Wednesday, 21 December 2016

PUBLIC NOTICE: SPONSORSHIP FOR HIGHER EDUCATION FROM THE ASHINAGA AFRICA INITIATIVE – 2017

Image result for SERIKALI YA TANZANIA

Kindly be informed that the Ashinaga Africa Initiative, is a Japanese – based, non-profit organization which offers training and sponsorship opportunities to Orphaned students who have completed their A – level studies.
Share:

New AUDIO | Queen Darleen Ft. Rayvanny - Kijuso | Download


Share:

Serikali Haijazuia Watumishi Wa Umma Kukopa Benki

Kumekuwa na taarifa inasambazwa katika mitandao ya kijamii, makundi ya ‘WhatsApp’, ‘Facebook’ na majukwaa mbalimbali ikieleza kuwa Serikali imepiga marufuku watumishi wa umma kukopa Benki,SACCOS,VICOBA na Taasisi mbalimbali za kifedha.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 20 Desemba 2016 na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeeleza kuwa taarifa inayosambazwa, ambayo imetafsiri mawasiliano ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni ya kupotosha, hivyo watumishi wote wa umma wanaombwa kuipuuza.

Vilevile watumishi wa umma wametakiwa kuzingatia kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali HAINA mamlaka ya kuzuia wala kuruhusu mtumishi yeyote wa Serikali kukopa au kutokopa katika Taasisi yoyote ya Fedha nchini.

Watumishi wa umma pia wamekumbushwa kuwa mikopo yote ya watumishi wa umma katika Taasisi za Fedha hutolewa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu zilizopo ili mradi mtumishi awe ametimiza vigezo.

Aidha, watumishi wa umma wameaswa kuacha tabia ya kusambaza taarifa zisizo za kweli na ambazo zina mamlaka husika ya kuzitoa ikiwa ni pamoja na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
***
 
Share:

AJALI YAUA WANNE WAKIWEMO POLISI WAWILI

Watu wanne wakiwamo polisi wawili, wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kupindua katika kijiji cha Seruka kata ya Chipogoro tarafa ya Rudi wilayani Mpwapwa mkoa wa Dodoma.

Ajali hiyo ilitokea Desemba 19, mwaka huu, saa 11:30 jioni katika kijiji hicho baada ya gari walilokuwa wakisafiria T517 CDL Toyota Alphat katika barabara kuu ya Dodoma- Iringa, kuacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi tisa.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ernest Kimola, amesema gari hiyo iliyokuwa ikiendeshwa na Aggrey Lucas, baada ya kufika katika kijiji hicho, liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo vya askari Konstebo Mahende na Konstebo Sasi Mwita ambaye ni askari mkoa wa Songwe.

Kamanda Kimola amewataja wengine waliofariki katika ajali hiyo ni mke wa Konstebo Mwita, Pendo Mwita na Emaculata Nyangi.

Amewataja majeruhi wa ajali hiyo ni Neema Mwita (8), Jenifa Mwita (4), Nyangi Wambura (23), Konstebo Nashon (23) ambaye ni polisi kituo cha Tunduma na Baraka Chacha (9).

Wengine ni Juli Mwita (6), Pc Enock ambaye ni mmiliki wa gari lililopata ajali, Makongoro Charles na Elizabeth Cosmas ambao wote wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.

Aidha, kamanda Kimola amesema miili ya marehemu hao waliofariki katika ajali hiyo, imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DECEMBER TAREHE 21.12.2016

Share:

RAIS MAGUFULI AKATAA SHULE ISIITWE JINA AKE


Rais John Magufuli amekataa shule ya msingi iliyojengwa hivi karibuni eneo la Bunju, Wilaya ya Kinondoni kuitwa kwa jina lake badala yake ameagiza iitwe kwa jina la Mkuu wa wilaya hiyo, Ally Hapi. 
Taarifa ya badiliko la jina haikutolewa na Idara ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu kama ilivyozoeleka bali na mkuu wa wilaya hiyo wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya usafi kwa uongozi wa shule hiyo. 
“Shule hii imejengwa kwa fedha zilizopatikana baada ya Serikali Kuu kubana matumizi. Tukaamua iitwe John Magufuli lakini yeye akatoa agizo shule ipewe jina la mkuu wa wilaya sina budi kukubaliana na hilo,” alisema Hapi. 
Shule hiyo mpya iliyopo Bunju jijini imejengwa kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi katika Shule ya Msingi Bunju A ambayo ilikuwa na wanafunzi 3,224.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo mpya, Ali Mwakapalila alisema ingawa inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi Januari 9 mwakani inakabiliwa na changamoto mbalimbali. 
“Hakuna umeme wala maji, hii inaweza kuleta madhara kwa wanafunzi hasa linapokuja suala la matumizi ya vyoo,” alisema. 
Baada ya hafla hiyo, Hapi alikwenda kwenye kiwanda cha saruji cha Twiga Cement ambako alipokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa madarasa na majengo mengine. 
Akipokea msaada huo, Hapi alisema msaada kutoka Twiga Cement unaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano inayoipa sekta ya elimu kipaumbele ili kuhakikisha inatolewa katika mazingira bora. 
“Msaada huu umekuja muda muafaka. Tumeshajenga shule ila tunataka kuongeza madarasa, maabara, ofisi ya elimu na kuzungushia uzio ili watoto wawe katika mazingira salama. Lengo ni kuifanya shule hii iwe ya kisasa na itakuwa mfano kwa shule zote za Wilaya ya Kinondoni,” alieleza. 
Pia, Hapi alisema wilaya hiyo ipo kwenye mipango ya kujenga maktaba ya kisasa kwa kushirikiana na kampuni hiyo ya saruji. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Twiga Cement, Alfonso Velez alisema kuchangia katika shughuli za kijamii ni moja ya mambo ambayo wamekuwa wakiyapa kipaumbele zaidi. 
“Kushiriki shughuli za maendeleo katika jamii ni jambo ambalo tunalipenda zaidi. Yalipo maendeleo Twiga Cement ipo pia,” alisema Velez.
Share:

Tuesday, 20 December 2016

Baba Mzazi Wa Ben Saanane Kukagua Maiti Iliyowekwa Kwenye Kiroba


Share:

Magazeti Ya Leo Jumanne ya Disemba tarehe 20.12.2016


Share:

Dar yakamatia uzazi wa mpango wa asili

Share:

Wahitimu udaktari kupelekwa vituo vya afya

Share:

Nassari aipa tano serikali ya JPM





Mwandishi Maalumu, Arusha MBUNGE wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari
Share:

Monday, 19 December 2016

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Wa Wakuu Wa Wilaya Wawili Na Wakurugenzi Watatu ,Nafasi ya Humphrey Polepole yachukuliwa na Kisare Makori

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 19 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 2 na Wakurugenzi 3 wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Share:

Uteuzi: Rais Dkt Magufuli ateua Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali, na pia ameteua Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania na Mjumbe mmoja wa Baraza la Taifa la Biashara.
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 19 Desemba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja walioteuliwa kama ifuatavyo;
 
1. Rais Magufuli amemteua Bw. Ali Mufuruki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Dhamana ya Hifadhi ya Mazingira.
 
Ali Mufuruki ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni za Infotech Investment na Mwenyekiti wa Taasisi ya Afrika inayojihusisha na uendelezaji wa vipaji vya uongozi katika ukanda wa Afrika Mashariki.
 
2. Rais Magufuli amemteua Mhandisi Christopher Kajolo Chiza kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
Mhandisi Christopher Kajolo Chiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Sabetha Mwambenja ambaye amemaliza muda wake.
 
3. Rais Magufuli amemteua Bw. Peter M. Maduki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
 
Peter M. Maduki anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Idrissa Mshoro ambaye amemaliza muda wake.
 
4. Rais Magufuli amemteua Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
 
Dkt. Yamungu Kayandabila ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Peter Ilomo ambaye amemaliza muda wake.
 
5. Rais Magufuli amemteua Prof. Godwin Daniel Mjema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Huduma za Fedha na Mikopo (UTT-MFI)
 
Prof. Godwin Daniel Mjema ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Fadhili D. Mbaga ambaye amemaliza muda wake.
 
6. Rais Magufuli amemteua Kepteni Ernest Mihayo Bupamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Bahari (DMI)
 
Kepteni Ernest Mihayo Bupamba ni Mwendesha Meli Mkuu (Principal Captain) Katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
 
7. Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce S. Hepelwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Miradi ya Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID)
 
Dkt. Aloyce S. Hepewa ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. John Jingu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi Tanzania.
 
Dkt. John Jingu ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Halikadhalika, Rais Magufuli amemteua Dkt. Rashid Adam Tamatama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI).
 
 Dkt. Rashid Adam Tamatama ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 
Pia, Rais Magufuli amemteua Bibi. Zuhura Muro kuwa Mjumbe wa Baraza la Taifa la Biashara (Tanzania National Business Council – TNBC).
 
Bibi. Zuhura Muro ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi inayojihusisha na huduma za ushauri wa ubora na mafunzo (Service Limited) katika ofisi zake za Dar es Salaam.
 
 Wateule wote waliotajwa hapo juu, uteuzi wao umeanza tarehe 17 Desemba, 2016
 
 Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Desemba, 2016
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DEC TAREHE 19.12.2016

Share:

Sunday, 18 December 2016

Msanii Darasa akiwa na Hanscana wapata ajali ya gari huko Kahama

Mwanamuziki Darasa amepata ajali maeneo ya Ntobo barabara yakuelekea mgodi wa Bullyanhulu wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga. Waliokuwa garini wote wamenusurika.

Katika gari hiyo pamoja na watu wengine alikuwa na mtayarishaji wa video aliye kwenye chart Hanscana.




15492537_10206378362818256_6093491712623732141_n.jpg 15492570_10206378362218241_7745684630275410784_n.jpg
 
Share:

Ma-DC hatarini kutumbuliwa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

WAKUU wa Wilaya (Ma-DC) na Wakurugenzi nchini, ambao hawajakamilisha kutengeneza madawati, yanayokidhi idadi ya wanafunzi katika shule za maeneo yao, wamepewa siku 14 kukamilisha kazi hiyo.
Imeelezwa kuwa wanafunzi watakapofungua shule, lazima wakae kwenye madawati hayo.
Wakuu wa wilaya na wakurugenzi, watakaoshindwa kutimiza agizo hilo hadi ifikapo Desemba 30, mwaka huu, watakuwa wamejifukuzisha kazi wenyewe.
Aidha, wametakiwa kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kwenda kidato kwanza mwakani, wanaanza masomo yao kwa awamu moja, badala ya awamu mbili tofauti.
Agizo hilo lilitolewa jijini hapa jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Arumeru katika ziara yake ya kikazi mkoani hapa.
Aliagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi wote nchini kuwa hadi Desemba 30, mwaka huu wilaya zote zenye upungufu wa madawati ziwe zimekamilisha.
“Wale ambao watashindwa kufanya hivyo, watakuwa wamejifukuzisha kazi wenyewe” alisema. Akizungumzia ukusanyaji wa mapato katika wilaya hiyo, Majaliwa alisema kuwa hadi Desemba 30, mwaka huu, wawe wamefikia asilimia 50, tofauti na hali ya sasa ambapo wamekusanya asimilia 30 tu. “Ongezeni kasi ya ukusanyaji wa mapato katika halmashauri zenu na mhakikishe kila mtu anafanya kazi zake kwa kumheshimu mwenzie,” alisema Waziri Mkuu.
Serikali inahitaji haraka madawati ili kuondoa uhaba unaozikabili shule za sekondari na msingi wa madawati. Hali halisi ikoje? Hadi sasa, zaidi ya madawati milioni moja, sawa na asilimia 88 ya madawati yanayohitajika katika shule za msingi na asilimia 95 kwa shule za sekondari, yamepatikana. Kwa shule za msingi, imebaki asilimia asilimia 12 kumaliza tatizo la madawati, huku shule za sekondari imebaki asilimia 5.
Mikoa sita ambayo ina hali mbaya na haijatekeleza kikamilifu agizo hilo la madawati ni Mwanza, Kigoma, Mara, Rukwa, Simiyu, Dodoma na Geita, ambapo Geita inadaiwa madawati zaidi ya 80,000 ya shule za msingi na sekondari.
Mwanza inadaiwa madawati 41, 438, Kigoma madawati 31,171, Mara madawati 16,978, Dodoma madawati 14,873, Rukwa madawati 10,978 pamoja na Mkoa wa Simiyu.
Mkoa wa Mwanza unaundwa na wilaya za Nyamagana, Ilemela, Misungwi, Kwimba, Ukerewe, Magu na Sengerema, wakati wilaya za mkoa wa Kigoma ni Buhigwe, Uvinza, Kakonko, Kasulu, Kibondo na Kigoma.
Wilaya za mkoa wa Mara ni Tarime, Bunda, Butiama, Musoma, Serengeti na Rorya na Mkoa wa Rukwa una wilaya za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi.
Mkoa wa Simiyu wilaya zake ni Bariadi, Maswa, Busega, Meatu, Itilima na Mkoa wa Dodoma wilaya zake ni Kondoa, Bahi, Mpwapwa, Kongwa, Dodoma, Chamwino na Chemba, wakati mkoa wa Geita wilaya zake ni Geita, Chato, Bukombe, Mbogwe na Nyang’hwale.
Mikoa ambayo imemaliza tatizo hilo la madawati kwenye shule za msingi na sekondari ni 14 ambayo ni Mtwara, Lindi, Dar es Salaam, Arusha, Iringa, Kilimanjaro, Mbeya, Ruvuma, Njombe, Manyara, Pwani, Shinyanga, Singida na Tabora.
Mikoa mingine iliyosalia, imebakiza idadi ndogo ya madawati ambayo inakaribia kukamilika. Tanzania Bara ina mikoa 26.
Share:

Marufuku matajiri kuwatumia polisi kupiga mabomu wananchi



WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku watu binafsi wenye uwezo kifedha kutumia Jeshi la Polisi kuwapiga mabomu na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapiga mabomu wanachi wasio na silaha.
Ameagiza nguvu hizo wazitumie kwenye maeneo ambayo yanahatarisha usalama wa nchi na wananchi.
Aidha amewaambia wananchi wa Kata ya Bwawani Kitongoji cha Omapinu kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi atafika kijijini hapo wiki ijayo, kuzungumza nao namna ya kutatua mgogoro wa shamba la Tanzania Plantation na wananchi hao.
Waziri Mkuu Majaliwa aliyasema hayo baada ya kusimamishwa na wananchi wa kitongoji hicho, wakati alipokuwa akiendelea na ziara yake mkoani hapa jana.
“Kuanzia sasa ni marufuku kwa watu binafsi wenye uwezo wa fedha kutumia Jeshi la Polisi kuwapiga mabomu na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwapiga mabomu wakati hawana silaha. “Polisi wanaruhusiwa kutumia nguvu hizo kwenye maeneo ambayo yanahatarisha usalama wa nchi na wananchi na si vinginevyo,” alisema Waziri Mkuu.
Kuhusu mgogoro wa shamba la Tanzania Plantation, Waziri Mkuu alihoji; “Ni kwanini polisi wawapige mabomu wananchi wanaozuiwa kulima au kuchota maji katika eneo hilo la shamba hadi kufikia hatua ya wanawake kuharibu mimba? “Nyie polisi kwanini mnawapiga mabomu hawa watu, nani anatoa amri ya kupigwa mabomu wananchi hawa. Nasema kuanzia leo msiwapige mabomu watu hawa na pia nawasihi nyie wananchi msifanye fujo, subirini Waziri Lukuvi anakuja wiki ijayo kwa ajili ya kutatua mgogoro huu wa shamba.”
Alisema polisi wanaruhusiwa kutumia nguvu, pale tu panapotokea jambo linaloweza kuhatarisha maisha au vurugu, ila si kuwanyanyasa wananchi wanaodai ardhi yao kwa kuwapiga mabomu.
Alisema Lukuvi atafika mkoani humo kwa ajili ya kushughulikia migogoro ya ardhi, ambayo ipo zaidi wilayani Arumeru, na atakaa muda mwingi kwa ajili ya kutatua kero za wananchi.
Alisema kuanzia sasa mwekezaji ambaye ana mashamba wilayani humo na hayaendelezi, mashamba hayo yatachukuliwa na serikali ili kugawanywa kwa wananchi.
Alisema Waziri Lukuvi akiwa wilayani humo pamoja na kushughulikia migogoro mingine, pia atatatua mgogoro huo baina ya shamba la Tanzania Plantation na wanachi hao.
Awali, Ofisa Ardhi Wilaya ya Arumeru, Rehema Jato alikiri kuwepo kwa mgogoro wa ardhi kati ya mwekezaji wa wa Shamba la Tanzana Plantation, Pradeep Lodhia na wananchi.
Alisema kuna kesi mahakamani na wanachosubiri sasa ni uamuzi wa Mahakama ndipo hatua zingine zichukuliwe. Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alexander Mnyeti alisema wilaya hiyo ni moja ya wilaya nchini zenye migogoro mingi ya ardhi na wakati mwingine watu wanauana.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger