Thursday 26 May 2022

BODI YA FILAMU YAWAPIGA MSASA WADAU WA FILAMU JIJINI DODOMA


Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Dkt. Kiagho Kilonzo akifungua Mafunzo ya Filamu kwa Wadau wa Filamu yaliyoandaliwa na Bodi kwa lengo la kuwajengea uwezo Wadau, Jijini Dodoma
Mkurugenzi Msaidizi Haki na Maendeleo ya Wasanii kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Asha Salim Mshana akisisitiza mbinu bora za kuzingatia katika utayarishaji wa Filamu wakati wa Mafunzo ya Filamu.
Mwezeshaji Bw. Sikalion Rwabona kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) akifafanua jambo wakati wa Mafunzo ya Filamu kwa Wadau wa Filamu

Sehemu ya Wadau wa Filamu wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa Mafunzo ya Filamu kwa Wadau wa Filamu yaliyotolewa leo jijini Dodoma.

...................................................

Bodi ya Filamu Tanzania katika jitihada za kuhakikisha kuwa Wadau wa Filamu wanaongeza ubora katika utayarishaji wa Filamu zinazokubalika Kitaifa na Kimataifa kwa lengo la kukuza masoko ya Filamu imezindua mafunzo kwa Wadau wa Filamu jijini Dodoma Mei 26,2022.

Akifungua mafunzo hayo Katibu Mtendaji wa Bodi Dkt. Kiagho Kilonzo amewataka Wadau wa Filamu kutumia fursa hiyo kujiongezea maarifa mbalimbali kupitia mada zitakazotolewa sambamba na mafunzo kwa vitendo yanayoendelea. Akieleza ni matarajio ya Bodi kuwa mafunzo hayo ni muhimu katika kuwaanda wataalamu watakatoa Filamu bora zitakazochangia kuongeza ajira na kipato kwa Wadau wa Filamu na Uchumi.

Aidha, ilibainishwa kuwa baadhi ya mada zitakazokuwa katika mafunzo hayo ni pamoja na masuala ya uandishi wa miswaada, upigaji picha, uhariri na uongozaji wa Filamu. Wawezeshaji katika Mafunzo hayo ni pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Haki na Maendeleo ya Wasanii kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Asha Salim Mshana, Bw. Sikalion Rwabona kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na Bw. Ally Makata kutoka Bodi ya Filamu.

Washiriki wa Mafunzo hayo ni Wadau mbalimbali wa Filamu wa Jiji la Dodoma wakiwemo Wapiga Picha, Waigizaji, Wahariri, Waongozaji, Waandishi wa Miswaada. Mafunzo hayo yanatarajia kufikia Tamati Mei 30, 2022 Jijini Dodoma.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 26,2022


Magazetini leo Alhamis May 26 2022






























Share:

MSANII SITI AMINA ATUNUKIWA UBALOZI WA UTALII ZANZIBAR



Na Rahma Idrisa - Zanzibar

Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Zanzibar imemtunukia ubalozi wa utalii na mambo ya sanaa mwanamuziki wa kike kutoka Zanzibar  Omar Juma maarufu kama Siti Amina. 


Akizungumza na vyombo vya habari katika makabidhiano hayo hafla iliyofanyika katika ukumbi wa wizara hiyo Wazir Simai Mohammed Saidi amesema kuwa wizara ya utalii na mambo ya kale imempa ubalozi huo kutokana na juhudi zake kubwa za sanaa ya muziki anayoifanya.


"Wizara tumempa ubalozi huu kwanza tumemuona kuwa ni mwanamke jasiri na mwenye ushawishi mkubwa ,amekuwa akiimba nyimbo ambazo zinaitangaza Zanzibar kwa kuzingatia maadili ya mzazibar .


" Hata ivyo tunaimani naye kubwa katika kuitangaza Zanzibar hasa kupitia sanaa yake ya mziki anayoifanya " amesema.


Ameongeza kuwa Amina Omar Juma maarufu kama Siti Amina ambaye ni muhitimu wa muziki kutoka chuo cha nchi ya majahazi ataenda kutembelea nchi za nje takriban 5 lengo ni kuutangaza utalii wa Zanzibar .


" Mtu yoyote anaweza kuchaguliwa kuwa balozi lengo ni kuiwakilisha Zanzibar kupitia sekta ya utalii ambapo ubalozi huu utakuwa kwa muda wa miaka 3.


Kwa upande wake Amina Omar Juma balozi wa utalii kwa upande wa sanaa ameishukuru serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kumuona kuwa anaweza kuifanya kazi hiyo kwani wanamuziki wapo wengi .


"Shukran zangu za dhati nizipeleke kwa Rais wa Zanzibar kwa juhudi kubwa anazoendelea kuzifanya katika kuhakikisha nchi yetu inapokea wageni wengi ambao wanafika Zanzibar kwa kufanya utalii katika maeneo mbalimbali hata hivyo naipongeza wizara ya utalii na mambo ya kale kwa kuniamini ahadi yangu ni kuwa nitakuwa balozi mzuri na wa mfano katika kuhakikisha Zanzibar inapokea wageni wengi" , amesema.


" Aidha ameipongeza wizara ya utalii kwa kuwashika mkono wasanii wa Zanzibar na kuthamini kazi mbali mbali wanazozifanya kupitia sanaa zao .


Katika hafla hio Wizara ilimkabidhi cheti balozi huyo pamoja na bendera ya Taifa ambapo nchi anazo tarajiwa kuenda ni Italia, Ujerumani, Swizland  na Spain
Share:

MADIWANI BARIADI WALIA UHABA WA EFD MASHINE



Na COSTANTINE MATHIAS, Bariadi.


MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu wamesikitishwa na uhaba wa mashine za kukusanyia mapato za kielektroniki (EFD-Machine) ambazo zimesababisha ukusanyaji wa mapato kuwa mdogo katika Halmashauri hiyo.


Aidha Madiwani hao wamemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo (Khalid Mbwana) kuchukua hatua kali kwa watendaji wa kata na vijiji ambao siyo waaminifu na wanakwamisha ukusanyaji wa mapato.


Hayo yamebainishwa kwenye baraza la Madiwani lililokutana kwa siku mbili kwa ajili ya kujadili taarifa za kata pamoja na maendeleo ya Halmashauri hiyo kwenye kikao cha robo ya tatu 2022 kilichofanyika makao makuu ya wilaya ya Bariadi-Dutwa.


Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mayala Lucas amesema mwezi May na June hali ya ukusanyaji wa mapato ni nzuri kwa sababu wamefikia asilimia 100 ya mapato ya ndani ambapo wamevuka lengo walilojiwekea.


‘’Mwezi May na June zaidi ya asilimi 100 tuliyojiwekea, tumezungumza na watendaji wanaokusanya mapato hali siyo nzuri wanaendelea lakini ukusanyaji siyo mzuri…tunahitaji kuwa na mashine za kielektroniki (POS) zaidi ya 50 lakini zilizpo ni 40, tumeweka utaratibu na mkurugenzi ili kupata zingine 10’’ amesema Mayala.


Diwani wa kata ya Mwadobana Duka Mapya Mashauri amesema Halmashauri ya wilaya ya Bariadi imezungukwa na halmashauri zingine na kwamba wamejiwekea mikakati ili kuhakikisha kila mwananchi anayekusanya mazao mchanganyiko anakatiwa ushuru kwa ajili ya maendeleo ya Halmashauri.


Amesema wananchi wanahitaji miundombinu ya barabara, madawa kwenye hospitali na kwamba bila ushuru halmashauri haiwezi kujiendesha wala kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo ina manufaa kwa wananchi.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Juliana Mahongo amesema kuna udhaifu kidogo kwa wakusanya mapato ambao ni watendaji wa serikali ambapo Halmashauri inategemea mapato ya ndani ili iweze ujiendesha.


‘’Kwa uzembe huu kama utaendelea tutashuka kimapato, Mkurugenzi simamieni suala la ushuru, msionyeshe uzembe, kamati ya fedha kaeni muone namna ya kupata mashine za kukusanyia mapato ili tusiendelee kupoteza mapato’’ amesema Mwenyekiti huyo.


Akizungumzia suala hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bariadi Khalid Mbwana amesema halmashauri hiyo ilikuwa na mashine (POS) za kukusanyia mapato 53 kati yake 10 zimezuiliwa kutumika na Tamisemi na 2 ni mbovu.


‘’Kutokana na mwongozo, hatutakiwi kutengenezewa na mtu mwingine bali msambazaji na gharama za kutengeneza ni kubwa bora kununua zingine, hivyo tuna mashine 41 ambazo haziwezi kukidhi mahitaji kwenye kata 21’’ amesema na kuongeza.


‘’Tunaangalia maeneo muhimu, kama kuna kata haijapata mashine ya kukusanyia mapato tuwasiliane, tuna mkakati wa kununua mashine zingine 10, muhimu siyo kuwa na mashine bali tunaangalia ukusanyaji wa mapato ‘’ amesema.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi Shigolile Chambitwe akiwa kwenye kikao cha Baraza la Madiwani liliofanyika leo katika makao makuu ya wilaya hiyo Dutwa.
Share:

Wednesday 25 May 2022

WALIMU WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA PROGRAM YA MAFUNZO ENDELEVU


Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha Seleman Msumi akifungua semina ya mafunzo ya walimu iliyofanyika katika halmashauri hiyo.


Na Rose Jackson,Arusha

Walimu halmashauri ya Arusha, wametakiwa kutumia fursa inayotolewa na serikali ya kupitia programu ya Mafunzo Endelevu kwa Walimu Kazini (MEWAKA), mafunzo yenye lengo la kuboresha utalamu kitaaluma kwa walimu, ili kuwa mahiri katika mbinu za ufundishaji zinazoendana na wakati.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, wakati akifungua semina ya Mafunzo ya Walimu Kazini, iliyojumuisha walimu wakuu wa shule za msingi pamoja na Maafisa Elimu wa kata zote za halamshauri hiyo, semina iliyofanyika kwenye Ukumbi wa shule ya Msingi Green Acress.

Mkurugenzi Msumi, amewataka walimu hao, kutumia fursa hiyo, inayotolewa na serikali kuhakikisha wanapanga muda wa kujifunza zaidi kupitia miongozo na utaalam uliotolewa kwenye moduli za MEWAKA, mafunzo ambayo yatawawezesha kupata maarifa mapya na mbinu shirikishi za ufundishaji, pamoja na kufanya tathmini kwa wanafunzi.

"Serikali inatambua na inathamini kazi kubwa inayofanywa na walimu, na kuona umuhimu wa kuandaa mkakati wa MEWAKA, utakowewezesha kapata mafunzo kazini, hivyo nitoe wito kwenu viongozi wa shule, kuratibu na kusimamia mpango huo katika maeneo yenu ya kazi, ili kufikia malengo ya serikali ya kuinua kiwango cha taaluma shuleni" amesisitiza Mkurugenzi Msumi.

Naye Afisa Elimu Msingi halmashauri ya Arusha, Salvatory Alute, amefafanua kuwa, lengo la semina hiyo kwa viongozi hao wa elimu ngazi ya kata na shule ni kuwajengea uwezo wa kuratibu na kusimamia programu ya MEWAKA katika maeneo yao ya kazi, ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kuwa wathibiti ubora wa ndani ya shule, kufuatilia utekelezaji wa MEWAKA na kufanya tathmini, kuwawezesha wadau wa elimu katika kupanga gharama za uendeshaji wa mafunzo na upatikanaji wa rasilimali pamoja na usimamizi wa rasilimali hizo.

Hata hivyo Afisa Elimu huyo, amebainisha kuwa mfumo wa MEWAKA umeondoa changamoto nyingi zilizokuwepo za mifumo iliyotumika hapo awali ya mafunzo kwa walimu, hivyo programu ya MEWAKA ni mfumo rasmi ambao umeandaliwa na Serikali kutekeleza mtaala wa elimu msingi, unaozingatia umahiri wa mbinu za kufundishia na kujifunzia, kufanya tathmini kwa wanafunzi, pamoja na kuendeleza mafunzo hayo kwa kuhawilisha taaluma kwa walimu wote.

"MEWAKA imeandaliwa na Taasisi ya Elimu kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI, kwa zingatia mitaala ya elimu inaozingatia umahiri, ndani yake kuna moduli mbalimbali zitakazowawezesha walimu kujinoa kitaaluma na kuwa mahiri katika ufundishaji pamoja na kujifunza namna ya kuendeleza mafunzo hayo kwa walimu wote ili kuwa na umahiri unaoendana na wakati" amefafanua Afisa Elimu Alute.

Aidha walimu hao wameweka wazi kuwa, MEWAKA imekuja wakati muafaka, kutokana na kasi ya maendeleo ya kisayansi, yanayotokana na mabadiliko ya teknolojia, mabadiliko yanayomlazimu mwalimu kujisomea sana ili kupata maarifa mapya, huku wakithibitisha kuwa, program ya MEWAKA, inawapa walimu fursa endelevu ua kujinoa kitaaluma kwa kusoma na kubadilishana uzoefu wa kazi.

Mwalimu Mkuu, shule ya Msingi Ngaramtoni, mwalimu Makanjo Twaty, amesema kuwa program ya MEWAKA ni muhimu kwa walimu, na watahakikishia kutumiammuda wa ziada kujifunza miongo yote iliyoainishwa bila kuathiri ratiba za masomo kwa wanafunzi, huku akisistiza kuwa MEWAKA itawafanya walimu kufundisha kwa kuendana na wakati, hasa kwa walimu waliosoma miaka mingi iliyopita.

Share:

JAMAA AMBAYE HAJASOMEA UFUNDI AUNDA GARI


Ochieng hakuwahi kusomea ufundi wa magari
***

Kipaji ni kitu ambacho watu wengi wamejaliwa kuwa nacho ila ni watu wachache huwa wanafanikiwa kugundua vipaji vyao nakuvifanyia kazi mpaka wanafanikiwa.

Kijana mmoja kutoka Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya anayetambulika kwa jina la Bernard Otieno Ochieng, ameshangaza watu kutokana na kipaji chake na uwezo wa ubunifu baada ya kubuni gari lake la siti mbili za kukaa.

Mwaka 2010, Ochieng aliacha shule baada ya kushindwa kulipa karo, baada ya hapo alianza kujifunza ufundi wa magari kwa sababu ni kitu ambacho alikuwa anakipenda tangu akiwa shule.

 Kipindi yupo shule alikuwa anapenda kutumia computer kuangalia mtandaoni jinsi magari yanavyoundwa na kujifunza.
Share:

JAMES MBATIA ASIMAMISHWA KUJIHUSISHA NA SIASA ZA NCCR - MAGEUZI


Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini imebariki uamuzi wa Halmashauri Kuu ya NCCR - Mageuzi ya kumsimamisha Mwenyekiti wa Chama hicho pamoja na Sekretarieti yake yote.

Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza amesema ofisi hiyo ya msajili inamsimamisha mwanasiasa huyo kujihusisha na siasa za chama hicho hadi pale uamuzi mwingine ndani ya Chama hicho utakapotolewa.

Ameeleza kuwa uamuzi wa Halmashauri kuu ya chama hicho ulikuwa halali kwa kuwa akidi ya kikao husika ilikuwa imetimia.

Mwishoni mwa wiki iliyopita siku ya Jumamosi Mei 21 mwaka huu, Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi ilimsimamisha Mbatia na makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi mkutano mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma zinazowakabili.

Chanzo - EATV
Share:

Tuesday 24 May 2022

WADAU WA UTALII TUMIENI FURSA YA MIKOPO ILI KUHIMARISHA MAZINGIRA YA VIVUTIO NCHINI" Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Dkt Francis Michael watatu kutoka kushoto  wakiingia kwenye kongamano la kimtandao la utalii,lililowakutanisha wadau wa utalii na Taasisi ya kifedha ya NMB na kufanyika jiji Arusha.

****************

Agness Nyamaru,Arusha.

Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na Utalii,Dkt Francis Michael amewataka wadau wa utalii mkoani Arusha kutumia fursa za mikopo nafuu ya Taasisi ya fedha(NMB) katika kuwekeza katika sekta ya utalii ili kuvutia wageni nchini.

Akizungumza katika kongamano la kimtandao la utalii(tourism Networking)Dkt.Michael alisema benki ya NMB imekuwa chachu katika kuhakikisha inawapa mikopo wadau wa sekta ya utalii katika kuhimarisha mazingira ya vivutio nchini.

"Tunaomba mfanye jitihada za kuijenga sekta ya utalii kwani serikali imeshaweka mazingira ya kuitangaza kupitia filamu ya The Royal Tour Tanzania hivyo kama wadau ni vyema mkatumia fursa hiyo katika kuweka mazingira sawa,"alisema Dkt.Michael.

Aidha aliwasisitiza wadau hao kutumia benki ya NMB katika kuhimarisha ulinzi na usalama wa watalii ikiwemo vituo vya polisi hivyo ni vyema wadau hao wakaongeza juhudi katika kuongeza idadi ya wageni nchini pamoja na kuwahudumia ipasavyo.

Naye Mbunge wa jimbo la Arusha mjini,Mrisho Gambo alisema ni vyema NMB ikaongeza muda kwa wateja wao waliokopa katika kipindi cha mlipuko wa ugonjwa wa covid 19 kuwaongezea muda marejesho pasipokuwa na riba.

Kwa upande wake Afisa mkuu wa biashara na wateja binafsi wa NMB Filbert Mponzi alisema benki hiyo wanaendelea kuunga juhudi za serikali ya awamu ya sita kupitia Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania,Rais Samia Suluhu Hassan.

Pia alisema uhitaji wa watalii wengi nchini imeongeza chachu katika kujiandaa kupitia Taasisi ya benki ya NMB kwa kuunga mkono watoa huduma katika sekta ya utalii kwa lengo la kuongeza ufanisi zaidi katika kuwapokea watalii nchini.

Mponzi alisema kuwa kwa miaka ya hivi karibuni wameanza kutoa huduma ya mikopo katika sekta ya utalii lengo ni kuhimarisha katika kutoa huduma kwa wageni wanaofika nchini kutalii na kuona vivutio vilivyopo nchini.
Share:

MWANAMKE AUAWA KWA KUCHOMWA KISU GESTI MJINI KAHAMA

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando

Na Marco Mipawa - Kahama

Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Zuena au Ashura Salum (25-30) mkazi wa Dar es Salaam, amekutwa chumbani akiwa ameuawa kwa kuchomwa kisu  na mtu anayedhaniwa kuwa ni mwenza wake katika nyumba ya kulala wageni ya Kalunde iliyoko mjini Kahama, usiku wa kuamkia Mei 22, 2022.


Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga George Kyando amethibitisha kutokea kwa  tukio hilo na kwamba, Zuena na mwanaume huyo waliingia chumbani hapo majira ya saa 11:00 alfajiri na kwamba mwanaume alitoka na kutokomea kusikojulikana kabla ya wahudumu wa nyumba hiyo kugundua mauaji hayo.


Kyando amesema, mapema asubuhi siku hiyo wahudumu wa nyumba hiyo waliukuta Mwili wa marehemu chumbani pamoja na simu mbili zenye laini zinaonesha majina hayo.

Amesema jeshi la polisi linaendelea kufuatilia tukio hilo, huku akitoa Rai kwa jamii kujihadhari na watu wasiotambulika vizuri.
Share:

Monday 23 May 2022

WAZIRI MABULA AFUNGUA MKUTANAO WA MAJADILIANO YA KISEKTA KATI YA WIZARA NA WADAU WA SEKTA YA ARDHI

Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula akizungumza katika mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi uliofanyika leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula akisisitiza jambo wakati akizungumza katika mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi uliofanyika leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Allan Kijazi akizungumza katika mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi uliofanyika leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam Kaimu mwenyekiti wa Sekta Binafsi (TPSF) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC), Bi.Mercy Silla akizungumza katika mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi uliofanyika leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC),Godwill Wanga akizungumza katika mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi uliofanyika leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam Wadau mbalimbali wa sekta ya ardhi wakiwa katika mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi uliofanyika leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

**********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WIZARA ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi imewezesha kutafuta fedha za kugharamia utekelezaji wa miradi ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi ambapo Wizara imetoa kiasi cha Bilioni 50 kwa halmashauri 55 ili kufanikisha mradi huu.

Ameyasema hayo leo Mei 23,2022 Jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula katika Mkutano wa majadiliano ya Kisekta kati ya Wizara na wadau wa sekta ya ardhi, Nyumba na Makazi.

Amesema utekelezaji huo unafanyika kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na TAMISEMI.

Aidha amesema Wizara imewezesha upatikanaji wa mkopo wa benki ya dunia kiasi cha shilingi Bilioni 340.5 ambao pamoja na kazi zingine uttawezesha kuimarisha miundombinu ya TEHAMA na Usalama wa miliki.

Hata hivyo amesema Wizara imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za utatuzi wa changamoto zinazojitokza ikiwemo, kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za ardhi, kuendelea kuimarisha na kuziwezesha Ofisi za Ardhi zilizopo katika kila mkoa katika kuhakikisha huduma zinapatikana karibu na wananchi.

"Wadau na wamiliki wote wa ardhi mtumie utaratibu wa ukadiliaji na upimaji kodi ya pango la ardhi ki-elekroniki kwa kuwa utaratibu huu ni rafiki, unaokoa muda na ni nafuu". Amesema Waziri Mabula.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt.Allan Kijazi amesema kupitia mkutano huo watapokea maoni ya sekta binafsi kuhusu maboresha yanayotakiwa kufanyika kwenye sekta ya ardhi na lengo ikiwa ni kuchochea mchango wa sekta hiyo katika kukuza uchumi jumuishi na kukuza maendeleo ya jamii na kuhakikisha uendelevu wa mifumo ya kimazingira.

"Sekta binafsi inamchango mkuwa kwenye maboresho ya sekta ya ardhi nchini kwani inatoa mchango mkubwa kwenye ubunifu, upatikanaji wa mitaji na uwekezaji ambao huchangia kwa kiasi kikubwa kwenye shughuli za uzalishaji hasa katika sekta ya viwanda, kilimo, mifugo na shughuli nyingine nyingi za maendeleo". Amesema

Amesema ufanisi wa sekta hizi unategemea kwa kiasi kikubwa kuwa na mifumo ya usimamizi na uendelezaji wa sekta ya ardhi ambayo inaweza kujenga mazingira wezeshi bila kukwamisha mipango ya sekta nyingine.

Nae Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC),Godwill Wanga amesema wameanzisha mkutano huo ili kukutanisha Wizara na Taasisi mbalimbali za serikali na wadau wa sekta binafsi ili kujadili changamoto, fursa na maboresho kwaajili ya kukuza mchango wa sekta katika maendeleo ya uchumi na jamiii nchini.

Share:

MBUNGE ABINUKA SARAKASI AKIONESHA HISIA ZAKE BUNGENI DODOMA



Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Massay akiwa amebinuka sarakasi ndani ya ukumbi wa Bunge alipokuwa akichangia mjadala wa kupitia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2022/2023 jijini Dodoma leo Mei 23,2022.

Flatei alichukua uamuzi huo ikiwa ni njia ya kuonyesha hisia zake kwa kero ya kutokuwa na barabara ya lami katika jimbo lake. Picha na Edwin Mjwahuzi
Chanzo #mwananchi



Share:

WATEJA KUOKOA HADI Tsh 1,000,000 KAMPENI MPYA YA "LGs SOMETHING BETTER"

Dar Es Salaam, , Kampuni mashuhuri kwa uuzaji wa bidhaa zinazotumia umeme ya LG Electronics East Africa imetangaza kuzindua Kampeni ya " LGs Something Better " kote nchini inayolenga kuboresha uzoefu wa ununuzi kwa wateja.

Kampeni hiyo, inatarajia kuendelea hadi tarehe 12 Juni 2022 kwa lengo la kuwapa wateja punguzo la hadi 20% kwa bidhaa zilizochaguliwa pamoja na thamani na manufaa zaidi kwa wateja wanaonunua bidhaa kutoka kwa maduka ya chapa ya LG.

 Kwa punguzo la ofa, wateja wanatarajiwa kuokoa kuanzia shilingi 50,000/= hadi kufikia Tsh 1,000,000/= katika kipindi cha wiki tano zijazo katika bidhaa zote katika kategoria ya Burudani , Vifaa vya Nyumbani na Viyoyozi vya Makazi. Akitoa maoni yake kuhusu kampeni hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa LG Afrika Mashariki, Sa Nyoung Kim alisema, “Kupitia ubunifu na bidhaa zetu za hivi punde, lengo letu ni kuwasaidia wateja wetu kuishi maisha bora na rahisi zaidi. Huu ukiwa ni mwezi wa Eid al-Fitr, tunatoa nafasi kubwa kwa kila mtu kuchagua maisha haya bora sio tu ya leo bali ya kesho pia”.

 "Hii pia ni fursa kwa Watanzania kubadilisha na kuboresha burudani zao za nyumbani au vifaa ambavyo wamekuwa navyo kwa muda mrefu hadi kufikia teknolojia mpya, ya kisasa na vifaa vya ufanisi zaidi". 

Hii si tu katika maduka yenye chapa ya LG bali pia katika maduka makubwa ya washirika kama vile Shoppers na Game Super Market. Wanunuzi wamehakikishiwa kupata punguzo kubwa la hadi Tsh 539,200/=kwenye jokofu za LG Instaview 668(L), na Tsh 225,000/= kwenye jokofu la LG Instaview 544(L).

 Kwenye mashine za kufulia zinazotolewa, punguzo linaanzia Tsh 100,000/= hadi Tsh. 300,000 kwa mashine za kufulia ya 8Kg hadi ya 15Kg / dryer. LG microwaves, Neo Chef 20L, 23LNeoChef na 42L Neo Chef zote zina punguzo la kati ya Tsh 81,600/= na TZsh 122,800/= Kufahamu zaidi kuhusu kampeni hii kabambe tafadhari tembelea mitandao ya kijamii ya LGs East Africa. 
    
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger