Tuesday, 27 August 2019

Waziri Simbachawene Aielezea Ya Kamati Bunge Mchakato Wa Tathmini Ya Athari Kwa Mazingira

Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) leo Agosti 27, 2019 imewasilisha taarifa zake mbili kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira jijini Dodoma.
 
Taarifa zilizowasilishwa ni ya Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge yanayohusiana na majukumu ya Wizara yaliyotokana na Mapendekezo ya Kamati hiyo katika taarifa yake ya mwaka iliyowasilishwa katika Mkutano wa Bunge wa Februari 2019.
 
Kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Suleiman Sadik pia imepokea taarifa ya Mazingira kwa ajili ya kujijengea uelewa kuhusu Tathmini ya Athari ya Mazingira (TMA). 


Share:

Maafisa mipango wahimizwa kushirikiana na idara za afya kujua miradi inayofadhiliwa na UNICEF

Na Amiri kilagalila-Njombe
Idara za maafisa mipango zilizopo kwenye halmashauri za wilaya nchini zimetakiwa kupata ushirikiano wa karibu na Sekta ya afya ili kusaidia kutokwamishwa kwa jitihada za shirika la kuhudumia watoto Unicef.

Wito huo umetolewa na wadau wa afya na lishe kutoka mikoa ya Iringa,Mbeya,Songwe na Njombe lli kufikia lengo la kulinda afya ya mama na mtoto.

Mratibu wa asasi zisizo za kiserikali kutoka ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa (Tamisemi), Dennis Londo wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau wa masuala ya afya na lishe kilichofanyika halmashauri ya mji Makambako mkoani Njombe amesema  maafisa mipango wengi wamekuwa hawafahamu kinachoendelea kuhusu miradi inayofadhiliwa na Unicef na badala yake taarifa sahihi zinafichwa.

“Ni vibaya kiasi ambacho DED kama accounting officer anaonekana kama mgeni katika miradi yake yeye mwenyewe,afisa mipanga ambaye ndio mkono wa DED katika kumuelezea mipango na utekekelezaji,changamoto na mafanikio, mara nyingi amekuwa hafahamu nini ambacho kinatokea hasa kwenye miradi ambayo inafadhiliwa na Unicef”alisema Dennis Londo

Afisa lishe wa Unicef, Abraham Sanga amesema wanaendelea kushirikiana na serikali katika kufuatilia fedha zinazotolewa  kuona zinawafikia walengwa hasa watoto ambao ndiyo walengwa.

“Tunashirikiana na serikali katika kufuatilia na  kuhakikisha fedha zinazotolewa zinawafikia walengwa hasa watoto kwa hiyo sisi kwa upande wetu tunaufuatiliaji huo wa mara kwa mara”alisema Abraham Sanga

Jachinda Chang’a  ni afisa mipango na uratibu ofisi ya mkoa wa Njombe  na  Theresia Yomo ni afisa ustawi wa jamii mkoa wa Njombe ambao kwa nyakati tofauti wameelezea manufaa yaliyopatikana katika mkoa wa Njombe kupitia ufadhili wa Unicef  huku wakikiri kuwepo kwa changamoto za ufuatiliaji wakati wa mipango.

“Wadau wetu wamekuwa wakituwezesha,katika sekta hizi lakini kumekuwa na changamoto mbali mbali za ufuatiliaji wakati wa mipango,na hili tumejipanga kuliboresha,hata hivyo sisi wataalamu tunapaswa kutathmini tumefanya kazi kwa kiwango gani na ni wapi ambapo palikuwa na gape”alisema Jachinda Chang’a


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521


Share:

Anayedaiwa kumuua na kumchoma mkewe Kwa Magunia Mawili ya Mkaa Aomba Apatiwe Simu Zake Ili Ahamishe Fedha Zake

Mshtakiwa Hamisi Luwongo anayetuhumiwa kumuua mkewe Naomi Marijani kisha kumchoma na magunia mawili ya mkaa, ameomba apewe laini  zake mbili  za simu zenye zaidi ya Sh milioni tano ili awape ndugu zake wakamlipie mwanawe ada.

Mshtakiwa huyo amedai hayo leo Jumanne Agosti 27, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Salum Ally, wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amedai upelelezi haujakamilika akaomba kesi iahirishwe.

“Kesi imekuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa,” amedai Simon.

Wakili Simon baada ya kueleza hayo, mshtakiwa alinyoosha mkono na kumueleza hakimu kuwa ana mambo mawili anataka kuyasema ambayo ni   nakala yake ya hati ya mashtaka na laini zake za simu.

Aliomba apatiwe laini hizo kusaidia familia yake na ada na kusisitiza kuwa katika kituo hicho kuna simu zake nne, mbili ndio zenye kiasi hicho cha fedha. 

 
“Mheshimiwa Kituo Kikuu cha Polisi (Central) kuna simu zangu nne lakini katika hizo simu kuna laini mbili ya Tigo na Airtel, zina zaidi ya Sh milioni tano, naomba simu ziletwe mahakamani nihamishie hizo fedha kwa ndugu yangu zikasaidie kumlipia mwanangu ada,” amedai.

Hata hivyo, wakili Simon amedai hawawezi kumpatia laini hizo kwa kuwa simu zake ni sehemu ya ushahidi wa kesi hiyo.

Amesema kama anahitaji fedha hizo aandike barua ya malalamiko na kuipeleka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania ( DPP) na nakala  aipeleke kwa Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini( DCI) huku hakimu Ally akimtaka mshtakiwa kufanya kile  alichoelezwa na upande wa mashtaka.

Baada ya kueleza hayo kesi hiyo iliahirishwa hadi Septemba 10, 2019 itakapotajwa tena huku mshtakiwa akirudishwa mahabusu.


Share:

Brazil yakataa msaada wa G7 kuzima moto wa Amazon

Brazil Jumatatu imekataa msaada wa kifedha wa dola milioni 20 wa kusaidia kuzima moto katika msitu wa Amazon kutoka kundi la (G7).

Nchi za kundi la mataifa saba yenye uchumi mkubwa wa viwanda G7 zimeahidi msaada wa dola milioni 20 kupambana na moto huo wakati wakiwa katika mkutano wa kilele mjini Biarritz, Ufaransa. 

Lakini  Rais wa Brazil Jair Bolsonaro amemuambia Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ashughulikie nchi yake na makoloni yake.

Macron ambaye alikuwa mwenyeji wa mkutano huo, aliwasisitizia wenzake kuwa wanapaswa kuupa kipaumbele moto unaowaka katika msitu wa Amazon. 

Mbali na fedha hizo, Uingereza kwa upande wake imeahidi kutoa dola milioni 12, na Canada itatoa dola milioni 11 pamoja na ndege za kuzima moto.

Onyx Lorenzoni, mkuu wa shughuli za ofisi ya rais wa Brazil ameiambia tovuti ya habari ya G1 kwamba wanashukuru lakini labda fedha hizo zitafaa zaidi kupanda miti na kuimarisha misitu barani Ulaya, huku rais Bolsonaro akisema hamna msaada unaotolewa bure.

"Macron ameahidi msaada kutoka nchi za kitajiri utumike Amazon. Kwa nini macho yao yote wameyaelekeza Amazon? Wanataka nini huko kwa muda mrefu?," amesema Bolsonaro.
 
Macron alimjibu Bolsonaro kwa kusema kwamba japo kuwa sehemu kubwa ya Amazon imo ndani ya Brazil, lakini hili ni suala la ulimwengu na ujumbe wake kwa kiongozi huyo ni kwamba ulimwengu hautomruhusu kuangamiza kila kitu.

Waziri wa Mazingira wa Brazil Ricardo Salles awali aliwaambia waandishi habari kwamba wanaukaribisha msaada wa nchi za G7 ili kuukabili moto huo unaoteketeza ekari milioni 2.3 katika msitu wa Amazon. Lakini baada ya mkutano na Bolsonaro pamoja na mawaziri wake, serikali ya Brazil ilibadilisha msimamo wake.

Ingawa asilimia 60 ya msitu wa Amazon imo ndani ya Brazil, msitu huo mkubwa unasambaa pia katika nchi nyingine nane ikiwa ni pamoja na Guiana iliyowahi kuwa koloni la Ufaransa na sasa ni sehemu ya Ufaransa kisiasa na kisheria.

-DW


Share:

Makamu wa Rais Samia Suluhu: Sina nia ya kugombea Urais wa Zanzibar

Makamu wa Rais wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa hana nia ya kugombea nafasi ya uongozi kwa ngazi ya Urais visiwani Zanzibar.

Makamu wa Rais ameyabainisha hayo Mkoa wa Kusini Unguja wakati wa sherehe  za kimila ya Wakizimkazi, ambazo hufanyika kila mwaka visiwani humo kwa lengo la kukuza na kudumisha mila na tamaduni za wakazi wake.

''Nataka kusema kwamba kuna maneno maneno kwamba Mama Samia Suluhu anataka kugombea Urais Zanzibar, nataka kuwaambia sio kweli na sina nia hiyo, ukiangalia ngazi ya uongozi ndani ya Tanzania mimi ni namba mbili sina kishawishi chochote kinachonivuta kunileta huku niwe namba tatu sina", amesema Mama Samia.

"Niliona  niliseme hukuhuku lilikotoka kwa sababu maneno yamekuwa mengi, chuki, ufisadi na majungu'', ameongeza.

Hivi karibuni kumekuwa na maneno yanayosambazwa hasa visiwani Zanzibar kuwa Mama Samia ana nia ya kugombea nafasi ya Urais visiwani humo.


Share:

Wawekezaji Sekta Ya Ngozi Kutoka Misri, Wawasili Nchini Kufuatia Wito Wa Waziri Mkuu Majaliwa

Na. Edward Kondela
Wawekezaji katika sekta ya ngozi wamewasili hapa nchini wakitokea nchini Misri kufuatia mwaliko wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa alipofanya ziara nchini humo kuanzia tarehe 8 hadi 10 Mwezi Julai Mwaka 2019 na kukutana na wadau wa ngozi nchini humo.

Akizungumza kufuatia ugeni huo uliowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Felix Nandonde, amesema umetokana na ziara ya kikazi aliyofanya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa nchini Misri ambapo alipokuwa nchini humo alitembelea mji wa viwanda vya ngozi Roubiki na kuzungumza na wazalishaji wa bidhaa za ngozi nchini humo na kuwapa mwaliko wa kuja nchini Tanzania kuwekeza katika sekta ya ngozi kutokana na ubora wa bidhaa ya ngozi inayopatikana hapa nchini.

“Jambo moja kubwa tumeweza kuwathibitishia hawa wawekezaji katika sekta ya ngozi kutoka nchini Misri ni kwamba Tanzania ina bidhaa bora za ngozi na wenyewe wamejionea bidhaa bora za ngozi na ngozi yenyewe ambayo inapatikana nchini, wamekiri ni ngozi bora, tunaamini kwamba matunda ya ziara ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa imeweza kufungua mlango wa sekta ya ngozi Tanzania.” Amesema Dkt. Nandonde

Kufuatia ugeni huo wa Bw. Mahmoud Sargy Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Sargy Tannery, Bw. Hisham Gazar Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Piel Color na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kutoka Kiwanda cha kuchakata ngozi Cairo for Investment and Development Mhandisi Yasser El Maghraby, Dkt. Nandonde amefafanua kuwa anaamini wawekezaji hao watapanga mipango ya muda mrefu na mfupi kuhakikisha wanashiriki kunyanyua sekta ya ngozi nchini Tanzania.

Kuhusu ubora wa ngozi Mkurugenzi huyo wa Uzalishaji na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Felix Nandonde amesema wizara imejipanga kuzidi kutoa elimu kwa wachunaji wa ngozi ili wapate elimu sahihi ya uchunaji na kuwapatia mbinu bora ya uchunaji wa ngozi kwa kuwa ngozi machinjioni imekuwa ikipoteza ubora wake kwa asilimia 50 kutokana na uchunaji usiyo sahihi.

 “Wizara kwa sasa imeanza kutoa mafunzo kwa wachunaji mfano Mkoa wa Morogoro kwa kuwa ngozi inapoteza ubora kutokana na kuharibiwa na visu wakati wa uchunaji hivyo kuwa na matundu na kupunguza ubora wa ngozi.” Ameongeza Dkt. Nandonde

Licha ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoa elimu ya ufugaji bora mkurugenzi huyo wa uzalishaji na masoko amewaasa wafugaji kufuga ng’ombe kwa njia bora, kuhakikisa wanawaogesha ili kujikinga dhidi ya magonjwa yanayoharibu ngozi pamoja na wafugaji kutowawekea alama mifugo yao sehemu zisizostahili ambazo zimekuwa zikisababisha kupoteza ubora wa ngozi.

Awali wawekezaji hao kutoka Misri mara baada ya kuwasili hapa nchini, waliambatana na maafisa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kutembelea Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi WOISO kilichopo eneo la Salasala jijini Dar es Salaam wakiwa na lengo la kujionea namna ngozi inavyotumika kutengenezea bidhaa mbalimbali.

Wakiwa kiwandani hapo wameshuhudia idadi kubwa ya vijana walioajiriwa wakiwa katika majukumu yao ya kutengeneza bidhaa mbalimbali vikiwemo viatu, mikanda na mabegi ambapo walitaka kufahamu utendaji kazi wa kiwanda, teknolojia zinazotumika kiwandani hapo pamoja na soko la bidhaa hizo ili kuangalia maeneo ambayo wanaweza kushirikiana na wawekezaji waliopo hapa nchini katika sekta ya ngozi.

Aidha wakiwa jijini Dar es Salaam wawekezaji hao walipata fursa ya kukutana na Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Ace Leather kilichopo mjini Morogoro Bw. Onorato Garavaglia, ambapo walitaka kufahamu pia namna kiwanda hicho kinavyopata ngozi na hatua inazopitia hadi kuchakata ngozi hiyo kabla ya kuipeleka sokoni.

Bw. Garavaglia aliwafahamisha umuhimu wa ujenzi wa kiwanda bora yakiwemo mazingira ambayo hayataathiri ubora wa ngozi na namna kiwanda chake kinavyozidi kujiimarisha kwa kufunga mitambo mipya ya kisasa zaidi ili kuchakata ngozi na kuiongezea thamani zaidi katika soko la kimataifa.

Baada ya mazungumzo hayo wawekezaji hao kutoka Misri Bw. Mahmoud Sargy Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Sargy Tannery, Bw. Hisham Gazar Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha kuchakata ngozi Piel Color na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kutoka Kiwanda cha kuchakata ngozi Cairo for Investment and Development Mhandisi Yasser El Maghraby ambao wameonesha nia ya kuwekeza nchini katika sekta ya ngozi walifika katika kiwanda hicho cha kuchakata ngozi Ace Leather mjini Morogoro na kujionea madaraja mbalimbali ya ngozi iliyochakatwa kiwandani hapo na kusema kuwa wamefurahishwa na ubora wa ngozi iliyopo hapa nchini.

Mwisho.


Share:

Serikali Yatenga Milioni 696 kukarabati Shule kongwe ya Galanos iliyopo Tanga

Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 696 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya shule kongwe ya sekondari Galanos iliyopo mkoani Tanga.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknlolojia William Ole Nasha alipotembelea shule hiyo kukagua maendeleo ya ukarabati wa miundombinu ambapo amesema fedha hizo zimetolewa kupitia mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) katika mpango unaolenga kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule hiyo kongwe.

Ole Nasha amesema fedha hizo ni sehemu ya fedha zilizopelekwa katika shule kongwe nchini ambazo zinafanyiwa ukarabati mkubwa lengo likiwa ni kuzirudisha katika hadhi yake ya awali ili ziwe na mazingira mazuri yanayomwezesha mwanafunzi kujifunza na kufaulu vizuri

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri huyo amemtaka Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Daudi Mayeji kufuatilia kwa karibu sababu zilizopelekea kukiukwa kwa masharti ya mkataba wa muongozo wa ukadiriaji majenzi (BOQ) ambao ulielekeza kuwekwa chuma katika varanda za madarasa zinazoruhusu hewa na badala yake yamewekwa matofali ya kuchoma.

“Galanos tumeleta fedha zaidi ya shilingi milioni 696 kwa ajali ya kukarabati miundombinu, baada ya kukagua maendeleo ya ukarabati nimegundua kuna mapungufu makubwa ya kimakusudi, Mfano kwenye madarasa kulitakiwa kuwekwe chuma lakini badala ya kuweka chuma wameweka matofali ya kuchoma bila hata kufuata taratibu wa kufanya mabadiliko” amesema Ole Nasha.

Amesema inashangaza kwani Mhandisi alishiriki katika uandaaji wa BOQ hiyo na ni mmoja wa walioshauri kuwekwa kwa chuma lakini katika utekelezaji wa BOQ hiyo iliyopitishwa amebadili maelekezo, hata baada ya kamati ya ujenzi kumkatalia na kumtaka kufata BOQ inavyotaka lakini bado aliendelea na utaratibu wa kuweka matofali hayo badala ya chuma.

“Ndio maana nimemwelekeza Mkurugenzi wa Jiji afuatilie kwanini kuna ukiukwaji wa makusudi wa kuacha kufuata BOQ na nimemwelekeza achukue hatua kwa yeyote anayehusika kubadilisha maelekezo ya BOQ” amesisitiza Ole Nasha

Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Daudi Mayeji ameahidi kufatilia suala hilo la uwekwaji wa matofali badala ya chuma na kwamba atachukua hatua kwa wale wote waliohusika katika kubadili maelekezo yaliyopo katika mkataba wa ukadiriaji majenzi (BOQ).


Share:

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa Kuongoza Ujumbe Wa Tanzania Kwenye Mkutano Wa Saba Wa Tokyo Kuhusu Maendeleo Ya Afrika (TICAD 7) Akimwakilisha Rais Maguful

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi amewasili jijini Yokohama, Japan tarehe 26 Agosti kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 7 wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (Tokyo International Conference on African Development-TICAD 7) utakaofanyika kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019.

Mkutano huu wa Saba utatanguliwa na kikao cha Maafisa Waandamizi wakiwemo Makatibu Wakuu na Mabalozi tarehe 25 na 26 Agosti 2019 ukifuatiwa na kikao cha Mawaziri tarehe 27 Agosti, 2019 na utahitimiswa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali tarehe 28 hadi 30 Agosti 2019. Kauli mbiu ya Mkutano huu ni “Kuendeleza Maendeleo ya Afrika kupitia Watu, Teknolojia na Uvumbuzi”.

Mkutano wa Saba pamoja na mambo mengine unatoa fursa ya kupanga mikakati ya ushirikiano na agenda za kimaendeleo zitakazotelezwa kati ya Japan na Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka 2019 hadi 2021.

Agenda za mkutano wa mwaka huu zinalenga kujadili mageuzi ya kiuchumi na kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kukuza sekta na uvumbuzi. Pia kuimarisha usalama na ustahimilivu endelevu kwenye jamii pamoja na kuendeleza jitihada za kuimarisha amani na usalama barani Afrika. Agenda za Mkutano wa Saba zinaenda sambamba na agenda 2063 ya Umoja wa Afrika, Agenda 2030 ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa na maazimio mengine ya kimataifa kama Mkataba wa Paris kuhusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa.

Kutokana na mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya kiuchumi barani Afrika, Mkutano wa TICAD 7 umeandaa ratiba maalum itakayozishirikisha taasisi binafsi na za umma kwenye majadiliano ya kibiashara yatakayofanyika tarehe 29 Agosti 2019. Lengo la majadiliano hayo ni kuwaleta pamoja wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi wa Serikali wamiliki wa Kampuni, wafanyabiashara na wawekezaji ili kujadili kwa pamoja masuala mbalimbali ya kukuza baishara, uwekezaji na utalii kati ya Japan na Afrika.

Kadhalika  wakati wa mkutano wa saba nchi zote za Afrika zimepatiwa nafasi ya kushiriki katika shughuli mbalimbali kwa lengo la kutangaza fursa za biashara, uwekezaji na vivutio vya utalii za nchi husika. Tanzania kupitia Bodi ya Utalii (TTB) imejipanga kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini wakati wa mkutano huo.

Mkutano wa Saba wa TICAD utahitimishwa kwa Wakuu wa Nchi kupitisha Azimio la Yokohama na Mpango Kazi wa utekelezaji wa Azimio hilo. Serikali ya Japan ilianzisha jukwaa la majadiliano kati yake na nchi za Afrika mwaka 1993 kwa ajili ya kujadili maendeleo na nchi hizo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ataongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Yokohama, Japan.
26 Agosti 2019


Share:

Jaji Mkuu Ataka Vipimo Vya DNA Kutumika Katika kesi za mauaji, ubakaji na unajisi

Na Lydia Churi- Mahakama Njombe
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma leo ameanza ziara ya kikazi katika mikoa ya Iringa na Njombe na kutaka kuwepo kwa matumizi ya vipimo vya vinasaba (DNA) katika kesi za mauaji, ubakaji na unajisi kwa watoto ili kurahisisha uendeshaji wa kesi hizo na kusaidia haki kupatikana kwa wakati.

Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka alipomtembelea ofisini kwake, Jaji Mkuu amesema matumizi ya vipimo vya DNA katika kesi yatasaidia haki kupatikana ambapo aliyetenda kosa atatiwa hatiani na asiyetenda kosa ataachiwa mapema.

“Kipimo cha DNA husaidia kuthibitisha kosa lililofanyika lakini bahati mbaya, kwa uzoefu wetu hatuoni matumizi ya kipimo hicho”, alisema Jaji Mkuu.

Alisema kutokutumika kwa kipimo cha DNA Mahakamani, mshtakiwa huweza kuachiwa huru kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

“Eneo hili tumeona huweza kusababisha mtuhumiwa kuachiwa huru kwa sababu sisi tunaangallia zaidi ushahidi” alisisitiza Jaji Mkuu.

Alisema wakati mwingine Jaji au Hakimu huweza kuona wazi kuwa mshtakiwa alistahili kutiwa hatiani lakini ushahidi unapokosa uzito mtuhumiwa huachiwa huru.

Akifafanua, Jaji Mkuu Alisema kesi kama hizi huchukua muda mrefu na kusababisha wakati mwingine ushahidi muhimu kufifia kiasi kwamba kesi inapofika mahakamani lile joto la ushahidi lililoonekana wakati wa tukio huweza kupotea.

Alisema kutokana na kukua kwa sayansi na Teknolojia hivi sasa hatua kubwa imefikiwa katika matumizi ya kipimo cha DNA na kurahisisha sana. Akitolea mfano wa kesi ya ubakaji au unajisi kwa watoto wadogo alisema badala ya kumuhoji mtoto mdogo mahakamani, kipimo hiki huweza kutumika ili kuthibitisha kosa lililofanyika.

Alisema Serikali kwa kushirikiana na Mahakama hawana budi kuifanyia kazi changamoto hii ili kila raia anayetenda kosa atiwe hatiani na asiye na kosa aachiwe huru mapema hata katika hatua ya upelelezi wa kesi husika.

 Wakati huo huo, Jaji Mkuu alisema suala la ujazaji wa fomu za taarifa ya Daktari yaani PF 3 halizingatiwi kwa kuwa fomu hizo hazijazwi kwa ufasaha na hivyo huweza kusababisha mtuhumiwa kuachiwa huru wakati mwingine.

“Fomu hii inayo maeneo muhimu ya kujazwa na hasa yanayohitaji vipimo na endapo itajazwa kwa ufasaha itasaidia sana katika kuhakikisha mtu anayetenda kosa anatiwa hatiani”, alisema.

Kuhusu kesi za Mirathi, Jaji Mkuu alisema eneo hili lina changamoto kwa kuwa kesi hizi pia huchukua muda mrefu zaidi hivyo elimu haina budi kutolewa hasa kwa wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini. Alisema wananchi wanatakiwa kufahamu kuwa kila mtu anapaswa kujitahidi kutafuta chake badala ya kutegemea cha marehemu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Njombe alimpongeza Jaji Mkuu wa Tanzania kwa kujitoa kwake katika kuhakikisha Mahakama inatoa mchango mkubwa kwenye maendeleo ya nchi na pia alimpongeza kwa kuendeleza ushirikiano na Mihimili ya Serikali na Bunge.

Aidha, Mhe. Ole Sendeka ameahidi kushirikiana kwa karibu zaidi na Mahakama ya Tanzania inapotekeleza majukumu yake ya msingi ya utoaji wa haki kwa wakati.  

Katika ziara iliyoanza leo, Jaji Mkuu ametembelea Mahakama ya wilaya ya Makete na kuzungumza na watumishi wa Mahakama hiyo lakini pia alipata nafasi ya kukagua ujenzi wa jengo la Mahakama ya Mwanzo Makete.


Share:

Mwanafunzi Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Ahukumiwa Jela Miezi 12 au Faini Milioni 5 Kwa Kuchapisha Maudhui Mtandaoni Bila Leseni

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam nchini Tanzania, imemhukumu mwanafunzi wa mwaka wa pili, Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Julius Warioba (23) kulipa faini ya Sh5 milioni au kwenda jela mwaka mmoja.

Ni baada ya kukiri shtaka la kuchapisha maudhui katika Mtandao bila kuwa na leseni kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Warioba ambaye ni mshereheshaji (MC) anadaiwa kuchapisha maudhui kupitia Televisheni ya mtandaoni  inayojulikana kwa jina Mc Warioba, bila kuwa na kibali kutoka TCRA wakati wakijua kuwa ni kinyume cha sheria ya Mtandao.

Mbali na faini, Mahakama hiyo, imetaifisha kompyuta aina ya Apple na simu ya mkononi aina ya Iphone ambavyo vilitumika katika kuchapisha maudhui hayo.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo amefanikiwa kulipa faini na hivyo kukwepa kifungo.

Hukumu hiyo imetolewa jana  Jumatatu Agosti 26, 2019 Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Janeth Mtega baada ya mshtakiwa kutiwa hatiani.


Share:

ZOEZI LA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA LAPIGWA KALENDA SHINYANGA....SASA KUANZA SEPTEMBA 2

Kamishina wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa nchini Tanzania,Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri 

Na Marco Maduhu - Malunde1 blog

Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura mkoa wa Shinyanga lililotakiwa kuanza Agosti 26,2019 hadi Septemba 1,2019 , limeahirishwa baada ya kudaiwa kutokea kile kimeitwa matatizo ya kiufundi na kusababisha kusogezwa mbele.

Akizungumza na Malunde1 blog Msimamizi wa Uchaguzi mkoani Shinyanga Amos Machilika, ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Utumishi na Utawala mkoani Shinyanga amesema zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura mkoa wa Shinyanga litafanyika kuanzia Septemba 2,2019. 

“Zoezi la maboresho ya uandikishaji wa daftari la kudumu la mpiga kura mkoani Shinyanga lilikuwa lianze Agosti 26,2019, lakini kuna matatizo ya kiufundi ambayo yamejitokeza ndipo ikabidi zoezi hili tuliahirishe na kulisogeza mbele ambapo litafanyika kuanzia Septemba 2 mwaka huu” amesema Machilika.

Alhamis Agosti 15,2019 Kamishina wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa nchini Tanzania,Mhe. Balozi Omari Ramadhani Mapuri akizungumza katika mkutano wa Tume na Wadau wa Uchaguzi mkoani Shinyanga kikiwa na lengo la kupeana taarifa kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, alitangaza zoezi la uboreshaji wa daftari la wapiga kura lifanyike Agosti 26 hadi Septemba 1,2019.

Aliwataka watu wenye sifa ya kujiandikisha wajitokeze kwa wingi ili waandikishwe na wanaohitaji kuboresha taarifa zao wakati wa zoezi hilo.
Share:

TETESI ZA SOKA LEO JUMANNE AGOSTI 27,2019

Huenda Manchester United ikasubiri ukaguzi wa mchezaji wa kiungo cha mbele raia wa Ufaransa Anthony Martial, mwenye umri wa miaka 23, kabla ya kuruhusu uhamisho wa mkopo wa mchezaji wa kimataifa wa Chile Alexis Sanchez, mwenye umri wa miaka 30, kwenda Inter Milan. (Guardian)

Paris St-Germain imeambia Real Madrid itatafakari kumuuza mchezaji wa Brazil wa kiungo cha mbele Neymar, mwenye umri wa miaka 27, iwapo mchezaji wa klabu hiyo ya Uhispania mwenye miaka 19 na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Jr iatakuwa sehemu ya makubaliano ya kudumu. (AS)

Wakurugenzi wa Barcelona wamekutana Jumatatu kujadili ombi la mchezaji wao wa zamani Neymar. (Marca)

Huenda Inter Milan ikamgeukia mchezaji wa kiungo cha mbele wa Manchester City Wilfried Bony, mchezaji huyo wa Ivory Coast mwenye miaka 30 kwa sasa haichezei klabu yoyote baada ya kuachiwa na Swansea msimu wa joto. (Goal.com)

Mchezaji wa kimataifa wa Serbia Nemanja Matic, mwenye umri wa miaka 31, ameitisha mazungumzo na meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer baada ya kuipoteza nafasi yake ya kwanza huko Old Trafford. (Mirror)

Arsenal ipo tayari kumruhusu mchezaji wa kimataifa wa Uhispani Nacho Monreal kujiunga na Real Sociedad wiki hii iwapo mchezaji huyo wa miaka 33 na mchezaji wa kiungo cha ulinzi ataomba kuondoka. (Sun)

Javi Gracia anapigania kuokoa nafasi yake kama meneja wa Watford baada ya kuanza msimu wa ligi kuu England kwa kushindwa mara tatu. (Telegraph)
Mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham anaelekea kupata mkataba mpya ambao huenda ukaongeza zaidi ya mara mbili malipo ya mchezaji huyo wa miaka 21 raia wa England ya £50,000 kwa wiki(Telegraph)

Wawakilishi wa Christian Eriksen hawatofikiria pendekezo la mkataba wa Tottenham la malipo ya £200,000 kwa wiki na mchezaji huyo wa miaka 27 ambaye mkataba wake hivi sasa unamalizika msimu ujao wa joto anatumai kupata uhamisho kwenda Uhispania. (Mirror)

Eriksen ni kama amejiuzulu kusalia Tottenham katika kipindi kifupii, huku ndoto yake ya kujiunga na Real Madrid au Barcelona msimu huu wa joto ikishindwa kufanikiwa. (Mail)

Winga wa Celta Vigo Pione Sisto, mwenye umri wa miaka 24, anakaribia kujiunga na Torino baada ya uhamisho kwenda Aston Villa kutofanikiwa. (Marca)

Mabingwa wa Italia Sampdoria wanataka kumsajili winga wa Swansea anayeichezea timu ya taifa ya Ghana Andre Ayew, mwenye umri wa miaka 29, kwa mkopo kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho Ulaya (Star)
Mlinzi wa Manchester United Luke Shaw, mwenye miaka 24, huenda akawa nje kwa hadi mwezi mmoja kutokana na jeraha katika msuli wake wa paja. (Talksport)

Huenda Sunderland ikawasilisha ombi la pili kwa mlinzi wa Sheffield Morgan Fox, 25 hapo kesho Jumatano (Newcastle Chronicle)

Jurgen Klopp anaamini mbinu yake ya usimamizi inaongeza uwezekano wa yeye kwenda mapumzikoni wakati kipindi chake cha usimamizi kitakapomalizika Liverpool mwaka 2022. (Times)

Kevin De Bruyne ameunga mkono mchezaji wa zamani wa timu ya Manchester City , Vincent Kompany kuwanyamazisha wakosoaji na kufungua ufanisi wa nafasi yake mpya kama bosi wa Anderlecht, baada ya kujizolea pointimbili katika mechi nne za kwanza msimu huu. (Manchester Evening News)

Mchezaji wa kiungo cha kati wa Spurs na timu ya taifa ya Kenya Victor Wanyama amepewa mkataba wa miaka mitano kwa malipo ya £65,000- kwa wiki na Club Bruges wakati anapokaribia kukamilisha uhamisho. (Scottish Sun)Mchezaji wa kiungo cha kati wa Spurs na timu ya taifa ya Kenya Victor Wanyama

Kalbu ya Fiorentina katika ligi ya Serie A inajitayarisha kuwasilisha ombi kwa mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United na timu ya taifa ya Brazil Fred, mwenye umri wa miaka 26. (Calciomercato)

Norwich itamfukuzia kipa wa Stoke na timu ya taifa ya England Jack Butland, mwenye umri wa miaka 26, ifikapo Januari na iwapo thamani yake itashuka. (Sun)

Bordeaux inataka kumchukua mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal na Misri Mohamed Elneny, mwenye umri wa miaka 27, kwenda Ligue 1 kwa mkopo. (Foot Mercato)

Leeds inatarajiwa kuanza mara moja mazungumzo na mchezaji wa kiungo cha kati Kalvin Phillips kuhusu mkataba mpya. Mchezaji huyo wa miaka 23 anataka kulipwa £40,000 kwa wiki ili kuendelea kusalia Elland Road. (Football Insider)

Aliyekuwa beki kamili wa Chelsea Filipe Luis, mwenye umri wa miaka 34, amekataa ombi la Manchester City, Lyon na Borussia Dortmund msimu huu wa joto kabla ya kujiunga na Flamengo kutoka nchini anakotoka Brazil. (Globo Esporte)Beki kamili wa zamani wa Chelsea Filipe Luis

Aliyekuwa beki wa kulia wa Leicester Danny Simpson, mwenye umri wa miaka 32, anafanya mazungumzo na klabu ya Ligue 1 - Amiens kuhusu uhamisho. (Sun)

Meneja wa Chelsea Frank Lampard amemkaribisha mchezaji wa kiungo cha kati wa Exeter Ben Chrisene kufanya mazoezi na klabu hiyo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 15 kutoka timu ya vijana wa timu ya taifa England alifanikiwa kucheza katika kikosi cha kwanza mwezi huu. (Sun)
Chanzo - BBC
Share:

ANUSURIKA KIFO BAADA YA KICHWA CHAKE KUKWAMA KWENYE NGAZI BAFUNI

Hili halikuwa katika muogozo wa ukarabati: mwanamume aliyekuwa anajaribu kukarabati na kulirembesha bafu lake huko mashariki mwa Ufaransa aliteleza akaanguka na kukwamisha kichwa chake kwenye ngazi kwa siku tano.

Vyombo vya habari nchini humo vinaeleza kuwa, mwanaume aliye katika miaka ya 60 alikuwa amepotewa na fahamu wakati wahudumu wa afya walipowasili.

Waliarifiwa na dadake , aliyemtembelea siku ya Ijumaa.

Kichwa chake , kilichokwama katikati ya ngazi , kilifura katika siku hizo tano na alishindwa kuifikia simu yake kuomba usaidizi.

Msukumo wa damu kichwani mwake ulipungua, na anafanyiwa ukaguzi hospitalini.

Jamaa huyo anayetoka Mattaincourt karibu na Épinal, ambaye jina lake halikuwekwa wazi alipatikana akiwa hana maji mwilini.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne 27 August




Share:

Monday, 26 August 2019

Naibu Waziri Wa Maliasili Aagiza Wananchi Waliovamia Msitu Wa Hifadhi Gairo Wakamatwe

FARIDA SAIDY, MOROGORO
Naibu waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii Mhe.Constantine Kanyasu ameagiza kukamatwa kwa  wananchi wote waliovamia na kukata miti bila kufuata taratibu za kisheria katika msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kumbulu uliopo wilaya ya Gairo mkoani Morogoro.

Naibu waziri ameyasema hayo alipotembelea eneo hilo na kujionea uharibufu mkubwa uliofanywa na baadhi ya wananchi waliovamia msitu huo licha ya kufahamu eneo hilo lilitengwa kuwa hifadhi ya serikali ya kijiji tangu mwaka 2008 akilenga kutafuta ufumbuzi wa mgogoro baina ya serikali ya kijiji na wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Gairo Bi. Siriel Nchemba amesema mgogoro huo umedumu kwa muda mrefu na hatua za ufumbuzi kwa ngazi ya wilaya zilielekea kushindikana, kutokana na vitisho kutoka kwa viongozi wa juu serikalini ambapo tayari baadhi ya viongozi wameondolewa katika nafasi zao.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger