Thursday, 16 May 2019

Tanzania yapongezwa kwa ukuaji mzuri wa Uchumi




Share:

Kampuni Ya Infinix Na TIGO Yaleta Mapinduzi Ya Selfie Kupitia Infinix S4 Yenye 32mp.


Kampuni ya simu ya Infinix inayozalisha simu zenye teknolojia ya hali ya juu, imezindua simu mpya aina ya Infinix S4 yenye megapixel 32 AI selfie kwajili ya kuwawezesha watanzania kufikia ndoto zao kupitia matumizi ya teknolojia. Na kwa ushirikiano wa TIGO na Infinix, Infinix S4 itapatikana katika maduka ya Infinix na TIGO ikiwa na ofa ya bundle la miezi sita.   

Infinix na Tigo zimeungana katika uzinduzi wa Infinix S4 kuhakikisha wateja na Watanzania kwa ujumla wanaingia katika mapinduzi ya simu zenye selfie bora, ambayo sio tu itainua ujuzi na maarifa ya selfie lakini pia itasaidia kuwasogeza katika ulimwengu wa kidigitali. 
 
Akizungumza wakati wa uzinduzi Mkurugezi mtendaji wa kampuni ya simu ya Infinix Bwana. Hauson Tu,alisema kwamba, “Uwezeshaji kupitia teknolojia ya simu unategemeana na uhakika wa sifa ya simu kama vile kamera ya nyuma, mwonekano mzuri wa screen ya simu, uwezo wa betri na kasi ya simu yenyewe. Kwa kulizingatia hilo Infinix S4 imeundwa ikiwa na kamera tatu za nyuma 13MP+8MP+2MP with a 6.2’ waterdrop display screen kwaajili ya picha bora. Kamera hizi tatu zenye kufanya kazi tatu tofauti ikiwemo kuhakikisha picha inaonekana kwa kina zaidi, hata kwa umbali wa 120ยบ”. 
 
Bwana Tu, “alisisitiza kuhusu umuhimu wa Betri yenye nguvu inayodumu na chaji zaidi akisema, “Infinix haijawahi kuwaangusha wateja wake katika suala la betri. S4 ina Smart power management system kwaajili ya kuzuia matumizi ya chaji kwa application ambazo hazitumiki kwa muda huo na betri hutumika pale tu ambapo application hiyo itakuwa katika matumizi”. 
 
Na kwa upande wake afisa mahusiano wa kampuni ya Tigo Bwana Tarik Boudiaf alisema “Kasi ya mtandao ni muhimu sana katika kumwezesha Mtanzania, ikiwa ni lengo mojawapo kwa kampuni ya Tigo kuhakikisha wateja na Watanzania kwa ujumla wanahamia katika ulimwengu wa kidigitali kama kampuni tumetoa ofa ya bundle la internet la muda wa miezi sita”. 
 
Kampuni ya simu ya Infinix imekuwa ikiwalenga zaidi vijana na watu wenye ushawishi katika maendeleo ya teknolojia, hii imepelekea uzinduzi wa Infinix S4 kuhudhuriwa na wasanii maaruufu kama Lulu Diva, Mimi Mars, Bi Dozen pamoja na vyombo vya habari maarufu. Infinix S4 kwa sasa inapatikana katika maduka yote ya Infinix na TIGO Nchini kote.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya May 16




Share:

Wednesday, 15 May 2019

Video Mpya ya Kisukuma : KISIMA - LIMI.....KALI BALAA


Hii hapa ngoma nyingine kali na matata ya Msanii wa Nyimbo za asili Kisima  inaitwa Limi... Ngoma  kali balaa mtu wangu..
Itazame hapa chini

Share:

SERIKALI YAGAWA BURE KONDOMU KIBAO KWENYE MAENEO YA STAREHE...MAKAHABA WAFURIKA

Maafisa wa afya kaunti ya Narok  nchini Kenya wamesambaza zaidi ya masanduku 4,000 ya mipira ya kondomu huku mamia ya makahaba wakifurika mjini Narok.

 Kulingana na afisa mkurugenzi mkuu wa afya Sereti Mpeti, serikali ya kaunti imegawa kondomu hizo bila malipo katika maeneo ya burudani na kwenye migahawa.

" Hii ni njia moja ya kuzuai kuenezwa kwa magonjwa ya zinaa kwani kaunti hii inatarajia watu mbali mbali kutoka sehemu kadhaa za nchi kufuatia sherehe ya Madaraka ambazo zitafanyika kaunti hii Jumamosi Juni 1," Ms Sereti alisema. 

Sereti pia aliwatahadharisha wakazi dhidi ya kushiriki ngono bila kinga akisisitiza hatari za maambukizi ya magonjwa ya zinaa. 

Imekisiwa kuwa idadi ya wafanya biashara wa ngono itaongezeka kaunti hiyo wakati wa sherehe za Madaraka ambazo zinatarajiwa kufanyika Jumamosi, Juni 1.

Aidha, kamishna mkuu wa kaunti ya Narok George Natembeya amewahakikishia wakazi usalama wa kutosha wakati wa sherehe hizo. 
Via Tuko
Share:

Video : TAZAMA HAPA NGOMA YA WAZULU WA AFRIKA KUSINI

Tazama Ngoma ya Wazulu wa Afrika Kusini hapa chini
Share:

Video Mpya : MAGODI ZE DON - UMAARUFU SI KITU


Hii hapa ngoma mpya ya msanii Magodi Ze Don inaitwa Umaarufu si kitu, itazame hapa
Share:

Video Mpya ya Asili : CHAMA MASUNGA - MACHIYA


Hii hapa video mpya ya Chama Masunga inaitwa Machiya,Itazame hapa chini
Share:

IUCEA-WORLD-BANK-MASTERS-SCHOLARSHIPS 2019

The Inter-University Council for East Africa (IUCEA) in partnership with the World Bank invites applicants to apply for the IUCEA-World Bank Masters Fellowships for 2019. To encourage the participation of young African female students at postgraduate level and to promote regional female student mobility, the fully funded fellowships are only open to females. To be eligible one must obtain an admission from an Africa Center of Excellence (ACE) outside of one’s own country of current nationality to study full-time in any of the priority disciplines of the ACE II Project: (i) STEM (Science, Technology, Engineering and Mathematics) or Industry (ii) Agriculture (iii) Health (iv) Education and (v) Applied Statistics. For more details on how to apply>>Read details below/ Download Application form

BACKGROUND

The World Bank is partnering with eight Governments in Eastern and Southern Africa in an innovative project with the aim of improving the quality of training and research in higher education and reducing the skill gaps in key development priority areas. The Eastern and Southern Africa Higher Education Centers of Excellence (ACE II) Project supports the governments of Ethiopia, Kenya, Malawi, Mozambique, Rwanda, Tanzania, Uganda, and Zambia in strengthening selected African Centers of Excellence (ACEs) to deliver quality post-graduate education and build collaborative research capacity in the following priority areas: (i) Industry, (ii) Agriculture, (iii) Health, (iv) Education, and (v) Applied Statistics.The ACE II Project implements three components, namely (i) strengthening the 24 higher education institutions into regional ACEs in Eastern and Southern Africa in a set of defined regional priority areas (US$ 140 million); (ii) providing capacity building support to these ACEs through regional activities (US$3 million); and (iii) supporting coordination and management of the implementation of components (i) and (ii) (US$5 million).

 As Regional Facilitation Unit (RFU) for the ACE II Project, the Inter-University Council for East Africa (IUCEA) leads the implementation of key elements of Component 2 of the project, aimed at building strong and sustainable regional partnerships and collaborations to produce competent Masters and PhD holders for the regional market and improve quality of teaching in higher education, and the quality of production and services in public and private sectors. To encourage the participation of young African female students at postgraduate level, IUCEA wishes to implement a Fellowship Program aimed at providing competitive Masters Scholarships to academically deserving future talents to promote regional female student mobility. Eligible female applicants who can demonstrate interest and ability in the priority areas are encouraged to apply for the 30 Fellowships available for the 2019/2020 academic year.

 ELIGIBILITY CRITERIA

                In order to be eligible for this Fellowship, the applicant must:

  1. i)be a female national of one of ACE II participating countries (Ethiopia, Kenya, Malawi, Mozambique, Rwanda, Tanzania, Uganda, and Zambia) or Burundi
  2. ii)    be under the age of thirty-five (35) years

iii)    be a holder of a Bachelor’s Degree from a reputable university in the relevant field, at the level of Upper Second Class Honours

  1. iv)have obtained admission from an ACE outside one’s own country of current nationality to study full-time in any of the priority disciplines of the ACE II Project: (i) STEM (Science, Technology, Engineering and Mathematics) orIndustry, (ii) Agriculture, (iii) Health, (iv) Education, and (v) Applied Statistics; and
  2. v)have demonstrated outstanding academic achievement as evidenced by academic transcripts, and academic awards, if any.

 ELIGIBLE SECTORS/DISCIPLINES

The Fellowship Program will provide support in the following broad areas of activities:

  1. i) In general, Eastern and Southern African countries experience low and, in some cases, declining levels of enrolment in areas associated with the growing industrial sectors which require skills in Science, Technology, Engineering and Mathematics or Industry – STEM. Thus, there is a huge demand for graduates in emerging sectors with high growth potential such as oil and gas, energy, extractives, and railways industries across the region. This Fellowship will contribute to improved availability of skilled professionals with specialized knowledge who can innovate and boost productivity in the STEM areas, such as engineers (civil, petroleum, and mechanical), geoscientists, mechanical technicians, etc.
  2. ii) Agriculture:Low levels of agricultural productivity has contributed to the shortage of food and overall food insecurity due to skills and labor constraints, as well as the slow adoption of technology. Primarily this low productivity is caused by factors such as frequent droughts, rampant diseases (crop and livestock), unimproved crop varieties, lack of access to quality seeds/fertilizers, and poor management of water resources. To address these challenges, this Fellowship will contribute to training of female graduates to become agribusiness specialists/managers, crop scientists, plant breeders, veterinarians, agronomists, water and irrigation engineers, and food preservation and processing specialists, who will contribute to innovative research and teaching for agricultural advancement, improved nutrition, and agricultural sustainability.

 iii)    Health: There is low life expectancy in Eastern and Southern African region. Both infectious and non-infectious diseases account for the highest proportion of illness in the region and include malaria and tuberculosis and other diseases that may have been eliminated elsewhere. Infectious diseases are also a major constraint to both the export of African livestock and the spread of diseases from animals to humans. This Fellowship will address development challenges in the areas of infectious diseases, public health, and drug development through training and research in molecular biology, analytical epidemiology, traditional medicine, and pharma-biotechnology.

  1. iv) Poor education quality, especially at the primary and secondary levels, is a significant obstacle to higher education access and outcomes. Poor teaching competencies, particularly in mathematics and science, are a barrier to the production of high-quality graduates and faculty in the field. This Fellowship will contribute to improved quality of tertiary education, leading to improved learning outcomes in the STEM disciplines.
  2. v) Applied Statistics. The absence of reliable and accurate data, data management systems, and skilled statisticians is a serious constraint to policymaking, adequate analysis of development challenges, and monitoring and evaluation (M&E) of interventions. In sub-Saharan African countries, across various sectors, there is a severe shortage of highly trained statisticians and of good quality data. This makes it difficult to provide analyses, plan and monitor interventions, inform fact-based policy, and track progress. This Fellowship will contribute to the capacity of research and training within higher education, with a focus on providing improved statistical skills.

Detailed information about eligible sectors and Universities/ACEs offering postgraduate training in the above-listed priority areas may be obtained from https://ace2.iucea.org

THE FELLOWSHIP AWARD

The provided financial support for each Fellowship Program will cover:

  1. i) University tuition fees: Approximately USD 3,000 per year (payable directly to the Host University according to an official invoice)
  2. ii)Stipend: USD 800 per month to support living expenses such as housing, food, utilities, local transportation, medication and settlement expenses

iii)    Research: USD 4,800 to support student research, payable upon approval of the research proposal

  1. iv)Allowance: USD 2,000 one-off allowance to cover visa, laptop, and books
  2. v)Air ticket: A round-trip economy fare for the most direct route between the beneficiary’s home country and the study destination of Host University

 NoteCandidates must complete all academic work within 24 months and the scholarship will not be extended beyond this period.

 

APPLICATION PROCESS AND PROCEDURES

 To apply for this Fellowship, interested candidates are advised to fill in the application form found at ace2.iucea.org  orwww.iucea.org attach all requested documents, and send by e-mail to exsec@iucea.org with a copy to ace2rfu@iucea.org.All applications must be received not later than 5.00 PM East African Time on June 30, 2019. For proof of eligibility, an applicant should ensure that the following is provided:

  1. i) Completed application form;
  2. ii)Recent passport-size photograph;

iii)          Summarized CV with names and contacts of two referees;

  1. iv)Certified copies of academic certificates and transcripts;
  2. v)Certified copies of passport or national identity card indicating citizenship;
  3. vi)Copy of admission letter from one of the host universities (please refer to the attached table on Countries, ACEs, and Universities); and

vii)        Two (2) reference letters with contact details.

The post IUCEA-WORLD-BANK-MASTERS-SCHOLARSHIPS 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

APPLY NOW: UDOM INNOVATION CHALLENGE-2019

CALL FOR PAPERS THE UNIVERSITY OF DODOMA INVITES RESEARCHERS TO SUBMIT PAPERS AND INNOVATIONS FOR INTERNATIONAL CONFERENCE WHICH WILL BE HELD ON NOVEMBER 7TH TO 8TH, 2019

About the Challenge
The University of Dodoma (UDOM) invites all UDOM community members to participate in the first
Innovation Challenge which is coordinated by UDOISIC. The challenge will support innovative ideas
from all fields which are environmental friendly, simple technology, commercially viable, sustainable
and bring solutions to societal problems. It will involve four stages which are innovative ideas
submission, screening, pitching and lastly the development of the prototypes. Winners of the Challenge
will be mentored and provided with some financial support to develop their prototypes.
Objective of the Challenge
The challenge aims at giving UDOM community a platform to engage in producing creative and
innovative ideas which might be solutions to some of the societal problems. Furthermore, it aims to
support the vision of the fifth government of attaining to middle economy through industrialization.
Evaluation Criteria
All submitted ideas will undergo screening to get viable ideas which will be invited for the pitching
stage. Evaluation criteria is detailed below:
i. Addressing any of SDG (1,2 5 and 9)
ii. Appropriate technology,
iii. Commercial viability,
iv. Environmental friendly,
v. Sustainability and
vi. Scalability
Eligible Applicants
All UDOM students and/or academic staff individually or in groups are eligible to apply.
Application Period
Application window closes on 31st of May, 2019.
Mode of application
Applicants can fill in the application form online by clicking here

Contacts
All inquiries may be directed to UDOISIC heads through 0755 498 126 and 0784 891 291 during work
hours.

The post APPLY NOW: UDOM INNOVATION CHALLENGE-2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

CALL FOR UDOM INNOVATION CHALLENGE, 2019

Share:

AAP African Futures Program – Call For Early Career Researchers

The Alliance for African Partnership (AAP) will establish its African Futures Research Leadership Program in Fall 2019. The competitive visiting scholar program will target early career female researchers from the eight AAP member institutions to be jointly supervised by faculty members from MSU and their home institution in research for impact, writing of scholarly and/or policy publications, dissemination of research results and grant proposals.

Early career researchers will also participate in a structured academic advancement program while building bridges and lasting connections with MSU and across their cohort.

They will also participate in the Future Africa Research Leadership Program at the University of Pretoria, which will provide them with training in the areas of thought leadership, team development, research development, engagement and collaboration, while building south-south collaboration with other African researchers.

The home insitution mentor will visit MSU for one week of collaboration discussions. Towards the end of the program, MSU faculty mentors will spend one week at the early career researcher’s home institution to continue research collaboration with the researcher and their African co-mentor.

For more information  click here

The post AAP African Futures Program – Call For Early Career Researchers appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

UDSM: Scholarship And Admission Into The Masters Degree In Intellectual Property (MIP) Programme

UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM SCHOOL OF LAW ANNOUNCEMENT FOR SCHOLARSHIP AND ADMISSION INTO THE MASTERS DEGREE IN INTELLECTUAL PROPERTY (MIP) PROGRAMME

Applications are invited from suitably qualified candidates for admission into the Masters Degree in Intellectual Property (MIP) Programme. The Degree is jointly offered by the University of Dar es Salaam (UDSM) in Dar es Salaam, Tanzania, and the African Regional Intellectual Property Organization (ARIPO), the World Intellectual Property Organization (WIPO), and the Business Registration and Licensing Agency (BRELA) – Intellectual Property Office of Tanzania.Click here for the summary of the programme.For more information see the attachment

 Attachment20190505_092221_UDSM_ANNOUNCEMENT FOR SCHOLARSHIP AND ADMISSION INTO THE MASTERS DEGREE IN INTELLECTUAL PROPERTY (MIP) PROGRAMME.pdf

The post UDSM: Scholarship And Admission Into The Masters Degree In Intellectual Property (MIP) Programme appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

SUA: BATCH 9 LOAN ALLOCATIONS FOR SUA STUDENTS WHO SECURED SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB, MAY 2019

Share:

RAIS MAGUFULI NA USHINDI WA KULINDA RASILIMALI ZA MADINI


Na Judith Mhina -Maelezo
Adhima ya Tanzania kuwa kinara uuzaji wa dhahabu Afrika Mashariki na kuzuia utoroshaji ya madini yake imetimia.

Hii imetokana na kutekelezwa kwa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli katika kuratibu na kutambua madini yote, kuanzishwa kwa masoko ya ununuzi ya dhahabu ndani na uuzwaji wa madini nje ya nchi.

Kuzinduliwa kwa soko kuu la kimataifa la uuzaji wa madini ya dhahabu Mkoa wa Mwanza, lililopo katika jengo la Rock City Mall, kumedhihirisha nia ya Tanzania kuhakikisha inalinda rasilimali za madini ya Tanzania. Hii inawahakikishia wachimbaji wadogo kunufaika na kazi yao, pamoja kuchangia pato la Taifa.

Akiongoza utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli mapema mwezi Machi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa alizindua mnada wa dhahabu katika Mkoa wa Geita, yenye masoko mawili, ili kuondoa changamoto ya wachimbaji wadogo kuhangaika kutafuta mahali pa kuuzia madini yao.

Baadhi ya Mikoa iliyotekeleza agizo la ujenzi vituo vya kuuzia dhahabu ni pampja na Geita, Mwanza, Shinyanga, Chunya (Mbeya) Mpanda, (Katavi), Mara, Arusha, Singida, Iringa, Mkinga (Tanga) na Manyara ambao wanajenga vituo viwili vya kuuzia madini ya Tanzanite na vito vingine.

Aidha, ujenzi huo utajengwa katika miji midogo ya Mererani maalum kwa ajili ya uuzwaji wa madini ya Tanzanite na vito, wakati soko la pilli linajengwa mji mdogo wa Orkesumet kwa ajili ya uuzwaji wa ruby, green tourmaline na vito vingine.

Jitihada za Rais Magufuli za kulinda na kupigania rasilimali za Watanzania zimemfanya Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Museveni kutuma ujumbe ulioongozwa na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Peter Crolies, kukiri kuwa uwekezaji nchini Tanzania katika sekta ya madini ni mfano wa kuigwa na nchi nyingine za Afrika.

Waziri Crories amesema hayo katika ziara ya siku nne mkoani Mwanza na Geita ambapo lengo ni kujifunza, jinsi Tanzania inavyoendesha sekta ya madini na kufanikiwa kuwa na uhusiano mzuri baina ya serikali, wachimbaji wadogo na wakubwa kwa kudumisha amani.

“Tanzania na Uganda zitaendelea kushirikiana katika Nyanja za kitekinolojia na taarifa za kiolojia Tumekuja hapa kujifunza jinsi ya usimamizi wa rasilimali ya madini ili nasi kupata ujuzi kutoka TZ ambao tutakwenda kufikisha jatika serikali yetu na kuwafundisha wananchi wetu wanaojihusisha na uchimbaji” Amesema Waziri Clories.

Amesema ziara hiyo imekuwa na mafanikio kwao kwa kuwa hajawahi kushuhudia na kujifunza rasilimali za madini zinavyotakiwa kuendeshwa na kutunzwa hadi kufikia hatua ya jamii na serikali wa kupata uchumi mzuri.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri wa Madini Stansilaus Nyongo amesema wachimbaji wadogo ndio watoroshaji wakubwa wa madini hususan dhahabu lakini Tanzania imejipanga kuthibiti na kupunguza namna ya utoroshwaji wa huo kwa kuanzisha masoko hayo ya kuuzia madini.

Watanzania wamekuwa na utamaduni au desturi ya kudharau na kubeza jambo lolote jema linaloanzishwa hapa nchini na kupenda kusifia na kuona mambo yanayofanyika nje ya Tanzania ndio mema tu. Waswahili husema “Mdharau kwao ni mtumwa”.

Lakini ubora wa Tanzania umethibitishwa na Waganda walioona ni vizuri kuja kujifunza kuhusu madini kutokana na nchi yetu kutunza vizuri rasilimali za madini hasa kwa wachimbaji wadogo. Ambapo imekuwa vigumu kwa nchi nyingine kufanya kazi kwa ushirikiano na kudumisha amani. Amesema Waziri Nyongo.

Ujumbe wa Uganda ulikuwa na maafisa waandamizi wa serikali pamoja na wachimbaji wadogo 35 ulitembelea maeneo yanayochibwa dhahabu katika migodi ya Geita Gold Mine- GGM Rwangwa Busonwa Mine, Msagano na maeneo ya kuchengulia dhahabu ya Rich Hill na Genge tatu.

Zoezi hili la uazishwaji wa vituo vya kuuzia madini ni utekelezaji wa maagizo kadhaa ya Rais Magufuli ambapo, itarahisisha serikali kuratibu wanunuzi wa madini na wanunuzi hao kujulikana wanapoyauza madini hayo, ndani na nje ya nchi, na kutambua kiasi cha fedha nchi ilizopata kutokana na mauzo hayo.

Aidha, kurejeshwa kwa utaratibu wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania-BOT, kuhusika na ununuaji na uuzaji wa dhahabu, iliyochenguliwa nje ya nchi na kuratibu mapato yatokanayo na uuzwaji wa dhahabu na madini mengine ambayo yanapatikana hapa nchini Tanzania. Itadhihirisha dhahiri kama nchi tunaongoza katika uuzaji wa dhahabu Afrika Mashariki.

Kulingana na taarifa ya mwezi April ya BOT kuna ongezeko la uuzwaji wa dhahabu nje ya nchi. Ongezeko hilo lililotokana na ulinzi na uangalizi sahihi wa uuzwaji wa madini ambapo watoroshaji walikuwa na mwanya wa kuiba katika migodi na kutorosha nje ya Tanzania.

Umakini wa serikali wa Awamu ya Tano umaezaa matunda katika migodi miwili mikubwa hapa Tanzannia ukiwemo Geita Gold Mining na North Mara Gold Mining baada ya kuzalisha kiasi kikubwa zaidi cha madini hayo na kuuzwa nje ya nchi .

Ongezeko hilo ni la Dolla za Marekani milioni 100 kuanzia Julai 2018, mpaka kuishia Machi 2019 ambapo ni sawa na fedha za Tanzania Bilioni 223. Ongezeko hilo ni la fedha za Marekeni ni sawa na bilioni 1.68 ikilinganishwa na mwaka 2018 mwezi Machi.

Pia, Mkoa wa Geita kilo 198 za dhahabu zimeuzwa kwa kipindi cha mwezi mmoja tangu soko hilo limeanzishwa tarehe 22 Machi mpaka April 2019. Vilevile Mkoa wa Mbeya Wilaya ya Chunya ndani ya siku nne tangu soko kuanzishwa, kilo 22 zimeuzwa wakati hapo nyuma zilirekosiwa kuuzwa kilo 12 tu kwa mwaka mzima.

Ongezeko hili la dhahabu kuuzwa nje ya nchi, imesababisha kukuza pato la bidhaa na huduma zitolewazo na nchi ya Tanzania zilizotolewa kuishia Machi 2019 kufikia Dola za marakani Milioni 8.5 kutoka milioni 8.4 dola za marekani kwa mwezi Machi 2018.

Soko la dhahabu la Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya lilofunguliwa tarehe 05 Mei 2019 na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila akifungua soko hilo amesema “ Serikali imejipanga kuhakikisha soko a madini linatatua changamoto kubwa zinazowakabili wadau wa sekta ya madini”

Ameongeza kwa kusema “Kwa kuanzia serikali imeanzisha soko la pamoja la madini ambalo litatoa fursa kuanzia mchimbaji mdogo mpaka mkubwa na kuuza dhahabu yake sambamba na kuwatafutia wanunuzi”

Aidha, wafanyabiashara wa Chunya waliomba serikali kuwahakikishia usalama wa mali zao –madini na fedha zao katika soko hilo lililofunguliwa mjini Chunya, lakini bado wana wasiwasi kuhusu usalama wao. Hivyo ni vema serikali kuimarisha ulinzi na usalama kwenye eneo la soko na kwenye migodi.

Pia wanaipongeza serikali kwa kuweka soko la pamoja la madini ambalo litatoa nafasi kila mfanyabiashara wa dhahabu kuwa kwenye ushindani wa bidhaa yake.

Akitoa kasoro kadhaa zilizokuwepo kwenye sheria ya madini ya mwaka 2007 na kanuni zake Rais Magufuli aliagiza kufanya marekebisho ya sheria ambayo yalifanyika mwaka 2018 na kuagiza kurekebisha kanuni zake wakati wa Mkutano Mkuu na Wadau wa Sekta ya Madini mapema Januari 2019.

Marekebisho hayo yalihusu utaratibu wa uchimbaji wa dhahabu ikiwemo kuweka kumbukumbu ya dhahabu inayopatikana na mauzo yake, na kusaidia kupata takwimiu sahihi. Vilevile kujua ukweli katika Afrika Mashariki nchi ipi inayoongoza kwa uuzwaji wa dhahabu na madini mengine.

Maagizo hayo ya Rais Magufuli yalitolewa wakati wa mkutano wa wadau wa madini uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere-JNCC uliofanyika kuanzia tarehe 22 Januari mpaka 24, Januari 2019 Jijini Dar-es-salaam.

Hata hivyo, zipo changamoto mbalimbali za madini ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi kwa kutoa elimu ya kutosha kwa wadau ili serikali iweze kufanya kazi kwa pamoja na wananchi – wachimbaji wadogo wadogo na migodi mikubwa ya wawekezaji.

Mfano hivi karibuni Wilaya ya Gairo Mkoa wa Morogoro wachimbaji wa madini kadhaa na mmliiliki wa madini wamewakimbia viongozi ambao ni Mwenyekiti wa Tume ya Madini Profesa Idris Kikula ambaye alifatana na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Seriel Mchembe na Kamishina wa Tume ya Madini Dkt. Athanas Machiyeke.

Wadau hao waliacha madini aina ya Ruby, Nut, pikipiki na vitendea kazi baada ya kuona wanamiliki madini hayo kinyume cha sheria bila kuwa na kubali cha kumiliki. Hii ni uthibitisho kuwa sekta ya madini bado inahitaji ushirikishaji wa karibu wa wadau ili wajue wajibu wao wa kufata sheria, taratibu, kanuni na miongozo ya sekta husika.


Share:

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA

Shahidi wa tatu, katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wenzake nane, Koplo Rahim amedai baadhi ya waandamanaji walivaa mzula hawakuonekana nyuso zao.

Amedai walikuwa wanarusha mawe na jiwe moja lilimpiga shingoni akapoteza fahamu na hakujua mahali ambako silaha yake aina ya SMG ilipo.

Koplo Rahim amesema hayo leo asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akiongozwa na Wakili wa Serikali, Simon Wankyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thoma Simba.

Amedai wanachama wa Chadema wakiongozwa na viongozi wao waliandamana kutoka viwanja vya buibui kuelekea kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni wakiwa na mawe, chupa za maji na baadhi walivaa mzula hawakuonekana nyuso zao.

Waandamamaji walizuia kuandamana lakini walikaidi ndipo ilipotolewa amri ya kuwapiga mabomu ya machozi ili wasiendelee.

“Moshi wa mabomu ya machozi ulikuwa unarudishwa na upepo upande ambao tulikuwepo askari, moshi ulirudi kwetu, nilipigwa jiwe nikapoteza fahamu, nikipelekwa Polisi Kilwa Road kwa matibabu, nililazwa hapo, nilipopata fahamu nikakumbuka sina silaha, sijui nani alinipiga jiwe.

“Alikuja afande Ndelengi hospitali nikamuuliza kuhusu silaha yangu, akaniambia alichukua mwenzangu iko Oystebay, ilirudishwa ikiwa na silaha zake.

Mbali na Mbowe, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya uchochezi ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika, mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk Vincent Mashinji na Mchungaji Peter Msigwa.

Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari mosi na 16, mwaka 2018, Dar es Salaam.


Share:

Bilioni 19 Zatengwa kwa ajili ya kulipa fidia za maeneo yaliyotwaliwa na jeshi.

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa imepokea jumla ya Sh19 bilioni kwa ajili ya kulipa fidia za maeneo yaliyotwaliwa na jeshi.

Hata hivyo, ni Sh3 bilioni ndizo zilizolipwa hadi sasa huku Sh16 bilioni zikisubiri uhakiki ili kukamilisha malipo hayo kwa ardhi ya wananchi.

Akijibu swali bungeni leo Jumatano Mei 15, 2019, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussen Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuwalipa wananchi fidia katika maeneo ambayo yalichukukiwa kwa shughuli za Jeshi.

Kauli ya Dk Mwinyi imekuja ikiwa ni siku chache tangu msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) alipotangaza wananchi wote wanaoishi katika maeneo ya Jeshi kuhama haraka vinginevyo wataondolewa kwa nguvu.

Mbunge wa Mtambile (CUF) Masoud AbdallaH Salim amehoji Serikali ina mpango gani wa haraka wa kulipa fidia kwa wananchi waliochukuliwa maeneo yao na Jeshi.

"Ni kweli yapo maeneo yaliyotwaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya ulinzi wa mipaka lakini baadhi ya maeneo yamelipwa fidia na mengine bado mchakato unaendelea," amesema Mwinyi.

Waziri Mwinyi amesema mpango wa Serikali ni kuendelea kulipa fidia kwa maeneo husika na mwaka 2018/19 wizara ilitenga Sh20.9 bilioni kwa ajili ya kulipa fidia hiyo lakini zilizotolewa ni Sh19 bilioni.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger