Thursday, 22 August 2024

WANAGDSS WATAKA WATUHUMIWA WANAODAIWA KUMBAKA BINTI WA YOMBO WASHUGHULIKIWE


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WANAHARAKATI wamepaza sauti zao kuhakikisha haki inatendekea kwa washtakiwa wanadaiwa kumbaka kwa kundi na kumlawiti binti aliyejitambulisha anatokea Yombo Dar es Salaam ambapo mpaka sasa kesi bado ipo mahakamani na watuhumiwa wameshakamatwa.

Wakitoa maoni yao leo Agosti 21, 2024 katika Semina za Jinsia na Maendeleo ambazo hufanyika kila Jumatano, wanaharakati hao wamesema jamii inatakiwa kujua kila hatua inayoendelea kama walivyofanya ukatili huo.

Wamesema kutokana kusemekana muhusika aliyewatuma watuhumiwa kufanya tukio hilo yupo basi anatakiwa kukamatwa na kujibu tuhuma hizo na pia kuchukuliwa hatua kama akikutwa na hatia ya kufanya kitendo hicho.
Aidha wamesema wameviomba vyombo husika kutoa taarifa sahihi kuhusu binti kuanzia alipo, na serikali kutengeneza NGO's yake itakayojenga na kumfariji binti huyo ambaye amefanyiwa ukatili.

Pamoja na hayo wanaharakati hao wameiomba jamii kuungana kwa pamoja kuhakikisha wanakemea vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa vikitokea mara kwa mara kwenye jamii ambayo inatuzunguka.
Share:

Wednesday, 21 August 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 22, 2024

Share:

MABORESHO HUDUMA YA MAJI GOBA

 


Kazi ya kuweka toleo la bomba la inchi 3 kutoka bomba la usambazaji maji la inchi 4 inaendelea kutekelezwa na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika eneo la Simba Oil

Kazi hiyo inahusisha utolewaji wa maji katika bomba la inchi 4 kuelekea bomba la usambazaji maji la inchi 6 pamoja na ulazaji wa bomba la inchi 3 umbali wa mita 60 ili kuongeza msukumo maji katika eneo ilo.

Kukamilika kwa kazi hiyo itasaidia kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa maeneo ya Simba Oil, Chasimba, Minji, River View, Goba Zahanati, Shimbi Kati na Mwamuyamu
Share:

WAKULIMA WA MWANI, WAFUGAJI WA MAJONGOO BAHARI NA WANENEPESHAJI KAA JIJI LA TANGA WAPEWA MBINU MPYA


Zaidi ya vikundi 21 vya wakulima wa mwani, wafugaji wa majongoo bahari na wanenepeshaji Kaa Jiji la Tanga wamepatiwa elimu ya kilimo na ufugaji bora wa mazao ya Bahari.

Akizungumza lengo la utoaji wa elimu hiyo mratibu kutoka chuo cha mipango ya maendeleo vijijini Dr. Bonamax Mbasa amesema utafiti uliofanywa na chuo cha mipango na UNDP ulibaini wakulima na wafugaji hawana uelewa wa kutosha wa kile wanacho kifanya ndiyo sababu zao hilo kushindwa kupanda thamani na kuleta tija kwa wanavikundi na jamii iliyopo.

"Tumeona tulete elimu hii ili iwape ujuzi utakao wasaidia wakulima na wafugaji wa mazao ya baharini kuondokana na ukulima wa mazoea"alisema Dr. Mbasa.

Aidha Dr. Mbasa amesema kwa sasa upo umuhimu mkubwa wa kuweka makaushuo pamoja na mashine ya kusaga unga wa mwani ili kusaidia kuongeza ubora kwa zao la mwani.

Naye mwakilishi kutoka UNDP Veronica  Sigala akaelezea mradi wa Bahari ni Maisha unavyofanya kazi na kuhakikisha wakulima na wafugaji wa mazao ya baharini wanapata faida kutokana na kazi zao.


Share:

WAFANYABIASHARA TANGA WATOA USHAURI KWA BENKI YA NMB WALIOCHUKUA MIKOPO NA KUSHINDWA KUIREJESHA

 

Katibu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Mkoa wa Tanga (JWT) Ismail Masoud akizungumza wakati wa mkutano huo 
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus akizungumza wakati wa mkutano huo




Na Oscar Assenga, TANGA.

JUMUIYA ya wafanyabiashara Mkoa wa Tanga JWT imeiomba Benki ya NMB nchini kuweka utaratibu nzuri wa kudai madeni yao kwa wafanyabiashara waliochukua mikopo kwa kuunda kamati kila wilaya ambazo zitaratibu na kufuatilia walioshindwa kuilipa waone njia sahihi ya ya kulipwa badala ya kufikiria kuwauzia nyumba zao na mali ili kufidia mikopo hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa leo na Katibu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Mkoa wa Tanga Masoud Ismail wakati wa mkutano wa Business Club 2024 uliofanyika Jijini Tanga ambapo alisema wanataka wafanyabiashara wasiuziwe nyumba zao na mali wanazomiliki bali ziundwe kamati za madeni kila wilaya zitakayowezesha upatikanaji wa fedha zinazodaiwa.

Alisema kwamba kamati hizo zihusishe wafanyabiashara wenyewe kwamba mfanyabiashara amekutana na changamoto badala ya kwenda kuuza nyumba yake deni lipelekewe kwenye kamati ya wafanyabiashara wenyewe kwamba anadaiwa na anatakiwa kwenda kuuziwa nyumba yake wafanyaje na itakuwa ni benki ya kwanza kuwashirikisha wafanyabiashara wenyewe kusaidia kulipa madeni badala ya kuuza nyumba.

“NMB chukueni Sera hii na mkiifanya mtafanikiwa nchini nzima kwamba kila wilaya kuwa na kamati ya Madeni ikihusisha wafanyabiashara na unakuta mtu nyumba ikienda kuuzwa anadaiwa milioni 3 hivyo wakikutana wanaweza kuchangishana na kuweza kumaliza deni hilo”Alisema

Aidha alisema kwamba biashara zimekuwa na changamoto nyingi hasa ushindani umekwa juu wafanyabiashara kupitia ushindani wa mifumo ya biashara unawaumiza na bahati mbaya wanashindana na watu wasiolipa kodi kwenye biashara ambazo wanazifanya wao.

“Lakini wengine hawalipi kodi hilo ni tatizo linawaumiza wafanyabiashara hivyo NMB lazima tubadilishe sera asilimia 60 ya wafanyabiashara nchini ni wamachinga hawalipi kodi asilimia 40 ni wafanyabiashara wanaolipa kodi na kuchukua mikopo kwao kuna namna mbili wanatakiwa kufanya biashara walipe kodi na wanatakiwa kufanya biashara kurudisha mikopo hivyo mifumo ya mabenki lazima ibadilike kulingana na hali biashara ilivyo”Alisema

Aidha alisema kwamba wasipobadilisha sera hali ya biashara itaendelea kuwa ngumu na wafanyabiashara hawataki akaunti zao zikamatwe na wanaaza kurudi nyuma kwenye mfumo wa Tanzania kutunza fedha kwenye vitanda kwa sababu akaunti zao zinakamatwa na TRA wafanyaboashara hawataki.

Alisema kwamba benki akaunti ni siri ya mtu na benki na wanataka mfumo wa kutumia fedha taslimu uachwe watumie swap sasa benki na JWT na TRA wanashindwa kutumia njia zipi za watu wanadaiwa wafanywaje walipe mpaka wanakwenda kuingilia akauti za watu wanalalami fedha zao.

“Niwaambie kwamba benki ndio zinafanya kazi sana kuliko mitandao lakini Tanzania mitandao ndio inafanya kazi zaidi kuliko benki na mifumo ya fedha Tanzania inazunguka sana kwenye mifumo ya mitandao kuliko benki inabidi tushirikina na sisi Jumuya za wafanyabiashara tuone namna ya kufanya mifumo ya fedha ipitie kwenye mabeki

Awali akizungumza Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini Baraka Ladislaus alisema kwamba leo la kuanzishwa kwa NMB Business ni kuwafanya wateja wao wawe karibu na wao lakini kupitia huko wanapat fursa ya kusikia changamotoo mbalimblai za wateja wao na hivyo kuwasaidia kufanya maboresho katika huduma ambazo wamekuwa wakizitoa.

“Ni matumaini yangu baada ya kusikia mada mbalimbali zitakazotolewa nanyi watapata fursa ya kuwapa maeneo yenu ili waendelea kuyachukua na kuyachakata na kuzipatia ufumbuzi na kujenga NMB na wateja walio imara”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba benki hiyo itaendelea kuboresha huduma zake katika maeneo mbalimbali na sasa wameendelea kuwafikia wateja wadogo wadogo wa kule chini na akaunti za NMB zimeboresha.

“Maboresho makubwa ni kiu ya Benki ya NMB kuendelea kuwa chaguo lako ukitaka kuchagua benki NMB iendelea kubaki kuleta huduma za kibunifu zitakazoleta matokeo chanya kwa wateja wetu”Alisema

Share:

Tuesday, 20 August 2024

IJUE DAWA YA MATAPELI WA VIWANJA

Jina langu ni Amosi kutokea Meru nchini Kenya, mwaka 2019 nilinunua kiwanja kwa ajili ya kuanza ujenzi baada ya kukusanya fedha zangu kwa miaka mingi sana.

Hii ilikuwa ni ndoto yangu ya miaka mingi kwamba siku moja nami nije kuwa na kwangu kisha kuanzisha familia yenye furaha.

Basi nilikutana na madalali na kuniambia kuna kiwanja kikubwa kinauzwa mahali na kipo katika eneo zuri hivyo naweza kuchangamkia fursa hiyo mara moja.

Nilienda kuona kiwanja hicho na kujidhirisha kweli ni kizuri, basi nilianza mchakato wa malipo mara moja ili asije akatokea mtu mwingine akakinunua kiwanja hicho.

Hatimaye nilifanikiwa kulipia na kupatiwa hati kuwa mimi ndiye mmiliki wa eneo hilo. Hapo moyo wangu ulitulia na kujua kilichobakia sasa ni hatua tu ya ujenzi ambao ulitarajia kuanza siku sio nyingi.

Cha kushangaza ni kwamba nilikuja kupata taarifa kuwa yule aliyeniuzia kile kiwanja ni mtu tapeli ambaye ameshatapeli watu wengi katika maeneo mengi nchini Kenya.

Ni mtu ambaye ana mtandao mrefu sana kiasi kwamba ni vigumu sana kumpata na hatia hata ukimfikisha mahakamani.

Kuna ndugu yangu aliniambia kuwa nikaonane na Dr Bokko atanisaidia kushinda kesi hiyo ya madai ambayo nilikuja kuifungua siku za mbeleni.

Nashukuru Dr Bokko alinifanyia tiba ya kweli na kunihahakikishia haki yangu itapatikana tena ndani ya muda mfupi tu. Basi nilifungua kesi ya utapeli mahakamani na shauri letu likaanza kusikilizwa.

Watu wengi walijua nitashindwa kesi hiyo maana mtu huyo ni tapeli aliyebobea. Lakini kwa nguvu ya dawa za Dr Bokko nilishinda kesi hiyo na kurudishiwa fedha zangu pamoja na gharama za kesi hiyo. Mpigie kwa namba +255618536050.

Mwisho.


Share:

Monday, 19 August 2024

KAMATI YA BUNGE YA SHERIA NDOGO YAIPONGEZA OSHA KWA KUTEKELEZA MAAGIZO YAKE

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, Mhe. Dkt. Jasson Rweikiza (Kushoto) akifuatilia wasilisho la Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Katambi, kuhusu utekelezaji wa maagizo ya Kamati hiyo yaliyotolewa Oktoba 2023.

**********************

Na Mwandishi Wetu

Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) umewasilisha maboresho ambayo yamefanyika katika kanuni mbili za usalama na afya mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo.

Maboresho hayo ambayo yamefanyika katika kanuni za Igonomia na Mazingira ya Kazi yalishauriwa kufanyika na Kamati hiyo katika kikao chake cha Oktoba 26, 2023 baada ya OSHA kuwasilisha kanuni hizo mpya mbele ya Kamati hiyo.

Wasilisho hilo limefanywa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi, ambaye alimwakilisha Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete. Katambi ameambatana na Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, Kamishna wa Kazi, Bi. Suzan Mkangwa na Watendaji wengine wa Wizara na Taasisi ya OSHA.

Mhe. Katambi ameiambia Kamati kuwa mapendekezo yote yaliyotolewa ikiwemo kujumuisha tafsiri ya neno Mamlaka pamoja kuondoa maudhui yanayojirudia katika kanuni hizo yameshughulikiwa ipasavyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Dkt. Jasson Rweikiza, ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) pamoja na Taasisi ya OSHA kwa kupokea na kutekeleza maagizo ya Kamati yake.

Aidha, ameahidi Kamati yake kuendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi chini yake katika kuwahudumia Watanzania kupitia ushauri na maelekezo mbalimbali yanayolenga kuboresha utendaji wa Serikali.

Wakati huo huo, OSHA imekutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na kufanya wasilisho kuhusu utendaji wa Taasisi hiyo ambapo Mtendaji Mkuu, Bi. Khadija Mwenda, ameieleza Kamati hiyo umuhimu wa kulinda nguvukazi ya Taifa kupitia uimarishaji wa mifumo ya usalama na afya katika sehemu za kazi.

“Hadi inapofika hatua ya mtu kuajiriwa kama mfanyakazi serikali inakuwa imewekeza rasilimali nyingi sana kwake kuanzia anapozaliwa, kukua, kusoma hadi kuajiriwa hivyo inakuwa ni hasara kubwa kwa Taifa endapo mfanyakazi huyu atapata ulemavu au kupoteza maisha kabla ya kutoa mchango wake wa kutosha katika uzalishaji,” ameeleza Mtendaji Mkuu wa OSHA na kuongeza:
“Tunachokifanya OSHA ni kushauri na kusimamia maeneo ya kazi kuweka mifumo madhubuti ya kuwalinda wafanyakazi dhidi ya vihatarishi vya magonjwa pamoja na kulinda mitaji ya wawekezaji ili kuleta tija katika uzalishaji pamoja na kulinda ustawi wa wafanyakazi.”

Akihitimisha mjadala wa wajumbe wa Kamati hiyo ya Bajeti baada ya wasilisho la OSHA, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Oran Njeza, amesema Kamati yake itaendelea kutoa ushauri unaolenga kuboresha utendaji wa Serikali ikiwemo Taasisi ya OSHA.
Mjadala ukiendelea katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo ambapo OSHA iliwasilisha maboresho ya kanuni mbili za usalama na afya.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi, akifanya wasilisho mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu maboresho ya kanuni za Igonomia na Mazingira ya Kazi ambayo Kamati hiyo ilielekeza yafanyike.

Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Kamishna wa Kazi, Bi. Suzan Mkangwa wakifuatilia wasilisho la Naibu Waziri, Mhe. Katambi katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria NdogoWatendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) na Taasisi ya OSHA wakifuatilia wasilisho la Naibu Waziri, Mhe. Katambi katika kikao cha Kamati ya ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo.



Share:

WALIOTUMWA NA AFANDE KUMDHALILISHA BINTI WAFIKISHWA MAHAKAMANI.. KESI KUSIKILIZWA SIKU TANO MFULULIZO



Na, Mwandishi wetu - Dodoma

Watuhumiwa wanne wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumwa na afande kumdhalilisha binti wa Yombo Dovya Jijini Dar es salaam Leo Agosti 19, 2024 na kusomewa mashtaka mawili ya kubaka kwa kikundi (gang rape) na kumwingilia kinyume na maumbile binti ambaye hakutajwa jina lake mahakamani.


Akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama kuu ya Tanzania Mkoani Dodoma Mkurugenzi msaidizi kutoka Ofisi ya Mashtaka Makao Makuu, Renatus Mkude amesema vijana hao wamekana mashtaka hayo na kutokana na unyeti wa shauri hilo wataendelea kuwa mahabusu huku shauri lao likisikilizwa kwa siku tano mfululizo.

Watuhumiwa hao waliofikishwa mahakamani ni MT. 140105 Clinton Honest Damas maarufu Nyundo,Amin Lord Lema ,Nickson Idala Jackson na C.1693 Playgod Edwin Mushi huku jina la binti aliyefanyiwa ukatili huo kutotajwa mahakamani ili kulinda utu wake kwa mujibu wa sheria za nchi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger