ya watu wengine ambao ni watumishi wa idara ya elimu, vitambulisho vya mpiga kura, fomu za utambulisho kutoka Jiji, fomu za mikopo kutoka benki ya Posta na barua za uthibitisho kutoka kwa mwajiri ambazo ni za kughushi.
Watuhumiwa wengine ambao ni HAMIS NGOWI [40] mfanyabiashara na mkazi wa Dar es salaama na OMARY MOHAMED [41] mwalimu na mkazi wa Nzovwe wamekamatwa wakati mtuhumiwa HAMIS NGOWI @ OPTATI NGOWI alipopekuliwa alikutwa na:-
1.     Mihuri 6 ya idara tofauti za serikali.
2.     Laini 10 za mitandao ya simu Vodacom, Tigo na Halotel,
3.     Picha ndogo 3 za watu tofauti ya jinsia ya kike,
4.     Funguo 2 za gari,
5.     Fomu za utambulisho kutoka Jiji,
6.     Fomu za mikopo kutoka benki ya Posta,
7.     ‘Salary slip’ pamoja na barua za uthibitisho kutoka kwa waajiri. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.
 
KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WAWILI WANAOJIHUSISHA NA MATUKIO YA UNYANG’ANYI, WIZI NA UBAKAJI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia vijana wawili ambao ni:-
1.     NASIBU JUMA [20] Mkazi wa Nzovwe Mbeya
2.     BRIGHT THOMAS [19] Mkazi wa Mtaa wa Ndanyella Mbeya
Kwa tuhuma ya kujihusisha na matukio ya unyang’anyi, wizi na ubakaji katika maeneo ya Nzovwe, Iyunga na Iwambi Jijini Mbeya.
Watuhumiwa walikamatwa mnamo tarehe 14/05/2019 huko Iyunga katika Klabu cha Pombe cha London kilichopo Jijini Mbeya na katika upekuzi watuhumiwa walikutwa na :-
1.     Mapanga mawili [02]
2.     Mizula miwili [02]
3.     Makoti meusi mawili [02]
Katika mahojiana na watuhumiwa wamekiri kuhusika katika matukio mbalimbali kama ifuatavyo:-
Mnamo tarehe 26/03/2019 saa 22:00 usiku huko Mtaa wa Inyala uliopo Kata ya Iyunga na Tarafa ya Iyunga ambapo walivamia nyumbani kwa Mwalimu wa Chuo MUST aitwaye WILLIAM MBATTA na kumjeruhi kwa mapanga sehemu ya kichwani na kisha kutoweka.
Mnamo tarehe 30/03/2019 saa 22:00 usiku katika viwanja vya MUST walimjeruhi ALLEN NYITTI kwa kumkata panga kichwani, kiunoni na tumboni na kupora simu aina ya Samsung Galaxy na pesa taslimu Shiling 21,000/=
Mnamo tarehe 05/04/2019 saa 02:00 usiku huko katika Mtaa wa Ndanyella, Kata ya Nzovwe, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya walimvamia FATUMA HAJI [21] walimbaka na kupora pesa taslimu shilingi 3,280,000/= pia waliiba TV aina ya LG na Redio Sub Woofer, Deck na simu ya mkononi aina ya Samsung J7. Mali zote zikiwa na thamani ya shilingi 4,120,000/=
Mnamo tarehe 04/05/2019 saa 02:45 usiku huko Kota za Tazara zilizopo Iyunga Mbeya walivamia nyumbani  kwa FRANK CHARLES na kumjeruhi kwa kumkata na mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake yeye na mke wake aitwaye VICTORIA SAMWEL pamoja na kupora TV aina ya Boss yenye ukubwa wa inchi 55.

KUKAMATA BIDHAA ZILIZOPIGWA MARUFUKU NCHINI.
Mnamo tarehe 16/05/2019 saa 05:00 Alfajiri huko maeneo ya Block “T”, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya, Askari Polisi wakiwa doria katika maeneo hayo waliliona gari lenye namba ya usajili T.937 CKD aina ya Toyota Mark II Blit na kulitilia mashaka na ndipo kukuta limebeba bidhaa mbalimbali zilizopigwa marufuku nchini ambazo:-
1.     Pombe kali aina ya PRINCE katoni sita @ chupa 20 sawa na chupa 120
2.     Pombe kali aina ya Officer”s Verve katoni 24 @ chupa 20 sawa na chupa 480
3.     Condom aina ya Ultimate Assured Protection katoni 63 ambazo zilitolewa na Serikali ya Marekani kwa nchi ya Zambia.
4.     Panga moja.
5.     Carolight 120ml pcs 36
6.     Citrolight 120ml pcs 84
7.     Coco Pulp 150mls pcs 24
8.     Coco Pulp 500mls pcs 06
9.     Coco Pulp 300mls pcs 36
10. Coco Pulp Lightening oil 50mls pcs 72
11. Coco Pulp 50g pcs 06
12. Carotone Crème ndogo 65mls pcs 24
13. Cocoderm pcs 06
14. Clinic Clear pcs 06
15. Extra Clair 120mls pcs 54
16. Elle 5 Crème pcs 3
17. Diproson tube 30g pcs 74
18. Diproson lotion 30mls pcs 48
19. Top Lemon Plus 170mls pcs 84
20. Carotone black spot corrector pcs 06
21. Dermotyl tube 15g pcs 10
22. Dermotyl lotion 30mls pcs 90
23. Dodo Crème ndogo pcs 06
24. Clairmen pcs 12
25. Bronz tone crème 125ml pcs 15
26. Miki Clair 160ml pcs 48
27. Movate Cream 30g pcs 50
28. Oranvate gel 30g pcs 50
29. Beaution Cream 330mls pcs 12
30. Miss Caroline 150mls pcs 12
31. Carolight Cream 120mls pcs 78
32. Diana lotion 30mls dozen 03 sawa na pcs 36
33. Teint Clair 150mls pcs 48
34. Betasol lotion 30mls pcs 36
35. Betasol tube 15g pcs 40
36. Perfect white cream 150mls pcs 12
37. Perfect white lotion 30mls pcs 06
38. Lemon vate cream 30g pcs 40
39. Mont Claire 30g pcs 10
40. Neoprosone Gel 30g pcs 10
41. Epiderm Creme 15g pcs 41
42. Epiderm Crème 30g pcs 24
Gari hilo lilikuwa likitokea Tunduma kuja Mbeya likiwa na bidhaa hizo. Gari pamoja na vielelezo vipo kituo cha Polisi. Msako mkali wa kuwatafuta watuhumiwa waliokuwa wakisafirisha bidhaa hizo unaendelea.

KUPATIKANA NA POMBE KALI ZILIZOPIGWA MARUFUKU NCHINI.
Mnamo tarehe 13.05.2019 majira ya saa 21:00 usiku huko maeneo ya Iwambi, Kata ya Iwambi, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya. Polisi walimkamata kijana mmoja aitwaye ELIA MWAKALIKWE [25] Mkazi wa Iwambi akiwa na Pombe Kali zilizopigwa marufuku nchini aina ya Verve katoni 27 zikitokea nchini Zambia.

Imetolewa na;
[ULRICH O. MATEI – SACP]
   KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:

Membe Amjibu Rostam Aziz Sakata La Kugombea Urais Mwakani

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya awamu ya nne, Bernard Membe amemjibu mfanyabishara Rostam Aziz kuhusu suala la kugombea urais 2020 akimtaka hivi sasa ajikite kwenye masuala ya kitaifa yanayohusu uchumi.

Membe ametoa kauli hiyo akiwa nje ya jengo la Mahakama kuu ya Tanzania, wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoka kusikilizwa kwa kesi anayodai fidia dhidi ya mmiliki wa gazeti la Tanzanite Cyprian Musiba, ambapo aliulizwa swali kuhusiana na kauli inayodaiwa kutolewa na mfanyabiashara Rostam Aziz kuhusiana na uchaguzi wa mwakani.

Jana Mei 16, 2019, picha moja ya video ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha Rostam akizungumzia suala la urais 2020 na kumshauri Membe asijitokeze kuwania nafasi hiyo badala yake aachiwe Rais John Magufuli kwa awamu nyingine.

Membe amesema kuwa ; "Kuhusu kugombea mwakani napata kigugumizi kumjibu Rostam, lakini yeye ni mchumi na nitakutana naye nimshauri anafanya vizuri kwa Watanzania anapozungumzia masuala ya uchumi, inabidi azungumzie 'main issue' za nchi sio 'personal', hizi tunaachia watu wa chini."

"Kwa 'level' yetu ni kuzungumzia masuala ya kitaifa masuala ya kiuchumi, kwanini uchumi wetu upo hapa ulipo? kwanini wafanyabiashara wanafunga biashara zao, Rostam ni 'economist' namshauri ajiadress kwenye masuala ya kiuchumi, Rostam wewe ni mwenzetu sisi tumekatwa mkia." amesema Membe.

"Ukikatwa mkia hata ujitahidi vipi mkia wako ni mfupi tu, tunayoyazungumza ni vizuri tuwe 'consistency' mdomoni na dhamira yetu, Rostam ni mchumi mzuri sana, tuzungumzie masuala ya uchumi wa nchi yetu, kuliko kujaribu kuwa mtoto mzawa badala ya kukubali 'status' ..Rostam na mimi ni watoto wa kambo." alimalizia Membe.


Share:

Serikali kuanzisha program maalum ya magonjwa yasiyoambukiza

Serikali iko mbioni kuanzisha program maalum ya magonjwa yasiyoambukiza kama ilivyo kwa magonjwa ya Ukimwi, TB na Marelia kwa kufikisha huduma ngazi ya zahanati.

Katika kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza wananchi wameshauriwa  kufanya mazoezi angalau mara tatu kwa wiki, kula mlo unaofaa, kutotumia tumbaku na pombe.

Hayo yameelezwa bungeni na Naibu waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile bungeni leo, Mei 17 wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mwantum Dau Haji (CCM).

Katika swali lake, Mwantum alitaka kujua serikali ina mpango gani kushughulikia magonjwa yasiyoambukiza kama vile, presha, kansa na kisukari.


Share:

Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Unaotokana Na Kisukari (Diabetic Nephropathy)

Ugonjwa wa kisukari (Diabetes Mellitus) huambatana na ongezeko la sukari(glucose) katika damu kwa kiwango kinachozidi kawaida. 

Homoni aina ya insulin ambayo hutolewa na kongosho ama hushindwa kufanya kazi yake vema kwa sababu ya kasoro za seli au hutolewa kwa kiasi kisicho kidhi uhitaji wa kuratibu sukari katika damu. 

Kwa hivyo sukari hubaki katika damu kwa wingi na kuleta madhara kadhaa.Wagonjwa wa kisukari pia huweza kuwa na kiwango kikubwa cha lehemu (cholesterol) katika damu. Na zaidi huweza kuwa na tatizo la mgandamizo wa damu (hypertension) au presha. Asilimia 55 ya wanaume wenye kisukari hupatwa na tatizo la nguvu za kiume.

Mambo haya matatu, Sukari, lehemu (Cholesterol) na Mgandamizo wa damu, Huweza kusababisha upungufu wa nguvu za kiume.(Erection dysfunction).

1. Sukari.
Sukari nyingi katika damu huweza kupelekea kuharibiwa kwa kuta za mishipa ya damu. Kisha kuta hizi hushindwa kuzalisha homoni aina ya Nitrogen Oxide ambayo husaidia kutanua mirija ya damu kwa ajili ya kupitisha damu kwa ufasaha. Ikitokea katika mirija ya damu inayotiririsha katika uume kushindwa kutanuka vema, ni wazi kuwa uume utapungua uimara wake.

2. Lehemu (Cholesterol).
Lehemu huganda kwenye kuta za mirija ya damu mithiri ya mafuta yanavyoganda katika chupa. Hali hii hupelekea kupungua kipenyo (diameter) cha mirija ya damu na kushindwa kupitisha damu vizuri.

3. Mgandamizo wa damu au Presha (Hypertension).
Katika hali hii moyo hushindwa kusukuma damu vizuri na hivyo kupungua kwa kasi na ujazo wa damu katika maeneo yaliopo mbali na moyo, ikiwa ni pamoja na viungo vya uzazi.

Pia, Mishipa ya fahamu (nerves) au Neva za fahamu huweza kuharibiwa na kupunguza ufanisi wake.Katika hali hii, maeneo yanayohudumiwa na neva hizo hupungua hisia na wakati mwengine kupata ganzi ya kudumu. Uume pia huweza kuathiriwa kwa namna hiyo.

 Kumbuka
Ili  mgonjwa  wa  kisukari  aweze  kupata  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, ni  lazima   apate  pia  tiba   itakayo  saidia  ku- control  sukari  kwenye  damu   yake.

Hivyo  basi ,  tiba  ya  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  inatakiwa  kwenda   sanjari  na  tiba  ya  ku - control  sukari  kwenye  damu  ya  mgonjwa.

Hii  ina  maana  kuwa,   ili  tiba  ya  nguvu  za  kiume  kwa  mgonjwa  wa  kisukari  iweze  kufanya  kazi  barabara, ni  lazima  mgonjwa  huyo, pamoja  na   kutumia  tiba  ya  nguvu  za  kiume , apate  pia  tiba  ya  sukari.


Kama unatatizo la Kisukari, lililosababisha upungukiwe nguvu za kiume basi wasiliana nami kwa ushauri zaidi. Simu:   0759208637 au 0620510598


Share:

Rais Magufuli Awataka Viongozi Anaowateua Washirikiane

Rais wa Tanzania John Magufuli amewataka viongozi wa kuteuliwa kuanzia ngazi ya ukuu wa mkoa mpaka ngazi za chini kujenga ushirikiano na uhusiano mzuri baina yao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao, vinginevyo hatasita kuchukua hatua.

Wito huo umetolewa kwa wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu tawala wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za wilaya, miji, manispaa na majiji.

Rais Magufuli ametoa maelekezo hayo jana Mei 16, 2019 katika kikao kazi kati yake na viongozi hao kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Amewaonya baadhi ya viongozi hao ambao wamekuwa na migogoro baina yao na hivyo kuathiri utendaji kazi na amesema endapo vitendo hivyo vitaendelea hatasita kuchukua hatua ikiwa ni pamoja kuwaondoa katika nyadhifa zao.



Share:

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036



Share:

Serikali kupitia upya mashamba yaliyofutwa na Rais Magufuli

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema wizara yake itapitia upya mashamba yote yaliyofutwa na Rais katika wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro.

Lukuvi amesema hayo tarehe 16 Mei 2019 katika kata ya Chanzulu tarafa ya Kimamba Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro alipokuwa akizungumza na wananchi wa kata hiyo ili kutatua mgogoro wa Ardhi katika wilaya hiyo ikiwa ni jitihada za wizara kumaliza migogoro ya ardhi nchini.

Waziri Lukuvi amesema, katika maeneo mbalimbali yapo mashamba yaliyofutwa na Rais lakini hayajawekewa utaratibu  wa kuyatumia na hivyo kutoa fursa kwa wajanja wachache kujigawia na mengine kuyauza kwa wananchi bila kufuata utaratibu.

Amesema katika kuhakikisha mashamba yote yaliyofutwa na Rais katika wilaya ya Kilosa na kuzua mgogoro baina ya wananchi na wamiliki, Wizara yake imeamua kupeleka timu kutoka wizarani kwa ajili ya kuyafanyia uhakiki mashamba yote yaliyofutwa katika wilaya ya Kilosa.

"Tutayapitia mashamba yote yaliyofutwa na Rais na kujua kilichomo ndani yake na timu ya uhakiki niliyokuja nayo itanilitea mapendekezo ya namna ya kutumia mashamba na mengine watapewa wanaostahili na si kila mtu atapewa", amesema Lukuvi

Mashamba yenye mgogoro na wananchi katika wilaya ya Kilosa ni Noble Agriculture Enterprises, Magereza dhidi ya wananchi wa Mabane, Mbigiri na Mabwegere, Chadulu Estate, Shamba la Swai dhidi ya wananchi wa Ilonga na shamba la Mauzi Estate Malangali.


Share:

MCHUNGAJI MSIGWA AHOJI UHALALI WA SPIKA NDUGAI KUMSIMAMISHA MASELE BUNGE LA AFRIKA


Makamu wa kwanza wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe.Stephen Masele akiwa ofisini kwake katika makao makuu ya Bunge la Afrika,Johannesburg nchini Afrika Kusini
***
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa amehoji nafasi ya wabunge wanaochaguliwa na Bunge kuwawakilisha katika mabunge mbalimbali duniani kusimamishwa na Spika bila uamuzi huo kujadiliwa na waliowachagua.

Akizungumza bungeni leo Ijumaa Mei 17, 2019 baada ya kuomba mwongozo kwa mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, mbunge huyo wa Iringa Mjini amesema uko wapi uhalali wa kiti cha spika kuwasimamishwa wawakilishi waliochaguliwa na chombo hicho cha kutunga sheria.

“Uhalali unatoka wapi na hawa hawakuteuliwa wamechaguliwa na nilitaka kujua anasimamishwa na kiti bila kujadili inatuchafua kama Taifa. Bunge litakuwa na nguvu gani ya kuwalinda hawa tunaowachagua,” amehoji Mchungaji Msigwa.

Ingawa Mchungaji Msigwa hakumtaja aliyekuwa akimlenga, lakini jana Alhamisi, Spika wa Bunge, Job Ndugai alitangaza kusimamisha uwakilishi wa mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele katika Bunge la PAP akimtuhumu kwa utovu wa nidhamu.

Ndugai alimtaka Masele ambaye ni makamu wa kwanza wa Rais wa PAP kuhojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na kamati ya maadili ya CCM.

Akijibu mwongozo huo, Chenge amemtaka Mchungaji Msigwa kutowahisha hoja kwa maelezo kuwa tayari jana Alhamisi, Spika Job Ndugai alilitolea uamuzi kwa kuomba wabunge wasubiri taarifa itakapowasilishwa bungeni watakuwa na nafasi ya kujadili kwani milango haijafungwa.

Na Ibrahim Yamola - Mwananchi 

Share:

Mchungaji Msigwa ahoji uhalali wa Spika Ndugai kumsimamisha Kuwasimamisha Uwakilishi wabunge wanaochaguliwa na Bunge kuwawakilisha katika mabunge mbalimbali

Mbunge wa Iringa Mjini, Mch. Peter Msigwa amehoji bungeni uhalali wa uamuzi wa Spika Job Ndugai kusimamisha uwakilishi wa Mbunge wa Shinyanga Mjini, Stephen Masele (CCM) katika Bunge la Afrika (PAP), bila Bunge la Tanzania kujadili

Jana Spika Job Ndugai alisema kuwa amemuandikia barua Rais wa PAP ya kusitisha uwakilishi wa Stehen Masele hadi Kamati ya Maadili itakapokamilisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake.
 

"Katika uwakilishi wa Bunge la Afrika kumetokea matatizo makubwa hasa kwa Mhe.Steven Masele matatizo ya kinidhamu,Tumelazimika kumrudisha nyumbani kuanzia Jumatatu, badala yake amekuwa akionyesha kugoma, ni kiongozi ambaye anafanya mambo ya hovyo hovyo". Alisema Ndugai.

“Uhalali unatoka wapi na hawa hawakuteuliwa wamechaguliwa na nilitaka kujua anasimamishwa na kiti bila kujadili inatuchafua kama Taifa. Bunge litakuwa na nguvu gani ya kuwalinda hawa tunaowachagua,” amehoji Mchungaji Msigwa.

Akijibu mwongozo huo, Chenge amemtaka Mchungaji Msigwa kutowahisha hoja kwa maelezo kuwa tayari jana Alhamisi, Spika Job Ndugai alilitolea uamuzi kwa kuomba wabunge wasubiri taarifa itakapowasilishwa bungeni watakuwa na nafasi ya kujadili kwani milango haijafungwa.


Share:

Picha : MKUTANO WA PILI WA BUNGE LA AFRIKA (PAP) WAFUNGWA

Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Tano wa Bunge la Afrika (Pan - African Parliament ulioanza Mei 6,2019 umefungwa leo Ijumaa Mei 17,2019 katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika,yaliyopo Midrand jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Kupitia mkutano huo Wabunge wa Bunge la Afrika walijadili masuala mbalimbali kuhusu bara la Afrika ambapo Kauli mbiu ya Bunge la Afrika mwaka huu ni "2019 mwaka wa Wakimbizi,wanaorejea nyumbani na wakimbizi wa ndani : Kuelekea kupata masuluhisho ya kudumu katika kulazimishwa kuhama makazi katika Afrika".
Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang akifunga mkutano wa bunge la Afrika leo Ijumaa Mei 17,2019 jijini Johannesburg,Afrika Kusini . Picha na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Rais wa PAP, Mhe. Roger Nkodo Dang akifunga mkutano wa bunge la Afrika. Kushoto ni Makamu wa Kwanza wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele (Tanzania) ,akifuatiwa na Makamu wa pili wa rais wa bunge la Afrika,Mhe. Haidara Aichata (Mali), Makamu wa tatu wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Bouras Djamel (Algeria) na Makamu wa nne wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe.Chief Charumbira (Zimbabwe).
Viongozi wa PAP wakiwa wamesimama wakati wa kuimba wimbo wa Umoja wa Afrika wakati wa kufunga mkutano wa bunge la Afrika leo Mei 17,2019. Katikati juu ni Rais wa PAP, Mhe. Roger Wa kwanza kushoto chini ni Makamu wa Kwanza wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele (Tanzania) ,akifuatiwa na Makamu wa pili wa rais wa bunge la Afrika,Mhe. Haidara Aichata (Mali), Makamu wa tatu wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Bouras Djamel (Algeria) na Makamu wa nne wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe.Chief Charumbira ( Zimbabwe).
Wabunge wakiimba wimbo wa Umoja wa Afrika.
Wabunge wakiwa ukumbini.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Share:

Serikali Yaanza mchakato wa kuanzisha BIma ya mazao

Serikali imeanza mchakato wa kuanzisha BIma ya mazao ili kuweza kukabiliana na changamoto za ukame, mafuriko, magonjwa na wadudu waharibifu.

Akiwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya Kilimo bungeni leo, Mei 17, waziri mwenye dhamana, Japheti Hasunga amelieleza Bunge kuwa mfumo huo utamwezesha mkulima kulipwa fidia pale anapopata hasara pamoja na kupata mkopo katika taasisi za fedha.

Amesema kwa kuanzia wizara imeanza kufanya vikao na wadau mbalimbali ili kufanya maandalizi ya awali kwa kuanza na maeneo machache.

“Maandalizi hayo yanaendelea kufanyika ili katika mwaka wa fedha 2019/2020 tuwe anglau na aina mbili za mifumo ya Bima ya mazao inayoweza kutumika nchini” alisema Waziri Hasunga.

Hata hivyo Hasunga alisema ili utaratibu huo uweze kufanikiwa kutahitajika takwimu sahihi za hali ya hewa pamoja na uzingatiaji wa kanuni bora za kilimo.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger