Wednesday, 9 January 2019

UPINZANI WAONYA MATOKEO YA UCHAGUZI NCHINI DRC

Mgombea wa urais wa upinzani nchini Congo DRC Martin Fayulu amewaonya maafisa wa uchaguzi dhidi ya ''kuficha ukweli'' huku hali ya taharuki ikiendelea kutanda baada ya matokeo ya uchaguzi kucheleweshwa.

Bwana Fayulu amesema watu wa Congo tayari wanajua  matokeo ya uchaguzi uliyofanyika Desemba 30 kuahirishwa kwa wiki moja.

Matokeo ya awali ya uchaguzi huo yalitarajiwa kutangazwa siku ya Jumapili ya Januari 6 lakini yakaahirishwa.

Uchaguzi huo ulikuwa wa kumtafuta mrithi wa rais Joseph Kabila, ambaye anaachia madaraka baada ya kuongoza nchi hiyo ya maziwa makuu kwa miaka 18.

Kabila ameahidi kwamba uchaguzi huo ambao ulikuwa umepangwa ufanyike miaka miwili uliyopita utakuwa wa kwanza wa kupokezana madaraka kwa njia ya kidemokrasia nchini DR Congo tangu taifa hilo lilipojinyakulia uhuru wake kutoka kwa Ubelgiji mwaka 1960.

Mrithi wake anayempendelea ambaye pia ni waziri wa zamani wa mambo ya ndani Emmanuel Shadary,anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa wagombea wa upinzani Martin Fayulu,tajiri mkubwa wa mafuta na Felix Tshisekedi, mwana wa kiume wa kigogo wa upinzani.

Chanzo:Bbc
Share:

Good News : Pakua Upya App ya Malunde 1 blog ...Imeboreshwa Kukupa Raha zaidi ...Bonyeza HAPA SASA

Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Share:

KUZIONA SIMBA NA JS SOUARA LAKI MOJA


Klabu ya soka ya Simba imetangaza viingilio vya mchezo wao wa klabu bingwa Afrika Jumamosi hii dhidi ya JS Souara kwenye uwanja wa taifa Dar es salaam.

Simba kupitia kwa msemaji wake Haji Manara imesema kiingilio cha chini ni shilingi 5,000 huku cha juu kikiwa ni laki moja.

''Viingilio vya mchezo mzunguko ni 5,000 huku VIP B ikiwa ni 10,000 lakini tutakuwa na tiketi za Platinums ambayo ni 100,000 itajumuisha kuchukuliwa na 'Luxury bus' kutoka Serena Hotel na kusindikizwa na polisi, jezi mpya ya Simba, 'Bites na soft drinks' muda wote utakaokuwa uwanjani pamoja na kurejeshwa Serena'', - Manara.

''Tunawasihi sana wanasimba na washabiki wote tujae kama kawaida yetu Jumamosi, na tuje kuhanikiza, tuje tukijua ujaji wetu ndio silaha yetu'', ameongeza Manara.
Share:

MAHAKAMA YAAMURU MWILI WA MAREHEMU UFUKULIWE ILI UCHUNGUZWE

Na Stephen Noel Mpwapwa . Mahakama ya Hakimu mkazi wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma imeamuru kufukufukuliwa kwa mwili wa marehemu Cosmas Msote aliye fariki miezi mitano ili ufanyiwe uchunguzi wa chanzo cha kifo chake. Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo baada ya kuwapo na ubishani Kati ya taarifa zilizo andikwa na Mganga wa hospital ya wilaya ya Mpwapwa juu chanzo cha kifo cha bwana Cosmas Msote aliye fariki dunia tarehe 5 October 2018. Kwa mujibu wa Hakimu mkazi wa Mahakama ya wilaya ya Mpwapwa bwana Pascal Mayumba amesema aliamua kutoa…

Source

Share:

HALMASHAURI ZA WILAYA KOTE NCHINI ZIMEAGIZWA KUTENGA FEDHA KUTOKA MAPATO YA NDANI,KWA KUSHIRIKIANA NA WANAINCHI KUJENGA NYUMBA ZA WATUMISHI WA JESHI LA POLISI.

MULEBA, KAGERA. Na Mwandishi wetu. Waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola ametoa agizo hilo jana Januari 8,2019 kwenye mkutano wa hadhara, uliofanyika uwanja wa Fatuma Muleba mjini mkoani Kagera na kwamba nyumba hizo zijengwe palipo na kituo cha polisi Lugola amesema askari wanatakiwa kuishi kambini kwenye makazi ya pamoja na kulinda maadiliyao ya kiutendaji wakiwa na familia zao badala ya kuishi mitaani na kukiuka misingi ya utumishi wa Umma na wengine kushawishiwa na rushwa Amesema halmashauri nyingi nchini kwa kutumia kamati za ulinzi na usalama zikijipanga zitaweza kuanzisha maboma…

Source

Share:

MAHAKAMA YAAMURU MWILI WA MAREHEMU UFUKULIWE ILI UCHUNGUZWE.

Na, Stephen Noel Mpwapwa . Mahakama ya Hakimu mkazi wa wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma imeamuru kufukufukuliwa kwa mwili wa marehemu Cosmas Msote aliye fariki miezi mitano ili ufanyiwe uchunguzi wa chanzo cha kifo chake. Mahakama hiyo imefikia waamuzi huo baada ya kuwapo na ubishani Kati ya taarifa zilizo andikwa na Mganga wa hospital ya wilaya ya Mpwapwa juu chanzo cha kifo cha bwana Cosmas Msote aliye fariki dunia tarehe 5 October 2018. Kwa mujibu wa Hakimu mkazi wa Mahakama ya wilaya ya Mpwapwa bwana Pascal Mayumba amesema aliamua kutoa…

Source

Share:

TIZAMA VICHWA VYA HABARI VYA MAGAZETI YA LEO YA TANZANIA JANUARI 9,2019.

Share:

Tuesday, 8 January 2019

BENKI KUU YA TANZANIA YATOA MAAGIZO

BENKI Kuu ya Tanzania(BoT) imetoa tangazo kwa umma kupitia tovuti yake (www.bot.go.tz) likiwataka watu na taasisi zote zinazofanya biashara ya huduma ndogo za fedha zilizoko Tanzania Bara (isipokuwa vyama vya ushirika vya akiba na mikopo – SACCOS) kutoa taarifa zitakazotumika katika utayarishaji wa Kanuni za Usimamizi wa Huduma Ndogo za Fedha. “Bali ni kukusanya taarifa za awali kuhusu huduma hizo, kama amnavyo ilivyoainishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa kupitisha Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018, lengo la sheria hiyo ni kuwalinda wadau…

Source

Share:

Picha : WAZIRI WA MAJI AMSWEKA RUMANDE MHANDISI WA MAJI SHINYANGA, AAGIZA WAHANDISI KUTEMBELEA MIRADI

Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso ameliagiza jeshi la polisi mkoani Shinyanga kumkamata mhandisi wa maji Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba  kushindwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mradi wa maji uliogharimu serikali kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni moja.


Agizo hilo amelitoa leo Januari 8,2019 wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Mwakitolyo kwenye mkutano wa hadhara ambapo wananchi waliopewa nafasi ya kuuliza maswali walijikita na changamoto ya upatikanaji wa maji kutokana na mradi uliopo kushindwa kutoa maji.

Hata hivyo majibu ya mhandisi wa maji Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba yalishindwa kujitosheleza licha ya serikali kutoa fedha kiasi cha shilingi bilioni moja,milioni mia nne na sitini na mbili.

Kufuatia kukosekana kwa majibu kuhusu namna pesa hizo zilivyotumika,Aweso alieleza kusikitishwa na ucheleweshwaji wa mradi huo akidai kuna uzembe wa Mhandisi huo hivyo kumwagiza Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Jasinta Mboneko na jeshi la polisi kumkamata mhandisi huyo.

“Mradi wa maji Mwakitolyo gharama yake ni shilingi bilioni 1.482 mpaka sasa serikali ya imelipa kiasi cha bilioni 1.462, sisi tunaumia sana wakati mwingine huyu angekuwa daktari si angeshaua watu, mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ita polisi peleka ndani mtu huyu” ,alisema Aweso.

Waziri Aweso pia alimuagiza kaimu mhandisi wa maji mkoa wa Shinyanga Julieth Payovela kuandika barua ya kujitathmini katika utendaji kazi wake,na kuwaagiza wahandisi wa maji nchini kutembelea na kukagua miradi ya maji iliyopo kwenye maeneo yao na kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo ili kufikia azma ya kumtua mama ndoo kichwani.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Solwa Ahmed Salum alisema wakazi wa jimbo hilo bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za miundombinu ya barabara, elimu, umeme na huduma za afya na kuiomba serikali kuwatazama wakazi wa jimbo hilo kwani wanajihisi kutengwa licha ya baadhi ya wataalamu kukwamisha juhudi za serikali kuwapatia wananchi wake huduma bora za kijamii.

“Jimbo la Solwa ni miongoni mwa majimbo nchini yanayokabiliwa na changamoto lukuki hasa katika sekta ya afya,elimu na miundombinu ya barabara, wananchi hawa hawana pa kukimbilia zaidi ya serikalini kutokana na mapato wanayoichangia serikali katika huduma za kimaendeleo” ,alisema Ahmed.

ANGALIA PICHA ZA MATUKIO HAPA CHINI

Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso  akizungumza na wakazi wa kata ya Mwakitolyo kwenye mkutano wa hadhara ili kusikiliza kero zinazowakabili - Picha zote na Malaki Philipo- Malunde1 blog
Mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba(kushoto) akihojiwa na Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso (kulia) kuhusu kushindwa kusimamia mradi wa maji kata ya Mwakitolyo.
Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso akizungumza na kuagiza Mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba akamatwe na polisi .
Polisi wakitekeleza agizo la kumshikilia na kumuweka chini ya ulinzi mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba.

Mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba akiwa chini ya ulinzi.
Wakazi wa kata ya Mwakitolyo wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea.
Tenki la maji Mwakitolyo,mradi wa maji ambao umeigharimu serikali kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni moja na mradi haujawanufaisha wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumza na wakazi wa kata ya Mwakitolyo.
Mbunge wa jimbo la Solwa Ahmed Salum akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wakati wa ziara ya Naibu waziri wa maji Mwakitolyo.
Wakazi wa Mwakitolyo wakiwa kwenye mkutano.
Awali Sada Khamis mkazi wa kijiji cha Mwakitolyo akieleza kero ya maji katika eneo hilo mbele ya Naibu waziri wa maji Juma Aweso.
Mwenyekiti wa kijiji cha Mwakitolyo Nuhu Nshomi akieleza changamoto za elimu,maji na umeme wakati wa mkutano.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko (wa kwanza kushoto), Naibu waziri wa maji Juma Aweso(katikati), Mbunge jimbo la Solwa Ahmed Salum(kulia) wakisikiliza kero za wananchi.
Mkutano ukiendelea...
Kaimu mhandisi maji Mkoa wa Shinyanga Julieth Pyovela akichota maji ya kunywa yanayopatikana Mwakitolyo baada ya kutakiwa anywe mbele ya Naibu waziri wa maji Juma Aweso.
Kaimu mhandisi maji Julieth Payovela akitekeleza agizo la kunywa maji alilopewa na Naibu waziri wa maji Juma Aweso.
Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso akinywa maji yanayopatikana Mwakitolyo.
Mbunge wa jimbo la Solwa Ahmed Salum akishiriki zoezi la kunywa maji ya Mwakitolyo.
Naibu waziri wa maji Juma Aweso akiwapigia simu wataalamu kutoka wizara ya maji kwa lengo la kuja kujiridhisha na majibu yaliyotolewa na Mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba kuhusu ucheleweshwaji wa huduma ya maji Mwakitolyo.
Mkutano ukiendelea
Afisa elimu kata ya Mwakitolyo Adam Lanja akieleza changamoto za elimu.
Awali Afisa tawala mkoa wa Shinyanga Albert Msovela (mbele kulia) akitoa taarifa ya mkoa kwa Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza ofisini kwake wakati Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso akipokea taarifa ya mkoa wa Shinyanga.
Mhandisi wa maji Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Sylivester Mpemba akielezea kuhusu miradi ya maji katika wilaya ya Shinyanga mbele ya Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso.
Maafisa kutoka SHUWASA NA KASHUWASA wakiwa katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Maji Juma Aweso. 

Picha zote na Malaki Philipo - Malunde1 blog

Share:

HUYU NDIO KOCHA ZAHERA AJA NA MPANGO HUU WA KUONDOA NJAA KWA WACHEZAJI WAKE WA YANGA

HUKU mashabiki wa Yanga wakiiona timu yao haina fedha na masikini kumbe wanajidanganya  baada ya kocha mkuu wao kipenzi, Mwinyi Zahera, kutamka wazi kwamba anaweza kuifanya klabu hiyo kumaliza ukata wa kifedha ndani ya miezi miwili kutokana na hazina kubwa ya wanachama na mashabiki iliyonayo. Yanga ni klabu kongwe nchini, lakini imekuwa ikishindwa kutumia rasilimali ilizonazo katika kujiletea maendeleo, huku baadhi ya wadau wakidai tatizo hilo linasababishwa na viongozi wanaojali masilahi yao binafsi na si ya klabu. Pamoja na kuwa na majengo mawili katika ya Jiji la Dar es Salaam,…

Source

Share:

SIMBA YAMUAANDAA BEKI HUYO KISIKI KUBEBA MIKOBA YA NYONI KWENYE MECHI NA WAARABU ,KOCHA MBELGIJI AFUMUA KIKOSI CHAKE

KOCHA Mkuu wa Simba, Mbelgiji Patrick Aussems, ameanza kumwandaa beki wake, Jjuuko Murushid, kuchukua nafasi ya Erasto Nyoni, ambaye hatakuwepo katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya JS Saoura ya Algeria Jumamosi ya wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. katika Mechi hiyo Simba wanahitaji kila aina ya njia kuwakalisha waarabu ambapo Nyoni ameondolewa katika mipango ya  kocha huyo katika mchezo huo wa kwanza wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuumia goti wakati wa mechi ya juzi ya Kombe la Mapinduzi…

Source

Share:

SHAMBULIO LA AIBU LAMFIKISHA MAHAKAMANI MWINGINE ASHITAKIWA KWA KUJARIBU KUBAKA

Watu wawili wamefikishwa mahakama ya wilaya ya Serengeti kujibu mashtaka katika kesi mbili tofauti mmoja akijaribu kubaka na mwingine akifanya shambulio la Aibu Mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya Ismael Ngaile mwendesha mashtaka wa Jamhuri Renatus Zakeo alisema katika shauri la jinai namba 2/2019 mshitakiwa Manyama Machota(36) mkazi wa kijiji cha Robanda wilayani hapa anashitakiwa kwa kosa moja la Shambulio la aibu Zakeo alisema mshitakiwa alitenda kosa hilo Juni 9 mwaka 2018 katika kijiji cha Robanda baada ya kumshika binti aitwaye Zawadi Peter(16) sehemu mbalimbali za mwili wake bila…

Source

Share:

YANGA WAANZA MIPANGO YA KUMTAFUTA MRITHI WA MANJI,WANACHAMA WAPEWA NENO HILI

WAKATI suala la Uchaguzi wa Yanga likiwa bado kizungumkuti huku ikitajwa uwenda siku ya uchaguzi kukatokea fujo ya kupinga uchaguzi,wanachama wa Yanga wametakiwa kujitokeza kwa wingi kwenye kampeni za uchaguzi ambazo zimezinduliwa rasmi leo katika Ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na viongozi wa Yanga pamoja na wale wa TFF kwa ajili ya kujaza nafasi zilizo wazi kuanzia ile ya Mwenyekiti iliyokuwa wazi baada ya Yusuf Manji kujiuzulu pamoja na Makamu Mwenyekiti na wajumbe wengine. Uchaguzi wa Yanga unatarajiwa kufanyika Januari 13 katika ukumbi wa Polisi Messi Oysterbay kuanzia…

Source

Share:

RC MAKONDA KUWAKAMATA WANAFUNZI WATORO

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amewataka wanafunzi wote waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kuripoti shuleni bila kisingizio chochote. Agizo hilo amelitoa mapema leo ofisini kwake wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuwataka wazazi kuwapeleka watoto wao mashuleni kujiandikisha kidato cha kwanza kwa wale waliofaulu na ikibainika mwanafunzi yeyote amefaulu kisha ameacha kwenda shuleni atakamatwa. “Tukibaini wewe ni mwanafunzi umefaulu halafu umeacha kwenda kwa sababu yoyote ile ya kisingizio tutakukamata,tunachotaka tutumie fursa hii watoto wote wa kitanzania na wanyonge ambao Rais Magufuli amekusudia wapate elimu…

Source

Share:

SPIKA NDUGAI ASUTWA KILA KONA,NI BAADA YA KUMTAKA CAG AJISALIMISHE ,WENGI WATAMANI KUONA CV YAKE

NI siku moja kupita tangu spika wa Bunge Job Ndugai akimtaka Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG)profesa MUSA ASSAD kufika mbele ya kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge Januari 21 mwaka huu  ili akajieleze na kuthibitisha maneno yake aliyoyatoa nchini Marekani wakati akihojiwa na chombo kimojawapo cha habari.Lakini hali na mapokeo kwa baadhi ya wasomi,viongozi na wanasiasa mbali mbali  nchini wamekuwa na mapokeo tofauti na kukosoa wazi wazi katika mitandao ya kijamii  juu ya agizo hilo kwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali.Agizo la Spika NDUGAI linatokana…

Source

Share:

MANARA : NITAONGOZA JESHI LA POLISI KUSAKA WANAOUZA JEZI FEKI ZA SIMBA


'Kwenye mambo muhimu yanayohusu klabu yangu nipo tayari nisiangalie mpira 'Yes' nitaongoza jeshi la polisi kusaka wanaouza jezi feki''.

Ni kauli ya msemaji wa Simba Haji Manara leo alipokuwa akiongea na wana habari kuelekea mchezo wa Klabu Bingwa Afrika hatua ya makundi dhidi ya JS Souara Jumamosi ya wiki hii.

Katika mchezo huo, Manara amesema moja ya jambo ambalo watalitilia mkazo siku hiyo ni kuuza jezi halisi za Simba na sio feki.

''Siku ya mchezo wetu dhidi ya JS Souara nitaongoza jopo la wanasimba wenzangu kwa kushirikiana na Polisi kukamata wale wote wanaoihujumu klabu kwa kuuza jezi feki'' ameongeza Manara.

Aidha Manara amebainisha kuwa wapinzani wao klabu ya JS Souara watafika hapa nchini Januari 10, na Ijumaa watafanya mazoezi kwenye uwanja wa Taifa ambao ndio utatumika kwenye mchezo wa Jumamosi.

Kwa upande wa kikosi cha kwanza cha Simba kinatarajiwa kurejea Dar es salaam kutoka Zanzibar kesho asubuhi tayari kwa maandalizi ya mchezo huo.

Chanzo- EATV
Share:

MAKONDA AFUNGUKA KUHUSU 'MA HOUSE GIRL DAR'


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema kuwa wanaoishi na wafanyakazi wa ndani, wanatakiwa kuona uchungu kuwatumikisha watoto wadogo wanaotakiwa kuwa shule.

Makonda ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na wanahabari, ambapo amesema kuwa kukaa na mtoto mdogo na kumuagiza kazi za nyumbani ni kuitumia vibaya kodi yao kwani Rais amelipia ada watoto wote.

"Rais Magufuli amelipa ada kwa watoto wote, muwaache wasome kwani kufanya hivyo ni kuharibu kodi zenu wenyewe maana ada iliyolipwa ni kodi zenu", amesema Makonda.

Aidha katika hatua nyingine amewataka wazazi kutowapeleka watoto kujiunga na elimu ya sekondari kwa kigezo cha mahitaji, kwani walitakiwa kujiandaa mapema pindi mtoto amemaliza darasa la saba na watakaofanya hivyo watachukuliwa hatua.

"Ada imelipwa na hakuna michango, lakini utakuta watu wanawaficha watoto kisa hana hela ya sare na madaftari", amesema Makonda.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger