Friday 28 June 2024

TBS KANDA YA KUSINI YATEKETA TANI 3.5 ZA BIDHAA HAFIFU


Na Mwandishi Wetu, Mtwara

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Kusini inayojumulisha Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma limetekeleza tani 3.5 za bidhaa hafifu zenye thamani ya sh. 20,054,000 ambazo zilikamatwa kwenye mikoa ya kanda hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuteketeza bidhaa hizo eneo la dampo la Manispaa ya Mtwara Mikindani, Kaimu Meneja wa Kanda ya Kusini, Bw.William Mhina alisema zilikamatwa kwenye ukaguzi uliofanywa na TBS ili kuhakikisha bidhaa hafifu zinaondolewa sokoni kwa lengo la kulinda usalama wa watumiaji wa bidhaa hizo.

Alisema bidhaa hizo zilikamatwa katika ukaguzi uliofanyika Januari 2024 hadi Juni, mwaka huu. Alitaja bidhaa zilizoteketezwa kuwa ni nguo za ndani za mitumba ambazo ni sidiria pamoja na chupi.

Aidha, alitaja nyingine kuwa ni vipodozi vilivyokatazwa kisheria kuingia nchini na kuuzwa kwenye soko laTanzania na za chakula ambazo zimeisha muda wake wa matumizi. "Bidhaa zote hizi zimekuwa zikikamatwa na wakaguzi wetu, wakati wa ukaguzi uliofanyika kwenye kanda yetu," alisema.

Alitaja sababu ya kuteketezwa kwa vipodozi hivyo, Bw. Mhina alisema ni kutokana na kuwa na viambata sumu.

Alisema vipodozi hivyo vimepigwa marufuku nchini kwa sababu husababisha kuathirika kwa mifumo ya uzazi kwa wanawake na wanaume, kuharibika kwa ngozi, kusababisha madhara kwa mtoto anaenyonyeshwa na aliyepo tumboni, kusababisha saratani za aina mbalimbali ikiwemo ya ngozi na kuathirika kwa mifumo wa umeng'enyaji wa chakula.

Alisema vipodozi vilivyoteketezwa vimepigwa marufuku katika soko la Tanzania kwa sababu vina viambata sumu ikiwemo hydroquinone, butylmethyl propional, steroids, zinc pyrothione na zebaki.

Kwa upande wa nguo za ndani, alisema nguo hizo zimepigwa marufuku kwa sababu zinasababisha maradhi ya ngozi kama vile fangasi na maambukizi ya bakteria yanayopelekea magonjwa ya ngozi kwenye maeneo mbalimbali za mwili

Alisisitiza wananchi kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio vya bidhaa wanazotaka kununua ili kujua kama hazijaisha muda wake wa matumizi na kama zimethibitishwa na TBS.

Kuhusu bidhaa zilizoisha muda wake, alisema usababisha magonjwa mbalimbali yakiwemo ya matumbo, hivyo alitoa rai kwa wananchi kuwa na utamaduni wa kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio vya bidhaa wanazotaka kununua ili kujua kama hazijaisha muda wake wa matumizi na kama zimethibitishwa na TBS.

Kwa upande wa wazalishaji, wasambazaji na wauzaji wa bidhaa mbalimbali aliwataka kuhakikisha kuwa wanaingiza sokoni bidhaa zenye Ubora

"Rai yetu ni kuwa wazalishaji, waingizaji, wasambazaji na wauzaji wa bidhaa kufuata kanuni, taratibu na Sheria ili kuepuka kupata hasara na kuchukuliwa hatua za kisheria. Ni vema wakawa wanawasiliana na Shirika la Viwango kwa kufika ofisi za TBS zilizo karibu nao au kwa mifumo yetu ya mtandaoni au kwa kupiga simu ya bure 0800110827 ili waweze kupewa maelezo au msaada," alisema .
Share:

Video Mpya : TOTO KHAN x SLYVEPO - POMBE


Hii hapa kazi mpya ya Msanii Toto Khan akimshirikisha Slyvepo inaitwa Pombe, Video hii imeongozwa na Director Dave Skerah, Producer Scardee
Tazama Video hapa chini
Share:

Thursday 27 June 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 28, 2024

Share:

ORYX GAS, VIGOR GROUP WAZINDUA BOHARI YA KUHIFADHI NISHATI YA GESI ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akikata utepe kuweka jiwe la msingi kuzindua bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx uliofanyika leo Juni 27, 2024 huko Mangapwani Zanzibar.


KAMPUNI ya Oryx Gas imeungana na kampuni ya TP Limited yenye makao yake Zanzibar ambayo ni  kampuni tanzu ya Vigor Turky’s Group of Companies (Vigor Group), kujenga bohari ya kwanza ya kuhifadhi nishati za gesi ili kuongeza usambazaji wa gesi ya LPG kisiwani humo.

Akizungumza  mbele ya wananchi wa Zanzibar baada ya kuzindua bohari hiyo ya kupokea na kuhifadhi gesi pamoja na miundombinu mingine jumuishi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amepongeza ujenzi wa bohari hiyo huku akizipongeza taasisi nyingine ambazo zimefanikisha ujenzi wa mindombinu jumuishi ya bandari ya Mangapwani ambayo itahusika na meli za mafuta na gesi pamoja na shughuli nyingine.

“Kwa muda mrefu tulikuwa tunamia bandari ya Malindi lakini kutokana na ongezeko la shughuli za kiuchumi bandari ile haitoshi, hivyo Serikali ilitangaza eneo la Mangapwani kuwa bandari kwa ajili ya nishati ya gesi, mafuta na miundombinu mengine.

“Sasa tutakuwa tunapokea meli kubwa na kuhifadhiwa katika  matanki mawili makubwa yenye uwezo wa kuhifadhi tani 130 yaliyojengwa na Oryx. Hivyo niziombe kampuni nyingine kufuata nyayo za Oryx kwa kujenga miundombinu yao katika eneo hili,”alisema.

Pia alisema kuanzishwa kwa bohari ya kuhifadhi ya gesi Zanzibar kutaongeza chachu ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi na hivyo kufikia malengo ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwamba ifikapo mwaka 2032 asilimia 80 ya wananchi itumie nishati safi ya kupikia huku akisisitiza umuhmu wa bei ya gesi kupunguzwa ili wananchi wengi watumie.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Limited, Benoît Araman alisema kufunguliwa kwa bohari ya gesi Mangapwani inanaonyesha dhamira ya Oryx Energies ya kuwekeza katika miundombinu muhimu inayosaidia matumizi salama na mapana ya gesi ya LPG nchini Tanzania.

Pia inakidhi ombi la Serikali la kuhakikisha usambazaji endelevu wa LPG kila mahali nchini.Soko la gesi la Tanzania limeshuhudia ongezeko la uagizaji wa bidhaa kutoka nje kwa karibu mara 13 katika muongo uliopita, kutoka tani 20,000 mwaka 2010 hadi tani 293,000 mwaka 2023.

Aliongeza Oryx Gas Zanzibar imeungana na kampuni ya TP Limited yenye makao yake Zanzibar ambayo ni  kampuni tanzu ya Vigor Turky’s Group of Companies (Vigor Group), kujenga bohari hiyo ya kimkakati  na kuongeza usambazaji wa gesi ya LPG kisiwani humo.

“Mkataba huu unaonyesha kujitolea kwa Oryx Energies katika kuendeleza ushirikiano na makampuni ya wazawa.Bohari ya Mangapwani, ambayo ilianza kufanya kazi mapema Mei ina uwezo wa kuhifadhi tani 1,300 za gesi ya LPG, na ilipokea meli yake ya kwanza ya tani 1,200  mnamo Mei 2, 2024.

 “Pia kusaidia Mpango wa matumizi wa nishati safi ya kupikia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Gesi ya LPG inazidi kuwa sehemu muhimu ya mchanganyiko wa matumizi ya nishati mbalimbali za kupikia Zanzibar, ikishughulikia mahitaji ya kaya, biashara, na sekta ya utalii inayokua kwa kasi,”alisema.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kampuni ya Oryx Gas Zanzibar Limited, Shuwekha Omar Khamis alisema: “Tunajivunia kuzindua bohari hii ya kisasa ya LPG ambalo itaimarisha usambazaji  wa gesi ya LPG katika visiwa hivyo. Tumedhamiria kuendelea kuchukua jukumu muhimu katika maendeleo haya, kwa kuwa tumeweka msingi wa kupanua usambazaji wa LPG Zanzibar.

Awali Mwenyekiti wa kampuni za Vigor Toufiq Salim Turky alisema wameungana Oryx kwasababu ya kutambua uwezo wao  wa miaka mingi katika soko la gesi nchini , hivyo ni imani yao sasa gesi itapatikana kwa wengi.

Pia alisema mpango wao ni kupunguza bei ya gesi Zanzibar kwa asilimia 20 kuanzia Julai 1 mwaka huu na baadae kupungua bei kwa asilimia 30. “Hivyo Oryx Gas wameiweka bohari hii katika viwango vya kimataifa, tunafahamu wao wako kwa miaka mingi, wana uzoefu mkubwa.

“Bohari hii inamilikiwa na Vigor kwa asilimia 100, lakini kwa uendeshaji tumamua kuwapa wenzetu wa Oryx .Uendeshaji tumeukabidhi kwa Oryx kwa kuamini wao ni kinara katika soko la Tanzania.Wakati tunaanza huko nyuma soko lilikuwa ni tani tatu lakini sasa soko lao limekuwa na kufikia tani 800,”alisema.

Hata hivyo alisema  ni asilimia 12 tu ndio wanaotumia gesi Zanzibar na upande wa Tanzania Bara ni asilimia 9 , hivyo safari safari bado ndefu,”alisema.

Kwa upande wake wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA), Omar Ali Yussuf alisema kwa miaka mingi sekta ya nishati hasa gesi, walikuwa wanatumia bandari ya malindi lakini sasa wamepeta bandari ambayo itashusha gesi, mafuta na itatumika kwa shughuli nyingine kwenye hilo la Mangapwani.

“Kabla ya kuwepo kwa bandari hii ya kushusha gesi na mafuta tulikuwa tunatumia majahazi na vyombo vingine ambavyo havina salama lakini kwa maelekezo ya Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi leo tumeweza kuwa na bandari kwa ajili ya meli zenye gesi na mafuta,”alisema.

Pia alisema kwa kupitia mipango ya Serikali pamoja na sera nzuri za uchumi wa bluu watahakikisha bandari ya Mangapwani wanataka iwe kituo kikuu cha kusafirisha gesi na mafuta kwa ukanda wa Afrika Mashariki huku akifafanua kuwa bei ya nishati ya mafuta na gesi kwa Zanzibar iko chini ukilinganisha nchi nyingine.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduz,  Dk. Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kuzindua bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya  kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group of Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar. Wengine kutoka kulia ni Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Injinia Zena Ahmed Said, Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Ltd, Benoite Araman, Mwenyekiti wa makampuni ya Vigor, Taufiq Salum Turky na kutoka kushoto ni Katibu wa NEC itikadi, uenezi na mafunzo CCM Zanzibar, Khamis Mbeto, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Hadid Rashid Hadid na Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Shaib Hassan Kaduara.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akipanda baada ya kuzindua bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx uliofanyika leo Juni 27, 2024 huko Mangapwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Limited, Benoît Araman akitoa maelezo wakati wa hafla ya uzinduzi wa wa bohari ya kuhifadhi nishati za gesi ya Kampuni ya Oryx leo Juni 27, 2024 Visiwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Limited, Benoît Araman alipokuwa akitoa maelezo wakati wa hafla ya uzinduzi wa wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Mhandisi wa Kampuni ya Oryx, Joseph Soka alipokuwa akitoa maelezo wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati za gesi ya  kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mwenyekiti wa Makampuni ya Vigor, Taufik Salim Turky pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Limited, Benoît Araman wakiwasili katika hafla ya a uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati za gesi ya  kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na viongozi mbalimbali wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Wakuu wa Idara Maalumu za SMZ na viongozi mbalimbali wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Mwenyekiti wa Makampuni ya Vigor, Taufik Salim Turky akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Limited, Benoît Araman akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar(ZURA), Omar Ali Yussuf akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.
Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Shaib Hassan Kaduara akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa na viongozi mbalimbali wakipata picha na wafanyakazi wa kampuni ya Oryx Gas Tanzania wakati wa hafla ya uzinduzi wa bohari ya kuhifadhi nishati ya gesi ya Kampuni ya Oryx na Vigor Group og Companies uliofanyika leo Juni 27, 2024  Mangapwani Zanzibar.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO

Share:

TANZANIA YASHINDA TUZO YA UBUNIFU KOREA KUSINI

 

Na Mwandishi wetu, Korea

Tanzania yashinda Tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Ubunifu bora katika huduma za umma kupitia mfumo wa e-Mrejesho. 

Tuzo za Umoja wa Mataifa za Ubunifu katika Huduma za Umma 'UN Public Service Innovation Awards' zimetolewa leo Juni 26 mwaka huu, nchini Korea Kusini kwenye Kilele cha Wiki ya Huduma kwa Umma ya Umoja wa Mataifa 'UN Public Service Week'.  

Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa 72 zimeshiriki ambapo mifumo 400 iliwasilishwa na mifumo 15 ilishindinda tuzo ukiwemo wa e-Mrejesho. 

Kutoka Afrika nchi zilizoshiriki na kushinda tuzo hizo ni Tanzania na Afrika Kusini pekee.  

Wiki ya Huduma kwa Umma ya Umoja wa Mataifa ni tukio la kila mwaka linaloadhimishwa kimataifa, kwa lengo la kusherehekea thamani na umuhimu wa huduma ya umma kwa jamii. 

Tukio hili linasisitiza kutambua mchango wa watumishi wa umma na kuhamasisha vijana kuchagua kazi katika sekta ya umma. 

Wiki hii kwa kawaida hujumuisha matukio, sherehe za tuzo, na majadiliano kuhusu jinsi ya kuboresha ufanisi wa utoaji huduma kwa umma duniani kote.

Mfumo wa e-Mrejesho unawawezesha wananchi kutuma kero au malalamiko, maoni, maswali, na pongezi kidijiti kwenda katika taasisi yoyote ya umma na kisha kupata mrejesho wa utekelezaji wake kidijiti mahali walipo.

Mfumo huu umetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Mfumo wa e-Mrejesho unapatikana  kwa njia tatu ambazo ni kupitia simu ya mkononi kwa kubofya *152*00# na kisha kuchagua namba 9 na kisha namba 2,  njia zingine ni kupitia simu janja kwa kupakua Aplikesheni tumizi (Mobile App) ya e-Mrejesho inayopatikana kwenye Play Store na Apple Apps Store, na kwa njia ya Tovuti ya e-mrejesho.gov.go.tz.

Share:

RAIS DKT. SAMIA ANAGUSWA NA KUJALI MAISHA YA WAFANYAKAZI

 

 *Amenyanyua kikokotoo, Ndejembi asema huo ni mwanzo tu

 Nukuu za Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi- Bungeni

 

"Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka wa fedha 2024/2025 ambayo tunaenda kuipitisha inaonyesha ni namna gani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anaguswa na maisha ya wafanyakazi wa nchi hii. Tangu aingie madarakani mwaka wake wa kwanza alipandisha madaraja yaliyokwama kwa miaka mingi, wafanyakazi waliokuwa hawajapandishwa maradaja kwa miaka Tisa (09), alipandisha zaidi ya watumishi 222,000" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi

 

"Mheshimiwa Rais aliguswa sana na madeni kwa watumishi wa Umma, alitoa fedha kwaajili ya kulipa madeni hayo ya watumishi" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi

 

"Julai 2022 kuna mabadiriko ya Kikokotoo yalifanyika, waliokuwa watumishi wa Umma walitoka kulipwa mkupuo wa Asilimia 50 na kushuka Asilimia 33. Waliokuwa Asilimia 25 walipanda kwenda Asilimia 33. Ilikuwa ni kilio kwa watumishi ambao mishahara yao ni ya chini na husubiria mkupuo wa fedha hizi kuanza maisha yao wanapokuwa wamestaafu" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi

 

"Wizara ya Fedha mwaka wa fedha 2024/2025 wameweka Shilingi Bilioni 155 kwaajili ya kulipa Kikokotoo kunyanyua kutoka Asilimia 33 kwa waliokuwa Asilimia 50 kabla ya Julai 2022 kwenda Asilimia 40. Waliokuwa Asilimia 25 wamekwenda Asilimia 35" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi

 

"Wabunge wengi mmezungumzia suala la kuangalia kiwango kiendelee kunyanyuka kurejea kilipokuwa Asilimia 50. Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri wameshukuru Asilimia 40 lakini wanaomba iweze kurudi Asilimia 50. Huu ni mwanzo mzuri ndiyo maana Asilimia 7 imewekwa" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi

 

"Serikali itazidi kuangalia ni namna gani itarudi katika Asilimia 50 ya Kikokotoo. Wanaoenda kulipwa siyo tu wanaokwenda kustaafu kuanzia 01 Julai, 2024. Wanaenda kulipwa wote hata wale waliostaafu kuanzia Julai 2022" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi

 

"Watumishi 17,068 toka Julai 2022 wanaenda kulipwa mapunjo yao ya Asilimia 7 waliyostahili kupata. Waliokuwa wanapata Asilimia 33 kwenda Asilimia 35 watalipwa mapunjo yao ya Asilimia 2. Tunatarajia kuona wengi wakija kudai mapunjo ya mafao yao" - Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger