Thursday 28 September 2023

WAVAMIZI HARAMU WAVAMIA MGODI WA NORTH MARA


NORTH MARA INTRUDER INCIDENTS

 

Dar es Salaam, Tanzania, September, 2023 – Barrick Gold Corporation (NYSE:GOLD) (TSX:ABX) – On 21 September an incident occurred where approximately 100 intruders unlawfully invaded the mine property during heavy rainfall.

Unarmed private security contractors responded in an attempt to repel the armed invaders but subsequently requested police intervention to remove the aggressive intruders from the mine site. Seven intruders were arrested and based on initial police findings, some had sustained injuries as a result of fighting amongst themselves. Another intruder, injured in the fighting amongst themselves, was found unconscious by the police but later succumbed to his injuries while being transported to the Tarime District Hospital.

On 22 September a second incident occurred where police once again engage with aggressive armed invaders in an attempt to prevent them from illegally entering the Gena Pit. During the incident, a policeman discharged his firearm and wounded an intruder. The intruder was transported to the Musoma hospital where he succumbed to his injuries on 27 September.

The police have launched investigations into both incidents.

 

 

 

Barrick Enquiries

Investor and media relations

Kathy du Plessis

+44 20 7557 7738

Email: barrick@dpapr.com

Corporate communications and
country liaison manager

Georgia Mutagahywa

+255 754 711 215
Email:georgia.mutagahywa@barrick.com

Website:
 www.barrick.com

 

Share:

Video : MWANAKWELA - TUPINGE UKATILI WA KIJINSIA

Share:

Video: KISIMA 'NYANDA MAJABALA' - UKIMWI




Ninayo hapa ngoma kali sana ya asili kutoka kwa msanii Kisima 'Nyanda Majabala' kutoka mkoani Simiyu inaitwa Ukimwi...Video imetengenezwa Makula Studio..itazame hapa kaimba kwa lugha mbili Kisukuma na Kiswahili..Hakika utaipenda


Bofya Play hapa chini

Share:

TRA IMEFANYA MABORESHO MAKUBWA KATIKA MIFUMO YA TEHAMA KUONGEZA UFANISI UKUSANYAJI MAPATO YA SERIKALI


 Gavana wa Benki kuu ya Tanzania Bw. Emmanuel Tutuba (katikati) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa huduma kwa mlipa kodi (TRA) Bw. Richard Kayombo (kulia) wakiangalia jinsi ya kuskani kinywaji kwa njia ya mfumo wa kielektroniki (ETS) unaotolewa na kampuni ya SICPA ili kuhakiki stempu na kuhakikisha kinywaji ni salama kwa matumizi ya binadamu katika kampeni iitwayo “Hakiki Stempu, Linda Afya yako”.
Maafisa kutoka Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) wakionesha jinsi mfumo wa kuhakiki stempu kielektoniki (ETS) unavyofanya kazi, ETS ni mfumo unaotolewa na kampuni ya SICPA ili kuhakiki vinywaji kwa watumiaji na pia wafanyabiashara..

-ETS NI MFUMO SAHIHI KATIKA UKUSANYAJI WA KODI – TRA.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewekeza na kufanya maboresho makubwa katika mifumo ya TEHAMA yenye lengo la kuongeza ufanisi, uwajibikaji, uwazi na kurahisisha ukusanyaji wa mapato ya serikali. Eneo mojawapo ambalo maboresho hayo yamefanyika ni katika stempu za Kodi za kieletroniki (ETS).

Mfumo huu wa stempu za kielektroniki umeunganishwa na mifumo ya TRA ili kupata takwimu sahihi za uzalishaji/uagizwaji kwa maana ya idadi, ujazo pamoja na ubora na viwango vya bidhaa. TRA inapenda kuwahamasisha wananchi wanaotumia bidhaa hizo kushiriki kulinda afya zao kwa kutambua bidhaa halisi na halali kwa matumizi yao.

Vilevile kutokana na wakusanya kodi kukabiliwa na changamoto ya kujua viwango vya kweli vya kodi kwa uzalishaji uliopo, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilifikiria kutafuta njia nyingine ya kisasa na sahihi ili kukabiliana na changamoto hiyo. Ambapo kampuni ya SICPA ilipewa jukumu hilo na kuja na mfumo wa stempu wa kielektroniki (ETS).

Kufanikisha utendaji wakeTRA iliweka awamu kadhaa za utekelezaji wa mfumo, ambapo katika awamu ya kwanza ya mfumo, iliyozinduliwa Januari 15,2019 stempu za kielektroniki ziliwekwa kwa kampuni 19 zinazozalisha bidhaa za pombe, mvinyo na vinywaji vikali nchini.

Awamu ya pili ya stempu za kielektroniki iliyoanza Agosti 1,2019 ziliwekwa kwenye bidhaa kama vile maji yaliyotiwa ladha tofauti na kwenye vinywaji vingine visivyo vya kileo.

Katika mahojiano na Meneja Miradi wa TRA wa Mfumo wa ETS mapema mwaka jana, Innocent Minja alisema...Lengo kuu la kutafuta mfumo mpya wa ukusanyaji kodi na uzinduzi wa ETS miaka mitatu iliyopita ni kulinda mapato ya serikali na kusaidia watumiaji wa bidhaa za vimiminika kulinda afya zao.

"Tulikuwa na changamoto kubwa ya ukusanyaji wa kodi kutokana na watu kutokuwa wakweli na pia uwapo wa uzito katika ulipaji kodi kwa hiari.

“Awali tulilazimika kuweka maofisa wetu kuangalia uzalishaji na kuhakikisha watengenezaji wanatangaza viwango vya kweli vya uzalishaji. Hata hivyo, hali hiyo ilikuwa na changamoto nyingi na kuonekana kama vurugu tukahitaji suluhu mpya,” alisema Minja.

Minja alisema kutokana na baadhi ya wazalishaji kutokuwa wakweli kuhusu uzalishaji wao na hivyo kusababisha ushindani usio wa haki wa bidhaa zao sokoni na wale wanaosema kweli na kulipa kodi stahiki.

Pia Minja aliongeza kwamba mfumo wa ETS katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita umeimarisha ulipaji wa kodi na hivyo kuimarisha ushindani wa haki sokoni.

"Hii imesababisha kila mtengenezaji wa bidhaa iliyomo kwenye mfumo kulipa kodi kwa haki," alisema Minja.

Ufungaji wa ETS umehakikisha kuwa TRA inapata data za uzalishaji kwa wakati (muda halisi) kutoka kwa watengenezaji.

"Hii ni kwa sababu ya kodi ya ushuru kwa bidhaa maalumu hutozwa kwa kiwango cha uzalishaji hivyo kujua takwimu za uzalishaji ni muhimu."

Kama ilivyotarajiwa, kuanza kwa mfumo wa ETS uliambatana na uwapo wa vifungo vya usalama kwenye teknolojia husika na kurahisisha usimamizi wa kodi nchini.

“Mfumo ulileta uwazi kwenye kodi hasa kwenye kodi ya ushuru, Kodi ya ongezeko la thamani (VAT) na kodi ya kampuni na hatimaye kupunguza manung’uniko ya walipa kodi,” alisema Minja.

Aliongeza kwa kusema ‘‘mchakato wa ufungaji ni endelevu haswa kutokana na viwanda kuendelea kuongeza viwango vya mitambo yao.’’

"Tayari tumeweka mfumo wa ETS kwa watengenezaji wote wanaostahiki wa bidhaa maalum. Takriban vifaa 135 vimefungwa kwenye viwanda vyenye mitambo inayojiendesha huku viwanda visivyojiendesha vikilazimika kuwasha mfumo huo kila wanapoanza uzalishaji,” alisema Minja.

Pamoja na kufanikisha uwekezaji wa mfumo mfumo wa ETS; mfumo huo umekuwa ni msaada mkubwa kwa wazalishaji na waingizaji wa bidhaa mbalimbali.

"Mfumo huu umeongeza uwazi, na kwa sasa, watengenezaji na waagizaji wa bidhaa zilizomo kwenye mfumo wanahakikishiwa usawa sokoni kwa kuwa kila mtu analipa ushuru wa kweli na sahihi wa bidhaa husika na kinyume na awali kabla ya mfumo."

Aliongeza kwamba ETS sio tu imerahisisha kadirio la makusanyo ya kodi, lakini pia mfumo umesaidia wazalishaji kutambua kiasi cha uzalishaji na muda ulitumika kuzalisha bidhaa husika. Pia imesaidia kujua changamoto zinazohusiana na mchakato wa uzalishaji na kutafuta suluhu za changamoto hizo. ETS ikitumika vizuri kwa usahihi malipo ya VAT pia yanakuwa sahihi na pia kurahisisha ukusanyaji na ulipaji wa kodi.

“Tunawaomba wazalishaji, waagizaji na wananchi kwa ujumla, kutumia kwa dhati mfumo huo na kuepuka matumizi ya stempu za kughushi,” anasema Minja na kuongeza kuwa TRA inafuatilia kwa makini ufanisi wa mfumo huo pote nchini.

Kuelekea Msimu wa Sikukuu TRA inatoa wito kwa watumiaji na wananchi kwa ujumla kupakua App ya Hakiki Stempu bure kwenye simu zao za kiganjani ambayo itawawezesha kutambua bidhaa inayofaa kwa matumizi ili kulinda afya zao pamoja na kuiwezesha serikali kukusanya kodi kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania. Vile vile inatoa wito kwa wazalishaji na waingizaji wa bidhaa zinazotozwa ushuru wa bidhaa kutumia mfumo wa ETS kwa uaminifu ili kulinda bidhaa zao sokoni dhidi ya bidhaa bandia pamoja na kusaidia makadirio halali ya kodi.
Share:

Wednesday 27 September 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 28,2023





























































Share:

E ' MAJOR AMEACHIA JARA


E'major ni mwimbaji kutoka Nigeria wa Afro-fusion na Afro-rnb, mtunzi wa nyimbo, na mwanamuziki anayeishi Amerika. Muziki wake unachukuliwa kuwa wa kipekee, wenye mvuto kutoka kwa aina mbalimbali za muziki, hasa Pop, RNB, Hip Hop, Highlife na Contemporary Gospel.

E'Major alikuwa mwimbaji mkuu wa bendi ya "Sound City," iliyoshirikisha wasanii kama vile Flavour Nabania na Chris Odor. Yeye ndiye mtoto wa mwisho kati ya watoto 9 aliyezaliwa na mfanyabiashara wa ndani na baba mtumishi wa serikali. 
Alianzisha kikundi cha watu watano cha a-cappella "Lace" mnamo 1996, wakati wa enzi ya Lord Eli, ambaye sasa anajulikana kama 2face Idibia/2Baba. Kisha akaondoka hadi Amerika, ambako alijiimarisha kama mwanamuziki wa kisasa mwenye msukumo na pia akaongoza kwaya katika makanisa kama vile Christ family church international.

Mnamo 2019, E'Major alisaini na Motion Major Records na ametoa kazi nyingi ikiwa ni pamoja na single, EP na nyimbo zingine chache ambazo ameshirikiana na nyota wengine wa Afrobeats.
E’Major ambaye anaendelea kuboresha uhalisia wake wa muziki anatumia nyimbo zake kila mara kuchunguza mada za mapenzi, mapambano, furaha na mafanikio.

Lakini kwa sasa E major ameachia wimbo wake mpya ambao unafahamika kwa jina la Jara unapatikana katika mitandao yote ya kijamii na kusambaza muziki .


 

Share:

JKT -TANZANIA KUTUMIA UWANJA CCM KAMBARAGE MECHI ZA LIGI KUU YA NBC.... YATANGAZA KICHAPO CHA KIZALENDO ‘DOUBLE K’ KWA KAGERA SUGAR


Afisa Habari na Mawasiliano wa Timu ya JKT Tanzania, Masau Bwire akizungumza na waandishi wa habari Mjini Shinyanga leo Jumatano Septemba 27,2023
Afisa Habari na Mawasiliano wa Timu ya JKT Tanzania, Masau Bwire akizungumza na waandishi wa habari Mjini Shinyanga leo Jumatano Septemba 27,2023


Na mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Timu ya mpira wa Miguu ya Jeshi la Kujenga Taifa(JKT)Tanzania  imethibisha rasmi kutumia uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga kama uwanja wake wa nyumbani katika michezo yote ya Ligu Kuu ya NBC -Tanzania hadi pale uwanja wao wa Meja Jenerali Isamuyo uliopo Mbweni Dar es salaam utakapokamilika baada ya matengenezo makubwa yanayoendelea kufanyika.

Hayo yameelezwa na Afisa Habari na Mawasiliano wa Timu ya JKT Tanzania, Masau Bwire katika Mkutano wake na vyombo vya habari  Mjini Shinyanga leo Septemba 27,2023.

Amesema wameuchagua uwanja wa CCM Kambarage kama uwanja wao wa nyumbani kwani wanataka maeneo yote nchini yanapata fursa hivyo furaha ya JKT Tanzania ni kuona wakazi wa Shinyanga wanapata furaha ya Soka hivyo kuwaomba wakazi wa Mkoa huo kuipa ushirikiano timu hiyo.

"Tutatumia uwanja huu hadi uwanja wetu utakapokamilika matengenezo..Uwanja wa CCM Kambarage umepitishwa na TFF kwa ajili ya kutumika kwa ajili ya mechi za ligi kuu ya NBC. Na tutaanza kuutumia uwanja huu katika Mchezo wetu na Kagera Sugar utakaofanyika Ijumaa hii Septemba 29,2023 ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme",amesema Bwire.

"Tunaomba wakazi wa Shinyanga  waichukue na kuipokea  JKT Tanzania kama timu ya nyumbani na kuipa ushirikianao wote katika kuendelea kutumia uwanja wa CCM Kambarage", ameongeza Bwire.

Mechi ya Kagera Sugar na JKT Tanzania inayotarajiwa kufanyika Septemba 29,2023 utakuwa na viingilio rafiki ili  kila mmoja kushiriki katika mechi hiyo na shinyanga imekuwa na ukame wa muda mrefu wa kukosa mechi za ligi kuu.

"Double  K ni kichapo cha kizalendo kiheshimike kwa kuwa kila timu itakayofika hapa lazima ipate kichapo.  Mechi ya Ijumaa na Kagera Sugar ni kichapo cha kizalendo,  Kagera Sugar tutaipa Double K kwani tuna kikosi bora na makini na wachezaji wenye vipawa zaidi",amesema.

"Tumepanga  kiingilio ni Tshs 2000/=  kwa mzunguko na  Jukwaa kuu ni Tshs 3000/= kwa maana ya jukwaa kuu. Pia Mfumo wa N Card utatumika ili kusaidia kutoa huduma kwa mashibiki kukata tiketi zao

"Tunatumia N Card ili kuepusha msongamano na malalamiko na tumewasiliana na mamlaka husika wa kutekeleza jukumu hilo kutoka Dar es salaam  na ofisi ya TTCL na utaratibu wa kuuza tiketi utafanyika katika vituo vya Soko Kuu, Uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga na ofisi za TTCL Shinyanga  na  siku ya mechi mageti katika uwanja wa CCM Kambarage  yatafunguliwa kuanzia  saa 4:00 asubuhi.

"Tungependa mashabiki wetu waje na sura ya JKT siku ya mechi kwa kuvaa jezi zenye ubora ambazo zinapatikana kwa Tshs 35,000/= na kofia kwa Tshs 10,000/=",ameeleza.

Share:

ZAIDI YA WAGONJWA 1000 WAFANYIWA UCHUNGUZI NA KUPATIWA MATIBABU KAMBI YA MADAKTARI BINGWA TANGA

 

Mratibu wa Kambi hiyo ambaye pia ni Mhazini wa Chama cha Madaktari Tanzania Dkt Mathew Shao kulia akiteta wakati wa kambi ya Huduma za Madaktari Bingwa wa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali inayoendelea kwenye viwanja vya Mkwakwani Jijini Tanga.

Wananchi wakiendelea kupatiwa huduma mbalimbali wakati wa kambi hiyo inayoendelea kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani Jijini Tanga






Na Oscar Assenga, TANGA

ZAIDI ya wagonjwa 1000 wamefanyiwa uchunguzi na kupatiwa matibabu katika kambi ya Huduma za Madaktari Bingwa wa uchunguzi wa magonjwa mbalimbali inayoendelea kwenye viwanja vya Mkwakwani Jijini Tanga.

Kambi hiyo iliyoandaliwa na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Tanga Mhe. Ummy Mwalimu iliyoanza Septemba 25 mwaka huu na inayotarajiwa kumalizika leo tarehe 27 September ilikuwa ikitoa huduma za kibingwa katika magonjwa mbalimbali.

Akizungumza leo Mratibu wa Kambi hiyo ambaye pia ni Mhazini wa Chama cha Madaktari Tanzania Dkt Mathew Shao alisema mwamko wa wananchi umekuwa kuridhisha kutokana na kuongezeka idadi yao kila siku.

Dkt Shao ambaye pia ni Daktari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa alitaja magonjwa hayo ya kibingwa ni Moyo,Sukari,Mifupa,Pua/koo,
masikio,wanawake na uzazi,kinywa na meno,watoto ,mfumo wa mkojo(Urojolia) na Macho.

Aliyataja magonjwa mengine ni ya Upasuaji,utoaji wa dawa na vipimo vya sukari,moyo-Echo,ECG,Utrasound,Sickle Cell,Uzito na urefu,hali ya lishe,ukimwi/TB,Ushauri na nasaha na elimu juu ya magonjwa yasiyoambukiza (NCD)

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 27,2023

 



















         








  

    Share:
    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    Popular Posts

    Unordered List

    Pages

    Blog Archive


    Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger