Friday 1 November 2019

TUZO YA "MWANZA QUALITY WINES" YAPOKELEWA KWA SHANGWE

 Kampuni ya Mwanza Quality Wines inayozalisha mvinyo wa matunda jamii ya Power Banana imeibuka mshindi wa jumla wa tuzo za kampuni 100 bora (Top 100 Awards) mwaka 2019/20 zinazotolewa chini ya uratibu wa kampuni ya ukaguzi wa hesabu za fedha KPMG kwa kushirikiana na Mwananchi Communications Limited (MCL).

Tuzo hizo zilitolewa Oktoba 25, 2019 jijini Dar es salaam huku mapokezi ya tuzo ya mshindi wa jumla yakifanyika Oktoba 31, 2019 katika uwanja wa ndege wa Mwanza ambapo hiyo ni hatua kubwa kwa kampuni ya Mwanza Quality Wines ambayo tuzo za mwaka 2018/19 ilishika nafasi ya 30.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kulia), Leopord Lema akijongea kupokea tuzo ya mshindi wa jumla wa kampuni 100 bora za kati Tanzania.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kulia), Leopord Lema akipokea tuzo hiyo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kulia), Leopord Lema akionesha tuzo hiyo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kulia), Leopord Lema
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kulia), Leopord Lema akifurahia tuzo hiyo pamoja na wafanyakazi wake.
Wafanyakazi wa Mwanza Quality Wines wakifurahia tuzo hiyo.
Wafanyakazi wa Mwanza Quality Wines wakifurahia tuzo hiyo.
Wafanyakazi wa Mwanza Quality Wines wakifurahia tuzo hiyo.
Wafanyakazi wa Mwanza Quality Wines wakiipokea kwa shangwe tuzo hiyo.
Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni ya Mwanza Quality Wines akifurahia tuzo hiyo.
Wafanyakazi wa Mwanza Quality Wines wakifurahia tuzo hiyo.
Huu ni mwaka wa tisa kwa tuzo za "Top 100 Awards" kutolewa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kushoto), Leopord Lema akifurahia tuzo hiyo pamoja na Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Florah Magabe (kulia).
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanza Quality Wines (kulia), Leopord Lema akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.
Viongozi, wafanyakazi na wadau mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Picha ya pamoja baada ya mapokezi ya tuzo.
Wafanyakazi wa Mwanza Quality Wines.
Wafanyakazi wa kampuni ya Mwanza Quality Wines wakiwa kwenye mapokezi hayo.
Habari kuhusu kampuni ya Mwanza Quality Wines kutwaa ushindi miongoni mwa makampuni 100 bora Tanzania yanayokua kwa kasi ilichapishwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari.
Tazama Video hapa chini


Share:

Procurement Officer Job Opportunity at HelpAge International

Position: Procurement Officer Location: Dar es salaam Job Summary HelpAge International wishes to recruit a Procurement Officer (PO) that will be based in Dar Es Salaam with frequent field visit to support programmes implemented in collaboration with different partners. A summary of the job purpose and person specification is indicated below while the full Job Description will be… Read More »

The post Procurement Officer Job Opportunity at HelpAge International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Communications Job Opportunity at Room to Read – Officer

Position: Officer, Communications Tanzania – Main – Dar Es Salaam Position Overview The person in this role spends the majority of his or her time providing global marketing and awareness, fundraising, and country-specific communications support. This primarily includes providing material development and donor engagement support. It also includes vendor management and reporting, as well as local awareness and… Read More »

The post Communications Job Opportunity at Room to Read – Officer appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

6 Jobs Opportunities at ELCT Eastern and Coastal Diocese

Position: Cleaners/ Room Attendants (3) Location: Dar es salaam Job Summary ELCT- ECD is actively looking for an outstanding Cleaners/ room attendant (3) Qualifications Applicant should possess the relevant skills and certificates from a recognized college. At least one year working experience in the similar position General conditions to be observed Good standard of personal presentation Should have… Read More »

The post 6 Jobs Opportunities at ELCT Eastern and Coastal Diocese appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Data Analytics and Visualization Specialist Job Opportunity at ICAP Tanzania

Data Analytics and Visualization Specialist Position Summary: The Data Analytics and Visualization Specialist is responsible for designing and implementing a strategic vision for electronic systems to analyze, report, visualize, and disseminate program data. S/he will work closely with the Project Director and project team to implement innovative data visualization tools. Major Accountabilities: • Working in close coordination with… Read More »

The post Data Analytics and Visualization Specialist Job Opportunity at ICAP Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Director Of Professional Development Job Opportunity UTUMISHI

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA PRESIDENT’S OFFICE PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT Ref.No.EA.7/96/01/K/98 31st October, 2019 VACANCY ANNOUNCEMENT- (RE- ADVERTISED) On behalf of The Procurement and Supplies Professionals and Technicians Board (PSPTB) President’s Office, Public Service Recruitment Secretariat invites competent, experienced, highly organized and self-motivated Tanzanians to fill 1 vacant post mentioned below;- THE PROCUREMENT AND SUPPLIES PROFESSIONALS AND TECHNICIANS… Read More »

The post Director Of Professional Development Job Opportunity UTUMISHI appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

5 Safety Officers Job Opportunities at HR World

Position: SAFETY OFFICERS (5 POSITIONS) Location: GEITA  NYAKANAZI HR World on behalf of our reputable client (Construction Company) we are looking for a safety Officer to work on a Transmission line project. QUALIFICATIONS: Bachelor degree in Environmental Engineering or any related field REQUIREMENTS: Minimum 3 years’ experience in similar position. Must have experience in electrical projects. RESPONSIBILITIES: Mantain… Read More »

The post 5 Safety Officers Job Opportunities at HR World appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali Yawatoa Hofu Wananchi Wa Handeni Mkoani Tanga

Serikali imewahakikishia wakazi wa Handeni, Mkoani Tanga uendelevu wa huduma ya maji licha ya kuharibika kwa miundombinu ya maji kulikosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga ametoa kauli hiyo hapo juzi wilayani hapa wakati wa ziara yake iliyolenga kukagua athari ya mvua kwenye miundombinu ya maji sambamba na kupata ufumbuzi wa haraka kufuatia hali ya mvua zilizonyesha kwa takribani wiki mbili mfululizo.

Mara baada ya kujionea hali halisi, Mhandisi Sanga aliwatoa hofu wananchi wa Handeni ambapo aliwataka kuwa watulivu na aliahidi kuwa Serikali itahakikisha huduma ya maji inarejea haraka iwezekanavyo.

"Ninawasihi wananchi kufanya subira na kuwa watulivu na kuzingatia maelekezo ya Serikali," alisisitiza Naibu Katibu Mkuu Sanga.

Mhandisi Sanga alibainisha kuwa zoezi la tathmini ya athari ya mvua hizo kwenye miundombinu ya maji wanaloendelea nalo halitochukua zaidi ya siku tatu kama ilivyoagizwa na Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa.

"Waziri wa Maji ametuagiza kuharakisha kukamilisha zoezi hili, nasi tutahakikisha linafanyika kwa kasi ikiwa ni pamoja na kutazama njia mbadala ili wananchi wapate huduma ya maji kwa haraka," alisema Mhandisi Sanga.

Aliongeza kuwa Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli haipo tayari kuona wananchi wake wanataabika na kwamba hatua madhubuti na za haraka zinachukuliwa ili kuhakikisha wananchi wanapata maji.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigela akielezea kwa ujumla athari za mvua hizo kwenye Mkoa wa Tanga, alisema kuwa zimeleta madhara kwenye miundombinu ya barabara na madaraja na kusababisha huduma ya usafiri katika maeneo mbalimbali kuathirika.

“Tulichokibaini katika mvua hizi zilizonyesha ni kuwa zimeharibu mabwawa ya maji na kusababisha maji yaliyotoka katika mabwawa hayo kuathiri miundondombinu mbalimbali ikiwemo ya maji na barabara,” alieleza Shigela.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe akielezea athari za mvua hizo alisema ni pamoja na kuharibika kwa mabwawa 11 ya maji yanayotumiwa na wakazi wa Handeni na maeneo jirani na kati ya hayo yapo mabwawa makubwa matano ambayo aliyataja kuwa ni Kwenkambara, Mandera, Suwa, Msomera na Mkomba.

Aidha, Gondwe alipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna inavyotekeleza majukumu yake kwa wakati na kwa hatua mbalimbali za haraka zinazoendelea kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kurejesha mawasiliano ya miundombinu ya barabara na maji iliyoathirika.

Sambamba na hilo, Gondwe alimpongeza Mhandisi Sanga na timu ya wataalam aliyoambatana nayo kutoka Wizara ya Maji na taasisi zake kwa kufika Wilayani hapa mapema ili kufanya tathmini ya uharibifu wa miundombinu ya mabwawa ya maji ili kupata ufumbuzi.

“Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Handeni tunatoa shukrani nyingi sana kwa Mheshimiwa Rais kwa kutujali na kuwatuma watendaji wa Serikali kufika hapa Handeni ili kutatua matatizo yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha,” alisema Gondwe.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA), Mhandisi Clement Kivegalo ambaye ameambatana na Naibu Katibu Mkuu Sanga alisema kuwa wanaendelea na tathmini ila kwa mabwawa yaliyopasuka wamebaini yalijengwa chini ya kiwango na pia hayakuwa yakitunzwa inavyostahili na hivyo kupelekea kuharibika wakati mvua hizo zilizonyesha.


Share:

Kundi la IS latangaza kiongozi mpya Atakayemrithi Abu Bakr al-Baghdadi

Kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS limemtangaza kiongozi wake mpya baada ya kuthibitisha kifo cha kiongozi wake Abu Bakr al-Baghdadi katika shambulizi lililofanywa na Marekani nchini Syria. 

Taarifa iliyotolewa kwenye chombo cha habari cha IS, al-Furqan imeeleza kuwa nafasi ya al-Baghdadi itazibwa na Abu Ibrahim al-Hashimi al-Qurayshi. 

Kundi la IS halikutoa taarifa zaidi kuhusu al-Qurayshi. Kiongozi huyo mpya anatambuliwa kama msomi, shujaa mashuhuri na kiongozi wa kivita ambaye amepambana na majeshi ya Marekani na ana ufahamu kuhusu vita hivyo. 

Taarifa hiyo pia imethibitisha kifo cha Abu Hassan al-Muhajir, msaidizi wa karibu wa al-Baghdadi ambaye alikuwa pia msemaji wa IS tangu mwaka 2016.

 Vifo hivyo ni pigo kubwa kwa kundi la Dola la Kiislamu karibu miezi saba tangu lilipofurumushwa kutoka kwenye ngome yake ya mwisho nchini Syria.


Share:

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro asimamia Zoezi la wanafunzi Watoro kuchapwa viboko mbele ya wazazi wao

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro jana Alhamisi  alisimamia zoezi la  kucharazwa viboko wanafunzi 3 ambao ni watoro sugu katika Shule ya Msingi Ligoma iliyoko wilayani humo ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kupambana na utoro sugu, nidhamu za wanafunzi na mimba za utotoni Tunduru.

Mkuu huyo wa wilaya  alimtaka mwalimu Mkuu wa shule hiyo kuwachapa viboko vinne wanafunzi hao na kuagiza  wapewe adhabu nyingine zisizohusiana na viboko, ikiwa ni pamoja na kuchimba visiki.

Baada ya viboko hivyo, aliwauliza wanafunzi hao lini wataanza kwenda shule na mmoja alijibu kuwa ataripoti Jumatatu,hata hivyo, mkuu huyo wa Wilaya alisema wote wanapaswa kuripoti leo.


Share:

Ahukumiwa Kifungo Cha Maisha Jela Kwa Kumbaka na Kumpa Mimba Mtoto wake wa Kumzaa

Mahakama ya  Wilaya ya  Mpanda  Mkoani  Katavi  imemuhukumu  Lazaro  Charles (35)  Mkazi    wa Mtaa wa  Mji   Mwema katika  Manispaa ya   Mpanda Mkoa wa  Katavi kutumikia jela kifungo cha maisha baada ya kupatikana na hatia ya kumpa mimba mtoto wake wa kumzaa  mwenye (14) ambaye ni, mwanafunzi wa  darasa la  saba shule ya msingi  Majengo Manispaa ya  Mpanda.

Hukumu  hiyo iliyovuta hisia za wakazi  wengi  wa  Manispaa ya Mpanda, ilitolewa na Hakimu Mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Gosper Luoga baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa Mahakamani na upande wa mashtaka.

Awali katika kesi hiyo Mwanasheria wa Serikali Gregory  Muhangwa aliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo kwa nyakati tofauti hapo Januari 1 mwaka 2017 na April 29, 2019.

Mshtakiwa huyo alikuwa akitenda kosa hilo huko nyumbani kwake wakati mke wake ambaye ni mama  mzazi wa mtoto huyo alipokuwa amesafiri ndipo alipokuwa akiingia kwenye chumba alichokuwa akilala mtoto wake huyo na kumbaka kwa nguvu.

Mwendesha mashtaka huyo alieleza kuwa baada ya kuwa anambaka  alikuwa akimwekea majani kwenye sehemu zake za siri kama dawa ya kienyeji  ya  kumwondolea maumivu.

Hakimu Luoga amemtaka mshtakiwa kama atakuwa na sababu yoyote ile ya msingi ambayo inaweza kuifanya mahakama iweze kushawishika ili kumpunguzia adhabu basi inatoa nafasi kujijitetea.

Lazaro Charles ameiomba mahakama  impatie nakala ya hukumu ya mwenendo wa kesi hiyo tu kwani hana utetezi wowote ule.

Baada ya ombi hilo la mshtakiwa mwanasheria wa Serikali Gregory Muhangwa aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa wazazi wengine wenye tabia kama hiyo.

Hakimu Luoga baada ya kusikiliza pande hizo mbili alisoma hukumu na kuiambia Mahakama kuwa mshtakiwa amepatikana na kosa la kifungu cha sheria Namba 158 (1) (a ) SURA YA 16 ya marejeo 2002, hivyo Mahakama inamuhukumu kutumikia kifungo cha maisha jela kuanzia leo Novemba 1, 2019.


Share:

Idris Sultan Aripoti Tena Polisi

Msanii wa vichekesho, Idris Sultan leo Ijumaa Novemba 1, 2019 saa 2 asubuhi ameripoti Kituo cha Polisi ‘Central’ jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya masharti ya dhamana aliyopatiwa jana October 31, 2019.

Idriss alitakiwa kwenda polisi baada ya kuweka picha yenye sura yake huku akiwa ameketi katika kiti chenye nembo ya Taifa na kuambiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuripoti kituo chochote cha Polisi.


Share:

Twitter yapiga marufuku matangazo ya kisiasa

Jukwaa la mtandao wa kijamii Twitter limetangaza kwamba halitatangaza tena matangazo yenye muelekeo wa kisiasa.

Kiongozi mkuu ( CEO) wa Twitter, Jack Dorsey amearifu kwamba shirika hilo halitatoa tena matangazo yenye muelekeo wa kisiasa.

Dorsey amearifu kwamba uamuzi huo mpya utaanza kutumika mwishoni mwa mwezi Novemba.

Washindani wa mtandao wa kijamii wa Facebook hivi karibuni walifutilia mbali mpango wa kupiga marufuku matangazo ya siasa ya kibiashara.

Taarifa ya marufuku hiyo imeibua mgawanyiko katika kambi za kisiasa nchini Marekani zinapojiandaa katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Brad Parscale,meneja wa kampeni ya Raisi Donald Trump, kugombea muhula wa pili, amesema marufuku hiyo ni jaribio jingine la kumnyamazisha Trump


Share:

WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO KUELEKEA UCHAGUZI

Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC) kwa kushirikiana na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Mwanza kwa lengo la kuwajengea uwezo kuripoti kwa weledi habari kuhusu ujenzi wa amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi. Mafunzo hayo yamefanyika Oktoba 31, 2019 Holmand Hotel jijini Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Edwin Soko akitoa salamu kwenye ufunguzi wa warsha hiyo.
 Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Rose Mwanga akitoa neno la shukurani wakati wa kuahirisha mafunzo hayo.
Wanahabari wakimsikiliza na kunasa habari kwenye warsha hiyo. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo yenye Tija kwa Watu wote (PCD), Prof. Francis Matambalya akitoa utambulisho kuhusu Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) kwenye warsha hiyo. PCD ni idara ndani ya MNF.
 Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo wanahabari mkoani Mwanza kuandika habari kwa weledi kabla, wakati na baada ya chaguzi.
Tazama Video hapa chini


Share:

Idris Sultan Aachiwa kwa Dhamana.....Kuripoti tena Polisi Leo

Msanii  Idris Sultan aliyehojiwa na polisi  jana Alhamisi Oktoba 31, 2019 kwa saa tano na kupekuliwa nyumbani kwake ameachiwa kwa dhamana usiku wa kuamkia leo.

Baada ya kuhojiwa, mchekeshaji huyo ambaye jana alitakiwa kuripoti polisi na mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alikwenda na polisi nyumbani kwake.
 
Wakili wake, Benedict Ishabakaki amesema licha ya kwamba Msanii huyo ameachiwa kwa dhamana usiku, atatakiwa kuripoti tena Kituo cha Polisi leo saa mbili asubuhi ili Polisi waendelee na upelelezi wao.

Idris alitakiwa kwenda polisi baada ya kuweka picha yenye sura yake huku akiwa ameketi katika kiti chenye nembo ya Taifa.

Pia, Idris aliweka picha nyingine inayoonyesha sura ya Rais Magufuli akiwa amesimama huku amevaa suruali yenye mikanda inayoshikizwa mabegani


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa November 1























Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger