Thursday 1 December 2022

TAKUKURU YASHIRIKIANA NA WADAU KUZIBA MIANYA YA RUSHWA, YATIA MGUU VIBANDA VYA BIASHARA MANISPAA YA SHINYANGA

...
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy  akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Desemba 1,2022
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy  akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Desemba 1,2022
Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy  akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Desemba 1,2022


Na Kadama Malunde- Malunde 1 blog

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga imeendelea kushirikiana na wadau wa sekta za umma kudhibiti mianya ya Rushwa na kufanya uzuiaji rushwa katika miradi ya maendeleo.

Akitoa Taarifa ya TAKUKURU katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023 (Julai – Septemba 2022) leo Alhamisi Desemba 1,2022, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy amesema katika kipindi hicho walijikita katika kuziba mianya ya rushwa na kuzuia rushwa kwenye miradi ya maendeleo.


“Katika ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo TAKUKURU Mkoa wa hinyanga ilishirikiana bega kwa bega na watendaji wa Halmashauri zote za mkoa wa Shinyanga wanaousika na utekelezaji wa miradi ya maendeleo”,amesema Kessy.

Ameeleza ufuatiliaji ulihusisha kazi za kutembelea miradi na shughuli zote za ujenzi katika miradi yote inayotekelezwa inakuwa na thamani halisi na ubora unaotakiwa.

“Kwa kufanya hivyo miradi 28 yenye thamani ya shilingi Bilioni 11.5 (11,573,687,057/=) iliyotembelewa kwa kipindi cha robo ya kwanza ikiwemo ya iliyotembelewa na Mwenge wa Uhuru 2022 iliweza kukamilika kwa ufanisi na ubora na hivyo kupelekea miradi kuwa na thamani halisi ya fedha”,ameeleza.

Ameongeza kuwa, TAKUKURU pia imeendelea kushirikiana na wadau wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kuhakikisha kunakuwepo na mazingira mazuri ya kufanyia biashara ikiwemo kupangisha vibanda vya biashara kwa wafanyabiashara kwa bei nafuu.

“Tunataka kuhakikisha vibanda vinatumiwa na wafanyabiashara halisi waliogawiwa vibanda na siyo wafanyabiashara waliopewa vibanda kuwapangisha wapangaji wengine au kuviuza kwa bei kubwa na kupelekea uwepo wa mazingira magumu ya kufanya biashara yanayoweza kuathiri pato la mkoa na taifa na hivyo kupelekea mfumuko wa bei”,amesema Kessy.


Katika hatua nyingine ameitaja mikakati ya utendaji kazi wa TAKUKURU mkoa wa Shinyanga kwa kipindi cha Mwezi Oktoba hadi Desemba 2022 kuwa ni pamoja na kukamilisha majukumu yake kwa kujielekeza zaidi kwenye ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa madarasa ili kuhakikisha inatekelezwa kwa thamani halisi ya fedha iliyoletwa na serikali.

“Pia tutaendelea kutoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa kwa wananchi kupitia Kampeni ya TAKUKURU inayotembea lengo likiwa ni kuwafikia wananchi walio maeneo ya ndani wanaoshindwa kufika TAKUKURU na kuwasaidia kutatua kero zao zinazowakabili hasa zinazohusiana na masuala ya rushwa”,ameongeza.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger