Thursday, 17 March 2016

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MARCH 17 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

Taarifa ya Wizara kuhusu filamu iliyompatia tuzo Elizabeth Michael "Lulu"

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kumekuwa na minongono mingi kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu Filamu ya Mapenzi ya Mungu ya msanii Elizabeth Michael (Lulu) iliyoshinda tuzo ya Filamu bora Afrika Mashariki mapema mwezi huu huko Lagos Nchini Nigeria katika tuzo za African Magic Views Choice Award (AMVCA).

Ili filamu ikamilike inahusisha watu mbalimbali wanaoshirikishwa kukamilisha filamu kuanzia mtoa wazo ambaye wazo hilo huwekwa katika mswada na mtaalamu jambo ambalo haliondoshi umiliki wa filamu.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa mmiliki halali wa Filamu ya Mapenzi ya Mungu ni Msanii Elizabeth Michael (Lulu) na ndiye aliyepata tuzo kwani ana haki zote za kupata tuzo hiyo kama mmiliki halali wa filamu hiyo.

Filamu ya Mapenzi ya Mungu imetengenezwa chini ya kampuni ya Proin Promotion na imesajiliwa kwa namba ya usajili CO831190.

IMETOLEWA NA
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
Share:

Mhandisi wa Maji Nyumbani Kwa Rais Magufuli atumbuliwa jipu na Waziri mkuu Majaliwa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rungu la kuwatumbua majipu watumishi wa umma wasiowajibika limetua kwa Mhandisi wa Maji Wilaya ya Chato, Peter Ngolemi baada ya Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa kuagiza kusimamishwa na kuamuru Takukuru kumchunguza kutokana na kumdanganya. 

Ngolemi, anadaiwa kumdanganya Majaliwa kuhusu mradi wa maji katika Kijiji cha Kalebezo ambao umesababisha wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo.
 
Mradi huo umesimama tangu mwaka 2011, kutokana na kukosa usimamizi baada ya mashine mbili kutofanya kazi. Licha ya kumsimamisha, Waziri Mkuu aliagiza Takukuru kumchunguza na kumchukulia hatua za kisheria. 

“Hatuwezi kuwa na kiongozi muongo, naondoka naye. Mtumishi huyu atakaa pembeni Takukuru wamchunguze,” alisema.

Kabla ya kuchukua uamuzi huo, Majaliwa alimwita jukwaani na kumtaka ajibu madai ya wananchi kukosa maji muda mrefu.

“Mheshimiwa Waziri Mkuu, kuna mashine mbili na hili suala lipo kwa Mamlaka ya Maji Bukoba, lakini zile pampu mbili zipo,” alijibu Ngolemi huku akitetemeka na wananchi wakimzomea.

Hatua hiyo ilisababisha Majaliwa kusema: “Huwezi kumdanganya Waziri Mkuu anayetegemewa na wananchi wengi, nimepita pale wananchi wana mabango wanadai mashine ziling’olewa na kupelekwa Morogoro, halafu leo unaniambia zipo!

“Sasa naondoka na wewe, kaa pembeni kuanzia sasa hakuna kazi, Takukuru mchunguze na kumchukulia hatua.”

Baada ya agizo hilo, maofisa wa usalama walimchukua mhandisi huyo na kuondoka naye kwenye Uwanja wa Chato.

Katika hatua nyingine, Majaliwa ameagiza kufutwa kwa umiliki wa mashamba makubwa 11 yakiwamo ya Kanisa Katoliki Jimbo la Rulenge yenye ukubwa wa ekari 7,700 kwenye vijiji vya Kasharazi na Rwakalemera, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, kutokana na kutokuwa na hati na kutelekezwa kwa muda mrefu.

Pia, Majaliwa ameagiza kusimamishwa kazi kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Colnel Ngudungi na kutaka arejeshwe wilayani hapa kujibu tuhuma za kuhusika na upotevu wa fedha za mauzo ya mbao kwenye Msitu wa Rumasi.

Ngudungi alihamishwa kwenda Sekretarieti ya Mkoa wa Shinyanga Agosti 2015, kwa kile kilichoelezwa kuwa anakwenda kwa kazi maalumu.

Majaliwa ambaye alikuwa njiani kuelekea Geita akitokea Kagera, alitoa maagizo hayo jana alipozungumza na wakazi wa vijiji vya Kasulo na Rwakalemera, baada ya kusimamishwa na wananchi wakiwa na mabango wakiomba kurejeshewa ardhi ya kijiji huku baadhi yao wakidai wanatishiwa kwa bunduki wanaposogelea mashamba hayo.

Waliendelea kuwa uongozi wa kijiji umekithiri kwa ubadhirifu kwani licha ya Msitu wa Rumasi kuuzwa na mapato kutoonekana, kijiji kina minada ya ng’ombe ambayo sheria inataka asilimia 20 ya mapato ibaki eneo hilo.

Awali, Waziri mkuu alimuita kwenye mkutano huo Ofisa Ardhi na Maliasili wa Wilaya, Betty Munuo ili aeleze chanzo cha mgogoro wa ardhi katika vijiji hivyo.

Akitoa ufafanuzi huo, Munuo ambaye amehamishiwa wilayani hapo Agosti mwaka jana, alisema malalamiko hayo ameyarithi kwa mtangulizi wake na amefanya uchambuzi wa majina ya wamiliki wote wa mashamba na kwamba, uongozi wa wilaya ulikuwa unapanga kuwapatia notisi ya kujieleza.

Munuo alisema kati ya wamiliki 18 wa mashamba makubwa, saba ndiyo wenye hati huku matatu pekee ndiyo yameendelezwa.

Kwa mujibu wa Munuo, mashamba yaliyoendelezwa yanatumika kwa kilimo, ufugaji na shule na kwamba Shamba namba 606 lenye ukubwa wa ekari 161 linamilikiwa na Kanisa Katoliki Dayosisi ya Rulenge, Dario Zakaria shamba ana ekari 282 na Masista wa Mtakatifu Fransisco wanamiliki ekari 759.

“Mashamba manne ndiyo yenye hati lakini yametelekezwa, yaliyotelekezwa yote yapo Kijiji cha Rwakalemera nayo ni ya Abdallah Sadalla (ekari 521); Mahsen Saidi (458); Mshengezi Nyambele (3,88) na Mushengezi Nyambele (497).

Majaliwa aliwataja wamiliki wa mashamba yasiyo na hati kuwa ni Joseph Rugumyamheto (505) lipo Rwakalemera, Nicholaus Kidenke, Gwasa Angas Sababili (236) lipo Kasharazi na Makumi Rufyega (500) lipo Rwakalemera.

Wamiliki wengine ambao mashamba yao yapo kijiji cha Rwakalemera na ukubwa wake kwenye mabano ni Paulo Shikiri (250), Frank Derila (750), Godfrey Kitanga (800), Phillemon Mpanju (200), Issa Sama (500), Hekizayo Mtalitinya (225) na Joel Nkinga (1,250).

Majaliwa aliagiza kurejeshwa mara moja aliyekuwa Ofisa Ardhi wa Wilaya hiyo, Enock Mponzi ambaye amehamishiwa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya mkoani Mara ili aende kusaidia uchunguzi.
Share:

Magufuli Apiga MARUFUKU Kukodi Mitambo ya Kuzalisha Umeme

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli jana tarehe 16 Machi, 2016 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Kinyerezi namba mbili, uliopo katika wilaya ya Ilala Mkoani Dar es salaam, ambao utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kuzalisha megawatts 240 za umeme.
 
Mradi huo ambao utazalisha umeme kwa kutumia gesi asilia inayosafirishwa kwa bomba kutoka Mtwara, unatarajiwa kuanza kuzalisha umeme katika kipindi cha kuanzia miezi 21 hadi 28 utakapokamilika kabisa.
 
Kuanza kwa ujenzi wa mitambo ya kuzalisha umeme huo, kunafuatia juhudi zilizofanywa na serikali ya awamu ya tano ya kufanikisha upatikanaji wa shilingi bilioni 120, ikiwa ni asilimia 15 ya fedha zilizopaswa kutolewa na Tanzania na fedha nyingine shilingi Bilioni 292 zimetolewa na Japan.
 
Mradi huu umetanguliwa na mradi wa Kinyerezi namba moja ambao una uwezo wa kuzalisha megawatts 150 za umeme, na mitambo yake tayari imeanza uzalishaji wa megawatts 105 zilizoingizwa katika gridi ya Taifa.
 
Pamoja na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa Kinyerezi namba mbili, Rais Magufuli amekagua mitambo ya kuzalisha umeme ya mradi wa Kinyerezi namba moja, ambapo Mkuu wa Kituo cha Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) cha Kinyerezi Mhandisi John Mageni, ametoa maelezo kuwa shirika hilo lina mpango wa kupanua uzalishaji wa umeme katika mradi huo kutoka megawatts 150 hadi kufikia megawatta 335, kwa kuongeza mitambo ya kufua umeme kwa teknolojia inayojumuisha matumizi ya gesi asilia na mvuke uzalishwao na mitambo hiyo.
 
Baadaya ya kupokea maelezo hayo, Rais Magufuli ameridhia kuwa serikali yake itatoa Dola za kimarekani milioni 20, kwa ajili ya kufanikisha upanuzi wa mradi huo na ameagiza kuwa wataalamu wa TANESCO washirikiane na Mkandalasi kuhakikisha upanuzi huo unafanyika haraka iwezekanavyo, badala ya muda wa miezi 12 uliopangwa.
 
Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika sherehe za uzinduzi wa mradi huo, Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati na Madini na TANESCO, kuanza kuachana na mitambo ya kukodi kwa ajili ya kuzalisha umeme, na badala yake nchi ijenge mitambo yake yenyewe ili kuondokana na gharama kubwa za nishati hiyo muhimu.
 
“Waziri, ukiona mtaalamu anakuletea mapendekezo ya kutaka kukodi mitambo ya kuzalisha umeme, badala ya kuleta mapendekezo ya kununua mitambo yetu wenyewe ujue mtaalamu huyo hafai, mtoe” Amesisitiza Rais Magufuli
 
Ameongeza kuwa tafiti zimethibitisha kuwa hadi sasa Tanzania ina zaidi ya futi za ujazo Trilioni 57 za gesi asilia, ambayo itazalisha umeme wa kutosheleza mahitaji ya ndani, na umeme mwingine kuuzwa nje ya nchi ikiwemo Kenya ambayo tayari imeomba kuuziwa umeme kutoka Tanzania.
 
Aidha, Rais Magufuli ametoa onyo kwa TANESCO kuwa hatarajii kusikia bwawa la maji la Mtera limeishiwa maji, kwa kuwa katika msimu huu wa mvua maeneo ya Iringa yalikuwa na mvua nyingi ambazo zimesababisha hadi mafuriko mafurukio.
 
Kwa upande wake, Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo amesema tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, juhudi zilizofanyika zimefanikisha kuongeza uzalishaji wa umeme kutoka megawatts 800 hadi kufikia megawatts 1,000 kiasi ambacho ni pungufu kwa megawatts 20 tu, ikilinganishwa na mahitaji ya megawatts 1020 za sasa.
 
Ameongeza kuwa pamoja na kuweka jiwe la msingi la mradi wa Kinyerezi namba mbili, hivi karibuni serikali inatarajia kujenga miradi mingine ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia, ikiwemo Kinyerezi namba tatu utakaozalisha megawatts 600, Kinyerezi namba nne utakaozalisha megawatts 300, na mingine itakayojengwa Lindi na Mtwara.
 
Prof. Muhongo amebainisha kuwa mpaka sasa gesi asilia inazalisha kati ya asilimia 50 na 60 ya umeme wote hapa nchini, Maji yanazalisha asilimia 30 hadi 40, na umeme unaozalishwa kwa mafuta hauvuki asilimia 10.
 
Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa Japani hapa nchini Mheshimiwa Masaharu Yoshida, Wabunge wa kamati ya Nishati na Madini, wafadhili wakiwemo Benki ya Dunia, Benki ya Afrika na Shirika misaada la Japan (JICA.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
16 Machi, 2016
Share:

Waziri Kitwanga Afanya Mazungumzo Na Wakuu Wa Vyombo Vya Ulinzi Na Usalama Zanzibar

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga amewataka wananchi wa visiwani Zanzibar kujitokeza kwa wingi Machi 20, 2016 ili waweze kupiga kura kwa amani na utulivu bila kubughudhiwa na mtu yeyote.
 
Kitwanga amesema kuwa ulinzi umeimarishwa na kuwataka wananchi visiwani humo kujitokeza kwa wingi kuja kumchagua kiongozi wanaompenda siku ya uchaguzi huo na watarejea nyumbani kwao salama mara baada ya kumaliza kupiga kura.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi Makao Makuu ya Polisi Zanzibar na baadaye kuzungumza na Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama, Waziri Kitwanga alisisitiza kuwa, vyombo vya ulinzi na usalama vimejiandaa vizuri na wananchi waondoe shaka kwani hawatakubali vurugu ya aina yoyote itokee.
 
“Jitokezeni kupiga kura siku ya uchaguzi kwani ni haki yenu, nawahakikishia usalama upo na wa hali ya juu, asijitokeze mtu yeyote akawatisha kutokuja kupiga kura, tumejipanga vizuri na lengo letu kubwa kabisa ni kuwalinda wananchi,” alisema Kitwanga.
 
Hata hivyo Waziri Kitwanga alisema hakuna mwananchi yeyote anayehama kwakuogopa vurugu siku ya uchaguzi bali watu wanasafiri kwasababu mbalimbali ikiwemo hiki ni kipindi cha maandalizi ya Sikukuu ya Pasaka, baadhi ya wananchi wanaenda kula sikukuu maeneo mbalimbali nchini na wengine wanasafiri kutokana na majukumu mbalimbali na sio wamekuwa wakimbizi wakikimbia sehemu zao kama inavyoenezwa.
 
“Acheni kusikia habari za mitaani amani ipo, jitokezi kupiga kura na hii habari mnayosikia eti watu wameanza kuyakimbia makazi yao ni uzushi tu, hakuna kitu kama hicho, wananchi wanaendelea na shughuli zako kama kawaida na vyombo vya ulinzi vimejipanga kwa ajili ya kulinda usalama wa raia na mali zao,” alisema Kitwanga.
 
Waziri Kitwanga aliwasili Zanzibar jana kwa ajili ya ziara ya kikazi ya kuimarisha usalama  zaidi visiwani humo pamoja na kujua mikakati iliyowekwa na vyombo vya ulinzi na usalama kuhusu usimamizi wa uchaguzi huo.
Share:

Wednesday, 16 March 2016

TAARIFA MUHIMU KWA WANAFUNZI WOTE WA UDOM WANASOMESHWA NA BODI YA MIKOPO-HESLB

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


THE UNIVERSITY OF DODOMA
THE DIRECTORATE OF UNDERGRADUATE STUDIES  

ATTENTION TO ALL STUDENTS WITH LOANS PROBLEMS
The Directorate of Undergraduate Studies needs to clear all problems that are facing
 loans beneficiaries. 
Therefore all students with loans allocations but have not received meals and accommodation
 for quarter I or/and II payments should register their cases with the Director of Undergraduate
 Studies.
This special exercise will start on 15th March and will be closed on 18th March 2016. Required 
details will be as indicated below:-
S/N
FORM IV INDEX NO.
NAME
SEX
REG.NO.

YOS

QUARTER I

QUARTER II
PROGRAMME
BANK
NAME
ACCOUNT NO.


Issued by the Office of the DVC-ARC
14th March, 2016
Share:

NAFASI ZA MASOMO CHETI NA DIPLOMA MWAKA WA MASOMO 2016/2017-SUA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Image result for SUANET

Application for Admission into Certificate and Diploma Programmes 2016-2017

Sokoine University of Agriculture invites applications from qualified Tanzanians and non-Tanzanians to certificate and diploma programmes offered by the University for academic year 2016/2017.
Read More:
Share:

MAJINA MAPYA YA WANAFUNZI WA ST.JOSEPH WALIOHAMISHIWA SUA,RUCO NA UDOM 2016

Share:

Mkuu Mpya Wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Mustafa Kijuu Atoa Onyo Kali Kwa Majambazi na Wahalifu.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Mustafa Kijuu amewataka watu wote wanaopindisha sheria, majambazi na wahalifu wote kutafuta kazi nyingine halali za kufanya.

Meja Kijuu aliyasema hayo baada ya kula kiapo cha utiifu na uadilifu kuwatumikia wananchi wa mkoa wa Kagera mkoa ambao upo pembezoni mwa nchi unaokabiliwa na matukio ya mara kwa mara ya uhalifu.

''Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyonayo kwangu na nitafanya kazi kwa kuzingatia yale ambayo ameyasema na kuhakikisha maendeleo yanapatikana''-Amesema Meja Kijuu

''Sitakubali watu wazurure hovyo na kuacha kufanya kazi za uzalishaji na nitahakikisha napambana na wahalifu wote kwa uwezo wote nilionao"-Amesisitiza Meja Kijuu.

Aidha Rais Magufuli aliwaapisha wanajeshi wastaafu Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Elias Kyunga, aliyekuwa Chuo cha Kamanda na Unadhimu (JWTZ) ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu, aliyekuwa Mkuu wa Kamandi ya Nchi Kavu ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Wengine ni Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga, aliyekuwa Makao Makuu ya Jeshi sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma lengo la Rais kuweka wanajeshi katika mikoa ya pembezoni ni kuleta usalama na kuimarisha amani katika mikoa hiyo.
Share:

MAAGIZO 12 YA RAIS MAGUFULI KWA WAKUU WA MIKOA,LIMO LA MAJAMBAZI NA VIJANA WACHEZA POOL

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


RAIS Dk. John Magufuli amewaapisha wakuu wa mikoa wapya 26, huku akiwapa maagizo 12 muhimu ikiwamo kuwaweka ndani watendaji wanaonyanyasa wananchi.

Pamoja na hayo, amesema kwamba baada ya kuapishwa kwa Kamishna mpya wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mkurugenzi wa Takukuru, anaamini watafanya kazi na mapato yanayokusanywa yanakwenda kwa wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Akizungumza jana Ikulu, Dar es Salaam baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa, alisema kwamba ni lazima nidhamu ya Serikali kwa wananchi wake iwe sambamba na viongozi na watendaji wa Serikali kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria.

Mkuu huyo wa nchi alikuwa akizungumza ikiwa ni utaratibu wake mpya tangu alipoteua viongozi ambapo awali alikuwa akiwaapisha na kuondoka bila kusema jambo lolote.

“Nimeamua kuwateua wakuu wa mikoa nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri katika mikoa yenu, napenda niwaombe mtakapowasili kwenye mikoa yenu mkitambua kwamba ninyi ndio wenyeviti wa kamati za ulinzi na usalama katika mikoa yenu na mnatuwakilisha sisi ambao tuko huku, mkatimize wajibu wenu.

“Kukubali kwenu kuapishwa na kusaini mtakuwa mmekubali kuingia kufanya kazi na mimi, nawapa pole kwa sababu mtakwenda kufanya kazi kweli kweli kutatua kero za wananchi, haiwezekani kero inajulikana mkoani na wewe upo ukisubiri hadi aje Waziri Mkuu, Makamu wa Rais au mawaziri au mimi kutatua, hiyo itajulikana kwamba mmeshindwa kazi,” alisema.



MISHAHARA HEWA

Akizungumzia juu ya uwepo wa mishahara hewa kwa wafanyakazi nchini, Rais Magufuli alisema kwa muda mrefu Taifa limekuwa likiumizwa kutokana na jambo hilo.

Kutokana na hali hiyo, amewataka wakuu wa mikoa yote nchini kuhakikisha wanakomesha vitendo hivyo ndani ya siku 15.

Alisema katika halmashauri nchini kuna uozo mkubwa ambapo alieleza namna walivyotuma watu kwa ajili ya kufanya utafiti katika mikoa ya Singida na Dodoma na kubaini mishahara hewa kati ya Desemba mwaka jana na Januari mwaka huu.

Rais Magufuli alisema katika mikoa hiyo walifanya utafiti kwa wafanyakazi 26,900 kwenye halmashauri 14 ambapo walibaini kuwapo kwa wafanyakazi hewa 202.

“Wapo waliokuwa wakilipwa mishahara wakiwa wamekufa, wafungwa, wastaafu. Lakini 202 wote wanalipwa mishahara huku wengine 3,200 wakati kazi hiyo ikifanyika hawakufanyiwa kutokana na sababu mbalimbali ambazo ni wengine kuwa masomoni, watoro na wengine walikuwa wagonjwa,” alisema Rais Magufuli.

Alitoa mchanganuo kwamba miongoni mwa wafanyakazi 202 waliokuwa wakilipwa mishahara hewa, sita ni walioacha kazi, waliokufa na kufungwa 27, waliofukuzwa 8 na wastaafu 58 na waliokuwa likizo bila malipo walikuwa watatu.

“Ukichukua kwenye halmashauri 180 tulizonazo ukafanya hesabu rahisi ya kukokotoa, utakuta kama halmashauri zote ziko hivyo, maana yake utakuta ni jumla ya wafanyakazi 2597.4 ambao ni hewa.

“Ukikadiria kwamba kila mmoja analipwa mshahara wa milioni moja kwa mwezi na wapo ambao wanalipwa zaidi, hivyo tutakuwa tunapoteza bilioni 2.5 kila mwezi,” alisema Magufuli.

“Kuna wafanyakazi 320 ambao hawajulikani kama wapo kazini, lakini bado wamekuwa wakilipwa mishahara hali inayosababisha Serikali kupoteza mapato makubwa.

“Kila mwezi tunalipa mishahara kati ya shilingi bilioni 549 hadi 550, kati ya hiyo ipo mishahara feki. Kutokana na hali hiyo, wakuu wa mikoa nendeni mkasimamie hilo na ninawapa grace time (kipindi), ndani ya siku 15 wakurugenzi wawe wamejumlisha na wamewatoa wafanyakazi hewa katika Payroll,” alisema Rais Magufuli.

Alisema ikiwa itabainika mkurugenzi atalipa mishahara hewa atachukuliwa hatua za kisheria ikiwamo kufikishwa mahakamani.

“Mshahara wa mwezi tukigundua mkurugenzi amelipa mshahara hewa ajue hana kazi na tunampeleka mahakamani. Kati ya halmashauti 14 za mikoa ya Dodoma na Singida imegundulika kuna wafanyakazi hewa 202, ninajua mawaziri mpo hapa, Waziri wa Fedha upo, komesheni wizi wa fedha.

“Nendeni mkawaambie wakurugenzi watoe wafanyakazi hewa kwani tunahitaji mapato tunayopata yaende kwa wananchi,” alisema.



ELIMU BURE

Akizungumzi suala la elimu bure, Rais Magufuli aliwataka wakuu hao wa mikoa kuhakikisha wanakwenda kusimamia suala hilo kwa vitendo.

Alisema kutokana na hali hiyo, hivi sasa Mkoa wa Dar es Salaam umeitikia wito huo vizuri kwa kuhakikisha elimu inatolewa bure kuanzia darasa la kwanza hadi kitado cha nne.

Pamoja na hali hiyo, aliwataka wakuu hao wa mikoa kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa madawati na majengo.

“Kuhusu suala la elimu bure ninajua hivi sasa Dar es Salaam imeitikia na kutekeleza suala hili, na hivi sasa wazazi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kupeleka watoto shule, sasa nyinyi (wakuu wa mikoa) nendeni mkasimamie upatikanaji wa madawati na majengo ya uhakika,” alisema.



UTEUZI KUCHELEWA

Rais Magufuli alitoboa siri ya kuchelewa kuteua wakuu wa mikoa akisema kuwa alikuwa akifanya uhakiki wa kina wa kubaini kama watu atakaowateua wataweza kazi hiyo.

“Nimeamua kuwateua wakuu wa mikoa nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri katika mikoa yenu, napenda niwape pole kwa sababu mtakwenda kufanya kazi kweli kweli kutatua kero za wananchi wetu.

“Ndiyo maana nilikuwa najiuliza huyo kweli ataweza, maana kama usipokuwa makini unaweza siku moja ukamfuta, kumsamehe. Lakini naamini mtaweza kazi hii na hamtaniungusha,” alisema.



AONYA SIASA

Rais Magufuli aliwataka wakuu hao wa mikoa kwenda kufanya kazi na si kutangaza siasa.

“Hamuendi kutangaza siasa, mnakwenda kufanya kazi na mkasimamie fursa kwa vijana wapate ajira,” alisema.



UTAWALA WA SHERIA

Aliwataka wakuu hao wa mikoa kuhakikisha wanakwenda kusimamia utawala wa sheria ili wananchi watii sheria bila shuruti.

Alisema hivi wapo baadhi ya watendaji, hasa wa ngazi ya kata ambao wamekuwa wakiwanyanyasa wananchi, na kama wapo viongozi wa aina hiyo wawekwe ndani ili nidhamu ya Tanzania mpya ipatikane.

“Msiogope kuchukua maamuzi magumu kama njia hii ndiyo itasaidia kujenga Tanzania mpya, nendeni mkawatumikie wananchi walio wanyonge,” alisema.

MAMLAKA YA WAKUU WA MIKOA

Rais Magufuli aliwataka wakuu hao wa mikoa kwenda kujipanga kikamilifu kwa kuhakikisha wanawachukulia sheria wale wanaokwenda kinyume.

“Nyinyi mna mamlaka ya kuwaweka watu ndani hata masaa 48, wekeni watu ndani ili wajue mnatakiwa kuheshimiwa. Tusiogope kuchukua maamuzi, nafuu uchukue maamuzi hata kama ni mabaya yatarekebika huko mbele,” alisema.



USIMAMIZI KWA MA-DC, MA-DED

Aliwataka wakuu hao wa mikoa kuhakikisha wanakwenda kuwasimamia vizuri wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri nchini kwa kuhakikisha wanawajibika ipasavyo.

“Mabadiliko huchukua muda na lazima yaonekane, ila ni lazima tubadilike,” alisema.



ULINZI NA USALAMA

Katika maeneo ya porini, hasa mikoa ya Kagera, Katavi na Kigoma, kumekuwa na mazoea kwa wasafiri wa mabasi kusindikizwa na askari polisi.

“Haiwezekani kwa nchi ambayo imejitawala zaidi ya miaka 50, eti raia wake wanaposafiri lazima wasindikizwe na polisi, ambayo inamaanisha kwamba hakuna usalama, hivyo nimeteua watu ambao nimefikiri watasimamia wananchi wasiendelee kusindikizwa na polisi.

“Ulinzi ukaimarike na wananchi watembee katika nchi yao wakiwa salama, nitashangaa sana iwapo Meja Jenerali Mustapha Kijuu ambaye umekuwa ukisimamia jeshi la nchi kavu nchi nzima ya Tanzania, sidhani kama utashindwa kusimamia Mkoa wa Kagera na watu wakashindwa kukaa kwa amani na ninajua uwezo huo unao,” alisema Rais Magufuli.

VIJANA NA POOL TABLE

Rais Magufuli aliwataka wakuu hao wa mikoa wasimamie watu wafanye kazi, hasa vijana ambao wamekuwa wakicheza Pool table saa mbili asubuhi halafu wanaokuwa mashambani ni akina mama na wazee pekee.

“Haiwezekani vijana wawe wanashinda vijiweni wanacheza pool, wakati wazee na akina mama wapo mashambani wanalima. Kawahimizeni wafanye kazi, wasipofanya kwa hiari walazimisheni kufanya kazi.

“Watanzania hawafanyi kazi na kama hawawezi kufanya kazi kwa kuambiwa, basi watafanya kazi kwa lazima, kwa sababu kama wamezoea kukaa bila kufanya kazi, shika wapelekeni kwenye mapori wakalime kwa nguvu, akitoka huko atakuwa ameelewa kwamba asiyefanya kazi na asile,” alisema Rais Magufuli.

RUNGU TRA
Akieleza hatua ya kumwapisha Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata pamoja na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), Valentino Mlowola, alisema anataka kuona mapato yanayokusanywa yanakwenda kuwanufaisha wananchi.

MAPIGANO MOROGORO

Katika hotuba yake hiyo, Rais Magufuli alieleza uamuzi wake wa kumwacha katika uteuzi aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk. Rajab Rutengwe kuwa ni kutokana na mapigano ya wakulima na wafugaji ambapo kila mara wananchi hupoteza maisha.

“Morogoro watu wanauana sana ndiyo maana sikuona sababu ya mkuu wa mkoa kubaki pale. ‘Message sent and delivered’,” alisema

ZIARA YA RAIS WA VIETNAM

Akizungumzia ziara ya siku tatu ya Rais wa Vietnam, Trough Tan Sang, aliyoifanya nchini Machi 8, mwaka huu, alisema anashangazwa na taifa hilo kupiga hatua kimaendeleo licha ya kupita katika changamoto kadhaa ikiwamo mapigano na vita.

Alisema pamoja na hali hiyo, nchi hiyo ilikuja nchini katika miaka 1970 na kuchukua mbegu za mpunga, korosho na samaki jambo ambalo sasa limeipaisha kiuchumi.

Rais Magufuli alisema mbegu hizo zilizochukuliwa miaka ya 1970, zimeifanya nchi hiyo kuwa kinara katika uzalishaji wa mazao hayo pamoja na ufugaji wa samaki.

“Hili nachomekea kidogo, licha ya Vietnam kupita katika changamoto kadhaa, lakini wamefanikiwa kupaa kichumi. Walikuja hapa na kwenda Mtwara kwa Mheshimiwa Dendegu (Halima) na kuchukua mbegu za korosho, leo wamekuwa wazalishaji wazuri kuliko hapa kwetu.

“Kule kuna bodi za ajabu na wananchi wanalalamika. Leo hii ndiyo wazalishaji wazuri na wakubwa wa samaki, korosho na hata kahawa duniani,” alisema.

Chanzo-Mtanzania
Share:

Uchomaji Kituo cha Polisi Bunju A....Watuhumiwa 17 Waachiwa huru

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru washtakiwa 17 kati ya 35 wanaokabiliwa na kesi ya kuchoma moto Kituo cha Polisi Bunju ‘A’ baada ya Upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashtaka

Hukumu hiyo imetolewa mahakamani hapo na Thomas Simba, Hakimu Mkazi huku upande wa mashtaka ukiwakilishwa na Hellen Moshi, Wakili wa Serikali.

Katika kesi hiyo, Hakimu Simba amesema hatua hiyo inatokana na upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao wakiwa na mashahidi 17 pamoja na vielelezo 19.

Amesema, kutokana na kushindwa kuthibitisha mashtaka kwa washtakiwa 17 mahakama imeamua kuwaachia huru kwa kuwa hawana hatia, huku washtakiwa waliobaki 18 wakipatikana na kesi ya kujibu.

Washtakiwa walioachiwa ni Halifan Mshengeli, Patrick Elias, Jacob Kasambo, Amos Machaka, Hamis Mohamed, Elia Nalomba, Juma Kapanga,

Wengine ni Josephine Machimo, Shadya Ismail, Aisha Husseion, Jenerose Urio, Suzan Shaulin, Mariam Mwinyi, Madgalena Nashokigwa, Mariam Rashid, Pili Ally na Said Mwindi.

Washtakiwa ambao wamepatikana na hatia baada ya kutolewa kwa ushahidi ni Yusuph Sungu, Juma Koza, Rashid Liwima, Mrisho Majaliwa, Hamis Ndege, Seleman Gwae, Baraka Nkoko, Mang’ enya Mang’enya.

Wengine ni Abuu Issa, Ramadhan Said, Rajab Ally, Ally Athuman, Abraham Nunge, Amina Matipwili, Mariam Hoza, Rehema Juma, Gudila Temba,  Veronica Ephraem (Mama Wambura).

Hakimu Simba amesema, washtakiwa hao wamepatikana na kesi ya kujibu katika mashtaka sita yanayowakabili, hivyo kutokana na wingi wa wananchi kesi hiyo itasikilizwa siku mbili mfululizo kuanzi Machi 29 hadi 30, mwaka huu kwa ajili ya kujitetea.

Baada ya kusema, hayo kuliibuka hoja za kisheria kati ya Wakili Moshi na wakili wa utetezi Felix Nkongwa kuhusu kupata dhamana kwa washitkiwa waliobaki.

Kutokana na mvutano wa hoja, Hakimu Simba amesema uamuzi wa kupata ama kutopata dhamana kwa washitakiwa hao utatolewa Machi 22, mwaka huu.
Share:

MATOKEO YA USAILI WA MCHUJO (16-03-2016)

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Wasailiwa waliochaguliwa 'SELECTED' wanatakiwa kufika ofisi za Sekretarieti ya Ajira Maktaba kuu ya Taifa  tarehe 17-03-2016, saa moja kamili asubuhi kwa ajili ya usaili wa mahojiano.
Wasailiwa wanakumbushwa kufika na vyeti vyao halisi (Original Certificates).
KADA: MKUFUNZI  - COMPUTER SCIENCE          
MWAJIRI: MDA's/LGA's          
          
SN    EXAM NUMBER        SCORES REMARKS
1    PSRS COMP SCI 0152    77    SELECTED
2    PSRS COMP SCI 0123    71    SELECTED
3    PSRS COMP SCI 0135    70    SELECTED
4    PSRS COMP SCI 0022    69    SELECTED
5    PSRS COMP SCI 0015    66    SELECTED

Share:

Jeshi La Ulinzi La Wananchi Wa Tanzania Lakanusha Kupeleka Wanajeshi Visiwani Zanzibar.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linapenda kutoa taarifa kwa Umma juu ya uvumi ulioenea katika mitandao ya kijamii kuwa, limepeleka Wanajeshi wengi visiwani Zanzibar kwa ajili ya kudhibiti Usalama wakati wa kipindi hiki cha uchaguzi marudio unaotarajia kufanyika tarehe 20 Machi, 2016

Habari hizo siyo za kweli na zina lengo la kupotosha Umma. Kimsingi JWTZ linao Wanajeshi visiwani Zanzibar wakati wote kwa majukumu yake ya msingi ya Ulinzi wa nchi yetu. 
Hivyo hakuna Mwanajeshi yeyote aliyeongezwa zaidi ya wale waliopo visiwani humo tangu awali. Taarifa hizo zipuuzwe,zisipewe nafasi yoyote ya kujenga hofu kwa Wananchi.

JWTZ linapenda kwa mara nyingine tena kuwahakikishia Wananchi kuwa wasiwe na wasiwasi wowote kuhusu ulinzi na usalama wa nchi yetu, kwani wakati wote Jeshi lao lipo imara kuwalinda.

Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0784-477638.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger