Monday 2 November 2020

Dk. Hsusein Mwinyi Aapishwa Kuwa Rais Wa Zanzibar


 JAJI Mkuu wa Zanzibar Mhe,Omar Othman Makungu akimuapisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Haasan Mwinyi (kulia) kuongoza Zanzibar kwa awamu ya kuanzia 2020-2025 ,sherehe za kiapo zilizofanyika leo katika uwanja wa Amaan Studium Jijini Zanzibar.Picha na Ikulu

Share:

INFINIX Yaendelea Kutamba Sokoni.......Kaa Tayari Kushuhudia Mp64 Za Kamera Ya Note 8 Zinavyofanya Kazi


Kama ni NOTE basi si nyengine hiyo ni Infinix NOTE 8 ndio mdahalo uliopo sasa kwenye page ya Infinix XClub Tanzania ‘http://www.infinix.club’. 


Kampuni ya Infinix imekuwa ikiaminika kwa mapinduzi wanayoendelea kuyafanya katika soko la simu na hivi punde kupitia picha zilizovuja katika mitandao ya kijamii inasemakana Infinix imejipanga kuendeleza mapinduzi hayo kwa ujio wa toleo la NOTE. 


Toleo hilo jipya linalosemekana ni Infinix NOTE 8 inasemekana huwenda ikawa simu kali zaidi kwa mwaka huu wa 2020 kutoka na processor yake aina ya Helio G80 kuwa moja ya processor zenye kasi ya ajabu zaidi ya processor yoyote kutokea kwa mwaka huu wa 2020 alisema Bwana Masawe Simba mdau wa simu za Infinix.

Baada ya tetesi hizi sikusita kumvutia waya Aisha Karupa Afisa wa Mahusiano wa Infinix na alikiri kuhusu ujio wa simu aina ya NOTE 8 na kudai ni kweli ni "simu yenye processor kubwa Helio G80 kwa kifupi si simu ya kulinganisha na toleo lolote la awali la Infinix lakini pia uzinduzi wake ni wakipekee haujawai fanyika na Kampuni yoyote ya simu nchini Tanzania. 


Alisistiza tuweni na subra, tujichange NOTE 8 si processor tu kali kwani hata kamera ni kali zaidi shuhudia 64MP Ultra HD 6 za kamera ya NOTE 8 zinavyofanya kazi kwenye NOTE 8 safari hii tumecheza na teknolojia vilivyo” 


Baada ya kuambulia machache kuhusu Infinix NOTE 8 nikaona sio mbaya kuwajuza na nyinyi wadau wenzangu wa simu nzuri lakini je unaisi hii simu uzinduzi wake utakuwa wa aina gani?




Share:

Viongozi wa CHADEMA wakamatwa kwa kuratibu maandamano


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ACP Lazaro Mambosasa amesema wanawashikilia watu kadhaa wakiwemo viongozi  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa tuhuma za kupanga maandamano.

Viongozi wa Chadema wanaowashikilia ni pamoja na mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe, Godbless Lema, na Boniface Jacob aliyekuwa Meya wa Ubungo na mgombea ubunge wa Jimbo la Ubungo.

Amesema wanawashikilia viongozi hao kwa kuwa wanahatarisha usalama wa raia na mali zao kwa kuwa wamepanga kuanza maandamano kitaifa yasiyokuwa na kikomo

Aidha, jeshi hilo linaendelea kuwasaka watu wanaowashawishi vijana kushiriki maandamano ambayo polisi wamesema ni ya vurugu. Wengine wanaosakwa ni viongozi wa chama cha ACT Wazalendo.


Share:

Makaa ya mawe Ruvuma yaingiza bilioni 400 na kutoa ajira 700


MADINI ya makaa ya mawe yanayochimbwa mkoani Ruvuma yameingiza zaidi ya shilingi bilioni 400 na kutengeneza ajira za watanzania zaidi ya 700. 


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amesema kiasi hicho  cha fedha kimepatikana kutokana na mauzo ya madini ya makaa ya mawe zaidi ya tani milioni  3.3 ambayo yameuzwa kuanzia Agosti 2017 hadi Oktoba 2020. 


Ameutaja uchimbaji wa madini ya makaa ya mawe unafanyika katika wilaya za Songea ,Mbinga na Nyasa na kwamba Mkoa wa Ruvuma una hazina kubwa ya mashapo ya madini ya makaa ya mawe yaliyofanyiwa utafiti na kampuni tatu kubwa za uchimbaji. 


“Kwa mujibu wa utafiti unaoendelea kufanyika,Mkoa wa Ruvuma una mashapo ya makaa ya mawe zaidi ya tani  milioni 457,mashapo hayo tulionayo,tunaweza kufanya uchimbaji kwa miaka 718 bila kumaliza hazina hii’’,amesisitiza Mndeme. 


Hata hivyo Mndeme amesema katika kipindi cha mwaka 2019/2020  zaidi ya tani 636,000 za makaa ya mawe yaliyochimbwa mkoani Ruvuma ziliuzwa ndani na nje ya nchi. 


Amesema Mkoa wa Ruvuma umebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali yakiwemo madini ya vito na dhahabu ambayo yanachimbwa kwa wingi katika wilaya za Tunduru,Songea ,Mbinga na Nyasa. 


Mndeme amesema katika Mkoa wa Ruvuma kuanzia Mei 2019 yalifunguliwa masoko ya madini ya vito na dhahabu  katika wilaya za Songea na Tunduru ambapo hadi sasa kupitia masoko hayo zimeuzwa gramu zaidi ya milioni moja zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 7.7 na kwamba watanzania zaidi ya 1000 wamepata ajira za uchimbaji kwenye madini hayo mkoani Ruvuma. 


Amesema tayari limejengwa jengo   kubwa la kituo cha umahiri cha madini la Mkoa ambalo litatumika kutoa elimu ya madini kwa wachimbaji wadogo,elimu ya upatikanaji wa masoko ya madini na elimu ya utambuzi wa madini. 


Imeandikwa na Albano Midelo
Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma



Share:

LIVE: Mwinyi Aapishwa Kuwa Rais wa Zanzibar


LIVE:  Mwinyi Aapishwa Kuwa Rais wa Zanzibar


Share:

Project Coordinator at Mzumbe University

Job Title: Project Coordinator, CDC grant GH20-2063 The Mzumbe University’s Centre of Excellence in Health Monitoring and Evaluation is currently seeking a highly motivated individual to join the Centre in a project on Technical Assistance to Government of Tanzania (GOT) and Public Health Institutions (PHIs) Toward Sustained Health Systems Strengthening in Tanzania under The President’s […]

The post Project Coordinator at Mzumbe University appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Consultancy at Nutrition International

Terms of Reference for conducting Sex and Gender Based Analysis of Maternal, Newborn, Child and Adolescent Health and Nutrition, Vitamin A Supplementation and Universal Salt Iodization Programs in Tanzania Introduction 1.1 About Nutrition International The Nutrition International (NI) formerly Micronutrient Initiative, is a global organization dedicated to delivery of proven nutrition interventions with a focus […]

The post Consultancy at Nutrition International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu November 02



Share:

Sunday 1 November 2020

ADAKWA MOCHWARI AKIHARIBU MIILI YA MAREHEMU

Mhudumu wa zamani wa makafani 'chumba cha kuhifadhai maiti'  ya Hospitali ya Rufaa ya Iten, Kaunti ya Elgeyo-Marakwet nchini Kenya amekamatwa na maafisa wa polisi kwa tuhuma za kuharibu miili iliyohifadhiwa hospitalini humo. 

Benson Kagari ambaye ni mhudumu wa zamani wa mochwari hiyo, anaripotwa kuingia katika mochwari ya hospitali hiyo Jumatano, Oktoba 28,2020 usiku, bila kugunduliwa na yeyote. 

Kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la Taifa leo, Waziri wa Afya katika kaunti hiyo, Isaac Kamar alisema mshukiwa aliingia katika hifadhi hiyo kupitia kwa dirisha na kuelekea hadi eneo ambapo miili hiyo ilikuwa imehifadhiwa.

 Inadaiwa mshukiwa alikuwa akiingia hospitalini humo kuharibu miiili iliyokuwa imehifadhiwa.

Kamar alisema mshukiwa alitimuliwa hospitalini humo kutokana na utovu wa nidhamu.

 “Tulipokea ripoti kwamba kulikuwa na mtu aliyeingia kwenye mochari ambapo alikuwa akiharibu miili iliyohifadhiwa na kuibadilisha ili kuwachanganya wahudumu.Tulifika kwa haraka na kubaini kuwa ni mhudumu wa zamani aliyefutwa kazi kutokana na utovu wa nidhamu,” akasema Bw Kamar. 

Kulingana na Kamar, baada ya kupokea ripoti hiyo maafisa wa afya waliingia chumbani humo kwa haraka na kumfumania mshukiwa ambapo walimkamata na baadaye walimkabidhi kwa polisi ili kuchunguzwa.

 Inasemekana kuwa mshukiwa alitumiwa na baadhi ya watu flani kuwaharibia jina wafanyakazi katika hospitali hiyo ili kuonekana watepetevu. 

Chanzo - Tuko News
Share:

JOGOO AUA ASKARI POLISI


Katika hali ya kushangaza  katika taifa la Ufilipino baada ya jogoo aliyekuwa akipigana kumuua afisa wa polisi baada ya polisi kuvamia mkoa wa Northern Samar kusitisha mchezo haramu wa vita vya jogoo. 

Afisa huyo wa polisi kwa jina Luteni Christine Bolok alikatwa na jogoo huyo akitumia wembe uliofungwa miguni ambapo ni kawaida katika mchezo wa vita vya jogoo.

SOMA ZAIDI HAPA CHINI

A Philippine police officer has been killed by a rooster during a raid on an illegal cockfight in the province of Northern Samar.

Lieutenant Christine Bolok was struck by the rooster's gaff - a razor-sharp steel blade which is typically attached to the leg of fighting roosters.

The blade cut his left thigh, slicing his femoral artery. He was rushed to hospital and declared dead on arrival.

Cockfighting has been banned during the virus outbreak.

Before the pandemic, it was allowed only in licensed cockpits on Sundays and legal holidays, as well as during local fiestas lasting a maximum of three days, according to the government news wire The Philippine News Agency (PNA).

Provincial police chief Colonel Arnel Apud told news agency AFP that the accident was "unfortunate", calling it "a piece of bad luck that I cannot explain".

"I could not believe it when it was first reported to me. This is the first time in my 25 years as a policeman that I lost a man due to a fighting cock's spur."

The police chief also sent his "deepest sympathy" to the victim's family, said PNA.

Three people were arrested and seven fighting roosters, two sets of gaff and 550 Philippine Peso ($11; £8) were confiscated, reported PNA.

Three other suspects remain at large.

Cockfighting is popular in the Philippines, typically attracting large crowds who bet on the outcome of fights between the birds.
Share:

KATIBU MKUU WA CCM AWATAKA WALIOSHINDA KATIKA UCHAGUZI MKUU KUWA NA NIDHAMU NA UWAJIBIKAJI


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi,(CCM), Dk.Bashiru Ally, amewataka viongozi wa chama hicho waliochaguliwa katika ngazi za Udiwani,Ubunge na Wawakilishi kuzingatia nidhamu ya chama na uwajibikaji.

Akizungumza hii leo Novemba 1,2020, Dk. Bashiru, amesema kuwa wanao mfumo kwenye jumuiya zao za chama na kamati za siasa za ngazi zote ambazo zitasimamia na kudai kuwa deni walilonalo ni kuhakikisha wanafanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

''Kwa mara ya kwanza chama chetu kimeingia na kumaliza uchaguzi kikiwa na umoja na mshikamano tukiwa tunaheshimiana na kusimamiana niwaombe wana CCM, wasianze kusherehekea ushindi huu kana kwamba kazi imeisha ila kiukweli kazi ngumu imeanza'',amesema Dk. Bashiru Ally

Aidha amesema siri kubwa ya ushindi walioupata ni umoja wao na kuongeza kuwa ushindi huo ni kutokana na kazi nzuri waliyoifanya katika miaka mitano iliyomalizika.

 Chanzo - EATV


Share:

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YATOA SIFA ZA VYAMA VYA SIASA KUPATA WABUNGE WA VITI MAALUM


Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Dkt. Wilson Mahera.
***
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesema kuwa tayari imeshatoa fomu kwa vyama vya siasa ili kupendekeza majina ya wabunge watakaopata nafasi ya kuwakilisha kupitia viti maalum na chama kitakachopata nafasi hiyo lazima kiwe na asilimia kuanzia 5% za kura za wabunge.

Akizungumza wakati akitoa taarifa fupi ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 28, 2020, katika hafla ya kumkabidhi cheti mshindi wa kiti cha Urais, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo, Dkt. Wilson Mahera, amesema kuwa chama kitakachopata angalau asilimia 5% ya kura za wabunge kitakuwa na uhalali wa kupata wabunge wa viti maalum.

"Chama kitakachopata angalau asilimia 5% ya kura za wabunge kitakuwa na uhalali wa kupata wabunge wa viti maalum", amesema Dkt. Mahera.

 Via EATV
Share:

POLISI SHINYANGA WAONYA WATAKAOTHUBUTU KUANDAMANA KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Debora Magiligimba 

Na Marco Maduhu- Shinyanga.
Jeshi  la Polisi mkoani Shinyanga, limewaonya viongozi wa vyama vya siasa pamoja na wafuasi wao, wasijaribu kufanya maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 28 mwaka huu ,bali waende mahakamani kupinga matokeo hayo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Debora Magiligimba ametoa onyo hilo leo Jumapili Novemba 1,2020 wakati akizungumza na waaandishi wa habari.

Amesema kuwa kuna matamko yametolewa na viongozi wa kisiasa kutaka kufanya maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima na kuanzia kesho ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu.

Kamanda Magiligimba amesema maandamano hayo ni batili, ambapo viongozi hao walipaswa kufuata sheria kwa kupinga matokeo hayo mahakamani, na siyo kufanya maandamano ambayo yana viashiria vya uvunjifu wa amani.

"Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga halitasita kamwe kuchukua hatua kali za kisheria, kwa kikundi chochote kile cha kisiasa chenye nia ya kuvuruga amani ya nchi," amesema Magiligimba.

"Kama wagombea hawajaridhika na matokeo ya uchaguzi mkuu wafuate sheria ,kanuni, na taratibu za nchi na kupeleka malalamiko yao Mahakamani na siyo kufanya maandamano ya bila kikomo yenye viashiria ya uvunjifu wa amani," ameongeza.

Pia amewataka wananchi wa mkoa wa Shinyanga kutojiingiza kwenye maandamano hayo, bali waendelee na shughuli zao za kila siku za kujiingizia kipato ,na wasiwe na hofu ikiwa ulinzi utaimarishwa kila kona.

Katika hatua nyingine amewaomba viongozi wa dini, kuendelea kusisitiza umuhimu wa amani kwa waumini wao,ili kuendelea kuilinda amani ya nchi iliyopo hivi sasa.

Share:

NEC YAMKABIDHI MAGUFULI CHETI CHA USHINDI KITI CHA URAIS TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akionesha Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais alichokabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage mara baada ya kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage mara baada ya kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, hafla hiyo ya kukabidhiwa Cheti imefanyika katika Makao Makuu ya Tume ya Uchaguzi NEC Njedengwa jijini Dodoma leo tarehe 01 Novemba 2020.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Makamu wa Rais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kiongozi wa Jopo la Waangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020 Rais Mstaafu wa Burundi Silvestre Ntibantunganya mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage leo tarehe 01 Novemba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama na Waliogombea Urais kupitia vyama Mbalimbali vya Upinzani nchini wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla fupi ya kukabidhi Cheti cha Ushindi kwa Kiti cha Urais zilizofanyika katika Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Njedengwa jijini Dodoma leo tarehe 01 Novemba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Ushindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wageni mbalimbali waliofika katika hafla fupi ya kukabidhiwa Cheti cha Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Share:

Dkt. Magufuli na Dkt. Mwinyi kuapishwa wiki ijayo


 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema shughuli ya kuapishwa kwa Rais Mteule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi na Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Magufuli zitafanyika wiki ijayo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama hicho jijini Dar es Salaam Polepole amesema Dkt. Mwinyi ambaye alishinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 28, 2020 ataapishwa Novemba 2, 2020 katika Uwanja vya Amani Zanzibar kuwa Rais wa awamu ya nane wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar baada ya rais Dkt. Ali Mohamed Shein kumaliza muda wake.

Siku mbili zimepita tangu Tume ya ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kumtangaza Dkt. Mwinyi kuwa mshindi wa kiti cha urais kwa kujipatia kura 380,02 sawa na asilimia 76.27 ya kura zote halali.

Kwa upande wa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, Polepole amebainisha kuwa shughuli ya kuapishwa kwake kuongoza dola kwa muhula itafanyika Novemba 5, 2020 katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma.

Dkt. Magufuli alitangazwa kuwa mshindi baada ya kupata kura 12,516,252 sawa na asilimia 84.4 ya kura zote halali.

Katibu mkuu huyo amewashukuru Watanzania wote kwa kuendelea kukiamini Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kukipatia ushindi wa kishindo, hivyo kuwataka kujitokeza kwa wingi katika matukio hayo muhimu la kuapishwa kwa viongozi wateule
.

Share:

Polisi yatoa onyo wanaotaka kuandamana


Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, CP Liberatus Sabas, amesema kuwa jeshi la polisi halitamvumilia mtu yeyote awe kiongozi wa chama au mfuasi, atakayefanya maandamano batili na kama kuna yeyote ambaye hakuridhika na matokeo afuate taratibu za kisheria kudai haki zao kama zipo.

CP Sabas ametoa kauli hiyo hii  Oktoba 31,2020, na kuwasihi akina mama kuongea na watoto wao kwamba, wasithubutu kushiriki katika maandamano hayo na wasije wakarubuniwa na watu ambao hawana nia nzuri na Taifa.

"Nasisitiza kwamba jeshi la polisi halitakuwa na simile kwa yeyote atakayejihusisha na chokochoko hizi ambazo tunaziona zinaanza kuanzishwa na watu hawa ambao hawalitakii mema Taifa hili, nawaomba akina mama mkanye mwanao kwa sababu mwisho wa siku mtoto atakapopata matatizo atakulilia mama, sasa kabla matatizo hayajamfika nakuomba mkanye mwanao", amesema CP Sabas.


Share:

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Aboubakar Kunenge atoa onyo kwa waliopanga kufanya vurugu Dar


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Aboubakar Kunenge ametoa onyo kwa watu au vikundi vya watu vilivyopanga kufanya vurugu mkoani kwake na kueleza kuwa sheria itachukua mkondo wake kwa yeyote atakayejaribu kuvuruga amani.

Kunenge ametoa onyo hilo wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC).

Mkuu huyo wa mkoa ameongeza kuwa jiji lipo kwenye hali ya amani na utulivu huku usalama ukiwa umeimarishwa
.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger