Wednesday, 24 February 2016

Video:nay wa mitego-shika adabu yako -behind the scene

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

MPYA:TAARIFA MUHIMU KUTOKA BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
                   Image result for HESLB
Share:

BREAKING NEWS:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WA ST.JOSEPH WALIOHAMISHWA CHUO KIKUU SUA,UDOM,RUCO NA MWENGE UNIVERSITY -TCU 2016

Share:

BREAKING NEWS:CHUO KIKUU CHA ST.JOSEPH -ARUSHA KIMEFUNGWA.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Baada ya kufungwa kwa chuo kikuu cha St.joseph tawi la songea,wanafunzi wa chuo kikuu cha st.joseph arusha wamekuwa katika hali ya wasiwasi wakiogopa kama ya waliowakutwa wenzao wa Songea ,na kuleta hali ya sintofahamu chuoni hapo.
 Kutokana na hali hio,Maswayetu blog imefuatilia swala hilo na kuhakikishiwa na chuo hicho  cha St.joseph Tawi la Arusha kufunga chuo hicho rasmi hadi hapo NOTICE itakapotolewa. 
Wanafunzi wametakiwa kurudi Nyumbani kwao,hadi hapo taarifa itakapotolewa. Barua ya kufunga chuo hicho ipo hapo chini,

"ENDAPO KAMA UNA TAARIFA YOYOTE TUTUMIE WATSUP THROUGH 0768260834"
Share:

NECTA Yasitisha Kugawa vyeti kwa Wahitimu wa Kidato cha Sita 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Baraza la Taifa la Mitihani (Necta), limeagiza kusitishwa kwa ugawaji wa vyeti vya kidato cha sita kwa wanafunzi waliohitimu mwaka 2015, huku vile vilivyokwisha gawanywa kwa watahiniwa hao vikitakiwa kurejeshwa kwenye chombo hicho.

Hali hiyo imeibua utata mkubwa, huku baadhi ya wadau wakiwamo maofisa elimu, wakihisi hatua hiyo ya Necta huenda inalenga kuvibadili vyeti hivyo kutoka kwenye mfumo wa wastani wa alama (GPA), kwenda kwenye ule wa jumla (division).

Ofisa Elimu Mkoa wa Dodoma, Juma Kaponda, alipoulizwa  kama amepokea agizo hilo, alithibitisha kuwa shule zote za mkoa huo zenye kidato cha tano na sita zimepewa taarifa ya kutakiwa kurudisha vyeti hivyo Necta.

Alisema sababu ya kuvirudisha vyeti hivyo anadhani ni kufanya mabadiliko kutoka GPA na kurudi kwenye divisheni.

Ofisa Elimu Mkoa wa Arusha, Nestory Mloka, alisema amepata barua ya maelekezo hayo kutoka Necta ikimuelekeza kuwataka maofisa elimu wilaya wawasiliane na wakuu wa shule za kidato cha tano na sita wasigawe vyeti vya wanafunzi waliohitimu mwaka 2015.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya St. Matthew iliyoko Kongowe, Mkuranga mkoani Pwani, Abraham Shafuri, naye alikiri kuwapo kwa agizo la Necta la kusimamisha utoaji wa vyeti hivyo kwa wahusika.

Alisema aliambiwa na maofisa wa Necta kuwa vyeti hivyo vinatakiwa kurejeshwa kwenye baraza hilo na kwamba sababu zilizotolewa ni kuwa kuna marekebisho kidogo yanapaswa kufanyika.

“Nilichoambiwa ni kwamba shule karibu zote za Dar es Salaam zimesharejesha vyeti hivyo na kwamba kwa sisi wa mkoa wa Pwani, maofisa hao watapita kuvichukua lakini hatujui ni lini watakuja,” alisema Shafuri.

Hata hivyo, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk, Charles Msonde, alipoulizwa   alikanusha vikali madai hayo, akisema vyeti hivyo havitabadilishwa kutoka kwenye mfumo wake bali vimesitishwa kugawanywa ili baraza lijiridhishe na baadhi ya vitu.
“Vyeti hivi baraza limevigawa hivi karibuni na lilichofanya sasa limezuia kwanza shule zisigawe mpaka litakapotoa maelekezo mengine, msingi huo wa kuzuia uko kwenye hoja ya kuhakikisha tu kwamba linajiridhisha kwenye takwimu zake kama zimekaa sawasawa katika vyeti vilivyokwenda kila shule.

“Baadhi ya vyeti kwenye mkoa wa Dar es Salaam vipo Necta, lakini kwenye mikoa mingine yote viko shuleni,” alisema Dk Msonde na kuongeza;
 
“Kama mkuu wa shule alikuwa amegawa vyeti viwili, vitatu kabla havijarejeshwa baraza ni suala jingine, lakini kiujumla kinachofanywa na baraza hapa ni kuhakiki cheti hiki, kama vimekaa kama utaratibu wetu ulivyo.”

Alisema suala la kubadilisha kutoka kwenye GPA kwenda kwenye divisheni halipo na kwamba matokeo yaliyotangazwa kwa utaratibu wa GPA vyeti vyake vitaendelea kuwa katika mfumo wa GPA na matokeo yaliyotangazwa kwenye utaratibu wa divisheni vyeti vyake vitabaki kuwa kwenye divisheni.

Alisema kwa wale ambao tayari wako nje ya nchi, hakuna atakayeathirika na kama baraza likihitaji cheti chake litafanya utaratibu wa kukipata.
Share:

Premier victory in London

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Leo Messi scores twice in a scintillating Champions League encounter to set Barça up nicely for the second leg at the Camp Nou


Barça will be defending a healthy 2-0 lead when they meet Arsenal at the Camp Nou for the second leg of their Champions League last sixteen tie. Leo Messi scored twice in a feverishly paced encounter on Tuesday night, including the 10,000th goal in club history.

Fast and furious

The game was intense from the very first second, with football of the kind of quality that one would expect from two sides like this. Arsenal started bravely, but as the action progressed found themselves pushed further and further back onto their own half.
But that’s a situation the Gunners are typically comfortable with and their rapid counter attacks caused plenty of early danger. Had Oxlade-Chamberlain made better contact in the 22nd minute, he would probably have had Ter Stegen beaten.
And so it continued, with Barcelona governing the possession but Arsenal creating more in the way of real danger and the home defence immediately putting a stop to any trickery from the trident.

Everything but the goal

In the last minute of the half, things finally started to click. Suárez had a fine chance but opted to pass to Messi when a shot might have been a better option, and the Uruguayan was alone when his head met Alves’ pass, but the ball skimmed just wide of the post. The way things had suddenly started going, it was probably Arsenal who appreciated the sound of the half-time whistle most.
But the Catalans fired the first shot of the second half too, home keeper Petr Cech doing well to deny Neymar in a one-on-one. What followed was the type of football that Premiership followers know and love: non-stop and physical with the action rapidly switching from one end to the other.
Giroud came closest to a goal with a header that brought out the best and a bit more from Ter Stegen, while a golden opportunity for Suárez found neither the net nor Neymar, who arrived just too late to tap home.

10K Messi 

And then after 71 minutes the game finally got the only thing it was lacking. A goal. Neymar charged through on the Arsenal area and laid the ball off to Messi, who for once was completely unmarked. The Argentinian rarely wastes chances like those, and at long last he’d scored his first goal against Cech.
The goal inspired the trident to unleash its full potential, and all three were involved in a lightning move that ended with Suárez slamming the ball onto the post. But Barça were now firing on all cylinders, and in the 83rd minute the lead was extended.
Flamini brought down Messi in the box and the Turkish referee had no option but to point at the spot. A spot from which the Argentinian made no mistake and the goal goes down in the record books as number 10,000 in FC Barcelona history.
There could have been another right at the end when Cech managed to get a stretched hand onto a Neymar header. But a 2-0 win against a very noble opponent is a result that Luis Enrique will be delighted to be taking to the Camp Nou for the second leg.
Share:

Ukata Wamkumba Ray C, Adai Analazimika Avae ‘Ninja’ ili Aweze Kutumia Usafiri wa Daladala....Aomba Msaada Kwa Wenye Uwezo

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Msanii wa muziki nchini, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amesema hali yake ya uchumi imekuwa mbaya zaidi hadi anashindwa kumudu baadhi ya gharama za maisha yake.

Muimbaji huyo ambaye yupo kwenye tiba ya methadone katika hospitali ya Mwananyamala kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya, amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Television Jumatatu hii kuwa, anatamani sana kurudi kwenye muziki ili apate kipato chake lakini anashindwa.

“Jamani kiukweli haya maisha ya wasanii nyie acheni tu, yaani inabidi tumuombe tu mungu, mtu akikuona msanii kwenye daladala nani atanunua albamu yako, nani atakuja kwenye show yako, lakini mama ananiambia vaa ninja mwanangu nenda kapate tiba. Kwa sababu kila siku kukodi taxi ni gharama sana, kutoa elfu 25000 kutoka Bunju mpaka hospitali kila siku ni nyingi sana. Sometimes namwambia mama inabidi tutoke mapema saa 11 hivi nivae ninja twende kwanza kanisani then naweza nikachukua hata bajaji kwenda hospitali. Haya ni maisha sio kitu cha kucheka ni lazima nifanye hivyo ili niweze kumaliza dozi,” alisema Ray C.

Pia Ray C ameomba wadau mwenye uwezo wamsaidie kupush muziki wake ili aweze kujisaidia mwenyewe.

“Hakuna masharti yoyote kwenye kunisaidia, mpaka mtu akitaka kuchangia, sijui elfu 10000, 2000, jamani unaweza kunisaidia kwa namna yoyote, kiukweli mimi nahitaji kurudi kwenye game na mtu ambaye alitaka kunisaidia ameniacha,” alisema Ray C.
Share:

Trafiki Dar es Salaam Wakusanya Bilioni 1.9 Mwezi February Kwa Makosa ya Barabarani Pekee

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Kikosi cha usalama barabarani Kanda maalumu ya Dar es salaam kimetangaza kukusanya kiasi cha shilingi BILIONI MOJA NUKTA TISA 1.9 kutokana na faini za ukamataji wa makosa ya usalama barabarani kwa kipindi cha kuanzia siku ya kwanza ya February 2016 mpaka tarehe 22 February 2016.

Taarifa yao imekuja siku moja baada ya Wizara ya fedha kutangaza jana kukusanya mapato ya serikali na kufikia zaidi ya TRILIONI MOJA kwa mwezi February 2016 pekee ambao bado haujamalizika kikiwa ni kiwango tofauti na mwaka uliopita ambapo walikua wakikusanya kwenye Milioni 800 n.k.
Share:

Mnaotarajia Kuoa au Kuolewa Chukueni Tahadhari Hii Mapema Usijejuta

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Ewe mwanaume ukioa mwanamke:

Mrefu, jua kwamba utaoa mwanamke mpenda maendeleo, mchapa kazi na mkarimu ila hawajui mapenzi na ni wavivu kujiweka safi kimazingira.

Mfupi kiasi, jua ya kwamba utaoa mwanamke mchangamfu na mpenda elimu sana ila tu wanapenda mnongono na hawaridhiki.

Mfupi kabisa.Jua ya kwamba utaoa mwanamke msikivu na mcha Mungu ila ni waroho kwa kula na wabishi sana.

Ewe mwanamke ukiolewa na mwanaume:

Mrefu, jua ya kwamba utaolewa na mwanaume mwenye upendo, utu na ubinadamu ila ni wabahili mno na hawapendi kupendeza.

Mfupi kiasi, jua ya kwamba utaolewa na mwanaume mwenye fikra na akili timamu za maendeleo, mbunifu, mcheshi na fundi wa mahaba ila ni wapenda ushirikina sana, wana wivu na wambea sana na mara nyingi hupenda kupiga chabo kwa watu wanaofanya mapenzi.

Mfupi kabisa, jua ya kwamba utaolewa na mwanaume mwaminifu, msikivu, mnyenyekevu ila huwa wepesi wa kujiua, kukata tamaa upesi, wanawivu sana na hawapendi kuoga.
Nawatakieni kila la kheri wale wenye wapenzi na ambao mnajiandaa kuoa au kuoelewa ila zingatia sana tabia hizo hapo juu za huyo unayetegemea kufunga nae pingu za maisha ili usije kutusumbua baadae. Chukueni tahadhari!
Share:

President Museveni Stoned By Rebellious Ugandan Kids (Video)


INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


President Museveni won the Thursday 18th poll by a landslide but funny Ugandans are not celebrating. Even kids don’t want the incumbent head of state!!

Yoweri Museveni emerged as the victor of the recently concluded Uganda’s presidential elections even though analysts pointed out various irregularities in the election.

Scooping a whopping 60% of the votes cast, you would expect Museveni to be a man of the people but his case is more of an enemy of the people.



Ugandan children were caught on camera stoning the de facto leader as they chanted words probably cursing him. (They were speaking in Luganda).

Watch the video below:

Share:

WAFUATAO WANAITWA KWENYE USAILI BIMA YA AFYA-NHIF DAR ES SALAAM

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
The Fund is informing all the candidates who applied for the November ,2015 advertised job that the names of the shortlisted candidates can be accessed on the following link http://www.nhif.or.tz/index.php/careers1
Interview will take place at Dar es Salaam University College of Education (DUCE) on 07th -11th March, 2016.
All applicants should observe the following during the interview;
  • Provide Original Certificates
  • Use of application number (as provided in the listed list) instead of names
  • Venue
  • Candidates for Driver position should provide original and valid driving license
  • To be in the interview rooms by 8:30 am, kindly observe time.

The Acting Director General
National Insurance Fund,
P.O. Box 11360
Dar Es Salaam
Toll Free: 0800 110063
Email:info@nhif.or.tz
Website: www.nhif.or.tz


Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARY 24 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY





Share:

Tuesday, 23 February 2016

Jerry Muro Atoa Mpya ''Simba si Washindani Wetu Tena...Watabaki Kuwa Watani Wetu Kama Wagogo na Wasukuma"

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Klabu ya soka ya Yanga imetangaza rasmi kuwa kuanzia leo wekundu wa Msimbazi Simba si washindani wao tena bali ni watani wa jadi kama walivyo wasukuma na wagogo.
Tamko hilo limetolewa hii leo na mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa wanajangwani hao Jerry Muro wakati akitoa salam za pongezi kwa wachezaji, benchi zima la ufundi na wanachama kwa kufanikisha kile walichokifanya Jumamosi iliyopita kwenye mtanange wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara walipoinyuka 2-0 Simba.
Aidha Muro ameongeza kuwa kwa sasa wanachotazama ni shughuli tatu zilizo mbele yao mechi ya kombe la shirikisho dhidi ya JKT Mlale, mchezo wa klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Cercke de Joachim ya Mauritius na mechi dhidi ya Azam ikiwa ni ya ligi kuu Tanzania bara.
Aidha amesema kuwa kikosi cha Yanga kimeanza mazoezi katika uwanja wa chuo cha polisi Kurasini kwa ajili ya mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya JKT Mlale Jumatano na mara baada ya mchezo huo kitaendelea na maandalizi ya mechi ya marudiano dhidi ya Cercle de Joachim.
Share:

Mapenzi Ndio Basi Tena...Wema Sepetu Afuta Picha zote za Aliyekuwa Mpenzi wake Idris Sultan Kwenye Page yake ya Instagram

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Looks like there is trouble in paradise.. Katika hatua ambayo wengi hawakuitarajia kama ingetokea mapema hivi, Wema Sepetu na Idris Sultan wanaonekana kuuvunja uhusiano wao.
Tetesi za kuwa uhusiano wao upo kwenye mawe zilianza baada ya ujauzito ambao Wema Sepetu alidaiwa kuwa nao kutoka.

Haijulikani ni nani kamkosea mwenzake lakini inaonekana kuwa ni Wema ndiye aliyechukia zaidi kiasi cha kuamua kufuta picha zote za Idris alizowahi kuzipost kwenye akaunti yake ya Instagram.

Wema aliwahi kueleza wazi jinsi ambavyo Idris alikuwa akimpenda Idris na namna alivyomfanya awe mtu mwema.

IDRIS SULTAN: NILIKUWA NAWAPENDA WEMA NA SAMANTHA KWA WAKATI MMOJA, ‘I WAS A VERY BAD GUY

Hata hivyo Idris anaonekana bado moyo wake haujamkatia tamaa Miss Tanzania huyo wa zamani. Jumapili alipost picha akiwa naya na kuandika: Only you know how much i love you, the rest doesn’t matter. #BeingAMan.”

Wengi walikuwa wameanza kuvutiwa na uhusiano wao na waliamini kuwa wawili hao wangekuja kuwa miongoni mwa couple zenye nguvu zaidi. Walikuwa wamepanga pia kuja na reality TV show yao.
Share:

CUF Watoa Tamko Zito Kuhusiana Na Kukamatwa Kwa Mwanamkakati wa Maalim Seif

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Wiki iliopita, mnamo tarehe 16 Februari, 2016, aliyekuwa mjumbe wa Timu ya Kampeni ya Chama Cha Wananchi (CUF), Ndugu Mohamed Ahmed Sultan Al-Mugheiry (maarufu kwa jina la Eddy Riyami), alipokea barua ya wito kutoka kwa Jeshi la Polisi Zanzibar ikimtaka kufika Makao Makuu ya Polisi, Ziwani, Zanzibar siku inayofuata, yaani tarehe 17 Februari, 2016, saa 2 asubuhi kwa kile kilichoelezwa kwamba “kuna mambo muhimu yanayomhusu” ambayo walitaka kuzungumza naye.
Bila ya kukosa, Eddy Riyami aliitikia wito huo na kufika Makao Makuu ya Polisi, Zanzibar na kuonana na SSP Simon S. Pasua wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CID). 
Hata hivyo, hakuhojiwa na badala yake alipewa simu na kutakiwa azungumze na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Bw. Salum Msangi ambaye alimwambia arudi tena Jumatatu, tarehe 22 Februari, 2016.
Eddy Riyami, akiwa raia mwema, alirudi tena jana kama alivyoagizwa. Alipofika hapo alihojiwa na Polisi na baadaye mwanasheria aliyefuatana naye akatakiwa kutafuta wadhamini wawili watakaomdhamini hadi atakapoitwa tena. 
Wakati mwanasheria wake aliporudi na wadhamini, akaelezwa kwamba Polisi imebadili uamuzi wake na imeamua kumuweka ndani hadi leo, tarehe 23 Februari, 2016. 
Mwanasheria na familia yake wakatakiwa kwenda tena Makao Makuu ya Polisi hiyo leo, saa 3 asubuhi. Walipofika leo asubuhi, wakaambiwa kwamba DCI kaacha maagizo kuwa suala la Eddy Riyami liachwe kwanza na wao warudi tena saa 6 mchana.
Hadi tunapotoa taarifa hii, hakujapatikana maelezo yoyote ya msingi juu ya kinachoendelea na wala Eddy Riyami hajafikishwa Mahakamani kusomewa mashtaka yoyote.
La ajabu zaidi, ni kwamba hata mke wake alipofika kituo cha polisi cha Madema anakoshikiliwa kwa ajili ya kwenda kumuona, hakuruhusiwa kumuona. 
Kutokana na mwenendo huu, Chama Cha Wananchi (CUF) kinalichukulia suala hili kwamba ni mwendelezo wa vitendo vya unyanyasaji wa kisiasa dhidi ya wapinzani wa CCM, vitendo ambavyo tunaamini vinafanywa kwa shinikizo la wanasiasa.
Itakumbukwa kwamba kwa muda mrefu tokea wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015 tumekuwa tukitoa tahadhari za kuwepo mipango ya kuwakamata viongozi wa CUF na wanaharakati wengine ili kufanikisha malengo ya kisiasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Tuna kila sababu ya kuamini kwamba hatua ya kumkamata Eddy Riyami na kumuweka ndani bila ya kumfikisha Mahkamani ni utekelezaji wa mipango hiyo. La si hivyo, ikiwa Eddy Riyami ametenda kosa basi angelishafikishwa Mahkamani ndani ya muda wa saa 24 tokea kukamatwa kama sheria inavyotaka.
Chama Cha Wananchi (CUF) kinalitaka Jeshi la Polisi kuacha kutumiwa na kutumika kisiasa kufanikisha malengo ya kisiasa ya CCM. 
Tunashangazwa kwamba siku zote wanaoitwa kuhojiwa, kukamatwa na kuwekwa ndani ni wanasiasa wa vyama vya upinzani na wanaharakati wengine lakini hatujawahi kushuhudia viongozi wa CCM kuitwa kuhojiwa, kukamatwa na kuwekwa ndani.
CUF imetoa taarifa kadhaa kwa Jeshi la Polisi zinazohusu matamshi na vitendo vya viongozi wa CCM vyenye mwelekeo wa uhalifu lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Hizo ni dalili za waziwazi za Polisi kutumiwa na kukubali kutumika kisiasa.
Tunalitaka Jeshi la Polisi iwapo kweli lina kesi dhidi ya Eddy Riyami basi limfikishe Mahkamani haraka ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake.
Na iwapo hawana kesi, basi wamwachie huru mara moja. Umefika wakati wa Jeshi la Polisi kufanya kazi zake kitaalamu kama sheria na kanuni zao zinavyoagiza badala ya kuwatumikia wanasiasa wa CCM.

HAKI SAWA KWA WOTE
HAMAD MASOUD HAMAD
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI NA MAWASILIANO NA UMMA – CUF
23 Februari 2016
Share:

Hemedy PHD na Rich Mavoko Wamewahi Kugombana Kwaajili Yangu - Gigy Money

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Akiongea katika kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Television, Gigy alisema kuna baadhi ya wasanii alishawahi kuwa nao kwenye mahusiano akiamini watamtoa kimaisha, lakini ilikuwa kinyume na kuishia kuchezewa tu.

"Mimi nilishawahi kudate na Hemed PHD nikiamni atanitoa nitatoboa, lakini wapi, Hemedi alishawahi kugombana na Rich Mavoko kwa ajili yangu, tena kipindi hiko niko form two, unajua maisha kila mtu kuna aliyopitia, nilishawahi kuwa na mtu ambaye hata hatuendani lakini nilikuwa nalazimika, mtu ameshanimilikisha gari, nyumba, tukitoka nalazimika kuvaa angalau nifanane nae kiutu uzima", alisema Gigy.

Akiendelea kuelezea harakati za maisha yake anasema pamoja na Rich Mavoko kugombana na Hemedi, lakini pia alishawahi kumuharibia kwenye mahusiano yake ambayo alikuwepo kwa wakati huo, na kumtaka kuacha tabia za kike.
"Richard akaharibu mahusiano yangu, Richard kama Richard aache tabia za kike", alisema Gigy
Share:

Mtoto wa Kanye West Amchanganya Wema Sepetu.....

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Siku moja baada ya mastar wakubwa Kim Kardashian na Kanye West kupost picha ya mtoto wao wa pili aitwaye ‘Saint West’ ameonesha kumchanganya sana bidada Wema Sepetu kwa kile alichokifanya kwenye mitandao yake ya kijamii.


Wema Sepetu jana amepost picha zaidi ya tatu Instgram za mtoto huyo huku akionesha ni jinsi gani ametokea kumpenda mtoto huyo na kudai ni mzuri sana, lakini haikuishia hapo Wema Sepetu aliamua kuweka picha hiyo kwenye Profile yake Instgram na kuweka picha hiyo kama Wall Paper na Screen save kwenye simu yake.

“Gnyt now… But Kimberly Kardashian sio kwa mtoto mzuri hivi jamani. Kama Pipi…!!! Mashallah jamani… God…! You are Able…! Saint West mzuri mno jamani… Dis Baby Boy too pretty ooo” Aliandika Wema Sepetu.

Kutokana na kitendo hicho mashabiki wa Wema ambao wanafahamika kama Team Wema walianza kumfariji Wema na kumpa maneno yenye faraja na yenye kumtia moyo kuwa ipo siku na yeye atapata mtoto, kwani Mungu ndiye anapanga kila jambo.

“Mungu hutoa kwa wakati wake na kwa sababu zake. Kama alivyowaona wengine na wewe atakuona hivyohivyo. Naatakupa haja ya moyo wako. Mungu tu ndio atakae weza kukusaidia my dear wema. Worry out your time will come soon keep on hoping that I love u.” Aliandika Hoperitha Minja

“Usijali iposiku utakuja kuzaa na mwanaume wa furaha yako ulio mpenda na yeye akakupenda, ninavyo kupenda kama mtanzania mwenzako kilasiku nakuombea kwa Mungu akupe afya na maisha marefu uzidi kututungia kazi nzuri na zitambulike dunia nzima I love you Wema” Aliandika king._of_ma_love_davi

Ingawa si watu wote walipendezwa na maneno ya Wema Sepetu kumsifia mtoto huyo ndipo hapo aliwaamsha watu ambao wamezoea kumtolea maneno machafu na wanaotumia lugha chafu na za kuudhi si kwake tu bali hata kwa watu waliostaarabika na watu wenye utu, kwani wasingweza kutumia maneno ambayo wanajua wazi yanaweza kuumiza wengine.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger