Friday 20 September 2024
CCM YASISITIZA UHUSIANO WA KIMATAIFA KUIMARISHA UCHUMI NA MAENDELEO YA WATU
AFISA MTENDAJI MKUU WAZOHURU ATOA RAI KWA WATANZANIA KUACHA KUMKEJELI RAIS SAMIA
Thursday 19 September 2024
JAMBO FOOD PRODUCTS YAJA NA MUONEKANO MPYA WA BIDHAA ZAKE
Kampuni ya Jambo Group imezindua muonekano mpya wa bidhaa zake za Jambo Food Products ‘Jamukaya’ zenye muonekano mzuri na wa kuvutia wenye radha ile ie.
Hafla ya uzinduzi huo umefanyika Septemba 17, 2024 kwenye kiwanda hicho ukiongozwa na Mkurugenzi Nassoro Salum Hamis pamoja na Meneja Mkuu wa Jambo Fm ambaye pia ni msimamizi wa Chapa group Nickson George, huku ukihudhuriwa na wananchi pamoja na wafanyakazi wa jambo.
Akizungmza wakati wa uzinduzi huo George amesema mbali na uzalishaji wa bidhaa bora pia imejidhatiti kutoa ajira za kudumu 400,000 ukijumlisha na wale wa ajira ya muda mfupi wanakuwa 600,000 hivyo kila siku watu hao wako kazini na serikali inapata mapato yake.
“Tumeamua kubadilisha muonekana wa sura ya mpya ya bidhaa baada ya kampuni kufikisha miaka 20 ya uzalishaji wa bidhaa zake hivyo tumeheshimu wateja wetu na hatua hiyi llni kuunga mkono juhudi za serikali kupunguza wimbi la vijana wasio na ajira,” amesema George.
Ameongeza kuwa mteja akiona muonekano mpya asiwe na mashaka kwani kuna usemi unaoeleza ‘Hawa ndio sisi’ ikimaanisha muonekano huo usiwape wasiwasi bali ni kampuni hiyo hiyo ikiendelea kuwapa furaha wateja wake.