Saturday 5 October 2024

DAWA ILIYONISAIDIA KUBEBA UJAUZITO BAADA YA KUSUMBUKA SANA

Naweza kusema hakuna furaha anayokuwa nayo mwanamke kama kuitwa Mama, daima siwezi kuisahau siku ambayo nilimshika kwa mikono yangu mtoto wangu wa kwanza kwa mara ya kwanza.


Chozi la furaha lilinitoka bila mwenyewe kujua, nilijikuta nalia tu kwa furaha niliyokuwa nayo, moyo wangu ulihemewa kwa furaha ambayo ni vigumu kuelezeka na kueleweka.

Nasema hivyo kwa sababu kuu mbili; kwanza kujifungua salama mtoto wangu wa kwanza akiwa na afya tele, pili ni kwamba niliangaika sana kutafuta mtoto hadi ukafikia wakati wa kuanza kukataa.

Jina langu kwa sasa naitwa Mama Anna, ni mkazi wa Katavi, katika ndoa yangu nilikaa miaka zaidi ya mwili bila kujaliwa mtoto ingawa nilikuwa na kiu sana kumzalia mume wangu. 

Mume wangu alikuwa ananipa moyo na kunishauri niwe na subra kwani kila jambo lina wakati wake, nilimkubalia ila moyoni nafsi yangu ilikuwa haijatulia kabisa. Kiu yangu ni kujaliwa mtoto tu.

Wakati mmoja nikiwa nasoma gazeti fulani, niliweza kuona tangazo la Dr Bokko kuwa wanatoa tiba kwa wanawake wanaosumbuka kupata mtoto, nilishawishika kuwasiliana nao licha ya kuwa tayari nilikuwa nimeshazunguka kwa wataalamu wengi.

Baada ya kuongea nao waliambia dawa zao zimewasaidia wanawake wengi kupata watoto, hivyo nisiwe na wasiwasi hata kidogo, basi walinitumia dawa zao na kunipati maelezo jinsi ambavyo naweza kuzitumia na kupata matokeo yaliyokusudiwa.

Nashukuru dawa zili ziliweza kunisaidia na sasa naitwa Mama Anna na Anna mwenyewe tayari ana mtoto wake, watoto wangu ndio furaha ya maisha yangu, kwa hakika kila siku siwezi kuacha kuwakumbuka Dr Bokko kwa msaada walionifanyia.

Ninatoa wito kwa wenye shida au magonjwa, kusumbuliwa na mapenzi, ndoa, biashara, kukosa ujauzito n.k, basi wasisite kuwatembelea Dr Bokko, sio lazima usafiri hadi ofisini kwao, unaweza kuongea nao kwa njia ya simu na utasaidiwa kwa haraka. Piga simu +255618536050.
Mwisho.
Share:

Friday 4 October 2024

RAIS SAMIA AJA NA HATUA MPYA KATIKA MABORESHO YA MFUMO WA KIKODI TANZANIA

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa kiongozi wa kwanza tangu Rais Benjamin Mkapa kuboresha mfumo wa kikodi nchini Tanzania, baada ya kuunda Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi. Tume hii ina lengo la kuangazia changamoto mbalimbali zinazokabili mfumo wa kodi na kutoa mapendekezo yanayoweza kuboresha ukusanyaji wa kodi na ufanisi wa matumizi yake.

Moja ya mambo makuu ambayo Rais Samia anatarajia kuyatekeleza kupitia tume hii ni kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa kodi. Hii ni muhimu katika kujenga imani ya wananchi kwa serikali na mfumo wa kodi, ambao mara nyingi umekuwa ukikabiliwa na malalamiko kuhusu ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Pia, tume hiyo inatarajiwa kuzingatia njia mpya za kukusanya kodi ambazo zitasaidia kuongeza mapato ya serikali bila kuweka mzigo mzito kwa wananchi. Hii inaweza kujumuisha matumizi ya teknolojia ya kisasa katika ukusanyaji wa kodi, kama vile mifumo ya kielektroniki inayorahisisha malipo ya kodi na kuondoa urasimu usio wa lazima.

Aidha, Rais Samia amesisitiza katika ushirikiano na sekta binafsi ili kuboresha mfumo wa kikodi. Ushirikiano huu unaweza kuleta mawazo mapya na mbinu za kisasa katika ukusanyaji wa kodi na pia kutoa fursa kwa sekta binafsi kushiriki katika maendeleo ya uchumi wa nchi.

Kwa kufanya hivi, Rais Samia atasaidia kukuza mazingira ya biashara yanayovutia wawekezaji na kuimarisha uchumi wa nchi. Hii ni muhimu katika kipindi ambacho uchumi wa dunia unakabiliwa na changamoto, na Tanzania inahitaji kuongeza mapato yake ya ndani ili kufikia malengo yake ya maendeleo.


Share:

HATMA YA KOMBO MBWANA KUJULIKANA OCTOBA 31

 

Na Oscar Assenga, TANGA

MAAMUZI ya Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya Handeni Mkoani Tanga Kombo Mbwana Twaha kupelekwa mahakamani Kuu kwa ajili ya kupewa haki zake ama la itabainika Octoba 31 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama baada ya shauri hilo kuhairishwa Wakili wa Upande wa Utetezi Paul Kisabo alisema kwamba wanaamini mahakama itatenda haki na kutafsiri sheria kama ilivyo watasikia na kukiwa na maamuzi tofauti sheria zitawaelekeza nini cha kufanya .

Shauri hilo lililetwa mahakamani hapo na lilipangwa kwa ajili ya kusikilizwa mbele ya Mhe.Jaji Happiness Ndesamburo ambapo kesi hiyo msingi wake waliifungua kwa ajili ya kuomba Kombo Mbwana Twaha aweze kupelekwa mahakamani ili aweze kupewa haki zake.

Aidha alisema kwamba Kombo anashikiliwa tokea 15 June 2024 alipokamatwa nyumbani kwake Handeni na mpaka leo bado anashikiliwa.

Alisema kesi hiyo msingi wake waliifungua kwa ajili ya kuomba kombo apelekwe mahakamni ili aweze kupewe haki zake kupitia maombi ya kuiomba mahakama kuu itoe amri mtu aletwe Yule aliyeshikiliwa kunyume cha sheria.

Wakili huyo alisema kwamba walifungua kesi hiyo na ilipangwa kusikiliza pande zote mbili wao upande wa mleta maombi Kombo Twaha Mbwana alikuwepo yeye na upande wa wajibu maombi ambaye ni kamansa wa RPC ,IGP,DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliwakilishwana mawakili wawili waliwasilisha hoja zao mahakamani hapo.

Awali akizungumza Katibu wa Chadema wilaya ya Tanga Shabani Ngozi alisema kwamba wamekuja Mahakam kuu kusikiliza kesi hiyo kwa mwenendo wa kesi wanawashukuru mawakili wao kwa kazi kubwa na ngumu wanayoendelea kuifanya kuhakikisha Kombo anapata haki yake ya msingi awe nje kwa dhamana .

Alisema kwa hiyo binafsi wanaendelea kushirikiana na mawakili wao na familia ili mwenzao awe huru waweze kuendeleza gurudumu la kuendeleza Taifa.

Share:

WANANCHI WA SHINYANGA WATAKIWA KUTUMIA ELIMU KAMA SILAHA YA UKOMBOZI WA MAENDELEO

 

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Wakili Julius Mtatiro akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka wananchi kutumia elimu kama silaa ya ukombozi wa maendeleo.

Amesema hayo Jana Oktoba 03, 2024 wakati akifungua maadhimisho ya juma la wiki ya Elimu ya Watu Wazima yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya stendi ya mabasi Iselemagazi Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Mhe. Wakili Mtatiro pia amewataka wazazi na walezi wa Mkoa wa Shinyanga kusimamia maadili ya watoto na vijana kwa kushirikiana na serikali kuhakikisha wanapata elimu bora na kuimarisha ulinzi na usalama wa watoto na vijana shuleni na Nyumbani.

"Mzazi atakae sababisha kukatishwa masomo kwa mtoto wake atachukuliwa hatua", amesema Mhe. Mtatiro 

Pia Wakili Mtatilo mewapongeza wazazi na walezi waliotoa ushirikiano mkubwa kuhakikisha vijana wao wanaenda shule wakiwemo wasichana waliokatishwa masomo wamerejea tena shuleni kuendelea na masomo ili watimize ndoto zao.

Aidha, Mhe. Wakili Mtatiro alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kushiriki zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaanza tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024.

Katika hatua nyingine, Mgeni Rasmi alipata fursa ya kutembelea banda ya Halmashauri za Mkoa wa Shinyanga na taasisi mbalimbali.








Share:

Wednesday 2 October 2024

WANAHARAKATI WATAKA MIFUMO YA ELIMU IBORESHWE KUPUNGUZA WATOTO KUKATISHA MASOMO

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WADAU wa Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) wamewasilisha ombi kwa serikali kuhusu kuboresha mifumo ya elimu ili kukabiliana na changamoto ya watoto wanaokatiza masomo. 

Katika semina iliyofanyika leo, Oktoba 2, 2024 Jijini Dar es Salaam, , Mwanaharakati wa Jinsia, Kennedy Anjelita, alisisitiza umuhimu wa kubadilisha mfumo wa elimu ili uwe rafiki kwa kila mwanafunzi, akiongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kupunguza idadi ya watoto wanaoshindwa kumaliza masomo yao.

Anjelita amesema kupitia semina hiyo wamesisitiza kurudishwa kwa elimu ya stadi za kazi shuleni, akisema kuwa inaweza kuwa njia ya kusaidia wanafunzi kujipatia kipato na kuleta manufaa katika shule, ikiwemo kusaidia na masuala ya chakula badala ya kutegemea michango ya wazazi. 

Pamoja na hayo Angelita alipendekeza pia uundaji wa utaratibu wa kukutana kati ya wazazi, walimu, na wanafunzi ili kujadili matatizo yanayowakabili watoto wanaokatisha masomo.

Aidha, Anjelita amesema wameshauri kuhusu adhabu zinazotolewa shuleni, akitaka zirekebishwe ili zisihamasishe wanafunzi kuacha shule. 

Vilevile wadau hauo wamesisitiza umuhimu wa sera itakayoshughulikia watoto wanaoacha shule bila sababu, waakipendekeza kwamba wapelekwe katika magereza ya watoto kwa ajili ya kujifunza.

Kwa upande wake Theodosia Stephano ambaye pia ni mdau wa semina za Jinsia na maendeleo, ameeleza kuwa miundombinu ya shule, ikiwemo ukosefu wa madawati na vyoo ni miongoni mwa sababu zinazowafanya watoto kukatisha masomo. 

Amesema kuwa uhaba wa chakula shuleni kutokana na hali duni ya kiuchumi ya wazazi ni sababu nyingine inayowakatisha tamaa watoto.

Theodosia ameshauri kuboreshwa kwa miundombinu ili iweze kuwasaidia watoto wenye changamoto na kuwapa fursa sawa za elimu kama wenzao.

Share:

UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA ZANZIBAR KUFANYIKA OKTOBA

 

Makamu Mwenyekiti Wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe.Jaji wa Rufaa(Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk, akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa Wadau wa Uchaguzi katika kisiwa cha Pemba, Zanzibar leo Septemba 30, 2024 ambapo Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imekutana na wadau mbalimbali wa uchaguzi kuwapa taarifa juu ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaotaraji kufanyika Visiwani Zanzibar kuanzia Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa Wadau wa Uchaguzi katika kisiwa cha Unguja, Zanzibar leo Septemba 30, 2024 ambapo Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imekutana na wadau mbalimbali wa uchaguzi kuwapa taarifa juu ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaotaraji kufanyika Visiwani Zanzibar kuanzia Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa Wadau wa Uchaguzi katika kisiwa cha Unguja, Zanzibar leo Septemba 30, 2024 ambapo Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imekutana na wadau mbalimbali wa uchaguzi kuwapa taarifa juu ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaotaraji kufanyika Visiwani Zanzibar kuanzia Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.
Na. Mwandishi Wetu
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Zanzibar utafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 07 hadi 13 Oktoba, 2024 ambapo vituo vitafunguliwa saa 02:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
 
Akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi Kisiwani Pemba, Zanzibar, Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufaa (Mstaafu), Mbarouk Salim Mbarouk amesema uboreshaji huo wa daftari utajumuisha mikoa ya Mjini Magharibi, Unguja Kaskazini, Unguja Kusini, Pemba Kaskazini na Pemba Kusini.
 
Jaji Mbarouk amesema uboreshaji huo ambao unafanyika kwenye mzunguko wa sita kwa mujibu wa kalenda ya Tume kwa upande wa Zanzibar utahusu kuwaandikisha watanzania wote wanaoishi Zanzibar ambao wanastahili kuandikishwa kuwa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
 
Akizungumza wakati akifungua mkutano kama huo Kisiwani Unguja, Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, Mhe. Asina Omari ameongeza kuwa kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na.1 ya Mwaka 2024, Tume itawaandikisha watanzania waliopo Zanzibar ambao wametimiza umri wa miaka 18 na zaidi au watakaotimiza umri huo wakati au kabla ya tarehe ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
 
Amefafanua kuwa mtanzania huyo atakeyandikishwa ni lazima awe hajapoteza sifa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi au sheria nyingine yeyote na awe anastahili kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
 
“Kwa lugha nyepesi ni kwamba, Tume itamwandikisha mtanzania yeyote aliyopo Zanzibar ambaye amekosa sifa za kuandikishwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC). Hivyo, atakayeandikishwa kwenye Daftari la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi atapiga kura moja tu ya kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” amesema Jaji Asina.
 
Uzinduzi wa uboreshaji wa Daftari ulifanyika tarehe 20 Julai, 2024 mkoani Kigoma na mpaka sasa uboreshaji umeshafanyika kwenye mikoa ya Kigoma, Tabora, Katavi, Geita, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Manyara, Singida na sehemu ya mkoa wa Dodoma. 
Wadau wa uchaguzi kutoka vyama vya Siasa, Makundi maalum ya Wanawake, vijana, watu wenye Ulemavu, Wazee wa Kimila, Wahariri wa vyombo vya Habari wakishiriki katika mkutano wa Tume na Wadau wa uchaguzi uliofanyika leo Septemba 30, 2024 katika kisiwa cha Unguja Zanzibar ikiwa ni maandalizi kuelekea zoezi la uboreshaji wa daftari la Kudumu la Wapiga Kura visiwani Zanzibar ambalo linataraji kuanza Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.

Wadau wa uchaguzi kutoka vyama vya Siasa, Makundi maalum ya Wanawake, vijana, watu wenye Ulemavu, Wazee wa Kimila, Wahariri wa vyombo vya Habari wakishiriki katika mkutano wa Tume na Wadau wa uchaguzi uliofanyika leo Septemba 30, 2024 katika kisiwa cha Unguja Zanzibar ikiwa ni maandalizi kuelekea zoezi la uboreshaji wa daftari la Kudumu la Wapiga Kura visiwani Zanzibar ambalo linataraji kuanza Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.

Wadau wa uchaguzi kutoka vyama vya Siasa, Makundi maalum ya Wanawake, vijana, watu wenye Ulemavu, Wazee wa Kimila, Wahariri wa vyombo vya Habari wakishiriki katika mkutano wa Tume na Wadau wa uchaguzi uliofanyika leo Septemba 30, 2024 katika kisiwa cha Unguja Zanzibar ikiwa ni maandalizi kuelekea zoezi la uboreshaji wa daftari la Kudumu la Wapiga Kura visiwani Zanzibar ambalo linataraji kuanza Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.
Wadau wa uchaguzi kutoka vyama vya Siasa, Makundi maalum ya Wanawake, vijana, watu wenye Ulemavu, Wazee wa Kimila, Wahariri wa vyombo vya Habari wakishiriki katika mkutano wa Tume na Wadau wa uchaguzi uliofanyika leo Septemba 30, 2024 Kisiwani  Zanzibar ikiwa ni maandalizi kuelekea zoezi la uboreshaji wa daftari la Kudumu la Wapiga Kura visiwani Zanzibar ambalo linataraji kuanza Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.


Wadau wa uchaguzi kutoka vyama vya Siasa, Makundi maalum ya Wanawake, vijana, watu wenye Ulemavu, Wazee wa Kimila, Wahariri wa vyombo vya Habari wakishiriki katika mkutano wa Tume na Wadau wa uchaguzi uliofanyika leo Septemba 30, 2024 Kisiwani  Zanzibar ikiwa ni maandalizi kuelekea zoezi la uboreshaji wa daftari la Kudumu la Wapiga Kura visiwani Zanzibar ambalo linataraji kuanza Oktoba 7 hadi 13, mwaka huu.


Wadau mbalimbali wakishiriki katika majadiliano. 


Wadau mbalimbali wakishiriki katika majadiliano. 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger