Thursday, 29 July 2021

Lead Generator Agency Nyanza Branch at NBC

Lead Generator Agency Nyanza  Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line with […]

This post Lead Generator Agency Nyanza Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lead Generator Agency Iringa Branch at NBC

Lead Generator Agency Iringa  Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line with […]

This post Lead Generator Agency Iringa Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Wachimbaji wadogo na malalamiko yasiyo na Mwisho Busega, Simiyu

Samirah Yusuph
Busega. Fukuto la mgogoro wa wachimbaji wadogo katika mgodi wa Imalamate wilayani Busega  Mkoa wa Simiyu baina ya wamiliki wa leseni na wenye mashamba kuhusu mgawanyo wa mazao ya dhahabu linaendelea kuibua malalamiko.

Wachimbaji hao wamekuwa wakidai kuwa hawatendewi haki na wamiliki  wa leseni katika mazao yanayopatikana hali inayowalazimu kutoa mgao hata katika huduma za kijamii kama usimamizi na ulinzi ambazo zilipaswa kulipwa na wenye leseni.

"Licha ya kuwa utaratibu unaelekeza majukumu ya mmliki wa leseni  lakini bado walinzi na "inspectors" tunawapa mgao jambo ambalo linakuwa ni unyonyaji kwa wachimbaji wadogo" alisema Jumanne Tembe mmoja wa wachimbaji wadogo katika mgodi wa Imalamate.

Licha ya malalamiko hayo Baadhi ya wachimbaji wamelaumu wasimamizi wa mgodi kutoza pesa ya usafi na kuweka alama katika mifuko ya mawe bila kutoa risiti jambo ambalo wamelishuku kuwa ni upotevu wa mapato ya serikali pamoja na dhuruma kwa sababu pesa wanayotozwa ni kubwa.

"Mfuko mmoja unalipiwa tsh27,000 unapo utoa kwenye duara na kuufikisha katika uzio ili uwekewe alama lakini pesa inapokelewa bila kutolewa risiti ni bora malipo yafanyike na risiti itolewa ili ijulikane pesa hiyo inaenda wapi na inafanya nini".alisema Amos Mwambebo mchimbaji katika mgodi huo.

Akitoa ufafanuzi dhidi ya mgawanyo wa mazao ya dhahabu yanayopatikana Afisa madini wa mkoa wa Simiyu Amin Msuya alisema kuwa mgawanyo unakakwenda katika makundi manne na kuyabainisha makundi hayo kuwa,

"Mrahaba wa serikali asilimia saba, mmiliki wa shamba asilimia 10, mmiliki wa leseni asilimia 20 na mwenye
 Duara anabakiwa na asilimia 70, mwenye jukumu la kulipa usimamizi na ulinzi ni mmliki wa leseni katika asilimia zake".

Akitatua kero hiyo mkuu wa wilaya ya Busega, Gabriel Zakaria aliwataka wasimamizi wa mgodi kutekeleza maagizo ya serekali ikiwa ni pamoja na kufuata mikataba ya makubaliano ya mgao, kuboresha miundombinu ya barabara na upatikanaji wa huduma za kijamii.

"Mapato ya serikali ni lazima yakusanywe, haki itendeke kwa kila mmoja hakuna sababu ya kuendelea kuwa na mgogoro halikuwa utaratibu upo wazi katika migodi niwakati wa  kutekeleza ili kila mmoja anufaike na madini yaliyopo".

Mwisho.


Share:

Mabula Atatua Mgogoro Wa Mpaka Kati Ya Newala Na Masasi


 Na Munir Shemweta, MTWARA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemaliza utata wa muda mrefu kuhusiana na mgogoro wa mpaka kati ya wilaya ya Masasi na Newala mkoani Mtwara baada ya kubainisha mpaka halisi baina ya pande hizo mbili.

Akiwa ameambatana na wataalamu wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Mtwara, Wakuu wa wilaya za Masasi na Newala, Wabunge pamoja na Wakurugenzi wa halmashauri zinazopakana ikiwa ni utelelezaji wa maagizo ya Makamu wa Rais Dkt Philip Isdor Mpango, Dkt Mabula alibainisha mpaka halisi uliopo kati ya kijiji cha Njenga na Miyuyu ikiwa ni takriban kilometa tano kutoka ulipoainishwa mpaka wa awali.

Akizungumza wakati wa usuluhishi wa mgogoro huo Julai 28, 2021 Naibu Waziri Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Mabula alisema, jambo kubwa lililotatiza kwenye  mgogoro huo wa mpaka ni uhitaji wa maeneo ya kiutawala ambapo upande wa wakuu wa wilaya alisema hawakuwa na tatizo.

‘’Jambo linalotatiza sisi wengine ni katika suala zima ni sisi wachaguliwa kutaka maeneo ya kiutawala na wakuu wa wilaya wanasema hawana matatizo na ndiyo watawala sisi wachaguliwa hatutakiwi kuingia kabisa kwenye migogoro’’ alisema Dkt Mabula

Dkt Mabula aliongeza kuwa, iwapo kuna tatizo la kiutendaji kwenye eneo hilo basi wakuu wa wilaya wa maeneo husika wanaweza kushughulikia lakini kwa shida ya mipaka ya kiutawala  basi wakurugenzi wa halmashauri wana mamlaka ya kukubalina kwa kuwa suala hilo  linaangukia TAMISEMI na kusisitiza kwamba halmashauri zikikubaliana kazi ya wizara ya ardhi ni kubainisha mipaka.

Aliwaagiza Wakurugenzi wa halmashauri za wilaya za Masasi na Newala mkoani Mtwara kwenda kwa wananchi wa vijiji vyenye migogoro kwa ajili ya kuzungumza na kuwapa elimu wakati kwa sasa mpaka unaotambuliwa ukiwa ni ule alioanishwa na yeye kulingana na vipo vya kitaalamu vinavyoonesha.

‘’Kama kuna maelezo mengine kuhusiana na mpaka huu wa Newala na Masasi basi itabidi watendaji na viongozi wa maeneo husika wakae pamoja na kushughulikia mgogoro huo ikiwa ni pamoja na kwenda uwandani, lengo ni kijiridhisha maana huwezi kupata suluhu ukiwa ofisini na mtkachokubaliana Wizara itakwenda kuweka alama za mipaka.

Diwani wa Kata ya Chilangala mkoani Mtwara Jamali Jafu aliutetea mpaka wa awali kati ya wilaya hizo mbili kwa kusema mpaka huo unapaswa kubaki eneo la Miyuyu  kwa kuwa ni mpaka wa asili tangu mababu kabla ya kuzaliwa wilaya ya Masasi.

Mkuu wa wilaya ya Masasi Claudia Kitta alisema, baada ya kuanishwa kwa mpaka huo kwa kuhusisha wataalamu wa pande zote sasa mpaka unaotambuliwa ubaki ulioanishwa na Naibu Waziri wa Ardhi na iwekwe alama katika eneo lililotambuliwa huku suala la vijiji vilivyoingia eneo lingine likifanyiwa kazi.

‘’Tukubaliane mipaka ni sahihi na vipimo vinaonesha na hili linguine la vijiji basi tutaangalia kijiji gani kimeingia huku au kimeingia kule na hili si tatizo kwa kuwa kinajitambua na huduma za jamii hazina mipaka’’ alisema Mkuu wa Wilaya ya Masasi Claudia Kitta

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Newala Alhaji Rajabu Kundya alisema, suala muhimu katika mgogoro huo ni kumaliza migogoro iliyopo kwenye vijiji vya mpaka na kueleza kuwa hatua hiyo itaoongoza maeneo ya uwajibikaji na kuonesha mpaka halisi wa wilaya na wilaya.


Share:

Dk. Mwinyi Umefika Wakati Wa Kuunda Tume Kupambana Na Udhalilishaji.

 Rais Wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi  amesema umefika wakati wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuunda tume ya kupambana na Udhalilishaji wa Kijinsia visiwani Zanzibar kwa ajili ya kupambana na udhalilishaji visiwani humo. 


Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo kwenye  kongamano la udhalilishaji liloandaliwa na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake wa Zanzibar katika ukumbi wa Shekh Idriss Abdul - Wakil, Kikwajuni Jijini Zanzibar.


 Aidha Mhe. Rais Mwinyi amewataka watendaji wa Taasisi zote zinazohusika na suala la udhalilishaji kujipima juu ya utendaji wao. Hii ni baada ya kuendelea kutolewa malalamiko Kwa baadhi ya watu ambao wanashutumiwa Kwa vitendo vya udhalilishaji kuachiliwa huru.


Udhalilishaji sio suala la ubakaji tu, kwani waathirika wakubwa japo wanaonekana ni wanawake lakini wapo wanaume wengi ambao wanadhalilishwa pia. Alisema Mhe. Rais Mwinyi.


“Nimekuja hapa kuwapeni Uhakika wa kwamba ninayo dhamira ya dhati kulimaliza tatizo la udhalilishaji visiwani kwetu. “


Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemtaka Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Omary Makungu kuwahimiza majaji na mahakimu waliochini ya Mhimili wake kutekeleza wajibu wao Kwa wakati na Kwa Uadilifu ili kulinda haki za watu ambao wametendewa unyanyasaji wa kijinsia.


Mhe.  Rais, Dk. Mwinyi, amezishukuru taasisi na asasi binafsi ambazo zimekuwa zikitoa misaada ya kisheria kwa Wananchi wa Zanzibar kwani licha ya Kwamba ni wajibu wa Serikali kutoa huduma na misaada ya kisheria, lakini taasisi hizi zimekuwa msaada mkubwa.



Share:

Waziri Ndugulile Aendesha Kikao Cha Mapato Na Matumizi Ya Wizara Na Taasisi Zake

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile ameendesha kikao cha mapato na matumizi ya robo ya nne ya mwaka wa fedha wa 2020/21 baina ya menejimenti ya Wizara hiyo na taasisi za Wizara hiyo ikiwemo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Shirika la Posta Tanzania (TPC), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Tume ya TEHAMA (ICTC) na Baraza la Watumiaji wa Huduma ya Mawasiliano (TCRA – CCC) ambacho kimefanyika kwenye ukumbi wa Kikwete, Dodoma

Ameongeza kuwa kwa kipindi hicho cha mwezi Aprili hadi Juni, 2021, Wizara kwa kushirikiana na taasisi zake imefanikisha utekelezaji wa majukumu yake ya kuongeza mapato ya taasisi hizo ikiwemo taasisi ya UCSAF, TTCL na TPC.

Amesema kuwa ameazimia kuzima laini za simu za mkononi 18,622 ambazo hazijahakikiwa pamoja na kuziua vitambulisho vya taifa 14,768 vilivyosajili laini za simu kwa utapeli na Serikali itawatafuta matapeli hao ili waweze kuchukuliwa hatua

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa kikao hicho kimefanyika ili kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu na mapato na matumizi ambapo Wizara imekusanya mapato ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ya shilingi bilioni 45 ambayo yamezidi makadirio ya shilingi bilioni 30. Pia, ameishukuru Serikali kwa kuongeza bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha wa 2021/22 kufikia shilingi bilioni 240 ukilinganisha bajeti ya shilingi bilioni 15 ya mwaka wa fedha 2020/21.

Naye Kaimu PostaMasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Macrice Mbodo amesema kuwa huu ni utaratibu mzuri baina ya Wizara na taasisi zake kwa kuwa kila baada ya miezi mitatu kikao kinafanyika na kwa kipindi hicho Shirika limezalisha faida ya shilingi bilioni 3.6; kuboresha huduma ya duka mtandao ambapo wajasiriamali wadogo wanafanya biashara duniani kote

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mwita Vedastus amesema kuwa Shirika limepata faida ya shilingi bilioni 12 kwa mwaka na kwa robo ya nne ya mwaka wa fedha wa 2020/21 wamepata faida ya shilingi bilioni 2 kwa mapato ambayo hayajakaguliwa pamoja na kutoa huduma ya data kwa wateja 223,000 wa taasisi za ndani na nje ya nchi na watu binafsi

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba amesema kuwa kikao hicho kinawezesha kupeana mrejesho baina ya Wizara na taasisi zake ili kufahamu mapato na matumizi kwa kipindi hicho ambapo UCSAF imezidi malengo kwa kukusanya mapato ya shilingi bilioni 9 tofauti na makadirio yaliyopangwa awali ya kukusanya shilingi bilioni 8

Ameongeza kuwa wamefanikisha ujenzi wa minara 60 ambayo imekamilika na kutangaza zabuni za kupeleka mawasiliano mipakani katika kata 190 na halmashauri 10 kwa kuwa zinahamia majengo mapya ili wapate huduma za mawasiliano


Share:

Waziri Ummy Atoa Siku 7 Kwa Vyombo Vya Usalama Kuchunguza Vifo Vya Wanafunzi Watatu Mpwapwa


Nteghenjwa Hosseah, Mpwapwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu ametoa siku 7 kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kuchunguza vifo vya wanafunzi 3 waliofariki kwa kufunikwa na kifusi katika Shule ya Msingi Mbori, Kata ya Motondo Wilayani Mpwapwa.

Wakati huo huo Mhe. Ummy amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuwaondoa Walimu wote wa shule ya Msingi Mbori kupisha uchunguzi unaondelea.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo wakati aliposhiriki kuaga Miili ya wanafunzi 3 waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na Mchanga katika shule ya Msingi Mbori tarehe 27.07.2021.

Akiwa shuleni hapo Waziri Ummy amelaani vikali Vitendo vya Walimu kuwafanyisha kazi siziso stahili za wanafunzi tofauti na ilivyoelekezwa kwenye Waraka wa Elimu bila Malipo No. 3 wa Mwaka 2016.

Amesema “ Hatukatazi mwanafunzi kufanya kazi zinazomjenga kama vile Stadi za kazi lakini sio kumfanya mwanafunzi kama Kibarua unawezaje kumwambia mtoto akachimbe mchanga wa kujengea au akaponde kokoto tena bila Uangalizi wa Walimu “ Alihoji

Katika Shule ya Msingi Mbori tumeleta sh. Mil.12 kwa ajili ya Ujenzi wa Choo na fedha za mchanga zimejumlishwa humo inakuwaje walimu watume watoto kwenda kuchimba mchanga wa mtoni,  kuna uzembe hapa umefanyika na tutachukua hatua.

Pia Waqziri Ummy aliwataka Wakuu wa shule zote Nchini na walimu wa ujumla kuacha kuwatumikisha wanafunzi wawapo shuleni na wazingatie Waraka wa Elimu bila Malipo no 3. wa mwaka 2016 ambao unatoa ufafanuzi wa kina wa jukumu la kila mdau wa Elimu.

“Jukumu la Ujenzi wa Miundombinu ya shule ni la Wazazi pamoja na Jamii inayozunguka na sio wanafunzi, Walimu na Kamati za shule mnatakiwa kuhamaisha Wazazi na jamii kujitolea kujenga miundombinu hiyo na sio kutumikisha wanafunzi” alisistiza Waziri Ummy.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe.Josephat Maganga  amesema watoto waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na kifusi shuleni hapo ni watatu ambao ni Isaya Lucas Hamis, Rehema Alex na Daud Enock Mchea na watoto wengine watano walijeruhiwa wametibiwa na kuruhusiwa kurejea majumbani kwao.

Tukio la Watoto kufukiwa na kifusi lilitokea Tarehe 27.07.2021 katika Shule ya Msingi Mbori iliyopo Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa baada ya watoto hao kupewa kazi na walimu wao kuchimba mchanga kwa ajili ya ujenzi wa choo unaondelea shuleni hapo.


Share:

TCRA YASHIRIKI MBIO ZA MWENGE MAALUM 2021 IPAGALA JIJINI DODOMA

Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mabel Masasi akiwapa maelezo viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru ulipowasili katika Shule ya Msingi Ipangala 'B' iliyopo jijini Dodoma wakati wa mbio za Mwenge Maalum 2020/21 ikiwa ni ishara ya TCRA kuunga mkono kauli mbiu ya mbio hizo isemayo "TEHAMA ni msingi wa wa Taifa endelevu; itumike kwa usahihi na uwajibikaji"
Afisa Habari wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Robin Ulikaye akiwapa elimu wanafunzi wa shule ya msingi Ipagala B Wakati TCRA ikiwa katika ushiriki wa kutoa elimu katika mbio za Mwenge wa Uhuru jijini Dodoma.
Afisa Mwandamizi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)Mabel Masasi akikabidhi kitabu cha Mwongozo wa Huduma kwa Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Tanzania kwa viongozi wa Mbio za Mwenge Maalum 2020/21 ikiwa ni ishara ya TCRA kuunga mkono kauli mbiu ya mbio za mwenge mwaka huu isemayo "TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu; itumike kwa usahihi na uwajibikaji"
Baadhi ya viongozi wakipata huduma za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Wakati Mwenge wa Uhuru ulipokwenda katika Shule ya Msingi ya Ipagala B jijini Dodoma.
Share:

Lead Generator Agency Kahama Branch at NBC

Lead Generator Agency Kahama Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line […]

This post Lead Generator Agency Kahama Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lead Generator Agency Musoma Branch at NBC

Lead Generator Agency Musoma Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line […]

This post Lead Generator Agency Musoma Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Board Member Vacancy at TOL Gases Limited

BOARD MEMBER VACANCY TOL Gases Limited is the leading manufacturer and distributor of Industrial and Medical Gases. Additionally the Company distributes high quality brands of welding and related consumables as well as medical oxygen related appliances within Tanzania and the neighbouring countries through distributorship arrangements. The Company was established in the 1950’s and has been […]

This post Board Member Vacancy at TOL Gases Limited has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

OFA! Viwanja vilivyopimwa vinauzwa Mbezi- Kwembe Kwa Bei Nzuri Kabisa


Ofa! Ofa! Viwanja vilivyopimwa vinauzwa Mbezi- Kwembe- Nyuma ya ofisi za halmashauri ya Ubungo, kituo cha Luguruni. Ukubwa ni kuanzia Sqm 400 Bei sqm 1 =17,500/= (7,000,000/=). 
 
Malipo ndani ya miezi sita. Kianzio 25% ya bei ya kiwanja. Eneo ni zuri lina Umeme, maji na kuna watu wa kutosha
0659 972868
0759 461893


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JULAI 29,2021









Share:

CHANJO YA CORONA YAMUIBUA MGEJA..AMPONGEZA RAIS SAMIA KURUHUSU WATANZANIA KUCHANJWA,WANAOPOTOSHA WAKAE KIMYA



Mwenyekiti wa Taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation ya Mjini Kahama mkoani Shinyanga, Khamis Mgeja akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jana ofisini kwake muda mfupi baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzindua chanjo ya kinga ya ugonjwa wa Covid 19 (Picha na Suleiman Abeid)

**
Na Suleiman Abeid,TimesMajira Online,Shinyanga

TAASISI ya Tanzania Mzalendo Foundation yenye Makao Makuu yake wilayani Kahama mkoani Shinyanga imempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa busara wa kuruhusu watanzania kupatiwa chanjo ya kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Covid 19.

Pongezi hizo zimetolewa jana na Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi hiyo, Khamis Mgeja katika maongezi yake na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kahama muda mfupi baada ya Rais Samia kuzindua rasmi chanjo Covid 19.

Mgeja amesema kitendo cha Rais Samia kinastahili kupongezwa na kila mtanzania mwenye mapenzi mema na nchi yake na kwamba hatua hiyo itanusuru maisha ya watanzania wengi watakaokubali kuchanjwa chanjo hiyo japokuwa wapo wachache wanaopingana na msimamo huo wa Serikali.

“Nichukue fursa hii kumpongeza Rais Samia kwa uamuzi wa kuruhusu chanjo ya kinga ya Corona kuingizwa hapa nchini, na ameonesha njia kwa yeye mwenyewe kuanza kuchanjwa chanjo hiyo na ameifanya nchi yetu iwe miongoni mwa mataifa mengine duniani yanayowajari wananchi wake,”

“Pia nawapongeza wadau wengine wote walioungana na Rais wetu ikiwemo viongozi wa madhehebu ya kidini katika kujitokeza kuchanja chanjo hii, hili suala linagusa hatima ya maisha yetu, kila anayejisikia ni muhimu akachanjwa maana Rais kaisha onesha njia,” ameeleza Mgeja.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo ambaye pia amewahi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Shinyanga ametoa wito kwa watanzania ambao bado wanatoa maneno ya upotoshaji kuhusiana na chanjo hiyo ya kinga ya Covid 19 wakidai haifai na ina madhara.

Amefafanua kuwa ni vyema watu wanaotaka kupotosha ukweli wakakaa kimya badala ya kuendelea kuwapotosha watu kwa maneno yasiyokuwa ya kitaalamu ambapo ameiomba Serikali iharakishe kusambaza chanjo hiyo katika mikoa yote nchini ili watu waweze kuchanjwa.

“Jambo hili ni la hiari basi, hawa wanaotaka kupotosha tunawaomba wakae kimya, suala hili ni la kihiari, ni muhimu watu waendelee kushauriwa wajitokeze kuchanjwa, na sisi huku mikoani tunasubiri chanjo hii ifike haraka mikoani na mawilayani ili watu waweze kuchanjwa,”

“Hawa wanaopinga ni vyema sasa wakatupa mbadala wa kitaalamu tutumie njia gani katika kujikinga na ugonjwa huu, na jambo hili ni la hatari kuona watu wasiokuwa na utaalamu wa kidaktari ndiyo wanaosimama kidete kupinga, na watuoneshe kwa vigezo kwa nini chanjo hii haifai,” ameeleza.

Vilevile amewataka watu hao wanaoupinga msimamo wa Serikali wakaacha mambo ya kitaalamu yasemewe na watu wenye utaalamu wa masuala ya kiafya, suala la kitaalamu lisiingizwe kwenye siasa na wanasiasa waachiwe wafanye kazi zao za kisiasa.

Mgeja ameonesha kushangazwa na kitendo cha wanasiasa kuingilia masuala ya kitaalamu kwa kuukataa ukweli na kuupinga ambapo amehoji ni vipi upande wa wataalamu hawaingilii masuala ya kisiasa ambapo alisema upotoshaji wao unaweza kuliingiza Taifa la Tanzania katika matatizo makubwa.

“Vilevile nichukue fursa hii kuwapongeza viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama hapa nchini na viongozi wote wa kidini na wale wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa jinsi walivyoonesha msimamo mzuri katika kuunga mkono maamuzi ya Serikali kuhusiana na janga la ugonjwa wa Covid 19,”

“Niwaombe tu watanzania hivi sasa tupo kwenye janga zito na tukifanya mizaha tunaweza kuteketeza maelfu ya watanzania kwa jambo ambalo linaweza kuzuilika mapema kabla halijatuletea madhara makubwa, wakumbuke ule usemi wa “….Akili za kuambiwa changanya na za kwako, watauona ukweli na msimamo wa Rais Samia,” ameeleza Mgeja.

Rais Samia Suluhu Hassan jana amezindua rasmi chanjo ya kujikinga na ugonjwa wa Covid 19 ambapo alisema japokuwa wapo baadhi ya watanzania wanaopinga chanjo hiyo lakini wengi wao wanaunga mkono na kwamba Serikali itahakikisha wale wote wanaotaka kuchanjwa wanachanjwa.
Share:

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE ATETA NA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA MADOLA MJINI LONDON UINGEREZA

Mhe. Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Mhe Patricia Scotland mjini London, Uingereza. Rais Mstaafu kama Mwenyekiti Mteule wa Bodi ya Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE) yupo huko kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi kwa ajili ya kuchangia Elimu utakaofanyika tarehe 28-29 Julai,2021.

Share:

ZU YAENDELEA KUNG'ARA MAONYESHO YA (TCU)



Chuo kikuu Cha Zanzibar, ZANZIBAR UNIVERISTY (ZU) Cha Tanzania visiwani kimeendelea kung'ara kwenye maonyesho ya kumi na sita (16) yanayoandaliwa na tume ya vyuo vikuu Tanzania.

Dr .Salama Yusuf ambaye ni muadhili Mkuu wa chuo hicho wakati wa mazungumzo yake  leo Julai 28,2021  amesema wanawakaribisha wanafunzi mbalimbali na wa jinsia zote kufika chuoni kwao.

Amesema kwenye maonyesho hayo wanafanya udahili na inakuwa rahisi kwa mzazi au mwanafunzi kufanyiwa udahili kwenye banda lao..

Aidha Dr. Salama aliwashauri waandaaji wa Maonyesho hayo kuyaboresha zaidi kwa sababu ni msaada mkubwa kwa wazazi ama wanafunzi,

Alisema pia (ZU)ni chuo kizuri chenye walimu wazuri na mwanafunzi akimaliza chuoni hapo anakuwa mbobezi wa suala ambalo alilisomea.

Aidha Alisema kutokana na wimbi la tatu (3)la Uviko-19 Zanzibar University inakabiliana sana kwani kuna sehemu maalumu yenye maji tiririka na sabuni

Alisema wanapokuwa sarasani wanawaweka anafunzi kwa umbali kidogo na hata mwalimu anahakikisha wanafunzi wote wamevaa barakoa
Share:

NABII JOSHUA: ACHENI KUPINGA CHANJO, RAIS SAMIA SONGA MBELE



Nabii Dkt.Joshua Aram Mwantyala


Na Mwandishi Wetu, Kihonda

KIONGOZI Mkuu wa Huduma ya Sauti ya Uponyaji Tanzania, Nabii Dkt.Joshua Aram Mwantyala amewataka viongozi wa kisiasa na kidini kuacha kutumia ushawishi walio nao katika jamii kuipinga chanjo ya virusi vya corona.

"Nampongeza sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa hekima yake ya kuruhusu chanjo ije nchini kwa ajili ya ustawi wa afya za wananchi wetu wa Tanzania;

Wito huo ameutoa muda mfupi baada ya maombi ya kuliombea Taifa ambayo alikuwa anayafanya maalum Yespa, Kihond mjini Morogoro ili Mungu aweze kuiponya Tanzania na watu wake huku akisisitiza kuwa, licha ya maombi pia ni jukumu la kila mmoja kuzingatia miongozo na kanuni zinazotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Afya ili kukabiliana na Corona.

"Ushauri wangu kwa viongozi wa kijamii hasa viongozi wa dini tusitumie ushawishi tulio nao miongoni mwa jamii yetu kupinga suala la chanjo, hilo ni jambo ambalo linaweza kuligawa Taifa na kulifanya lisitawalike na jambo ambalo si nzuri kwa kuwa linawazoeza watu kupingana na maamuzi ya mamlaka za nchi.

"Tabia hii ya viongozi wa dini kuipinga Serikali hadharani wakati tunayo fursa ya kuishauri Serikali bila vipaza sauti kwa hakika inatengeneza watu wenye kiburi wasiotii viongozi wa nchi na kutokutii mamlaka maandiko yanasema ni uasi na huko ni kugombana na Mungu,"alifafanua Nabii Dkt.Joshua.

Pia aliwaomba wananchi wasiogope juu ya chanjo, "Serikali yetu ipo makini sana na inaongozwa na Mungu, kamwe haiwezi kuwaangamiza watu wake. Mwisho namuomba Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aendelee kuwaa hodari na moyo wa ushujaa, asiyumbe anapoyumbishwa sisi wananchi na kanisa tunamuombea sana na tupo pamoja na serikali yake.

"Mimi binafsi ninamwahidi kuwa nitazunguka nchi nzima kwa gharama zangu kuisaidia Serikali kutoa elimu kwa wananchi ili waokoe afya zao dhidi ya Corona kwa njia ya chanjo,"alisema Nabii Dkt.Joshua.

Wito huo ameutoa ikiwa leo Julai 28, 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiongozana na viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali wamezindua rasmi chanjo ya corona nchini.

Uzinduzi huo umefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo Rais Samia Suluhu Hassan amesema chanjo hiyo ni salama na asingekuwa tayari kuhatarisha maisha yake kwa kuchanjwa chanjo ya Corona kama ingekuwa si salama.

Hatua hiyo inakuja baada ya wiki iliyopita Tanzania kupokea zaidi ya dozi milioni 1.05 za chanjo aina ya Johnson & Johnson zilizotolewa na Marekani kupitia mpango wa upatikanaji wa chanjo wa Covax.

Katika mpango huo, wapo baadhi ya watu wanaopingana na harakati hizo wakieleza chanjo hizo sio salama na wapo wanaounga mkono, lakini kiongozi huyo mkuu wa nchi amewaondoa hofu wananchi kuhusiana na hilo.

Rais Samia alisema yeye ni mama wa watoto wanne, ni bibi wa wajukuu kadhaa wanaompenda sana na yeye kuwapenda, ni mke pia lakini mbali ya yote ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi wa nchi hii.

“Nategemewa kama mama, kama bibi, kama Rais, kama Amiri Jeshi Mkuu, nisingejitoa mwenyewe nikajipeleka kwenye kifo, nikajipeleka kwenye hatari nikijua kwamba nina majukumu yote haya yananitegemea .

“Lakini nimetoka kuonyesha umma wanaonifuata nyuma nikijua kama Rais ni mchungaji na nina watu wengi nyuma nawachunga na wananitazama mimi hivyo nisingetoka kujihatarisha,”amesema Rais Samia.

Rais amebainisha kuwa amekubali kwa hiari yake kuchanja akijua kwamba ndani ya mwili wake ana chanjo kadhaa ambazo ameishi nazo kwa miaka 61 sasa kwani tangu amezaliwa kuna chanjo mbalimbali wamekuwa wakichanjwa, mbali na zingine wanazochanjwa njiani wakiwa wanasafiri ikiwemo ya homa ya manjano.

Hivyo kwake haoni hatari iliyoko na baada ya wanasayansi kujirishisha hivyo yupo tayari kuchanja na kuwa kuwaomba Watanzania wapuuze yote wanayoyasikia kuhusiana na chanjo hiyo.

“Kwa wale ambao koo zao hazijaguswa, hawajapata madhara ya maradhi haya wanaweza kusema wanavyotaka. Lakini nenda leo Moshi, nenda Arusha ,nenda Kagera, hata Dar es Salaam uonane na zile koo ambazo zimeshaguswa na haya maradhi wana maneno ya kukuambia na kama wangeweza leo wote wangekuwa hapa kutaka kuchanja kuepukana na ile hasara walioipata,"alisema.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger