Monday, 6 May 2019

Chenge aagiza serikali kutoa taarifa kupotea kwa Mdude Chadema

Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge, ameitaka Serikali kufuatilia na kutoa taarifa za kutekwa kwa kijana na kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mdude Nyagawa ambaye anadaiwa kutekwa.

Mdude anadaiwa kuchukuliwa na watu wasiojulikana kwenye ofisi yake Mbozi, mkoani Songwe juzi, Mei 4 wakiwa na silaha za moto.

Chenge ametoa maelekezo hayo bungeni jijini Dodoma leo Jumatatu Mei 6, wakati akijibu hoja ya Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa aliyetoa hoja ya kuahirisha Bunge kwa kutumia kanuni ya 64 kuhusu kujadili jambo la dharura.

Katika hoja yake, Msigwa alisema hivi karibuni kumekuwapo na matukio ya watu kutekwa, kupotea na hata kuuawa, huku akitolea mfano madai ya kutekwa kwa kada wa chama hicho, Mdude.

Akitoa maelezo ya hoja hiyo, Chenge ameitaka Serikali kutolea ufafanuzi jambo hilo.

“Ni kweli suala lolote linalohusu uhai wa binadamu, itakuwa vizuri Serikali itoe maelezo ili wananchi wajue hali ilivyo,” amesema Chenge.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Yusufu Masauni amesema Jeshi la Polisi limeanza kufanyia uchunguzi tangu jana, Mei 5, na wameongeza nguvu kutoka makao makuu ya jeshi hilo lakini akapinga madai ya Mdude kutekwa.

"Mbunge Msigwa amesema kuwa Mdude Chadema ametekwa na Polisi wamekataa kufungua jarada kitu ambacho sio sahihi, ukweli wa mtu huyu hakuonekana na ukisema ametekwa inamaana wewe unajua na bila shaka Msigwa ana taarifa hizo na nilielekeze Jeshi la Polisi limtafute Msigwa ili aisaidie Polisi” Amesema Hamad Massauni


Share:

Mfungo Wa Ramadhani Kuanza Kesho, Mei 07

Kadhi Mkuu wa Tanzania, Abdallah Mnyasi amesema mfungo mtukufu wa ramadhani utaanza kesho Jumanne ya Mei 7, 2019.

Akizungumza jana Jumapili Mei 5,2019 kupitia televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wakati akifafanua kuhusu mwandamo wa mwezi alisema haujaonekana.

Alisema Waislamu kote nchini wataanza mfungo wa ramadhani mara baada ya kukamilika siku 30 za mwezi Shaaban.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum  amesema kwa kushirikiana na Mufti wa Zanzibar, Sheikh Saleh Omar Kaabi,na wa Tanzania Bara, Abubakar Zuber  wamekubaliana mwezi haujaonekana.


Share:

LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bungeni Dodoma

LIVE: Fuatilia kipindi cha maswali na majibu kutoka Bungeni Dodoma


Share:

Israel, Hamas Waendelea Kudundana Kwa Makombora na Ndege za Kivita

Jeshi la Israel linasema limemuuwa kamanda wa ngazi za juu wa kundi la Hamas kwenye mashambulizi yake katika Ukanda wa Gaza, huku pande zote mbili zikiapa kuendelea na mapigano.

Taarifa ya pamoja kati ya jeshi na shirika la ujasusi la Israel, Shin Bet,  inasema kamanda huyo, Hammed Al-Ghudari, alikuwa anahusika na kusafirisha fedha kutoka Iran kuyapelekea makundi ya wanamgambo kwenye Ukanda wa Gaza. Mashahidi wanasema aliuawa kwa shambulio la anga akiwa kwenye gari yake siku ya Jumapili (Mei 5). Wizara ya Afya ya Palestina ilithibitisha kifo hicho.

Hayo yanajiri huku idadi ya raia wa Israel waliouawa na maroketi yaliyorushwa kutoka Gaza ikifikia wawili na mwengine wa tatu akiripotiwa kuwa hali mbaya.

Maroketi yalikishambulia kiwanda kimoja kwenye mji wa Ashkelon na gari moja katika kijiji cha Kibbutz Yad Mordechai, huku kipande cha roketi jengine kikitua na kuharibu hospitali moja mjini Ashkelon, ingawa hakuna majeruhi walioripotiwa.

Kwa upande wa Wapalestina, mbali na Ghudari, wapiganaji wengine wawili waliuawa kwa mashambulizi ya anga ya Israel mashariki mwa Gaza, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Palestina. 
 
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, alisema kwamba ameliagiza jeshi kuongeza mashambulizi yake kuelekea Ukanda wa Gaza.

Netanyahu aliamuru kutumwa kwa magari zaidi ya kijeshi, mizinga na kikosi cha wanajeshi wa ardhini na alitoa wito wa mashambulizi makubwa zaidi dhidi ya kile alichokiita makundi ya kigaidi, kwa mujibu wa taarifa ya ofisi yake.

Mahmoud al-Zahar, kiongozi wa ngazi za juu wa Hamas, aliwaambia waandishi wa habari kwamba wasingealiacha kushambulia na kwamba walikuwa wanafuta makubaliano ya kusitisha mapigano baina yao na Israel.

Jeshi la Israel lilisema kwamba kufikia Jumapili mchana lilishalenga shabaha 260 dhidi ya makundi ya wanamgambo mjini Gaza, huku wanamgambo hao wakirusha makombora na maroketi 450 ndani ya Israel tangu siku ya Jumamosi.
 
Usiku wa Jumamosi, raia mmoja wa Israel aliuawa, huku raia watatu wa Kipalestina, akiwemo mwanamke mja mzito na mtoto wake, waliuawa, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Palestina. Wapiganaji wengine wanne wa Kipalestina waliuawa siku ya Jumamosi.

Hata hivyo, jeshi la Israel limekanusha kuhusika na kifo cha mwanamke huyo mjamzito na mtoto wake mwenye umri wa miezi 14, likisema wahanga hao waliuawa kwa roketi lililopotea njia kutoka upande wa Hamas.

Shirika la uokozi la Israel, Magen David Adom, lilisema kuwa liliwatibu zaidi ya watu 80, wengine wakiwa na majeraha kutokana na vipande vya maroketi, huku wengine wakiwa na majeraha yaliyotokana na kukimbilia maeneo salama. Wengi zaidi ni wale waliopata mshituko.

Makabiliano haya ya sasa yanakuja baada ya Wapalestina wanne kuuawa na wengine 51 kujeruhiwa na jeshi la Israel mpakani mwa pande hizo mbili siku ya Ijumaa. Wawili kati ya hao, walikuwa wanamgambo wa Hamas, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Palestina.

-DW


Share:

Watu 41 Wafariki Dunia Baada ya Ndege Kulipuka Moto Wakati Ikitua

Watu 41 wameuawa baada ya ndege ya Urusi kutua kwa dharura na kulipuka moto katika uwanja wa ndege wa Sheremetyevo mjini Moscow.

Video katika mitandoa ya kijamii zinaonyesha baadhi ya abiria wakitumia mlango wa dharura na kutoka kwenye ndege hiyo ya Aeroflot iliyokuwa inateketea moto.

Watoto wawili na mhudumu mmoja ni miongoni mwa waliofariki kwa mujibu wa vyombo vya habari Urusi.

Shahidi mmoja amesema ilikuwa ni "miujiza" kwamba kuna aliyenusurika mkasa huo wa ndege, iliyokuwa imebeba abiria 73 na maafisa watano wa ndege.

"Watu 37 wamenusurika - Abiria 33 na maafisa wanne wa ndege hiyo," amesema afisa wa kamati ya uchunguzi, Yelena Markovskaya.

Aeroflot, shirika la ndege la kitaifa Urusi limesema ndege hiyo ililazimika kurudi katika uwanja wa ndege " kutokana na sababu za kiufundi", lakini halikufafanua zaidi.

Ndege hiyo aina ya Sukhoi Superjet-100, iliondoka uwanja wa ndege wa Sheremetyevo mwendo wa saa 18:02 kwa saa ya huko kutoka eneo la Murmansk.

Maafisa wa ndege wakatoa tahadhari ya wasiwasi wakati kulishuhudiwa " hitilafu" muda mfupi baada ya ndege kuondoka.

Baada ya kutuwa kwa dharurua katika uwanja huo wa ndege , injini za ndege hiyo ziliwaka moto katika njia kuu wa ndege, Aeroflot limesema katika taarifa.

Maafisa hao wa ndege "walijitahidi kadri ya uwezo wao kuwaokoa abiria ," waliofanikiwa kutolewa katika muda wa sekundi 55, shirika hilo la ndege limeeleza
 
Kaimu Gavana wa mji eneo hilo la Murmansk, Andrey Chibis inaarifiwa amesema familia za waliofariki katika mkasa huo watalipwa $15,300 kola mmoja, huku waathirikwa watatibiwa katika hospitali na watapewa $7,650 kila mmoja..


Share:

AGPAHI YAADHIMISHA SIKU YA MKUNGA DUNIANI KWA KUCHUNGUZA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI KWA AKINA MAMA


Shirika lisilokuwa la kiserikali Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) limeshiriki maadhimisho ya siku ya mkunga duniani kwa kutoa huduma ya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama pamoja na upimaji wa Virusi Vya Ukimwi (VVU) mkoani Simiyu.



Maadhimisho hayo  kitaifa yamefanyika leo Mei 5, 2019 kwenye uwanja wa michezo wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile akimwakilisha Makamu wa Rais,Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mratibu wa Shirika la AGPAHI mkoa wa Simiyu Dafrosa Charles,alisema shirika la AGPAHI limeshiriki maadhimisho ya siku ya mkunga duniani kwa kutoa huduma ya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama pamoja na upimaji wa Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Amesema kati ya akina mama 205 waliowafanyia uchunguzi wa saratani hiyo ya mlango wa kizazi, wawili waligundulika kuwa na tatizo hilo na wamepatiwa rufaa ya kwenda kutibiwa kwenye hospitali ya rufaa Bugando Jijini Mwanza, huku 166 waliowapima VVU, mmoja kati yao amebainika kuwa ana maambukizi ya VVU na ameanzishia huduma ya dawa za kupunguza makali ya VVU.

Aliongeza kuwa Saratani hiyo ya mlango wa kizazi kwa sasa ndiyo imekuwa ikisababisha vifo vingi vya akina mama wakati wa kujifungua kutokana na kuvuja damu kwa wingi na kuwataka akina mama wajenge tabia ya kupima afya zao mara kwa mara ili waweze kupata matibabu mapema na ili kumaliza vifo hivyo.

Baadhi ya akina mama waliopatiwa huduma kwenye banda la Shirika la AGPAHI akiwemo Pendo Mboje, wamelipongeza Shirika hilo kwa kuwapelekea huduma hiyo, ambapo walikuwa hawajui visababishi vya kuugua saratani ya mlango wa kizazi pamoja na athari zake na kuahidi kujilinda zaidi na kwenda kutoa elimu kwa wenzao.

Maadhimisho hayo ya siku ya mkunga dunia kitaifa hapa nchini yamefayika mkoani Simiyu yakiwa na kaulimbiu isemayo,”Wakunga watetezi wa haki za wanawake”.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alimewataka wakunga kuendelea kutoa huduma nzuri kwa akina mama wajawazito na kuwaasa kuacha tabia ya kuwatolea lugha chafu ili kuongeza idadi kubwa ya wanawake kupenda kujifungulia kwenye vituo vya afya hali ambayo itapunguza tatizo la vifo vitokanavyo na uzazi.

“Licha ya Serikali kupunguza tatizo la vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi bado hali siyo ya kuridhisha ambapo awamu hii ya tano tumedhamiria kabisa kumaliza changamoto hiyo kwa kuhakikisha tunaendelea kuboresha huduma za afya hasa za mama na mtoto,”aliongeza.


Rais wa Chama cha Wakunga Tanzania (TAMA) Feddy Mwanga, alisema kilianzishwa mwaka 1992 kwa lengo la kuunganisha wakunga wasajiliwa nchini ili kuwa na nguvu moja katika kupambana kumaliza tatizo la vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi wakati wa kujifugua.

“Hapa mkoani Simiyu Chama cha Wakunga Tanzania kimeadhimisha siku hii kuanzia Mei 3 hadi leo Mei 5,2019 kwa kushirikiana na wadau wenzetu ambao wametoa huduma mbalimbali za afya ukiwamo upimaji wa VVU, huduma za uzazi wa mpango na uchuguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na matiti,”alisema Mwanga.

Naye katibu tawala wa mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini alisema takwimu za vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi kuwa vimepungua ambapo mwaka 2017 vilikuwa 48 ambapo mwaka 2018 vilitokea vifo 40 na kubainisha kuwa tatizo ni kuwapo kwa upungufu wa wakunga .
ANGALIA PICHA


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Faustine Ndugulile akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya mkunga duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Simiyu na kuwataka wakunga kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na kuacha lugha za matusi kwa wajawazito ili kuhamasisha kujifungulia kwenye huduma za kiafya na ili kumaliza vifo vitokanavyo na uzazi.Picha na Marco Maduhu- Malunde 1 blog

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile (wa pili kulia) akiwa na viongozi wa mkoa wa Simiyu kwenda kukagua mabanda ya wadau wa sekta ya afya likiwemo shirika la AGPAHI ambao wametoa huduma mbalimbali za kiafya kwenye maadhimisho hayo ya siku ya mkunga duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Simiyu.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile akiwa kwenye banda la Shirika la AGPAHI akipewa maelezo na Mratibu wa AGPAHI mkoa Simiyu Dafrosa Chalres namna linavyotoa huduma ya uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama pamoja na kuwapima maambukizi ya VVU na kuanza kuwapatia huduma wale ambao wanagundulika kuwa na magonjwa hayo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile , akipokea kijizuu kwenye banda la Shirika la AGPAHI.

Muuguzi mkunga Conchesta Alexander kutoka kituo cha afya Muungano Bariadi mkoani Simiyu, akitoa elimu kwa akina mama mkoani humo juu ya kujikinga na saratani ya mlango wa kizazi ugonjwa ambao unaua akina mama wengi wakati wa kujifungua.

Muunguzi mkunga kutoka kituo cha afya muungano Bariadi , Elizabeth Holela akitoa elimu kwa akina mama juu ya saratani ya mlango wa kizazi, madhara yake pamoja na namna ya kujikinga.

Muuguzi mkunga kutoka hospitali ya mkoa wa Simiyu Conchesta Alexander akiendelea kutoa elimu kwa akina mama mkoani humo kwenye Banda la AGPAHI namna ya kujiepusha na magonjwa ya saratani ya mlango wa kizazi.

Akina mama mkoani Simiyu wakiwa kwenye Banda la Shirika la AAGPAHI kupewa elimu ya saratani ya mlango wa kizazi, ili kutokomeza vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi.

Akina mama mkoani Simiyu wakiwa kwenye Banda la Shirika la AGPAHI kupewa elimu ya saratani ya mlango wa kizazi, ili kutokomeza vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi.

Mratibu wa Shirika la AGPAHI mkoani Simiyu Dafrosa Charles akitoa elimu kwa mmoja wa wanaume mkoani Simiyu namna ya kumkinga mke wake kutopata saratani ya mlango wa kizazi.

Muuguzi mkunga Mwaisha Yoma kutoka kituo cha afya Muungano Bariadi akichukua maelezo kwa mmoja wa akina mama ambaye amejitokeza kufanyiwa uchuguzi wa saratani ya mlango wa kizazi kutoka kwenye Banda la AGPAHI.

Pendo Mbonje ambaye ni mmoja wa akina mama mkoani Simiyu ambao wamejitokeza kufanyiwa uchunguzi wa Saratani ya mlango wa kizazi katika banda la AGPAHI, wakati wa maadhimisho ya ukunga duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo Simiyu.

Seke Ndongo akielezea namna alivyofanyiwa uchuguzi wa Saratani ya mlango wa kizazi na alivyopewa elimu ya kujikinga na saratani hiyo.




Katibu tawala wa mkoa wa Simiyu Jummane Sagini akiiomba wiraza ya afya impatie wauguzi wakunga ili kukabiliana na tatizo la vifo vya uzazi mkoani humo, ambapo kwa mwaka jana walipoteza maisha akina mama 40.

Rais wa Chama cha Wakunga Tanzania Feddy Mwanga akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya mkunga duniani kitaifa mkoani Simiyu, na kuelezea malengo ya maadhimisho hayo kufanyika mkoani Simiyu kuwa ni kuunganisha nguvu za pamoja kupambana kumaliza tatizo la vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi.

Wakunga wakiwa kwenye maadhimisho yao kitaifa mkoani Simiyu wakisikiliza nasaha za Naibu waziri wa afya ,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Faustine Ndugulile namna ya kuzingatia maadili ya kazi yao kiufasaha ili kutokomeza vifo vya uzazi.

Wananchi mkoani Simiyu wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya mkunga duniani mkoani humo.

Awali naibu waziri wa afya maendeleo ya jamiim jinsia wazee na watoto Dkt Faustine Ndugulile mwenye kaunda suti akipokea maandamano ya wakunga kwenye maadhimisho hayo kitaifa mkoani Simiyu.

Wakunga wakiingia kwa maandamano kwenye uwanja wa michezo wa halmashauri ya mji wa Bariadi wakitokea kwenye kituo cha afya cha Muungano mjini Bariadi.

Wauguzi wakunga nao hawakuwa nyuma kutoa burudani kwenye maadhimisho yao ya siku ya mkunga duniani, yaliyofanyika kitaifa mkoani Simiyu.

Wakunga wakiendelea kutoa burudani.
Picha na Marco Maduhu- Malunde 1 blog

Share:

Dr. Msola Ateuliwa Kuwa Mwenyekiti Mpya wa Klabu ya Yanga.....Mwakalebela Kachaguliwa Kuwa Makamu Mwenyekiti

Klabu ya Yanga imemchagua Dkt. Mshindo Msolla kuwa mwenyekiti wake huku Fredrick Mwakalebela akishinda katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti.

Katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo uliofanyika jana kwenye ukumbi wa Bwalo la Polisi Oysterbay Dar es salaam, Dkt. Msola amepata kura 1,276 akimshinda mpinzani wake Dkt. Jonas Tiboroha aliyepata kura 60.

Katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Mwakalebela amepata kuara 1,206 akiwashinda Janneth Mbene aliyepata kura 61, Titus Osoro aliyepata kura 17, Yono Kevela aliyepata kura 31 na Chota Chota aliyepata kura 12.

Walioshinda nafasi za Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Hamad Islam aliyepata 1,206, Mhandisi Bahati Faison Mwaseba kura 1,174, Dominick Ikute kura 1,088, Kamugisha Kalokola kura 1,072, Arafat Haji kura 1,024, Salum Ruvila kura 976, Saad Khimji kura 788 na Rodgers Gumbo kura 776. 

Uchaguzi huu umefanyika kufutia  kujiuzulu kwa viongozi wote waliongia madarakani Juni 11 mwaka 2016, Mwenyekiti Yussuf Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na wajumbe wao, Siza Augustino Lymo, Tobias Lingalangala, Samuel Lukumay, Hussein Nyika, Omary Said Amir, Salum Mkemi, Ayoub Nyenzi na Inspekta Hashim Abdallah.

Pamoja na kuwa kocha wa Taifa Stars, Dk. Msolla pia amewahi kuwa mtumishi wa Serikali kwa nafasi mbalimbali, ikiwemo Ukurugenzi wa Uendelezaji wa Mazao katika Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika wakati wa awamu ya Nne chini ya Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu May 6





















Share:

Sunday, 5 May 2019

BUNGE LA AFRIKA KUSHIRIKIANA NA BUNGE LA NCHI ZA FALME ZA KIARABU( UAE)

Share:

Hizi Ndizo Sehemu utakazopita mwili wa Dr. Mengi Kesho

Ratiba ya kuupokea mwili wa Dr. Reginald Mengi, Uwanja wa Ndege wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere imeelezwa kuwa itafanyika kesho, Jumatatu, saa 8:00 mchana.

Mwili wake utaletwa na ndege ya Shirika la Ndege la Emirates kutokea Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (U.A.E).

Baada ya mwili kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa JNIA, utapitishwa maeneo ya Tazara, Buguruni, Ilala, Kigogo, Magomeni hadi Kinondoni.

Kutoka Kinondoni, mwili wake pia utapitishwa hadi katika maeneo ya Morocco, barabara ya Bagamoyo, Sayansi, Mwenge hadi katika hospitali ya Lugalo ambako mwili wa Dr. Reginald Mengi utahifadhiwa.

Ratiba hiyo itaendelea siku ya Jumanne ya Mei 7, 2019, ambapo mwili utapelekwa katika ukumbi wa Karimjee, kwaajili ya watu wote kuuaga na kisha utarejeshwa nyumbani kwake. Siku ya Jumatano mwili utasafirishwa kupelekwa Moshi Machame ambako Ibada ya mazishi itafanyika siku ya Alhamis katika kanisa la Kisereni (KKKT).


Share:

Kikwete ataka habari za mtandaoni kifo cha Dkt. Mengi zipuuzwe

Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete amewataka watanzania kupuuzia taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijami kuhusiana na sababu za kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Media, Regnald Abraham Mengi kilichotokea Mei 2 mwaka huu, Dubai, Falme za Kiarabu.

Dkt. Kikwete ambaye jana  alifika nyumbani kwa Marehemu, Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa pole kwa familia amesema kuwa ukweli wa sababu za kifo cha Mengi wanaoufahamu ni binti yake na mdogo wake Benjamin.

Hivyo amewaomba watanzania kutulia hadi wawili hao wataporejea nchini na kueleza chanzo cha kifo chake kwani walikuwepo Dubai pindi mzee Mengi alipopatwa na umauti.

”Sisi wengine tuendelee kuwa watulivu, tuache uongo tuache kuingiza yasiyokuwepo tukaichanganya jamii,” amesema Dkt. Kikwete akiongea na waandishi wa habari baada ya kutoa pole kwa familia.

“Kama kweli tunampenda Mengi haya mengine ya uongo uongo, hadithi za kutunga hizi tuachane nazo, tusubiri ukweli, ukweli tutaupata. Alifariki Dubai mdogo wake Benjamin alikuwepo pamoja na binti yake, hao ndio wana ukweli kwahiyo hayo mengine mnayosoma-soma hayo nadhani kwa sasa yaacheni tusibiri wakirudi hao naamini watatuambia ni nini hasa kilitokea na ilikuaje mpaka kile kifo kilitokea,” Dkt. Kikwete aliongeza.

Aidha, Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Sirro amesema anafuatilia yanayoendelea kwenye mitandao kuhusu kifo cha Dkt. Mengi na kwamba wameanza kufanya uchunguzi kwa kufungua ‘dokezo’ ili kubaini ukweli.

Kama alivyosema Dkt. Kikwete, IGP pia aliwataka Watanzania kuwa watulivu na kumpumzisha marehemu na baada ya hapo jeshi hilo litaendelea na uchunguzi wake.


Share:

Watahiniwa 91,442 Wa Kidato Cha Sita Kuanza Mitihani Ya Taifa Kesho

Watahiniwa 91,442 wanatarajiwa kufanya mitihani yao ya kumaliza kidato cha sita kuanzia kesho Jumatatu Mei 6 hadi 23, 2019.

Mbali na hao, watahiniwa 12,540 wanatarajiwa kufanya mitihani yao ya kumaliza kozi ya ualimu katika ngazi ya cheti na stashahada.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Mei 5, 2019 Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde, amesema kumekuwa na ongezeko la watahiniwa wa shule wanaomaliza mtihani wa kidato cha sita kwa asilimia 4 ikilinganishwa na mwaka jana huku idadi ya watahiniwa wa ngazi ya ualimu wakiongezeka kwa asilimia 41.
 
Akitoa ufafanuzi wa watahiniwa wa mtihani wa kidato cha sita waliosajiliwa mwaka huu, amesema kati 80,305 ni watahiniwa wa shule na 11,117 ni wa kujitegemea

“Katika watahiniwa wa shule kati yao 46,224 sawa na asilimia 57.56 ni wavulana na 34,081 sawa na asilimia 42.44 ni wasichana huku watahiniwa walio na uhitaji maalumu wapo 102 kati yao, 67 ni wenye uoni hafifu; 16 ni wasioona; 18 wenye ulemavu wa kusikia; na 1 ni mwenye ulemavu wa afya ya akili,” amesema Dk Msonde.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger