Tuesday, 7 April 2020

Mbowe Ashauri kuundwa kwa kikosi kazi cha Taifa kwa ajili ya kuangalia athari za uchumi zinazotokana na Ugonjwa wa Corona

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Bunge, Freeman Mbowe, ameshauri  kuundwa kwa kikosi kazi cha Taifa kwa ajili ya kuangalia athari za uchumi za ugonjwa huo.

Mbowe aliyasema hayo jana April 6, 2020  wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2020/21.
 
Alibainisha kuwa sekta ya utalii imeanguka kwa asilimia 99 na kwamba kuna makampuni yamefungwa huku mapato ya nchi yatapungua kwa asilimia 40 kwa miezi sita ijayo.

“Kumekuwa na kauli tofauti,mikusanyiko ambayo haifai na kwamba kuna mikusanyiko ambao wakuu wa mikoa ndio wamekuwa wakiifanya, wanakusanya watu, wanahutubia watu kwamba ugonjwa uko mbali hii ni hatari,”amesema.

Aliongeza “Ningetamani tumsikilize Rais, Waziri Mkuu na Waziri wa Afya kama nchi ikienda kwa kila kiongozi kutoa taarifa ugonjwa huu utawafikisha mahali pabaya.”

Alisema jambo hilo linahitaji kikosi cha Taifa kwa ajili ya kuangalia athari za uchumi na kijamii na pia kuangalia vipaumbe vya Taifa hivi sasa ni vipi.


Share:

Serikali kutoa vitabu Msingi, Sekondari kwa mtandao bure ili Wanafunzi Wajisomee Wakiwa Nyumbani

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Joyce Ndalichako amesema kwasasa serikali inatoa huduma ya upatikanaji wa vitabu vyote kuanzia shule za msingi na sekondari kwenye maktaba bila malipo yeyote kwa njia ya mtandao

“Tunatambua kwamba wanafunzi wapo nyumbani na wanahitaji kuendelea kupata elimu hata wakiwa nyumbani, tunayohuduma ya maktaba inayotolewa na Taasisi ya Elimu Tanzania ambayo kiutaratibu ili uweze kupata vitabu ilipaswa mtu kulipa, sasa serikali inatoa huduma ya upatikanaji wa vitabu vyote kuanzia shule za msingi na sekondari bila malipo yeyote,”amesema.

Amewataka wanafunzi kutumia muda wao kusoma vitabu ambavyo serikali imewapa fursa bila gharama yeyote badala ya kuzurura mitaani na kujiweka  kwenye hatari ya kupata maambukizi ya corona.


Share:

Trump na viongozi wengine duniani wamtakia ahueni Waziri Mkuu Uingereza Ambaye Yuko ICU Kwa Corona

Rais wa Marekani Donald  Trump ameungana na Viongozi wengine Duniani, kutoa pole kwa swahiba wake, Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson kutokana na kuugua corona. 

"....tumehuzunika kusikia ameingizwa ICU,Marekani inamuombea, tumewasiliana na Madaktari wake kuona kama tunaweza kusaidia"

Waziri Mkuu Johnson alipelekwa hospitali na kulazwa baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya kutokana na kuambukizwa Virusi vya Corona.

Kansela wa Ujerumani Angela merkel na rais wa Marekani Donald Trump ni miongoni mwa viongozi wa ulimwengu waliotuma salamu za kumtakia afya Waziri mkuu wa Uingereza.

Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen amemtumia salamu waziri mkuu Johnson na amemtakia kupona haraka.

Naye rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema anasimama pamoja na bwana Johnson, familia yake na watu wa Uingereza katika wakati huu mgumu.

Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO bwana Tedros Adhanom Ghebreyesus amemtumia kiongozi huyo wa Uingereza salamu za dhati wakati anapopambana na maambukizi ya virusi vya Corona.


Share:

Regional Manager Job opportunity at Save the children Tanzania – Dodoma

Regional Manager Job opportunity at Save the children Tanzania – Dodoma Regional Manager – Dodoma – (2000021O) TITLE: Regional Manager TEAM/PROGRAMME: Programme Operations LOCATION: Dodoma GRADE: 2 CONTRACT LENGTH: 1 year, renewable CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more) or intensively… Read More »

The post Regional Manager Job opportunity at Save the children Tanzania – Dodoma appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

System Administrator: Data Warehousing & Reporting Job vacancy at Vodacom Tanzania

System Administrator: Data Warehousing & Reporting Posting Country:  Tanzania, United Republic of Date Posted:  06-Apr-2020 Full Time / Part Time:  Full Time Contract Type:  Permanent Joining Vodacom is more than a job, what we do matters. We don’t just carry minutes, texts and data – we carry people’s lives. And that’s a huge responsibility. If you think for a minute about the… Read More »

The post System Administrator: Data Warehousing & Reporting Job vacancy at Vodacom Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MWANAFUNZI AFARIKI DUNIA KWA KUNASWA UMEME JUU YA MTI


Mwanafunzi wa darasa la saba Shule ya Msingi Mrunyigo, Kijiji cha Kiemba mkoani hapa, Calvin Eranga (14) , amefariki dunia baada ya kunaswa akiwa amepanda juu ya mti uliokuwa umegusana na nyaya za umeme.

Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme (Tanesco), Mkoa wa Mara, Meshak Laurent, akizungumzia tukio hilo alisema, mwanafunzi huyo alifikwa na mauti mwishoni mwa wiki baada ya kupanda juu ya mti ambao ulikuwa jirani na nguzo zenye nyaya za umeme.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa, elimu kwa wananchi ya kuchukua tahadhari na kulinda miundombinu inatolewa kwa umma, lakini shughuli za kibinadamu na uzalishaji zinaendelea kandokando ya njia za umeme licha ya tahadhari kutolewa mara kwa mara.

Alisema ni jukumu la jamii wakiwamo viongozi wa serikali na kijamii kushirikiana kuhifadhi miuondombinu ikiwamo ukataji miti iliyopadwa jirani na njia za umeme kutokana na kutoruhusiwa kuikata isipokuwa Tanesco. 

Baba mkubwa wa marehemu, Katekista Leo Ekingo, alisema mwanafunzi huyo alipanda katika mti wa mchongoma ambao ulikuwa unagusana na nyaya za umeme na kusababisha kifo chake.

“Miti ilikuwa inagusana na nyaya za umeme, kijana akiwa juu ya mti wa mchongoma akanaswa na akawa ananing’inia kwa muda kisha umeme ukamwachia akadondoka chini na kufariki dunia…,” alisema.

Ofisa wa Baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za nishati na maji (Ewura CCC), Mkoa wa Mara, Dennis Ndanu, alisema ofisi za baraza hilo limepata taarifa ya kifo cha mwanafunzi huyo na linafuatilia ili kuhakikisha haki na stahiki za muathirika zinapatikana kwa mujibu wa taratibu za kisheria.
Share:

WHO: AFRIKA HAITAKUWA UWANJA WA KUFANYIA MAJARIBIO CHANJO YA CORONA


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amekosoa vikali matamshi ya kibaguzi ya madaktari wawili wa Ufaransa waliopendekeza kufanyia majaribio chanjo ya corona barani Afrika.

Dakta Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema, "Afrika haiwezi na wala haitofanywa uwanja wa majaribio ya chanjo yoyote ya Covid-19. 

WHO itafuata kanuni zote na kufanya majaribio ya chanjo yoyote au matibabu duniani kote, bila kujali ni Ulaya, Afrika au pahala popote pale.

Matamshi ya madaktari hao waliyoyatoa kwenye mjadala wa runinga yamezua ghadhabu, na wametuhumiwa kwa kuwachukulia Waafrika kama "nguruwe wa kufanyiwa majaribio ya maabara".

Mkurugenzi Mkuu wa WHO ameonekana kuongea na ghadhabu kwenye kikao na waandishi wa habari mjini Geneva ameeleza bayana kuwa, matamshi ya wanasayansi hao wa Kifaransa katika karne hii ya 21 ni ya kibaguzi, ya kufedhehesha, na yanayoashiria mabaki ya fikra za kikoloni.

Viongozi wa nchi za Afrika wameendelea kukosoa matamshi ya madaktari hao wakubwa wa Ufaransa, Camille Locht na Jean-Paul Mira, ambao hivi karibuni katika kipindi cha runinga, walipendekeza kwa kejeli na dharau kufanyika majaribio hayo ya chanjo ya corona barani Afrika.

Siku chache zilizopita, wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo walikosoa vikali mpango huo wa kufanyia majaribio chanjo ya corona nchini humo ambao serikali ya Kinshasa imeafiki wakisisitiza kuwa, ni fedheha kwa serikali kuruhusu taifa hilo ligeuzwe 'panya wa maabara'.
Afrika hadi saa imeripoti kesi elfu 10 pekee

Hii ni baada ya Jean-Jacques Muyembe, Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Biolojia anayeongoza jopokazi la kupambana na janga la corona nchini DRC kusema kuwa, "tumeteuliwa kufanya majaribio haya. Chanjo hiyo itazalishwa Marekani, Canada au China. Utafika wakati fulani ambapo itashindikana kudhibiti virusi vya corona, njia pekee ya kuidhibiti ni chanjo. Chanjo ndiyo iliyotusaidia kudhibiti Ebola."

Pendekezo hilo la Wamagharibi la kuwageuza Waafrika 'panya wa maabara' linakuja katika hali ambayo, aghalabu ya makumi ya maelfu ya vifo na kesi zaidi ya milioni moja na laki tatu za ugonjwa wa Covid-19 (corona) zimeripotiwa katika nchi za Ulaya na Marekani.


Share:

Assistant Representative, Dodoma, Tanzania at UNFPA – United Nations Population Fund

Assistant Representative, Dodoma, Tanzania at UNFPA – United Nations Population Fund Job Description Job Title National Post: Assistant Representative, NOD, Dodoma, Tanzania Job ID 29096 Location East and Southern Africa Full/Part Time Full-Time Regular/Temporary Regular Rotation This post is non-rotational. Duty Station: Dodoma, Tanzania Closing Date: 14 April 2020 (5 pm, New York time) Duration: One Year (*)… Read More »

The post Assistant Representative, Dodoma, Tanzania at UNFPA – United Nations Population Fund appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

New Jobs at Public Service Recruitment Secretariat, April 2020

PRESIDENT’S OFFICE  PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT  Ref.No.EA.7/96/01/K/181 6th April, 2020  VACANCY ANNOUNCEMENT  On behalf of the Tanzania Smallholder Tea Development Agency (TSHTDA), Tanzania  Coffee Board (TCB) and the Institute of Judicial Administration Lushoto, President’s Office, Public Service Recruitment Secretariat invites qualified Tanzanians to fill 3 vacant posts mentioned below;-    GENERAL QUALIFICATIONS All applicants must be Citizens of Tanzania generally… Read More »

The post New Jobs at Public Service Recruitment Secretariat, April 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Logistics Associate(Dar Port warehouse) Job vacancy at The United Nations World Food Programme

Logistics Associate(Dar Port warehouse) Job vacancy at The United Nations World Food Programme WFP seeks candidates of the highest integrity and professionalism who share our humanitarian principles. Selection of staff is made on a competitive basis, and we are committed to promoting diversity and gender balance. ABOUT WFP The United Nations World Food Programme is the world’s largest… Read More »

The post Logistics Associate(Dar Port warehouse) Job vacancy at The United Nations World Food Programme appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Health and Nutrition Coordinator – Tanzania

Health and Nutrition Coordinator – Tanzania Tracking Code 659-566 Job Description PCI is a non-profit organization dedicated to preventing diseases, improving community health, and promoting sustainable development worldwide. With support from United States Department of Agriculture (USDA), PCI Tanzania will be implementing the final phase of Food for Education (FFE) programming in the Mara region (2017-2021). The goal of the… Read More »

The post Health and Nutrition Coordinator – Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Monitoring, Evaluation and Learning Officer at Danish Refugee Council (DRC)

Monitoring, Evaluation and Learning Officer, Tanzania, Kibondo, Tanzania at Danish Refugee Council (DRC) Monitoring, Evaluation and Learning Officer Danish Refugee Council – Tanzania MEL Officer Position Title:        Monitoring, Evaluation and Learning Officer Reporting to:        Quality Assurance Coordinator Duty Station:        Kibondo, Tanzania Area of Operation:    Nduta and Mtendeli camps Application due: 4/8/2020 Workplace: Kibondo Department/Country: Tanzania… Read More »

The post Monitoring, Evaluation and Learning Officer at Danish Refugee Council (DRC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

EDUCATION OFFICER (TANZANIA NATIONALS ONLY) Tanzania at Norwegian Refugee Council

NRC is looking for a qualified candidate to work as Education Officer base  at Nyarugusu,Kigoma. The purpose of  Education Officer  is responsible for implementation of the Education projects . All NRC  employees are expected to work in accordance with the organisation’s core values: dedication, innovation, inclusivity and accountability. These attitudes and believes shall guide our actions and relationships.… Read More »

The post EDUCATION OFFICER (TANZANIA NATIONALS ONLY) Tanzania at Norwegian Refugee Council appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Awards Management Specialist Job Opportunity at Plan International

The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected. Working together with children, young people, our supporters and partners, we… Read More »

The post Awards Management Specialist Job Opportunity at Plan International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

KARIBU NNIENET UNDERWEAR SHINYANGA MJINI KWA NGUO ZA NDANI

Share:

Mkandarasi Azuiwa Kutoka Nje Ya Mkoa Wa Songwe

Mkandarasi wa Mradi wa maji wa Iyula uliopo Wilaya ya Mbozi amezuiwa kutoka Nje ya Mkoa wa Songwe huku akiwekwa chini ya uangalizi wa jeshi la Polisi mpaka atakapo kamilisha vifaa na wataalamu watakaomalizia Mradi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela ametoa zuio hilo leo mara baada ya kutembelea Mradi wa maji wa Iyula ambao ulitarajiwa kukamilika tangu mwaka 2017 huku ukiwa na thamani ya shilingi bilioni tano.

Brig. Jen. Mwangela amesema mkandarasi huyo anatakiwa aweke vifaa vyote na wataalamu wote watakao muwezesha kukamilisha ujenzi wa mradi huo ndipo ataruhusiwa kutoka nje ya Mkoa wa Songwe.

Ameongeza kuwa mkandarasi huyo aliweka masharti ya kupewa fedha nyingi ambapo tayari ameshapewa sehemu ya fedha hizo lakini bado utendaji wake wa kazi umekuwa wa kusuasua huku wananchi wakiendelea kupata adha ya kukosa maji.

Meneja wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi na Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Songwe Mhandisi Charles Pambe amesema mradi wa Maji wa Iyula una gharimu shilingi bilioni tano na tayari Mkandarasi ameshapewa bilioni 2.2

Mhandisi Pambe amesema kutokana na kusuasua kwa mkandarasi huyo RUWASA wana angalia uwezekano wa kuujenga mradi huo wenyewe kwa kutumia Force Account.

Naye Mkandarasi wa Mradi wa maji wa Iyula kutoka STC Construction ya Dar es Salaam Alan Makame amesema kusuasua kwa mradi huo ni kutokana na kucheleweshewa malipo pamoja na RUWASA kutotembelea mradi huo.

Amesema ndani ya siku tatu atakuwa ameanza kazi ya kuweka baadhi ya mabomba katika mradi huo na kuwa baada ya wiki mbili atakuwa amekamilisha mradi huo.


Share:

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson Apelekwa ICU Baada ya Hali Kuwa Mbaya kwa Virusi vya Corona

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amepelekwa katika chumba cha kuhudumia wagonjwa mahututi ICU baada ya hali yake kiafya kuwa mbaya kwa siku kumi zaidi kwasababu ya ugonjwa wa virusi vya Corona, kwa mujibu wa msemaji katika makazi ya Waziri Mkuu.
 
Johnson amemuambia Waziri wa mambo ya nje Dominic Raab kuchukua usukani pale ambapo kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.

Waziri Boris ,mwenye umri wa miaka 55, alilazwa katika hospitali ya St Thomas mjini London wakati hali yake ya kiafya ilipokuwa haina ahueni huku homa na kukohoa kukiongezeka zaidi siku ya Jumapili. Hatua hiyo imechukuliwa baada ya ushauri kutoka kwa timu yake ya matibabu na anaendelea kupata huduma stahiki.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger