Sunday, 22 December 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 23, 2024

Share:

KAMPENI YA SELEBRETIKA KIJAMUKAYA YA JAMBO GROUP YAFIKIA KITUO CHA AFYA KAMBARAGE...WAZAZI WAPEWA ZAWADI KUFURAHIA LADHA YA SIKUKUU!

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampeni ya Selebretika Kijamukaya 'Sisi Ndio Sikukuu Yenyewe' inayoendeshwa na Kampuni ya Jambo Group Msimu huu wa Sikukuu imezinduliwa rasmi na sasa imefika katika Kituo cha Afya Kambarage kilichopo Manispaa ya Shinyanga. 

Katika hatua hiyo, akina mama wajawazito na waliojifungua wamefikiwa na kufurahia bidhaa maalumu za Jambo, ikiwa ni pamoja na biskuti na vinywaji vyenye chapa au logo maalum ya Jambo Msimu wa Sikukuu, vyote vikiwa na ladha ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya 2025.

Kampeni hii ilizinduliwa rasmi Desemba 21, 2024, kwenye Ofisi za Jambo Media zilizopo Ibadakuli Mjini Shinyanga.

Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George, amesema kampeni hiyo ni sehemu ya juhudi za kuwafikia wateja na watumiaji wa bidhaa za kampuni hiyo, ili waweze kufurahia bidhaa za Jambo na familia zao wakati wa msimu wa sikukuu.

“Lengo letu ni kuleta furaha na ladha ya Jamukaya kwa familia nyumbani, hivyo tumekuja na vinywaji maalumu vyenye logo maalum ili kufanya sikukuu iwe tamu zaidi. Vinywaji vyetu pia ni vya manufaa kwa afya, kwa sababu vina sukari rafiki kwa wale wanaochangia damu,” amesema George.


Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (kushoto) akizungumza wakati akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group Msimu wa Sikukuu katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga

Ameeleza kuwa baadhi ya vinywaji vya kampuni hiyo vitahifadhiwa kwenye benki ya damu ya Kituo hicho cha afya, na kwamba wananchi watakaohudhuria kutoa damu watapewa vinywaji hivyo kama sehemu ya mchango wao katika kuokoa uhai. 

Amesisitiza kuwa vinywaji vya Jambo, ambavyo vimebeba ladha ya Sikukuu, vitakuwa na manufaa kwa watu wote, hasa wale watakaoshiriki katika michango ya damu, kwani vina sukari rafiki kwa afya na vinasaidia kuongeza nguvu.

Amefafanua kuwa, Kampeni ya Selebretika Kijamukaya inalenga kuhamasisha jamii kufurahia bidhaa za Jambo na kusaidia kuokoa maisha kwa kuchangia damu wakati wa msimu wa sikukuu.
“Mwenyekiti wa Kampuni za Jambo Salum Khamis hakuanzisha kampuni hizi kwa ajili ya kupata faida tu,bali ni kugusa pia maisha ya watu,na ndiyo maana leo tumeamua kuleta furaha kwa wagonjwa na watumishi wa kituo hiki cha Afya Kambarage kwa kuwapatia vinywaji na biskuti zenye chapa ya Selebretika Kijamukaya kwa ajili ya kufurahia msimu wa sikukuu,”ameongeza George.

Ameongeza kuwa ili familia iweze kufurahia sikukuu ipasavyo, bidhaa za Jambo zinapaswa kuwa sehemu ya meza ya chakula kila siku: Asubuhi ukiamka, vitafunwa vya Jambo, maji ya Jambo, juisi za Jambo, biskuti za Jambo, Ice Cream za Jambo - bidhaa hizi zitafanya sikukuu iwe yenye ladha ya kipekee.

 Kampeni ya Selebretika Kijamukaya inaendelea kuhamasisha watu kufurahia bidhaa za Jambo wakati wa msimu wa sikukuu na kuhakikisha kuwa nyumbani kunakuwa na ladha ya Jambo muda wote.

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Kambarage, Ernest Magula, pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi wa Kituo hicho, Adolf Nsanzungwanko, wameishukuru Kampuni ya Jambo Group kwa kutoa zawadi za Sikukuu kwa wagonjwa, wakiwemo akina mama wajawazito na waliojifungua katika msimu huu wa Krismasi na Mwaka Mpya.

Magula na Nsanzungwanko wameeleza kuwa zawadi hizo zimeleta faraja kwa wagonjwa, huku wakisisitiza umuhimu wa ushirikiano na wadau wengine ili kuendelea kusaidia katika kuboresha huduma za afya. 

Wamesema changamoto zinazokikabili kituo hicho ni pamoja na upungufu wa damu salama na ukosefu wa uzio wa kuimarisha usalama.

Kwa upande wao, akina mama waliokutwa katika wodi ya wazazi, akiwemo Fortunatha Athanas na Juliana Shija, wameishukuru Kampuni ya Jambo Group kwa kutoa zawadi hizo za Sikukuu, huku wakiipongeza kwa ubunifu wake. 

Wamesisitiza kuwa watendelea kutumia bidhaa za Jambo hata majumbani mwao kwa sababu wanaziamini na kuzithamini.

Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (katikati) akizungumza katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga leo Desemba 22,2024 wakati akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group Msimu wa Sikukuu kwa ajili ya akina mama wajawazito na waliojifungua katika kituo hicho cha afya - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (wa pili kushoto) akizungumza wakati akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group Msimu wa Sikukuu kwa ajili ya akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (wa pili kushoto) akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group Msimu wa Sikukuu kwa ajili ya akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (wa pili kushoto) akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group Msimu wa Sikukuu kwa ajili ya akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Sehemu ya bidhaa za Jambo Group zenye chapa/logo ya Jambo zilizokabidhiwa na Jambo Group kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George akikabidhi bidhaa  maalum za Jambo Group  msimu wa sikukuu kwa mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Mmoja wa akina mama katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga akiishukuru Kampuni ya Jambo Group kwa kuwapatia bidhaa maalum za Jambo Group kwa ajili ya Msimu wa Sikukuu
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (kushoto) akizungumza wakati akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group msimu wa sikukuu kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (kushoto) akizungumza wakati akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group msimu wa sikukuu kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga

Kiongozi Mkuu wa Jambo Media na Kiongozi wa Ubunifu na Chapa wa Kampuni ya Jambo Group, Nickson George (kushoto) akizungumza wakati akikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group msimu wa sikukuu kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Kambarage, Ernest Magula akizungumza wakati Jambo Group ikikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group msimu wa sikukuu kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Kambarage, Ernest Magula akizungumza wakati Jambo Group ikikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group msimu wa sikukuu kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage
Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi wa Kituo cha Afya Kambarage, Adolf Nsanzungwanko akizungumza wakati Jambo Group ikikabidhi bidhaa maalum za Jambo Group msimu wa sikukuu kwa akina mama wajawazito na waliojifungua katika Kituo cha Afya Kambarage.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

AJALI YA BASI YAUA WATU 11 , KUJERUHI KAGERA



Watu 11 wamefariki dunia huku 16 wakijeruhiwa katika ajali ya basi iliyotokea katika Kijiji cha Kabukome Kata ya Nyarubungo kwenye mlima wa kuanzia pori la Kasindaga lililopo Wilaya ya Biharamulo na Muleba Mkoani Kagera.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera Blasius Chatanda amelitaja gari hilo kuwa lina namba za usajili T 857 DHW linalofanya safari zake kati ya Kigoma na Bukoba ambapo liliacha njia na kupinduka na hatimaye kusababisha vifo vya Watu 11 kati ya hao Wanaume ni wanne Watu wazima na Wanawake watano, Mtoto wa kiume mmoja na Mtoto wa kike mmoja na miili yote ipo Hospitali teule ya Wilaya ya Biharamulo huku kati ya 16 waliojeruhiwa baadhi yao wanaendelea vizuri na muda wowote wataruhusiwa.


Amesema kuwa chanzo cha ajali ni kufeli kwa mfumo wa gari zima "Gari hili lilipotoka Biharamulo kwenda Bukoba lilimpitiliza kituo cha kushuka Mtoto mmoja sasa Ndugu zake wakapiga simu kuwa wamempitisha, Dereva akakutana na Coaster kwenye mlima ule kwa sababu ya haraka akasimamisha gari mlimani konda akashuka na mtoto ili amuwaishe kwenye gari ambalo linawahi Biharamulo kwa bahati mbaya mfumo wa gari ukagoma, mfumo wa breki mfumo wa gia vyote vikagoma gari likaanza kuserereka na likawa limemshinda Dereva likatoka nje ya barabara na kubinuka na Watu wengi wamepoteza maisha kwasababu walilaliwa na gari"

CHANZO - MATUKIO DAIMA 
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DESEMBA 22,2024




 
Share:

Saturday, 21 December 2024

TANZANIA, SAUDI ARABIA KUIMARISHA USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI


📌 Waziri Kapinga afanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Nishati Saudi Arabia

📌 Wajadili ushirikiano katika Mafuta, Gesi Asilia, Nishati Jadidifu na Nishati Safi ya Kupikia

📌 Saudi Arabia yaeleza kutambua juhudi za Tanzania kuimarisha Sekta ya Nishati

📍SAUDI ARABIA

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na Saudi Arabia katika kuimarisha Sekta ya Nishati hususan katika Mafuta na Gesi, Nishati Safi ya Kupikia na Nishati Jadidifu.

Mhe. Kapinga amesema hayo wakati alipokutana na Naibu Waziri wa Nishati wa  Saudi Arabia,         
Mhandisi Mohammed  Albrahim katika Mji wa Riyadh tarehe 19 Desemba, 2024 nchini Saudi Arabia.

Amesema kuwa, Tanzania imekuwa ikishirikiana na nchi hiyo kwa muda mrefu katika Biashara ya Mafuta na Maeneo Mengine ya Maendeleo hivyo mahusiano hayo yanaendelea kuimarika zaidi kwa kuwa mahitaji ya nishati yanazidi kuongezeka   na uwekezaji zaidi unahitajika katika kuendeleza Sekta ya Nishati ikiwemo Mafuta na Gesi Asilia, Nishati Jadidifu na  Nishati Safi ya Kupikia.

"Mahusiano ya Tanzania na Saudi Arabia katika Sekta ya Nishati ni ya muda mrefu, nchi hizi mbili zimekuwa na lengo la kuboresha ushirikiano wao katika kuendeleza sekta ya nishati." Amesema Kapinga

Aidha, ameeleza kuwa Tanzania kama nchi inayoendelea inahitaji kuimarisha zaidi miundombinu yake ya nishati katika maendeleo hivyo imekuwa  ikishirikiana na nchi zenye uzoefu mkubwa katika sekta hizo ili kupata matokeo chanya kwa kuwa nishati ni msingi mkuu wa maendeleo.

Amesema Saudi Arabia imekuwa ikijulikana kwa uwezo wake mkubwa katika uzalishaji wa mafuta na gesi, na imekuwa ikiwekeza katika maeneo mbalimbali ya Dunia, ikiwemo Afrika Mashariki, ambapo kwa upande wa Tanzania yenye rasilimali za Gesi Asilia na viashiria vya uwepo wa Mafuta inapata  uzoefu, ujuzi na teknolojia kutoka Saudi Arabia katika kuchimba, kusafisha na kusafirisha mafuta na gesi pamoja na kuimarisha miundombinu ya rasilimali hizo.

Vile vile, Mhe. Kapinga amesema kuwa kuimarika kwa Sekta ya Nishati nchini kutaiweza nchi kuweza kusambaza Umeme utakaozalishwa nchini kwa nchi jirani ambazo zimeonyesha nia ya kuhitaji Nishati.

Kwa upande wake, Waziri wa Nishati wa Saudi Arabia, Mhandisi Mohammed  Albrahim amesema kuwa nchi yake inajipanga kuwekeza zaidi katika ujenzi wa Miundombinu ya barabara, utunzaji wa mazingira na kuwekeza zaidi katika Sekta ya Mafuta na Gesi,  Nishati Jadidifu na  Nishati safi ya kupikia. 

Amesema, pamoja na kwamba wamegundua mafuta mengi, wanajipanga kuendana na sera za kidunia kwa kuwekeza katika Nishati Safi ambayo inahifadhi mazingira. 

Ameongeza kuwa, Saudi Arabia inatambua  juhudi zinazofanywa na Tanzania kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt
Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara katika kutekeleza Ajenda wa Nishati safi ya kupikia.

Share:

TBS YAWATAKA WAINGIZAJI WA BIDHAA ZA CHAKULA NA VIPODOZI KUSAJILI BIDHAA ZAO


WAFANYABIASHARA wanaoingiza bidhaa za chakula na vipodozi kutoka nje ya nchi wametakiwa kusajili bidhaa hizo Shirika la Viwango Tanzania (TBS), kwa kuwa kufanya hivyo ni kutekeleza matakwa ya sheria.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Usajili wa Bidhaa na Majengo wa TBS kutoka Idara ya Udhibiti Ubora TBS, Habakuki Kalebo, wakati akizugumza na waandishi wa habari, leo Desemba 19,2024 jijini Dar es Salaam.

Amesema usajili wa bidhaa za chakula na vipodozi unafanyika kupitia mfumo wa Online wa TBS ambao unaitwa OAS, ambapo ili mtu aweze kusajili bidhaa zake anatakiwa kujisajili kupitia mfumo huo.

Amesema usajili wa bidhaa na majengo ya biashara ni takwa la kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Viwango 2 ya Mwaka 2009 ambayo imefanyiwa mabadiliko katika Sheria ya Fedha ya Mwaka 2019.

Kalebo amesema kwa mujibu wa sheria hiyo mfanyabiashara yeyote yule anatakiwa kusajili bidhaa zake chakula, lakini pia kusajili na majengo.

"Sheria hii inasema mtu yeyote yule haruhusiwi kuzalisha, kuingiza bidhaa ya chakula au vipodozi ndani ya nchi wala kusambaza, wala kuuzwa kabla bidhaa hiyo haijasajiliwa na TBS," amesema Kalebo.

Aidha, amesema sheria hiyo inaeleza kwamba mtu yeyote yule haruhusiwi kuuza, kusambaza au kuhifadhi chakula au vipodozi katika jengo lolote lile ambalo halijasajiliwa na TBS .

Amefafanua kuwa hiyo inafanyika ili kulinda ubora wa bidhaa, usalama na kulinda umma ili uweze kutumia bidhaa ambazo ni salama kwa lengo la kulinda afya za watumiaji.

"Umuhimu wa kusajili bidhaa ni kuhakikisha ubora umezingatiwa na umehakikiwa vizuri na kuhakikisha usalama wa bidhaa hizo umezingatiwa vizuri.

Ikumbukwe kuwa hizo bidhaa watu wanakula zinaingia ndani ya mwili, kwa hiyo zisipokuwa zimethibitishwa ubora wake, kuthibitishwa usalama wake zitakuwa na athari kubwa kwenye afya za watu na zinaweza kupelekea kifo pamoja na magonjwa mengine.

Kwa hiyo lengo la TBS ni kuhakikisha bidhaa zote zinazoingia lazima ziwe zinakidhi hayo matakwa, iwapo mwananchi atanunua bidhaa ambazo hazijatibitishwa anaweza kukutana na madhara ya kiafya." Amesema

Ametoa wito kwa wananchi wanapokwenda kununua biadhaa kuangalia kama bidhaa hiyo ina nembo ya ubora ya TBS. " Lakini bidhaa ambazo tunazisajili kutoka nje ya nchi kuna zile ambazo zina nembo ya ubora na zile ambazo hazina nembo ya ubora," amesema.

Aidha, amesema usajili wa bidhaa ambazo zinazalishwa ndani ya nchi unafanyika kukupitia utaratibu unaoitwa Product Certification kwa kuwapatia leseni wazalishaji yakutumia nemno ya ubora na hapo moja wanakuwa wamesajili kupitia huo utaratibu.

Kwa upande wa majengo, Kalebo amesema yanasajiliwa ili kuhakikisha bidhaa za vipodozi pamoja na bidhaa za vyakula haziathiriwi na mazingira ambayo vinatunzwa .

"Kwa hiyo tunakagua majengo ili kujiridhisha kuwa yana mazingira ambayo ni wezeshi ambayo hayasababisha kuharibika kwa ubora na usalama wa bidhaa husika," amesema Kalebo,

Ameongeza kwamba bidhaa zozote zile ambazo zinagundulika zimeingia nchini kinyemela na zile ambazo huenda zina madhara kwa watumiaji kama vile vipodozi ambavyo vinakuwa na viambato sumu, TBS huwa inahuwisha taarifa hizo kwenye kanzi data yake kila mwezi na kuorodhesha bidhaa zile ambazo zinaonekana zilikuwa na viambata sumu na hazitakiwi kutumika nchini.

Ameongeza kwamba wananchi wanashauriwa kutembelea tuvuti ya TBS kuweza kujua bidhaa ambazo zimesajiliwa na shirika hilo.
Share:

Friday, 20 December 2024

MRADI WA BRT WACHOCHEA URAFIKI KATI YA CHINA NA TANZANIA


Mwakilishi wa Mkandarasi kutoka kampuni ya Ujenzi wa Mawasiliano ya China(CCCC) You Xudong akionyesha namna mradi huo awamu ya nne sehemu ya tatu unaotekelezwa Kivukoni Jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Mkandarasi kutoka kampuni ya Ujenzi wa Mawasiliano ya China(CCCC) You Xudong akionyesha namna mradi huo awamu ya nne sehemu ya tatu unaotekelezwa Kivukoni Jijini Dar es Salaam.

Na Hellen Kwavava-DAR ES SALAAM

MRADI wa mabasi yaendayo kwa haraka (BRT) umekuwa ni kichocheo cha ukuaji wa Uchumi katika Jiji la Dar es Salaam pamoja na kurahisisha hali ya usafiri kwa Jamii hiyo.

Meneja Usalama Tawi la Tanzania, kutoka Kampuni ya Ujenzi na Mawasiliano ya China (CCCC), Li Yuling amesema hayo jijini Dar es Salaam alipozungumza na Waandishi wa habari katika kuadhimisha siku ya Jiao Zhu China -Tanzania.

Wakati anazungumzia mradi huo wa BRT, awamu ya nne sehemu ya tatu amesema mradi huo ni sehemu muhimu ya urafiki wa  China na Tanzania, na kwamba sio tu unaboresha usafiri wa umma wa Dar es Salaam ambao ni mji wa kibiashara wa Tanzania.

 "Mradi huu unajumuisha ujenzi wa vituo muhimu vya usafiri, vituo vya mabasi na vifaa vingine vya trafiki. Unalenga kuboresha ufanisi wa usafiri wa mijini, kupunguza msongamano na kuimarisha hali ya usafiri ya wakazi wa eneo hilo," amesema.

Li amesema nia yao kubwa katika kuadhimisha siku hii ni kuonyesha watanzania juu ya dhamira ya makampuni ya Kichina katika maendeleo ya miundombinu inayoyafanya.

"Ili kuendeleza mafanikio hayo na kuadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya China na Tanzania, kampuni ya ujenzi ya China tawi la Tanzania imekutana na waandishi wa habari, kuzungumzia mafanikio hayo," amesema.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkandarasi katika mradi huo, You Xudong amesema mradi huo unaendelea katika eneo la Kivukoni, utachukua miezi 18.

Amesema wanajenga jengo la ulinzi, choo, jengo la tiketi namba moja na jengo la tiketi namba mbili.

Pamoja na hayo Mradi huo unaoendelea katika eneo la kivukoni jijini Dar es Salaam umeweza kushirikisha wanafunzi wazawa wanaosomea uhandisi kutoka Taasisi ya teknolojia Dar es Salaam(DIT).

Kwa upande wake Mwalimu Alvin Rujweka kutoka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam ( DIT), amesema wamekuwepo na wanafunzi wao wanaosomea uhandisi kwa ajili ya masomo ya vitendo katika kampuni hiyo ya kichina ya CCCC.

"Wanafunzi wanaoandaliwa kuwa wahandisi, wanapewa elimu ya vitabu na vitendo.  Njia nyingine tunawapeleka kwenye miradi mbalimbali inayoendelea nchini, tunawaunganisha na soko kupitia fani walizosomea, " amesema.

Naye Mhitimu wa Diploma  DIT mwaka huu 2024, Benson Mbilinyi amesema amepata nafasi ya kujiunga na kampuni hiyo ya CCCC na anafanya kazi kama mhandisi msaidizi Jambo ambalo anajivunia kupata nafasi hiyo hasa kwa vitendo.


Hata hivyo Mhitimu huyo ameendelea kutoa Ushauri kwa wanafunzi kujitokeza kwenye fursa mbalimbali zinazojitokeza ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kuondoa utegemezi katika Jamii.

Share:

Wednesday, 18 December 2024

KAPATA MCHUMBA ILA KIFAFA KINAMZUIA ASIOLEWE JAMANI

Naitwa Pendo Ambani kutoka Ruvu, Tanzania, kwa muda mrefu tulikuwa tunazunguka na ndugu yetu ambaye alikuwa anaugua ugonjwa wa kifafa ambao ni hatari sana kwa sababu mtu anaweza kuanguka popote pale hata eneo la hatari.

Huyu ndugu yetu ambaye ni mtoto wa shangazi yangu, tulimpeleka Hospotali za kiserikali na kibinafsi ili aweze kupata tiba ila ikawa anapata nafuhu kwa wakati fulani kisha kinarudi tena kwa nguvu kubwa ajabu.  

Tuliamua kumtafutia dawa za mitishamba kutoka wa waganga mbalimbali lakini bado hakupona licha ya waganga kutuambia angepona moja kwa moja lakini kadiri siku zilizovyokuwa zinasonga tulijikuta kama famili tunazidi kutoa fedha nyingi bila kupata majibu yaliyo sahihi.

Ugonjwa huu ulitufanya baadhi ya ndugu tushindwe kujikita katika shughuli za uzalishaji mali maana ilikuwa ni lazima mtu mmoja kubaki nyumbani kumuangalia asije akaangukia maeneo hatari kama kwenye moto na umeme wa ndani.

Kilichoumiza zaidi ndugu yetu huyu alikuwa amefikia umri  wa kuoa kabisa na tayari alishapata mchumba lakini ugonjwa huo ndio ukawa ni kikwazo kwake, wasichana wote wa rika lake tayari walishaolewa.

Kuna siku nikiwa natokea mjini katika kutafuta zangu riziki niliamua kuingia mtandaoni kusoma kiundani kuhusiana na ugonjwa wa kifafa na tiba yake ya uhakika ni ipi.

Katika kusoma kwangu niliweza kubaini Dr Bokko anatoa tiba ya ugonjwa huo na mengine kama kisukari, upungufu wa nguvu za kiume, presha, kisonono, kaswende, miguu kuwaka moto n.k.

Mara moja niliwasiliana na Dr Bokko kwa namba zake +255618536050 na akapendekeza tumpeleke mgonjwa ofisini kwake kwa ajili ya tiba, tulipofika alitupokea vizuri, alimfanyia matambiko yake.

Ndani ya siku chake ndugu yetu afya ilizidi kuimarika ingawa tulikuwa na wasiwasi kuwa anaweza kurejea kwenye hali yake ya kawaida lakini haikuwa hivyo hata mara moja.

Baada ya miezi mitatu ndugu yetu alionyesha kupona kabisa na yeye mwenyewe akasema anataka kuanza kazi.

Kweli akaanza kwenda kazini kwa mara ya kwanza baada ya muda mferu, huko kazini kwake aliweza kumpata mchumba ambaye hivi karibuni walifunga ndoa na tukawafanyia sherehe kubwa sana.

Sisi kama familia tunamshukuru sana Dr Bokko na ndugu yetu kasema sehemu ya vitu alivyozawadi kama zawadi atampatia iwanga kama zawadi kwa kumponya.

Sisi pia kama familia tumepanga kukutana tuzungumze tuone ni kwa namna gani tunaweza kumpatia chochote kitu Dr Bokko kama shukrani yetu kwake. Mpigie kwa namba +255618536050.

Mwisho.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger