Friday 17 February 2023

IDADI WALIOFARIKI KWENYE TETEMEKO LA ARDHI NI ZAIDI YA 41,000

...

Uharibifu wa miundombinu iliyosababishwa na tetemeko huko nchini mnamo Februari 6 unaweza kufikia asilimia 2.5 ya ukuaji wa bidhaa za ndani au dola bilioni 25 kwa mujibu wa wachumi.

Idadi ya pamoja ya vifo kutokana na mitetemeko ya ardhi nchini Uturuki na Syria imepanda hadi zaidi ya 41,000, huku mamilioni wakihitaji misaada ya kibinadamu, na manusura wengi wakiachwa bila malazi katika joto la karibu la majira ya baridi.

Shughuli za uokozi zinaendelea, ambapo wafanyakazi wa uokozi wamempata msichana mmoja mwenye miaka 17 akiwa hai kutoka kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka katika mkoa wa Kahramanmaras, saa 248 baada ya tetemeko la ardhi kukumba eneo hilo.

Hospitali mjini Aleppo hazina nafasi ya kutosha kwa wagonjwa wapya kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililotokea wiki iliyopita,

Maelfu ya watu sasa wanaishi katika makanisa, misikiti au katika maeneo ya umma na mbuga za wanyama baada ya kupoteza makazi yao.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger