Tuesday, 17 September 2019

Dereva taksi kesi ya Mo Dewji aendelea kusota....Watuhumiwa Wengine bado Wanasakwa

...
Upande wa Jamhuri katika kesi inayomkabili dereva taksi mkazi wa Tegeta, Mousa Twaleb (46) ya uhujumu uchumi ikiwamo kusaidia kutendeka uhalifu, kutakatisha Sh. milioni nane na kumteka Mohamed Dewji maarufu kama ‘Mo’ umedai kuwa bado unaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine wanne kwa ajili yakuwaunganisha katika kesi hiyo.

Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, alidai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa, na kwamba bado upande wa Jamhuri unaendelea na juhudi za kuwatafuta watuhumiwa wengine.

Alidai kuwa upande wa Jamhuri unaomba tarehe nyingine ya kutajwa. Hakimu alisema kesi hiyo itatajwa tena Septemba 30, mwaka huu na mshtakiwa ataendelea kukaa mahabusu.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger