Saturday, 9 March 2019

MTANGAZAJI WA CLOUDS FM KIBONDE AZIKWA MAKABURI YA KINONDONI DAR

...
Aliyekuwa Mtangazaji wa Clouds Media Group (CMG), Ephraim Kibonde amezikwa leo Machi 10 katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es salaam majira ya saa Kumi jioni.

Amezikwa na maelfu ya watu ambao ni ndugu, jamaa na marafiki aliokuwa akifanya nao shughuli mbalimbali enzi za uhai wake na wengine waliomjua kupitia kazi yake ya utangazaji.

Kibonde amefariki dunia Machi 7 mwaka huu baada ya kuugua Presha kwa muda mfupi katika hospitali ya Bugando iliyopo mkoani Mwanza.

Ameacha watoto watatu, wakike wawili na mmoja wakiume.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger