• Home
  • About
  • Support
  • Contact
  • Advertise

MASWAYETU BLOG

  • Home
  • Business
    • Internet
    • Market
    • Stock
  • Downloads
    • Dvd
    • Games
    • Software
      • Office
  • Parent Category
    • Child Category 1
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • Featured
  • Health
    • Childcare
    • Doctors
  • Uncategorized
Menu
  • Home
  • Business
    • Internet
    • Market
    • Stock
  • Downloads
    • Dvd
    • Games
    • Software
      • Office
  • Parent Category
    • Child Category 1
      • Sub Child Category 1
      • Sub Child Category 2
      • Sub Child Category 3
    • Child Category 2
    • Child Category 3
    • Child Category 4
  • Featured
  • Health
    • Childcare
    • Doctors
  • Uncategorized

Thursday, 8 August 2019

Mkongo: Kibongo ya Tatizo la Nguvu za Kiume

 Unknown     16:59:00     NEWS     No comments   
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- maumbile kusimama kwa kulegea
-  kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________

WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia


Share:
Read More →

AKINA MAMA WAANDAMANA KUOMBA TENDO LA NDOA ...WADAI WANA KIU SANA!!

 Unknown     16:49:00     NEWS     No comments   
Akina mama katika Kaunti ya Kiambu nchini Kenya wameandamana wakililia haki yao baada ya kukosa kutimiziwa mahitaji yao ya ndoa na waume wao.

 Akina mama hao Jumatano, Agosti 7,2019 waliandamana na kuteta kuwa kiu cha mapenzi kimezidi huku wazee wao wakiendelea kuwa magofu tu kitandani. 

Waandamanaji hao walisema wengi wa wanaume huondoka nyumbani saa moja asubuhi kwenda kubugia kinywaji kwenye maeneo yaliyogeuka kuwa mwizi wa mahaba kaunti hiyo.

 Susan Nyambura ambaye aliongoza maandamano hayo alisema hali ni mbaya sana katika maeneo ya Limuru mjini ambapo alidai kuna dada mmoja ambaye amewateka waume wao kwa kuwauzia pombe kwenye nyumba yake. 

Aliongeza kuwa kwa sasa akina mama wana wasiwasi kwani wazee wao wameshindwa kushiriki tendo la ndoa.

 "Wakifika kitandani atakuguza halafu anakuwacha kama hajakutosheleza. Sasa hata huwa hatutaki watuguse. Lakini tunashangaa tutazaa na kina nani?," alisema Nyambura. 

"Mama Wengi wameachana na mabwana wao kwani hawawezi kazi kitandani, na hawaleti chakula nyumbani," aliongeza. 

Kwenye maandamano yao, wakazi hao walimtaka Rais Uhuru Kenyatta kuingilia kati na kuwasaidia kupigana na pombe haramu.

 Walisema maeneo ambayo yameadhirika sana ni Limuru mjini, Nazareth, Ngarariga, Farmers Corner, Kwambira baadhi ya wengine. 
Chanzo- Tuko
Share:
Read More →

Kuzinduliwa Kwa Mfumo Rasmi Wa Mauzo Ya Mazao Ya Kilimo Kutaimarisha Maendeleo Ya Kilimo Na Ushirika Nchini– Mhe Hasunga

 Unknown     16:44:00     NEWS     No comments   
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo, Simiyu
Serikali imesema kuwa kuwa maendeleo ya Sekta ya Kilimo na Tasnia ya Ushirika nchini itaimarika baada ya kuzinduliwa mfumo rasmi wa mauzo ya mazao ya kilimo kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

TMX ina lengo la kuongeza ufanisi katika juhudi za Serikali za kurasimisha mifumo ya masoko ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu; kwa kuwaunganisha Wauzaji na Wanunuzi wa bidhaa, kuleta ushindani kwenye bei, kupunguza gharama za uendeshaji biashara na kuweka uwazi.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema hayo tarehe 8 Agosti 2019 wakati wa kilele cha maadhimisho ya sherehe za wakulima (Nanenane) zinazofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi Katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Amesema kuwa mbali na soko la bidhaa pia kuzinduliwa kwa Mfumo wa Kielektoniki wa usajili wa wakulima na mfumo wa kielekroniki wa Kusimamia Biashara (Agricultural Trade Management Information System – ATMIS) utaimarisha makusanyo ya maduhuli na tozo kwa kuhakikisha huduma zote za utoaji vibali, leseni na vyeti unafanyika kielektroniki na pia kudhibiti udanganyifu katika hati na nyaraka za huduma hizo.

Alizitaja faida zingine kuwa ni pamoja na Kuhakikisha kuwa kazi ya kumhudumia mteja inafanyika kwa wakati mara tu baada ya hatua zote za maombi ya utoaji vibali, na vyeti kumalizika na kuimarisha upatikaji wa taarifa na takwimu muhimu za uingizaji na usafirishaji mazao ya kilimo nje ya nchi na Kuondoa tatizo la nyaraka bandia ambalo huchangiwa na matumizi ya mfumo

Mhe Hasunga ameyataja maeneo maalumu ya kimkakati katika sekta ya kilimo ambacho kinafanyiwa maboresho ili kuimarisha usimamizi wa kilimo na kuwapatia Wakulima huduma kwa urahisi zaidi ambayo ni Bima ya Mazao, Ambapo wizara ya Kilimo imeanzisha mwongozo wa Bima ya Mazao kwa Wakulima ambao ukielekeza jinsi ya kujiunga, kutekeleza na kuwasilisha madai ili kumwezesha kulipwa fidia pale anapopata hasara.

Mapitio ya Sera na Sheria, Mhe Hasunga amesema kuwa Wizara imeanza na itaendelea kuipitia Sera ya Taifa ya Kilimo ya mwaka 2013 na sheria mbalimbali kwa lengo la kubaini maeneo ambayo yatapaswa kuhuishwa ili kwenda na hali halisi ya sasa na mwelekeo wa Serikali wa kubadili kilimo kuwa kilimo cha kibiashara.

“Mtazamo wa Wizara ni kuwa na Sheria moja itakayosimamia rasilimali watu, matumizi bora ya pembejeo, ardhi ya kilimo na maeneo mengine muhimu” Alikaririwa Mhe Hasunga

Zingine ni Mfumo wa upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo, Wizara inaendelea na zoezi la kupitia kwa kina mifumo iliyopo ya uzalishaji, uagizaji na usambazaji wa mbegu, mbolea na viuatilifu. Aidha wizara inaendelea kutoa elimu kwa Wakulima ili wazalishe kulingana na mahitaji ya soko na kufanya kazi kwa karibu na Taasisi nyingine zinazohusika na masoko nchini ikiwemo TANTRADE na Soko la Bidhaa (TMX).

Sambamba na hayo amesema kuwa wizara ya Kilimo imejipanga kuhakikisha kuwa kupitia Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (ASDP II) Sekta ya Uvuvi inaongeza ufugaji wa samaki wenye tija na endelevu katika mabwawa ili kuwe na uwezekano wa kuzalisha samaki wengi zaidi na kuondoa kabisa uvuvi haramu.

“Ni imani yangu kuwa kama ASDP II itatekelezwa vizuri, Tanzania itakuwa nchi ya kipato cha kati kabla ya mwaka 2025” Alisisitiza


Share:
Read More →

Tiba Halisi ya Tatizo la Nguvu za Kiume

 Unknown     16:44:00     NEWS     No comments   
*NKOLOMIJE*/
√Ni dawa bora ya mitishamba yenye kuimarisha, kurefusha na kukufanya uwe imara hata kama umelala pia huimarisha na kukuza  maumbile yaliyosinyaa na kuwa regevu

*📌SUPER GAFINA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri ya uume ulio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/


Bado hujachelewa

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM  AU UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO SIMU NO:/
*📞0752723508*


Share:
Read More →

Waziri Mkuu Atoa Maagizo Mazito Kwa Wizara Tano

 Unknown     16:29:00     NEWS     No comments   
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza Wizara za Kilimo, Viwanda na Biashara, Uvuvi na Mifugo kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji kutengeneza mkakati wa kuanzisha viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini.

Amevitaja viwanda kuwa ni pamoja na vya nyuzi, nguo, ngozi, maziwa, minofu, nyama, kubangua korosho, kutengeneza unga, mafuta ya kula, sabuni, usindikaji wa matunda na mbogamboga, “Kwani ndiyo msingi wa kauli mbiu yetu ya kufikia uchumi wa viwanda 2025”.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu amsema sambamba na mkakati huo, pia ameagiza kuimarishwa kwa vyama vya ushirika ili kumwezesha mkulima kuendelea kumiliki zao lake mpaka hatua ya kuuza sokoni. “Vyama vya ushirika vikiweza kuchakata mazao na kuyaongeza thamani vitamuwezesha mkulima kuwa na umiliki na kufaidika na bei ya soko”.

Amesema mfano uliooneshwa katika zao la Kahawa kupitia Chama Kikuu cha Ushirika Kagera (KCU) ni mzuri ambapo wanamiliki asilimia 100 ya Kiwanda cha Kukoboa Kahawa (BUCOP), pamoja na asilimia 54 ya Kiwanda cha Kuzalisha Kahawa – Tanganyika Instant Coffee (TANICA).

“Kwa upande wa Pamba, Nyanza Cooperative Union (NCU) walianza vizuri kwa kumiliki viwanda vinane vya kuchambulia pamba. Tunataka jitihada za namna hii zianzishwe katika shughuli za wakulima wetu na zilizopo ziimarishwe”.

Hivyo, ameitaka Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa kushirikiana na wadau, ifanye tathmini kwenye vyama vya ushirika vinavyomiliki viwanda ili kubaini hali ilivyo kwa sasa na kuweka mikakati ya kuvifufua na kuviongezea uwezo.

Amesema safari ya kujenga uchumi wa viwanda itaiwezesha Tanzania kuwa nchi yenye kipato cha kati imeanza na inaendelea vizuri na  matarajio yake ni kuona wananchi wote bila kujali tofauti za kiitikadi, wataendelea kuunga mkono juhudi hizo kwa kuwa maendeleo wanayoyapigania ni kwa manufaa ya wote waliopo leo na vizazi vijavyo.

Waziri Mkuu amesema kwa mantiki hiyo, kila Mtanzania hanabudi kuongeza bidii katika kufanya kazi, kupiga vita rushwa, kulipa kodi ya Serikali na kulinda rasilimali za Taifa ili ziweze kutumika sasa na kwa faida ya vizazi vyetu vijavyo.

“Niwaombe muendelee kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna ambavyo imeamua kwa makusudi kuanzisha miradi mikubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi inayoendelea kujengwa nchini ikiwemo reli ya kisasa ya mwendokasi, mradi mkubwa wa umeme wa Mto Rufiji, upanuzi wa viwanja vya ndege, bandari na ununuzi wa ndege kubwa”.

Amesema kuboreshwa kwa miundombinu hiyo, pamoja na mambo mengine kutachochea uwekezaji mkubwa katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, kurahisisha usafirishaji wa mazao, mifugo, samaki, na kupunguza gharama za uzalishaji na hivyo kuwezesha viwanda vya ndani kushindana kibiashara na bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya nje ya nchi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoawito kwa viongozi wa Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kuendelea kushirikiana na Wizara za Sekta ya Kilimo kuhakikisha viwanja hivyo vya Nyakabindi, vinakuwa kituo cha mafunzo ya wakulima, wafugaji na wavuvi. 

“Kumbukeni kuwa kila mmoja wetu akitimiza wajibu wake ipasavyo, maendeleo ya viwanda yanawezekana, ajira zitapatikana, uhakika wa chakula na lishe bora itakuwepo na sote kwa pamoja tutasonga mbele kufikia nchi yenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025”.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea na kukagua mabanda mbalimbali katika maoneosho hayo. Miongoni mwa mabanda aliyoyatembelea ni pamoja na banda la EPZA, NMB, CRDB, NBC, BOT kitengo cha mifumo ya malipo ya Kielektroniki ya Serikali, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na JKT.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.
 


Share:
Read More →

Ucheleweshwaji Malipo Ya Wakulima Kuwa Historia

 Unknown     16:29:00     NEWS     No comments   
*Ni baada ya Serikali kuzindua mfumo wa uuzaji wa mazao kupitia TMX

CHANGAMOTO ya ucheleweshwaji wa malipo kwa wakulima baada ya kuuza mazao yao inatarajiwa kuwa historia baada ya Serikali kuzindua mfumo wa uuzaji wa Mazao kupitia Soko la Bidhaa (TMX) ambao kuanzia mwaka ujao utaanza kutumika kununua na kuuza baadhi ya mazao ndani na nje ya nchi.

Ununuzi wa mazao ya wakulima kupitia Soko la Bidhaa unalenga kuongeza ufanisi katika mifumo ya masoko ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu kwa kuwaunganisha wauzaji na wanunuzi wa bidhaa, kuleta ushindani kwenye bei, kupunguza gharama na kuweka uwazi.

Uzinduzi wa mfumo huo umefanywa leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima nane nane Kitaifa kwenye viwanja vya maonesho Nyakabindi mkoani Simiyu kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

Waziri Mkuu amesema mfumo huo utawahakikishia wakulima upatikanaji wa malipo kwa muda mfupi na wanunuzi kuwa na uhakika wa kupata mazao na bidhaa zenye ubora na zinazotosheleza mahitaji yao.

“Baadhi ya mazao tunayotarajia kuanza nayo ni pamoja na dengu, choroko, mbaazi, ufuta, korosho, kahawa na kokoa. Mfumo huu utasaidia upatikanaji wa masoko ya uhakika na kwa uwazi na hivyo kuifanya nchi ijulikane kimataifa juu ya uzalishaji wa mazao hayo na mengine”.

Pia, Waziri Mkuu amesema katika kuhakikisha mafanikio yanapatikana kwenye sekta za kilimo, viwanda na biashara ni lazima soko la bidhaa lipewe ushirikiano kwenye ngazi zote kuanzia Wizara, Mikoa na Halmashauri za Wilaya ili mazao ya kimkakati pamoja na yale yenye changamoto ya masoko yauzwe kupitia soko hilo muhimu.

“Taratibu zote za unedeshaji wa biashara hiyo zikamilike kwa ushirikiano wa vyama vya ushirika, TAMISEMI, Wakala wa Stakabadhi Ghalani na Wizara ya Kilimo, Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Fedha na Mipango. “Pia elimu kwa wadau wote itolewe kwa muda wote ili kuwaandaa washiriki wa mnyororo mzima wa thamani za mazao”.

Waziri Mkuu amesema Soko la Bidhaa Tanzania ni taasisi iliyoanzishwa na kusimamiwa kwa mujibu wa Sheria ya Masoko ya Bidhaa ya mwaka 2015 na Kanuni za Masoko ya Bidhaa za mwaka 2016.

“Aidha, napenda kusisitiza kuwa kuanza kufanya kazi kwa mfumo huu ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ibara namba 22(g)(ii) ya 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2016/17– 2020/21) na Awamu ya Pili ya Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP II)”.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amezindua mfumo mwinginewa Kielektroniki wa Kusimamia Biashara za Kilimo (Agricultural Trade Management Information System – ATMIS).“Mifumo hii inalenga kuongeza ufanisi wa shughuli mbalimbali za kuendeleza sekta za kilimo nchini na kuimarisha biashara ya mazao na bidhaa za kilimo.

Vilevile, Waziri Mkuu aliongeza kuwa Serikali inasimamia utekelezaji wa BluePrint inayolenga kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini. “Kupitia BluePrint hiyo, changamoto mbalimabali zimeainishwa na kuwekewa utaratibu wa kutatuliwa”.

Amesema miongoni mwa changamoto hizo ni kuwepo kwa mlolongo mrefu wa kupata vibali na leseni za uwekezaji na biashara na wateja kulazimika kufuata vibali hivyo kwenye Ofisi za Taasisi zilizopewa mamlaka ya kutoa leseni na vibali hivyo.

“Niwapongeze Wizara ya Kilimo na Taasisi ya TradeMark East Africa kwa kusanifu na kuanza kutumia mfumo wa kielektroniki wa kutoa vibali, leseni na huduma za malipo kwa wafanyabiashara”.

Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa Wizara ya Kilimo kusimamia utekelezaji wa mfumo huo ili lengo linalotarajiwa na Serikali hususani kurahisisha biashara liweze kufikiwa. Pia, Taasisi na Idara zote zinazotumia mfumo huo zihakikishe zinatoa elimu kwa watumiaji na wadau wote wa mfumo kwa lengo la kuondoa urasimu katika kuwahudumia wateja.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema katika kutekeleza mkakati wa kuimarisha mfumo wa biashara za mazao nchini Serikali imetengeneza Mfumo wa Kielektroniki wa utoaji wa leseni, vibali na malipo ya huduma (ATMIS) ili kurahisisha biashara za mazao ya kilimo.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi wa Wizara ya Kilimo wahakikishe wanashirikiana na viongozi wa Wizara ya Viwanda na Biashara kusimamia mifumo hiyo sanjari na kupambana na wanunuzi nje ya mifumo iliyokusudiwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga amesema kuwa maendeleo ya Sekta ya Kilimo na Tasnia ya Ushirika nchini itaimarika baada ya kuzinduliwa mfumo rasmi wa mauzo ya mazao ya kilimo kupitia Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

Amesema kuwa TMX imeanzishwa kwa lengo la kuongeza ufanisi katika juhudi za Serikali za kurasimisha mifumo ya masoko ambayo imekuwa na changamoto kwa muda mrefu; kwa kuwaunganisha Wauzaji na Wanunuzi wa bidhaa, kuleta ushindani kwenye bei, kupunguza gharama za uendeshaji biashara na kuweka uwazi.

Mbali na soko la bidhaa pia amesema kuwa kuzinduliwa kwa Mfumo wa Kielektoniki wa Kusimamia Biashara (Agricultural Trade Management Information System – ATMIS) utaimarisha makusanyo ya maduhuli na tozo kwa kuhakikisha huduma zote za utoaji vibali, leseni na vyeti unafanyika kielektroniki na pia kudhibiti udanganyifu katika hati na nyaraka za huduma hizo.

Amesema faida zingine ni kuhakikisha kuwa kazi ya kumhudumia mteja inafanyika kwa wakati mara tu baada ya hatua zote za maombi ya utoaji vibali, na vyeti kumalizika.  Pia kuimarisha upatikaji wa taarifa na takwimu muhimu za uingizaji na usafirishaji mazao ya kilimo nje ya nchi na Kuondoa tatizo la nyaraka bandia ambalo huchangiwa na matumizi ya mfumo.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya Nane Nane ya mwaka huu inasema: - “Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Ukuaji wa Uchumi wa Nchi”.Kaulimbiu hiyo inakwenda sambamba na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kukuza uchumi wa viwanda na biashara, ikilenga kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, Pato la Taifa na wakati huo huo kupunguza umaskini.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally, Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina, Naibu Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Josephat Kandege, Naibu Waziri wa Madini, Stansalaus Nyongo pamoja na maafisa wengine wa Serikali.
 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:
Read More →

HOSPITALI YENYE HADHI YA KUWA HOSPITALI YA RUFAA YAFUNGULIWA KIJIJI CHA MARUA -KILIMANJARO

 Unknown     15:19:00     NEWS     No comments   
Hospitali mpya ya St Monica iliyojengwa na Taasisi ya Kirua Children Care Foundation katika kijiji cha Marua ,kata ya Kirua Vunjo Magharibi katika wilaya ya Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira akiwa ameongozana na Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia pamoja na Mwenyekiti wa Taasisi ya Kirua Children Care Foundation ,Padri Amedeus Macha wakielekea katika ufunguzi rasmi wa Hosptali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira akitia saini katika kitabu cha wageni alipofika katika Hosptali hiyo kwa ajili ya ufunguzi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Kirua Children Care Foundation ,Padri Amedeus Macha akimueleza jambo mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira wakati akitembelea vyumba vya kulaza wagonjwa katika Hosptali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira akitizama baadhi ya mashine zilizoko katika Hospitali hiyo.
Chumba cha kulaza wagonjwa.
Padri Amedeus Macha akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira chumba maalumu kwa ajili ya wanawake kujifungulia.
Baadhi ya Vifa vilivyopo maabara ya Hospotli hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira  akikata utepe kuashiria kufunguliwa rasmi kwa Hospitali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira akitoa kitambaa kufungua jengo hilo la Hosptali ya St Monica.
Padri Amedeus Macha akifanya Ibada mara baada ya kufunguliwa rasmi kwa Hospitali hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira akizungumza wakati wa ufunguzi wa Hospitali ya St Monica iliyopo jimbo la Vunjo wilaya ya Moshi.
Baadhi ya wananchi wakifuatilia hotuba ya Mkuu huyo wa mkoa.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo,James Mbatia akizungumza katika hafla ya ufunguzi rasmi wa Hospitali ya St Monica.
Baadhi ya wananchi waliofika katika ufunguzi wa Hospitali hiyo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Kirua Children Care Foundation ,Padri ,Amedeus Macha akizungumza katika ufunguzi wa Hosptli hiyo.
Mkuu wa mkoa wa Kiliamanjaro Dkt Anna Mghwira akiwa katika picha ya pamoja na wageni waliofika kwa ajili ya kushuhudia ufunguzi rasmi wa Hospitali ya St Monica iliyopo kijiji cha Marua ,wilaya ya Moshi .

  Na Dixon Busagaga wa Michuzi TV .

MBUNGE WA Jimbo la Vunjo ,James Mbatia ameshauri kuanzishwa kwa Utalii wa Tiba (Medical Tourism) katika eneo linalozunguka Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) ili kurahisha utoaji wa huduma kwa wageni wanaopata matatizo wakati wa kupanda mlima Kilimanjaro.

Mbatia aliyasema hayo jana wakati wa ufunguzi rasmi wa Hospitali ya St Monica iliyopo jirani na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro katika kijiji cha Marua ,kata ya Kirua Vunjo Magharibi,katika wilaya ya Moshi  huku akiiomba serikali kusaidia katika uboreshaji wa Miundombinu ya barabara.


Akizungumza  mara baada ya kufungua na  kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali Hospitali iliyojengwa na Taasisi ya Kirua Children Care Foundation Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira ameipongeza taasisi hiyo kwa kujenga Hosptali hiyo ambayo itasaidia kupunguza changamoto za kiafya kwa wakazi wa maeneo hayo na mkoa wa Kilimanjaro kwa ujumla.
.
Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya Kirua Children Care Foundation Padri Amedeus Macha amesema Hospitali hiyo itakayo kuwa na uwezo wa vitanda zaidi ya 100 imelenga kutoa huduma za matibabu kwa wazee na watoto ambao  kwa muda mrefu wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma za Afya.

Dkt.Bogias Mwamgunda ni mwakilishi wa mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro hapa akaeleza namna ambavyo Hosptali hiyo itasaidia Wazee na watoto katika kupambana na magonjwa yatokanayo na Baridi .

Taasisi za Dini katika jimbo la Vunjo zimekuwa mstari wa mbele katika uwekezaji wa masuala ya huduma za afya ,hali inayochangia urahishaji wa upatikanaji wa matibabu tofauti na ilivyokuwa kwa kutembea umbali mrefu  hasa nyakati za mvua na usiku .

Mwisho






Share:
Read More →

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

 Unknown     13:24:00     NEWS     No comments   
Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka, ni mtu aliye jaliwa kubuli Shufaa pia anatoa Duah  za Ruhia. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho,  UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu  Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!? Muone Akutatulie,
 
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa..Unataka nyota ing'ae Au huna hamu na Mkeo/ Mumeo.
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa.
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu.Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN

Mawasiliano: Sheikh Omary 0673531992. WhatsApp/Call
Tembelea Page ya @Mtabibu_Omar  @Mtabibu_Omar
Usome Makala Tofauti Tofauti Kama.


Share:
Read More →

Serikali Yawataka Wanunuzi Wa Pamba Waongeze Kasi

 Unknown     13:14:00     NEWS     No comments   
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wanunuzi wa zao la pamba katika maeneo mbalimbali nchini wahakikishe wanaongeza kasi ya ununuzi wa zao hilo ili wakulima waweze kupata fedha zao kwa wakati.

Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga pamoja na Manaibu Waziri wake kubaki katika mikoa yote inayolima zao la pamba hadi wakulima wote watakapolipwa fedha zao na kuhakikisha pamba yote iliyomo mikononi mwa wakulima inauzwa.

Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Agosti 8, 2019) wakati alipotembelea Chama cha Msingi cha Itemelo kilichoko eneo la Dutwa wilayani Bariadi, Simiyu kwa ajili ya kujionea mauzo ya zao la pamba.

Waziri Mkuu amesema ataendelea kusimamia mwenendo wa zao hilo kwa ukaribu lengo likiwa kuona wakulima wananufaika kwa kupata tija. “Ilani ya CCM ya 2015/2020 inasisitiza kilimo na inataka wakulima wapate masoko ya uhakika na tunalitekeleza jambo hilo na pamba yote itanunuliwa.”

Amesema Serikali inataka kuona pamba yote iliyoko kwa wakulima inatoka ili wakulima waweze kulipwa fedha ambazo zitawawezesha kujikimu kimaisha pamoja na kununua pembejeo kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa AMCOS wahakikishe wanawatambua wakulima kwa majina, maeneo wanayoishi pamoja na ukubwa wa mashamba yao ili waweze kuagiza pembejeo kulingana na mahitaji halisi.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewasihi wakulima kufungua akaunti katika taasisi mbalimbali za kifedha lengo likiwa ni kuhifadhi vizuri fedha wanazozipata kutokana na mauzo ya pamba ili ziweze kuwasaidia baadaye.

Pia, Waziri Mkuu amewasisitiza wakulima hao waendelee kutunza vizuri pamba yao na kuipeleka ghalani ikiwa katika hali nzuri ya usafi na ubora wa hali ya juu, kwani kwa sasa pamba ya Tanzania inasifika kwa ubora katika soko la dunia.

Kwa upande wa masoko hususan ya pamba, Waziri Mkuu aliwasisitizia wananchi wa Dutwa na Watanzania kwa ujumla kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. Magufuli inaendelea kuhakikisha uwepo wa masoko ya uhakika wa mazao yote hususan yale ya kimkakati.

Pia, Waziri Mkuu ameongeza kuwa moja ya agenda muhimu ya ziara yake ya Kiserikali aliyoifanya nchini Misri mwezi Julai 2019 ilikuwa ni kutafuta masoko ya uhakika ya mazao ya Tanzania likiwemo na zao la pamba.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally alipokaribishwa kuwasalimu wananchi alimshukuru Waziri Mkuu kwa kutoa msukumo katika ununuzi zao la pamba. Aidha alimuomba Waziri Mkuu aongeze msukumo zaidi ili wakulima walipwe fedha zao kwa wakati.

Naye,Waziri wa Kilimo Hasunga amesema kuwa hali ya malipo kwa wakulima wa zao la pamba kwa sasa ni ya kuridhisha kwa kuwa wakulima katika maeneo mbalimbali wameanza kulipwa.

Pia Waziri huyo amemuahidi Waziri Mkuu kwamba wataendelea kubakia katika mikoa inayolima pamba kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa mauzo ya pamba ili kuhakikisha wakulima wote wanalipwa fedha zao kwa wakati.

Kuhusu suala la makato ya fedha za pembejeo ambazo wakulima wanalalamikia kukatwa kiasi kikubwa kuliko kiwango halisi wanachostahili, Waziri huyo wa Kilimo amesema atalishughulikia.

Aidha,Mbunge wa jimbo la Bariadi, Andrew Chenge amesema amefanya ziara katika kata 20 kati ya 30 kwenye jimbo hilo na changamoto kubwa ya wananchi ni mauzo ya pamba. “Ujio wa Waziri Mkuu umeleta manufaa kwani wanunuzi wameanza kuja kwa kasi”.

Mbunge huyo amemuomba Waziri Kuu awafikishie salamu zao kwa Rais Dkt. John Magufuli kwamba wanamshukuru kwa namna anavyowajali wakulima mbalimbali nchini wakiwemo na wa zao la pamba.

Kwa upande wake, Mbunge wa jimbo la Itilima, Njalu Silanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Nsangali ambayo inanunua pamba amemuahidi Waziri Mkuu kwamba ifikapo kesho (Ijumaa, Agosti 9, 2019) saa nane mchana atakuwa amelipa sh. milioni 135 zinazohitajika na amcos ya Itemelo ili kulipia deni la pamba iliyoko ghalani.

Awali, Katibu wa Amcos ya Itemelo, Lucas Ephraim alimuomba Waziri Mkuu awasaidie kuyahimiza makampuni mbalimbali yanayonunua yapeleke fedha kwa wakati ili kukidhi makisio tarajiwa.

Katibu huyo alisema chama chao kinahudumia vijiji vitano vikiwa na jumla ya wakulima 2,665 wa pamba wenye jumla ya ekari 9,675. Pia chama chao kinahitaji sh. milioni 135.139 ili kulipia deni la pamba ambayo iko ghalani.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:
Read More →

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Yaupongeza Mfuko Wa Mawasiliano Kwa Wote Nchini

 Unknown     13:14:00     NEWS     No comments   
Na Mwandishi Wetu.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeupongeza Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) nchini kwa kuipa kipaumbele miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mfuko huo kwa upande wa Zanzibar.
 
Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Dk. Sira Ubwa Mamboya alipotembelea Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) jijini Dodoma akiongozana na mwenyeji wake Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Atashasta Nditiye (Mb) pamoja na ujumbe wake kutoka katika Wizara anayoiongoza. 
 
Akizungumza na Uongozi wa Mfuko huo, alisema UCSAF imetoa kipaumbele kwa miradi mikubwa mitatu ambayo itaongeza maendeleo ya matumizi ya TEHAMA Visiwani Zanzibar.
 
“Nawashukuru sana kwa kujenga vituo vya mawasiliano Zanzibar na minara ya mawasiliano ambapo inawawezesha wananchi kutuia huduma za mawasiliano kwa shughuli za kijamii na kiuchumi visiwani humo. Aidha, ameongeza kuwa amefurahishwa  na mkakati wa kuwahamasisha wasichana kujitokeza na kupata mafunzo katika programu ya Wasichana na TEHAMA, “Hii itawafanya wasichana wa Zanzibar kuwa mstari wa mbele kutumia TEHAMA na kuingia katika mfumo wa Elimu ya TEHAMA,” amesema. 

Pia, ameishukuru na kuipongeza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana  na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji katika kupanga na kutekeleza mipango mbali mbali inayohusu Sekta ya Mawasiliano kwa kuwa mawasiliano ni suala la Muungano. 
 
Naye Mhe. Nditiye (Mb) alisema kuwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imefarijika sana kuupokea ujumbe wa Mheshimiwa Dk. Mamboya ambao umekuja Tanzania Bara kujifunza na kubadilishana uzoefu kuendana na utendaji kazi wa kila siku wa taasisi za Mawasiliano kwani mawasiliano ni suala la Muungano. 

Nditiye alimhakikishia Mhe. Dk. Mamboya kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itahakikisha inaendelea kutoa ushirikiano kwa SMZ kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ili kuendelea kutekeleza majukumu na kuhudumia wananchi katika nyanja ya mawasiliano.
 
Wakati akitoa taarifa ya Wizara kwa ugeni huo, Nditiye alisema kuwa tayari Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imejenga na kufikisha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo Unguja inaunganishwa na Mkongo huo kupitia mkongo wa baharini uliopo kwenye waya wa umeme kutoka Dar es Salaam na Pemba imeunganishwa kutoka Tanga. 

Pia, aliongeza kuwa vituo kumi vya TEHAMA vimejengwa na UCSAF kwa gharama ya shilingi milioni 754.8 ambapo vituo sita vimejengwa Unguja na vituo vine vimejengwa Pemba na tayari kila kituo kimepewa kompyuta saba na printa moja kutoka UCSAF
 
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya UCSAF aliishukuru Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ya SMZ kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa Mfuko wakati wa kutekeleza miradi ya TEHAMA kwa upande wa Zanzibar. Alisema Wizara hiyo imekuwa karibu na Mfuko jambo ambalo limepelekea mafanikio ya miradi ya TEHAMA visiwani humo.
 
Akielezea utekelezaji wa miradi ya TEHAMA Visiwani Zanzibar, Kaimu Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Bibi Justina Mashiba amesema, jumla ya wasichana 40 kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamepewa mafunzo ya utengenezaji wa mifumo ya TEHAMA kutoka mikoa ya Kaskazini Pemba na Mjini Magharibi. Aidha alisema Mfuko umetoa vifaa vya TEHAMA kwa shule 16 Zanzibar, uboreshaji wa mawasiliano kwenye Kata 10 zenye vijiji 18 Zanzibar.
 
Ujumbe wa Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ukiongozwa na Mhe. Dkt. Sira Ubwa Mamboya pamoja na kutembelea Ofisi za Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, pia, ulitembelea mradi wa TEHAMA katika Shule ya ekondari ya Wasichana Msalato, Dodoma uliofadhiliwa na UCSAF na kutembelea mnara wa mawasiliano uliofadhiliwa na UCSAF uliopo Dodoma, Wilayani Bahi kijiji cha Makanda. Pia, ujumbe huo utaendelea na ziara yake kwa kutembelea taasisi mbalimbali za Mawasiliano za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Tanzania Bara.

Imetolewa na Prisca Ulomi,
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano


Share:
Read More →

Dampo la taka laendelea kuzigombanisha halmashauri mbili Njombe

 Unknown     13:14:00     NEWS     No comments   
Na Amiri kilagalila-Njombe
Baadhi ya madiwani akiwemo diwani wa kata ya Saja wilayani Wanging’ombe mkoani Njombe Adrew Mangula wamelitaka baraza la madiwani la halmashauri hiyo kuridhia hoja ya kutaka Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania atoe tamko rasmi juu ya matumizi ya dampo lilipo katani kwake linalotumiwa na halmashauri ya mji wa Makambako licha ya malalamiko yao kufikishwa kwa naibu waziri wa mazingira na baraza la taifa la mazingira(NEMC).

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani katika halmashauri hiyo,diwani huyo amesema kuwa anashindwa kuelewa kinacho endelea juu ya matumizi ya dampo hilo kwa kuwa naibu waziri wa mazingira na baraza la taifa la mazingira lilitoa zuio kwa halmashauri ya mji wa makambako kutotumia dampo hilo lakini bado linaendelea kutumika.

“Hivi ni waziri wa namna gani ambaye anaweza kuja kusema ,mimi naona sasa hivi anayeweza kusema neno ni Rais mwenyewe wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,labda mwenyekiti uridhie  kwa baraza lako hili tukufu kwamba Rais aseme neno ili kuwaokoa wananchi wale wa Itengeru na Saja maana yake hata sielewi nani anaweza kusema ni mkuu wa wilaya,mkuu wa mkoa, ni waziri ama ni nani mimi naona amebaki Rais”alisema diwani Mangula

Aidha madiwani wa halmashauri hiyo wamesema hatua za haraka zinatakiwa kuchukuliwa ikiwemo kufika mahakamani na kwenda kufunga dampo hilo ili kuwanusuru wananchi wao na athali ambazo zinaweza kujitokeza hapo baadae hususani magonjwa ya mlipuko.

“Sisi tunaona kuna mtu anafumba macho kwa maslahi yake,eneo lile lipo ndani ya halmashauri yetu tunajitambua sisi ndio wenyewe tununue makufuri tukafunge tuandike bango litakaloonesha ni marufuku kutumia hili”walisema madiwani

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Wanging'ombe Antony mawata amesema anashangazwa na kitendo cha halmashauri ya mji wa Makambako kuendelea kutumia dampo hilo licha ya zuio la naibu waziri na athali ambazo zinaweza kuwapata wananchi wa Saja.

“Ivi mamlaka yanayoendelea kutumia na kubeza nini na mkurugenzi wa Makambako nimewahi kumsikia akisema sasa tumeshapanga na tumeingiza kwenye bajeti na tunahela ya kwenda kutengeneza mifereji ili tuendelee kutumia hii sio sawa hawa wamepanga kutudhulumu na kuendelea kutuulia watu wetu”alisema Mawata

Hata hivyo hii leo hoja za madiwani wa halmashauri hiyo zimeibuka katika baraza la madiwani halmashauri ya mji w Makambako huku mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa makambako Hanana Mfikwa akisema kuwa wao wanaendelea kutumia dampo hilo kutokana na kibali halali ambacho wamekipata kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Njombe,na hakuna barua yoyote ambayo wameipata ya kuzuia wasiendelee kutumia dampo hilo.

“Kimsingi lile dampo ni la halmashauri yetu na lilijengwa na hao hao wanaolalamika wakiwa Wanging’ombe lakini wote tukiwa Njombe tulipanga kwa pamoja tukajenga hilo dampo,kwa hiyo sisi kama Makambako tulipewa barua rasmi na mkuu wa mkoa kwamba tutupe taka pale kwa hiyo tunategemea kupata barua kwa vyombo vyenye mamlaka,Nemc wamekuja ni sahihi lakini kama hawajatoa waraka wowote  kusimama kutupa taka pale sisi hatuwezi kusimama,lakini kimsingi lile dampo liko salama na wala halina madhara kwa kuwa hata wenyewe wanaweza kutumia”alisema  Hanana Mfikwa

Joseph Makinga ni katibu tawala msaidizi osifi ya Rais na serikali za mitaa tamisema mkoa wa Njombe,akizungumza katika baraza la madiwani halmashauri ya mji wa Makambako amesema kwa sasa swala hilo lipo mezani kwa mkuu wa mkoa wa Njombe lakini waendelee kuwa na subira kwani bado halijashughulikwa.

Zaidi ya miaka mitano sasa kumekuwa na mgogoro kati ya h almashauri hizo kuhusu matumizi ya dampo hilo


Share:
Read More →

Rais wa Venezuela asitisha mazungumzo na upinzani kutokana na vikwazo vya Marekani

 Unknown     12:59:00     NEWS     No comments   
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameilaumu Marekani kwa vikwazo ilivyoiwekea nchi hiyo na kuamuru wawakilishi wa serikali yake kutosafiri kuelekea Barbados kwa mazungumzo yaliyopangiwa kufanyika na wanasiasa wa upinzani. 

Taarifa ya serikali ya Venezuela imesema Maduro ameamua kutowatuma maafisa wake kwa mazungumzo hayo yaliyopangiwa kufanyika leo Alhamis na kesho pamoja na kiongozi wa upinzani Juan Guaido kutokana na uchokozi mkubwa unaoendelezwa na utawala wa rais Trump. 

Rais Trump ameagiza kufungiwa kwa mali zote za serikali ya Venezuela zilizoko Marekani na pia amezuia kufanyika kwa biashara ya aina yoyote na uongozi wa nchi hiyo.


Share:
Read More →

Mwalimu Atiwa Mbaroni Kwa Rushwa ya Laki Moja

 Unknown     12:59:00     NEWS     No comments   
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa Temeke, imemkamata Mwalimu Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi Real Hope iliyopo Mbagala Majimatitu, Dar es Salaam, Ayubu Mtondo kwa kosa la  kuomba na kupokea rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Mkuu wa Takukuru, Ramadhani Ndwatah, alisema mwalimu huyo alipokea Sh 100,000 ili kumsaidia kumrudisha kazini mtumishi mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa.

Ndwatah alisema Februari 28, mwaka huu, saa 11 jioni,  mwalimu huyo akiwa ofisini kwake, alipokea fedha za mtego ili aweze kumsaidia mtumishi wake aliyesimamishwa kazi kurudi kazini.

Alisema uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo umekamilika na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka kwa kosa la kushawishi kuomba na kupokea rushwa.


Share:
Read More →
← Newer Posts Older Posts → Home
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

  • MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG katika nusanusa yetu tumefanikiwa kunasa hii ambayo ilikuwa ikisubiriwa na watu wengi,ni kuhusu ...
  • UPDATED:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA SELECTION YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa m...
  • NECTA:HAYA HAPA MATOKEO DARASA LA SABA 2017
    NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2017 EXAMINATION RESULTS ANGALIA MATOKEO YAKO KWA KUBONYEZA MKOA WAKO HAPO CHINI, ...
  • MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI 10,027 WALIOKOSEA KUJAZA FORM ZA MIKOPO BODI YA MIKOPO 2016/2017
      KUONA MAJINA HAYO   << BONYEZA HAPA--PDF >>
  • BREAKING NEWS:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO MWAKA WA MASOMO 2016/2017
      Bodi ya mikopo ya elimu ya juu wametangaza majina ZAIDI YA 20000 ya wanafunzi waliopata mkopo 2016/2017. Kama utahitaji kuangaliziwa j...
  • MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SECOND ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa ma...
  • MPYA:HAYA HAPA MAJINA (KATIKA PDF) WANAFUNZI SPECIAL DIPLOMA WALIOPANGIWA KURUDI UDOM &VYUO VINGINE 2016
    >>> CLICK HERE FOR LIST OF SELECTED STUDENT - UDOM (53.28 kB)<<<  CLICK HERE FOR LIST OF SELECTED STUDENTS - TEACHER ...
  • ANGALIA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWAPAMOJA NA APPLICATIONS FOR ADMISSION INTO NON DEGREE (DIPLOMA AND CERTIFICATE) PROGRAMMES FOR ACADEMIC YEAR 2016/2017-NACTE
                      Nacte wametoa majina ya wanafunzi waliofanikiwa kuchaguliwa  katika vyuo mbalimbali  afya,ualimu ,kil...
  • MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SECOND ROUND VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017
    Habari yako, Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa mjini,Tumeamua kukuwekea list ya vyuo vikuu ambavyo vimetoa ma...

Unordered List

Pages

Blog Archive

  • ▼  2026 (71)
    • ▼  January (71)
      • NITASIMAMIA KILA MWANANCHI MWENYE UHALALI WA KUMIL...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 30, 2026
      • SERIKALI YATOA MIKOPO KIASI CHA SHILINGI MILION...
      • KIJANA APITIA MATESO MAZITO LAKINI AKAJA KUWA MTU ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 28,2026
      • TWIGA, TANGA CEMENT WAPEWA SAA 48 KUJISALIMISHA
      • WAASISI CCM RUVUMA WATOA WITO WA KUZINGATIA KATIBA...
      • CCM MIAKA 49: WAZAZI WAONGOZA MAPAMBANO YA UTUNZAJ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 27,2026
      • WAKULIMA TABORA WALALAMIKIA UPUNGUFU WA TAARIFA ZA...
      • RAIS SAMIA AMEIMARISHA UCHUMI GEITA KUPITIA UJENZI...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 25,2026
      • MV NEW MWANZA: MKOMBOZI WA UCHUMI NA BIASHARA KAND...
      • BILIONI 67 ZIMETUMIKA KUJENGA BARABARA NA MASOKO M...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 24, 2026
      • TUTACHUKUA HATUA KALI KWA WATAKAOTUMIA TAARIFA BIN...
      • MASLAHI YA TAIFA KWANZA: MAPINDUZI YA KIFIKRA NA K...
      • ILALA TUNAJIVUNIA RAIS SAMIA, AMETULETEA MAENDELEO...
      • WANANCHI WA UKONGA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUDUM...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 22,2026
      • Tanzia : MUASISI NA MWENYEKITI WA KWANZA WA CHADEM...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 21, 2026
      • KANISA LA MLIMA WA MOTO LAZINDUA MAOMBEZI YA KUIOM...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 20,2026
      • HUWEZI KUISHIWA PAWA UKIPANDA MLIMA LOLMALASIN
      • SIMBA WA TERANGA WANG’ARA MOROCCO, WANYAKUA UBINGW...
      • WANA SANTA RC BUNJU WAPIGWA MSASA MATUMIZI SAHIHI ...
      • SAUTI ZA WANANCHI: AMANI NDIO MSINGI WA MAENDELEO ...
      • WAZIRI AWESO ATAKA KAZI ZIFANYIKE USIKU NA MCHANA ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 18,2026
      • MCHINJITA AONYA SIASA ZA MIHEMKO, APINGA MIITO YA ...
      • VIJANA 5,746 WACHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UA...
      • WATUMISHI WAPYA TASAC WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 17,2026
      • HAPA KUNA MKAKATI PEKEE UNAOWEZA KUIFANYA BIASHARA...
      • WANANCHI MSATA WAFAIDIKA NA ZOEZI LA MEDANI LA EX...
      • KWA NINI UNAPOTEZA KAZI KILA MARA? USILAUMU UZEMBE...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 15, 2026
      • INAMAANISHA NINI WAKATI HUWEZI KUSHIKILIA KAZI KWA...
      • YANGA BINGWA MAPINDUZI CUP
      • MTOTO WANGU ALICHELEWA KUTEMBEA NA KUONGEA HATUA M...
      • WANAOSEMA 'SAMIA MUST GO' AKITOKA UNAMUWEKA NANI P...
      • MWANAMKE HUYU ANASIMULIA JINSI MGANGA WA JADI ALIV...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 13,2026
      • Tanzania: IPTL's Patience Pays Off in $168m Disput...
      • BILIONI 6.7 KUBORESHA AFYA YA MAMA NA MTOTO KAHAMA
      • PROF. MKENDA AIPONGEZA LALJI FOUNDATION KUUNGA MKO...
      • MAKAMU WA PILI WA RAIS KUZINDUA MASHINDANO MAKUBWA...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 9,2026
      • SERIKALI IMEFANIKISHA AJIRA 1400 NJE YA NCHI: SANGU
      • KILA MTU NILIYEMWAMINI ALIISHIA KUNISALITI, HADI N...
      • HAPPY BIRTHDAY MALUNDE!
      • VETA MOSHI YATAJWA MFANO WA MAFANIKIO YA ELIMU YA ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 8, 2026
      • KILA MTU NILIYEMWAMINI ALIISHIA KUNISALITI, HADI N...
      • SERIKALI YASEMA BARRICK NI MFANO WA KUIGWA KWA KUW...
      • START NEW YEAR 2026 WITH GOOD NEWS DOING BUSINESS ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 7,2026
      • RAIS MSTAAFU WA DKT. KIKWETE, AZINDUA JENGO LA AFI...
      • RAIS MSTAAFU WA DKT. KIKWETE, AZINDUA JENGO LA AFI...
      • CHADEMA WAJIFUNZE KUTOKA KITABU CHA HESABU: KUKIRI...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 5,2026
      • SH MILIONI 500 ZA RAIS SAMIA KWA TAIFA STARS NI UW...
      • TAHADHARI: ‘UTANDAWAZI NI CHUI’, TUJILINDE NA UTEK...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 4,2025
      • SHAMRASHAMRA ZA MWAKA MPYA 2026: AMANI YA TANZANIA...
      • CHIKAMBO AKAGUA MIUNDOMBINU KOROFI MASONYA TARURA ...
      • HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 3,2026
      • WANANCHI KIJIJI CHA LAJA WILAYANI KARATU WAISHUKUR...
      • WAKAZI WA JIJI LA DODOMA WAKISHEREHEKEA MWAKA MPYA...
      • DC NKINDA ACHUKUA HATUA ZA HARAKA KUTATUA KERO YA ...
  • ►  2025 (993)
    • ►  December (73)
    • ►  November (67)
    • ►  October (72)
    • ►  September (92)
    • ►  August (82)
    • ►  July (84)
    • ►  June (76)
    • ►  May (92)
    • ►  April (86)
    • ►  March (91)
    • ►  February (83)
    • ►  January (95)
  • ►  2024 (1017)
    • ►  December (89)
    • ►  November (89)
    • ►  October (73)
    • ►  September (94)
    • ►  August (86)
    • ►  July (85)
    • ►  June (86)
    • ►  May (94)
    • ►  April (92)
    • ►  March (101)
    • ►  February (30)
    • ►  January (98)
  • ►  2023 (1772)
    • ►  December (99)
    • ►  November (101)
    • ►  October (130)
    • ►  September (102)
    • ►  August (150)
    • ►  July (162)
    • ►  June (165)
    • ►  May (178)
    • ►  April (172)
    • ►  March (188)
    • ►  February (162)
    • ►  January (163)
  • ►  2022 (1846)
    • ►  December (173)
    • ►  November (161)
    • ►  October (190)
    • ►  September (188)
    • ►  August (185)
    • ►  July (146)
    • ►  June (116)
    • ►  May (130)
    • ►  April (126)
    • ►  March (120)
    • ►  February (136)
    • ►  January (175)
  • ►  2021 (7035)
    • ►  December (284)
    • ►  November (598)
    • ►  October (641)
    • ►  September (638)
    • ►  August (619)
    • ►  July (616)
    • ►  June (617)
    • ►  May (637)
    • ►  April (581)
    • ►  March (621)
    • ►  February (539)
    • ►  January (644)
  • ►  2020 (7392)
    • ►  December (597)
    • ►  November (589)
    • ►  October (586)
    • ►  September (618)
    • ►  August (680)
    • ►  July (625)
    • ►  June (614)
    • ►  May (591)
    • ►  April (606)
    • ►  March (632)
    • ►  February (624)
    • ►  January (630)
  • ►  2019 (7895)
    • ►  December (611)
    • ►  November (643)
    • ►  October (673)
    • ►  September (664)
    • ►  August (679)
    • ►  July (677)
    • ►  June (619)
    • ►  May (725)
    • ►  April (622)
    • ►  March (477)
    • ►  February (604)
    • ►  January (901)
  • ►  2018 (409)
    • ►  December (388)
    • ►  August (1)
    • ►  July (1)
    • ►  June (2)
    • ►  May (2)
    • ►  April (7)
    • ►  March (2)
    • ►  February (1)
    • ►  January (5)
  • ►  2017 (450)
    • ►  December (1)
    • ►  November (1)
    • ►  October (119)
    • ►  September (7)
    • ►  August (2)
    • ►  July (10)
    • ►  June (23)
    • ►  May (28)
    • ►  April (39)
    • ►  March (16)
    • ►  February (77)
    • ►  January (127)
  • ►  2016 (2803)
    • ►  December (246)
    • ►  November (198)
    • ►  October (274)
    • ►  September (286)
    • ►  August (251)
    • ►  July (233)
    • ►  June (260)
    • ►  May (309)
    • ►  April (210)
    • ►  March (233)
    • ►  February (264)
    • ►  January (39)
  • ►  2015 (1416)
    • ►  December (24)
    • ►  November (102)
    • ►  October (186)
    • ►  September (89)
    • ►  August (80)
    • ►  July (229)
    • ►  June (197)
    • ►  May (61)
    • ►  April (266)
    • ►  March (105)
    • ►  February (50)
    • ►  January (27)
  • ►  2014 (1347)
    • ►  December (21)
    • ►  November (33)
    • ►  October (51)
    • ►  September (43)
    • ►  August (40)
    • ►  July (202)
    • ►  June (287)
    • ►  May (328)
    • ►  April (159)
    • ►  March (61)
    • ►  February (118)
    • ►  January (4)

Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger