Sunday, 19 October 2025

DKT. JUDITH AWAOMBA WATANZANIA KUENZI AMANI



Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwanamke na Nguvu ya Kijani, Dkt. Judith Mhina Spendi, ametoa wito kwa Watanzania wote kusimama pamoja kulinda amani ya taifa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Dkt. Judith alitangaza kongamano la amani litakalofanyika kuanzia Oktoba 25 hadi 27, 2025 katika Viwanja vya Posta Kijitonyama, likiwakutanisha viongozi wa dini, vijana, wafanyabiashara, na taasisi mbalimbali zenye malengo ya kuhamasisha amani na mshikamano wa kitaifa.

Dkt. Judith alisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo, akieleza kuwa Tanzania imeendelea kupiga hatua kubwa kiuchumi kutokana na utulivu wa kisiasa na kijamii uliopo.

“Hakuna maendeleo bila amani, hakuna uchaguzi huru bila utulivu, na hakuna taifa imara bila mshikamano,” alisema Dkt. Judith.

Aidha, alitoa rai kwa Watanzania wote kuwa sauti ya amani, umoja na ukweli, akihitimisha hotuba yake kwa ujumbe wenye mguso wa kipekee kwa taifa:

Kongamano hilo linatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kuimarisha ari ya amani na utulivu kabla, wakati, na baada ya uchaguzi, huku likiwakutanisha wadau mbalimbali wanaojali mustakabali wa taifa.





Share:

Saturday, 18 October 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOB 19,2025

 

Magazeti
Share:

TUTAWADHIBITI WOTE WANAOCHOCHEA HOMA ZA UCHAGUZI :KANALI MTAMBI



Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi amewaonya wale wote watakaojaribu kuhamasisha ama kuleta uvunjifu wa amani wakati wa mchakato wa uchaguzi Mkuu hapo Oktoba 29, 2025 akitahadharisha wale wote wanaotaka kupandisha homa ya uchaguzi kutojaribu kufanya hivyo kwani watashughulikiwa ipasavyo kwa mujibu wa sheria za nchi.

Kanali Mtambi ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Oktoba 17, 2025 katika ukumbi wa Mwembeni Complex katika ufunguzi wa Mafunzo ya walimu kutoka mikoa minane ya Kanda ya ziwa na Kanda ya Magharibi, mafunzo yanayofanyika Mkoani humo, akiwahakikishia waalimu hao na wananchi wa Mkoa huo kuwa wamejipanga kikamilifu ,kuhakikisha kila mmoja anatumia haki yake ya kuchagua Kiongozi amtakaye katika mazingira tulivu na yenye amani na usalama wa kutosha.

"Huu ni mwaka wa uchaguzi na mwezi huu ndiyo hasa tumefika kunako sasa shughuli za kisiasa zimekuwa zikiendelea vizuri katika Mkoa wetu, Vyama vyote vimepata fursa sawa, Wagombea wamepata muda mzuri wa kunadi sera zao, Wananchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kusikiliza Wagombea kupitia Vyama mbalimbali, demokrasia Mkoa wa Mara imekua na inaendelea kupevuka."


"Naomba pia nitumie fursa hii kama Mwenyekiti wa Kamati ya usalama Mkoa, niwatanabaishe wale ambao wakati wa uchaguzi homa ya uchaguzi inapopanda inakimbilia kichwani na kuleta mfetuko wa vichwa, sasa vichwa vikifetuka wengine hufanya mambo yasiyokubalika, 

nitumie fursa hii kutoa onyo kwao, homa ya uchaguzi ikikupanda tafakari vizuri sera na itkadi ya Chama chako, usiniletee fujo katika Mkoa wa Mara na kama utajaribu utakutana na moto mkali kweli kweli na hapa sipepesi macho, hatutamvumilia yeyote atakayechafua hali ya hewa kwasababu tu amepata homa ya uchaguzi akaamua kujifanya kuwa kichaa, naomba asiwepo yeyote mwenye wazo la namna hiyo." Amesema Mhe. Mtambi.

Mtambi Alisema Mkoa wa mara Vyama vyote katika Mkoa huo vinaendelea kufanya kampeni zake za Amani na Utulivu suala linalotoa fursa ya ushiriki wa wananchi kwenye mikutano ya Kampeni kwa Vyama mbalimbali vya siasa katika Mkoa huo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 18,2025



Magazeti


Share:

Friday, 17 October 2025

TMA YATANGAZA MWELEKEO WA MVUA ZA MSIMU WA NOVEMBA 2025 HADI APRILI 2026


:::::::::::

Na Mwandishi Wetu

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza mwelekeo wa mvua za msimu wa Novemba 2025 hadi Aprili 2026 kwa maeneo yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka, ikidai kuwa msimu huo utatawaliwa na vipindi virefu vya ukavu pamoja na mtawanyiko wa mvua usioridhisha katika maeneo mengi.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk. Ladislaus Chang’a ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa (IPCC), amesema mvua zinatarajiwa kuanza mwezi Novemba na kumalizika kati ya Aprili na Mei 2026, lakini hazitakuwa za kuridhisha katika maeneo mengi.
Maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni pamoja na mikoa ya magharibi (Kigoma, Tabora, Katavi), kanda ya kati (Singida, Dodoma), nyanda za juu kusini magharibi (Njombe, Iringa, Mbeya, Songwe, Rukwa), kusini (Ruvuma), ukanda wa pwani ya kusini (Lindi, Mtwara), pamoja na kusini mwa Morogoro.

Amesema mvua hizo zinatarajiwa kuisha kati ya wiki ya nne ya mwezi Aprili na wiki ya kwanza ya mwezi Mei 2026 katika maeneo mengi yanayopata mvua za msimu.

Dk. Chang'a amesema ongezeko la mvua linatarajiwa katika kipindi cha nusu ya pili ya

msimu unaonza mwezi Februari mpaka Aprili, 2026 ikilinganishwa na nusu ya kwanza ya mwezi Novemba, 2025 mpaka Januari, 2026.

Pamoja na mvua hizo kuwa za wastani hadi chini ya wastani, Dk. Chang'a ametoa angalizo uwepo wa matukio ya vipindi vya mvua kubwa yanaweza kujitokeza hata katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua za chini ya wastani. Dk. Chang'a amewashauri wadau kufuatilia taarifa za utabiri wa saa 24, siku 10, mwezi na tahadhari kama zinavyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ili waweze kujua mabadiliko yanayotokea katika mifumo ya hali ya hewa kwa kila siku.




PICHA ZOTE NA JAMES SALVATORY TORCH MEDIA
Share:

WENJE AFUNGUKA: KUHAMA SI USALITI, NI KUTAFUTA ‘LIGI KUU’ YA MAENDELEO



Aliyekuwa nguli wa siasa za upinzani na Mwenyekiti wa Kanda ya Victoria (Kanda ya Ziwa) wa Chadema, Ndugu Ezekia Wenje, amesisitiza  kuwa uamuzi wake wa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) haupaswi kuchukuliwa kama kitendo cha usaliti, bali ni uamuzi wa uzalendo wa kimkakati wa kutafuta eneo bora la kufanyia siasa kwa maendeleo ya wananchi.

Akizungumza kwa hisia kali wilayani Muleba, mkoani Kagera, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wenje alibainisha kuwa CCM ndicho chama kinachompa fursa kiongozi kushiriki moja kwa moja katika kutatua changamoto za wananchi na kusukuma mbele ajenda za maendeleo ya Taifa.

Wenje, ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Nyamagana na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alifichua wazi sababu kuu za chama hicho kususia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akieleza kuwa chama hicho kimepoteza mwelekeo na kufilisika kisiasa.

Alisema, uamuzi wa kususia Uchaguzi Mkuu unaonyesha wazi ukosefu wa mshikamano na udhaifu mkubwa wa chama hicho kisiasa. Wenje alibainisha kuwa migogoro ya muda mrefu, hasa mivutano baina ya viongozi wake wakuu (akiitaja Team Mbowe na Team Lissu), imevuruga misingi ya chama, kuharibu umoja, na kuwavunja moyo maelfu ya wanachama, na hivyo kusababisha Chadema kutokuwa na nguvu za kushindana kihalali.

"Ukiona kiongozi wa Chadema anasema yuko tayari kwa lolote, ujue amekata tamaa. Kazi ya kiongozi ni kuonesha njia, si kukatisha tamaa wafuasi wake," alisema Wenje kwa msisitizo, akisisitiza kuwa chama hicho kimegeuka kuwa chombo cha misukumo ya wanaharakati wanaofadhiliwa na taasisi za kimataifa, badala ya kuwa chama cha kisiasa kinacholenga kuunda sera.

Wenje alihitimisha kwa kusisitiza, "CCM ni chama chenye mfumo, maono na dira. Ndiyo maana nimeondoka kwenye siasa za mchangani na kurudi hapa kushiriki katika kazi ya kweli ya kujenga Taifa, kwa kushirikiana na Dkt. Samia Suluhu Hassan na chama chake."

Share:

WANANCHI WASHANGILIA TASNIA YA MICHEZO KUWA AJIRA, AFYA

Tanzania inaelekea katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 ikiwa na taswira mpya katika sekta ya michezo, shukrani zikielekezwa moja kwa moja kwa jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ameigeuza tasnia hiyo kuwa nyenzo muhimu ya kiuchumi na kijamii. Maendeleo haya yametajwa kuwa maajabu na wananchi ambao wamepaza sauti zao kuelezea furaha yao.

Katika kipindi chote cha uongozi wake, na hasa katika mwanzo wa kampeni za uchaguzi, Rais Samia amesisitiza mara kwa mara kwamba michezo siyo tu burudani, bali ni ajira na afya. Kauli hii imefuatiwa na hatua madhubuti za serikali za kuboresha miundombinu, kuongeza motisha kwa wachezaji na kuvutia wawekezaji katika ligi za kitaifa. Matokeo yake, thamani ya vilabu na ligi za Tanzania imepaa kwa kasi isiyokuwa ya kawaida.

Uwekezaji Mkubwa Kwenye Miundombinu ya Michezo

Sehemu kubwa ya mwelekeo huu imejikita katika uwekezaji mkubwa wa kimkakati katika viwanja na miundombinu. Serikali imeendelea kuboresha na kujenga viwanja kote nchini, hatua ambayo imefanya mazingira ya kufanyia michezo kuwa ya kisasa na kufikia viwango vya kimataifa.

Mfumo huu unahakikisha kuwa wanamichezo hawapati tu vifaa bora, bali pia wanakuwa na maeneo salama na yenye kuvutia kwa ajili ya mashindano. Bw. Issa Mfaume, mkazi wa Mwanza, alisema, "Tunajua michezo inahitaji uwanja mzuri. Kuona Rais Samia akisimamia ujenzi na ukarabati wa viwanja kumeongeza heshima ya nchi yetu kimataifa na kufanya ligi zetu ziwe tamu na zenye ushindani."

Michezo Kama Nyenzo ya Kujiajiri na Kuimarisha Afya

Huku kampeni zikiendelea, wananchi wamekuwa wakitamka bayana jinsi wanavyofurahishwa na mabadiliko haya. Bw. Juma Kikwete, fundi  katika soko la Kariakoo, alisema, "Kupitia michezo, watoto wetu sasa wana matumaini. Ligi Kuu imekuwa na mvuto mkubwa, hapa Kariakoo tunaona biashara ya jezi na vifaa vya michezo ikipanda kila siku. Rais Samia ametupa fursa mpya ya kujipatia kipato, siyo kwa wachezaji tu bali hata sisi wafanyabiashara wadogo."

Mbali na faida za kiuchumi, jukumu la michezo katika afya limekuwa wazi. Mama Asha Mussa, mkazi wa Kijitonyama na mwanachama wa kundi la mazoezi, alieleza, "Siku hizi kuna uhamasishaji mkubwa wa mazoezi. Mimi na wenzangu tunakimbia kila asubuhi. Hili limetokana na msisitizo wa kiongozi wetu kwamba afya ni mtaji. Tunanunua viatu, tunavaa nguo za michezo, tunaburudika. Tunashukuru kwa sababu ni njia bora ya kuepuka magonjwa na kuishi miaka mingi."

Wachambuzi wa masuala ya michezo wanabainisha kuwa mikakati ya Rais Samia ya kuweka mazingira mazuri kwa uwekezaji imefanya michezo kutoa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja kwa maelfu ya vijana. Hali hii inaonesha jinsi michezo ilivyokuwa chombo madhubuti cha diplomasia na utambulisho wa Taifa chini ya uongozi wake.

Kwa ujumla, wananchi wameonesha kufurahishwa sana na taswira mpya ya michezo nchini. Wanaamini Rais Samia ameweka msingi thabiti utakaodumu, na wanasubiri kuona mafanikio makubwa zaidi katika miaka ijayo, hasa baada ya uchaguzi wa 2025.



Share:

Thursday, 16 October 2025

OKTOBA 29: PIGA KURA KUENDELEZA SAYANSI NA TEHAMA – MSINGI UMESHAJENGWA!

 

Na Mwandishi wetu

Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, tunawaomba Watanzania wote kutambua ukweli mmoja muhimu: Misingi imara ya Sayansi, Teknolojia, na Ubunifu (STI) tayari imewekwa. Kura zetu sasa zinapaswa kuelekezwa katika kuhakikisha kunakuwa na mwendelezo thabiti ili kufikia malengo ya Tanzania kuwa kitovu cha Kidigitali Afrika Mashariki.

Serikali ya sasa imesisitiza wazi kwamba sayansi na teknolojia ni nguzo kuu ya uchumi wa kisasa. Hii si ahadi tu, bali ni utekelezaji unaoonekana kwenye Ilani ya Chama Tawala (CCM) na matendo ya Serikali.

Hatua Zilizopigwa Zisikatishe Tamaa:

Dhamira ya Satelaiti (Tanzanisat): Hatua ya kurusha satelaiti za kimkakati si mchezo, bali ni uwekezaji mkubwa unaoonyesha utayari wa nchi kutumia teknolojia za juu kwa mawasiliano, utafiti, na ufuatiliaji.

Kutengeneza 'Hub' ya Mitandao: Lengo la kuhakikisha huduma za intaneti ya kasi zinafikia hadi asilimia 80 ya nchi linahitaji mwendelezo. Kusimama sasa kutamaanisha kuacha kazi imara ikiwa nusu.

Kituo cha Usalama wa Mtandao: Kujengwa kwa miundombinu hii kunahitaji ulinzi, na kuanzishwa kwa Kituo cha Taifa cha Usalama wa Mtandao ni uthibitisho kwamba Serikali imejipanga kulinda ubunifu wa vijana wetu.

Kura Yako Ihakikishe Mwendelezo

Kazi kubwa imefanyika katika kuanzisha vituo atamizi (Innovation Hubs), kuendeleza sera za Akili Bandia (AI), na kuleta uwazi wa kidigitali katika huduma za Serikali (asilimia 50 ya huduma kutolewa kidigitali).

Misingi Ilishawekwa, Tunahitaji Jengo la Kudumu:

Wakati wa kampeni, kuna vyama na wagombea wengi wanaoweza kuahidi 'mapinduzi' mapya. Lakini kwa sasa, Tanzania haihitaji kuanza upya; inahitaji kujenga juu ya misingi iliyopo!


Kama unataka kuona:

Ajira zaidi katika uhandisi wa kielektroni na Ujasiriamali wa TEHAMA.

Ufanisi zaidi katika huduma za Serikali.

Tanzania ikiwa kiongozi wa uchumi wa kidigitali Afrika Mashariki.

Basi, kura yako ya Oktoba 29 inapaswa kuelekezwa kwa mgombea na chama chenye uwezo na dhamira ya kuendeleza na kukuza yale yote mema yaliyojengwa, badala ya kuanzisha safari mpya yenye mashaka.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger