Wednesday 26 June 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 26,2024

Share:

KLINIKI YA KISHERIA YAZINDULIWA DODOMA


Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi amezindua Kliniki ya Ushauri na elimu ya Sheria kwa Umma inayokusudia kusogeza huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi ili kupunguza migogoro dhidi ya Serikali na kupata suluhu ya changamoto. 

Kliniki hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  kwa kushirikiana na Chama cha Mawakili wa Serikali ni agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutaka viongozi kuwa na utaratibu wa kusikiliza malalamiko ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuwaongoza katika taratibu za kupata haki. 

Akizindua Kliniki hiyo leo June 26,2024 Jijini Dodoma, Dkt. Feleshi amesema Kliniki hiyo itaimarisha utawala wa Sheria nchini ikiwa ni pamoja na kuchochea mazingira ya amani kwa wawekezaji ndani na nje ya nchi. 

"Kipekee natoa rai kwa Mawakili wote wa Serikali hapa nchini kutenga muda na kusikiliza wananchi kupitia maeneo yao, niwakumbushe pia wakuu wa mikoa na Wilaya ambao bado hawajakamilisha kuteua wajumbe wawili wa kamati za ushauri wafanye hivyo ili kamati hizo zianze kusikiliza malalamiko ya wananchi kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa, "amesema

Kipekee, Mwanasheria huyo Mkuu wa Serikali amevikumbusha vyama vya Mawakili wa Serikali (TPBA)pamoja na Mawakili wa Tanganyika (TLS)kuendelea kushirikiana na Serikali na kamati za ushauri wa kisheria ngazi za mikoa na Wilaya ili kusikiliza malalamiko na kuyatatua kwa wakati. 

Amesema Kliniki zitakazo endeshwa na Kamati hizo zitakuwa endelevu kwa nchi nzima na hivyo kuwataka wananchi wa Dodoma na Mikoa jirani kupata huduma ya Ushauri wa kisheria bure kuanzia June 26 hadi Julai 3,2024 kuanzia saa 2.00 asuhubi hadi saa 10.00 jioni.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Mary Makondo ameeleza kuwa wananchi wakiendelea kutatuliwa kero zao uzalishaji utakua kwa kasi. 

Amesema Serikali kupitia kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia wananchi wamekuwa sehemu ya mabadiliko kwa kuelewa namna ya kutafuta suluhu ya malalamiko yao. 

"Kezo za wananchi ni wajibu wetu, tuendelee kuwa pamoja katika kuzitatua kupitia ushirikiano wetu, kupitia hizi siku zilizoyengwa wananchi wataendelea kuzitumia vizuri kuelimishwa zaidi ili wapate haki yao na kuwa na amani, " amesema

Amesema wataendelea kuboresha mifumo ya msaada wa kisheria kupitia digitali na simu za kawaida ili kufanikisha huduma bora kwa wananchi. 





Share:

NOTI BANDIA ZAKAMATWA SHINYANGA, JESHI LA POLISI LATAHADHARISHA WAKULIMA KUPOKEA FEDHA ZA MAVUNO USIKU


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha noti bandia zilizokamatwa

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata noti bandi 42 zenye thamani ya shilingi 420,000/= huku likiwatahadharisha wananchi hasa wakulima wanaouza mazao kuepuka kupokea fedha nyingi nyakati za usiku kutokana na kwamba wimbi la noti bandia lipo.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumatano Juni 26,2024 ambapo amesema Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia tarehe 26/05/2024 hadi 25/06/2024 kwa kushirikiana na jamii katika falsafa yake ya Polisi Jamii, limeendelea kuimarisha hali ya usalama wa raia na mali zao kwa kukabiliana na vitendo mbalimbali vya kihalifu na wahalifu kupitia misako na doria katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Shinyanga.

"Hizi fedha zilizokamatwa kama zingekuwa ni halali zingekuwa na thamani ya shilingi 420,000/=, haziihitahji hata utaalaamu kwa tupeleke Benki Kuu lakini tutapeleka kwa ajili ya hatua zingine ili kuthibitisha. Mtanzania aliyezoea kutumia fedha hata kwa macho tu anaona kabisa hizi ni noti bandia.

Katika kipindi hiki cha mavuno ili kukabiliana na matukio ya uhalifu mbalimbali ni pamoja na hizi fedha bandia zimekamatwa wakati zikiwa zinatakiwa kuingia kwenye mzunguko wa ununuzi wa mazao ya wakulima wetu, tunaendelea kutoa elimu kwa wananchi wawe makini kupokea fedha nyingi hasa nyakati za usiku, kwani wimbi la noti bandia lipo, watoe ushirikiano pindi wanapotilia mashaka kwamba mbona hizi noti hazipo katika uhalali",amesema Kaimu Kamanda Mgani.

Ameongeza kuwa kutokana na misako na doria zilizofanywa na Jeshi la Polisi pia vielelezo mbalimbali vilikamatwa katika matukio ya kihalifu ikiwemo Silaha moja aina ya Browning Pistol ambayo ilitumika katika tukio la unyang'anyi huko Halmashauri ya wilaya ya Msalala, Mabomba 10 ya maji, pamoja na Pikipiki 05, vitu mbalimbali vinavyotumika katika masuala ya ramli chonganishi, mtambo 01 wa kutengenezea Pombe haramu ya moshi, TV 01, meza 02, kabati 01 la kuwekea TV, milango 02 na madirisha 04 ya chuma.

Mgani amesema jumla ya watuhumiwa 25 wanashikiliwa katika vituo mbalimbali vya Polisi kuhusiana na tuhuma za kufanya uhalifu huku wakisubiri kufikishwa mahakamani na wengine wakipewa dhamana.

Amebainisha kuwa katika kipindi hicho cha mwezi mmoja, jumla ya kesi 08 zilihukumiwa mahakamani kwa mafanikio kama ifuatavyo. Kesi 02 za kulawiti zilihukumiwa kifungo cha maisha jela, Kesi 01 ya kujeruhi ilihukumiwa kifungo cha miaka 03, Kesi 02 za wizi zilihukumiwa kulipa fine ya Tsh, 300,000/, Kesi 01 ya kupatikana na Bangi ilihukumiwa kifungo cha nje miezi 12, na kesi moja ya kubaka ilihukumiwa kifungo cha nje miezi 06, mtuhumiwa alikuwa na umri wa miaka 17.

"Kwa upande wa usalama barabarani jumla ya makosa 3438 ya magari yalikamatwa ma makosa ya pikipiki na Bajaji yalikuwa ni 1,496 huku dereva 01 wa magari akifungiwa leseni yake kwa kukiuka sheria za usalama barabarani",ameeleza.

"Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuzingatia sheria za nchi ili kuweza kushughulika na kazi zingine za ki uchumi ambazo ni halali",amesema.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Jumatano Juni 26,2024 - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akitoa taarifa kwa vyombo vya habari 
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha noti bandia zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha noti bandia zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha Silaha aina ya Browning Pistol ambayo ilitumika katika tukio la unyang'anyi huko Halmashauri ya wilaya ya Msalala
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha Silaha aina ya Browning Pistol ambayo ilitumika katika tukio la unyang'anyi huko Halmashauri ya wilaya ya Msalala
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha vitu mbalimbali vinavyotumika katika masuala ya ramli chonganishi
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha mali mbalimbali zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha mtambo wa kutengenezea gongo
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha pikipiki zilizokamatwa
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP, Kennedy Mgani akionesha mabomba na mageti yaliyokamatwa.


Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

INEC YATOA VIBALI KWA ASASI 191 ZA KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA NA WAANGALIZI WA UBORESHAJI

 


 
Share:

Tuesday 25 June 2024

DC KILAKALA AVALIA NJUGA VITENDO VYA UBAKAJI NA ULAWITI



Na Hadija Bagasha Pangani

Mkuu wa Wilaya ya Pangani Mussa Kilakala ameanza kuvalia njuga vitendo vya ubakaji na ulawiti huku akiliagiza jeshi la polisi Wilayani humo kumfuatilia na kumkamata mtu mmoja kwenye kijiji cha Bushiri ambaye ameripotiwa kwa tuhuma za kuwashawishi watoto wa kiume ili afanye nao vitendo hivyo. 

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya amepiga marufuku uuzwaji wa pombe majumbani ambao umebainika kuwa chanzo cha ukatili wa kijinsia kwa familia hususani wakati ambao watu wanaanza kulewa.

Kilakala ametoa maagizo hayo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi ccm Wilaya ya Pangani huku akiitaka jamii kuungana kuhakikisha wanafanikiwa kwenye vita dhidi ya ukatili huo kwa watoto. 

Mkuu huyo wa Wilaya alitolea mfano mwanafunzi mmoja wa kidato cha tatu kwenye kijiji hicho ambaye mara kadhaa mtu huyo amekuwa akimrubuni kwa kutaka kumlawiti na kwamba ameripoti maeneo kadhaa lakini mtu huyo bado hajachukuliwa hatua. 

"Ndugu Mwenyekiti nilikwenda kwenye shule moja ( jina lake limehifadhiwa) hapa Bushiri mtoto mmoja jasiri,  tungekuwa na watoto majasiri kama yule hili tatizo lingekwisha kabisa kwa muda mfupi,  yule mtoto alizungumza kwa uchungu nadhani alikuwa form 3 au form 4 ameonyesha maigizo akaimba baadae akachukua maiki na kuzungumza kunambia mkuu wa wilaya mimi binafsi nimefanyiwa ukatili wa kijinsia kuna mzee ananitaka mimi kimapenzi hali yakuwa anajua mimi ni mtoto wa kiume, "alisema DC Kilakala

"Nimekwenda kushitaki kijijini nimekwenda kushitaki kwenye kata sijapata msaada nimempongeza yule kijana kwa kuwa jasiri nimempongeza yule kijana kwa kuwa jasiri watoto wetu mpaka wanaharibika ndio tuchukue hatua nimeliagiza jeshi la polisi yule mzee anayetuhumiwa wamuhoji atuambie kazi zile anazifanya na nani na ameshawaharibu watoto wangapi Bushiri ndugu mwenyekiti mambo haya si kana kwamba hayapo yapo tukikaa na watoto wetu tutayajua taratibu, "alisema Kilakala. 

Kuhusu uuzaji wa pombe majumbani Kilakala amesema baadhi ya kaya zinazouza pombe watu wanapoanza kulewa wanawabaka watoto wa familia bila mama mzazi au baba mzazi kujua kutokana na kuwa bize na biashara hiyo. 

Kufuatia hali hiyo Kilakala amepiga marufuku pombe kuuzwa majumbani na tayari wameshaanza kuyafungia baadhi ya maeneo ambayo walevi hufanya vitendo vya hovyo eneo ambalo wanafunzi wanapita wakitoka mashuleni wa wengine kwenda kuiga na kupelekea mmomonyoko wa maadili. 

"Nimemuelekeza afisa biashara kupitia Mkurugenzi maeneo yote yanayoendesha biashara kiholela yafungiwe mpaka hapo yatakapopata leseni lakini tumemwelekeza Mkurugenzi watoto hakuna kurudi shule usiku,  masomo gani yanapatikana usiku watoto wanarudi nyumbani saa mbili usiku mpaka saa nne usiku wanatoka wapi nielekeze muda wa masomo uzingatiwe na watoto warudi muda waliopangiwa na mzazi ukiona mtoto hajarudi mpaka saa kumi uanze kuwa na wasiwasi sio mtoto anarudi saa nne usiku unasema hiyo kawaida yake, "alisisitiza Kilakala. 

Awali akizungumzia mafanikio waliyoyapata katika Wilaya hiyo Kilakala amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amewafanyia maendeleo makubwa ikiwemo katika sekta ya elimu,  afya,  maji na barabara. 

"Nimshukuru sana Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan katika kutuletea miradi mikubwa ya maendeleo lakini nimshukuru na nimpongeze Mbunge wetu na Waziri wetu wa maji Jumaa Aweso kwa namna anavyopambana kupigania kuchochea kuhakikisha Pangani tunapata miradi mikubwa ya maendeleo katika sekta zote bila kumsahau Mwenyekiti wetu wa Mkoa Rajab Abrahaman kwa kazi kubwa anayoifanya katika Mkoa Tanga lakini katika kuchochea maendeleo katika wilaya yetu ya Pangani na kuwa chachu ya miradi mikhbwa ya maendeleo inayogusa wananchi moja kwa moja, "alisisitiza DC Kilakala. 


Share:

Monday 24 June 2024

MTATURU AISHAURI SERIKALI KUONDOA URASIMU KWENYE BIASHARA



MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu amechangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2023 huku akiainisha maeneo manne ya msisitizo kwa serikali ili kuweza kuongeza mapato kupitia sekta ya biashara.

Akichangia Juni 24,2024, Bungeni Jijini Dodoma Mtaturu ametaja eneo la kwanza kuwa ni biashara na kuishauri serikali kuondoa urasimu uliopo ili kuweza kukuza biashara.

Amesema katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)ya mwaka 2020/2025,Sekta ya biashara imetajwa kwa msisitizo mkubwa sana kupitia Ibara ya 49 ukurasa wa 60.

“Ibara hiyo imeeleza kuwa CCM inatambua kwamba biashara ni chanzo cha mapato na hivyo kitaendelea kuelekeza serikali kuimarisha biashara ya ndani nan je ya nchi,na imeahidi katika kipindi cha miaka mitano Chama kitahakikisha mchango wa sekta ya biashara kwenye pato la Taifa unaendelea kuimarika,

“Ninataka kukumbusha kwenye eneo hili kwamba sekta ya biashara ikisimamiwa vizuri inaweza kuongeza mapato ya nchi na fedha ambazo leo tuna changamoto kwenye miradi,tukiweza kuwekeza vizuri tutaweza kufanya miradi yetu vizuri,

Amesema katika biashara kuna urasimu mkubwa ambapo mtu akitaka kuwekeza kwenye biashara ni lazima aache kazi nyingine zote ili ashughulikie.

“Taasisi zetu zinazosimamia utoaji wa vibali zitazamwe upya ,ninaamini tukitazama kwenye eneo hilo itasaidia uwekezaji,leo Mh Rais wetu analeta wawekezaji nchini lakini ili mtu awezek uanzisah kampuni inamchukua mwezi mzima,sasa kwa hali hii unategemea wapi kodi itapatikana wakati mtu hajaanzisha biashara,

“Nikupe mfano mmoja leo mtu akitaka kujenga hoteli ya ghorofa hata ikianza ghorofa moja, mbili anaanza kupewa vikwazo kwamba kuna watu wazima moto nao wanataka fedha sasa tunakwenda wapi,

Suala la pili ni miundombinu ambayo ni uti wa mgongo wa biashara nchini na katika eneo hili ameomba serikali kujenga barabara ili kurahisisha sekta ya usafirishaji ikiwemo kusimamia ujenzi wa madaraja.

Amesema kunapokuwa na usafirishaji wa bei nafuu utasaidia kupunguza ushuru wa bidhaa mbalimbali na hivyo kuiomba serikali isimamie mpango wak ujenga barabara na kuongezewa nguvu ili kuhakikisha nchi inafunguka zaidi.

“Nitoe ombi kwenye eneo hili la barabara hatujafanya vizuri kwenye barabara ya za EPC+H,tulisainiwa mkataba toka mwaka jana mpaka tunavyoongea leo mwezi wa sita mwingine barabara hazijaanza ,barabara zenye urefu wa kilomita 2,035,kuna barabara ile ya kutoka Singida-Kwamtoro –Kiblash Tanga yenye kilomita 460 haijaanza kufanya kazi,wananchi wale tunawaambia nini,

Mtaturu ametaja eneo la tatu kuwa ni ardhi ambayo ndio msingi katika ujenzi wa Taifa lakini kuna migogoro mingi na hivyo kuomba bajeti hiyo ikajibu changamoto ambazo zipo kwa wakulima na wafugaji nchini.

“Leo hii watu wakitaka kutumia ardhi unaambiwa hii ardhi ni ya mtu fulani amechukua heka zaidi ya 1,000,heka zaidi ya 2,000 peke yake, watu wanaotaka kuwekeza katika nchi yetu wanakosa maeneo,hatujapima ardhi yetu tupime sasa na kuweka mpango wa matumizi bora ya ardhi ambao ndio utaondoa migogoro katika nchi hii,”amesema.

Mtaturu ametaja eneo la nne kuwa ni kilimo ambacho ni uti wa mgongo na kinaajiri wananchi zaidi ya asilimia 65.

“Ibara ya 35 ya Ilani ya CCM ukurasa wa 33 unasema kilimo kitaendelea kuwa mhimili wa Taifa letu, niombe sana jitihada zinazofanyika tunaziona uwekezaji wa mbolea ya ruzuku ,tumeona kwenye mbegu na utaalam mbalimbali ,tuendelee kuongeza uwezo wa wale watumishi wa kilimo ambao wapo kwenye maeneo yetu wakiwemo maafisa ugani

Mbali na mambo hayo manne amegusia pia uzalishaji wa sukari eneo ambalo amesema ni lazima serikali iingilie kati na kuweza kusimamia.

“Hatuwezi kuacha soko huria kwa jambo ambalo ni muhimu kwa wananchi,kilicholetwa hapa tupitishe ili NFRA waweze kununua sukari kwa niaba ya serikali na watanzania,leo hatuwezi kuona watu wanazunguka wanaitumia siasa sukari hatuwezi kukubali,

“Serikali makini na kiongozi makini anaposikia changamoto ni lazima atafute njia ya kutatua ambayo mojawapo ni hii ambayo tunayo sasa hivi ya kuweza kumonopoly soko la sukari ili kuwafanya watanzania wawe salama,sukari leo ni kila kitu ndio maisha,”.amesema.

Share:

MABORESHO YALIYOFANYWA NA TANROADS KWENYE MIZANI YADHIBITI MIANYA YA RUSHWA-MHANDISI KYAMBA


Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia TANROADS imekamilisha ujenzi wa Mzani mpya wa kisasa wa Mikumi uliopo barabara kuu ya Morogoro - Iringa, pamoja na maboresho katika mizani ya mikese uelekeo wa barabara ya Dar-es Salaam - Morogoro kwa gharama ya shilingi bilioni 1.9, hatua ambayo imesaidia kumaliza msongamano wa magari katika barabara hizo.

Baada ya kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji na Usafirishaji katika barabara ya TANZAM Highway Serikali iliona Mzani uliopo kuwa hautoshelezi mahitaji ya kupima magari kwa wingi, hivyo iliamua kufanya maboresho ya mzani uliopo pamoja na kujenga Mzani mwingine mpya na wa kisasa ili kuendana na mahitaji ya sasa.

Maboresho hayo yameenda sambamba na kuweka vifaa maalum (Sensor) ambavyo vitafanya kazi ya kuchuja na kutoa taarifa ya uzito wa gari husika, kama limezidisha mzigo ama la na kama halikuzidisha basi linaendelea na safari moja kwa moja bila kupita katika Mzani na lile lililozidisha mzigo litalazimika kupita kwenye mzani.

Ili kukabiliana na vitendo vya rushwa serikali kupitia TANROADS iliamua kujikita kwenye utengenezaji wa teknolojia kwa kufunga mifumo ya CCTV kamera na mifumo ya usimamizi wa taarifa kwenye maeneo yenye mizani za kupima uzito wa magari barabarani jambo ambalo kwa sasa kadhia ya rushwa imepungua kwa kiasi kikubwa kama sio kumalizika kabisa.

Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania TANROADS wa mkoa wa Morogoro Mhandisi Alinanuswe L. Kyamba ameyasema hayo leo tarehe 23 Juni 2024 mara baada ya kutembelea na kukagua shughuli za ufanyaji kazi zinazofanywa katika Mzani wa Mikumi katika barabara ya Morogoro-Iringa, Mzani wa Dakawa barabara ya Morogoro-Dodoma na Mzani wa Mikese barabara ya Morogoro-Dar es salaam.

Mhandisi Kyamba amesema kuwa kwa sasa kwenye uendeshaji wa Mizani inatekelezwa sheria ya Jumuia ya Afrika Mashariki iliyoanza kutumika mwaka 2019 mwezi Machi ya namna ya udhibiti wa mizigo na kuzilinda barabara ziwe salama wakati wote, ambapo kwa sasa elimu inayotolewa imewezesha wasafirishaji wengi kufuata sheria na hivyo kusababisha idadi ya magari yanayozidisha uzito kupungua.

Amesema kuwa mifumo hiyo imewezesha shughuli zote za mizani kufanyika kwa uwazi, ambapo Meneja wa TANROADS wa Mkoa husika ataweza kuona kile kinachofanyika kwenye kituo chake cha mzani.

Ameomgeza kuwa kupitia mifumo hiyo TANROADS Makao Makuu na Wizara ya Ujenzi ina uwezo pia wa kuona kile kinachofanyika kwenye mzani na pale itakapobainika kuna uvunjivu wa sheria au viashiria vya rushwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi watu wanaohusika na vitendo vya rushwa.

Mhandisi Kyamba amewapongeza wafanyakazi wa mizani kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya usiku na mchana lakini amewasihi kuendelea kujiepusha na vitendo vya rushwa ili kulinda miundombiniu ya barabara na kufanya kazi kwa tija.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger