Thursday, 16 May 2019

Picha : SAVE THE CHILDREN,KIWOHEDE WAENDESHA TAMASHA LA MWANAUME JASIRI USHETU - KAHAMA



Mashirika yasiyo ya kiserikali mkoani Shinyanga Save The Children na KIWOHEDE, yameendesha Tamasha Mwanaume Jasiri la Kupinga Mila na Desturi kandamizi katika Kata ya Ulowa halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama, kwa lengo la kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.


Tamasha hilo limefanyika leo Mei 16, 2019 katika kijiji cha Kangeme Kata ya Ulowa, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Afisa Maendeleo Jamii wa halmashauri ya Ushetu Aminael John akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha.

Tamasha hilo liliambatana na kauli mbiu isemayo “Mwanaume Jasiri ana mlinda mtoto wa kike dhidi ya mimba na ndoa za utoton”.

Akizungumza kwenye Tamasha hilo mgeni rasmi Afisa Maendeleo wa halmashauri  ya Ushetu Aminael John, amewataka wanaume kuacha kuendekeza mila na desturi kandamizi zilizopitwa na wakati, ambazo zimekuwa zikichangia kuendelea kuwepo kwa tatizo la mimba na ndoa za utotoni.

Amesema wanaume wanatakiwa kubadilika na kutambua umuhimu wa elimu, kwa kumlinda mtoto wa kike dhidi ya matukio hayo ya kupewa ujauzito na kuolewa ndoa za utotoni, ili waweze kutimiza malengo yao na kuja kuwasaidia hapo baadae.

“Natoa wito kwa wanaume wa kata hii ya Ulowa na Ushetu kwa ujumla, acheni kuendekeza mila na desturi kandamizi ambazo zimekuwa zikiwanyima haki watoto wa kike kuweza kutimiza malengo yao, na kuishia kupewa ujauzito ama kuolewa ndoa za utotoni na kuacha shule,”amesema John.

“Tambueni kuwa mtoto anapopata elimu ataweza kuja kuwa kiongozi mkubwa hapa nchini au kupata ajira yake nzuri, ambapo atawasaidia katika maisha yenu kuliko hata hao ng’ombe mnawategemea na kuona wa thamani sana, na kuamua kuwaozesha ndoa hizo za utotoni kwa tamaa ya kupata mifugo,”ameongeza.

Naye Mtendaji wa kata ya Ulowa Geofrey Philip, ametaja takwimu za wanafunzi ambao walikatishwa masomo mwaka jana (2018) kwa sababu ya kupewa ujauzito kuwa walikuwa 10, ambapo kwa mwaka huu (2019) tayari wameshapewa mimba wanafunzi wawili.

Aidha Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Save The Children mkoa wa Shinyanga Alex Enock, amesema wameanzisha mradi huo katika kata nane za halmashauri hiyo ya Ushetu, kwa lengo la kutokomeza mila na desturi kandamizi, ambazo zimekuwa kikwazo katika kumaliza tatizo la mimba na ndoa za utotoni.

Amezitaja kata hizo kuwa ni Ulowa, Ushetu, Ukune, Kisuke, Uyogo,Kimampula, Bulungwa, na Ulewe, kwa kutoa elimu mbalimbali ambazo zinahusu malezi bora kwa watoto, kwa kushiriki wazazi wa pande zote mbili baba na mama na siyo kumwachia mzazi mmoja, likiwamo pia na suala la kutokomeza mila na desturi kandamizi.

Kwa upande wake, Mratibu wa mradi huo wa kupinga mila na desturi kandamizi kutoka Shirika la KIWOHEDE Victor Reveta, ambao ndiyo wanatekeleza mradi huo kwenye kata nane za halmashauri ya Ushetu, amesema ulianza mwaka 2017 na unatarajiwa kukoma mwaka huu 2019, ambapo pia wamewajengea uwezo wanaume 25 kwa ajili ya kuendelea kutoa elimu kwa wanaume wenzao dhidi ya kutokomeza tamaduni hizo ambazo zimeshapitwa na wakati.

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Afisa Maendeleo wa halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama Aminael John akizungumza kwenye Tamasha la Mwanaume Jasiri la Kupinga Mila na Desturi Kandamizi ambazo zimekuwa zikichangia mimba na ndoa za utotoni kuendelea kuwepo kwenye kata ya Ulowa na kuwaasa wanaume waachane na mila hizo. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Afisa maendeleo wa halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama Aminael John, akielezea madhara ya mimba na ndoa za utotoni kuwa athari zake kuwa ni ongezeko la vifo vitokanavyo na uzazi, kuugua fistula, pamoja na magonjwa mengine ya ikiwa via vyao vya uzazi vinakuwa bado havijakomaa.

Kaimu Mkurugenzi kutoka shirika la Save The Children mkoani Shinyanga Alex Enock akielezea malengo ya mradi huo wa kutokomeza mila na desturi kandamizi kwenye halmashauri hiyo ya Ushetu wilayani Kahama, kuwa ni kutokomeza tatizo la mimba na ndoa za utotoni.

Mratibu wa Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi kutoka Shirika la KIWOHEDE wilayani Kahama Victor Reveta akielezea namna wanavyoutekeleza mradi huo katika halmashauri ya Ushetu katika kata nane, kuwa ni utoaji wa elimu wa kupinga mila hizo, elimu ya malezi pamoja na kuunda vikundi vya Wanaume Jasiri ambao watakuwa mabalozi wa kutoa elimu ya kutokomeza mila kwa wanaume wenzao.

Mtendaji wa kata ya Ulowa Geofrey Philip, akitaja takwimu za wanafunzi ambao walikatishwa masomo mwaka jana sababu ya kupewa ujauzito walikuwa 10, ambapo kwa mwaka huu (2019) tayari wameshapewa mimba wanafunzi wawili.

Askari wa dawati la Jinsia Rhoda Athony akiwataka wananchi wa Kata hiyo ya Ulowa pamoja na wanafunzi pale wanapokuwa wakifanyiwa matukio ya ukatili wawe wanatoa taarifa mapema kwenye dawati hilo ili matatizo yao yapate kushughulikiwa mapema na kuweza kupata haki zao.

Lenard Mboje akisoma risala kwa niaba ya Wanaume Jasiri 25 ambao wamejengewa uwezo wa kutoa elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi kwa wanaume wenzao ,amebainisha kuwa kwa sasa kumeibuka mbinu mpya ya kuozesha wanafunzi ndoa za utotoni kwa kuweka ma Bibi harusi bandia ambao wemetimiza umri wa miaka 18, lakini kumbe muolewaji ni chini ya umri huo.

Wananchi wakiendelea kusikiliza nasaha mbalimbali kutoka kwa viongozi juu ya kupinga mila na desturi kandamizi, ambazo zimekuwa zikisababisha kuendelea kuwepo kwa mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni na kuweza kutimiza ndoto za mtoto wa kike kielimu.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni na kuweza kutimiza ndoto za mtoto wa kike kielimu.

Wananchi wakiendelea kusikiliza nasaha mbalimbali kutoka kwa viongozi juu ya kupinga mila na desturi kandamizi, ambazo zimekuwa zikisababisha kuendelea kuwepo kwa mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza nasaha mbalimbali kutoka kwa viongozi juu ya kupinga mila na desturi kandamizi, ambazo zimekuwa zikisababisha kuendelea kuwepo kwa mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni na kuweza kutimiza ndoto za mtoto wa kike kielimu.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.

Wananchi wakiendelea kusikiliza elimu ya kupinga mila na desturi Kandamizi, ili kumuokoa mtoto wa kike kielimu kwa kutokomeza tatizo la mimba na ndoa za utotoni.

Burudani ya uvutaji kamba ikitolewa kwenye tamasha hilo la mwanaume jasiri la kupinga mila na desturi kandamizi ili kutokomeza tatizo la mimba na ndoa za utotoni.

Burudani ikiendelea kutolewa kwenye Tamasha hilo kwa kukimbia mbio za kwenye magunia.

Burudani ya kukimbia mbio na mayayi nayo ikitolewa kwenye Tamasha hilo la Mwanaume Jasiri katika kata ya Ulowa.

Mchezo wa kukimbiza kuku nao ulikuwepo ambao washindi walipewa zawadi zao.

Mchezo wa kukimbiza kuku ukiendelea.


Mshindi wa kufukuza kuku Valentina John akiondoka na kuku wake.


Mshindi wa kufukuza kuku Matongo Kani akiondoka na kuku wake.

Wasanii nao walikuwepo kwenye Tamasha hilo la Mwanaume Jasiri la kupinga mila na desrturi Kandamizi, ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.


Wasanii wakiendelea kutoa burudani kwenye Tamasha hilo la Mwanaume Jasiri la kupinga mila na desrturi Kandamizi, ili kutokomeza mimba na ndoa za utotoni.

Washindi walioshiriki michezo mbalimbali kwenye Tamasha hilo la Mwanaume Jasiri wakiondoka na zawadi zao.

Washindi walioshiriki michezo mbalimbali kwenye Tamasha hilo la Mwanaume Jasiri wakiondoka na zawadi zao.

Mshindi wa kukimbia na mayayi akipokea zawadi zake.

Baadhi ya wanaume Jasiri ambao wamejengewa uwezo wa kuwa mabalozi wazuri wa kutoa elimu ya kupinga mila na desturi kandamizi kwa wanaume wenzao.

Afisa Maendeleo ya jamii wa halmashauri ya Ushetu akipanda mti katika ofisi ya kijiji cha Kangeme kaya ya Ulowa halmashauri hiyo kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Kahama Anamringi Macha.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:

STAND UNITED YATEMBEZA KICHAPO KWA WABABE WA SIMBA SC

Wababe wa Simba msimu huu, Kagera Sugar ambao waliifunga Simba nje ndani na kuwa timu ya kwanza kubeba pointi sita leo wamepoteza mchezo wao mbele ya Stand United kwa kufungwa mabao 3-1 mchezo uliochezwa uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Stand United walianza kucheka na nyavu mapema dakika ya 3 kipindi cha kwanza kupitia kwa Charles Chinonso kabla ya mshambuliaji machachari wa Kagera Sugar, Kassim Khamis kusawazisha bao hilo dakika ya 45.

Kipindi cha pili Jacob Masawe dakika ya 48 alipachika bao la pili kabla ya bao la tatu la ushindi kupachikwa dakika ya 90 na Datius Peter lililoipa pointi tatu timu yake ya Stand United.
Share:

MENEJA WA WAKALA WA VIPIMO (WMA) BANDARINI AELEZEA UMUHIMU WA KUPIMA MAFUTA KATIKA HATUA MBALIMBALI


Bw. Peter Chuwa Meneja Wakala wa Vipimo (WMA) Bandarini akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi za (WMA) zilizopo kwenye Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) Barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam leo wakati akifafanua masuala mbalimbali yanayohusu vipimo vya mafuta kwenye Meli Kwenye Matanki ya kuhifadhia na kwenye maroli yanayosafirisha nishati hiyo hapa nchini na nchi mbalimbali. 

Bw. Peter Chuwa amesema kuna umuhimu mkubwa sana kupima mafuta katika hatua yoyote ile iwe kwenye meli , kwenye matanki na hata kwenye maroli yanayosafirisha ili walaji waweze kupata ujazo ulio sahihi kabisa na wauzaji pia wauze kwa viwango na vipimo vinavyostahili na vilivyothibitishwa.

Mei 20 mwaka 1875 makampuni kadhaa huko ufaransa yalikutana na kujadili kuhusu vipimo hivyo ambapo yalikipitisha kipimo cha ujazo wa mita baada ya hapo tarehe ya Mei 20 kila mwaka iliteuliwa kuwa siku ya vipimo na imekuwa ikiadhimishwa duniani kote, Siku ya Jumatatu Mei 20,2019 ya wiki ijayo maadhimisho hayo yatafanyika jijini Dar es salaam.
Peter Chuwa Meneja Wakala wa Vipimo (WMA) Bandarini akifafanua mambo mbalimbali wakati akizungumza na 
waandishi wa habari leo katika ofisi (WMA) zilizopo Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) Barabara ya Nyerere jijini Dar es salaam leo kuhusu vipimo vya mafuta kwenye Meli 
Kwenye Matanki ya kuhifadhia na kwenye maroli yanayosafirisha nishati  hiyo hapa nchini na nchi mbalimbali. 
Mjasiriamali na Mbunifu wa mashine mbalimbali za kutengenezea sabuni Bw. George Butafwe akifafanua jambo kwa waandishi wa habari waliotembelea katika karakana yake iliyopo (SIDO) jijini Dar es salaam kuhusu vipimo sahihi katika kila kitu unachokifanya, Butafwe amesema vipimo ndiyo kila kitu kwani hata wabunifu kama yeye hawawezi kubuni mashine bila vipimo "Lazima ujue kwamba mashine hii naitengeneza itazalisha sabuni katoni ngapi kwa siku, Nitatumia Mawese kiasi gani labda malighafi nyingine kiasi fulani kwa hiyo vipimo ndiyo kila kitu". 
Mjasiriamali na Mbunifu wa mashine mbalimbali za kutengenezea sabuni  Bw. George Butafwe akifafanua jambo kwa waandishi wa habari waliotembelea katika karakana yake iliyopo (SIDO) jijini Dar es salaam akiielezea mashine ya kutengenezea sabuni aliyoibuni mbele ya waandishi wa habari. 
Mjasiriamali na Mbunifu wa mashine mbalimbali za kutengenezea sabuni  Bw. George Butafwe akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari wa TBC wakati wanahabari hao walipotembelea katika karakana yake iliyopo (SIDO) jijini Dar es salaam leo.
Afisa Vipimo II, Joram Joshua akiwa melini kwa ajili ya kupima ujazo wa mafuta Bandalini kabla hayajaanza kushushwa kwenye meli.

Share:

WAKULIMA KISARAWE WAANZA KUPATA MAFUNZO YA KILIMO MKATABA


Afisa wa Shirika la The Winamwanga Cultural Heritage Association (TWCHA), Veronica Kilango, akisoma risala mbele ya Afisa Mtendaji Kata ya Mzenga, Godfrey Ambelle kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe jana, wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya kilimo cha mkataba na ufugaji kwa vikundi 27 vilivyopo katika Tarafa ya Mzenga.
Wawakilishi wa wakulima ambao ni viongozi wa vikundi wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Uzinduzi ukiendelea.
Mratibu wa Mradi wa Shirika la The Winamwanga Cultural Heritage Association (TWCHA), Saidi Simkonda, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya kilimo cha mkataba na ufugaji kwa vikundi 27 vilivyopo katika Tarafa ya Mzenga vyenye wanachama 850 wilayani Kisarawe mkoani Pwani jana. Kushoto ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Mzenga, Godfrey Ambelle na Diwani wa Kata hiyo, Mohammed Rubondo.
Afisa wa Shirika la The Winamwanga Cultural Heritage Association (TWCHA), Veronica Kilango (kulia), akimkabidhi risala, Afisa Mtendaji Kata ya Mzenga, Godfrey Ambelle kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe jana, wakati wa hafla ya uzinduzi wa mafunzo ya kilimo cha mkataba na ufugaji kwa vikundi 27 vilivyopo katika Tarafa ya Mzenga.
Afisa Ustawi wa Jamii Kata ya Mzenga, Agness Msanya akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Mwalimu Willbroad Rosper kutoka Taasisi ya Family Hope Foundation Tanzania (FAHOT), akiwa pamoja na Afisa Kilimo, Fatuma Kipingu katika hafla hiyo.
Afisa Mtendaji Kata ya Mzenga, Godfrey Ambelle kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, akizungumza.
Diwani wa Kata ya Mzenga, Mohammed Rubondo akizungumza.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya hiyo, ambaye ni Afisa Tarafa ya Mzenga, Mulael Angelo akizungumza.
Afisa Ugani kutoka Kampuni ya Kilimo Joint, Joel Nchimbi akizungumza.
Mkulima wa Kata hiyo, Salum Kiame, akichangia jambo kwenye uzinduzi huo.

Na Dotto Mwaibale, Kisarawe

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na Shirika la The Winamwanga Cultural Heritage Association wameanza kutoa mafunzo ya kilimo cha mkataba na ufugaji kwa vikundi 27 vilivyopo katika Tarafa ya Mzenga vyenye wanachama 850.

Mafunzo hayo ya mwezi mmoja ambayo yameanza jana yatafanyika katika Kituo cha Agricuture Resouce Center kilichopo Kata ya Mzenga ambayo yatawakutanisha wadau wa kilimo wa wilaya hiyo wakiwemo wawakilishi wa vikundi vya wakulima, watengenezaji na wasambazaji wa pembejeo za kilimo, Taasisi za kifedha pamoja na wanunuzi wakubwa wa mazao.

Akizungumza juzi wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo Mratibu wa Mradi wa shirika hilo, Saidi Simkonda alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wakulima wa kujua mbinu za kukabiliana na changamoto mbalimbali zitokanazo na kilimo ili kufanya kilimo chenye tija.

Simkonda aliongeza kuwa pamoja na mambo mengine Bodi ya shirika hilo ilikaa na kuona ni bora kuwa na leseni ya biashara ili shirika liweze kuanza kununua mazao ya wakulima wake kwa wakati ili kufanya kilimo cha mkataba kiwe cha moja kwa moja ambapo Halmashauri ya wilaya hiyo imetoa leseni ya biashara kwa shirika hilo yenye namba B.2874206.

Mratibu huyo alitaja mafanikio waliyopata katika kufanikisha kilimo hicho cha mkataba kuwa ni kupata ardhi yenye ekari 50 toka Serikali ya Kijiji cha Gwata kwa ajili ya kuwekeza kiwanda cha kusindika nafaka na kutoa unga wa mahindi chenye uwezo wa kusindika tani 20 kwa masaa 24 kupitia mtambo wenye thamani ya kiasi cha shilingi milioni mia moja na kumi na mbili za kitanzania kutoka Kampuni ya Shijia Nhuang Hongdefa Machinery Comp Ltd ya Nchini China.

Afisa Mtendaji Kata ya Mzenga, Godfrey Ambelle akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa wilaya hiyo ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo, alisema elimu watakayoipata ndiyo itakayopelekea kuwatoa katika dimbwi la umaskini kupitia kilimo hicho cha mkataba na kuwa kinachohitajika ni soko la uhakika wa mazao ya wakulima.

Share:

MBUNGE AOMBA KURA KWA KUTUMIA VIDEO TOVUTI YA VIDEO ZA NGONO


Joachim B. Olsen.
Mbunge mmoja nchini Denmark Joachim B. Olsen ameamua kuweka tangazo la kampeni yake ya kuchaguliwa tena kuwa Mbunge nchini humo kwenye tovuti ya video za ngono.


Mbunge huyo alipoulizwa kwanini amefanya hivyo, akasema ni lazima uwafuate wapiga kura kila sehemu walipo jambo ambalo liliwaacha watu wengi katika hali ya mshangao.

"Ndiyo, mimi ambaye nimeweka lile tangazo lakini hakuna kingine kinachoendelea zaidi ya kuwafuata wapiga kura wangu popote walipo najua wengine limewafurahisha na wengine litawaachia maswali, lakini ni namna tu ya utafutaji kura katika uchaguzi ujao", amesema Olsen.

Joachim B. Olsen, mwenye umri wa miaka 41 kitendo chake hicho kimeungwa mkono na baadhi ya wabunge wa chama cha Liberal Alliance, ambao wamedai kuwa aina hiyo ya utafutaji wa kura, itamsaidia kupigiwa kura kwa wingi katika uchaguzi wa Juni, 2019.
Share:

CUHAS: Diploma application 2019/20- Now open!!

INVITATION FOR ADMISSION INTO DIPLOMA IN MEDICAL LABORATORY SCIENCES, PHARMACEUTICAL SCIENCES AND DIAGNOSTIC RADIOGRAPHY PROGRAMMES FOR THE
ACADEMIC YEAR 2019/20

The Catholic University of Health and Allied Sciences is pleased to invite applications from qualified
candidates who completed either form IV or form VI wishing to pursue studies in Diploma in: (i). Medical
Laboratory Sciences, (ii). Pharmaceutical Sciences and (iii). Diagnostic Radiography at the Catholic University
of Health and Allied Sciences for the academic year 2019/20.

1. DIPLOMA PROGRAM IN:
i. Pharmaceutical Sciences
ii. Medical Laboratory Sciences and
iii. Diagnostic Radiography.
2. DURATION: Three (3) years.
3. ENTRANCE QUALIFICATIONS:

(I) DIPLOMA IN PHARMACEUTICAL SCIENCES (DPS)
The entry qualification for this programme shall be holders of Certificate of Secondary
Education (CSEE) with four passes including “C” pass in Chemistry and Biology; and “D” pass
in Physics/Engineering Sciences and any other subject. Pass in Mathematics and English will
be an added advantage.

(II) DIPLOMA IN MEDICAL LABORATORY SCIENCES (DMLS)
The entry qualification for this programme shall be holders of Certificate of Secondary
Education (CSEE) with five passes including “C” pass in Chemistry and Biology; and “D” passes
in Physics/Engineering Sciences, Mathematics and English.
(III) DIPLOMA IN DIAGNOSTIC RADIOGRAPHY (DDR)
The entry qualification for this programme shall be holders of Certificate of Secondary
Education (CSEE) with four passes including “C” pass in Physics/Engineering Sciences,
Biology; and Chemistry and “D” pass in any other subject. Pass in Mathematics and English will
be an added advantage.

4. INSTRUCTIONS TO APPLICANTS:
a) All application will be done through Online Student Information Management System (OSIM).
CLICK HERE TO APPLY

b) Applicants must ascertain themselves that they possess the minimum entrance qualifications
before they pay for application fees as the fees will not be refunded under any
circumstances.
 Online Application is available in our web page. (www.bugando.ac.tz)
 Deadline for receiving application is strictly at 3.00pm on 30th August, 2019

The post CUHAS: Diploma application 2019/20- Now open!! appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RAIS WA PAP AKUTWA NA KESI YA KUJIBU TUHUMA ZA UNYANYASAJI WA KINGONO, UMOJA WA AFRIKA KUCHUKUA HATUA


Mheshimiwa Stephen Masele akiandika dondoo muhimu wa wakati wa kikao cha bunge la Afrika leo,Midrand,Johannesburg nchini Afrika Kusini.


Hatimaye Kamati Maalumu iliyoundwa na Wabunge wa Bunge la Afrika (Pan- African Parliament – PAP) imetoa ripoti ya uchunguzi dhidi ya Rais wa Bunge hilo,Mhe. Roger Nkodo Dang.

Nkodo anatuhumiwa kwa unyanyasi wa kingono kwa watumishi wa kike walioko Makao Makuu ya PAP,matumizi mabaya ya madaraka, upendeleo dani ya bunge hilo na unyanyasaji kwa watumishi wa ofisi hiyo hali iliyosababisha kuwepo kwa mgomo wa watumishi wiki iliyopita.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Maalumu  ya Uchunguzi,Jaji mstaafu wa mahakamani kuu ya kenya Mh Stewart Madzayo ametoa ripoti hiyo leo jioni katika kikao cha bunge kikiongozwa na Makamu wa nne wa rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Chief Charumbira.

Ripoti ya kamati hiyo imeonesha kuwa Rais wa PAP, Nkodo Dang amekutwa na kesi ya kujibu na hivyo wabunge wa wameazimia kuikabidhi Umoja wa Mataifa (AU) kwa ajili ya uchunguzi wa kina(forensic investigation)ambapo Rias huyo ametakiwa apishe ili uchunguzi uweze kufanyika.

Akizungumza na waandishi wa habari,baada ya kutoka kwenye kikao cha bunge ambacho waandishi wa habari hawakuruhusiwa,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele amesema Kamati hiyo imefanya kazi nzuri.

“Kwanza Nimefurahi kwamba Kamati Maalumu iliyoundwa na Bunge kuchunguza tuhuma dhidi ya rais wa PAP anazotuhumiwa imefanya kazi vizuri”,

“Na mimi kama mkuu wa Utawala wa Bunge la Afrika na wafanyakazi wote wa PAP, nina wajibu wa kuhakikisha kwamba haki za wafanyakazi hususani wanawake ambao wanamtuhumu rais kwa kuwanyanyasa kingono zinalindwa”,amesema Masele.

 “Utafiti wa Kamati umethibitisha kuwa alifanya hivyo na yeye mwenyewe amekiri kuwa alifanya na ameomba msamaha,Bunge limeazimia asimamishwe kupisha Umoja wa Afrika ufanye uchunguzi wa kina”.



Share:

Breaking News !! RAIS MAGUFULI ATUMBUA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI



Share:

Marekani yazionya nchi za Ulaya kuhusu mkakati wao wa kutoishirikisha Marekani katika ulinzi

Moja ya hitilafu kuu baina ya Marekani na nchi za Ulaya wakati huu wa urais wa Donald Trump huko Marekani, ni misimamo ya kukinzana ya pande mbili kuhusu siasa na miundo ya ulinzi ya Ulaya na nafasi ya shirika la kijeshi la nchi za Magharibi, NATO.

Suala hilo limepelekea nchi za Ulaya kuangalia upya siasa zao za kiulinzi na kufikiria kuwa na ulinzi huru wa bara Ulaya usioihitajia Marekani. 

Hata hivyo serikali ya Trump haifurahishwi hata kidogo na jambo hilo. Kama kawaida yake, Trump anatumia lugha ya vitisho hata kwa waitifaki wakuu wa Marekani yaani nchi za Ulaya na kuzionya kuwa Washington itachukua hatua kali dhidi yao iwapo zitaamua kutekeleza mipango yao huru ya kiulinzi na kisilaha na kuiweka pembeni Marekani. 

Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon imetishia kuwa, iwapo Umoja wa Ulaya utaendelea kutekeleza kivyake-vyake mipango yake ya ulinzi, Washington itazichukulia hatua nchi hizo. 

Hii ina maana ya kwamba Marekani inaweza kutumia masuala ya kibiashara na kisiasa kukabiliana na nchi za Ulaya iwapo zitaendelea kuchukua misimamo ya kujitegemea katika mambo yao ya kiulinzi bila ya kuishirikisha nchi ya nje ya Umoja wa Ulaya kama Marekani.

Ellen Lord, naibu waziri wa ulinzi wa Marekani, mwanzoni mwa mwezi huu wa Mei 2019 alimuandikia barua Federica Mogherini, Mkuu wa Siasa za Kigeni na Kiusalama wa Umoja wa Ulaya na kulalamikia siasa huru za umoja huo za kujitegemea katika sekta ya ulinzi na silaha. 

Barua hiyo ilizitishia nchi za Ulaya kuwa Washington itazichukulia hatua iwapo zitaendelea na mipango yake ya kiulinzi isiyoishirikisha Marekani. 

Katika barua hiyo, Ellen Lord aliandika: Umoja wa Ulaya umetekeleza kivyake-vyake mipango yake ya kiulinzi na kisilaha, suala ambalo linatishia ushirikiano wa kijeshi wa Marekani na Ulaya na ni kinyume na makubaliano ya NATO.

Naibu huyo wa waziri wa ulinzi wa Marekani amesisitiza kuwa, kama Washington itajibu siasa hizo za Umoja wa Ulaya, basi majibu hayo hayatokuwa na mambo mazuri kwa washirika wa Washington huko Ulaya. 

Lord alidai kwenye barua yake hiyo kwamba: Sisi (Marekani) hatutaki tufike mahala tuchukue maamuzi kama hayo katika siku za usoni kwani uamuzi huo utakwenda sambamba na hasara ya mamilioni ya dola kwa mashirika ya kutengeneza silaha ya barani Ulaya.

Marekani imetoa vitisho hivyo katika hali ambayo tarehe 18 aprili 2019, Bunge la Ulaya lilipasisha mpango wa kuanzishwa mfuko maalumu wa kiulinzi wa Ulaya wenye thamani ya Euro bilioni 13 kwa ajili ya mwaka 2021 hadi 2027. Zaidi ya hayo, Washington inapinga masharti jumla yaliyoainishwa katika mpango wa ushirikiano wa kudumu unaojulikana kwa jina la PESCO. 

Kwa mujibu wa mpango huo, nchi 25 za Ulaya zimepanua miradi yao 34 ya silaha. Kinachoichukiza Marekani ni kwamba mpango huo wa PESCO unahusiana tu na Umoja wa Ulaya na kwamba nchi nyingine yoyote iliyoko nje ya eneo la umoja huo haiwezi kuwa na udhibiti wa silaha zinazozalishwa na kusafirishwa nje chini ya mpango huo. 

Miradi iliyoko chini ya mpango wa PESCO pia imeitia woga Marekani kwani mradi wowote ule lazima upate ridhaa ya nchi zote za Umoja wa Ulaya, sasa Washington ina hofu kwamba veto ya nchi moja tu ya Ulaya inaweza kukwamisha ushirikiano wake wa kijeshi na nchi yoyote ile ya Umoja wa Ulaya.

Juhudi za kuwa na kikosi huru cha kijeshi cha Ulaya, kuandaliwa mkakati wa kimataifa wa Umoja wa Ulaya na pia kuanzisha taasisi za kijeshi na kiusalama zinazohusiana na Ulaya tu ni kampeni ambayo imepata nguvu sana katika kipindi cha miaka minne iliyopita. 

Ujerumaini na Ufaransa ambazo ni miongoni mwa nchi muhimu zaidi za umoja wa Ulaya zina nafasi kubwa katika juhudi za kufanikisha jambo hilo na zinataka Umoja wa Ulaya uweze kujitegemea haraka sana kiulinzi. 

Lakini kama tulivyosema, Marekani haifurahishwi hata kidogo na jambo hilo. Katikati ya mwaka 2018, Donald Trump alimlaumu vikali Rais Nicolas Macron wa Ufaransa kwa kampeni yake ya kutaka bara la Ulaya liwe na jeshi lake huru la kujitegemea. 

Trump aliandika katika ukurasa wake wa Twitter kwamba: Macron amependekeza bara la Ulaya liwe na jeshi lake maalumu kwa ajili ya kujilinda mbele ya Marekani, China na Russia. Jambo hilo ni udhalilishaji mkubwa.

Hata hivyo inaonekana wazi kuwa Umoja wa Ulaya umekusudia kikweli-kweli kukabiliana na Marekani na NATO na kuhakikisha kuwa bara hilo linakuwa na uhuru wa kijeshi na kiulinzi haraka iwezekanavyo.


Share:

Video Mpya : Ice Boy - Kama Unajikuna

Msanii wa muziki Bongoi, Ice Boy anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake uitwao Kama Unajikuna.


Share:

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.



Share:

Tanzania Kufikia Asilimia 70 Ya Kuondoa Uhaba Wa Watumishi Katika Sekta Ya Afya

Na.WAMJW,Dodoma
Tanzania imeazimia kufikia asilimia sabini kutoka arobaini na nane ya uhaba wa watoa huduma za afya kwa nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika ifikapo mwaka 2022.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akifungua kikao cha kujadili changamoto za rasilimali watu katika sekta ya afya kati ya viongozi kutoka Wizara ya Afya, Tamisemi pamoja na washirika wa maendeleo nchini.

Waziri Ummy amesema lengo la kikao hicho ni kujadili changamoto mbalimbali zinazohusu rasilimali watu ikiwemo ya upungufu wa watumishi, ajira, mafunzo pamoja na mahitaji ya watumishi kuanzia ngazi za zahanati hadi hospitali za wilaya nchini.

Amesema upungufu huo umetokana na ongezeko la miundombinu ambayo imewekwa na serikali ya awamu ya tano licha ya kazi kubwa iliyofanyika ya kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba.

”ingawa bado ipo changamoto ya rasilimali watu katika sehemu za kutoa huduma za afya nchini ambapo pengo ni takribani asilimia 52 kwa kila watumishi wa afya mia moja tunawahitaji watumishi arobaini na mbili”. Amesisitiza Waziri Ummy.

Aidha, etaja sababu nyingine ya upungufu wa watumishi wa sekta ya afya kuwa ni pamoja na ongezeko la magonjwa yasiyo ya kuambukiza hivyo inahitajika watoa huduma wa afya wengi katika kuwahudumia wananchi wenye matatizo hayo.

Hata hivyo Waziri Ummy amesema kikao hicho kitaweka mikakati ya pamoja na ya ubunifu ya kuona kunakuwa na maboresho ya uzalishaji wa wataalam wa afya na wale wanaozalishwa ni kiasi gani wanaweza kuajiriwa na kuwekwa kwenye utumishi wa umma hususan kwenye ngazi ya zahanati na hospitali za wilaya.

“Tutaweka ubunifu ambao utawawezesha mfano wauguzi kupatiwa mafunzo ya kutoa dawa za usingizi na hii ni kuona wanao uwezo wa kufanya kazi nyingine tofauti, kwa ujumla sekta ya afya nchini inaenda vizuri na nina amini kwa pamoja tunaweza kutatua uhaba wa watumishi katika sekta ya afya.


Share:

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036



Share:

JWTZ Watumia Ndege Ya ATCL Kusafirisha Wapiganaji Kuishiriki Ulinzi Wa Amani Darfur

Na Luteni Selemani Semunyu
Maafisa na Askari wa jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanaoshiriki Ulinzi wa Amani katika  Jimbo la Darfur nchini Sudan kwa Mara ya kwanza  kwa kipindi cha Miaka 10 ya Ulinzi wa Amani Jimboni humo wametumia Ndege ya Shirika la Ndege ya  Serikali ya ATCL ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Mhe Rais wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu katika  kulifanya Shirika hilo linapiga hatua zaidi kwa maslahi ya Shirika na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita wa JWTZ Meja Jenerali Alfred Kapinga amesema Jeshi ni Taasisi inayoongozwa na Uzalendo,uadilifu, uhodari  hivyo ni faraja kubwa kwa Jeshi  na wapiganaji kuunga mkono jitihada za Serikali katika Kuboresha Uchumi  ikiwa ni  sehemu ya mchango wao katika kuonesha  uzalendo kwa vitendo kwa  kutumia vitu vya nyumbani kwa maslahi mapana ya Taifa.

“ Tumekuwa tukitumia Ndege zetu za Jeshi lakini tumekuwa tukitumia Ndege za mataifa mengine kwa Mikataba kutoka Umoja wa Mataifa lakini sasa ni faraja kwani tumefanikiwa kuwashawishi Umoja wa Mataifa kutumia Ndege zetu” Alisema Meja Jenerali Kapinga.

Aidha,Meja Jenerali kapinga alisema   mbali na kutumia Ndege hiyo lakini aliwaasa Maafisa na Askari hao kuhakikisha wanapeperusha vema Bendera ya Nchi na kuendelea kuitangaza kwa  sifa nzuri za Utendaji Kimataifa.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Ndege la la Tanzania (ATCL),  Mhandisi Ladislaus Matindi  Alisema ni Fursa Nzuri kwa ATCL na wanalishukuru Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kupitia kwa mkuu wa majeshi ya Ulinzi  kwa Mchango mkubwa   kufanikisha kupata tenda hiyo.

“ Namshukuru Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo na watendaji wake kwa Uzalendo wake na kuhakikisha anafanikisha ATCL kupata fursa kwa mara ya kwanza na hii itakuwa mwanzo mzuri na tutahakikisha tunaitumia vizuri  fursa hii kujitangaza zaidi Kimataifa kwa maslahi  ya Nchi “ Alisema Mhandisi Matindi.

Vilevile  Mhandisi Matindi aliongeza kuwa Ndege ya Dream Liner ina uwezo wa kusafiri kwa saa 12 bila kusimama, hivyo kwa  kutumia saa tatu kusafiri kutoka hapa mpaka nchini Sudan  ni sehemu ndogo ya Uwezo wake na ni nafasi ya kuwajaribisha watendaji wa Ndege wa ATCL katika kuhudumia safari Ndefu.

Naye Kamanda wa Kikosi cha TANZBATT- 13,  Luteni Kanali Khalfan Kayage  anayekwenda na  Kikosi hicho  alisema kuwa  inawapa nguvu kupeperusha Bendera yetu kupitia Ndege na ameahidi kufanya kazi kwa Bidii kuendeleza jina na sifa nzuri ya Tanzania Kimataifa.


Share:

Upelelezi kesi ya kina Maimu haujakamilika

Upande wa Jamhuri kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA), Dickson Maimu na wenzake, umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa kesi inayowakabili vigogo hao haujakamilika.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo  ni Meneja Biashara wa (Nida), Avelin Momburi, Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Brokers,  Astery Ndege, Ofisa Usafirishaji, George Ntalima, Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond na Xavery Kayombo.

Wakili wa Serikali, Janeth Magoho, alieleza hayo juzi mbele ya Hakimu Mkazi Augustina Mmbando  wakati kesi hiyo ilipokuwa inatajwa na kuiomba Mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hata hivyo, Hakimu Mmbando aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 28, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa tena.

Maimu na wenzake wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi pamoja na kuisabishia Serikali hasara ya Sh bilioni 1.175.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 100 kati ya hayo, 24 yakiwa ni ya utakatishaji fedha zaidi ya Sh bilioni 1.1,   23 ya kughushi nyaraka; 43 ni kiwasilisha nyaraka za uongo  kumdanganya mwajiri wao  na kuisababishia mamlaka hiyo hasara.


Share:

Kisena Na Mke Wake Wakamatwa Tena na Kufunguliwa Kesi ya Uhujumu Uchumi

Mkurugenzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam (Udart), Robert Kisena na mkewe,  Frorencia Mshauri Membe pamoja na wenzao watatu wameunganishwa katika kesi ya uhujumu uchumi wakikabiliwa na mashtaka 19 likiwamo la kuisababisha hasara ya Sh2.4bilioni kampuni ya Udart.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Kulwa Kisena (33), Charles Newe (47) na Chen Shi (32).

Watano hao  waliunganishwa pamoja katika kesi hiyo jana Jumatano Mei 15, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustine Rwizile na wakili wa Serikali, Grolia Mwenda.

Hatua hiyo ilikuja ikiwa ni muda mfupi baada ya  washtakiwa hao waliokuwa wakikabiliwa na kesi mbili tofauti kufutiwa mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na Rwizile.

Uamuzi wa kuwafutia mashata ya awali ulitokana na upande wa  mashtaka kuomba chini ya kifungu cha 91 (1) cha mwenendo wa Makosa ya jinai (CPA) sura 20 iliyofanyiwa marejeo 2002 kwa maelezo kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)  hana nia ya kuendelea a kesi hizo, mahakama kuridhia.

Hata hivyo, waliendelea kushikiliwa na baadaye kusomewa kesi mpya ya uhujumu uchumi wakikabiliwa na mashtaka 19 ikiwa ni pamoja na kuongoza genge la uhalifu, kujenga kituo cha mafuta bila kibali cha Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), kuuza mafuta kwenye makazi yasiyoruhusiwa eneo la maegesho ya magari.

Mengine ni utakatishaji fedha, mashtaka manne ya kutoa nyaraka za uongo, mashtaka manne ya kughushi, mawili kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kusababisha hasara.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, washitakiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kuahirishwa hadi Mei 28, 2019.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger