Friday 28 April 2023

CPB YATANGAZA FURSA KWA WADAU WA MAZAO



Baadhi ya wadau waliokusanyika katika kikao cha wadau wa mazao na CPB kilichofanyika Iringa janaa.
Mkurugenzi wa Biashara na Masoko  wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB)  Evans Mwaning'go akiongea na wadau wa mazao katika kikao kilichofanyika Jana Iringa

Mwenyekiti wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ( CPB)  Salum Awadh akiongea na wadau wa mazao
 katika kikao cha wadau na CPB kilichofanyika Iringa jana.

Na Mwandishi wetu, Malunde I Blog-IRINGA.

MWENYEKITI wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) Salum Awadh ametangaza fursa mbalimbali zinazotolewa na CPB kwa wakulima na wafanyabiashara wa Mazao hapa nchini.

Ametaja baadhi ya fursa zinazotolewa na CPB ni pamoja kilimo cha mkataba ambacho kitaanzia na hekali 1000 na kuendelea.

Akizungumza katika kikao cha wadau kilichofanyika leo Iringa Awadh alisema Kilimo cha mkataba CPB kitakuwa na uwezo mkubwa kutoa maelekezo na ufuatiliaji kwa urahisi.

" Kilimo cha mkataba kitasaidia kuwa na uhakika wa wakulima watakaotuletea mazao, yatakuwa katika ubora"' alisema Awadh.

Mwenyekiti huyo amesema fursa zingine ni pamoja na kuhitaji Mawakala ambao wataingia nao mkataba kwaajili ya uuzaji wa bidhaa zinazozalishwa CPB na kununua mazao kutoka kwa wakulima na wafanyabishara.

Awadh amesema CPB ni Shirika la Kibiashara la Serikali hivyo linafanya biashara kwa lengo la kuinua Uchumi wa Nchi lakini na mtu mmoja mmoja.

"Biashara ambayo CPB inafanya hatuwezi kumlalia mkulima au mfanyabiashara wa mazao, Sisi lengo letu, Sisi tupate na nyie mpate,alisema Mwenyekiti huyo wa Bodi.

Aidha Awadh amesema CPB ina maghala ambayo hutumia kuhifadhia mazao na bidhaa zao, hivyo wanafanya pia biashara ya kuhifadhi mazao katika maghala hayo ambayo yapo katika Mikoa mbalimbali.

vilevile Mwenyekiti huyo amesema kuwa CPB pia inatafuta masoko kwa Wakulima kama wanunuaji lakini kuwatafutia wakulima na wafanyabiashara kuwa inganisha na masoko ya nje.

" CPB inaongezea thamani mazao kwa kuchakata mazao kama Mpunga, Mahindi, Ngano, Alizeti na Siagi kupitia Viwanda vya CPB vilivyopo katika baadhi ya Mikoa ikiwemo Iringa,"amesema Mwenyekiti huyo akiwataka wafanyabiashara na wakulima wa mazao watumie fursa hiyo ili kuinuana kiuchumi.

Mwenyekiti huyo pia amesema katika kujiimarisha katika uchakataji wa mazao wanatarajia kujenga viwanda vingi zaidi katika Mikoa mbalimbali.

Ametaja Mikoa ambayo tayari kuna viwanda vya kuchakata mazao kuwa ni , Dodoma ambapo kuna kiwanda cha kuchakata Mahindi na Alizeti.

Mikoa mingine ni Arusha kuna kiwanda cha kuchakata Mahindi na Ngano, Iringa kiwanda cha kuchakata Mahindi, Mwanza kiwanda cha kuchakata Mpunga na Dar eslaam kuna Kiwanda cha kuchakata Siagi ya Korosho.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa  Iringa Elia Luvanda  ambaye alifungua kikao hicho aliitaka CPB kuangalia uwezekano wa kujenga kiwanda cha unga wa lishe kwaajili ya wanafunzi mashuleni.

"Unajua ukanda huu wa Nyanda za juu kuna tatizo la watoto kukosa lishe,hivyo niwaombe CPB mbali na kufanya biashara ya mazao,wajenge kiwanda cha kutengeneza lishe ili watoto wetu waondokane na utapiamlo', amesema Luvanda.

VvBjanaJG56ao katika kikao kilichofanyika Jana Iringa

Nnnnm
Hawa no wadau nbNnUeudJh katika kikao cha wadau wa mazao na CPB kilichofanyika Iringa janaa
Share:

UTEUZI: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAADILI

Share:

BODI YA MFUKO WA BARABARA YASHIRIKI MANESHO YA TEKNOLOJIA NA UBUNIFU

Kaimu Meneja wa Mfuko wa Barabara Eng. Rashid Kalimbaga, akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu Mfumo wa ufuatiliaji hali ya barabara unaotumiwa na wananchi katika kutoa taarifa za hali ya barabara, katika kilele cha maonesho ya Teknolojia na Ubunifu jijini Dodoma.
Meneja Msaidizi Utawala na Fedha CPA John Aswile, kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara (wa kwanza kushoto), akiwa kwenye banda la Bodi hiyo baada ya kutembelea maonesho ya Teknolojia na Ubunifu jijini Dodoma.
Bwana Comfort Mgalula kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara akigawa vipeperushi vinavyoelezea matumizi ya mfumo wa ufuatiliaji wa hali ya barabara (BARABARA APP) kwa baadhi ya watoto waliotembelea banda la la Bodi hiyo. Kwenye maonesho ya Teknolojia na Ubunifu jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Agnes Agustine na Joseph Mwabulwa
Bw. Comfort Mgalula kutoka Bodi ya Mfuko wa Barabara akizungumza na Bw. Elibariki Eliud (wa kwanza kushoto) kuhusu utendaji kazi wa mfumo wa ufuatiliaji wa hali ya barabara unaotumiwa na wananchi kupitia simu ya kiganjani katika maonesho ya Teknolojia na Ubunifu jijini Dodoma

Picha na RFB

Share:

RAIS SAMIA AONGEZA PESA MAGOLI YA SIMBA NA YANGA....MAGOLI YA PENATI HAPANA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamua kuongeza fedha za motisha kwa timu za Simba na Yanga kutoka shilingi Milioni 5 hadi Shilingi Milioni 10 endapo timu hizo zitafuzu kucheza nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika na Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Simba inacheza mchezo wa marudiano leo dhidi ya Wydad Casablanca nchini Morocco wakati Yanga itacheza mchezo wa marudiano siku ya Jumapili (keshokutwa) dhidi ya Rivers United ya Nigeria katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Simba inacheza mchezo wa marudiano ikiwa na mtaji wa ushindi wa 1-0 ilioupata katika mchezo wa kwanza wa robo fainali uliofanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam wakati Yanga itacheza mchezo wa marudiano ikiwa na mtaji wa ushindi wa 2-0 ilioupata ugenini huko nchini Nigeria.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan anazitakia kila la kheri Simba na Yanga na amewataka wachezaji kujituma uwanjani na kutumia maarifa yao yote kuhakikisha wanashinda michezo ya kukamilisha robo fainali ili wafanikiwe kuingia nusu fainali ambapo kila goli litakuwa shilingi Milioni 10.

Aidha, Msigwa amesema magoli yatakayolipiwa shilingi Milioni 10 ni yale yatakayofungwa katika dakika 90 za mchezo au dakika 120 na sio magoli ya penati.


Chanzo - Michuzi blog
Share:

GGML YAJA NA TEKNOLOJIA ZA KISASA MAONESHO YA OSHA, WANANCHI WAVUTIWA MIFUMO YA USALAMA

Afisa Mwandamizi wa Usalama na afya mahali pa kazi, Sospeter Mkombati akifafanua kuhusu chumba maalumu cha dharura wakati wa uokozi ndani ya mgodi (refugee chamber) ambacho kimebuniwa na kampuni hiyo katika uokozi wa wafanyakazi wake. Chumba hicho kipo kwenye maonesho ya usalama na afya mahali pa kazi yanayoendelea mkoani Morogoro.



NA MWANDISHI WETU

KATIKA kuadhimisha siku ya usalama na afya mahala pa kazi duniani - 2023 ambayo kitaifa yanafanyika mkoani Morogoro, Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imekuja na teknolojia mpya za kisasa katika kudumisha usalama na afya mahala pa kazi hali ambayo imekuwa kivutio kwa wananchi wanaotembelea banda la kampuni hiyo kwenye uwanja wa Tumbaku.

Teknolojia hizo ambazo ni mahsusi kwa afya na usalama wa wafanyakazi wanaofanya kazi migodini, zimetajwa kuwa za kipekee kutokana na ubunifu wa uhakika uliotekelezwa na kampuni hiyo kuleta mageuzi kwenye sekta ya uchimbaji madini.

Akifafanua kuhusu bunifu hizo mjini Morogoro katika banda la maonesho GGML, Afisa Mwandamizi wa Usalama na afya mahali pa kazi, Sospeter Mkombati amesema licha ya kwamba kampuni hiyo ni mdau namba moja wa maonesha hayo, mwaka huu imeamua kuja na vitu tofauti.

Amesema GGML kwa miaka mingi iliyoshiriki maonesha hayo yanayoratibiwa na Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa kazi (OSHA), ililenga kuelimisha umma kuhusu masuala ya usalama mahala pa kazi, lakini safari hii inataka kuwafundisha ili wananchi wanaotembelea banda hilo wakalete mageuzi kwenye kampuni zao.

Amesema teknolojia hizo ambazo GGML imekuja nazo katika maonesho ya mwaka huu ambayo kauli mbiu yake inasema “Mazingira salama na afya ni kanuni na haki ya msingi mahali pa kazi”, zinathibitisha kipaumbele cha kwanza cha kampuni hiyo ambacho ni usalama na afya mahali pa kazi.

Mkombati ametaja teknolojia ya kwanza kuwa ‘Refugee chamber’ ambayo ni chumba maalumu cha dharura ambacho huwekwa ndani ya mgodi chini ya ardhi ili kuwawezesha wafanyakazi waliopo ndani ya mgodi kwenda kukusanyika hapo wakati wakisubiri uokozi mwingine kutoka juu.

“Refugee chamber ni kifaa ambacho hutumia underground kwa kumsaidia mfanyakazi pale kunapotokea ajali mbalimbali labda mwamba umeshuka au ajali ya moto, mfanyakazi badala ya kuhaha namna ya kutoka anakwenda kwenye chumba hicho chenye uwezo wa kuchukua zaidi ya watu 20 huku kikiwa kimesheheni vifaa mbalimbali vya uokozi kama vile mitungi ya hewa ya oksijeni pamoja na mitambo ya kutoa taarifa.

“Kwa hiyo waliopo nje watajua waandae uokoaji wa aina gani kuelekea kwenye chumba hicho ambacho hakiwezi kupenya moto wala mawe ya miamba huko chini ya ardhi,” amesema.

Ameitaja teknolojia nyingine waliokuja nayo kuwa ni ya mifumo ya kudhibiti ajali za moto kwenye magari ambapo sasa magari yote ya kampuni hiyo ikiwamo mitambo, imefungwa mifumo hiyo kwenye injini.

Amesema mifumo hiyo inauwezo wa kutoa maji maalumu kuzima moto wowote unaoweza kutokea ndani ya injini ya gari au mtambo bila dereva kuamuru au kushuka kwenye gari kutafuta kizima moto.

Mkombati ameongeza kuwa teknolojia ya tatu ambayo GGML imekuja nayo kwenye maonesho hayo, ni matumizi ya ndege zisizo na rubani (drone) katika kupiga picha na video ndani ya mgodi ili kutambua usalama wa miamba kabla ya mfanyakazi kwenda kuchimba.

“Wafanyakazi walikuwa wanakwenda kuchimba, muda mwingine ndani ya miamba wanakuta mawe hayajakaa vizuri na kuleta wasiwasi kuhusu uthabiti wa miamba hiyo lakini sasa tumekuja na teknolojia ya drone ambayo huenda ndani kuchukua picha kisha tunaangalia wapi pako salama na sio salama ili kuhakikisha mazingira salama kwa wafanyakazi wetu,” amesema.

Teknolojia nyingine ameitaja kuwa ni ngazi maalumu ya uokozi ambayo inatumika kwenye njia ya dharura wakati wa kujiokoa kutoka ndani ya mgodi mbali na njia kuu ya kuingia na kutoka mgodini.

“Ukiacha chumba cha dharura “refugee chamber”, GGML imebuni njia ya dharura au escape way ambayo ina ngazi za kisasa zinazomuwezesha mfanyakazi anayejiokoa kutoka mgodini kupanda ngazi hizo bila kuteleza lakini pia kila baada ya mita sita anaweza kupumzika maana muda mwingine kunaweza kuwa na umbali wa mita 150 kutoka ndani ya mgodi kuja nje.

“Teknolojia hii inatumia kitu kama drum za plastic ambapo ndani kuna ngazi zisizoteleza na sehemu za kupumzika (platform) hivyo ni teknolojia mpya ambayo makampuni ya sekta hii ya madini yanaweza kuiga na kuitumia,” amesema.

Ofisa huyo mwandamizi wa usalama, pia ameongeza kuwa GGML sasa imekuja na choo maalumu ambacho kimebuniwa kwa ajili ya kuwasitiri wafanyakazi wanaochimba madini ndani ya mgodi.

Amesema choo hicho kinawawezesha wafanyakazi kujisitiri humohumo ndani ya mgodi bila kutoka nje ya mgodi kwenda kujisaidia haja kubwa au ndogo.

“Vyoo hivi vinapelekwa ndani ya mgodi ambapo mfanyakazi anatembea mita chache na kujisitiri. Ni vyoo vya kisasa, vina dawa za kuua wadudu na vikikaribia kujaa vinachukuliwa na mashine kupelekwa nje ya mgodi kusafishwa,” anasema.

Ameongeza kuwa wananchi waliotembelea banda hilo wameeleza kuvutiwa na vifaa hivyo vya ubunifu hali inayozidi kuwaongezea ari wafanyakazi wa kampuni hiyo kuzidi kuzingatia masuala ya usalama na afya mahali pa kazi na kufanya kazi kwa bidii.

Mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML, Novatus Chuwa amesema amejifunza vitu vingi ambavyo ni vigeni, lakini sasa vinamvuti kuchagua kufanya kazi migodini kwa sababu ya uhakika wa usalama mahali pa kazi.

Naye Alice Kyando amesema uwingi wa watu wanaokimbilia kwenye banda la GGML umethibitisha kuwa namna gani kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha mazingira ya kazi yanaandaliwa vema na kumfanya mfanyakazi anafanya kazi mahali salama na kwa kufuata miongozo ya kimataifa usalama na afya mahala pa kazi.
Share:

CHANZO CHA SISI KUHAMISHIWA KWENYE NYUMBA YA SERIKALI GHOROFANI



Wilayani Kyela Mbeya ndipo nilipokulia huko ila kuzaliwa nilizaliwa Tabora mjini pale Cheyo ‘A’ sijui ni lini familia yetu ilihamia huko Kyela kwa kuwa tumeanza kuishi huko kuanzia nikiwa mdogo kabisa. 

Mafuriko ndio changamoto kubwa sana ni sehemu ya familia zote za wanakyela kila mwaka mwezi wanne  angalau familia nyingi huwa zimejiandaa kwa janga hilo la mafuriko.

Mwaka wa 2022 kabla ya kuanza kwa mafuriko tulikuwa na changamoto kubwa sana ya umeme, hakukuwahi kuisha siku nzima bila ya umeme kukatika, mwanzoni tulipata shida lakini baadaye tulizoea na serikali ilitoa tamko kuwa changamoto hiyo ni kwa sababu vyanzo vya maji vimepunguwa sana na mvua zitakapoanza kunyesha vina vya maji vikirejea kila mahali tatizo hili litakwisha, tukavumilia.


Miezi mitatu tu baadaye tukaingia kipindi cha mafuriko awamu hii hali haikuwa shwari kabisa wapo walioingiliwa na mamba, wadudu ndani lakini sisi tuliingiliwa na maji na kila kitu kinachotumia umeme kilikufa palepale choo chetu cha shimo cha nje kilijaa na kufukiwa kabisa tukaanza kuishi bila ya choo, serikali iliamuu kila aishiye mahali pale ahame lakini kwetu hatukuwa na pahali pakukimbilia tulinyong'onyea na kuendelea kuishi hapohapo.


Mafuriko yakaendelea na serikali ikageuka mbogo sasa ikaamua kuwaleta migambo mtaani watutoe kwa nguvu sote tuliokatalia kwenye miji yetu, walifanikiwa wakatufukuza kwa jitihada zao na kwa mabavu.


Baba kichwa cha familia akaanza kupambana kupata haki kupitia marafiki zake wa serikalini na viongozi wadogowadogo wa mtaa lakini haikuleta matunda, kesi dhidi ya Jamhuri ni nzito siyo ya mtu mmoja hakuna aliyetusikiliza.


Miezi saba tukawa tunaishi kama wakimbizi kwenye nyumba za kupanga huku na huko, mpaka pale tulipopata msaada wa daktari BAKONGWA kupitia whatsapp +243990627777.

Mjomba wangu, shemeji wa baba ndiye aliyetupa taarifa hizi kuwa tunaweza kupewa rejesho letu kama tukimpata mtu sahihi wa kutusaidia akamtaja daktari huyo.

Tulimtafuta daktari na kwenye tovuti zake https://bakongwadoctors.com tukatembelea akatupa dawa ya kutusafisha nyota na kuondoa pingamizi tuliporudi serikalini tena waliliona hilo na kutupa haki yetu stahiki walituhamishia kwenye nyumba za serikalini New Forest tena kwenye ghorofa sasa tumeanza maisha mapya na shida za nyuma zote tumesahau, asante sana kwa daktari bakongwa na tiba zako.

 


Share:

MIGODI YA BARRICK YA BULYANHULU, NORTH MARA NA BUZWAGI YATOA ELIMU YA USALAMA NA AFYA KWA JAMII KATIKA MAONESHO YA OSHA MJINI MOROGORO


Mwenyekiti wa Bodi ya OSHA Dkt. Adelhelm Meru (mwenye suti) akikabidhiwa Sanduku maalimu lenye vifaa maalimu vya huduma ya kwanza na Safety Coordinator wa mgodi wa Bulyanhulu , Hassani Kallegeye, Kwa ajili ya kuwagawia wajasiriamali wa mkoa wa Morogoro waliopewa mafunzo na Barrick wakati wa wiki ya OSHA Maonesho usalama na Afya katika Kuadhimisha siku ya Usalama na Afya mahala pa kazi Duniani yanayofanyika kitaifa mkoa wa Morogoro wengine kwenye picha ni wafanyakazi wa Barrick.
Wajumbe wa kamati ya majaji wa tuzo za OSHA na wageni mbalimbali walipata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya migodi ya Barrick.
Wajumbe wa kamati ya majaji wa tuzo za OSHA na wageni mbalimbali walipata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya migodi ya Barrick.
Wajumbe wa kamati ya majaji wa tuzo za OSHA na wageni mbalimbali walipata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya migodi ya Barrick.
Wajumbe wa kamati ya majaji wa tuzo za OSHA na wageni mbalimbali walipata fursa ya kutembelea mabanda ya maonesho ya migodi ya Barrick.
Waendesha pikipiki wakipatiwa mafunzo ya usalama yanayoendeshwa na Barrick North Mara.
Waendesha pikipiki wakipatiwa mafunzo ya usalama yanayoendeshwa na Barrick North Mara.
Baadhi ya mama lishe mkoani Morogoro walipata fursa ya kupata mafunzo ya kuzima moto yanayoendeshwa na wataalamu wa usalama kutoka migod yab Barrick.
Baadhi ya mama lishe mkoani Morogoro walipata fursa ya kupata mafunzo ya kuzima moto yanayoendeshwa na wataalamu wa usalama kutoka migod yab Barrick.

***

Migodi ya Barrick ya Bulyanhulu,North Mara na Buzwagi imetumia maadhimisho ya siku ya Usalama na Afya mahali pa kazi Duniani kwa kutoa elimu ya usalama katika makundi mbalimbali kwa jamii mjini Morogoro sambamba na kugawa vifaa vya kinga ya majanga.
Makundi ambayo yamefikiwa na mafunzo hayo ni waendeshaji pikipiki za biashara maarufu kama ‘bodaboda’mama lishe pia wananchi kutoka maeneo mbalimbali wamekuwa wakitembelea mabanda ya maonesho ya migodi hiyo kwenye maonesho yanayoendelea yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalamana Afya Mahali pa Kazi (OSHA)
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 28,2023





















Share:

Thursday 27 April 2023

MILEMBE AUAWA NA WASIOJULIKANA KISHA KUTUPWA KWENYE NYUMBA YAKE


Milembe Selemani(43)

Milembe Selemani(43), mkazi wa mtaa wa Mseto halmashauri ya mji Geita, aliyekuwa kitengo cha ugavi mgodi wa GGML, ameuawa kwa kukatwa viungo vya mwili wake na watu wasiojulikana na mwili wake kutupwa kwenye moja ya nyumba alizokuwa anajenga zilizopo mtaa wa Mwatulole Kata ya Buhalahala.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Geita Berthaneema Mlay, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku watu wanne wakishikiliwa kwa ajili ya uchunguzi.

Share:

KATIBU MKUU IKULU ATAKA WAFANYAKAZI TASAF KUZINGATIA MAADILI

Mwandishi Wetu

WAFANYAKAZI wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) wametakiwa kufanya kazi kwa ueledi na kuzingatia maadili huku wakiepuka ubaguzi wa aina yoyote katika utekeleaji wa majukumu yao.

Hayo yamesemwa leo AAprili 27, 2023 na Katibu Mkuu Ikulu, Mululi Mahendeka alipokuwa akifungua Mkutano wa Mwaka wa wafanyakazi hao unaofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa APC Bunju, Dar es Salaam.

Mahendeka amesema kwa moja ya changamoto zinazoukabili mfuko huo ni baadhi ya wanasiasa kupotosha lengo halisi ya Mfuko na kuhusisha kazi zake na itikadi za kisiasa na ukabila.

Amesema kwa kuwa wako wanasiasa, kwa malengo wanayoyajua wao, wamekuwa wakieneza habari potofu kuwa kazi wa Mfuko zinahusiana na ikitadi za kisiasa, ni jukumu la wafanyakazi hao kuhakikisha wanafanya kazi kwa kufuata taratibu zilizopo na hivyo kuepuka ubaguzi wa itikadi za kisiasa, kidini na kikabila.

“TASAF ni taasisi ya Serikali na hivyo inafuata taratibu za kiserikali. Hakikisheni mnafanya kazi kwa bidi ueledi na maarifa. Fuateni miongozo ya Serikali ikiwemo kutunza siri za Serikali,” amesema.

Ameitaka menejienti ya TASAF kutambua majukumu yake na kuyatekeleza kwa ukamilifu , kutembelea miradi katika mamlaka za utekelezaji, kuzungumza na walengwa na kujua changamoto zao ii iwe rahisi kuzitatua. “Fanyeni kazi sawasawa na jina la mfuko na muweke kipaumbele kwa maendeleo ya jamii,” amesisitiza.

Amewataka kwafanyakazi kutunza rasilimali za taasisi ikiwemo magari, kompyuta. mifumo na kompyuta mpakato na kufanya kazi zilizopo na kulingana na sera kukidhi matarajio ya Serikali kwa mfuko huo.

“Mambo ya uendeshaji wa miradi yameainishwa vizuri katika andiko la mradi lililosainiwa kati ya Serikali na wadau wa maendeleo. Someni andiko la mradi kwa makini ili mjue mnachotarajiwa kufanya,” amesema.

Akitoa shukurani kwa Katibu Mkuu, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Kitaifa ya TASAF, Peter Ilomo amesema Kamati yake na Menejimenti inazingatia maelekezo hayo na wakati wa mkutano kama huo watatoa mrejesho kuhusu utekelezaji wa maelekezo.
Katibu Mkuu Ikulu Mululi Mahendeka akizungumza wakati akifungua mkutano wa mwaka wa wafanyakazi wa TASAF unaoendelea jijini Dar es Salaam
Share:

BARRICK KUENDELEA KUTOA FURSA KWA WANAWAKE KUFANYA KAZI KWENYE SEKTA YA MADINI

Baadhi ya wahitimu wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi

Baadhi ya wahitimu wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi
Meneja Mawasiliano wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa akiongea wakati wa mahafali ya kidato cha sita katika shule ya sekondari ya sekondari ya Jenerali David Musuguri iliyopo wilayani Muleba mkoani Kagera.
Wahitimu wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi na wageni waliohudhuria mahafali hayo.
Baadhi ya wazazi wa wahitimu wakifuatilia matukio wakati wa mahafali hayo.
Wahitimu wa kidato cha sita wakitoa burudani wakati wa mahafali hayo.
Wahitimu wa kidato cha sita wakitoa burudani wakati wa mahafali hayo.

Kampuni ya Barrick nchini imeeleza dhamira yake ya kuendelea kutoa fursa kwa Wanawake kufanya kazi kwenye migodi yake nchini ili kuondoa dhana iliyojengeka kwa muda mrefu kuwa ajira za migodini ni kwa ajili ya wanaume na imewataka wanafunzi walioko mashuleni na vyuoni kuchangamkia kusoma masomo yanayoendana na sekta ya madini kwa kujiamini.

Hayo yamebainishwa na Meneja Mawasiliano wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa , wakati wa mahafali ya kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Jenerali David Musuguri, iliyoko Kata muhutwe wilayani Muleba Mkoani Kagera ambapo alikuwa ni mgeni rasmi.

Aliwaasa wahitimu hususani wasichana watakapojiunga na vyuo wasiogope kusoma masomo ya Jiorogia na mengine yanayohusiana na sekta ya madini kwa kuwa sekta hiyo bado inazo fursa nyingi na wanawake hawapaswi kuachwa nyuma kuchangamkia fursa hizo kama ilivyo sasa idadi ya wanawake ni wachache katika sekta ya madini kwa kulinganisha na Wanaume.

“Kampuni ya Barrick imedhamiria kwa dhati kuhakikisha inaongeza idadi ya wafanyakazi wanawake katika migodi yake ya Bulyanhulu na North Mara na hivi sasa tunao wafanyakazi Wanawake ambao wanaendelea kufanya kazi zao kwa ufanisi na weledi mkubwa”, alisema Mutagahywa.

Pia aliwataka wahitimu kutobweteka bali watumie elimu waliyoipata na watakayoendelea kuipata kuwa wabunifu ili watakaokosa ajira waweze kujiajiri na kutatua changamoto mbalimbali zilizopo kwenye jamii hususani kipindi hiki ambacho kuna upungufu mkubwa wa ajira nchini na katika nchi nyingi duniani kote.

Mkuu wa shule hiyo, Alchard Kashamba, alisema shule hiyo imefanya mahafali ya sita tangu, kupandishwa hadhi ya kuwa na kidato cha sita mwaka 2007 kwa kuongeza udahili wa masomo ya sayansi na Sanaa na kwa mwaka huu ikiwa na jumla ya wahitimu 264 wasichana.

Alisema kwa Sasa shule ina majengo 26 mabweni matano,bwalo la chakula Moja,maktaba na madarasa licha ya kuwa na changamoto ya baadhi ya vifaa vya kujifunzia na kufundishia kama wahitimu walivyoeleza katika risala yao kwa mgeni rasmi.

Mmoja wa wakazi wa kata ya Muhutwe Ansbert Mushumbushi, ambaye ni miongoni mwa wazazi waliohudhuria katika mahafali hayo alisema wanafurahishwa shule hiyo inavyoendelea kuwa na miundo mbinu mizuri na kufanya vizuri kitaaluma.

Share:

WADAU MBALIMBALI WATEMBELEA BANDA LA NACTVET KWENYE MAONESHO YA WIKI YA UBUNIFU

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), linashiriki katika maonesho ya wiki ya ubunifu yanayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma.

 Maonesho hayo yameandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na yanatarajiwa kudumu kwa siku tano, kuanzia tarehe 24 hadi 28 Aprili 2023.

Lengo la ushiriki wa NACTVET katika maonesho hayo ni kukutana na wadau mbalimbali ili kutoa elimu kuhusu majukumu ya Baraza na kutoa ufafanuzi kuhusu mambo mbalimbali yanayosimamiwa na kutekelezwa na Baraza.

Akizungumza katika maonesho hayo, Afisa Habari na Uhusiano wa Baraza , Bi. Casiana Mwanyika, amesema kuwa ushiriki wa NACTVET katika maonesho hayo ni muhimu ili kuwawezesha wadau kufahamu shughuli za Baraza na kujenga uelewa kwa wananchi.

 Hivyo basi, amewakaribisha wadau na wananchi kwa ujumla kutembelea banda la NACTVET ili kupata taarifa mbalimbali zinazofanywa na Baraza, ikiwemo kusimamia ubora wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH Dkt. Amos Nungu akiweka saini alipotembelea banda la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), katika Maonesho ya Wiki ya Ubunifu yanayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma.
Afisa Uhusiano wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) Casiana Mwanyika akiwa na mdau katika Maonesho ya Wiki ya Ubunifu yanayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma.
Wadau mbalimbali wakipata maelezo mara baada ya kutembelea banda la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), katika Maonesho ya Wiki ya Ubunifu yanayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma.
Baadhi ya wanafunzi walipotembelea banda la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), katika Maonesho ya Wiki ya Ubunifu yanayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri, Jijini Dodoma.
Share:

POLISI SHINYANGA WAKAMATA KONDOMU, BUNDUKI ZA MAKAMPUNI YA ULINZI ZIKIAZIMWA NA WAHALIFU

Na Halima Khoya  & Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limefanya ukaguzi wa kushitukiza kwenye malindo ya kampuni mbalimbali za ulinzi na kufanikiwa kukamata Bunduki 5 ambazo hazikufuata utaratibu wa kisheria zikitumika kuazimishwa kwa wahalifu huku likikamata vipodozi vyenye viambata vya sumu ambavyo haviruhusiwi kwa matumizi ya binadamu pamoja na bidhaa mbalimbali yakiwemo maboksi 9 ya kondomu zinazopaswa kutumika kwenye vituo vya afya na mashirika yanayosika na masuala ya kudhibiti UKIMWI.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamisi Aprili 27,2023, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amezitaja zilizokamatwa kufuatia ukaguzi wa kushitukiza wa malindo ya kampuni mbalimbali kuwa ni Bunduki aina ya MARK IV yenye namba TZ car 89936 na risasi 04 na Bunduki aina ya MARK IV yenye namba K 9239 na risasi 03.


Silaha zingine ni Bunduki aina ya MARK IV yenye namba D 6000 na risasi 01, Bunduki aina ya MARK IV yenye namba MG 564884 na risasi 02 na Short gun Birmingham England na risasi.


“Tumekamata bunduki hizi tano ambazo zilikuwa zikimilikiwa kinyume cha utaratibu chini ya kifungu 10(7) na 60 Cap 38 cha Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Silaha na Risasi ya Mwaka 2015 pamoja na kanuni zake GN 334 ya tarehe 30/12/2016 kanuni namba 14(2) na (3).
“Pia kupitia misako na Operesheni mbalimbali katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia tarehe 22/03/2023 hadi tarehe 26/04/2023 tumefanikiwa kukamata vitu na vielelezo mbalimbali ambavyo ni magodoro mawili, TV 05, Remote 01 ya Star X, Pard 05, PlayStation PS-3 01, Pikipiki 06 (MC 248 CYP- SANLG, MC 700 AQL-SANYA, MC 815 DQC, MC 494 DCM- KINGLION, MC 909 CEV-HAOJUE na MC 134 DDL-KINGLION), Redio Subwoofer 03, Redio ndogo 02, Sigara aina ya CLUB box 3 na pakiti 15 aina mbali mbali, Computer 02, Vitenge doti 05, Simu smart aina ya Honor, Saa 02 aina ya Titarium, Mtungi wa Gesi, Draya 01, Pombe ya moshi lita 120, Meza ya kuchezea kamari na karata zake tatu, Vifaa vya kupiga ramli chonganishi maarufu MBIGI, Panga 02 kubwa, Viuatilifu vya Serikali vya kuua wadudu wa Pamba”,ameeleza Kamanda Magomi.

Amevitaja vitu vingine vilivyokamatwa ni pamoja na Flash Disk ya 16GB aina ya Toshiba 02, Bhangi Kilogram 327 na kete 85, Mirungi bunda 05, Madumu tupu 14 yenye ujazo wa lita 20, Madumu 16 yenye ujazo tofauti tofauti yakiwa na mafuta ya Petrol Lita 269 yote yakidhaniwa kuibiwa kwenye mradi wa ujenzi wa reli ya SGR.
“Vitu vingine ni Vipodozi vyenye viambata vya sumu ambavyo haviruhusiwi kwa matumizi ya binadamu (Epiderm crème box 01, Betasol crème box 03, CaroLight box 01), Pombe kali aina ya Hakiri box 12, Kondom box 09 zikiwa kwenye maduka ya watu binafsi ambazo zinazopaswa kutumika kwenye vituo vya afya na mashirika yanayosika na masuala ya kudhibiti UKIMWI.
 Mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku pakiti 100, Kiberiti bunda 02, Extention 02, Lita 67 ya mafuta ya kula na bidhaa mbali mbali za madukani”,amesema.


Katika hatua nyingine amesema Jeshi la Polisi kupitia kitengo chake cha Upelelezi kwa kipindi hicho cha mwezi mmoja limewafikisha watuhumiwa 132 mahakamani katika kesi 129 zilizoripotiwa katika kipindi hicho ambapo mpaka sasa kesi zilizopata mafanikio ni kesi 62 ikiwa ni pamoja na watuhumiwa kufungwa jela/kifungo cha nje pamoja na kulipa faini.


Miongoni mwa kesi hizo 62 zipo kesi ambazo zimehusisha makosa ya ukatili wa kijinsia ambazo ni kumpa mimba Mwanafunzi kesi 04, kubaka kesi 02 na kulawiti kesi 01.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea kuwaasa wananchi kufuata sheria za nchi wakati wote na kutojihusisha na vitendo vya kiuhalifu kwa namna yoyote ile.


Aidha Jeshi la polisi linatoa wito kwa wananchi kutoa taarifa dhidi ya uhalifu na wahalifu ili kutokomeza vitendo hivyo miongoni mwa jamii inayotuzunguka na halitokuwa na muhali kwa yeyote yule ambaye atajihusisha na vitendo vya kiuhalifu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Aprili 27,2023. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Aprili 27,2023
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Aprili 27,2023
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Aprili 27,2023

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Aprili 27,2023
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vitu mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vitu mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vitu mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akionesha vitu mbalimbali vilivyokamatwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger