Friday 1 November 2019

WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAKUMBUSHWA WAJIBU WAO KUELEKEA UCHAGUZI

...
Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC) kwa kushirikiana na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari mkoani Mwanza kwa lengo la kuwajengea uwezo kuripoti kwa weledi habari kuhusu ujenzi wa amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi. Mafunzo hayo yamefanyika Oktoba 31, 2019 Holmand Hotel jijini Mwanza.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Edwin Soko akitoa salamu kwenye ufunguzi wa warsha hiyo.
 Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Rose Mwanga akitoa neno la shukurani wakati wa kuahirisha mafunzo hayo.
Wanahabari wakimsikiliza na kunasa habari kwenye warsha hiyo. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo yenye Tija kwa Watu wote (PCD), Prof. Francis Matambalya akitoa utambulisho kuhusu Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF) kwenye warsha hiyo. PCD ni idara ndani ya MNF.
 Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo wanahabari mkoani Mwanza kuandika habari kwa weledi kabla, wakati na baada ya chaguzi.
Tazama Video hapa chini


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger