Wednesday, 8 April 2020
Chief of Party, Sub-Saharan Africa, Tanzania Development Alternatives, Inc. (DAI)
DAI is an international development company. For more than 45 years, we have worked on the frontlines of international development, tackling fundamental social and economic development problems caused by inefficient markets, ineffective governance, and instability. Currently, DAI is delivering results that matter in some 80 countries. Our development solutions turn ideas into impact by bringing together fresh combinations… Read More »
The post Chief of Party, Sub-Saharan Africa, Tanzania Development Alternatives, Inc. (DAI) appeared first on Udahiliportal.com.
Livelihood Officer Job Opportunity at Save The Children – Morogoro Tanzania
Livelihood Officer Job Opportunity at Save The Children – Morogoro Tanzania Job Description Livelihood Officer- Morogoro – (2000024M) TITLE: Livelihood Officer- Morogoro TEAM/PROGRAM: Programme Operations LOCATION: Morogoro GRADE: 4 POST TYPE : NATIONAL CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more) or… Read More »
The post Livelihood Officer Job Opportunity at Save The Children – Morogoro Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
DC WA SINGIDA AJA NA OPERESHENI TOKOMEZA CORONA
Na John Mapepele ,Singida
Mkuu wa Wilaya ya Singida Injinia Paskasi Damian Muragili amefanya Operesheni Maalum kwenye maeneo mbalimbali ya Mji wa Singida kutoa elimu na kuona jinsi wananchi walivyotekeleza maelekezo ya Serikali kuhusu ya kujikinga na ugonjwa unaoambukizwa na Virusi vya Corona (Covid 19).
Licha ya kutoa elimu hiyo pia amewapiga faini za hapo hapo watu waliobainika kukiuka maagizo huku akisisitiza kuwa Serikali itawanyang’anya lesseni za biashara na kufunga biashara hizo wote ambao wataendelea kukaidi maelekezo hayo
Mhandisi Muragili amefanya Operesheni hiyo maalum akiwa na Kikosi Kazi cha wataalam mbalimbali kwenye Wilaya yake ambapo ilianza alfaji hadi usiku wa kuamkia leo ambapo alitembelea maeneo yote ya huduma katika Mji wa Singida iliyojumuisha maeneo ya Standi Kuu ya Mkoa wa Singida ya Misuna, Soko Kuu la Singida na maeneo ya biashara ya Bajaji.
Akiwa katika Soko Kuu la Singida, Mkuu wa Wilaya alifanikiwa kukuta maduka ya nguo ya Kikundi cha Ushonaji cha Singida yakiwa hayana vitakasa mikono lakini wauzaji walikuwa wakiendelea na shughuli za biashara na kuwatoza faini ya shilingi elfu 50 papo hapo.
Akilipa faini hiyo baada ya kukiri kosa hilo, Mwenyekiti wa kikundi hicho ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Soko Kuu Singida Amina Msaghaa aliomba samahani kwa Mkuu wa Wilaya na kuahidi kutoendelea kufanya kosa hilo na kwamba faini hiyo imekuwa fundisho kwao na kwa hiyo wao kama kikundi watakuwa mfano wa kuwafundisha wafanyabiashara wengini
“Mhe. Mkuu wa Wilaya naomba kukueleza kuwa tumetoa faini hii kwa masikitiko makubwa, lakini hii inatupa ujasiri wa kushirikiana na Serikali yetu kuhamasisha kuhusu kujikinga na ugonjwa huu, naahidi tutakuwa walimu wazuri” alisitiza Msaghaa
Mwenyekiti wa Waendesha Bajaji Mkoa wa Singida Hemed Juma amesema katika kupambana na ugonjwa wa Corona chama chao kimechukua tahadhari zote zinazoelekezwa na Serikali kuhusu ugonjwa huu na kwamba yoyote atakayekaidi atashughulikiwa kikamilifu na chama chao ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kwenye Vyombo vya Sheria.
Akifanya ukaguzi kwenye mabasi yanayoingia na kutoka kwenye Stendi Kuu Mkuu wa Wilaya amesema abiria wanatakiwa kutumia vitakasa mikono wanapoingia na kutoka kwenye mabasi hayo kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa huu
Aidha amesema Operesheni hiyo imeanza na itakuwa endelevu na ya kushitukiza kila wakati hadi ugonjwa huu utakapoisha.
Amewataka kila mwananchi wa Wilaya ya Singida kuwa mzalendo kwa kuzingingatia maelekezo ya Wizara ya Afya ya kujikinga na ugonjwa huu kwa kujitenga na kuchukua hatua zinazotakiwa ili kujilinda na kuwalinda wengine na kwamba wanapohisi kuwa kuna mgeni ambaye ameingia na hajapimwa watoe taarifa kwenye Mamlaka zilizo katika maeneo yao
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi katika siku za hivi karibuni ameanza ziara maalum ya kuhamasisha wananchi wa mkoa wake kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa huu kwa kufuata taratibu zote zinazotolewa na wataalam wa afya za kudhibiti na kujikinga na ugonjwa, wa Covid-19, kumwomba Mungu na kuendelea kuchapa kazi ili kunusuru kupoteza maisha na kushuka kwa uchumi wa nchi yao
Akiwa kwenye Soko maarufu la viazi lishe kwenye Kitongoji cha Kideka katika Kijiji cha Nkunikana aliwapongeza wafanyabiashara hao kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 kwa kuandaa miundombinu ya maji ili kunawa mikono kwa sabuni katika maji yanayotiririka wakati wote.
Aidha aliwataka wakulima wa viazi lishe kuendelea kulima kwa bidii ili wananchi wapate lishe bora kutokana na viazi hivyo na majani yake ambapo alisisitiza kuwa katika kipindi hiki ni muhimu kusanitaizi mikono na kusanitaizi afya zao
“Naelekeza wakulima waache visingizio nao waendelee kwenda mashambani kujitenga na kulima kwa bidii katika kipindi hiki ili waweze kupata mazao mengi na wakati huo huo watekeleze matakwa ya Serikali ya kujitenga na mikusanyiko isiyo ya lazima ambayo ingeweza kusababishia maambukizi endapo mmoja ana maambukizi.”
Wadau Wamkabidhi Waziri Mkuu Sh. Bil 6.226 Kukabili Corona
Baada ya kupokea kupokea msaada huo, Waziri Mkuu amewashukuru wadau hao kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, ambapo hadi sasa kesi 24 zimeripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huo nchini na wagonjwa watano wamepona.
Waziri Mkuu amepokea msaada huo leo (Jumatano, Aprili 8, 2020) katika Ofisi Waziri Mkuu Mlimwa, jijini Dodoma. Amewataka Watanzania waendelee kushirikiana na Serikali katika kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo.
Amesema hadi sasa jumla ya watu 396 wapo kwenye karatini katika maeneo mbalimbali yaliyotengwa wakiwemo wageni wanaoingia nchini ambao wanafuatiliwa afya zao na baada ya siku 14 kama watakuwa hawana maambukizi wataruhusiwa kuungana na familia zao.
Waziri Mkuu amesema Serikali kwa upande wake imeendelea kuchukua mbalimbali katika kupambana na ugonjwa wa COVID-19 na kwa sasa imejiimarisha kwenye utoaji wa elimu kwa wananchi juu ya namna ya kujikinga na virusi vya corona.
“Serikali inatoa misitizo kwa wananchi wazingatie maelekezo yanayotolewa kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ikiwemo kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka pamoja na kujiepusha na mikusanyiko isiyokuwa ya lazima.”
Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka wakazi wa mkoa wa Dar es Salaam waendelee kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo ili kuzuia usisambae kwa sababu hadi sasa mkoa huo unaongoza kwa kuwa na wagonjwa zaidi wa corona nchini.
Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuvishukuru vyombo vya habari nchini kwa ushirikiano wanaoutoa katika kuelimisha umma namna ya kujikinga na virusi vya corona pamoja na wasanii waliotunga nyimbo za kuuelimisha umma namna ya kujikinga na ugonjwa huo.
Miongoni mwa wadau waliotoa msaada huo ni kampuni ya Madini ya Twiga iliyotoa sh. bilioni nne, mfanyabiashara maarufu nchini Rostam Aziz ametoa sh. bilioni moja, kampuni ya Taifa Gesi imetoa sh. milioni 100 na kampuni ya mafuta ya Puma imetoa msaada wa mafuta lita 50,000 zitakazotumika katika magari yanayotoa huduma za kupambana na corona nchini yakiwemo magari ya kubebea wagonjwa.
Wengine ni kampuni ya TEHAMA ya Huawei imetoa vifaa kuendeshea mikutano kwa njia ya video ambavyo ni cloudlink camera tatu, Cloudlink Mic tatu, Cloudlink TV terminal tatu, Cloudlink Platform pamoja na Thermal Imaging Temperature Measuring System moja vyote vikiwa na thamani ya sh. milioni 940, Asasi za Kiraia (AZAKI) zimetoa sh. milioni 79.
Baada ya kupokea misaada hiyo, Waziri Mkuu kwa niaba ya Rais Dkt. Magufuli aliwashukuru wadau hao kwa vitu mbalimbali walivyovitoa kwa ajili ya kupambana na COVID-19 kwani vifaa pamoja na fedha walizozitoa zitaisadia Serikali katika kukabiliana na ugonjwa huo.
Kuhusu wadau wengine wanaohitaji kutoa misaada, Waziri Mkuu amesema ofisi yake iko wazi pia wanaweza kupeleka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kwa walio nje ya nchi au sehemu yoyote wanaweza kutuma fedha kupitia akaunti Na: 9921159801 yenye jina la National Relief Fund Electronic.
Awali, mfanyabiashara maarufu nchini, Rostam Azizi alisema ametoa sh. bilioni moja ambayo ameielekeza katika kununua vitakasa mikono ambavyo vitatumiwa na wasafiri wa daladala wa Dar es Salaam na Zanzibar ili waweze kutumia kabla ya kupanda usafiri huo, hivyo kuweza kujikinga.
Pia, Mfanyabiashara huyo ametumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. John Magufuli kwa kuwaongoza Watanzania kwa hekima na busara na kuwaepusha na taharuki kama ilivyotokea katika mataifa mengine. Amempongeza Waziri Mkuu na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa namna wanavyoshiriki katika kukabiliana na corona.
(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
Serikali Yaipa Mwezi Mmoja Benchmark Kumlipa Mshindi wa BSS 2019
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe.Juliana Shonza ametoa mwezi mmoja kuanzia Aprili 08, 2020 kwa Kampuni ya Benchmark Production inayoendesha mashindano ya Bongo Star Search chini ya Mkurugenzi wake Madam Ritha Paulsen kumlipa kiasi cha Shilingi milioni 50 mshindi wa kwanza wa mashindano hayo kwa mwaka 2019, Bw.Meshack Fukuta.
Naibu Waziri ametoa maelekezo hayo leo Jijini Dodoma baada ya kupokea barua kutoka kwa familia ya mshindi huyo iliyoeleza kutokutekelezwa kwa ahadi hiyo kwa takriban miezi minne sasa ilioanisha utaratibu wa malipo hayo kuwa milioni 30 ni kwa ajili kutengeneza kazi za muziki na matangazo kwa kipindi cha mwaka mmoja na milioni 20 ni ya kukabidhiwa mkononi ambapo Mhe. Naibu Waziri amesisitiza makubaliano yote yalioanishwa kufanyiwa kazi.
“Mimi kama mlezi wa tasnia ya Sanaa ambaye pia nilikua mgeni rasmi siku ya fainali nimesikitishwa sana na malalamiko haya, hivyo naitaka kampuni ya Benchmark kutekeleza ahadi hiyo na wasipofanya hivyo ndani ya muda huo, Serikali haitasita kufungia mashindano hayo”, alisema Mhe.Shonza.
Mhe. Naibu Waziri ameongeza kuwa Wizara iliwasiliana na uongozi wa Benchmark kuhusu malalamiko hayo mbapo Kampuni hiyo ilieleza kuwa imeshindwa kumlipa msanii huyo kutokana na viongozi wa Kampuni iliyodhamini shindano hilo ya Startimes kuwepo nchini China na kushindwa kusafiri kuja nchini kutokana na uwepo wa ugonjwa wa Corona.
Hata hivyo Mhe.Naibu Waziri ameleeza kuwa Wizara iliwasiliana na uongozi wa Startimes ambao umekiri kuwa umeshalipa fedha kwa Kampuni ya Benchmark tangu mwezi Januari 2020.
Aidha, Mhe.Shonza ameitaka kampuni hiyo kuhakikisha inamtengenezea msanii huyo wimbo bora pamoja na kuufanyia matangazo ya kutosha katika kipindi cha miezi miwili kuanzia leo pamoja na kuwasilisha nakala ya mkataba wa washiriki waliofikia hatua ya kumi bora ndani ya wiki moja kuanzia leo machi 08,2020.
Katia hatua nyingine Mhe.Shonza ameliagiza Baraza la Sanaa na Taifa (BASATA) kusimamia utaratibu wa uaandaji wa mashindano mbalimbali ikiwemo kuwepo kwa mikataba kati ya wasanii na wanaondesha mashindano au shughuli yoyote ya sanaa na wasanii pamoja na kuhakikisha ahadi wanazopewa washindi ikiwemo zawadi zinakuwepo na zinakabidhiwa kwa wahusika mara baada ya mashindano.
Kwa upande wake Bw.Meshack Fukuta mshindi wa shindano hilo kwa mwaka 2019 ameishukuru Serikali kwa namna ambavyo imechukua hatua katika malalamiko yake ambapo ameahidi kufanya juhudi katika Sanaa yake ili kuitangaza nchi vizuri ndani na nje ya nchi pamoja na kujipatia kipato kupitia kipaji hicho.
Serikali Na Wadau Waja Na Elimu Juu Ya Corona Kwa Watoto
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa kushirikiana na Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN), Taasisi ya Chakula na Lishe, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Watoto (UNICEF) wameandaa mkakati wa kufikisha ujumbe kwa watoto kuhusu kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona.
Akizungumza leo katika kikao kazi kilichowakutanisha wadau hao jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania (TECDEN) Bruno Ghumpi amesema kumekuwepo na ujumbe mbalimbali katika kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona ila kumekosekana ujumbe maalum unaolenga makundi maaalum ikiwemo wanawake wajawazito na watoto wadogo kuanzia miaka 0 hadi minane.
Ameongeza kuwa kuwepo kwa elimu sahihi kwa watoto hao kuhusu ugonjwa wa COVID 19 itawasaidia wazazi au walezi na watoto wenyewe kupata taarifa zitakaziwasaidia kujikinga na Virusi hivyo ili kupunguza au kuondokana na maambukizi ya Virusi hivyo katika maeneo yao.
“Ujumbe huu kwa watoto ni muhimu sana kwani kundi hili kwa sasa lipo nyumbani kutokana na kufungwa kwa shule hivyo ni vizuri wazazi na walezi wakazingatia masuala muhimu ya kuwafundisha watoto wao kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona” amesema
Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bw. Mathias Haule amesema kuwa ni muhimu kwa wadau kuhakikisha wanafikisha elimu katika ngazi ya chini kuanzia familia, kijiji/mtaa ili kuwezesha watu hao kupata taarifa na elimu sahihi juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.
“Elimu ifike katika ngazi ya familia hasa katika maeneo ya vijijini ambako bado elimu haijawafikia kwa kasi inayotakiwa ili kuondokana na maambukizi ya virusi vya Corona nchini.” Amesema
Mmiliki Jamii Forom ahukumiwa kwenda jela au alipe faini Milioni 3
Pia Mahakama hiyo, imemuachia huru mshitakiwa mwenzake Mickie Mushi baada ya kutotiwa hatiani katika makosa yao.
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo upande wa utetezi umedai kuwa utakata rufaa kupinga adhabu hiyo.
Melo yupo chumba cha mahabusu kusubiri kulipa faini hiyo ama akishindwa atumikie kifungo cha mwaka mmoja.
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuzuia Polisi kufanya uchunguzi kinyume na kifungu cha 22 (2) cha Sheria ya Makosa ya Mtandano namba 14 ya mwaka 2015.
Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kati ya Aprili Mosi, 2016 na Desemba 13, 2016 katika maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni.
LUKUVI AAGIZA KUFANYIKA UHAKIKI WA KINA UTEKELEZAJI MAAMUZI YA KUTOONDOLEWA VIJIJI 920
Trump aionya India kuhusu kusitisha mauzo ya Hydoxy-chloroquine....Asema Atalipa Kisasi
Taarifa Kwa Umma Kufuatia Kuondolewa Karantini (LockDown) Katika Mji Wa Wuhan Vilikoanzia Virusi Vya Corona
Taarifa Kwa Umma Toka Baraza la Mitihani Tanzania-NECTA
Baraza linapenda kuwajulisha kwamba ratiba ya Mtihani wa Kidato cha Sita 2020 inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Mtihani wa Kidato cha Sita umpangwa kufanyika kuanzia tarehe 9/10/2020 hadi 23/10/2020 ni ya Uongo. Hadi sasa ratiba ya mtihani huo bado haijatoka.— Necta Tanzania (@NectaTz) April 7, 2020
Wasio Chukua Tahadhari Ya Corona Songwe Kutozwa Faini
Mkuu wa Wilaya ya Songwe Samuel Jeremia Opulukwa amebainisha hayo jana mara baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Songwe kufanya ukaguzi wa utayari wa kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Ugonjwa wa Corona katika Wilaya hiyo.
Opulukwa amesema, “Sasa tunaanza kutoza faini wote wasiofuata maelekezo ya wataalamu wa Afya kuhusiana na Corona, mfano tukipita dukani au sehemu ya biashara na hakuna maji na sabuni, tuta toza faini na kufunga kwa mda biashara hiyo mpaka mtu huyo azingatie maaelekezo hayo”.
Ameongeza kuwa lengo la Wilaya hiyo ni kuhakikisha kuwa mahali pa kufanyia biashara ni salama kwa wafanyabiashara na watumiaji wa huduma hizo huku akieleza kuwa wanawa fuatilia wageni wote wanao toka nje ya wilaya waliopo katika nyumba za kulala wageni na kuchukua maelezo yao kwa ajili ya tahadhari endapo wana dalili za Ugonjwa wa Virusi vya Corona.
Opulukwa ameongeza kuwa elimu inaendelea kutolewa kwa wananchi wote wa Wilaya ya Songwe hususani katika maeneo ya migodi ambapo kuna mikusanyiko ya watu wengi pia ameielekeza kamati inayohusika kutoa elimu ifanye ufuatiliaji wa kina endapo wananchi wanazingatia wanayo waelekeza.
Aidha amesema mara baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa kufanya ukaguzi wa utayari wa Wilaya hiyo katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Virusi vya Corona, Kamati hiyo imebaini baadhi ya mapungufu ambayo kama wilaya itasimamia kuyarekebisha.
Amefafanua kuwa yote yaliyoonekana kama mapungufu yapo ndani ya uwezo wa Wilaya ikiwa ni pamoja na kuhakikisha eneo la kuwatenga washukiwa wa Corona lina vitanda vya kutosha na kujenga kichomea taka katika Zahanati ya Saza ambayo itatumika kutibu wagonjwa wa Corona.
Naye Mganga Mkuu wa Wilaya ya Songwe Dkt Humphrey Masoke amesema wameshaagiza vifaa kinga na tiba vyote muhimu katika Bohari kuu ya Dawa ili kuongezea katika vifaa vichache walivyo navyo tayari.
Dkt. Masoke ameongeza kuwa wana endelea kutoa maelekezo na elimu kwa jamii juu ya tahadhari ya ugonjwa wa Virusi vya Corona kwakuwa bado baadhi ya wananchi wanaamini ugonjwa wa Corona ni wa wazungu hivyo hauwahusu.
Estin Nyangito Mkazi wa Mkwajuni Songwe amesema wamesha pewa elimu ya kuchukua tahadhari ya kujikinga na Virusi vya Corona na elimu hiyo wataisambaza kwa wananchi wengine ili nao waweze kuchukua tahadhari.
Kwa upande wake Jakson Mwampashi Mkazi wa Songwe amemuomba Mkuu wa Wilaya hiyo kuweka utaratibu wa kutoa elimu mara kwa mara na kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutumia magari ya matangazo ya barabarani ili wananchi wote waweze kupata elimu ya Corona
































