Wednesday, 15 May 2019

Watumishi Wa Umma Watakiwa Kufanya Kazi Kwa Kuzingatia Maadili Ya Utumishi Na Kujiepusha Na Rushwa.

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Watumishi wa Umma kote nchini wametakiwa  kuzingatia maadili ya utumishi wa Umma na kujiepusha na masuala ya rushwa na utovu wa nidhamu kazini 

Rai hiyo imetolewa  Mei 14,2019  jijini Dodoma na Naibu katibu mkuu Utumishi, Bw.Francis Michael katika ufunguzi wa  mkutano Mkuu wa Mwaka wa Baraza la wafanyakazi wa ofisi ya Taifa ya Ukaguzi hesabu za Serikali C.A.G. 

Bw.Michael amesema kuna baadhi ya watumishi wa Umma wamekuwa wakikiuka maadili ya kazi na taaluma zao na kujikita wakiwa watovu wa nidhamu na kujikita kwenye masuala ambayo yako kinyume na utaratibu wa kazi hivyo ni vyema kwa kila mfanyakazi akazingatia maadili ya kazi zake. 

Hata hivyo,Bw.Francis ameipongeza ofisi ya ukaguzi wa hesabu za serikali ,C.A.G ikiongozwa na  kiongozi wake Mahiri Profesa Musa Assad kwa kuendelea kutoa ripoti  ya ukaguzi kwa wakati kila mwaka bila upendeleo wowote katika kusukuma gurudumu la Maendeleo kwa  kuelekea  Uchumi wa kati wa Tanzania ya  viwanda. 

Kuhusu changamoto zinazoikabili ofisi ya Mkaguzi wa Hesabu za serikali C.A.G hususan upungufu wa wafanyakazi Bw.Francis amesema ofisi yake ipo tayari kutatua tatizo hilo ambapo ameitaka ofisi ya C.A.G kufanya mchakato wa kuorodhesha idadi husika ya upungufu huo. 

Katibu wa TUGHE Taifa Heri Mkunda amezungumzia juu ya Ushirikishwaji wa wafanyakazi  katika bajeti ili kujenga dhana ya utawala bora . 

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi ofisi ya Taifa ya ukaguzi C.A.G Prof.Musa Assad  amesema ofisi yake ina watumishi 957  huku kukiwa na upungufu wa watumishi zaidi ya hamsini  kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu,kufariki au kuhamishwa taasisi nyingine.

Kaulimbiu ya mkutano  mkuu wa mwaka wa Baraza la Wafanyakazi  ya ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ni Ukaguzi Shirikishi ,Uwazi na Uwajibikaji ni nguzo muhimu katika kufikia uchumi wa kati.


Share:

Taarifa kwa umma kuhusu Nafasi za Kazi na Masomo

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi za kazi na masomo zilizotangazwa na jumuiya za kimataifa kama ifuatavyo:

        i.        Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola;

Afisa Msaidizi wa Programu katika Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini (Assistant Program Officer-Monitoring and Evaluation Unit na

Meneja wa Utafiti–Uchumi, Vijana na Maendeleo Endelevu (Research Manager–Economic, Youth and Sustainable Development.

Maelezo kamili kuhusu nafasi hizi yanapatikana katika tovuti: http://thecommonwealth.org/jobs.  Mwisho wa kuwasilisha maombi ni tarehe 23 Mei 2019.

Aidha, Jumuiya ya Madola imetangaza nafasi za ufadhili wa masomo kwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo katika ngazi ya shahada ya uzamili (masters degree). Mwisho wa kuwasilisha maombi ya nafasi hizo zinazojulikana kama Queen Elizabeth Commonwealth Scholarship ni tarehe 26 Juni 2019.

Maelezo kuhusu taratibu za kuomba nafasi hizo yanapatikana kupitia tovuti: http://bit.ly/2Ytd8jJ. 

      ii Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi (UNHCR);

Kamishina Mkuu Msaidizi wa Masuala ya Hifadhi kwa Wakimbizi (Assistant High Commissioner for Protection).

Maelezo kuhusu nafasi hii yanapatikana kupitia tovuti: https://www.unhcr.org/career-opportunities ambapo mwisho wa kuwasilisha mombi ni tarehe 20 Mei 2019 katika baruapepe recruitment.AHC-P@unhcr.org.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Share:

Tanzania Tunao Uwezo Mkubwa wa Kuzalisha Mifuko Mbadala - Makamba

Na: Mwandishi Wetu
Tanzania inao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko mbadala ambayo itatosheleza kufanikisha azma yake ya kupiga marufuku biashara na matumizi ya mifuko ya plastiki. 

Hayo yamebainishwa na Waziri wa nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, mhe. Januari Makamba wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa leo Jijini Dodoma. 

Makamba amesema kuwa ni jambo la kushangaza kuona asilimia 100 ya mifuko ya karatasi inayotumika nchini Rwanda na asilimia hamsini nchini Kenya inazalishwa Tanzania huku Tanzania ikitumia zaidi ya asilimia 80 ya mifuko ya plastiki inayozalishwa nje ya nchi jambo linalokinzana na dhana ya kukuza uchumi wa viwanda. 

“ Tunao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko mbadala, wazalishaji wa mifuko hiyo wameithibitishia Serikali kuwa wanao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko hiyo ambapo Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi kimesema kitaongeza uzarishaji zaidi ya maratatu huku wawezkezaji zaidi ya 50 wakiwa wameagiza mashine za kuzalishia mifuko hiyo,”Alisema Waziri Makamba. 

Makamba aliongeza kuwa nchi ya Tanzania inaweza kufanikiwa katika zoezi hili kwa kuwa inazalisha mifuko mbadala ya karatasi ambayo hutumiwa kwa kiasi kikubwa na nchi jirani za  Rwanda huku kenya wakitumia asilimia kubwa ya mifuko kutoka Kiwanda cha Karatasi cha Mufindi cha hapa nchini, Kenya ikitumia asilimia 50, jambo linalotoa tafsiri kuwa tunaouwezo wa kuzalisha mifuko mbadala  itakayotosheleza,” Alisema Januari Makamba. 

Waziri Makamba amesema kuwa wazalishaji wa mifuko mbadala wameithibitishia Serikali kuwa wanao uwezo mkubwa wa kuzalisha mifuko hiyo ambapo Kiwanda cha Karatasi Mufindi kitaongeza uzalishaji zaidi ya mara tatu kinavyozalisha sasa huku wawekezaji zaidi ya 50 wakiwa wameagiza mashine kwa ajili ya kuzalishia mifuko hiyo. 

Katika hatua nyingine Waziri Makamba alitumia fursa hiyo kutoa rai kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa kushirikiana kwa karibu na mamlaka zingine zitakazo husika katika zoezi la kutokomeza biashara na matumizi ya bidhaa za Plastiki zilizopigwa marufuku.

Akizungumzia marufuku hiyo Makamba amesema kuwa katika awamu ya kwanza marufuku hiyo inahusisha mifuko ya plastiki tu huku bidhaa zingine zinazotumia plastiki vifungashio vya plastiki kuendelea kutumika wakati utaratibu ukiendelea. Alizitaja bidhaa hizo kuwa ni bidhaa za chakula, kilimo na dawa. 

Utekelezaji wa katazo hilo la matumizi ya bidhaa za plastiki nchini linafuatia utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyotoa tarehe 26, April, 2019 katika maadhimisho ya Muungano jijini Dodoma. 

Mwisho.


Share:

TCU Admissions Almanac for 2019/2020 Cycle

The TCU University Institutions Admissions Almanac for 2019/2020 Admission Cycle – Admissions Almanac for 2019/2020 – tcu guide book , faas tcu, tcu guide book for diploma, tcu guide book 2019/20, www.tcu.go.tz guide book 2019/20, tcu news today, tcu habari mpya 2019/2020, tcu accreditation

This is to inform the General Public and all prospective applicants for admission into various undergraduate degree programmes that pursuant to section 12(2)(a)(b) of the Universities Act, Cap. 346 of the Laws of Tanzania, The Tanzania Commission for Universities (TCU) is mandated to coordinate admissions to Universities in the United Republic of Tanzania. In this regard, TCU announces the almanac for 2019/2020 admission cycle for purposes of ensuring a smooth and timely coordination of admissions activities in Tanzania.

CHECK THE PDF BELOW………….

The post TCU Admissions Almanac for 2019/2020 Cycle appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TCU Admissions Almanac for 2019/2020 Cycle

The TCU University Institutions Admissions Almanac for 2019/2020 Admission Cycle – Admissions Almanac for 2019/2020 – tcu guide book , faas tcu, tcu guide book for diploma, tcu guide book 2019/20, www.tcu.go.tz guide book 2019/20, tcu news today, tcu habari mpya 2019/2020, tcu accreditation

This is to inform the General Public and all prospective applicants for admission into various undergraduate degree programmes that pursuant to section 12(2)(a)(b) of the Universities Act, Cap. 346 of the Laws of Tanzania, The Tanzania Commission for Universities (TCU) is mandated to coordinate admissions to Universities in the United Republic of Tanzania.

In this regard, TCU announces the almanac for 2019/2020 admission cycle for purposes of ensuring a smooth and timely coordination of admissions activities in Tanzania.

CHECK THE PDF BELOW………….

The post TCU Admissions Almanac for 2019/2020 Cycle appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

NACTE online Application Window for 2019 to be Open soon

NACTE, nacte application 2019/2020, nacte health application 2019/2020, nacte verification, nacte 2019/2020, www.nacte.go.tz application online, nacte health application 2019/20, www.nacte.go.tz 2019/2020, www.nacte.go.tz selection

The National Council for Technical Education (NACTE) is a corporate body established by the National Council for Technical Education Act, 1997 (Act No. 9 of 1997). The Act provides a legal framework for the Council to coordinate provision of technical education and training and establish an efficient national qualifications system that will ensure that products from technical institutions are of high quality and respond to changing needs as well as technological innovations in the world.

Kindly be informed that the Admission Cycle for 2019/2020 Academic year shall be opened soon. Thus be patient.

 

SEE ALSO

The post NACTE online Application Window for 2019 to be Open soon appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

The list of Institutions allowed to admit students in 2019/2020 academic year by the TCU

TCU Institutions allowed to admit students in 2019/2020 academic year – tanzania commission for universities, tcu 2019/2020, breaking news from tcu, www.tcu.go.tz 2019/2020, www.tcu.go.tz 2019/20, tcu habari mpya, www.tcu.go.tz 2019/2020, 

The post The list of Institutions allowed to admit students in 2019/2020 academic year by the TCU appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

List of approved and accredited institutions by TCU 2019/20

TCU List of approved and accredited institutions – TCU List of University Institutions in Tanzania – international universities recognized by tcu, www.tcu.go.tz student registration, tcu accreditation, tcu 2019/2020, www.tcu.go.tz 2019/20, faas tcu, breaking news from tcu, www.tcu.go.tz 2019/2020

The post List of approved and accredited institutions by TCU 2019/20 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali kuhakiki Taasisi za Kidini na Jumuiya za Kijamii




Share:

Makonda Atembelea Maeneo Yaliyoathiriwa na Mafuriko Jijini Dar.....Bilioni 200 Yaandaliwa Kukarabati Mto Msimbazi

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana amefanya ziara ya ukaguzi wa athari za mafuriko ambapo amesema serikali imeanza kukarabati miundombinu iliyoathiriwa na mvua zinazoendelea kunyesha ikiwemo madaraja, barabara, mito na mifereji.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo Makonda,  amesema miongoni mwa maeneo yanayoboreshwa na pesa ipo tayari ni mto msimbazi wenye urefu wa km 19 na eneo la Jangwani ambalo maboresho yake yatagharimu zaidi ya shilingi Bilioni 200 ikiwa ni mkopo kutoka Benki ya Dunia.

Aidha Makonda amesema hadi sasa jumla ya watu wawili wamefariki kutokana na mvua ambapo amewapa pole wananchi waliokumbwa na athari za mafuriko ikiwemo wale ambao mali zao zimeharibiwa na wengine kulazimika kuyahama makazi yao.

Katika hatua nyingie Makonda amewataka wananchi kuchukuwa tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Dengue kwa kuhakikisha wanatokomeza mazalia ya mbu na kuhakikisha wanawahi vituo vya afya pindi wanapoona dalili za homa.



Share:

Kesi ya Vigogo CHADEMA: Mchomelea Vyuma atoa ushahidi Mahakamani

Shahidi wa pili katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa CHADEMA, Shaban Abdallah (19), amedai alimuona Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe akiwahamasisha wananchi kuendelea kuandamana.

Shahidi huyo ambae ni Mchomelea Vyuma anayeishi Kinondoni Moscow ameeleza hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati akitoa ushahidi wake.

Shahidi Abdallah amedai Februari 16, 2018 majira ya saa 11 jioni alikuwa dukani eneo la Kinondoni Mkwajuni alisikia zogo likisogea karibu na eneo hilo ambapo aliona waandamanaji wakiwa katika hali ya shari wakiimba ‘Hatupoi mpaka mmoja afe watatuua’ ambapo alijua ni watu wa CHADEMA kutokana na mavazi yao na bendera.

Ameeleza kuwa wakati wakiendelea kuwaangalia waandamanaji hao waliona gari la polisi likiwa nyuma yao likiwatangazia watawawanyike, lakini waliendelea kulisogelea na kuanza kurusha chupa za maji na mawe..


Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 15, 2019 ambapo washitakiwa wengine ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu,Mbunge wa Kibamba,John Mnyika,Mbunge wa Kawe,Halima Mdee,Mbunge wa Tarime Mjini,Esther Matiko,Mbunge wa Iringa Mjini,Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Vijijini,John Heche.


Share:

Rais Magufuli Amtumbua Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Amos Makala

Rais Magufuli amempandisha hadhi aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Juma Homera kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi kuanzia  jana  Mei 14,2019.

Uteuzi huo wa Homera umetokana na uamuzi wa wa Rais kumpumzisha aliyekuwa mkuu wa mkoa huo, Amos Makala.

Taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa kurugenzi ya mawasiliano ikulu, Gerson Msigwa inasema “uteuzi wa mkuu wa Wilaya ya Tunduru utafanywa baadaye.”




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya May 15




Share:

Tuesday, 14 May 2019

Breaking News ; RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKUU WA MKOA WA KATAVI AMOS MAKALA

Share:

MAFURIKO YA WANAWAKE YAIKUMBA ESWATINI..MFALME MSWATI AAGIZA KILA MWANAUME AOE WAKE WAWILI LA SIVYO UTUPWE JELA

Mfalme wa Eswatini, Mswati wa III amewataka vijana wa nchini kwake waliofikia umri wa kuoa, waoe haraka na kusisitiza kuwa wanatakiwa waoe wake wawili au zaidi, kinyume na hapo atawatupa lupango wote wasiotekeleza agizo hilo kuanzia Juni, mwaka huu.
Mswati wa III ana jumla ya wake 15 na watoto 25. Baba yake ambaye pia alikuwa mfalme wa nchi hiyo, alikuwa na wake 70 na watoto zaidi ya 150.

Mswati alitoa onyo kali kwa mwanaume au mwanamke atakayekiuka agizo hilo atahukumiwa kifungo cha maisha jela.

Eswatini ni nchi ya Afrika yenye idadi kubwa zaidi ya wanawake kuliko wanaume, hivyo wanawake wengi hukosa waume wa kuwaoa.
***

King Mswati III of Swaziland has declared in Mbabane Swaziland that men will from June 2019 be required to marry at least two or more wives or be jailed if they fail to do so.

The king, who has 15 wives and 25 children,While his father and predecessor has more than 70 wives and 150+ children revealed that Swaziland is facing a very serious problem as there are more women than men in his country.
Men from Swaziland are therefore required and expected to take more wives so that every woman gets a husband.

The country which is known to be full of virgins, is also said to have more women than men.

In a statement, king Mswati called for all men in the country to marry at least five wives and the government assured the men that it would pay for the marriage ceremonies and buy houses for them.

ing Mswati warned that any man or woman who opposes the decision “will face a life sentence”.

Share:

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWASIMAMISHA KAZI WAKURUGENZI SABA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Wakurugenzi saba wa Tume ya Umwagiliaji akiwemo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa tume hiyo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

“CAG afanye haraka uchunguzi wa kina, tunataka kujua ni nani alikuwa mlango wa ubadhirifu huu. Hatutamuonea mtu, wote watakaothibitika kuhusika na matumizi mabaya ya fedha watachukuliwa hatua.”

Waziri Mkuu amechukua hatua hiyo leo (Jumanne, Mei 14, 2019) wakati wa kikao na viongozi wa tume hiyo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Mawaziri, Manaibu Waziri na Makatibu Wakuu. 

Mbali na kuwasimamisha kazi wakurugenzi hao, pia Waziri Mkuu ameagiza watumishi wengine 21 wa tume hiyo wachukuliwe hatua za kinidhamu kutokana na utendaji usioridhisha kwenye miradi mbalimbali inayosimamiwa na tume hiyo.

Waziri Mkuu amesema Serikali imechukua hatua hiyo kutokana na udhaifu wa kiutendaji ndani ya tume hiyo ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za miradi, rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, upendeleo na kukosa umakini. “Hatua kali zitachukuliwa dhidi ya ubadhirifu uliofanyika katika miradi ya umwagiliaji.”

Amesema hali ya kilimo cha umwagiliaji nchini hairidhishi na Serikali haijafurahishwa na utendaji wa Tume ya Umwagiliaji licha ya kuwekeza nguvu kubwa, hivyo inataka kuona mabadiliko.

“Miradi mingi inayotekelezwa na Tume ya Umwagiliaji nayo ina hali mbaya zaidi. Miradi mingi ya tume hiyo imejikita katika mafunzo, semina na warsha badala ya kujenga na kuendeleza skimu za umwagiliaji.”

Waziri Mkuu amesema tume hiyo imeshindwa kusimamia miradi takribani 10 katika maeneo mbalimbali nchini na kusababisha sekta ya umwagiliaji kushindwa kupata mafanikio yaliyotarajiwa kutokana na ubadhirifu.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na mradi wa umwagiliaji wa Luiche unaokadiriwa kumwagilia hekta 3,000 ambao upo katika hatua za awali za utekelezaji lakini tayari pamekuwepo na matumizi mabaya ya fedha za mradi.

“Kaimu Mkurugenzi Mkuu alitoa kibali na kulipa fedha taslimu masurufu ya jumla ya sh. milioni 100.7 kwa Wahandisi wa Makao Makuu, Maafisa wa Idara ya Mipango, Tathmini na Ufuatiliaji kwenda kufanya ukaguzi badala ya kujenga. Mkaguzi wa nje alihoji uhalali wa malipo hayo na hajapata majibu hadi leo.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga akamilishe mchakato wa kuwapata wajumbe wa bodi wa tume hiyo ambayo imemaliza muda wake.

Pia amemtaka Waziri huyo ahakikishe Wizara ya Kilimo inaisimamia tume kukamilisha ujenzi wa skimu zote za umwagiliaji zilizoanza kujengwa miaka ya nyuma zikiwemo za wakulima wadogo.

Kadhalika, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo afanye mabadiliko ya muundo wa tume hiyo na kuwa na maafisa wa umwagiliaji katika ngazi za mikoa na wilaya ili kusogeza huduma kwa wananchi.

Awali, Waziri wa Kilimo alisema skimu zinazofanya kazi hazizidi 10 kati ya 2,678 hali iliyosababishwa na kuwepo kwa dosari katika usimamizi na pia matumizi ya fedha za miradi katika Tume ya Umwagiliaji si mazuri.

Kwa upande wake, Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa alisema miradi mingi ya umwagiliaji ilifeli kwa sababu ya ilijengwa chini ya kiwango hususani mabwawa na pia haikuwa ikilingana na kiasi cha fedha kilichokuwa kinatolewa. “Mradi wa kutumia sh. bilioni mbili wanatumia sh. bilioni nne.”

Kikao hicho kimehudhuriwa na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa, Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Kilimo, Omar Mgumba, Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa, Makatibu Wakuu wa Wizara hizo pamoja na maofisa wengine wa Serikali.


(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Share:

WHATSAPP SIYO SALAMA...WADUKUZI WAMEFANYA YAO

Wadukuzi wanaweza kuweka programu ya Sofware ya kuchunguza taarifa kwenye simu yako na vifaa vingine vinavyotumiwa kwa kutuma ujumbe wa WhatsApp, imethibitishwa.

WhatsApp, ambayo inamilikiwa kampuni ya Facebook, inasema wanaodukua walilenga "namna walizochagua " za watumiajina waliongozwa na "watumiaji wakuu wa mtandao ".

Udukuzi huo ulibainika siku ya Ijumaa.

Jumatatu WhatsApp iliwaomba watumia bilioni 1.5 wa mtandao huo kufungua upya app zao kama njia zaidi ya kuepuka udukuzi.

Shambulio hilo dhidi ya WhatsApp, lililogunduliwa mapema mwezi huu ,lilikuwa ni la kwanza kuwahi kuripotiwa katika gazeti la Financial Times.

Unawahusisha wadukuzi wanaotumia sauti ya WhatsApp kuzipigia simu wanazozilenga. Hata kama simu hizo hazitapokelewa tayari programu ya udukuzi huwa imewekwa ndani ya simu inayolengwa na mara moja ujumbe wa kumuonyesha mwenye simu kuwa aliitwa na simu fulani hutoweka mara moja kwenye orodha ya simu zilizokuita.

BBC inafahamu kuwa kikosi cha usalama wa WhatsApp kilikuwa cha kwanza kubaini udukuzi huo, na kushirikisha taarifa hiyo makundi ya kutetea haki za binadamu , makampuni kadhaa ya usalama na wizara ta sheria ya marekani mapema mwezi huu.

"Wadukuzi wana kampuni ya kibinafsi ambayo inaripotiwa kufanya kazi na serikali ambazo huwapatia mfumo wa udukuzi ambao huchukua udhibiti wa mfumo mzima wa simu ," ilisema kampuni Jumatatu katika mazungumzo na waandishi wa habariUvamizi huo wa mtandao wa WhatsApp ulibuniwa na kampuni ya usalama ya Israeli inayofahamika kama NSO Group

Imeripotiwa kuwa uvamizi huo wa mtandao wa WhatsApp ulibuniwa na kampuni ya usalama ya Israeli inayofahamika kama NSO Group, kampuni ambayo awali ilielezewa kama "cyber arms dealer".

Programu yake kuu ya software, Pegasus, ina uwezo wa kukusanya taarifa za siri kutoka kwa mlengwa, ikiwemo kuchukua data kwa kutumia kipaza sauti(microphone) na kamera na kukusanya taarifa za mahali alipo mtumiaji wa simu.

Katika taarifa yake kundi hilo lilisema kuwa : "NSO's technology ina kibali cha utendaji wake na imeidhinishwa na wakala wa serikali kwa malengo ya kukabiliana na uhalifu pamoja na ugaidi.

"Kampuni haitumii mfumo wenyewe, baada ya kupewa kibali na kuchunguzwa, ujasusi na watekelezaji wa sheria huamua namna ya kutumia teknolojia kusaidia kazi yao ya kuhakikisha kunakuwa na usalama wa umma. Huwa tunachunguza madai yoyote ya kuaminika ya matumizi mabaya ya data na ikiwezekana tunachukua hatua, ikiwemo kuzima kabisa mfumo.

" Hakuna namna yoyote NSO inaweza kuhusika katika utendaji au kutambua walengwa wa teknolojia yake , ambayo hutumiwa na ujasusi na wakala wa utekelezaji wa sheria. NSO isingeweza au haiwezi kutumia teknolojia yake tkwa haki zake kumlenga mtu yeyote au kampuni , wakiwemo watu binafsi ."
WhatsApp imesema ni mapema kujua ni watumiaji wangapi wameathiriwa na udukuzi huo, ingawa washukiwa wengi walilengwa kwa kiwango kikubwa.

Kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni za Facebook , WhatsApp inajumla ya watumiaji bilioni 1.5 kote duniani.
Chanzo - BBC
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger