Thursday 30 September 2021

KIJANA AUAWA KWA VISU KISHA KUNING'INIZWA JUU YA MTI WA MPARACHICHI



Kijana Melkezedik Robert mwenye umri wa miaka 35, mkazi wa kijiji cha Nyerezi, Arumeru mkoani Arusha, amekutwa amekufa huku mwili wake ukiwa umening’inizwa juu ya mti ya mparachichi.

Mwenyekiti wa ulinzi wa wa Kitongoji cha Achi, aliyejitambulisha kwa jina moja la Agesmun, amesema walikuta mwili wa kijana huyo ukiwa umekatwakatwa visu katika maeneo mbalimbali mgongoni.

Alisema mara baada ya polisi kufika, waliwashikilia baba na mdogo wa marehemu ambaye inasadikika alikuwa na ugomvi na marehemu kaka yake.
Share:

Retention Officer (RO) at MDH

POSITIION: Retention Officer (RO) (8 Posts)   LOCATION:        Geita, Kagera, Tabora and Dar es Salaam REPORTS TO:    District Project Manager/ Regional Retention Manager Job Summary: The Retention Manager (RO) is responsible for the day to day implementation of MDH’s retention and continuity of care programs and services. She/he work with Council Health […]

This post Retention Officer (RO) at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Community ART Officer (CAO) at MDH

POSITION: Community ART Officer (CAO) (8 Posts)   LOCATION:        Kagera, Geita & Dar es Salaam REPORTS TO:    District Community Services Manager (DCSM) Job Summary:  The Community ART Officer (CAO) is responsible for the day-to-day field implementation of MDH’s community ART program and services. She/He will work with the Council Health Management Teams […]

This post Community ART Officer (CAO) at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

TAMISEMI: Call for Work at Benjamin Mkapa Foundation (BMF) Released Today 29th September, 2021 | Download All Names Here

Overview   The Benjamin William Mkapa Foundation (BMF) is a non- profit Trust, established in 2006 with the vision towards healthy lives and well-being for all, in Tanzania and the rest of Africa. Its strategic focused results areas include to combat HIV and AIDS, TB, Malaria and Reproductive, Maternal New Born, Child and Adolescent Health […]

This post TAMISEMI: Call for Work at Benjamin Mkapa Foundation (BMF) Released Today 29th September, 2021 | Download All Names Here has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

TB/HIV Officers at MDH

POSITION: TB/HIV Officers (6 Posts)   LOCATION:        Geita, Kagera & Tabora REPORTS TO:    TB/HIV Manager Job Summary:  The TB/HIV Officer works with and supports the MDH RTB-HIV Manager to ensure efficient implementation, M&E and reporting of TB/HIV services in her/his respective region including direct field coordination of key program priorities such as […]

This post TB/HIV Officers at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Maternal and Child Health (MCH) Officers at MDH

POSITION: Maternal and Child Health (MCH) Officers (7 Posts)   LOCATION:        Geita, Kagera, Tabora & Dar Es Salaam REPORTS TO:    Regional Maternal and Child Health (MCH) Manager Job Summary:  The Maternal and Child Health (MCH) officer works with and supports the MDH RMCH Manager to ensure efficient implementation, M&E and reporting of reproductive, maternal, […]

This post Maternal and Child Health (MCH) Officers at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Grants Manager at MDH

POSITION:   Grants Manager (1 Post)   LOCATION:   Dar es Salaam REPORTS TO:    Director of Grants and Compliance Job Summary:  Reporting to the Director of Grants and Compliance, the Grants Manager is responsible for overall oversight and coordination of donor engagement and proposal development. She/He will work with all other staff to develop and submit high […]

This post Grants Manager at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Wednesday 29 September 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 30, 2021
















Share:

SERIKALI YADHAMIRIA KUENDESHA SEKTA YA SANAA KIBIASHARA


Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kuendesha sekta ya Sanaa kibiashara na kuongeza tija ikiwa ni pamoja na kuwezesha sekta hii kutumika kama nyenzo ya kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu masuala ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe Septemba 29, 2021 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Sekta ya Sanaa 2021 ambao lengo lake ni kujadili kwa Pamoja masuala yanayohusu Sekta ya Sanaa kati ya Serikali na wadau ili kufikia lengo la kuifanya sekta hii kuendeshwa kibiashara ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni “Sanaa Biashara”

“Serikali imejipanga kuweka mazingira wezeshi ya kukuza Sanaa zetu ili kufikia viwango vya kimataifa na kuboresha mbinu na Mikakati ya Utekelezaji wa sera na Sheria za kuimalisha kazi za Sanaa nchini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Sanaa hususani wasanii” amaeeleza Mhe. Exaud Kigahe

Aidha, Mhe. Exaud Kigahe ameeleza kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara ni mdau mkubwa wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo kwani Sekta ya Sanaa ni kiwanda kinachozalisha bidhaa na huduma za sanaa ambazo zinahitaji mchango mkubwa wa Wizara ya Viwanda na Biashara katika kuweka sera, sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ya kusimamia uendeshaji wake na kuiendeleza kama inavyofanyika katika Sekta nyingine za kiuchumi hapa nchini.

Kwa upande wake, Dkt. Emmanuel Ishengoma Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaaa wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo ameeleza kuwa ili kuendesha Sanaa kibiashara, Serikali imeanzisha mfuko wa Utamaduni na Sanaa ambao utasaidia kuimarisha sekta hiyo kwa kudhamini mafunzo vilevile kutoa mkopo kwa mashariti nafuu ya kusaidia Sanaa na utamaduni na mpaka sasa Serikali imeshatoa billioni moja na milioni mia tano za kuwezesha mfuko huo.
Share:

WAZIRI MHAGAMA AKAGUA MIFUMO YA USALAMA NA AFYA MGODI WA SHANTA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge,Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb) akikagua maeneo ya mgodi mpya wa dhahabu wa Shanta uliopo Wilayani Ikungi Mkoani Sindiga alipofanya ziara ya kukagua usimikaji wa mifumo Usalama na Afya katika mgodi huo kabla ya kuanza rasmi shughuli za uchimbaji zinazotarajiwa kuanza mwakani. Alioambatana nao ni Meneja Mkuu wa Mgodi huo Mhandisi Jiten Divecha (Kushoto), Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtatulu (Kulia) pamoja na viongozi wa Wilaya ya Ikungi na baadhi ya wafanyakazi wa mgodi huo.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge,Kazi, Vijana,Ajira na wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb), akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Mgodi mpya wa Dhahabu wa Shanta Singida pamoja na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Ikungi, wakati wa ziara yake katika mgodi huo iliyolenga kukagua usimikaji wa mifumo Usalama na Afya katika mgodi huo kabla ya kuanza rasmi shughuli za uchimbaji dhahabu zinazotarajiwa kuanza mwakani. Wengine ni Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtatulu (Kulia) na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi Dijovison Ntangeki (Kushoto).


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana,Ajira na wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb), akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wanaojenga miundombinu mbalimbali katika Mgodi wa Dhahabu wa Shanta Singida alipotembelea maeneo mbalimbali ya mgodi huo yanayoandaliwa kwaajili ya uchimbaji wa dhahabu unaotarajiwa kuanza rasmi mwakani. Waziri Jenista aliambatana na viongozi mbalimbali wakiwemo Mkurugenzi wa Usalama na afya kutoka OSHA, Mhandisi Alexander Ngata (wakwanza kushoto kwa Mhe. Waziri), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi Dijovison Ntangeki (Mwenye koti la suti) pamoja na Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtatulu (wakwanza kulia) na Meneja Mkuu wa Mgodi huo Mhandisi Jiten Divecha (wapili kushoto).


Mkurugenzi wa Usalama na afya kutoka OSHA, Mhandisi Alexander Ngata, akitoa taarifa juu ya hali ya utekelezaji wa Sheria ya Afya na Usalama na Afya ya mwaka 2003 katika Mgodi wa Dhahabu wa Shanta Singida katika kikao baina ya Waziri pamoja na menejimenti na wafanyakazi mgodi huo wakati wa ziara ya Waziri iliyokuwa na lengo la kukagua usimikaji wa mifumo Usalama na Afya katika mgodi huo kabla ya kuanza rasmi shughuli za uchimbaji dhahabu.


Mkurugenzi wa Usalama na afya kutoka OSHA, Mhandisi Alexander Ngata (mwenye kofia ya bluu) na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, Venance Buliga (mwenye barakoa nyeupe), wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb), alipokuwa akizungumza na menejimenti pamoja na wafanyakazi wa Mgodi wa Dhahabu wa Shanta Singida alipofanya ziara katika mgodi huo

******************************

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, amefanya ziara katika Mgodi wa Dhahabu wa Shanta uliopo Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida kwa lengo kukagua usimikaji wa mifumo ya Usalama na Afya katika hatua za awali za maandalizi ya uchimbaji madini katika mgodi huo.

Waziri amesema ni muhimu kwa sehemu mbalimbali za kazi zinazoanzishwa hapa nchini ikiwemo migodi kuwahusisha wataalam wa Usalama na Afya katika hatua za awali za ujenzi wa miundombinu ili waweze kupata ushauri utakaowawezesha kujenga miundombinu inayozingatia viwango vya Usalama na Afya mahali pa kazi na hivyo kuepuka kuweka miundombinu ambayo ipo kinyume na Sheria na kanuni za usalama na afya mahali pa kazi.

“Kwetu sisi na wenzangu wa OSHA tutakachojitahidi ni kuendelea kuwapa elimu ya kutosha kuhusu masuala ya usalama na afya mahali pa kazi ili mbobee kwenye eneo hilo kusudi muondoshe migogoro katika eneo lenu la kazi na ndio maana ninaomba muwaruhusu hapa wawe na tawi la wafanyakazi. Lakini tutawasadia pia kukagua na kuangalia mifumo yenu ya usalama na afya kama itaweza kulinda afya za wafanyakazi hususan pale mtakapoanza rasmi uzalishaji kwani tunatambua kwamba shughuli hizi za uchimbaji madini huambatana na vihatarishi vingi vya usalama na afya ambavyo vinahitaji mifumo madhubuti ya kukabiliana navyo,” amesema Jenista Mhagama.

Akiwa ameambatana na Waziri Mhagama katika ziara hiyo, Mkurugenzi wa Usalama na Afya wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Mhandisi Alexander Ngata, ametoa wito kwa makampuni makubwa ambayo yanafanya kazi na makampuni saidizi (sub-contractors) kuhakikisha kwamba makampuni hayo yanazingatia Sheria na kanuni za usalama na afya mahali pa kazi.

Awali akiwasilisha taarifa yake kuhusu hali ya usalama na afya katika mgodi huo mbele ya Waziri, Mkurugenzi wa Usalama wa OSHA, Mhandisi Ngata alieleza kwamba kampuni hiyo imekuwa ikijitahidi kutekeleza matakwa yote ya Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi kama ambavyo wamekuwa wakielekezwa na wataalam kutoka OSHA. Aidha, alibainisha kwamba changamoto iliyopo ni kwa makampuni saidizi (sub-contractors) yanayofanya kazi na Shanta ambayo bado hayazingatii utekelezaji wa Sheria tajwa.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati inayojumuisha mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora na Kigoma, Venance Buliga, amesema wamekuwa wakishirikiana ipasavyo na uongozi wa mgodi huo katika hatua mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya uchimbaji madini katika mgodi huo ambapo wamekuwa wakifanya ukaguzi na kutoa ushauri wa kitaalam kuhusu namna bora ya kujenga miundombinu inayozingatia afya na usalama wa wafanyakazi.

Aidha, menejimenti ya mgodi huo pamoja na wafanyakazi wameeleza kuwa usalama na afya kwa wafanyakazi ni miongoni mwa vipaumbele vya kampuni hiyo.

“Tunafanya kazi kwa kuzingatia misingi mitatu ambayo ni biashara, mahusiano na jamii inayotuzunguka pamoja na afya na usalama wa watu wetu kama kama tulivyoeleza katika taarifa yetu kwa Mheshimiwa Waziri na yeye pamoja na wataalam wa OSHA wamethibitisha hilo walipotembelea sehemu mbalimbali katika mgodi,” amesema Mhandisi Jiten Divecha, Meneja Mkuu wa Mgodi wa Shanta wa Ikungi Mkoani Singida.

“Kwa masuala ya usalama na afya hapa Shanta tuko vizuri sana, kila sehemu ambayo watu wanafanya kazi masuala ya matumizi sahihi ya vifaa kinga yanazingatiwa ipasavyo na pia wakaguzi wa OSHA huwa wanatutembelea kuangalia namna tunavyofanya kazi na kutushauri kuboresha endapo tunakuwa kinyume na taratibu za usalama na afya mahali pa kazi,” amesema Ferdinand Cyprian, Mfanyakazi wa Mgodi wa Shanta-Ikungi katika kitengo cha upakaji rangi majengo.

Taasisi ya OSHA ambayo ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) ina dhamana ya kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 pamoja na kanuni zake ambayo pamoja na mambo mengine inawataka wamiliki wa sehemu za kazi nchini kusajili maeneo yao na OSHA, kufanyiwa ukaguzi wa usalama na afya, kuchunguza afya za wafanyakazi pamoja na kuwapa mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi.
Share:

DKT. NDUMBARO AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUUTUMIKIA UMMA KWA UZALENDO, UADILIFU NA WELEDI


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akifungua kikao kazi cha ofisi yake na Taasisi zinazosimamia Maadili na vyama vya kitaaluma chenye lengo la kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa maadili, kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.


Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Taasisi zinazosimamia Maadili na vyama vya kitaaluma chenye lengo la kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa maadili wakimsikiliza Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) wakati akifungua kikao kazi hicho kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Leila Mavika (wa kwanza kushoto) akitoa neno la utangulizi wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha ofisi yake na Taasisi zinazosimamia Maadili na vyama vya kitaaluma chenye lengo la kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa maadili, kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.


Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Taasisi zinazosimamia Maadili na vyama vya kitaaluma chenye lengo la kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa maadili, wakifuatilia moja ya mada iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Leila Mavika katika kikao kazi hicho kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.


Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kikao kazi cha Taasisi zinazosimamia Maadili na vyama vya kitaaluma chenye lengo la kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa maadili mara baada ya kukufungua kikao kazi hicho, kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI Mtumba jijini Dodoma.

*********************************

Na Veronica Mwafisi-DODOMA

Tarehe 29, Septemba, 2021



Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro amewataka Watumishi wa Umma nchini kuutumikia umma kwa uzalendo, uadilifu na weledi ili kutimiza azma ya Serikali ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Dkt. Ndumbaro ametoa wito huo wakati akifungua kikao kazi cha siku mbili cha taasisi simamizi za maadili na vyama vya kitaaluma chenye lengo la kubadilishana uzoefu wa usimamizi wa maadili, kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya RaiS-UTUMISHI Mtumba, jijini Dodoma.

Dkt. Ndumbaro amesema uzalendo, uadilifu na utendaji kazi unaozingatia weledi ndio nguzo kuu ya utendaji kazi wa Watumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na ustawi wa taifa.

Ameongeza kuwa, ofisi yake imekuwa na utamaduni endelevu wa kushirikiana na taasisi zinazosimamia maadili na vyama vya kitaaluma ili kujenga taifa imara lenye Watumishi wa Umma wazalendo na waadilifu.

“Ushirikiano uliopo kati ya ofisi yangu na taasisi simamizi za maadili na vyama vya kitaaluma, utasaidia kujenga uadilifu kwenye utumishi wa umma na jamii kwa ujumla”, Dkt. Ndumbaro amefafanua.

Dkt. Ndumbaro amesema, Watumishi wa Umma nchini wanao wajibu wa kuunga mkono kwa vitendo azma ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya kuujenga Utumishi wa Umma kuwa wenye kuzingatia uadilifu, uwajibikaji, Kanuni, Sheria, Taratibu na miongozo iliyopo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bi. Leila Mavika amesema lengo kuu la kikao kazi hicho ni kukumbushana uzingatiaji wa maadili, kujadili changamoto za usimamizi wa maadili katika Utumishi wa Umma na kuzitafutia ufumbuzi.

Mwanasheria wa Bodi ya Wataalamu ya Ununuzi na Ugavi, Bw. Suleiman Mzava ambaye ni mmoja wa washiriki wa kikao kazi hicho amesema, kikao kazi hicho kitasaidia kujenga uadilifu miongoni mwa taasisi za umma hivyo ameipongeza Serikali kwa kuweka nguvu kubwa katika usimamizi wa maadili.

Watumishiwa Umma wa wakizingatia uzalendo, uadilifu na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, watatoa huduma bora kwa wananchi na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa.
Share:

NYUKI WAVAMIA GHAFLA MSIBANI...WAUA MZEE WA KIJIJI WAKATI WA MAZISHI

Kundi la nyuki walivuruga hafla moja ya mazishi eneo la Gatundu Kaskazini, kaunti ya Kiambu nchini Kenya na kuua mmoja wa waombolezaji.

Katika kisa hicho kisichokuwa cha kawaida, kilichotokea siku ya Jumamosi, Septemba 25, 2021 marehemu Mungai Mburu ambaye ni mzee wa kijiji, alikuwa amehudhuria hafla ya mazishi ya mjukuu wake wakati nyuki hao wenye hamaki walimvamia.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mke wake marehemu, Wanjiku Mburu, baada ya maombi kufanywa kwenye kaburi, nyuki waliwavamia huku kila mmoja akichana mbuga kuokoa maisha yake.

Wanjiku alielezea kuwa ni katika taharuki hiyo ndipo mume wake aliyekuwa na umri wa miaka 85, alianguka chini baada ya kusukumwa na umati wa watu na kukumbana na mauti yake mikononi mwa nyuki hao.

Juhudi za wasamaria wema kujaribu kuokoa maisha yake hakizikufua dafu kwani alithibitika kufariki alipofikishwa katika Hospitali ya Igegania.

Chanzo - Tuko News
Share:

MREMBO AMKIMBIA MUME MTARAJIWA SIKU YA HARUSI


Jackline Wanjiru kutoka Kenya aliamua kuchanja mbuga muda mfupi kabla ya harusi yake baada ya kugundua kuwa bwana harusi Alfred Musa alimdanganya kuwa ni mfanyakazi wa benki kumbe sio ni dereva Teksi.

Katika mahusiano yao yaliyodumu kwa miaka minne, Alfred alimwambia Jackline kuwa yeye ni mfanyakazi wa benki ya biashara katika tawi la Malindi ila baada ya kugundua kuwa mumewe anafanya kazi kama dereva wa Teksi na sio Benki aliamua kukimbia katikati ya shughuli.
Share:

Resilience and livelihoods Team Lead at World Vision

JOB PURPOSE   To provide technical leadership and coordination of all resilience, livelihoods and economic development interventions for WV Tanzania to ensure the realization of World Vision Tanzania’s Country Strategy. The incumbent staff will lead the development of all related technical approaches for the NO. S/he will actively pursue resource mobilization strategies for the sector, […]

This post Resilience and livelihoods Team Lead at World Vision has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Request for Proposal – Senegal and Tanzania at Palladium

Request for Proposal – Senegal and Tanzania   Company Overview: About Palladium – Palladium is a global leader in the design, development and delivery of Positive Impact – the intentional creation of enduring social and economic value. We work with governments, businesses, and investors to solve the world’s most pressing challenges. With a team of more than […]

This post Request for Proposal – Senegal and Tanzania at Palladium has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Video : NYANDA MADIRISHA OBHADO 'MALIGANYA' - STAREHE

Nakualika kutazama Video ya wimbo mpya wa Nyanda Madirisha Obhado ' Maliganya' (Shikomba Bhulolo) kutoka Kahama Mkoani Shinyanga inaitwa Starehe...Ngoma hii imetengenezwa katika Studio za Hardtone.
Tazama video hapa chini
Share:

BONDIA MAARUFU MANNY PACQUIANO ATANGAZA KUSTAAFU MASUMBWI




Manny Pacquiao

Bondia maarufu Manny Pacquiao ametangaza kustaafu mchezo huo baada ya kuutumikia kwa miaka 26.

Pacquiao ambaye ndiye bondia pekee kutwaa ubingwa wa Dunia mara 8 katika uzani tofauti tofauti, anastaafu akiwa na umri wa miaka 42, akiwa amepigana mara 72, ameshinda mara 62, kapoteza mara 8 na sare mara 2.

Tamko lake kupitia mitandao ya kijamii linakuja ikiwa ni siku chache baada ya kupoteza pambano dhidi ya Yordenis Ugas

Wiki kadhaa zilizopita, Pacquiao alitanganza kuwa yupo tayari kugombea nafasi ya Urais katika Uchanguzi Mkuu wa nchini Ufilipino utakaofanyika mwakani na itajwa kuwa pia ni sababu kubwa iliyopelekea astaafu kucheza masumbwi.

''Kwenu mashabiki wakubwa na mchezo mkubwa ulimwenguni, asante! Asante kwa kumbukumbu zote nzuri. Huu ni uamuzi mgumu zaidi ambao nimewahi kufanya, lakini nina amani nao. Kimbilia ndoto zako, fanya kazi kwa bidii, na uangalie kinachotokea. Kwaheri ndondi.''ameandika Manny Pacquiao.

Via EATV

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger