Thursday 27 January 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 27,2022

 

Magazetini leo Alhamisi January 27 2022

















Share:

Wednesday 26 January 2022

MTATURU ASISITIZA VIPAUMBELE MFUKO WA JIMBO



............................................................

KAMATI ya mfuko wa kuchochea maendeleo ya jimbo imeketi chini ya mwenyekiti wake Mbunge wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu na kugawanya fedha kiasi cha Sh Milioni 44,024,000 ikiwa ni mgao kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Akimkaribisha mwenyekiti kwa ajili ya kufungua kikao, katibu wa mfuko ambaye ni afisa mipango wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi Joyce Emmanuel amemshukuru mbunge huyo kwa utayari wa kuitisha kikao mapema na kusoma maombi yanayofikia Sh Milioni 157 yaliyoletwa kutoka kwenye vijiji na kata mbalimbali.

Baada ya kupokea taarifa hiyo Mh Mtaturu kabla ya kufungua kikao aliwaomba wajumbe wayapitie maombi kwa kina na kupitisha vipaumbele ili kuunga mkono juhudi za wananchi kwenye miradi yao.

“Ndugu zangu miradi tuliyoiunga mkono mwaka wa fedha wa 2020/20 21 imeonyesha tija na kuna maeneo tayari imeanza kutoa huduma,niwasihi wajumbe na mratibu wa mfuko kufuatilia utekelezaji wa miradi hii ili ilete tija kwa wananchi,”alisema.

Amewaahidi wajumbe kuendelea kuibana serikali kutenga fedha zaidi za miradi kwenye jimbo na wilaya.

Wakizungumza katika kikao hicho baadhi ya wajumbe wameshauri miradi iliyoanzishwa na nguvu za wananchi iungwe mkono kupitia fedha hizo ili iwe chachu kwenye jamii.

“Tunakupongeza Mh Mbunge kwa juhudi zako ukiwa bungeni kuomba fedha ambazo zinatekeleza miradi mingi jimboni kwa sekta za elimu, afya, Maji, umeme na barabara,”alisema.
Share:

BODI YA FILAMU YAWATAKA WADAU KWENDA NA TEKNOLOJIA


Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo akifafanua masuala ya tasnia ya Filamu wakati wa kikao na wadau wa tasnia ya Filamu , Viwanja vya Chinangali park Jijini Dodoma.


Afisa Maendeleo ya Filamu Happy Maduhu akieleza jambo wakati wa kikao na wadau wa tasnia ya Filamu , Viwanja vya Chinangali park Jijini Dodoma


Gosbert Mvungi moja ya Mzalishaji wa kazi za Filamu wakati wa kikao na wadau wa tasnia ya Filamu , Viwanja vya Chinangali park Jijini Dodoma

........................................................

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Kiagho Kilonzo amewataka wadau wa Tasnia ya Filamu kutumia fursa za teknolojia ili kuongeza wigo wa masoko ya kazi za Filamu kwa lengo la kujiongezea kipato na manufaa kwa jamii.

Ameyasema hayo wakati akiongea na wadau wa tasnia ya Filamu wakiwemo wazalishaji, waigizaji, waandishi wa miswada ya Filamu wa Jiji la Dodoma Januari 25,2022 katika Viwanja vya Chinangali Park, Jijini hapo.

Akifafanua kuhusu suala la matumizi ya Teknolojia katibu amebainisha kuwa ili kazi za Filamu ziweze kuwafikia watu wengi na kuwa na manufaa makubwa kwa wanatasnia ni vyema kujielekeza katika kupeleka kazi hizo kwenye vingamuzi vya Televisheni zenye Chaneli za Filamu, matumizi ya mitandao ya kijamii kama Youtube na mitandao mingine. Jambo ambalo linaongeza tija ya usambazaji wa kazi hizo kwa urahisi tofauti na hali ilivyokuwa awali.

“Nitoe rai kwenu kwamba tusibaki nyuma katika matumizi ya Teknolojia, twende na kasi ya teknolojia Pamoja na kuongeza ubunifu katika kazi zetu ili twende na kasi ya ushindani wa dunia,” alisema Dkt. Kilonzo

Aidha, Katibu amesema miongoni mwa mikakati mahususi ya Bodi ya Filamu katika kuweka mazingira wezeshi kwa wanatasnia ya Filamu wa mikoa yote ili kuweza kufikia malengo yao ni pamoja na kuendelea na mradi wa kurasimisha Vibanda Umiza kupitia maafisa Utamaduni wa mikoa. Vilevile Bodi kuendelea kutoa mafunzo kwa wadau ili kuboresha na kuinua tasnia ya Filamu nchini.

Sambamba na mikakati hiyo, ilielezwa kuwa Bodi itaendelea kushirikiana na kutoa tuzo mbalimbali za kutambua utendaji mzuri wa wanatasnia kwa lengo la kuwaongezea ari na motisha ya kazi za Filamu.

Kwa upande wake mzalishaji wa kazi za Filamu Bw. Gosbert Mvungi ameshauri Bodi kuendelea kutafuta fursa za wawekezaji kuwekeza katika Tasnia ya Filamu hasa katika masoko ya Televisheni kwaajili ya kazi za Wanatasnia. Jambo ambalo litaongeza fursa ya kuwainua na kuwaendeleza tasnia ya Filamu nchini.

Pamoja na mambo mengine wadau hao wamebainisha kuwa matumizi ya lugha ya Kiswahili ni moja ya suala muhimu linalosaidia uuzaji mzuri wa Filamu za Kitanzania na kuwezesha Filamu hizo kushika nafasi bora kitaifa na Kimataifa.
Share:

MIGODI YA BARRICK NCHINI TANZANIA MBIONI KUFIKIA DARAJA LA KWANZA LA UZALISHAJI


Rais na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow (kushoto) akiwaeleza Waziri wa Madini,Dk. Doto Biteko, Waziri wa Tamisemi, Innocent Bashungwa, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Sophia Mjema (wa nne kushoto) jinsi mtambo wa kielekitroniki wa uchumbaji madini chini ardhi unavyofanya kazi wakati wa kutangaza uzalishaji wa dhahabu kufikia wakia 500,000 kwa migodi North Mara na Bulyanhulu mwishoni wa mwaka 2021.
Wataalamu wa uchimbaji madini wa Mgodi wa Bulyanhulu wakionyesha jinsi mtambo wa kielekitroniki wa uchimbaji unavyofanya kazi.
Rais na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow, akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea mgodi wa Bulyanhulu mkoani Shinyanga juzi wakati wa kutangaza uzalishaji wa dhahabu kufikia wakia 500,000 kwa migodi North Mara na Bulyanhulu mwishoni wa mwaka 2021. (Kushoto) ni Waziri wa Madini Dk. Doto Biteko na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Sophia Mjema.
Waziri wa Madini, Dk.Doto Biteko akizungumza waandi wa habari alipotembelea mgodi wa Bulyanhulu mkoani Shinyanga jana wakati wa Rais na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Britow (katikati) akitangaza uzalishaji wa dhahabu kufikia wakia 500,000 kwa migodi North Mara na Bulyanhulu mwishoni wa mwaka 2021. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa shinyanga, Sophia Mjema.
Waziri wa Madini,Dk.Doto Biteko na ujumbe wake wakitembezwa katika maeneo ya mgodi wa Bulyanhulu

****
Kampuni ya Barrick Gold Corporation (NYSE:GOLD) (TSX: ABX) – Migodi ya North Mara na Bulyanhulu, iliyokuwa imesimamisha uzalishaji wakati Barrick ilipoichukua na kuwa chini ya usimamizi wake miaka miwili iliyopita, imeweza kufikisha uzalishaji wa zaidi ya wakia 500,000 za dhahabu kufikia mwishoni mwa mwaka 2021, hivyo kufikia vigezo vya uzalishaji vya daraja la juu (Tier one)

Mafanikio haya yamefikiwa wakati migodi yote miwili ikiendelea kuwa na hadhi ya ubora wa kimataifa ISO 45001 katika uzingatiaji usalama na ISO 14001 katika utunzaji mazingira. Kama ilivyo migodi mingine inayoendeshwa na Barrick.

Kwa upande wa North Mara, mgodi uko mbioni kuwa kwenye mfumo wa uzalishaji uliounganishwa kikamilifu kufuatia mpango wa uchimbaji dhahabu katika mashimo ya Nyabirama katika kipindi hiki cha robo mwaka na Nyabigena katika kipindi cha tatu cha robo mwaka wa 2022.Hatua hii inatarajiwa kuuongezea rasilimali mgodi huo na kuuwezesha kuwa na mfumo wa uendeshaji wa shughuli zake unaokidhi mahitaji yake.

Mgodi wa Bulyanhulu nao kwa sasa umeimarishwa upya na kuwa mgodi wenye hadhi ya kimataifa, unaoendeshwa kwa gharama ya chini. Aidha, hatua yake ya kuanzisha uchimbaji wa chini ya ardhi (underground mining) umeuongezea mgodi huo muda mrefu zaidi wa kuendelea na uzalishaji tangu Desemba 2021.

Migodi yote miwili inatarajiwa kuripoti ukuaji mkubwa wa raslimali zake katika kipindi cha mwaka 2021.

Barrick inaendelea kujiimarisha katika maeneo ya Bulyanhulu kutokana na kupata leseni sita za kutafiti madini katika maeneo yanayopakana na mgodi huo. Timu ya wataalamu wa jiolojia na utafiti wa kampuni hiyo inaendelea kutafuta fursa katika sehemu nyinginezo nchini Tanzania

Akizungumza na vyombo vya habari vya hapa nchini hapa leo, Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick Mark Bristow, alisema utendaji mzuri wa migodi hiyo umetokana na kuzingatia miongozo ya kukabiliana na ugonjwa wa UVIKO-19 na utoaji wa chanjo kwa wafanyakazi wake, asilimia 26.45% kati yao tayari wamechanjwa na 20.25% wamepata chanjo kamili ya UVIKO-19 . Alisema, Barrick inafanya kazi kwa karibu na mamlaka za afya nchini na katika siku za usoni inatarajia kutoa msaada wa mashine nne za kupima Covid -19 (PCR) kwa hospitali zinazozunguka maeneo ya migodi.

Migodi pia iliendelea kuajiri na kuwapatia ujuzi Watanzania. Asilimia 97% ya wafanyakazi ni watanzania , huku 41% wakitoka katika vijiji vinavyoizunguka. Pia imeimarisha ushirikiano na wazabuni wa ndani. Tangu Barrick ilipoingia tena Tanzania mwaka 2019, imetumia Zaidi ya dola bilioni 1.8 katika kodi, mishahara na malipo kwa wafanyabiashara wa ndani. Pia imewekeza dola milioni 6.7 katika miradi ya elimu katika jamii, afya na miundombinu.

Akirejelea Ripoti ya Haki za Binadamu ya Barrick iliyochapishwa hivi karibuni, Bristow alisema masuala ya mazingira na mengine ambayo kampuni hiyo iliyarithi kutoka kwa waendeshaji wa awali wa migodi hiyo, yanaendelea kutatuliwa au yametatuliwa kabisa.

Maendeleo makubwa ya kampuni katika suala hili yalidhihirishwa mwezi uliopita, pale ambapo timu ya Barrick ilitumia ufundi na ubunifu wa hali ya juu kuhakikisha kwamba bwawa la kuhifadhi mabaki ya taka zitokanazo na mchakato wa uzalishaji dhahabu unahifadhi maji yanayoendana na muundo wake wa awali katika mgodi wa North Mara”, Bristow alisema. Utendaji wa bwawa hilo unasaidiwa na mtambo mpya na wa kisasa wa kutakatisha maji.


Share:

WAZIRI BITEKO : UBIA BAINA YA SERIKALI NA BARRICK UMELETA TIJA KUBWA

 
Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa ubia baina ya Serikali na kampuni ya Barrick (Barrick Gold Corporation) uliounda kampuni tanzu ya Twiga (Twiga Minerals Corporation Limited) umeleta tija kubwa katika sekta ya madini nchini.

Waziri Dkt. Biteko ameyasema hayo Januari 25, 2022 alipotembelea mgodi wa Bulyanhulu uliopo Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ikiwa ni miongoni mwa migodi inayoendeshwa na kampuni ya Twiga kwa ubia baina ya Serikali yenye asilimia 16 na Barrick yenye asilimia 84.


Amesema ubia huo umechochea fursa zaidi za ajira kwa watanzania ambapo katika mgodi wa Bulyanhulu zaidi ya asilimia 96 ya wafanyakazi ni watanzania ambapo asilimia 41 wanatoka katika maeneo yanayozunguka mgodi.


Aidha Waziri Dkt. Biteko ameongeza kuwa hatua hiyo imechochea ongezeko la makusanyo ya Serikali katika Sekta ya madini kutoka chini ya shilingi 115 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi bilioni 528 mwaka 2020/21 huku pia ikifungua ubia zaidi baina ya Serikali na makampuni mengine.


Katika hatua nyingine Dkt. Biteko amewatoa hofu wafanyakazi katika mgodi wa Bulyanhulu kuwa hawatapoteza ajira zao kufuatia mabadiliko yanayofanywa na mgodi huo kutoka kwenye mitambo inayoendeshwa na binadamu chini ya mgodi kwenda kwenye mitambo inayoendeshwa kwa kompyuta (automine) kwani bado watakuwa na fursa ya kuendesha mitambo hiyo wakiwa ofisini.


Kwa upande wake Rais na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Barrick duniani, Dkt. Mark Bristow amekiri kuwa ubia baina ya Serikali ya Tanzania na kampuni yake umeleta tija kubwa hususani uzalishaji katika migodi ya Bulyanhulu na North Mara hadi kufikia wakia laki tano za dhahabu hadi kufikia mwishoni mwa mwaka jana 2021 huku ukiifanya migodi hiyo kuwa na hadhi ya kimataifa.


Naye Mkuu wa Mkoa Shinyanga, Dkt. Sophia Mjema amesema atahakikisha mgodi unashirikiana kwa ukaribu na Serikali za Mitaa/ Halmashauri na kwa kuwashirikisha wananchi ili kuibua miradi ya uwajibikaji kwa jamii (CSR) itakayokuwa na tija badala ya kusubiri kuletewa miradi bila makubaliano ya pamoja.


Ziara ya Waziri Dkt. Biteko katika Halmashauri ya Msalala ilitamatika katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kakola ambapo alitumia fursa hiyo kusisitiza kuwa Serikali imeweka msisitizo wa kuhakikisha wananchi wananufaika na uwepo wa mgodi wa Bulyanhulu huku ikihakikisha wenye madai halali ya fidia ikihakikisha wanalipwa.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Waziri wa Mdini, Dkt. Doto Biteko akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kakola Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama.
Mkuu wa Mkoa Shinyanga, Dkt. Sophia Mjema.
Rais na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Barrick duniani, Dkt. Mark Bristow akiwa kwenye kikao baina yake na Waziri wa Madini, Dkt. Doto Biteko (hayuko pichani).
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye kikao hicho.
Wafanyakazi wa mgodi wa Bulyanhulu wakiendesha mitambo ya kuchoronga miamba ya madini chini ya mgodi kwa kutumia mfumo wa kidigitali (automine) wakiwa ofisini.
Waziri wa Madini, Dkt. Dkt. Biteko pamoja na ujumbe alioambatana nao akiangalia mfumo wa kidigitali uliofungwa katika mgodi wa Bulyanhulu kwa ajili ya kuendesha mitambo ya kuchoronga miamba ya madini chini ya mgodi kwa kutumia kompyuta (automine).
Tazama Video hapa chini

Share:

THRDC YAPAZA SAUTI KUHUSU MGOGORO WA ARDHI WILAYANI NGORONGORO

Share:

Tuesday 25 January 2022

MRADI WA AKILI BANDIA WAZINDULIWA UDOM



Serikali ya Tanzania imezindua mradi wa maabara ya akili bandia (artificial intelligence) utakaosaidia kurahisisha shughuli za maendeleo nchini.

Hayo yamesemwa jana Jumatatu Januari 24, 2022 na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mohamed Khamis Abdullah akizindua mradi huo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

“Kama hivi wengi tunavyoangalia dunia za sasa hivi wenzetu wameshakwenda mbele zaidi. Sometimes (wakati fulani) unakuta watu wanavyokwenda makazini wanajibiwa na robot, unapopanda lifti, mwendo kazi,” amesema.

Naibu Waziri huyo amesema teknolojia hiyo inatumika hata mashambani ambapo badala ya kwenda mtu linatumika robot na maofisini.
Share:

WADAU WA MASUALA YA ELIMU WAGUSWA NA MPANGO MKAKATI WA MAMLAKA YA ELIMU TANZANIA (TEA)

Wadau kutoka sekta na Idara mbalimbali za Serikali wamekuta leo jijini Dar es Salaam kujadili rasimu ya mpango mkakati wa nne wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ambao utatumika kwa miaka mitano hadi 2026. Katika kikao kazi hicho cha siku moja, wadau wamefurahishwa na jinsi ambavyo TEA imeweka vipaumbele katika mambo ya kimkakati ikiwemo TEHAMA.

Katika majadiliano hayo, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imepongezwa kutokana na jitihada zake za kusimamia na kuboresha miundombinu ya Elimu hasa katika mazingira ambayo ni magumu kufikika kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa elimu bora na kwa usawa.

Mkurugenzi Msaidizi kutoka TAMISEMI Bw. Musa Otieno ambaye alikuwa mmoja wa wadau katika kikao hicho amesema, TEA imefanya kazi nzuri sana ya kuboresha miundombinu ya shule ambapo imejenga madarasa, nyumba za waalimu, matundu ya vyoo, mabwalo ya vyakula pamoja na kununua madawati kwenye maeneo ya pembezoni mwa miji ambako ni ngumu kufikika.

Jitahada zote hizi zinalenga kusogeza huduma za sekta ya elimu karibu na wananchi ili kuhakikisha kila mtoto anapata nafasi ya kusoma karibu na mazingira anayoishi na hili linadhihirika wazi kwani mpango mkakati wa miaka mitano ijayo umebainisha kazi zinazooenda kufanyika katika kusimamia upatikanaji wa elimu bora, alisema Otieno

Nae mdau mwingine kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw.Gerald Sando, ameishukuru Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kazi zake na kusema kazi hizo ni endelevu na zinaonekana kwa macho.

Sando amesema, kazi za TEA zinagusa maisha ya wananchi moja kwa moja na kuongeza thamani kwenye maisha ya wale wa kipato cha chini kupitia mradi wa kuongeza ujuzi (SDF) ambao unafadhiliwa na TEA.

Kikao kazi cha kupitia rasimu ya mpango mkakati wa Mamalaka ya Elimu Tanzania (TEA) wa miaka mitano hadi 2026 kimefanyika jijini Dar es Salaam na mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi Mkuu Bi. Bahati Geuzye.

Akitoa salaam za ukaribisho Mkurugenzi wa huduma za Taasisi Dr. Erasmus Kipesha ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho alisema, tangia Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imeanzishwa mwaka 2001, hii ni rasimu ya nne ya mpango mkakati.

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ni Taasisi ya umma iliyoanzishwa kwa Sheria ya Mfuko wa Elimu Na. 8 ya mwaka 2001 ikiwa na jukumu la kusimamia uendeshaji wa Mfuko wa Elimu wa Taifa kwa lengo la kuongeza nguvu za Serikali katika kuinua upatikanaji wa elimu bora kwa usawa katika ngazi zote za elimu Tanzania Bara na elimu ya juu kwa Tanzania Zanzibar.

 
Mkurugenzi wa huduma za Taasisi kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha akitoa salaam za ukaribisho kwa wajumbe (hawapo pichani) waliohudhuria kikao kazi cha siku moja kujadili rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Bi. Bahati Geuzye akitoa hotuba ya ufunguzi katika kikao kazi cha siku moja cha kujadili rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA kwa wadau wa masuala ya elimu (hawapo pichani)

 Baadhi ya wadau waliohudhuria kikao kazi cha siku moja wakifuatilia uwasilishwaji wa rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA.

Baadhi ya wadau waliohudhuria kikao kazi cha siku moja wakifuatilia uwasilishwaji wa rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA.
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais -TAMISEMI Bw. Musa Otieno akichangia maoni yake kuhusu rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA


Bw.Gerald Sando kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa – Dar es Salaam akitoa maoni yake kuhusu rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA.

Mkurugenzi wa huduma za Taasisi kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt Erasmus Kipesha akiwasilisha rasimu ya mpango mkakati wa miaka mitano wa TEA kwa wadau wa masuala ya elimu.


Share:

WASINDIKAJI NA WAZALISHAJI WA MAZIWA WAMETAKIWA KUHAKIKISHA BIDHAA HIZO KUWA BORA

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto SSI.Mbarak Alhaji Batenga ( kati kati), Katibu Tawala Wilaya ya Kiteto Bw. Fadhili D. Alexander (Kushiro) na Meneja kanda ya Kaskazini (TBS) Bi Happy B. Kanyeka (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo kwa wasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa maziwa na bidhaa za maziwa. Mafunzo haya yanalenga kuwaelimisha wadau wa maziwa kuhusu viwango vya maziwa na bidhaa za maziwa , utaratibu wa kuthibitisha ubora wa maziwa na bidhaa za maziwa, kanuni bora na taratibu za kusindindika maziwa na bidhaa za maziwa pamoja na kanuni bora za ufugaji.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Muhandisi Richard Runyango akifungua mafunzo kwa wasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa maziwa na bidhaa za Maziwa wilayani Arumeru.
Mhe. Runyango aliwataka washiriki kuzingatia mada zote zinazotolewa na kuzifanyia kazi ili waweze kuzalisha Maziwa na bidhaa za Maziwa bora zitakazoweza kushindana katika soko la ndani na nje ya nchi.
Mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Hai Bw. Yassin A Zayumba akifungua mafunzo kwa wasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa Bidhaa za Maziwa wilayani Hai.
Maafisa wa TBS wakitoa mada kuhusu faida na matakwa ya kiwango cha maziwa na bidhaa za maziwa pamoja na kaununi bora za usindikaji, vifungashio na ufungashaji wa maziwa na bidhaa za maziwa . Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha washiriki kuboresha na kuongeza thamani katika mnyororo wa uzalishaji wa bidhaa husika na hatimae kuzalisha bidhaa bora na salama.




************************


Wajasiriamali wanaojishughulisha na ufugaji, ukusanyaji, ubebaji na usindikaji wa maziwa na bidhaa za maziwa wameshauriwa kuzalisha na kusindika maziwa yenye ubora ili kufanikisha azma ya Serikali ya kukuza sekta ya viwanda nchini.




Ushauri huo ulitolewa na Bi Happy Kanyeka wakati wa mafunzo kwa wafugaji, wasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa maziwa na bidhaa za maziwa yaliyofanyika katika wilaya za Kiteto (Manyara), Arumeru (Arusha) na Hai(Kilimanjaro)




Mafunzo hayo yamelenga kuwaelimisha wajasiriamali walio katika myororo wa thamani ya ufugaji, ukusanyaji wa maziwa ghafi, ubebaji na usindikaji wa maziwa na bidhaa za maziwa juu ya kanuni na matakwa ya msingi kuhusiana na shughuli wanazozifanya.




Akizungumza wakati wa mafunzo haya Bi Happy Kanyeka meneja wa kanda ya kaskazini (TBS) alisema, tunatambua kuwa sekta hii ya maziwa ina wajasiriamali wengi wadogo na wa kati ambao husindika na kupeleka sokoni maziwa na bidhaa za maziwa na walio wengi hufanya hivyo bila kufuata kanuni na taratibu zinazotakiwa hivyo kupelekea uwepo wa maziwa na bidhaa za maziwa hafifu sokoni pamoja na uharibifu na upotevu wa maziwa mengi sokoni.




“Kuna baadhi ya wasindikaji wa maziwa tayari walishaanza taratibu za kuthibitisha ubora wa bidhaa zao ili kukidhi matakwa ya viwango husika lakini kutokana na changamoto za kukosa elimu juu ya viwango imepelekea mchakato wa uthibitishaji ubora kuonekana mgumu hivyo basi katika mafunzo haya tumeelekezana kuhusu kanuni bora za usindikaji, kanuni bora za ufungaji, kanuni bora za afya, faida na matakwa ya kiwango cha maziwa na bidhaa za maziwa pamoja na utaratibu wa kuthibitisha ubora wa maziwa na bidhaa za maziwa” aliongeza Bi Kanyeka




Bi. kanyeka alisisitiza kuwa wilaya za Kiteto, Arumeru na Hai ni wilaya amabazo zinajihusisha na ufugaji wa ng’ombe wengi wakiwemo wa kienyeji na wa kisasa na usindikaji wa maziwa na bidhaa za maziwa ni moja ya shughuli inayofanya na wajasiriamali katika wilaya hizo.




“Mafunzo haya yametolewa katika maeneo muhimu sana yanayojishughulisha na Ufugaji wa Ng’ombe, usindikaji, usambazaji na uuzaji wa maziwa na bidaa za maziwa, pia ni azima ya serikali kukuza viwanda nchini endapo washiriki wa mafunzo haya watazingatia yale yote walioelekezwa taifa litakuwa na bidhaa bora na salama zitakazoweza kushindanishwa vyema katika sekta ya maziwa na bidhaa za maziwa ndani na nje ya nchi.”




Na katika kuhakikisha elimu inayotolewa inakidhi matarajio ya washiriki TBS imeshirikiana na taasisi nyingine ikiwemo SIDO, Bodi ya Maziwa (TDB) na TAMISEMI( ambao ni Afisa Afya, Afisa Mifungo, Afisa Biashara na Afisa Maendeleo ya Jamii)
Share:

Monday 24 January 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 25,2022

Magazeti ya leo Jumanne January 25 2022


MAGAZETI MENGI ZAIDI TUNALETA HIVI PUNDE.....

Share:

JESHI LAPINDUA SERIKALI...RAIS WA BURKINA FASO HAJULIKANI ALIPO


Jeshi limesema hali mbaya ya usalama ndio iliolishinikiza kumuondoa madarakani rais Kabore


Jeshi nchini Burkina Fasso linasema kwamba limechukua mamlaka na kumuondoa madarakani rais Roch Kabore.

Tangazo hilo lilitolewa katika runinga ya taifa na afisa mmoja wa jeshi , ambaye alisema kwamba serikali na bunge limevunjwa.

Kufikia sasa haijulikani bwana Kabore yuko wapi , lakini afisa huyo amesema kwamba wale wote wanaozuiliwa wapo katika eneo salama.

Mapinduzi hayo yanajiri siku moja tu baada ya wanajeshi hao kudhibiti kambi za jeshi huku milio ya risasi ikisika katika mji mkuu wa Ouagadougou..

Mapema , Chama tawala cha peoples Movement PMP kilisema kwamba wote Kabore na waziri mmoja wa serikali walinusurika jaribio la mauaji.

Siku ya Jumapili, wanajeshi waasi walitaka kufutwa kazi kwa maafisa wa jeshi na kuongezwa kwa raslimali za kukabiliana na wapiganaji wa Kiislamu.

Taarifa hiyo ilitolewa na kundi ambalo halijasikika hapo awali, Vuguvugu la Patriotic for Safeguard and Restoration au MPSR, kifupi chake cha Kifaransa.

"MPSR, ambayo inajumuisha vitengo vyote vya jeshi, imeamua kusitisha wadhifa wa Rais Kabore leo," ilisema.

Kabla ya tangazo hilo, Muungano wa Afrika na Umoja wa Afrika Magharibi Ecowas walilaani kile walichokiita jaribio la mapinduzi nchini Burkina Faso.


Ecowas imesema kwamba wanajeshi watawajibikia usalama usalama wa Bw Kaboré iwapo lolote litatokea.
Rais Roch Kabore

Video kutoka mji mkuu inaonekana kuonyesha magari ya kivita - yanayoripotiwa kutumiwa na rais - yakiwa na mashimo ya risasi na kutelekezwa mitaani.

Huduma za mtandao wa simu za mkononi zimekatizwa, ingawa mtandao wa laini zisizobadilika na wi-fi ya nyumbani zinafanya kazi

Bw Kaboré hajaonekana hadharani tangu mzozo huo uanze lakini machapisho mawili yalionekana kwenye akaunti yake ya Twitter kabla ya afisa huyo kutangaza kuwa amepinduliwa.

Baadaye alitoa wito kwa wale waliochukua silaha kuziweka chini "kwa maslahi ya taifa". Hapo awali Bw Kaboré alipongeza timu ya taifa ya kandanda kwa ushindi wao katika mechi ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Haijulikani ikiwa Bw Kaboré au mtu mwingine alichapisha tweets hizo.

Baadhi ya vyanzo vya usalama vinasema rais na mawaziri wengine wa serikali wanazuiliwa katika kambi ya Sangoulé Lamizana katika mji mkuu.

Siku ya Jumapili, mamia ya watu walijitokeza kuwaunga mkono wanajeshi hao na baadhi yao walichoma moto makao makuu ya chama tawala. Amri ya kutotoka nje wakati wa usiku imewekwa.

CHANZO - BBC SWAHILI
Share:

USAHA NA VIJIDUDU VILINITOKA, NILIVYORAMBA ASALI YA RAFIKI YANGU

 Niliishi katika kaunti ya Marsabit karibu na jirani yangu Kim ambaye alikuwa pia ni rafiki wangu wa dhati kwani alinisaidia mambo mengi maishani. 

Urafiki ule ulikuwa wenye kutamaniwa na wengi kwani hata watu wengi walisema kuwa tulikuwa marafiki lakini hiyo ilikuwa ni propaganda isiyo na msingi wowote.

 Siku ziliposonga, Kim alifanikiwa kupata jiko na hapo ikawa urafiki wangu na wake ukaanza kudidimia kwa kuwa wakati mwingi alitumia kukaa na mke wake. Hatungepata tena wakati wa kwenda kutazama mechi, kulewa vilabuni na kadhalika. 


Kwa wakati ule wote sikuwa nimefanikiwa kuoa kwani nilidhani kwamba wakati wangu murua haukuwa umefika. Kwa mara nyingi nilitembelea nyumba yao tukapiga gumzo na hata kushiriki vyakula kwa pamoja.

 Kwa vile Kim alikuwa akifanya kazi ya bawabu wa usiku ilikuwa ni fursa muhimu kwangu kupata upenyo hadi nyumbani mwake kupiga gumzo na mke wake kwa wakati wowote.

 Nilifanya mazoea ya kuingia kwenye nyumba ya Kim kila wakati alipokuwa katika shuguli za kazi usiku. Mke wake alikuwa mrembo ajabu mtoto wa kidigo aliyeumbwa akaumbika na hapo damu ilinichemka.

 Mara nyingi tulizungumza hadi usiku wa manane lakini hakuna kitu kama uhusiano kilinukia kwa ajili ya uoga flani. Baada ya wiki hivi mazungumzo yetu yalianza kubadilika kwani tulianza kuzungumzia mambo ya mapenzi.

 Dada yule alinielezea bayana kwamba hakufurahia kazi ya mume wake ya bawabu wa usiku kwani hali ile ilimwacha akisononeka na mwenye upweke. Alisema kuwa alitamani mume wake aiache kazi ile lakini hakuwa na budi kwa kuwa pato lao lilitoka kwenye kazi ile. 

Nilifahamu fika kwamba alikuwa akizungumzia suala zima la lungula na hapo nilijiambia akilini kuwa ni mimi pekee nilikuwa shujaa wa kumwondolea upweke wake wakati wa usiku. Mapenzi yetu na mke wa Kim yalinoga kwani hata tulianza kushiriki uroda. 

Nilirauka asubuhi na mapema kabla mume wake hajaingia ili kuepuka magombano au vita kwani nilikuwa nakula tunda la wenyewe. Nilifanya kitendo hiki kwa muda wa wiki tatu hivi.

 Kim hakugundua lolote wala hakuuliza mke wake chochote na hii ilinipa fursa ya kujiita kinara katika shughuli nzima hii ya kutafuna mke wake.

 Nilifahamu kwamba Kim asingegundua chochote. Baada ya siku majuma kadhaa mambo yalianza kuenda mrama. Usaha ulinitoka kwenye sehemu yangu ya siri huku ukiandamana na vijidudu vidogo mithili ya funza. Niligutushwa na mambo haya kwani hata sehemu zile zilikuwa kubwa ajabu hata kuvaa suruali ndefu ilikuwa ni mapigano kwa ajili ya uchungu.

 Nilijiambia moyoni kwamba Kim alikuwa ametembelea mahali ili kukinga mke wake kutokana na anasa. Hili lilikuwa ni kweli baada ya Joseph rafikiye Kim kuniambia kwamba Kim alikuwa amemfunga mke wake kushiriki mapenzi na mume mwingine na kwamba daktari aliyefanikisha suala hili lote alijiita Kiwanga.

 Niliposikia yale maneno machozi yalinitiririka kwa mpigo. Nilimwelezea Joseph anielekeze kwa daktari Kiwanga ili nirejeshe mambo kuwa kawaida. Nilipofika kwa ofisi za daktari Kiwanga alisema kuwa mtu aliyekuwa na uwezo wa kutatua shida yangu ni mume wa mke niliyeshiriki mapenzi naye na iwapo tu ningemuomba msamaha basi mambo yangu yangekuwa shwari. 

Nilifunga safari na kurejea kwangu na hapo siku iliyofuatia nilipiga moyo konde na kumtafuta Kim ili nimwombe msamaha. 

Alikubali kuzika mambo hayo kwenye kaburi la sahau na hali ikarejea shwari. Tangu siku ile mimi huona wake wa watu kama sumu. 

Daktari Kiwanga ana uwezo wa kutatua migogoro ya mashamba, kumaliza swala zima la wizi na mengineyo. Anatibu magonjwa kama vile kifua kikuu, kifaduro, msukumo wa damu na mengineyo kwa siku tatu tu. 

Kwa mengi zaidi wasiliana na Dkt. Kiwanga kutumia wavuti www.kiwangadoctors.com au kupitia barua pepe kiwangadoctors@gmail.com ama pia unaweza kupiga simu/WhatsApp kwa nambari +254769404965 kupata usaidizi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger