Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Thursday 4 June 2020

FULL POWER , ZAT 50 NI SULUHISHO LA KUDUMU TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50



⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4


⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

WAZIRI JAFO AZINDUA MRADI WA BARABARA KIGOMA UJIJI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jafo akizundua barabara ya km 12 ya zaidi ya Sh bilioni 18 katika Manispaa ya Kigoma Ujiji leo.

Na Moureen Tesha - Kigoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jafo amezindua mradi wa barabara wenye zaidi ya thamani ya bilioni 18 katika manispaa ya Kigoma Ujiji, uliojengwa chini ya mradi wa uendeshaji wa miji na majiji kimkakati Tanzania TSCP kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Akizindua mradi huo hii leo Alhamis Juni 4,2020 Waziri Japo amesema lengo la serikali ni kuhakikisha miji na majiji kote nchini inabadilika kwa kujengwa kwa kiwango cha lami bora, na kuweka taa za kisasa huku akiridhika mradi huo kwa namna ulivyo jengwa kwa lami ya kisasa na nzito.


Jafo amesema barabara hizo za Manispaa ya Kigoma Ujiji ni miongoni mwa barabara zinatekelezwa katika miji nane nchini akiwemo Mwanza,Dodoma, Mtwara, Tanga,Arusha kwa fedha za mkopo nafuu zaidi ya dola za kimarekani Milioni 343 sawa na zaidi ya Sh bilioni 800.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga amewataka wananchi kuboresha mazingira ya makazi ili kuendana na hali ya mji ulivyo kwa sasa ambapo wakazi wengi huishi kwenye nyumba za majini jambo ambalo amekuwa akilikemea mara kwa mara.

Nao wakazi wa manispaa ya Kigoma Ujiji wamepongeza hatua ya serikali kujenga barabara hizo za kiwango cha lami nzito na kwamba shughuli za uzalishaji zimeongezeka ikiwemo za madereva bodaboda na bajaji, hatua ambayo imepunguza wimbi la uporaji mitaani.

Mkazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Maclena Paulo, amesema uwepo wa barabara hizo kumerahisisha usafiri na mizunguko ya wananchi.
Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo akizungumza na wananchi kabla ya  kuzindua barabara ya km 12 ya zaidi ya Sh bilioni 18 katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Share:

Polisi Wengine Watatu Washitakiwa Kwa Mauaji ya Mmarekani Mweusi George Floyd

Mwanasheria Mkuu wa Minnesota, Keith Ellison ametangaza kuwa maafisa watatu wa Polisi waliokuwepo wakati George Floyd anakandamizwa shingoni hadi kufariki wamefunguliwa mashtaka

Thomas Lane (37), J. Alexander Kueng (26) na Tou Thao (34) wameshtakiwa kusaidia mauaji ya daraja la pili. Mashtaka ya Afisa aliyemuwekea goti Floyd, Derek Chauvin yamebadilishwa na sasa anatuhumiwa kwa mauaji ya daraja la pili

George Floyd alifariki dunia baada ya Chauvin kumkandamiza na goti shingoni huku maafisa wengine wakishuhudia. Mara baada ya kifo chake, Polisi hao wote walifukuzwa kazi lakini Chauvin pekee alishtakiwa kwa mauaji

Baada ya wote wanne kushtakiwa, Mwanasheria wa familia ya Floyd, Benjamin Crump amesema hii ni hatua kubwa kuelekea kupata haki na wamefarijika kwamba uamuzi huo umetolewa kabla George hajazikwa


Share:

UMEMEJUA WAPIGA JEKI ELIMU SHULE YA SEKONDARI MORETO


Na Nyamiti Kayora

Shule nyingi za Sekondari hususani za vijijini zimekuwa zikikabiliwa na ukosefu wa nishati ya kuendesha maabara na mwanga wa kujisomea kwa wanafunzi waishio katika mazingira ya shule (bweni).



Uhaba huo umesababisha maeneo hayo kutofanya vyema kimasomo kuliko wale wenye nishati hiyo.

Shule zinazojiweza zimeweka umemejua wakati baadhi ya zile zisizokuwa na uwezo huo hasa za umma zimekuwa zikifadhiliwa na wahisani mbalimbali kama ilivyo shule ya sekondari Moreto. Shule hii ya sekondari Moreto ambayo ni ya bweni iko kwenye kijiji cha Mindutulieni,wilayani Chalinze mkoani Pwani.

Shule hii ilianzishwa na Chifu wa kabila la kimasai Moreto Lapa aliyekuwa akiongoza ukoo wa kimasai na jamii nzima ya kifugaji kwa mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro.

Chifu Moreto alitoa wazo la kujenga shule na alihamasisha wanakijiji kujenga madarasa manne kisha Serikali ikaendeleza ujenzi na kuifanya shule kuwa na madarasa 13 ili kukidhi mahitaji ya mwingiliano wa jamii ya wafugaji na wakulima kijijini hapo.

Tangu kuanzishwa kwa shule hii mwaka 2011, haikuwahi kuwa na nishati yoyote ya umeme hadi mwaka 2017 ilipopata umeme jua.

Kazi kubwa ya umemejua shuleni hapo ni kuendesha maabara kwa masomo ya sayansi, kuwaangazia wanafunzi kwenye mabweni wakati wakijisomea masomo ya jioni baada ya kukamilisha vipindi vya darasani.

Vilevile umemejua huo umewezesha mazingira ya walimu kuishi shuleni hapo.

Moja kati ya wanafunzi waliohitimu mwaka 2019, Jacob Ibrahimu anasema walikuwa wakitumia tochi tangu alipoanza kidato cha kwanza hadi cha tatu hali ambayo iliwafanya baadhi kuacha shule kwa kukosa pesa za kununua betri.

“Tulikuwa tunatumia vitochi, hali hii iliwafanya wengine kutokuhudhuria darasani, ila tulipofika kidato cha tatu ndipo wakaleta sola, walimu waliongezeka na walianza kutufundisha masomo ya sayansi kwa vitendo katika maabara,” alisema Jacob.

Mbali na kuepusha gharama za betri na wanafunzi kuacha shule, umemejua huo umefanya wanafunzi waanze kufaulu masomo.

Janeth Ibrahimu mwanafunzi shuleni hapo anabainisha kuwa umemejua uliowekwa shuleni kwao umewasaidia kuongeza ufanisi katika masomo yao hasa kwa masomo ya sayansi.

“Sasa tunasoma masomo ya sayansi vizuri , lakini bado umeme unaleta changamoto mvua zikifululiza hivyo, tunaomba serikali ituwekee mazingira ya kupata umeme wa uhakika,”alisema Janeth.

Makamu mkuu wa shule ya Moreto mwalimu Ngasa Charles Madata anasema umemejua huo walioupata kupitia wadau wa nishati jadidifu shirika la Innovation Afrika 2017,umesaidia wanafunzi kuachana na kadhia ya kujisomea kwa kutumia tochi za betri hali iliyoathiri maendeleo ya kielimu hasa katika mitihani ya kidato cha nne .

“Hali ya ufaulu ilikuwa chini sana na wanafunzi wengi walikuwa wakiacha shule,ila baada ya ujio wa hizi sola, utoro umepungua na ufaulu ulianza kujitokeza mwaka huo huo wa 2017,” alisema Mwalimu Mdata.

Kwa mjibu wa Takwimu za matokeo ya kidato cha nne toka Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) wanafunzi 32 walifaulu mwaka 2016 kati ya 60.

Mwaka 2017 wanafunzi 33 walifaulu kati ya wanafunzi 67.

Huku mwaka 2018 walifaulu wanafunzi 34 kati ya 53.
Aidha mwaka 2019 walifaulu wanafunzi 51 kati ya 70 ikiwa ndiyo ufaulu wa juu kufikiwa ndani ya muda mfupi.

Licha ya ongezeko la wanafunzi kufaulu shuleni hapo, na kupenda kusoma masomo ya sayansi kutokana na maabara iliyopo kuanza kufanya kazi mwaka 2019,imeelezwa bado wanakumbana na changamoto ya kuwa na chumba kimoja cha maabara kinachopelekea masomo yote ya sayansi yafanyike humo.

“Tangu kuanza kutumika kwa maabara mwanafunzi wengi wanatamani kusoma masomo ya sayansi,na hali hii inatupa shida kidogo kufanya practical za masomo hayo hasa pale zinapofatana mana tuna maabara moja,”aliongeza mwalimu Madata.

Pia Umemejua shuleni hapo umewafanya angalu walimu wavutike kuendelea kufundisha.

“Tangu tumepata umeme nimehamia shuleni hapa,ingawaje umeme wetu huu si wa kudumu lakini navutika hata kuwafundisha wanafunzi usiku,” aliongeza Mwalimu Hamisi.

Jamii ya Kijiji cha Mindutulieni pia wanaona fahari ya uwepo wa umemejua katika shule ya Moreto unaonyesha matumaini kwa elimu ya watoto wao.

Furaha yao kubwa ni kuona ufaulu kwa watoto wao ukiongezeka na kuwapa chachu wanafunzi kusoma masomo ya sayansi wanayoamini miaka ya mbeleni watapa wataalumu wengi wa kisayansi kijiji hapo.

Moja kati ya wazazi kijijini hapo Magreth Katei anasema amefurahi kupunguziwa mahitaji ya mwanafunzi awapo shule na amefarijika mwanae kusoma masomo ya sayansi.

“Sola zimetupunguzia gharama sisi wazazi, sahivi hatununui tena tochi wala betri,pia mwanangu anasema kuna mabara hivyo anasoma sayansi, yani namuombea awe Daktari ili aje atusaidie katika familia,” alisema Magreth.

Pamoja na furaha hiyo bado wazazi wanatamani kupata umeme kijijini kwao ili watoto wanapofunga shule wawe na uhakika wa kujisomea nyumbani.

“Tunatamani sana kupata umeme huku majumbani, kwani watoto wakifunga shule ni changamoto, unakuta tunatumia tochi moja sijui upikie jikoni mtoto naye anataka kusoma, kweli hapa inakuwa shida,”aliongeza Magreth.

Naye Deogratius Shayo, Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari Moreto anasema mwaka 2015 ndo alishika wadhifa huo na kulikuwa na changamoto ya umeme hivyo kitaaluma ingeshuka tu kwani wanafunzi wasingeweza kufanya vizuri katika mazingira ya giza.

“Kwa kweli tangu tumepata umeme Watoto wanaelewa, na walimu wamejitolea kufundisha muda wa ziada hasa wanafunzi wa kidato cha pili na nne kwa kuwajengea uwezo zaidi na ufaulu kweli umeongezeka,” alisema Shayo.

Wachambuzi wa masuala ya elimu wanasema ufaulu wa mwanafunzi hautegemei umeme tu, bali hata mazingira tulivu anapoishi, uwezo na malezi,ingawa kwa miaka ya sasa umeme unatajwa kuwa muhimu zaidi hasa kwa masomo ya Sayansi.

Profesa Omary Minz kutoka chuo cha Muhimbili anabainisha kuwa, shule zenye changamoto ya kutokuwa na umeme wa Grid ya Taifa watumie nishati jadidifu ili kusaidia ufanisi wa ufaulu wa masomo ya sayansi.

“Uwepo wa umeme katika shule za sekondari ni muhimu na ni muhimu kupindukia hasa katika kufanikisha masomo ya sayansi yanayomtaka mwanafunzi kutumia maabara kusoma kwa vitendo,”alisema Prof. Minz.

Si kufaulu tuu katika masomo ya sayansi bali Profesa Minz aliongeza kuwa mwanga shuleni unasaidia pia kumpatia chachu mwanafunzi kusoma kwa bidii nyakati za usiku au alfajiri ambapo wengi wamepumzika na mazingira kuwa na utulivu.

“Sisi tulikuwa tunaamka usiku kujisomea, unalala saa nne usiku kwenye saa kumi alfajiiri kale ka utulivu unaamka akili ikiwa imetulia unasoma, sasa kama hakuna mwanga hata wa sola kwa kweli ufaulu kwa wanafunzi utausikia kwa wachache,”aliongeza Prof. Minz.

Kufuatia hali hii inayoleta tija ya utumiaji wa nishati jadidifu ya mwanga wa jua, makamu mwenyekiti wa jumuiya ya wazalishaji wa nishati hizi Tanzania, mhandisi Prospel Magali ambaye pia ni mkurugenzi wa miradi ya ENSOL Tanzania anasema umemejua umekuwa mkombozi wa shule nyingi nchini Tanzania.

Magali anasema taasisi nyingi zilizo pembezoni mwa miji na ambazo hazijafikiwa na umeme wa grid ya taifa zimekuwa zikinufaika na nishati jadidifu.

Amesisitiza pia watumiaji wa nishati jadidifu wanao wajibu wa kuchagua vifaa vyenye ubora na kuzingatia makadilio sahihi ya matumizi ya umemejua na vifaa gani na vitumikeje.

Aidha aliongeza kuwa mtuaji azingatie Makadilio sahihi ya kitaalamu ya mfumo wa umemejua unaoendana na matumizi sahihi ya umeme.

Hata hivyo amesema nishati jadidifu zimekuwa mkombozi kwa shule nyingi ambazo sasa zinaendesha masomo ya sayansi kutumia maabara na kuongeza chachu ya ufaulu kwa wanafunzi akitolea mfano shule ya msingi Mpale iliyopo wilayani Korogwe mkoani Pwani ambayo imefaidika na umeme jua toka kampuni ya ENSOL uliochangiza ufaulu shuleni hapo.












Share:

SERIKALI YA MAREKANI YATOA DOLA MILIONI 3.6 KUPAMBANA NA COVID-19 TANZANIA


 
Serikaliya Marekani imetenga kiasi cha dola millioni3.6 ( Shilling billioni  7.8) kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Tanzania katika mapambano dhidi ya janga la Korona (COVID-19).

Pia serikali hiyo imetoa kiasi cha dola millioni 1.9 ( shilingi Billioni 4.4) kupitia shirika lake la msaada la USAID ili kuisaidia Tanzania kukabiliana na mlipuko huo.

Mwakilishi Mkazi wa shirika la USAID
nchini Tanzania Andy Karas alisema haya katika mkutano wake na waandishi wa habari. Alisema kuwa kuwa ni jambo la muhimu sana kuendeleza juhudi nyingine za kusaidia huduma za afya hata kipindi cha mlipungu wa janga hili la COVID-19

“ Kiasi hiki kinakadiriwa kuwa jumla ya dola
milioni 5.3 ambazo zilitolewa katika programu ya rasilimali,
Mawasiliano kuhusu athari ya magonjwa kuboresha mawasiliano, upatikanaji wa maji na usafi wa mazingira Kudhibiti na kuzuia maambukizi zaidi,”

“Ukijumuisha msaada wa pesa mpya na pesa kutoka miradi mingine zilizobadilishiwa kazi, jumla inakuwa ni dola za kimarekani milioni 5.3 (sawa na shilingi
bilioni 12.2 fedha za kitanzania).,” Alisema Karas .

Alielezea zaidi kuendelea kujitoa ili kushirikiana na kusaidiana na jamii ili kuhakikisha kuwa rasilimali za kutosha zinawekezwa kusaidia mapambano dhidi ya COVID 19 nchini.

Karas alisema kuwa msaada huo kwa Tanzania, ni sehemu ya takribani dola billioni 6.5 zilizotolewa na watu
wa serikali Marekani na wasio wa serikali ikiwa ni msaada wa jumla kwa dunia ili kusaidia mwitikio wa COVID-19 ambapo msaada huo ni sawa na asilimia 60 ya jitihada kwa dunia nzima.

Mkurugezi mkazi wa USAID pia alielezea ahadi na utayari wa Serikali ya Marekani ya kuendelea kuishauri Serikali ya Tanzania ili kuweza kushinda vita dhidi ya COVID-19 Kituo cha Kudhibiti na kuzuiaMagonjwa (CDC)

Kwa upande mwingine, Karas alidhihirisha msaada mkubwa uliotolewa na Kituo cha Kupambana na Magonjwa (The U.S. Centers for Disease Control and Prevention (CDC)ambacho kimetoa dolla milioni 3 katika mfuko mpya fedha
zake na kutenga zaidi ya dola 600,000 katika fedha zake zilizokuwa
zimepangwa kwa matumizi mengine ili kuunga mkono katika uchunguzi, maabara, na kuzuia na kupambana na maambukizi ya CIVID 19 nchini Tanzania.

Alisema kuwa CDC itaendelea kutafuta njia bunifu ili
kusaidia juhudi za mwitikio hasa msaada wa kiufundi na usimamizi huduma za afya za Mikoa na Wilaya. Na kuwa kwa sasa CDC inasaidia  maeneo yafuatayo:

Aliongeza kuwa CDC inaendelea kutafuta njia za
ubunifu kusaidia juhudi za kukabiliana na janga ikiwa ni pamoja na
kusaidia walengwa ambao ni timu ya wataalamu wa afya ngazi ya
mkoa/wilaya. Jitihada zilizofanywa na CDC ni pamoja na:

CDC ilikuwa imejikita katika uchunguzi wa wagonjwa wa kwanza wa COVID-19 nchini Tanzania (bara na Zanzibar). Ilitoa msaada wa rasilimali za uchunguzi, mikakati na interventions.

Pia, Timu ziliandaliwa katika mikoa mbali mbali ili kuleta mwitikio na kutoa msaada wa kitaalamu. Pamoja na kazi nyingine, timu ziliendelea kufanya uchunguzi, contact tracing tools

Kwa upande wa ufanisi wa upimaji wa
COVID-19, zaidi ya dolla milioni 1.8 imetengwa kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za maabara nchini, ambapo takribani dolla 270,000 imekwisha tolewa kwa ajili ya vifaa vya maabara, na uchunguzi.

Athari za COVID-19 (Kwa sekta mbalimbali)
Kutokana na madhara ya maradhi ya COVID-19 na usitishwaji wa ndege za kimataifa, uuzaji wa mazao ya matunda na mboga mboga ( horticultural products) ulisitishwa kwa muda, na kusababisha madhara katika uzalishaji na ajira.

Bidhaa nyingi za matunda na mboga mboga
nchini Tanzania, huandaliwa kwa ajili ya usafirishaji nje ya nchi
(export market), ambapo uhitaji (demand) ni mkubwa kuliko uzalishaji (suppy), hivyo  USAID inawekeza katika taasisi ya Tanzania Horticultural Association (TAHA) na Serikali ya Tanzania.

Juhudi pia zinahusisha kutoa muda wa maongezi kwa walimu upima na kusambaza  ujumbe juu ya uzuiaji wa COVID-19 (ikihusisha usafi),Ukatili kinyume na wanawake na wasichana unaongezeka kidunia huku kukiwa na maradhi COVID- 19, Tanzania haina tofauti na nchi nyingine.

Share:

Rukwa: Hoja za CAG zawaweka matatani watumishi watatu wa Halmashauri

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Nkasi kuwakamata watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kwa kula fedha zilizotokana na makusanyo ya Halmashauri na kujikopesha bila ya kuziwasilisha Benki na hatimae kuendelea kuibua hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali nchini (CAG).

Mh. Wangabo ameipa TAKUKURU siku saba kuhakikisha watumishi hao waliokula kiasi cha Shilingi 27,674,300/= wanarudisha fedha hizo na endapo watashindwa kufanya hivyo basi wafikishwe mahakamnami haraka iwezekanavyo na kuonya kuwa wadaiwa wa makusanyo ya halmashauri wamekuwa kama ugonjwa wa saratani uliokosa dawa huku Mkurugenzi na Madiwani wanaosimamia halmashauri hiyo wakishindwa kuwawajibisha.

“Nimeambiwa hizi fedha zinawahusu watumishi wa halmashauri watatu, mmoja anadaiwa milioni nane, na wengine wawili milioni tisa tisa, imesemwa tu wachukuliwe hatua za kisheria, lakininhaikutoa muda, hadi lini hawa watu wawe wamechukuliwa hatua hizo za kisheria, n ahata kwenye maeneo mengi hakuna muda wa kushughulikia hizi hoja kwamba kufikia tarehe Fulani hii iwe imekwisha, hakuna, sasa hawa watumishi watatu, TAKUKURU mko hapa, kamata hawa watumishi watatu, shughulikeni nao haraka iwezekanavyo kuanzia leo,” Alisema.

Pia ameeleza kuwa kwa mujibu wa taarifa za CAG kwa mwaka wa fedha 2018/2019, mapato yaliyokusanywa bila ya uthibitisho wa kupelekwa benki ni shilingi 47,725,415/= huku shilingi 20,051,115 zikiwa zimerudishwa, lakini wadaiwa hao hawajirekebishi na matokeo yake taarifa za mfumo wa ukusanyaji wa mapato hadi tarehe 31, Mei, 2020 unaonesha makusanyo ambayo hayajapelekwa benki kufikia Shililingi 53,813,308.38/= na hivyo kuiamrisha TAKUKURU kuwashughulikia.

Mh. Wangabo ametoa maelekezo hayo leo 3.6.2020 katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kuhusu utekelezaji wa hoja za Ukaguzi na Mapendekezo ya CAG ambapo pia amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha analipa madeni ya Madiwani ndani ya siku saba.

Mh. Wangabo amechukua hatua hizo ikiwa ni miongoni mwa utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Suleiman Jafo ambaye hivi karibuni katika ziara yake mjini Sumbawanga alimtaka Mkuu huyo wa Mkoa kutumia vyombo alivyonavyo kushughulika na wadaiwa wa fedha za makusanyo ambazo hazikuwasilishwa Benki.


Share:

RC Kagera Awataka Wanunuzi Wa Kahawa Kuingia Sokoni....Hatutaki Maneno Tunataka Wanunuzi Wenye Fedha

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Kagera
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti amesema kuwa serikali inaunga mkono wanunuzi binafsi kwenye zao la Kahawa japo wamechelewa sana kuingia sokoni kuanza kununua kahawa za wakulima.

Gaguti ameyasema hayo leo tarehe 4 Juni 2020 wakati akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania Prof Jamal Adam ofisini kwake Mkoani mjini Bukoba na kuwataka wanunuzi hao kuingia sokoni.

"Serikali haitaki maneno inataka wakulima wapate fedha kwa wakati, wanunuzi binafsi wamechelewa sana kuingia sokoni tulitegemea waingie sokoni tangu mwezi wa pili waanze kuingia makubaliano na Vyama vya Ushirika, lakini hawajachelewa sana waje ofisini kwangu waeleze wazi wanataka kahawa kiasi gani kisha tuingie makubaliano ya awali" Alikaririwa Rc Gaguti

Ameongeza kuwa Wanunuzi binafsi wanapaswa kujitokeza hadharani watoe ofa yao ikieleza kuwa wanataka kununua kiasi gani cha kahawa ili kuhuisha maneno yao kwa matendo.

Awali katika mkutano uliofanyika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Richard Ruyango alisisitiza kuwa serikali itaendelea kusimamia mipango yake katika zao la Kahawa hususani kuimarisha usimamizi madhubuti ili kuwa na kahawa Bora kwa kuongeza tija na Uzalishaji.

Kuhusu wanunuzi binafsi amesema kuwa wanapaswa kutekeleza sheria, na taratibu za ununuzi wa zao hilo ikiwa ni pamoja na kuwa na kibali cha ununuzi kinachotolewa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halamshauri husika pamoja na kuwa na leseni ya Biashara inayotolewa na Bodi ya Kahawa Tanzania.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Tanzania Prof Jamal Adam akizungumza na wanunuzi wa Kahawa katika kikao kazi kilichofanyika kwenye ukumbi wa ELCT Mjini Bukoba ameweka bayana utaratibu wa ununuzi wa kahawa ya wakulima katika Mkoa wa Kagera ambapo Wanunuzi watakaoruhusiwa kununua kahawa ni wale waliopata leseni za kununua kahawa kwa mujibu wa kanuni ya 26 ya Kanuni za Kahawa 2013.

Ameongeza kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri watapaswa kutoa vibali kwa haraka kwa wanunuzi wenye sifa ili kuiwezesha Bodi kutoa leseni kwa wakati.

Kadhalika, Prof Jamal amesisitiza kuwa Wakurugenzi wanapaswa kuwajulisha kwa maandishi waombaji watakaonyimwa vibali wakiweka bayana sababu za kutowapatia vibali na nakala ya barua hiyo iwasilishwe Bodi ya Kahawa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wao wanunuzi wa kahawa wamepongeza uamuzi huo wa serikali kuwaruhusu kununua kahawa kwenye vyama vya Ushirika huku wakiahidi kutekeleza taratibu na sheria za ununuzi wa Kahawa.

Akizungumza kwa niaba ya wanunuzi hao Afisa Masoko wa Kampuni ya Karagwe Estate Ltd Ndg Kamanzi Mombeki amesema kuwa Kampuni hiyo imejipanga kurejea tena katika ununuzi wa kahawa baada ya kusimamia kwa zaidi ya miaka miwili kufanya Biashara hiyo.

"Sisi kama Kampuni tunampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kurejesha wanunuzi binafsi kununua kahawa hivyo nasi tumerejea kwa nguvu na Ari kubwa katika ununuzi wa kahawa" Alisema Mombeki

Amesema kuwa maagizo yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kuhusu wanunuzi binafsi wakati akizungumza na wananchi wa Kyaka, Rwamisheye, Kemondo Muleba, Nyakabango na Kyamyorwa mkoani Kagera tarehe 11 Julai 2019 yalilenga kuongeza ushindani wa kibishara jambo ambalo linamnufaisha zaidi mkulima mwenyewe.

Mombeki ameonyesha kuwashangaa watu wanaopinga maelekezo ya Mhe Dkt Magufuli yenye lengo la kumkomboa mkulima.



Share:

Picha : KAMPUNI YA VINYWAJI VIKALI EAST AFRICAN SPIRITS (T) LTD YATOA MSAADA WA VIFAA VYA KISASA KUJIKINGA NA CORONA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SHINYANGA


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga inayotengeneza vinywaji vya Diamond Rock na Hansons Choice imekabidhi msaada wa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona vyenye thamani vya shilingi Milioni 8 katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.


Vifaa vilivyotolewa na Kampuni hiyo ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga ni pamoja na kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki chenye thamani ya shilingi Milioni 6.8 kikiwa na masinki matano na tenki la maji lenye ujazo wa lita 1000 na vifaa vingine vya kujikinga na COVID-19 ikiwemo Vitakasa mikono,barakoa,gloves, pamba, sabuni za maji, cord clamp na pulse Oximeter vyenye thamani ya shilingi milioni 1.2.

Msaada huo umekabidhiwa leo Alhamis Juni 4,2020 na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.

Akikabidhi vifaa hivyo, Gasper Kileo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) amesema vifaa hivyo vitatumika katika kuiongezea nguvu serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona.

“Ninaishukuru sana serikali  ya awamu ya tano inayoongozwa na Amiri Jeshi wetu Mkuu, Rais wetu Mpendwa, Dkt. John Pombe Magufuli namna ilivyopambana na ugonjwa wa COVID – 19. Tumepambana na COVID-19 tofauti na nchi zote duniani na sasa wote ni mashahidi kwenye vyombo mbalimbali vya habari na Mitandao ya Kijamii kwamba dunia sasa inaangalia Tanzania imefanya nini kuiondoa Corona. wenzetu ndiyo wanafuta kile tunachofanya Tanzania”,amesema Kileo.

“Nimpongeze pia Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack kwa namna mnavyopambana dhidi ya Corona. Lakini pia niwapongeze Madaktari wetu wote nchi nzima mmepambana kwa kushirikiana na serikali na Mungu ametusaidia tumeweza. Naomba tuendelee kupambana mpaka pale Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli atakaposema silaha zetu tuziweke chini”,ameongeza Kileo.

Mkurugenzi huyo pia amewashauri wananchi kuendelea kunawa mikono na kwamba zoezi hilo liwe endelevu hata siku watakapotangaziwa kuwa Corona imefutika nchini Tanzania.

Akipokea vifaa hivyo, Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack ameishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa mchango huo kwa ajili ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali katika mapambano dhidi ya Corona.

“Mheshimiwa MNEC uliniambia utaleta vifaa kwa ajili ya kupambana na Corona lakini sikujua kama utaleta vikubwa namna hii. Umetuwekea masinki ya kunawia mikono na tenki kubwa la maji na umeweka hadi kivuli ili watu wetu wanaponawa mikono wawe kivulini. Mwenyezi Mungu akubariki sana na abariki Biashara yako na shughuli unazofanya ziendelee na kukua ili uweze kutupa misaada mingine zaidi”,amesema Telack.

“Kimsingi mimi nimepokea vifaa hivi kwa niaba ya wananchi lakini hawa wananchi wanaonawa hapa wataendelea kukuombea kwa Mungu. Umetengeneza kitu kikubwa sana na pengine ndiyo maana walikuchagua kuwa MNEC wao hata wale wasiokuwa wa CCM sasa wanaona jinsi viongozi wa CCM na serikali ya CCM inavyojali wananchi. Huu ni mfano wa kutosha,niombe na viongozi wengine waige mfano wako”,amesema Mkuu huyo wa mkoa.

“Umeenda kisasa zaidi,umetuletea vifaa vya kisasa,na naomba uongozi wa hospitali hii uweke mtu wa kuwaelekeza wananchi namna ya kutumia kifaa hiki, wasianze kugusa gusa wakavunja hapa,wajue kwamba akisogeza mikono yake maji yanatoka. Na pengine hapa patakuwa mahali pa kujifunzia masuala ya teknolojia ya kisasa.

Yaani MNEC unafundisha watu teknolojia ambazo zipo,wataambiana ukienda hospitali,ukisogeza tu mkono maji yanatoka,yaani hiyo nayo ni sehemu ya kujifunzia. Ninategemea tutapata wageni wengi zaidi,wengine watakuja kunawa tu mikono ili waone jinsi maji yanavyoka bila kugusa,wananchi watakuja kujifunza. RMO naomba vifaa hivi vitunzwe ili visiharibike”,amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Katika hatua nyingine,Mkuu huyo wa mkoa amewataka wananchi kuendelea kunawa mikono mara kwa mara ili kupunguza maradhi mengine yanayotokana na kutozingatia taratibu za afya

“Kunawa mikono ni ustaarabu. Sasa hivi siyo COVID -19 peke yake tumegundua kwamba kunawa mikono kunatupunguzia maradhi mengine kama vile tumbo na kuharisha,huko wodini sasa hivi watu waliokuwa wanakuja kwa matatizo ya tumbo na kuhara wamepungua kwa kiasi kikubwa sana”,amesema.

“Niwaombe wananchi wa Shinyanga hii tabia ya kunawa mikono iwe endelevu siyo kwa sababu ya Corona tu,hata baada ya Corona unaingia hospitali nawa mikono yako,unaingia sokoni nawa mikono yako ili pia tuweze kupunguza maradhi mengine yanayotokana na kutozingatia taratibu za afya”,ameongeza Telack.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Timoth Sosoma ameishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa msaada huo na kueleza kuwa vifaa hivyo vitasaidia katika kukabiliana na ugonjwa wa Corona huku akiwataka wananchi wasiwe wagumu kunawa mikono.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Muonekano wa Masinki ya kunawia mikono bila kugusa koki ambayo ni sehemu ya kifaa cha kisasa cha kunawia mikono kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga inayotengeneza vinywaji vya Diamond Rock na Hansons Choice  kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga leo Alhamis Juni 4,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (katikati) akikata utepe wakati akipokea kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona kutoka Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (aliyevaa kilemba cha bluu) namna ya kunawa mikono kwa kutumia kifaa cha kisasa cha kunawia mikono.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga,Jasinta Mboneko akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga, Albert Msovela akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akiishukuru Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa mchango wa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu palipowekwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono iliyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu palipowekwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono iliyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu wa tanki la maji ambalo ni sehemu ya kifaa cha kisasa cha kunawia mikono kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu palipowekwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono iliyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya vifaa kwa ajili ya kujikinga na COVID-19 ikiwemo Vitakasa mikono,barakoa,gloves, pamba,cord clamp na pulse Oximeter vyenye thamani ya shilingi milioni 1.2 vilivyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akizungumza wakati akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (aliyevaa kilemba cha bluu kushoto) kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona  katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akiipongeza serikali inayoongozwa na  Rais Dkt. John Pombe Magufuli namna ilivyopambana na ugonjwa wa COVID – 19. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (wa tatu kulia) akiishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa mchango wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona
Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack sabuni ya kunawia mikono ili kukabiliana na COVID - 19 katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack Vitakasa mikono ili kukabiliana na COVID - 19 katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Timoth Sosoma akiishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa msaada wa vifaa vya kujikinga na COVID- 19 ambavyo vitasaidia katika kukabiliana na ugonjwa wa Corona katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis Amtuhumu Trump Kwa Kutaka Kuwagawa Wamarekani Kwa Matabaka

Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis  ametangaza kuwaunga mkono wananchi wa Marekani wanaondamana kulaani ubaguzi wa rangi na mienendo ya polisi ya Marekani hususan dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika.

Mattis alitangaza msimamo huo katika taarifa iliyochapishwa jana Jumatano na gazeti la The Atlantic, ambapo amemtuhumu Trump kuwa anajaribu kuwagawanya Wamarekani kimatabaka.

Ameeleza bayana kuwa, "Donald Trump ni rais wa kwanza katika uhai wangu ambaye hawaunganishi Wamarekani, bali hata hajifanyi kana kwamba anajaribu kuwaunganisha." 

Amesema taifa hili linashuhudia matokeo ya jitihada za makusudi za miaka mitatu za Trump za kuwagawa wananchi wa Marekani.

James Mattis amesema ;, "tunaweza kuungana bila yeye (Trump), hili si jambo jepesi, lakini linawezekana kwa ushirikiano."

Kadhalika amekosoa hatua ya rais huyo kutumia jeshi la taifa kuzima maandamano ya kiraia, ambayo ni haki ya msingi iliyoanishwa kwenye katiba ya nchi hiyo. 

 Mattis ambaye ni jenerali mstaafu aliachia ngazi mwishoni mwa mwezi Februari mwaka 2018, baada ya kuhitalifiana na Trump

 Kama jibu lake kuhusu ukosoaji huo, Trump alituma mfululizo wa ujumbe kwenye Twitter ambapo alisema..."Sikupenda mtindo wake( James Mattis  )  wa uongozi au yeye mwenyewe sikumpenda na wengine wengi wanakubaliana na hilo, "Afadhali  aliondoka mapema"


Wananchi wa Marekani wamekuwa wakiandamana kwa zaidi ya wiki moja sasa, tangu alipouawa kikatili na polisi mweupe, George Floyd, Mmarekani mweusi katika mji wa Minneapolis jimboni Minnesota.


Share:

Vigogo Wanne Wizara ya Maliasili na Utalii Wasimamishwa Kazi

Katibu Mkuu  Wizara ya Maliasili na Utalii ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Utalii, Deogratius Mdamu na kumsimamisha kazi Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa wizara, Flora Masami kutokana na mapungufu na ubadhirifu mkubwa kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Utalii (TDL).



Share:

Watatu Watiwa Mbaroni Dar es Salaam kwa tuhuma za mauaji ya dereva tax (UBER)

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya dereva tax (UBER) aliyefahamika kwa jina la Joseph Tillya Mpokala,(51),Mkazi wa Mbezi kwa Msuguli .

Watuhumiwa hao :-

1. Godson Laurent Mzaura,(29),Mkazi wa Mbezi Beach,Mpiga picha.

2. Said Mohamed Mahadhi (38),Mkazi wa Afrikana,Fundi simu na

3. Denis Urassa @ Pasua,(45),Mkazi wa Makongo Juu,Fundi simu.

Mnamo tarehe 26.05.2020 Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dsm lilipata taarifa kutoka kwa mke wa marehemu kuwa Mume wake ametoweka tangu tarehe 21.05.2020 na simu zake zote hazipatikani.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM kupitia kikosi chake cha kupambana na uhalifu kilianza ufuatiliaji mara mmoja.

Mnamo tarehe 27.05.2020 alikamatwa mtuhumiwa Godson Laurent Mzaura na kuhojiwa kisha kukiri kufanya mawasiliano na marehemu ambapo alieleza kuwa Mnamo tarehe 21.05.2020 majira ya saa saba mchana walimkodi marehemu ili awapeleke maeneo ya Mbezi na walipofika Mbezi Juu watuhumiwa hao walimuua Joseph Tillya na kumfukia kwenye shimo katika eneo la wazi lenye uzio wa ukuta ambao hujamalizika kujengwa(pagale).

Mnamo tarehe 02.06.2020 watuhumiwa Wote watatu walihojiwa kwa kina na kukiri kuwa walifanya mauaji hayo na kuchukua gari la marehemu lenye T 139 DST Toyota IST na kwenda kulificha huko Kimara Baruti katika nyumba ya wageni ya Api Forest logde.

Jeshi la Polisi kanda Maalum DSM linakamilisha taratibu za kupeleka jalada kwa mwasheria wa serikali na watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Imetolewa na Kamanda wa Polisi,
Kanda Maalum ya Dar es Salaam,
SACP-Lazaro Mambosasa,
03/06/2020


Share:

JNHPP MW 2115, uchimbaji kina cha lango la kuingilia maji kwenye mitambo wakamilika.

Ujenzi wa eneo la lango (Water Intake) la kuingilia maji kwenda kwenye mitambo ya kufua umeme katika Mradi wa Julius Nyerere (Mw 2115) unatarajiwa kukamilika Februari 2022.

Mhandisi Dismas Mbote, Mhandisi wa ujenzi njia za maji pamoja na Bwawa kwenye Mradi wa Julius Nyerere amesema utekelezaji wa njia hiyo ulianza Mwezi Oktoba 2019.

Aliongeza kuwa kazi ya uchimbaji wa lango imekamilika kwa kuchimbwa kina cha mita 53 ambapo hivi sasa kazi inayoendelea ni uondoaji wa kifusi na uchimbaji wa mahandaki matatu yatakayotumika kupitisha maji.

“Vifusi ambavyo vinachimbwa katika mradi huu wa Julius Nyerere havitupwi, mawe yanasagwa na kuwa mchanga, kokoto na mawe mbalimbali ambayo hutumika kwenye ujenzi”, alisema Mhandisi Mbote.

Aidha, zitafanyika kazi za kuchoronga miamba pamoja na kuimarisha kuta kwa zege.

Maji yatakayo fua umeme kabla ya kwenda kwenye mitambo ya kufua umeme yataingia kwanza kwenye lango.

Pia kwa hivi sasa imeletwa mashine ya kuchoronga miamba ambayo ni ya kwanza kwa Tanzania na inayotarajiwa kuongeza kasi katika uchimbaji wa mahandaki ya kupeleka maji kwenye mitambo.

Handaki la kwanza litakuwa na urefu wa mita 350, la pili mita 410 na la tano mita 570 hadi kwenye mitambo ya kufua umeme.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis June 4



















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger