Wednesday, 21 December 2016

New AUDIO | MIKE TEE Ft. CHEGE - UMENIKUTAGA | Download

Share:

EXCLUSIVE[AUDIO] Baghdad & ROMA Ft. Snura - K | Download [SINGELI]

Share:

PUBLIC NOTICE: HIGHER EDUCATION OPPORTUNITIES IN THE KINGDOM OF NORWAY 2017

Image result for SERIKALI YA TANZANIA

The International Summer School (ISS) at the University of Oslo, invites applications for admission into either Self-financed/sponsored or Scholarships to vie for higher education training opportunities tenable in the Kingdom of Norway.

The detailed information about Scholarships, the application process and the program itself can be found on the University’s website namely:- www.uio.no/summerschool  .
Kindly note that, the deadline for scholarship application is 1st February, 2017 and that for qualified self-financed/sponsored is 1st March, 2017.
You are strongly advised to read thoroughly and understand the details on how and where to apply.
Share:

PUBLIC NOTICE: SPONSORSHIP FOR HIGHER EDUCATION FROM THE ASHINAGA AFRICA INITIATIVE – 2017

Image result for SERIKALI YA TANZANIA

Kindly be informed that the Ashinaga Africa Initiative, is a Japanese – based, non-profit organization which offers training and sponsorship opportunities to Orphaned students who have completed their A – level studies.
Share:

New AUDIO | Queen Darleen Ft. Rayvanny - Kijuso | Download


Share:

Serikali Haijazuia Watumishi Wa Umma Kukopa Benki

Kumekuwa na taarifa inasambazwa katika mitandao ya kijamii, makundi ya ‘WhatsApp’, ‘Facebook’ na majukwaa mbalimbali ikieleza kuwa Serikali imepiga marufuku watumishi wa umma kukopa Benki,SACCOS,VICOBA na Taasisi mbalimbali za kifedha.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 20 Desemba 2016 na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeeleza kuwa taarifa inayosambazwa, ambayo imetafsiri mawasiliano ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni ya kupotosha, hivyo watumishi wote wa umma wanaombwa kuipuuza.

Vilevile watumishi wa umma wametakiwa kuzingatia kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali HAINA mamlaka ya kuzuia wala kuruhusu mtumishi yeyote wa Serikali kukopa au kutokopa katika Taasisi yoyote ya Fedha nchini.

Watumishi wa umma pia wamekumbushwa kuwa mikopo yote ya watumishi wa umma katika Taasisi za Fedha hutolewa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zilizopo ili mradi mtumishi awe ametimiza vigezo.

Aidha, watumishi wa umma wameaswa kuacha tabia ya kusambaza taarifa zisizo za kweli na ambazo zina mamlaka husika ya kuzitoa ikiwa ni pamoja na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
***
 
Share:

AJALI YAUA WANNE WAKIWEMO POLISI WAWILI

Watu wanne wakiwamo polisi wawili, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupindua katika kijiji cha Seruka kata ya Chipogoro tarafa ya Rudi wilayani Mpwapwa mkoa wa Dodoma.

Ajali hiyo ilitokea Desemba 19, mwaka huu, saa 11:30 jioni katika kijiji hicho baada ya gari walilokuwa wakisafiria T517 CDL Toyota Alphat katika barabara kuu ya Dodoma- Iringa, kuacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi tisa.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ernest Kimola, amesema gari hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na Aggrey Lucas, baada ya kufika katika kijiji hicho, liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya askari Konstebo Mahende na Konstebo Sasi Mwita ambaye ni askari mkoa wa Songwe.

Kamanda Kimola amewataja wengine waliofariki katika ajali hiyo ni mke wa Konstebo Mwita, Pendo Mwita na Emaculata Nyangi.

Amewataja majeruhi wa ajali hiyo ni Neema Mwita (8), Jenifa Mwita (4), Nyangi Wambura (23), Konstebo Nashon (23) ambaye ni polisi kituo cha Tunduma na Baraka Chacha (9).

Wengine ni Juli Mwita (6), Pc Enock ambaye ni mmiliki wa gari lililopata ajali, Makongoro Charles na Elizabeth Cosmas ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.

Aidha, kamanda Kimola amesema miili ya marehemu hao waliofariki katika ajali hiyo, imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DECEMBER TAREHE 21.12.2016

Share:

RAIS MAGUFULI AKATAA SHULE ISIITWE JINA AKE


Rais John Magufuli amekataa shule ya msingi iliyojengwa hivi karibuni eneo la Bunju, Wilaya ya Kinondoni kuitwa kwa jina lake badala yake ameagiza iitwe kwa jina la Mkuu wa wilaya hiyo, Ally Hapi. 
Taarifa ya badiliko la jina haikutolewa na Idara ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu kama ilivyozoeleka bali na mkuu wa wilaya hiyo wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya usafi kwa uongozi wa shule hiyo. 
“Shule hii imejengwa kwa fedha zilizopatikana baada ya Serikali Kuu kubana matumizi. Tukaamua iitwe John Magufuli lakini yeye akatoa agizo shule ipewe jina la mkuu wa wilaya sina budi kukubaliana na hilo,” alisema Hapi. 
Shule hiyo mpya iliyopo Bunju jijini imejengwa kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi katika Shule ya Msingi Bunju A ambayo ilikuwa na wanafunzi 3,224.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo mpya, Ali Mwakapalila alisema ingawa inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi Januari 9 mwakani inakabiliwa na changamoto mbalimbali. 
“Hakuna umeme wala maji, hii inaweza kuleta madhara kwa wanafunzi hasa linapokuja suala la matumizi ya vyoo,” alisema. 
Baada ya hafla hiyo, Hapi alikwenda kwenye kiwanda cha saruji cha Twiga Cement ambako alipokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa madarasa na majengo mengine. 
Akipokea msaada huo, Hapi alisema msaada kutoka Twiga Cement unaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano inayoipa sekta ya elimu kipaumbele ili kuhakikisha inatolewa katika mazingira bora. 
“Msaada huu umekuja muda muafaka. Tumeshajenga shule ila tunataka kuongeza madarasa, maabara, ofisi ya elimu na kuzungushia uzio ili watoto wawe katika mazingira salama. Lengo ni kuifanya shule hii iwe ya kisasa na itakuwa mfano kwa shule zote za Wilaya ya Kinondoni,” alieleza. 
Pia, Hapi alisema wilaya hiyo ipo kwenye mipango ya kujenga maktaba ya kisasa kwa kushirikiana na kampuni hiyo ya saruji. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Twiga Cement, Alfonso Velez alisema kuchangia katika shughuli za kijamii ni moja ya mambo ambayo wamekuwa wakiyapa kipaumbele zaidi. 
“Kushiriki shughuli za maendeleo katika jamii ni jambo ambalo tunalipenda zaidi. Yalipo maendeleo Twiga Cement ipo pia,” alisema Velez.
Share:

Tuesday, 20 December 2016

Baba Mzazi Wa Ben Saanane Kukagua Maiti Iliyowekwa Kwenye Kiroba


Share:

Magazeti Ya Leo Jumanne ya Disemba tarehe 20.12.2016


Share:

Dar yakamatia uzazi wa mpango wa asili

Share:

Wahitimu udaktari kupelekwa vituo vya afya

Share:

Nassari aipa tano serikali ya JPM





Mwandishi Maalumu, Arusha MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
Share:

Monday, 19 December 2016

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Wa Wakuu Wa Wilaya Wawili Na Wakurugenzi Watatu ,Nafasi ya Humphrey Polepole yachukuliwa na Kisare Makori

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 19 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 2 na Wakurugenzi 3 wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Share:

Uteuzi: Rais Dkt Magufuli ateua Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali, na pia ameteua Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania na Mjumbe mmoja wa Baraza la Taifa la Biashara.
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 19 Desemba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja walioteuliwa kama ifuatavyo;
 
1. Rais Magufuli amemteua Bw. Ali Mufuruki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Dhamana ya Hifadhi ya Mazingira.
 
Ali Mufuruki ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni za Infotech Investment na Mwenyekiti wa Taasisi ya Afrika inayojihusisha na uendelezaji wa vipaji vya uongozi katika ukanda wa Afrika Mashariki.
 
2. Rais Magufuli amemteua Mhandisi Christopher Kajolo Chiza kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
Mhandisi Christopher Kajolo Chiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Sabetha Mwambenja ambaye amemaliza muda wake.
 
3. Rais Magufuli amemteua Bw. Peter M. Maduki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
 
Peter M. Maduki anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Idrissa Mshoro ambaye amemaliza muda wake.
 
4. Rais Magufuli amemteua Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
 
Dkt. Yamungu Kayandabila ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Peter Ilomo ambaye amemaliza muda wake.
 
5. Rais Magufuli amemteua Prof. Godwin Daniel Mjema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Huduma za Fedha na Mikopo (UTT-MFI)
 
Prof. Godwin Daniel Mjema ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Fadhili D. Mbaga ambaye amemaliza muda wake.
 
6. Rais Magufuli amemteua Kepteni Ernest Mihayo Bupamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Bahari (DMI)
 
Kepteni Ernest Mihayo Bupamba ni Mwendesha Meli Mkuu (Principal Captain) Katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
 
7. Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce S. Hepelwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Miradi ya Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID)
 
Dkt. Aloyce S. Hepewa ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. John Jingu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi Tanzania.
 
Dkt. John Jingu ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Halikadhalika, Rais Magufuli amemteua Dkt. Rashid Adam Tamatama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI).
 
 Dkt. Rashid Adam Tamatama ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Pia, Rais Magufuli amemteua Bibi. Zuhura Muro kuwa Mjumbe wa Baraza la Taifa la Biashara (Tanzania National Business Council – TNBC).
 
Bibi. Zuhura Muro ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi inayojihusisha na huduma za ushauri wa ubora na mafunzo (Service Limited) katika ofisi zake za Dar es Salaam.
 
 Wateule wote waliotajwa hapo juu, uteuzi wao umeanza tarehe 17 Desemba, 2016
 
 Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Desemba, 2016
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DEC TAREHE 19.12.2016

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger