Friday, 16 August 2019

Kasi Ya Maendeleo Ya Rais Magufuli Kusaidia Kuimarisha SADC

Na Judith Mhina-Maelezo
Kasi ya Maendeleo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliyoionyesha katika kipindi cha miaka minne akiwa madarakani, itaamsha ustawi wa miradi ya kimkakati katika Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika –SADC.

Dhahiri, bila kificho kitendo cha kumkabidhi na kuwa Mwenyekiti wa SADC Rais Magufuli kitachochea ongezeko la shughuli za miradi mbalimbali ya kimkakati ya maendeleo, ambayo haikutegemewa na jamii ya Jumuiya SADC kama inaweza kutekelezwa na Tanzania na kuwa mfano wa kuigwa.

Mafanikio ya Rais Magufuli yameonekana waziwazi katika miradi mikubwa ya maendeleo, matukio kadhaa ya kitaifa na kimataifa, ambayo yamedhihirisha kuwa juhudi na mtazamo wa Rais Magufuli ni faraja na muelekeo mzuri wa kufanikisha maendeleo katika nchi wanachama wa- SADC.

Akitoa hotuba ya kumkaribisha Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini Cyril Ramaphosa Rais Magufuli amesema”Katika kutekeleza mipango ya maendeleo na dira ya kufikia uchumi wakati ifikapo 2025, Tanzania inawakaribisha wawekezaji mbalimbali na kwa kuwa Afrika ya Kusini imepiga hatua kubwa katika Viwanda nawaaalika wafanyabiashara kuja kuwekeza katika Viwanda mbalimbali hudusan vya dawa na vifaa tiba, kuchakata madini na kwamba serikali iatatoa ushikiano  utakaohitajika”.

Aidha, Rais Magufuli amesema kuwa sisi Tanzania tumeamua  kununua bidhaa kutoka Afrika ya Kusini, ambapo, hata pikipiki zinazotumika katika  mapokezi ya wajumbe kutoka nchi za SADC zimetoka Afrika ya Kusini. Amesisitiza Rais Magufuli.

Kama hiyo haitoshi, amemuomba Rais Ramaphosa kuongeza ushirikiano katika utalii hasa kwa kuwa wao wanapokea watalii takriban milioni 10 kwa mwaka ikilinganishwa na Tanzania inapokea watalii milioni 1.5 kwa mwaka. Katika hilo alitoa wito Afrika ya Kusini kuongeza safari za treni ya watalii na wawekezaji wake kuja kuwekeza katika hoteli  na fukwe za Tanzania, dhamira ambayo si kwa Afrika Kusini tu bali kwa nchi zote za SADC.

 Akiongea mara baada ya kuwasili nchini Zimbabwe mapema mwezi  Mei, Rais Magufuli amesema “Wakati umefika Jumuia ya Kimataifa kuiondolea nchi ya Zimbabwe vikwazo kwa kuwa vikwazo hivi vinaadhiri wananchi wanyonge wa Zimbabwe”

Aidha, Rais Magufuli amewaambia mabalozi wa nchi mbalimbali walioko Zimbabwe kuwa vikwazo hivi pamoja na kuwaadhiri Wazimbabwe pia, vinawaadhiri mabalozi na familia zenu mlioko hapa. Wakati umefika mliangalie hili na kuliondoa. Ili kila raia, aishiye Zimbabwe afurahie maisha mapya  na kuweza kushirikiana katika nyanja za uchumi kuongeza biashara na ushirikiano kati yetu.

Hakika Rais Magufuli amedhamiria kwa dhati kuleta maendeleo katika SADC, hakuna nchi  yeyote ya Afrika na dunia kwa ujumla iliyowahi kutamka nchi ya Zimbabwe iondolewe vikwazo kutoka kwa bwana wakubwa wa dunia. Hii inadhihirisha Rais Magufuli atachochea  ukuaji wa miradi ya kimkakati ya maendeleo, kuhakikisha ushirikiano na nchi za Kusini mwa Afrika na kuleta ustawi wa hali za maisha za wananchi wanyonge katika jumuiya.

Katika hotuba yake aliyoitoa wakati wa ziara yake nchini Namibia Rais Magufuli alihakikisha anaelekeza kuondolewa kwa vikwazo vya kibiashara katika nchi za Kusini mwa Afrika ili kukuza zaidi ushirikiano ambao utawaletea maendeleo wananchi wa pande zote mbili

Akifungua msimu wa ununuzi wa tumbaku  nchini Malawi Rais Magufuli amesema “Wananchi walio wengi Barani Afrika wapo katika sekta ya kilimo, hapa Malawi nimeambiwa zao  la Tumbaku linachangia asilimia 80 ya ajira, asilimia 60 ya fedha za kigeni na asilimia 37 ya pato la Taifa”.

Uchumi wa nchi nyingi za Afrika zinategemea kilimo kinachochangia pato kubwa la Taifa  pia, ni sekta inayoajiri watu wengi katika nchi zetu, Tanzania inatoa ajira kwa asilimia 70, mali ghafi asilimia 60 asilimia 30 inachangia pato la Taifa  na huingiza asilimia 20 ya fedha za kigeni. Hii inadhibitisha kilimo ni sekta muhimu Barani Afrika. Amesema Rais Magufuli

Rais Magufuli aliongeza  na kusema “Nimeambiwa katika uzinduzi wa zao la Tumbaku Serikali imeweka njia mbili za ununuzi kwa njia ya mkataba au mnada na Serikali imweka bei elekezi lakini, niwaomba wanunuzi msisite kununua kwa bei ya juu  ili kuwapa motisha wakulima wa zao la tumbaku pia mzingatie ubora na msichafue tumbaku kwa lengo la kuongeza uzito”.

Hotuba hii dhahiri inaonesha nia  hakika unaona dhamira yake ya kuhakikisha wakulima wadogo wa tumbaku wananufaika na kilimo wanachokifanya  badala ya kunufaisha watu wa kati na wenye Viwanda bila kujali uwepo wa bei nzuri kwa wakulima. Rais Magufuli anatambua ukubwa wa kundi hili ambalo likiinuliwa uchumi wake maendeleo kwa nchi za SADC yataonekana.

Akionyesha Afrika ilivyo tegemezi kitu ambacho sio kizuri Rais Magufuli ameongeza kwa kusema kuwa, mazao ya chakula kwa sasa ni mazao ya biashara, kwa sasa Afrika wastani wa chakula kinachoingizwa kutoka nje kina gharama ya Bilioni 35 za Marekani. Ambapo soko la chakula Barani Afrika  ni Dola za Marekani 300.

Vilevile, dhamani ya soko la mazao ya chakula kwa soko la Afrika itafikia dola Trilioni 1 mwaka 2030. Tanzania mwaka 2019 imevuna mazao ya chakula ya ziada ikilinganishwa na Malawi, hivyo tunawakaribisha Malawi kuja kununua chakula kutoka Tanzania

Akielezea mikakati sita ya kukuza uchumi wa SADC, Rais Magufuli amesema “Ni lazima kuondoa vikwazo visivyo na maana kama ututuri wa kodi, kuondoa utitiri wa Taasisi zinazothibiti biashara, ili kuchochea kasi ya viwanda na maendeleo katika Jumuia ya SADC”.

Pia, Rais Magufuli amependekeza mambo kadhaa katika hotuba yake ya ufunguzi ya wiki ya Viwanda kama vile, tekinolojia ya viwanda, ambapo anahakika hii italeta mapinduzi makubwa katika sekta ya viwanda ndani ya Jumuiya ya SADC.

Akiangalia soko la SADC, Rais Magufuli amesema soko la watu milioni 350 na zaidi ni kubwa, idadi hii ya watu inatupa  jukumu la kujenga uchumi ndani ya Jumuiya husika. Pia, ubunifu ni kitu ambacho Rais amekiona ni muhimu katika Jumuiya, na kuhamasisha matumizi ya tekinolokia rahisi kwa kuwa rasilimali ya vijana wengi ipo, wenye vipaji katika sayansi na tekinolojia.

Aidha, uanzishwaji wa Viwanda vidogo vidogo kwa sababu hivyo ndivyo vinavyogusa watu wengi na kusisitiza viwanda hivi ndivyo vitakavyo inuka na kuwa viwanda vikubwa hapo baadaye. Hivyo ni lazima Jumuia iweke mazingira wezeshi katika kukuza sekta ya Viwanda. Amesisitiza Rais Magufuli.

Hii ikiwa ni pamoja na uwepo wa nishati ya umeme ya uhakika na bei nafuu, sekta ya usafiri na usafirishaji iwe rahisi na ya uhakika mfano reli ya kisasa (SGR), miundombinu ya barabara, usafiri wa anga wa uhakika.  Pia, kuruhusu idadi ya watu ndani ya Jumuia kutumia soko lililopo bila vikwazo kutoka nchi moja kwenda nyingine na kuhakikisha sekta binafsi inashiriki ipasavyo katika kujenga viwanda.

Rais Magufuli amesema”Tuhimize sekta binafsi, iache kulalamikia badala yake ipambane na changamoto zilizopo na kushirikiana na Serikali husika kuzitatua,  ili kutumia fursa zilizopo ipasavyo”.

Rais Magufuli ameonesha dhahiri nia yake ya kuhakikisha nchi za SADC zinafanya biashara, uwekezaji kuboresha miundombinu, kuongeza uzalishaji wa nishati ili kujenga Viwanda zaidi,  kuimarisha ulinzi na usalama na kulinda historia yetu kwa sasa na vizazi vijavyo ili kutambua tulipotoka, tulipo na tuendapo.

Pamoja na yote Rais Magufuli hakuacha ajenda yake ya lugha adhimu ya Kiswahili ambayo kwa hakika binafsi  nasema yeye ni shujaa wa kupigia chepuo lugha hii. Kila mtu ni shahidi hapa Tanzania kuwa tangu aingie madarakani amehakikisha anaitendea haki lugha hii kwa kuitumia katika shughuli  zake zote za Kitaifa na Kimataifa.

Ukiacha hafla zake chache kama pale alipoongea na wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Afrika ya Kusini  mwaka 2017 ziara ya Rais Jacob Zuma wakati huo, kwa sasa ni msataafu Ambapo aliomba radhi Watanzania kuwa atatumia lugha ya Kiingereza,  ili wafanyabiashara na wawekezaji waone umuhimu wa kumuelewa na kuwekeza nchini Tanzania.

Pamoja na mambo mengine muhimu, ziara hiyo ilizaa  makubaliano ya pamoja kuwa Afrika ya Kusini itaingiza  mitaala ya lugha a kiswahili katika shule zake za msingi na sekondari, hivyo kuwa na hitaji la  Waalimu kutoka nchini Tanzania. Ambapo Rais Magufuli aliwataka Waalimu kuchangamkia fursa hiyo.

Bila kificho tunajivunia lugha hii yenye  historia ya kujenga umoja na mshikamano, pia ni lugha ambayo inaasili  ya Afrika ambapo haimilikiwi na kabila lolote bali na Jumuia ya Afrika Mashariki na Tanzania ndio nyumbani kwake.

Ziara ya Rais Magufuli nchini Namibia mapema mwezi Mei mwaka huu,  imezaa kusainiwa kwa makubaliano ya pamoja ya kuwa lugha ya kishwahili iwe katika mitaala wa shule za msingi na sekondari  nchini Namibia. Hivyo nchi hiyo inahitaji kupatiwa waalimu wa lugha husika kutoka Tanzania.

Kama alivyoelezea  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Paramagamba Kabudi na ajenda ya kunadi lugha ya kishwahili  iwe moja wapo ya lugha rasmi za SADC . Hakika ni kielelezo kuwa ikitumika katika nchi wananchama wa SADC itafufua ari ya umoja na mshikamano wa kweli katika kuwaletea wananchi wake maendeleo.

Ajenda hii ya matumizi ya lugha ya kiswahili iliyoibuliwa na kushikiwa bango na Rais Magufuli wakati alipohudhuria mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Afrika, mapema mwaka 2017. Alihutubia Mkutano huo kwa lugha ya kishwahili wakati wa ufunguzi wa jengo la kihistoria  la Julius Nyerere la Amani na Usalama Jijini Adiss Ababa Ethiopia kama Makao makuu ya Jumuia hiyo.

Juhudi hizo za Rais Magufuli  hatimaye zimeleta ajenda itakayowasilishwa leo katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa nchi za Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika. Hivyo Lugha ya Kiswahili iwe lugha rasmi ya Mawasiliano SADC kama Kiingereza, Kifaransa na Kireno.

Nchi nyingine zilizoridhia kuingiza lugha ya Kiswahili katika mitaala ya shule zake za msingi na sekondari ni pamoja na Sudan Kusini, Rwanda, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ikiwa ni pamoja na kuomba kupatiwa waalimu wa lugha hiyo kutoka Tanzania.


Share:

Okoa Ndoa Yako Na Afya Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Kisukari

Ni dawa zilizopimwa na mkemia na kupewa no 341/VOL,XV/36 na TFDA no 0127/F/F/1819/ MTINJETINJE ni dawa ya kisukari .....Hurudisha kongosho katika hali ya kawaidi hata kama limefeli haijalishi unatumia vidonge au sindano za insulin, itaifanya sukari kuwa normal

SUPER MAJINJA ni dawa inayotibu nguvu za kiume yani matatizo yafatayo (1) kushindwa kurudia tendo na mwili kuchoka (2)kuwai kufika kabla ya  mwenzi wako (3)maumbile ya kiume kulegea na kusinyaa (4)maumbile ya kiume  kuingia ndani na kuwa mafupi kwa wale walio jichua (5)miuungurumo ya tumbo,ngiri,kukosa choo,kiuno kuuma

ACHA KUONGOPEWA SASA DAWA HIZI NI TOFAUTI NA ULIZOWAI KUTUMIA

NJOO OFISINI KWANGU MBAGALA KARIBU NA BENK YA KCB NA mwanza yupo wakala piga simu ya DR AGU whatsapp 0783185060. 0620113431


Share:

Mabalozi 42 wa Tanzania Nje ya Nchi Wasifu ujenzi wa mradi wa Jengo la Tatu la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3)

Na Mwandishi Wetu
Mabalozi  42 wa Tanzania kutoka nchi mbalimbali Duniani wamesifu ujenzi wa mradi wa Jengo la Tatu la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3) kwa kuwa umekuja wakati muafaka, ambapo wawekezaji wengi wanapenda kwenda nchi zenye miundombinu bora nay a kisasa.

Mabalozi hao wametoa kauli hiyo leo walipofanya ziara ya Kikazi ya kutembelea Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3).

Balozi Wilson Masilingi anayeiwakilisha nchi nchini Marekani, amesema jengo hili ni la kisasa na linavifaa bora, ambapo Watanzania wanapaswa kujivunia maendeleo haya, ambapo sasa kuna mpango wa safari za kutoka moja kwa moja kutoka Tanzania hadi Marekani.

Naye Balozi Abdallah Possi anayeiwakilisha Tanzania nchini Ujerumani, kwa jengo hili sasa kutachagiza uwingi wa watalii kutoka nchi mbalimbali duniani, ambapo ndege nyingi zitatumia JNIA.

“Miradi hii ukiwemo huu wa jengo la tatu la abiria ni muhimu kwa wageni wanaoingia nchini, kwani litarahisisha usafiri kwa watu wa Mataifa mbalimbali wanaoingia nchini na kutoka nchini,” amesema Dkt. Possi.

Balozi Fatma Mohamed Rajabu anayewakilisha nchi nchini Qatar, amesema anatarajia ongezeko la ndege ya Air Qatar kwa safari za Tanzania, pamoja na kuja kila siku mara moja.

“Nitaenda kueleza ubora wa jengo letu hili na ninaimani pamoja na ndege ya Qatar inakuja kila siku lakini wanaweza kuongeza safari kwani tumekuwa na jengo la kisasa zaidi na lenye kupokea abiria wengi,” amesema Balozi Fatma.

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Dkt. Wibroad Slaa ametoa wito kwa Mabalozi wenzake kuitangaza zaidi Tanzania Kimataifa kwa kuonesha miradi yote mikubwa na uwekezaji wanaoweza kuwekeza sehemu mbalimbali nchini.

“Msiogope kulitangaza Taifa letu katika maendeleo yanayofanyika sasa chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuweza kuwekeza kwa ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati,”amesema.

Hatahivyo,  mabalozi hao wamesifu juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano iliyopo chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa ujenzi wa Jengo la Tatu la Abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius  Nyerere.

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale alisema jengo hilo linauwezo wa kuhudumia abiria milioni sita kwa mwaka, ambapo linavifaa vya kisasa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mhandisi Julius Ndyamukama amesema jengo hilo pia lina ukumbi wa Wafanyabiashara Mashuhuri.


Share:

Waziri Mkuu: Tupo Tayari Kushirikiana Na Afrika Kusini

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Afrika Kusini katika kutimiza azma yake ya kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo 2025.

Amesema Tanzania inahitaji uungwaji mkono na Serikali ya Afrika Kusini hususan katika kipindi hiki ambacho imedhamiria kuimarisha shughuli za uzalishaji kupitia viwanda kwa lengo la kufikia uchumi wa kati..

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Agosti 16, 2019) wakati wa ziara ya Kiserikali ya Rais wa Afrika Kusini, Cyril Matamela Ramaphosa katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Mazimbu Campus mjini Morogoro.

Ameyasema kwa kuwa changamoto zinazoikabili Tanzania katika nyanja mbalimbali zinafanana kwa kiasi fulani na zile za Afrika Kusini kwani historia za nchi hiyo na jiografia vinafana na Serikali ya Tanzania.

Akizungumzia kuhusu eneo la Mazimbu, Waziri Mkuu amesema kuwa lina uhusiano mkubwa na historia ya nchi hizo mbili kwa sababu huwezi kuulezea vizuri uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini pasi na kulitaja eneo hilo.

Waziri Mkuu amesema eneo la Mazimbu limebeba historia muhimu ya kumbukumbu ya vuguvugu la ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika pamoja na mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini.

“Mheshimiwa Rais, Tanzania ikishirikiana na nchi tano zilizokuwa katika kundi la mstari wa mbele (Angola, Tanzania, Zambia, Botswana na Msumbiji) ilijishughulisha sana katika ukombozi kusini mwa Afrika na katika kukomesha sera za ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini”.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema kuwa sera za ubaguzi wa rangi zilikoma mwezi Februari 1994 na kufuatiwa na uchaguzi huru na wa haki uliopelekea kupatikana kwa Rais wa kwanza mzalendo wa nchi hiyo, Hayati Mzee Nelson Mandela mwezi Mei 1994.

“Tunapoongelea kukoma kwa sera za ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, siku zote tutawakumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwal. Julius Nyerere na Hayati Mzee Nelson Mandela kwa utumishi wao uliotukuka kwa kujenga misingi imara ya umoja katika mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini”.

Amesema misingi imara iliyojengwa na wazee wetu hao, imekuwa chachu ya ushirikiano kwenye majukwaa ya Kimataifa hususani katika kupambana na ubaguzi wa kiuchumi na unyanyasaji wa aina mbalimbali.

Waziri Mkuu amesema namna pekee ya kuwaenzi viongozi wetu hao ni kuendelea kujenga umoja na kushirikiana katika kuimarisha Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa ajili ya maslahi ya wananchi.

Kwa upande wake, Rais Ramaphosa amesema anaishukuru Serikali ya Tanzania kwa mchango mkubwa ulioutoa kwa nchi ya Afrika Kusini wakati wa harakati za kupigania uhuru wa nchi hiyo, hivyo wataendelea kuimarisha ushirikiano.

Rais huyo wa Afrika Kusini amesema Serikali yake ipo tayari kushirikiana na Serikali Tanzania katika kuboresha masuala mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo kubadilishana uzoefu katika maeneo mbalimbali na kukuza teknolojia.

Pia amesema watairisha chuo cha SUA kwa kuboresha miundombinu mbalimbali ili kulifanya eneo hilo kuwa la kisasa. “Tutaboresha na shule katika eneo hili na kuweka utaratibu wa walimu wake kutembeleana na wa Afrika Kusini kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.”

Rais Ramaphosa aliwasili katika uwanja wa ndege wa Morogoro saa 4.21 asubuhi na kupokelewa na Waziri Mkuu. Kisha alitembelea campus ya Solomon Mahlangu na kujionea maeneo ambayo wapigania uhuru wa Afrika Kusini walikuwa wakikutana na kupanga mipango mbalimbali.

Pia kiongozi huyo ambaye kwa mara ya kwanza amefika mkoani Morogoro leo alitembelea campus ya Mazimbu na kujionea sehemu ambazo waliishi wapigania uhuru wa nchi yake na kisha aliweka shada la maua kwenye makaburi ya wapigania uhuru. Ameondoka uwanja wa ndege wa Morogoro na kuelekea jijini Dar es Salaam saa 1.59 mchana.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,        
IJUMAA, AGOSTI 16, 2019.


Share:

Mgogoro Wa Mpaka Na Mapato Ya Madini Halmashauri Mbili Wamalizwa

Na Issa Mtuwa “WM” Nachingwea Mtwara
Mgogoro ulio dumu kwa muda mrefu  kuhusu mpaka wa uchimbaji madini uliohusisha eneo (leseni) moja kwenye ardhi ya halmashauri za wilaya mbili ya Nachingwea na Liwale  kila upande ukiwa na wachimbaji wadogo umetatuliwa na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo tarehe 15/08/2019 mara baada ya kufanya ziara katika eneo hilo na kufanya mkutano na wachimbaji wadogo wa pande zote mbili na viongozi wa kuu wa wilaya zote mbili.
 
Mgogoro huo wa mpaka na leseni umedumu kwa muda mrefu ukiwa na vyanzo viwili vikuu vya mgogoro. Moja,  mgogoro wa eneo ambalo wachimbaji wadogo wananchimba hivi sasa wamedai eneo hilo lilikuwa la Omar Said Kojogo ambae kwa mujibu wa wachimbaji wadogo walimlipa fidia ndugu Kojogi ili eneo hilo limilikishwe kwa jumuia ya wachimbajio wadogo lakini bado walikuwa hawajapatiwa leseni hiyo kama wamiliki wapya. 
 
“Mhe. Naibu Waziri tatizo la mgogoro wa leseni hapa bado haujatatuliwa kwa kuwa sisi wenyewe wanaaporo tulichangishana na kumpa Omar Said Kojogo Tsh.  2,852,000/= ili leseni hiyo iwe ya wanaaporo (Wachimbaji wadogo) lakini mpaka leo hatujapatiwa” alisema Machui Bausi.
 
Chanzo cha pili cha mgogoro huo ni mgao wa mapato yanayopatikana katika eneo hilo. Kila halmashauri inataka ichukuwe  mapato kitu ambacho kilikuwa kinaleta mvutano nani anastahili kwa kuwa leseni ya eneo hilo ipo katika halmashauri zote mbili. za Nachingwea na Liwale zote za mkoa wa Lindi.
 
Aidha, changamoto nyingine ambayo wachimbaji wadogo wamemwambia Naibu Waziri ni tatizo la soko la kuuzia madini ambapo wamemuomba Naibu Waziri kuwasongezea soko la madini katika eneo hilo ili kuwaondolea ushawishi wa kutorosha na kwenda kutafuta soko kwingine na ili mapato ya serikali yasipotee.
 
“Mhe. Naibu Waziri sisi hapa kiliochetu ni soko, hapa tulipo hata ukitaka kuuza madini lazima uende Ruangwa au Tunduru umbali uliopo ni mkubwa kufika huko. Na soko kubwa la Madini ya vito ni Tunduru, kwa hiyo ili mapato ya serikali yasipoteee tunaomba soko liwe hapa hapa sisi tuuze madini yetu na watu wa TRA wawepo ili tukiuza tuu serikali inachukuwa chake hapo hapo” alisema Ijumaa Iddi mwenyekiti wa wachimbaji wadogo katika eneo hilo.
 
Katika kupatia majibu hoja zote zilizo wasilishwa, Naibu Waziri alianza kwa kusema.
 
“Mimi na waziri wangu Biteko iwe mchana iwe usiku, tutafika mahali popote ili kuhakikisha serikali inapata mapato kupitia madini, hivyo uwepo  wangu hapa  ni kwa sababu hiyo na ili pesa hiyo ipatikane lazima migogoro na hizi kero lazima zimalizwe ili mchimbe, muuze na kisha mlipe mapato ya serikali” alisema Nyongo.
 
Katika kujibu hoja, Naibu Waziri alianza kwa msimamisha Kaimu Afisa Madini Mkazi mkoa wa Lindi Mhandisi Iddi atoe ufafanuzi kuhusu  leseni na umiliki wa eneo hilo. 
 
“Mhe. Naibu Waziri, kwanza kabisa niseme eneo hili lina leseni halali inayo milikiiwa na ndugu Omar Said Kojogo anae miliki kihalali kwa leseni Na. PML 36821 Southern Zone ya Tshs. 1,937,000. Na kwa mujibu wa sheria ya madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 hairuhusu kutoa leseni kwenye eneo moja ambalo teyari ilishatolewa na mahali hapa palishatolewa leseni kama nilivyosema, na kama itakuwa hivyo mlabda kwa kesi maalum, hata hivyo suala hili lilishashugulikiwa na muda si mrefu leseni yao itakuwa teyari” alisema Mhandisi Idd Msikozi. 
 
Kuhusu kilio cha masoko, Naibu waziri alisema kwanza anawashukuru wachimbaji hao kwa kitendo chao cha kulilia soko ili madini yao yakauzwe kwenye masoko rasmi. Amesema serikali imetoa agizo kila mkoa uwe na soko la madini ili serikali ipate fedha za kutosha kupitia madini ili fedha hizo zikatumike kwenye shuguli nyingine za maendeleo.
 
Amesema mpango wa sasa wa wizara ni kuhakikisha kuwa kuna vituo vya kununulia madini kwenye maeneo ya wachimbaji ili wanaporo wasitembee mwendo mrefu kufuata soko.
 
“Ndugu zangu wanaaporo, kiliochenu kuhusu soko kimenigusa sanaa, na sisi kama wizara ndio kitu ambacho tunakisisitiza kila mahali, kwa hiyo hapa hapa naagiza Afisa Madini Mkoa na Uongozi wa Wilaya kaeni chini kwa haraka mjadili ili kituo cha kununulia madini hapa kianzishwe  mara moja na serikali ianze kukusanya mapato yake”. Aliongeza Nyongo.
 
Baada ya kutolea majibu ya hoja za wachimbaji hao, Naibu waziri pia aliwaagiza wachimbaji kuanzisha mfuko wa mahafa na dharula ili uwezo kuwasaidia mara miongoni mwao anapopatwa na tatizo ahudumiwe kwa huduma ya awali huku akisubiri utaratibu binafsi wa kutatua tatizo lake.
 
Kwa upande mwingine Nyongo ameuagiza uongozi wa Wilaya zote mbili ukae pamoja na kuweka utaratibu utakao wezesha kuwa na kituo cha kutolea huduma ya kwanza kwa maana pawe na “Nurse” kwenye eneo hilo kwa utaratibu watakao ukubaliana. Aidha, halmashauri hizo ziweke vyoo maeneo hayo kwa kuwa wachimbaji hao wanalipa fedha serikalini hivyo wanastahili huduma hiyo.
 
Wakati huo huo Naibu Waziri amewapongeza viongozi wa Wilaya zote mbili kwa jitihada zao za kutatua mgogoro huo awali kabla hajafika hasa katika kukubaliana namna kukusanya mapato ya kila upande kwani mapato yote yanakwenda kwenye mfuko mmoja wa serikali. 
 
Kwa upande wao viongozi wa wilaya ya Nachingwea Katibu Tawala Husna Sekibobo na Mkuu wa Wilaya ya Liwale Sarah Chiwamba kwa pamoja walimshukuru Naibu Waziri kwa kufika katika eneo hilo na kujione hali halisi kutoa majibu ya moja kwa moja ya hoja zilizo wasilishwa na waliahidi maelekezo na maagizo yake watayatekelezwa.
 
Ziara ya Naibu Waziri ilikuwa ya kukamilisha ratiba ya ziara ya Waziri wa Madini Doto Biteko aliesitisha ziara yake mkoani humo na kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya majukumu mengine.


Share:

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...


Share:

Tanzania Universities and colleges Prospectus 2019/2020

Download Undergraduate and Postgraduate Prospectus For all Universities In Tanzania – Undergraduate Prospectus 2019 / 2020 University Prospectus introduces you to life at University , describing the campus and detailing the services, admission requirements and facilities that the university provides for students. Details of all undergraduate programmes are provided. Download University Prospectus to Find a list of all… Read More »

The post Tanzania Universities and colleges Prospectus 2019/2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nyumba ya Biashara Inauzwa: Tabata Relini (DSM)

Nyumba ya Biashara Inauzwa: Tabata Relini (DSM)


Nyumba ina vyumba 6, iko main road (Tabata Reli)
Nyumba ina kiwanja cha sqm 400 kinafaa kwa kujenga jengo la Biashara (commercial building)

Bei ya nyumba hii ni tsh 105 milion na maongezi yapo.
Call 0758603077


Share:

VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE KUANZA AGOSTI 19.....MKUTANO WA BUNGE SEPT 3,2019



Share:

Wadaiwa Sugu Kodi Ya Ardhi Sikonge Kubanwa

Na Munir Shemweta, WANMM SIKONGE
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameiagiza idara ya ardhi katika halmashauri ya Sikonge mkoani Tabora kuhakikisha inawafikisha kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya wadaiwa wote sugu wa kodi ya pango la ardhi katika wilaya hiyo wanaodaiwa kiasi cha takriban milioni 150.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo tarehe 15 Agosti 2019 katika halmashauri ya Wilaya ya Sikonge wakati wa ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi sambamba na kukagua masiajala ya ardhi na mifumo ya ukusanyaji kodi kwa njia ya kielektroniki mkoani Tabora.

Dkt Mabula alishangazwa na idara ya ardhi katika halmashauri hiyo kushindwa kuwafikisha wadaiwa sugu wa kodi ya pango la ardhi kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba wakati sheria inaelekeza baada ya siku kumi na nne mdaiwa asipotii wito afikishwe kwenye Baraza.

Alisema, katika halmashauri ya Sikonge kuna baadhi ya wamiliki wa ardhi ambao kwa mara ya mwisho walilipa kodi ya ardhi mwaka 2000 lakini idara ya ardhi imeshindwa kuwadai ama kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria jambo alilolieleza kuwa halikubaliki.

Kaimu Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Sikonge Martin Ukongo alieleza kuwa ofisi yake tayari ilishasambaza ilani 105 kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi kuanzia januari hadi machi 2019 lakini baadhi yake pamoja na kushindwa kulipa hawajafikishwa kwenye Baraza la Ardhi jambo lililomfanya Naibu Waziri kuagiza hatua za kuwafikisha kwenye Baraza zifanyike.

Dkt Mabula pia ameigiza halmashauri ya wilaya ya Sikonge kupitia idara ya ardhi kuhakikisha inapima mashamba yote yaliyopo katika halmashauri hiyo na kueleza kuwa kutopimwa kwa mashamba hayo kunatoa fursa kwa wamiliki wake kutolipa kodi ya ardhi.

‘’Sikonge mna mashamba hayajapimwa wakati ni ya wafanyabiashara wakubwa hapa wanakwepa kulipa kodi why hamjawapimia na kuwapatia hati ili walipe kodi?’’ Alihoji Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula

Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Denis Masami alisema kuwa Wizara yake kwa sasa imeimarisha mfumo wa ukusanyaji kodi ya pango la ardhi kwa kurahisisha ukadiriaji na kufanya malipo kupitia kupitia simu ya mkonini jambo linalowarahisishia wamiliki kuepukana na usumbufu wa kufika ofisi za ardhi kwa ajili ya malipo.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Peres Magiri alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa katika kipindi cha mwaka 2018/2019 wilaya hiyo ilifanikiwa kukusanya kodi ya pango la ardhi shilingi milioni 29,127,334.50 sawa na asilimia 87.55 wakati lengo ilikuwa kukusanya milioni 33.2. Hata hivyo Magiri alisema wilaya yake imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kama vile kutoa matangazo na kuelimisha jamii kupitia mikutano umuhimu wa kulipa kodi kwa wakati.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Sikonge Joseph Kakunda alimpongeza Naibu Waziri Dkt Mabula kwa uamuzi wake wa kufanya ziara katika wilaya hiyo na kueleza kuwa huyo ni Waziri wa Ardhi wa kwanza kuitembelea wilaya hiyo toka ianzishwe.

Hata hivyo, Kakunda alimueleza Dkt Mabula kuwa wilaya ya Sikonge ni wilaya iliyoko nyuma   katika suala la Mapango wa Matumizi Bora ya Ardhi na kuomba Wizara ya Ardhi kuipa kipaumbele katika upimaji ili kuepusha migogoro ya ardhi hasa ile ya wakulima na wafugaji.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521


Share:

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kuanza Kwa Vikao Vya Kamati Za Bunge

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kuanza vikao vya kamati za kudumu siku ya Jumatatu tarehe 19 Agosti hadi tarehe 02 Septemba 2019, Jijini Dodoma, kabla ya kuanza kwa mkutano wa kumi na sita wa Bunge uliopangwa kuanza tarehe 3 Septemba 2019.

Taarifa iliyotolewa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa cha Bunge leo Ijumaa 16 septemba 2019 imesema pamoja na mambo mengine kamati tisa za sekta na kamati ya bajeti zitachambua taarifa za taasisi na wizara za Serikali kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali.

Mbali na kupokea taarifa mbalimbali za wizara/taasisi, kamati hizo zitachambua taarifa ya CAG.

Shughuli nyingine zitakazofanywa na kamati hizo ni pamoja na uchambuzi wa sheria ndogo, pamoja na uchambuzi wa taarifa za uwekezaji wa mitaji ya umma.


Share:

POLISI WAZUIA MKUTANO WA ZITTO KABWE....KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI WA ACT- WAZALENDO ACHUKULIWA KWA MAHOJIANO


Katibu wa  Itikadi na Uenezi wa ACT- Wazalendo, Ado Shaibu  amechukuliwa  na Jeshi la Polisi kwa Mahojiano  alipokuwa katika Makao Makuu ya chama hicho, Kijitonyama jijini Dar es salaam  akiandaa mkutano wa kiongozi mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kwa ajili ya kuzungumza na waandishi habari.

Jeshi la Polisi Kanda Maalim ya Dar es Salaam lilifika katika makao makuu ya chama hicho  na kuzuia  mkutano  huo ambao ulitarajiwa kufanyika leo Ijumaa Agosti 16,2019 saa 5 asubuhi.

Polisi waliwasili Makao Makuu ya chama hicho  na kumhitaji kiongozi yoyote wa chama baada ya kumkosa Zitto Kabwe.

"Ndugu waandishi huu mkutano usubiri kwanza, kwa hiyo ninawaomba mtawanyike mara moja," alisema askari mmoja.

Wakati waandishi wakitawanyika aliwasili Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mawasiliano wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu ambaye walimchukua  na kuondoka  naye kwa ajili ya mahojiano.


Share:

#Kimataifa: Israel yawazuia wabunge wa kiislamu wa Marekani kuingia nchini humo

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Israel imetangaza kuwa waziri mkuu Bw. Benjamin Netanyahu amewazuia wabunge wanawake wawili wa kwanza wa kiislamu kuchaguliwa kuwa wabunge wa Marekani, Rashida Tlaib na Ilhan Omar, kuingia nchini mwake kwa madai kuwa wanapambana na Israel.

Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya Rais Donald Trump kuandika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa Omar na Tlaib wanaichukia Israel na Wayahudi. 

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Bibi Nancy Pelosi amekosoa vikali hatua hiyo na kusema imeonyesha dalili ya udhaifu na kupunguza uadilifu wa Israel.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Marekani, viongozi hao wawili walikuwa na ziara ya kikazi Jumapili hii, ambayo pia ingelijumuisha wao kufika eneo tata la Temple Mount mjini Jerusalem, linalotambuliwa na Waislamu kama Haram al-Sharif.

Pia walikuwa na mpango wa kukutana na wanaharakati wa amani wa Israel na Palestina na kusafiri hadi ukingo wa Magharibi wa Jerusalem katika miji ya Bethlehem, Ramallah na Hebron.



Share:

PICHA: Rais wa Shelisheli Danny Faure Awasili Nchini kwa ajili ya kushiriki mkutano wa 39 wa SADC

Rais wa Shelisheli Danny Faure, amefika nchini na kupokelewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa, kwa ajili ya kushiriki mkutano wa 39 wa SADC utakaofanyika kesho.

Rais Faure ni Rais wa pili kuja nchini baada ya kutanguliwa na Rais wa Afrika Kusini


Share:

Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) Yatakiwa Kuwezesha Kampuni Nyingi Kuorodheshwa Soko La Hisa

 Na Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Serikali imeitaka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kuhakikisha Kampuni nyingi zinaorodheshwa katika Soko la hisa ili kuweka uwazi zaidi katika utendaji wa kampuni hizo na hivyo kuwezesha Serikali kukusanya kodi stahiki na kuchangia katika ongezeko la mapato ya Serikali.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara katika Mamlaka hiyo ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 katika Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Dkt. Kazungu, alisema kuwa CMSA iendelee kusimamia masoko ya Mitaji ya Dhamana kwa kuorodhesha Kampuni nyingi zaidi katika soko hilo la hisa kwa kuzingatia masharti ya kuorodheshwa kampuni ili kuongeza uwazi, utawala bora na ufanisi wa kampuni hizo kwa kuweka mazingira mazuri ya uendeshaji na uwazi wa hesabu zao, hatua itakayochangia kukuza uwekezaji na mapato ya Serikali hususani katika eneo la kodi.

“Muendelee na kasi ya kutoa elimu kwa wananchi wengi ili waweze kujiunga na Masoko ya Hisa hususani kwa wananchi walio katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi”, alieleza Dkt. Kazungu.

Alisema kuwa iwapo wananchi wengi watajiunga katika Masoko la Hisa kutawafanya kuongeza mapato yao lakini pia kushiriki katika umiliki wa uchumi wa nchi yao.

Dkt. Kazungu alisema kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa uchumi wa viwanda, uchumi unaotarajiwa kujengwa katika kipindi kifupi wakati wa kuelekea katika uchumi wa kati hivyo ni vema wawekezaji wakahimizwa kupata mitaji ya kuendeleza na kupanua uwekezaji kupitia masoko ya mitaji na kutoa fursa nyingi za uwekezaji kwa wananchi.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Bw. Nicodemus Mkama, amesema Mamlaka yake imeweka mkakati wa kutoa elimu kwa umma na wawekezaji mbalimbali jinsi ya kutumia masoko ya mitaji kupata fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo.

“CMSA inaendelea kutoa elimu kwa umma na kwa makundi mbali mbali ya wanataaluma, wanafunzi wa elimu ya juu, watunga sera ikijumuisha Kamati za Bunge. Elimu hii inalenga kuelimisha umuhimu na fursa ya masoko ya mitaji katika kukuza uchumi na ushirikishwaji wa wananchi katika Sekta ya Fedha hususani masoko ya mitaji” alifafanua Bw. Mkama.

Alisema kutokana na jitihada hizo, kwa sasa uhitaji katika uwekezaji katika Soko ni mkubwa, hii inawafanya kuongeza bidhaa zinazokidhi matakwa ya wawekezaji ndani na nje ya nchi.

“Hii imejidhihirisha hivi karibuni kwa kuongezeka kwa kampuni nyingi katika sekta ya fedha kuorodhesha hatifungani ikiwa ni njia sahihi ya taasisi hizo kupata fedha za mahitaji mbalimbali ya utoaji mikopo na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Alisema elimu hiyo pia imeleta matokeo chanya na mwitikio wa matoleo ya hatifungani za Kampuni ya Kuendeleza Sekta ya Nyumba – TMRC, Benki ya Biashara ya DCB na Benki ya Biashara ya NMB na unaonyesha wazi kuwa kuna ongezeko kubwa la uelewa wa wananchi kushiriki katika uwekezaji kwenye masoko ya mitaji.

Toleo la hatifungani ya NMB Bank limeweka historia kubwa katika maendeleo ya masoko ya mitaji hapa nchini kwa kupata kiwango cha shilingi bilioni 83.3, ikiwa ni mafanikio ya asilimia 333 ikilinganishwa na shilingi bilioni 25 zilizotarajiwa kukusanywa.

Bw. Mkama alisema kuwa mauzo hayo yamekuwa na idadi na thamani kubwa kuliko mauzo yote ya hatifungani yaliyowahi kufanyika hapa nchini, ambapo jumla ya wawekezaji 2,264 wameweza kushiriki. Kati ya wawekezaji hao, asilimia 99.5 ni wawekezaji wadogo wadogo, na wawekezaji Kampuni ni asilimia 0.5.

“Tumeshatoa maelekezo kwa watendaji na washiriki (wanaotoa dhamana) katika Masoko ya Mitaji kuhakikisha wanakuja na bidhaa zinazokidhi mahitaji ya wawekezaji ili kuvutia wawekezaji wengi zaidi watakao sababisha ongezeko la mapato yao na upatikanaji wa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo jambo litakalochangia kushiriki kikamilifu katika uchumi wa nchi”, alieleza Bw. Mkama.

Alisema kuwa katika utoaji wa elimu, CMSA inatumia mbinu mbalimbali za kibunifu ikiwa ni pamoja na kuweka mashindano kwenye Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania Bara na Visiwani kwa kuwezesha wanafunzi kujifunza elimu ya masoko ya mitaji kwa njia ya kujibu maswali na kuandika insha

Alibainisha kuwa, wanafunzi wanaofanikiwa kushinda nafasi ya kwanza hadi ya tatu wanapewa tuzo mbalimbali zikiwemo fedha taslimu kuanzia shilingi milioni moja hadi milioni 1.8 kama kivutio cha ushiriki huku wanafunzi walioshika nafasi 20 za juu wanazawadiwa shilingi laki 2 kila mmoja na kwamba washindi wa nafasi ya kwanza hadi ya tatu wa mwaka huu (2019) watapelekwa nchini Namibia kwa ziara ya mafunzo.


Share:

Mabalozi 42 watembelea mradi wa SGR.....Dr Wilibrod Slaa Ammwagia Sifa Rais Magufuli

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa amewataka mabalozi wa Tanzania kushirikiana na shirika hilo ili kuweza kuleta maendeleo ya mradi inayoendelea hapa nchini na pia kulitangaza taifa kwa ujumla.

Akizungumza na Mabalozi hao waliotembelea mradi mkubwa wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge(SGR) unaendelea, Kadogosa amesema kuwa mpaka sasa ujenzi umefika asilimia 60.4 hivyo amewashukuru mabalozi waliokuja kuangalia mradi wa kimkakati kwani kutawawezesha kulitangaza taifa kwa mazuri yanayoendelea.

“Kama tunaweza kutekeleza miradi hii kwa pesa yetu, watu wa nje wanatuheshimu kwahiyo uwekezaji mkubwa kama huu unawagusa wawekezaji wa nje kwahiyo sisi tunawashukuru mabalozi kuja kuangalia miradi hii hivyo watakaporudi huko watawaelezea watu wa huko miradi hii walioyoiona kwa ukubwa wake,”amesema Kadogosa.

Aidha, Kadogosa amesema kuwa gharama za kutengeneza fensi katika ujenzi wa reli hiyo kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro ni dola bilioni 1.2 kujumlisha na kodi na kutoka Morogoro kwenda Maktupola Singida ni dola bilioni 1.9 pamoja na kodi hivyo jumla ya gharama zitakazotumika ni takribani bilioni 3.1.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Swedeni, Wilibrod Slaa amewataka watanzania waweze kujivunia kumpata Rais mwenye kufanya maamuzi kwani wameona miradi mingi ikifanyika hapa nchini kwani hata nchi zilizoendelea wamekuwa wakifanya uwekezaji na ulipaji kodi ambazo zinasaidia kuibua miradi mbalimbali.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger