Wednesday 21 April 2021
Tuesday 20 April 2021
Naibu Waziri Masauni Awataka Vijana Kuchangamkia Fursa Za Uchumi Wa Blue Zanzibar
Na Benny Mwaipaja, Zanzibar
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amewahimiza vijana Visiwani Zanzibar kuchangamkia fursa za uchumi wa blue unaotokana na shughuli za uvuvi na uchakataji wa samaki ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Mhe. Masauni ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni-Zanzibar, ametoa rai hiyo wakati akizungumza na viongozi na baadhi ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi katika Jimbo la Kikwajuni akiwa katika ziara yake ya kikazi visiwani humo.
Amesema kuwa yeye binafsi na Mwakilishi wa Jimbo hilo katika Baraza la Wawakilishi Mhe. Nasor Ali Jazeerah pamoja na viongozi wengine wamejipanga kutoa vifaa vitakavyotumiwa na vijana kwa ajuili ya shughuli za uvuvi katika sekta hiyo ya uchumi wa blue ili waweze kujitegemea kwa kujipatia kipato cha uhakika.
“Tunataka tuangalie uwezekano wa kujenga mazingira mazuri ya kuwatafutia “ndoano” na siyo “samaki” na tumeandaa vitu vikubwa ambavyo sitaki niseme mapema hapa nitaondoa radha, mkawaambie vijana wa Kikwajuni kama hawatatoka kimaisha kipindi hiki hawatatoka maisha” alilisisitiza Mhe. Masauni.
Pamoja na kusisitiza masuala ya kiuchumi, Mhandisi Masauni alisema kuwa mipango mingine iliyowekwa na uongozi katika Jimbo la Kikwajuni ni kuendesha mashindano ya kusoma qoran kwa vijana na kuwataka wazazi kuwahimiza watoto wao kushiriki mashindano hayo.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Nasor Ali Jazeerah, aliwaahidi wakazi wa Jimbo la Kikwajuni-Zanzibar kwamba ahadi zote zilizoahidiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopita zitatekelezwa kikamilifu.
Alitoa wito kwa wakazi wa Jimbo hilo kushikamana, kupendana na kuacha majungu ili mipango ya maendeleo iliyopangwa iweze kutekelezwa kwa kasi zaidi.
Aliwashukuru wananchi kwa kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ili waendelee kuingoza nchi kwa umahili mkubwa.
Mwisho.
Dkt. Kalemani : Marufuku kuuza mafuta yasiyo na vinasaba
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amepiga marufu uuzaji wa mafuta ya Petroli, Dieseli, na Mafuta ya Taa yasiyo na vinasaba unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara nchini.
Dkt. Kalemani alitoa maagizo hayo Jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kushtukiza ya kukagua vinasaba kwenye mafuta yaliyopo katika vituo vya kuuzia mafuta mkoani humo, iliyofanyika Aprili 20, 2021.
Katika ziara hiyo aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Leonard Masanja, Naibu Katibu Mkuu, Kheri Mahimbali na Kamishna wa Petroli na Gesi, Adam Zuberi wa wizara hiyo, pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini( EWURA),Mhandisi Godfrey Chibulunje.
Dkt. Kalemani Alisema kuwa vinasaba vinadhihirisha viwango na ubora wa mafuta nchini.
“Maelekezo yangu kwa wauzaji wa mafua nchini ni lazima muendelee kuuza mafuta yenye vinasaba kwa sasa ili kujiridhisha na kiwango na ubora wa mafuta nchini, na kama mafuta hayana vinasaba ni marufuku kuyachukuwa na kuuza, kuna minong’ono katika baadhi ya maeneo kuwa kuna mafuta yanayouzwa ya aina hiyo, tutakayembaini tutachukua hatua stahiki”, alisema Dkt. Kalemani.
Katika ziara hiyo, hakuna kituo hata kimoja kilichobaininika kuuza mafuta yasiyo na vinasaba.
Alieleza kuwa kwa sasa Shirika la Viwango nchini (TBS), ndiyo llililopewa kazi ya kupima na kuweka vinasaba katika mafuta yote yanayoingia nchini ili kudhibiti ubora na tayari kazi hiyo imeanza kufanyika.
Alisisitiza kuwa kuanzia sasa mafuta yote nchini yatakuwa yakipimwa na kuwekwa vinasaba na TBS na ikibainika kuna mafuta ambayo hana vinasaba hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watendaji husika.
“TBS ni chombo cha serikali, kinachofanya kazi ya kudhibiti ubora na viwango ikiwepo wa mafuta nchini hivyo kuanzia sasa ndiyo kifanya kazi ya kupima na kuweka vinasaba kwenye mafuta yote nchini, endapo atatokea mwingine mtaelekezwa na serikali”, alisisitiza Dkt. Kalemani.
Lengo la serikali kuipa TBS kazi ya kuweka vinasaba katika mafuta yote nchini ili kuokoa fedha za serikali zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa mwezi ambazo awali alikuwa akilipwa aliyekuwa akifanya kazi hiyo.
Vilevile ni kuijengea uwezo taasisi hiyo na kuongeza ajira kwa watanzania.
Katika ziara hiyo, aliitoa maelekezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Wizara ya Maji kuwachukulia hatua waafisa wawili katika idara ya manunuzi wa Mamlaka wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini( EWURA), pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Manunuzi wa taasisi hiyo kwa kushindwa kutekeleza maelekezo ya serikali kwa wakati.
Dkt. Kalemani alisema kuwa watumishi hao, hawakutekeleza maagizo ya serikali yaliyotolewa tangu Februari 5, 2021, kwa sababu zao wenyewe, pia wachunguzwe kwa nini hawakutekeleza maagizo hayo, na kusababisha migogoro.
MGANGA ARUDISHA PESA BAADA YA NDUMBA ZAKE KUFELI KUNASA MCHEPUKO UNAOPAKUA ASALI YA JAMAA
WEKUNDU WA MSIMBAZI WAWASILI BUKOBA KUKABILIANA NA WAKATA MIWA KAGERA SUGAR
SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).
AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).
AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.
CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1. Shinikizo la damu (B.P)
2. Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3. Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4. Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5. Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6. Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7. Uzito na unene uliozidi
8. Kutofanya mazoezi
9. Umri
10. Kurith
UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1. Kusikia njaa mara kwa mara
2. Kusikia kiu mara kwa mara
3. Kupungua uzito
4. Maono machafu
5. Uchovu mara kwa mara
6. Ukipata kidonda hakiponi
7. Kushuka kwa kinga mwili
DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo kama cha mbuzi
DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi ya gonzi kukakamaa
TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.
Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.
Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.
BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152
MAJALIWA: SERIKALI IKO IMARA, WATANZANIA ENDELEENI KUIAMINI
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ipo imara na miradi yote ya kimkakati inaendelea kujengwa, hivyo Watanzania waendelee kuwa na imani nayo.
Amesema Serikali inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ipo makini na inaendelea kuwatumikia Watanzania. ”Tuendelee kuchapa kazi”.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Aprili 20, 2021) baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, Dar es Salaam.
”Siri ya kuwepo mafanikio na maendeleo nchini ni utulivu na amani. Tulianza vizuri tangu Serikali ya Awamu ya kwanza, tutaendelea kuimarisha amani na utulivu.”
Mheshimiwa Majaliwa ametumia fursa hiyo kuwaasa Watanzania watumie muda mwingi kufanya shughuli za maendeleo kuliko mambo mengine yasiyo na tija.
Akizungumzia kuhusu mradi huo, Mheshimiwa Majaliwa amesema amefurahi kukuta majengo yamekamilika na kwamba ameridhika na maendeleo ya ujenzi wake.
Waziri Mkuu ameuagiza uongozi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wahakikishe wanakamilisha kazi iliyosalia haraka ili mwaka huu wananchi waanze kuishi hapo.
Naye, Mtendaji Mkuu wa TBA, Bw. Daud Kondoro amesema mradi huo una jumla ya block tano na ambazo zinauwezo wa kuchukua familia 656.
Amesema mbali na ujenzi wa nyumba hizo za makazi pia katika eneo hilo wanajenga maduka makubwa pamoja na vizimba kwa ajili ya wajasiriamali kufanya biashara.
Mradi ulianza kutekelezwa mwaka 2016 na unatarajiwa kukamilika Mei 2021. Hadi sasa umefikia asilimia 94 ya utekelezaji wake na gharama yake ni shilingi bilioni 50.
Baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za makazi za Magomeni Kota, Waziri Mkuu alikagua kituo cha Reli ya Kisasa cha Tanzanite jijini Dar es Salaam.
(Mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU
RAIS SAMIA AKUTANA NA SPIKA NDUGAI IKULU DODOMA
MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AKUTANA NA KATIBU MKUU KIONGOZI
WAZIRI UMMY AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI HALMASHAURI YA SENGEREMA
NAIBU WAZIRI KATAMBI: SERIKALI KUENDELEA KUWAPATIA VIJANA WA KITANZANIA MAFUNZO YA STADI ZA KAZI
RAIS WA CHAD AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WAASI
Jeshi la Chad limetangaza kuwa Rais wa nchi hiyo Idriss Deby amefariki baada ya kupata majeraha kwenye mapambano dhidi ya waasi.
Deby alienda mwishoni mwa wiki kuvitembelea vikosi vya nchi hiyo ambavyo vinapambana na waasi kaskazini mwa nchi hiyo. Waasi hao wamevuka mpaka wakitokea Libya.
Kifo chake kimetokea ikiwa ni saa chache tu tangu matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika Aprili 11 kuonesha kuwa anaongoza kwa asilimia 80. Kwa ushindi huo, Deby angeiongoza nchi hiyo kwa awamu ya sita mfululizo.
Serikali na bunge vimevunjwa na sasa baraza la kijeshi ndilo litakaloiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miezi 18 ijayo.