Saturday, 31 January 2026

WAZIRI MKENDA AWAAGA VIJANA 16 WANAOKWENDA KUSOMEA MASOMO YA SAYANSI AFRIKA KUSINI


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amewaaga vijana 16 watakaokwenda kusomea masomo ya sayansi na teknolojia katika Chuo Kikuu cha Johannesburg, Afrika Kusini kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended.

Akizungumza leo Januari 30, 2026 jijini Dar es Salaam katika hafla hiyo iliyofanyika katika Ofisi za Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Prof. Mkenda amesisitiza kuwa mpango huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuongeza idadi ya wataalamu wa sayansi na teknolojia nchini, hususan katika nyanja za Data Science, Akili Unde na Allied Sciences.

Mpango wa Samia Scholarship Extended unalenga kutoa fursa kwa wanafunzi bora wa Kitanzania waliopata ufaulu wa juu katika Kidato cha Sita, hasa kwenye masomo ya sayansi ikiwemo Advanced Mathematics.

Prof. Mkenda amesema wanufaika wote 50 wanatoka shule mbalimbali za kata, serikali na binafsi, jambo linaloonyesha kuwa fursa hii inatolewa kwa wote wenye uwezo bila kujali asili ya shule au familia.

Ameongeza kuwa Baada ya kundi la kwanza, serikali imepanga kupeleka wanafunzi wengine 34 katika vyuo vya kimataifa vilivyoko Ireland Kaskazini.

Aidha ameeleza kuwa Tanzania inahitaji wataalamu wengi zaidi katika nyanja za sayansi na teknolojia ili kuendana na kasi ya maendeleo ya dunia.

Prof. Mkenda alisisitiza kuwa teknolojia ni matokeo ya matumizi ya sayansi, hivyo serikali imeweka mikakati madhubuti ya kuandaa wataalamu kupitia programu ya Samia Scholarship Extended.

"Mpango huu unalenga kuongeza idadi ya wataalamu wa fani muhimu ikiwemo Data Science, Artificial Intelligence, Allied Sciences na Sayansi ya Nyuklia, ambapo wanafunzi wa shahada ya kwanza na uzamili wanapatiwa ufadhili wa masomo ndani na nje ya nchi". Amesema 

Prof. Mkenda amebainisha kuwa kuanzishwa kwa ufadhili wa masomo ya Sayansi ya Nyuklia ni kutokana na uwepo wa madini ya urani nchini na umuhimu wake katika tiba na kilimo.

Amesema kuwa tayari wanafunzi wa shahada ya uzamili wameanza kusomea fani hiyo nje ya nchi na wanafunzi bora wa shahada ya kwanza watapelekwa kusomea nje ya nchi katika vyuo vikuu mahiri.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa Nombo, amesema serikali itaendelea kuwekeza kwenye programu za kimkakati kama Samia Scholarship Extended DS/AI, kwa kuwa zinasaidia kujenga msingi wa maendeleo ya muda mrefu kupitia sayansi na teknolojia.

Profesa Nombo amewataka wanafunzi kuzingatia kuwa wao ni mfano kwa vijana wengine waliopo mashuleni, na kwamba nafasi hizo zinapatikana kwa misingi ya ushindani wa kitaaluma (merit-based), hivyo wanafunzi wajitahidi katika masomo hasa ya sayansi na TEHAMA.

Amesema uwepo wa taasisi kama Nelson Mandela Institute of Science and Technology umechangia kwa kiasi kikubwa kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kitaaluma na maisha, ikiwemo financial management na stadi za karne ya 21.

Mmoja wa wanufaika wa programu hiyo, Malaika Florence, amesema mafunzo ya awali waliyopata kupitia boot camp yamewajengea uwezo mkubwa katika masuala ya usimamizi wa fedha, matumizi ya teknolojia na kujiamini katika mazingira ya kimataifa.

Amesema awali wengi wao walikuwa hawana ujuzi wa msingi wa matumizi ya kompyuta, lakini sasa wamejifunza stadi za kisasa ikiwemo uandishi wa codes, matumizi ya lugha mbalimbali za programu kama Python na Java, pamoja na mbinu za kujifunza kwa kujitegemea.

Malaika ameongeza kuwa wamejifunza pia sera za uhamiaji, namna ya kuishi na watu wa tamaduni tofauti, pamoja na umuhimu wa kujenga mitandao ya kitaaluma, akisisitiza kuwa “maisha ni watu” na mafanikio yanahitaji ushirikiano.

Naye Aswile Simon, ambaye amepata nafasi ya kwenda kusoma katika Chuo Kikuu cha Johannesburg nchini Afrika Kusini, amemshukuru Rais Samia kwa kuanzisha programu hiyo, akisema pasipo uongozi wake vijana wengi wasingeweza kupata fursa adimu kama hiyo.

Aswile amesema wanafunzi wanatambua imani kubwa waliyopewa na Taifa, hivyo wana wajibu wa kusoma kwa bidii na kurejea nchini wakiwa na maarifa yatakayosaidia kuendeleza sekta ya teknolojia, uchumi wa kidijitali na ubunifu.

Sambamba na hayo wanafunzi wote nchini wameaswa kuchangamkia masomo ya sayansi na teknolojia, huku serikali ikiombwa kuendelea kupanua wigo wa programu za ufadhili wa masomo ili kuzalisha wataalamu wengi watakaoliwezesha Taifa kufikia malengo ya maendeleo ya muda mrefu
Share:

Friday, 30 January 2026

NITASIMAMIA KILA MWANANCHI MWENYE UHALALI WA KUMILIKI ARDHI, ANAPATA HATI YAKE: NAIBU WAZIRI MMUYA

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya amesema atahakikisha anasimamia kila mwananchi mwenye  uhalali wa kupata hati milki ya eneo lake analomiliki anapata hati.

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye Kliniki Maalum ya Ardhi inayoendelea katika Ofisi za Ardhi Mkoa wa Dodoma tarehe 28 Januari, 2026 Mhe. Mmuya amesema, upo umuhimu wa kuhakikisha wananchi waliokamilisha taratibu za kumilikishwa wanapata hati zao kwa kuwa wapo waliofuatilia kwa muda mrefu. 

"Nitasimamia kuhakikisha kila mwananchi mwenye uhalali wa kumiliki Ardhi anapata hati yake kwa wakati”  amesema Naibu Waziri Mmuya.

Ili kutoa huduma bora, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amewataka wataalamu wa Sekta ya Ardhi nchini kuhakikisha wanatoa elimu ya matumizi bora ya ardhi pamoja na jinsi ya kupata hatimiliki za ardhi, hatua aliyoieleza itasaidia kuepusha ujenzi holela  unaoenda kinyume na matumizi yaliyopangwa.

Mhe. Mmuya amesema, Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kusimamia haki ya umiliki wa ardhi kwa vitendo na kuhakikisha wamiliki wa ardhi wanapata hati zao.

Ameeleza kuwa, Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inawahakikishia wananchi kuendelea kupata huduma za hati katika maeneo mbalimbali nchini.

Ameongeza kuwa, wizara hiyo chini ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Leonard Akwilapo imeweka mkakati wa siku 14 kuhakikisha  kila mwananchi wa Jiji la Dodoma aliyekidhi vigezo vya kupata hati milki ya ardhi anapata hati yake hatua aliyoieleza kuwa,  itaidia kurahisisha huduma na kulinda haki za wananchi.

Awali, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga amesema, wamiliki wa ardhi waliokamilisha taratibu za umiliki wapewe Hatimiliki zao na hawahitaji maneno mengi.

Mhandisi Sanga amesisitiza kuwa, ni marufuku kwa mtumishi wa sekta ya ardhi anayefutwa na mwanachi mwenye shida kumwambia aende kwa mtu mwingine kupata huduma na kueleza kuwa, atasimamia msimamo huo kwa kuwa mwananchi anachohitaji ni huduma.

Katika siku ya kwanza ya zoezi hilo, tayari zaidi ya Hatimiliki 150 zimetolewa  ambapo Edward Aloyce na Colletha Magema miongoni mwa wananchi waliopata hati zao wamethibitisha kwamba, zoezi hilo ni muhimu na linawasaidia wananchi kupata hati za ardhi kwa lengo la kumiliki maeneo yao kihalali.

Zoezi la Kliniki Maalum ya Ardhi ambayo imejikita kutoa Hatimiliki za Ardhi katika jiji la Dodoma ni la siku 14 kuanzia 28 Januari hadi Februari 10, 2026.


Share:

Thursday, 29 January 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 30, 2026

Share:

SERIKALI YATOA MIKOPO KIASI CHA SHILINGI MILIONI 600 KWA WANANCHI



Na Josephine Manase, Morogoro

Halmashauri ya Mji Ifakara Januari 27,2026 imetoa mikopo ya asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi milioni 600 ikiwa ni Mikopo ya Asilimia 10 inayotokana na Mapato ya ndani kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ikiwa ni utekelezaji wa sera ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo hiyo iliyofanyika katika Viwanja vya Stendi ya mabasi kibaoni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felista Mdemu, ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kuendelea kutekeleza kwa vitendo azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo isiyo na riba.

Mdemu amevitaka vikundi vilivyonufaika kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa, kuzingatia masharti ya mikataba, pamoja na kurejesha mikopo kwa wakati ili kutoa fursa kwa wananchi wengine kunufaika.

Shilingi 404,787,300 tayari imekwishatolewa kwa vikundi 41, vikiwemo vikundi 20 vya wanawake, 17 vya vijana na 4 vya watu wenye ulemavu na Shilingi 195,212,700 zitatolewa kwa vikundi 17 vilivyosalia mara baada ya kukamilisha maboresho yaliyoelekezwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara, Pilly Kitwana amewasihi wananchi wa Halmashauri ya Mji Ifakara kuendelea kuunda Vikundi kwani pesa bado zipo ambazo zitasaidia kuwainua pia ameahidi kuendelea kufanya tathimini na ufuatiliaji kwa vikundi vilivyonufaika ili kuhakikisha mikopo hiyo inaleta tija na kuchangia maendeleo ya kiuchumi kwa wanufaika na jamii kwa ujumla.





Share:

Wednesday, 28 January 2026

KIJANA APITIA MATESO MAZITO LAKINI AKAJA KUWA MTU MAARUFU DUNIANI



Nilizaliwa kwenye familia ya kawaida sana, bila jina, bila mtaji, na bila mtu wa kunisukuma mbele. Wakati wenzangu walionekana kuwa na mwelekeo maishani, mimi nilikuwa napambana na umaskini, kejeli na kukataliwa kila mahali nilipojaribu.

Shuleni nilidharauliwa, mitaani nilionekana kama asiye na maana, na hata nyumbani nilionekana kama mzigo. Kila nilipoonyesha ndoto zangu, watu walicheka. Mateso yangu hayakuishia hapo. Nilipofika utu uzima, nilipitia kushindwa mara kwa mara.

Kazi nilikosa, miradi ilifeli, marafiki walinigeuka. Nililala njaa siku kadhaa, nikihama makazi mara kwa mara, nikiishi kwa msaada wa watu. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa na kipaji, lakini kilionekana kama kimefungwa.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 28,2026




Magazeti






Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger