Monday, 21 August 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 21,2023

































Share:

Sunday, 20 August 2023

NAIBU WAZIRI WA MAJI AFANYA ZIARA KUTEMBELEA MRADI WA MAJI MSHIKAMANO



Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amewataka wananchi hususani wa Kata ya Mbezi, Ubungo na Mshikamano ambao ni wanufaika wa mradi wa maji Mshikamano kuwa na subira ya kuwaunganisha na huduma kwa kuwa kazi ya ufundi huwa inatekelezwa kwa kuzingatia utaratibu.

Ameeleza hayo wakati wa ziara yake ya siku ya pili alipotembelea utekelezaji wa mradi wa maji Mshikamano uliotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).

Amesema kuwa mradi huu wa Mshikamano umetekelezwa kwa ufanisi mkubwa na DAWASA na ni mradi ambao utajibu shida ya maji kwa wananchi wengi wa maeneo haya.

"Tumesikia shuhuda nyingi kutoka kwa wananchi kuwa maeneo haya yalikuwa makame kwa mrefu, lakini kwa jitihada kubwa za DAWASA maeneo mengi yameanza kupata maji, tunaishukuru DAWASA kwa namna ambavyo wanaiwakilisha vizuri Wizara ya Maji," ameongeza Mhandisi Maryprisca.

"Wito wangu kwa wananchi ambao wameshalipia maunganisho ya maji wawe na subira kwa kuwa kazi za kiufundi zinakwera kwa utaratibu, tayari vifaa vya maunganisho mapya vimeshanunuliwa na wateja mtaanza kuunganishiwa hivi karibuni," Mhandisi Marryprisca Mahundi Naibu Waziri wa Maji.

Mhandisi Maryprisca amefafanua kuwa utoaji wa kumbukumbu namba za wananchi walioomba maji ulisimama kwa muda ili kufuatilia upatikanaji wa vifaa vya maunganisho ya maji, na kwa sasa vifaa vimepatikana hivyo wananchi watapewa namba na kuunganishiwa na huduma.

Tunampongeza sana Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa uzalendo wake wa kutoa fedha za mfuko wa Uviko kiasi cha bilioni 2.5 kwenye mradi wa maendeleo ili wananchi wapate maji.

Nae Mwakilishi wa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Ndugu Shaban Mkwanywe amesema anaishukuru Serikali kupitia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuwezesha kutekeleza mradi huu na kuukamilisha.

Mradi huu unatuwezesha kujibu hoja za shida ya maji kwa wananchi, kwa sasa kazi tunayoendelea nayo ni kusambaza maji kwa wananchi kwa kasi.

"Kwa mwaka huu wa fedha 2023/24 tumetenga fedha za ndani bilioni 2.5 kwa ajili ya kusambaza maji kwa wananchi wote wa kata ya Mbezi, Msakuzi kusini na kaskazini kuwa wasiwe na wasiwasi huduma itafika," ameeleza Mhandisi Mkwanywe.

Mkazi wa Kata ya Mshikamano Ndugu Sanga Mbowe ameishukuru Serikali kupitia DAWASA na kuomba kazi ya kusambaza maji ifanyike kwa haraka ili wananchi wote waweze kunufaika na huduma.

Share:

FOXPOT SLOTI BORA KUTOKA MERIDIANBET!




KUWA KWENYE NAFASI NZURI YA KUSHINDA MKWANJA MREFU, BONASI KIBAO KUTOKA KASINO YA MTANDAONI YA MERIDIANBET NI SLOTI YA FOXPOT

Fahamu Kuhusu Sloti ya Foxpot

 

Unapoitazama sloti hii ya Foxpot, utashangazwa wapi hizi shilingi zinatoka. Jibu ni rahisi sana, sloti ya Foxpot inakujia na Jackpoti tatu kubwa na Mbweha akiwa kama alama ya malipo ya Wild/windoKasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, ni sehemu sahihi kwa wachezaji wa kasino!

 

Sio hayo tu, Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet kupitia sloti ya Foxpot inakuletea Gurudumu 12 ambalo litakupa fursa ya kushinda bonasi mbalimbali.

 

Unasubiri nini? ingia mchezoni kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet kwa kugusa hapa na ufurahie ushindi mkubwa.

 

Jinsi ya Kucheza Sloti ya Foxpot

 

Ni rahisi sana! Unachotakiwa kufanya ni kuingia kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet na kuchagua mchezo huu wa Foxpot ujishindie mamilioni!

 

Sloti hii ya Foxpot ina alama na machaguo mbalimbali. Ili ushinde, unatakiwa upate alama tatu zenye kufanana kwenye sloti hii yenye kolamu 5 na mstari mmoja wa malipo.

 

Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet ina machaguo mbalimbali ambayo yanakupa fursa ya wewe mchezaji kuucheza mchezo huu kiurahisi. Kwa kubofya alama ya + na – ambazo zipo kwenye kitufe cha Bet, itakupa nafasi ya kuweka dau lako unalolitaka.

 

Kuna chaguo la Autoplay ambalo litakuwezesha wewe (mchezaji) kuzungusha mizunguko kiatomatiki. Alama za sloti hii ni ya matunda ambayo ni Cherry ambalo lina thamani ndogo, Zambarau ambalo litakurudishia mara 1.5 ya dau lako huku likufuatiwa na Ndimu ambalo litakulipa mara 2.5 ya dau uliloliwaka.

 

Endapo utapa alama 1, 2 au 3 za Lucky 7 basi utalipwa mara tatu ya dau uliloliweka huku alama moja ya Lucky 7 ikiwa ina uwezo wa kukulipa mara 10 ya dau lako, na alama 2 mbili za Lucky 7 zikitakurudishia mara 15 wakati alama 3, zitakurudishia mara 25 ya dau lako.

 

Sio hivyo tu, kama ukipata alama ya Wild utarudishiwa mara 40 ya dau lako. Kumbuka, alama ya Wild inauwezo wa kubadilisha alama zozote kwenye mchezo huu na kukupatia ushindi isipokuwa alama ya bonasi. Unasubiri nini? Jiunge leo na Meridianbet na upate bonasi kubwa, Odds kubwa na Jackpoti kabambe.


Share:

TANZANIA, INDIA ZAIMARISHA USHIRIKIANO KIUCHUMI


*Dkt. Biteko asema biashara nyingi Sekta ya Madini inafanywa na India

Arusha

Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko amesema  ushirikiano wa kidiplomasia baina ya Serikali ya Tanzania na nchi ya India umeimarika na umeendelea kuzinufaisha nchi hizo kiuchumi.

Dkt. Biteko amesema  hayo katika sherehe za Maadhimisho ya Miaka 77 ya Uhuru wa India zilizoandaliwa na watanzania wenye asili ya nchi hiyo yaliyofanyika Agosti 19 jijini Arusha.

"Kama mnavyofahamu nchi ya India na Tanzania zimekuwa na mahusiano ya muda mrefu ya kidiplomasia kiuchumi na jamii ya wahindi katika nchi yetu inajishughulisha na uwekezaji mwingi katika biashara na viwanda," amesema Dkt. Biteko.

Aidha, Dkt. Biteko amesema nchi ya India imefanya biashara nyingi kwenye Sekta ya Madini ikiwa pamoja na  uuzaji na ukataji wa madini na mnyororo mzima wa shughuli uongezaji thamani madini.

Amesema hapa nchini wapo watu wenye asili ya India wapatao elfu 50 na kati ya hao wageni wenye pasipoti ya India wapo kati ya elfu 15 na elfu 20 na Arusha pekee ina zaidi ya watu 2000 wenye asili ya India na wamewekeza kwenye maeneo mengi na kufanya biashara mbalimbali.

Dkt. Biteko ameongeza kuwa, wageni wanaofika nchini kutoka India wamekuwa mstari wa mbele katika kuwekeza na kuchangamkia fursa mbalimbali za kibiashara kwenye Sekta ya Madini, viwanda na maeneo mengine.

"Tumeungana nao kusheherekea uhuru wao na kuwatia moyo, kuwatakia kila la heri kama Serikali tunawaunga mkono kwenye kila juhudi wanazozifanya na tunaliombea mema Taifa la India liendelee kuimarika ni Taifa kubwa lenye watu wengi na mchanganyiko mkubwa wa utamaduni," amesema Dkt. Biteko.

Kwa upande wake, Balozi wa India nchini Mhe. Binaya Srikanta Pradhan amesema Tanzania imekua sehemu salama pa kuishi na kufanya biashara na kuendeleza shughuli za utamaduni za nchi yao. Ameongeza kuendelea kuimarisha ushirikiano huo katika nyanja zote.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mrisho Gambo amesema anajivunia umoja, upendo na mshikamano uliopo kati ya Watanzania wenye asili ya India wanaoishi hapa nchini hususan wanavyochangia katika masuala mbalimbali ya maendeleo.

"Ukiangalia kwenye ajira wametoa ajira nyingi  kwenye viwanda, lakini pia wanalipa kodi kwa Serikali. Nawaahidi kuwapa ushirikiano jamii ya Wahindi ili shughuli zao ziweze kuwa salama zaidi," amesema Gambo.


Nchi ya India huadhimisha sherehe za Uhuru kila  ifikapo tarehe 15 Agosti ya kila mwaka ambapo jamii ya wahindi nchini pia imeadhimisha sherehe hizo mkoani Arusha.
Share:

WEKEZA KWENYE KILIMO CHA VANILLA UONE MAAJABU - 0629300200




Zao la Vanilla ambalo sasa limeanza kuchangamkiwa duniani linatajwa kuwa zao linalouzwa kwa bei kubwa zaidi duniani inayofikia dola 430 kwa kilo moja sawa na shilingi Milioni ya Tanzania.

Kutokana na faida kubwa ya Vanilla, Kampuni Vanilla International Ltd ambayo ina mashamba ya Vanilla "Vanilla Village" katika maeneo mbalimbali duniani imeweza kujitwalia wawekezaji (wakulima) wa zao la Vanilla kufikia 1350 nchini Tanzania ambapo kabla ya uhamasishaji huo wawekezaji wa zao la Vanilla walikuwa hawafiki 50. 

Mkurugenzi Mwanzilishi wa Makampuni ya Vanilla International Limited, Simon Mnkondya anasema zao la Vanilla ni zao lenye bei kubwa kuliko Silver (fedha) na linachuana na dhahabu.


Kampuni ya Vanilla International inatumia namba za simu +255629300300, +255769300200 na +255624300200 kwa ajili ya kufundishia wananchi bure kuhusu Kilimo cha Vanilla. 






SOMA ZAIDI KUHUSU VANIILA


Share:

KWA DAKIKA CHACHE TU!! JIPATIE TIKETI YA NDEGE UNAYOIPENDA!!


Kwa dakika chache tu unajipatia Tiketi ya Ndege unayoipenda! Na safari yako iwe salama, kata Tiketi 🎫🎟️ na #JovisonInsuranceAgencyCoLtd #GoodHandsForTheGoodLife

#airticketing #airtanzania #precisionair
Share:

Saturday, 19 August 2023

USHIRIKISHWAJI WA TAASISI ZA UMMA KATIKA KUANDAA VIWANGO NA MIONGOZO YA E-GA



Maafisa TEHAMA kutoka katika taasisi mbalimbali za umma wameshiriki katika kikao kazi cha kuandaa na  Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, ili kuhakikisha inaendana na Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya mwaka 2019.  

Lengo ni kuhakikisha Serikali inakua na Serikali mtandao yenye tija na inayoongeza ufanisa katika utendaji kazi na utoaji huduma kwa umma.

Kikao hicho kilichoandaliwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), kilifanyika kwa siku 3 kuanzia Agosti 15, 2023 katika ukumbi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijijini Dodoma.

Viwango na Miongozo hiyo inapatikana katika Tovuti ya e-GA kupitia kiungohttps://www.ega.go.tz/standards

Share:

MADEREVA WASHAURIWA KUPATA MAFUNZO YA UDEREVA

 


Na Okuly Julius-Dodoma

MKUU wa chuo cha mafunzo ya udereva cha Wide Institute of Driving jijini Dodoma, Faustine Matina ameishauri serikali kuweka mikakati ya kukomesha ajali nchini ikiwemo mafunzo maalum ya mara kwa mara kwa madereva wa serikali ambao wamekuwa wakilalamikiwa kutozingatia sheria za usalama barabarani.


Matina, amesema hayo Leo Agosti 19,2023 jijini Dodoma, wakati wa mafunzo kwa madereva wa malori wasiokuwa na vyeti vya udereva ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Jeshi la Polisi.


Mapema mwaka huu waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Hamad Yusuf Masauni, alitoa maagizo kwa jeshi la polisi kufanya ukaguzi wa leseni za madereva wa malori na mabasi ili kukomesha ajali zilitokea mfululizo katika maeneo mbalimbali nchini.


Masauni, aliagiza madereva wote ambao wanaleseni lazima wawe na vyeti vya mafunzo ya udereva kutoka vyuo vinavyotambulika na atakaye kosa sifa hatua zichukuliwe.


“Kazi ya vyuo vya udereva ni kuhahakikisha kuwa tunaandaa madereva bora ili kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani kutokana na uzembe hapa leo tunao madereva wa malori ambao wanaleseni lakini hawana mafunzo ya udereva tunawafunisha sheria za usalama barabarani, utii wa sheria bila shurti kuwa watiifu wanapokuwa njiani na vyombo vya moto”amesema Matina


Aidha, amesema pamoja na serikali kutoa maagizo hayo utaratibu huo unapaswa kuwa endelevu ili kusaidia madereva wote ambao wanaendesha vyombo vya moto bila kuwa na mafunzo.


“Tunaomba hili liwe endelevu ili madereva wote wapate mafunzo na kukomesha ajali zinazotokea kwa makosa ya kibinadamu lakini pia serikali iandae program maalum kwa ajili ya madereva wa serikali ambao wamekuwa wakilalamikiwa namna wanavyoendesha vyombo vyao hawazingatii sheria za usalama barabarani”amesema Matina


Amesema madereva ni binadamu ambao wanahitaji kupata muda wa mafunzo ya kukumbushwa wajibu wao mara kwa mara kwakuwa mambo mengi yanabadilika kila siku hivyo serikali inapaswa kuzingatia ushauri huo kwa ajili ya kukomesha ajali.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa madereva Tipa Dodoma (UMATIDO) Praygod Malle,alikishukuru chuo hicho kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kikosi cha usalama barabarani kwa kutoa mafunzo hayo.


“Tunaishukuru serikali yetu kwa kutoa maagizo ambayo yamewezesha leo madereva kupata mafunzo ambayo yatakwenda kupunguza tatizo la ajali nchini ambazo nyingi zimekuwa zikitokea kwa makosa ya kibinadamu”amesema Malle


Hata hivyo, ametoa wito kwa madereva wote ambao wanaendesha vyombo vya moto bila kuwa na mafunzo kuchangamkia fursa hiyo ili kuepuka kusumbuliwa na mamlaka katika oparesheni mbalimbali za ukaguzi wa leseni.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger