Tuesday 28 September 2021

Wakuu Wa Mikoa Wana Jukumu Kubwa Mradi Bomba La Mafuta Ghafi La Afrika Mashariki ( Eacop) -Waziri Makamba


Na Dorina G. Makaya na Janeth Mesomapya – Tanga.

Waziri wa Nishati, Mh. January Yusuf Makamba ameeleza kuwa Wakuu wa Mikoa minane (8) ambapo utapita mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) wanajukumu kubwa katika kufanikisha utekelezaji wa mradi huo kwa kuimarisha ulinzi na usalama pamoja na kuhakikisha fursa zitakazopatikana zinanufaisha wananchi wa mikoa yao husika.

Waziri Makamba ameyasema hayo , Septemba 27, 2021 wakati wa semina kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa minane itakayopitiwa na mradi huo, inayofanyika jijini Tanga.

“Moja ya sababu za bomba hili kupita nchini kwetu ni uhakika wa ulinzi na usalama uliopo. Usalama huo utaendelea kuwepo kama wanaosimamia usalama huo kwenye maeneo linapopita bomba wana uelewa kuhusu mradi na kile kinachohitajika kufanywa ili walioamua bomba hili lipitie kwetu wawe na imani kwamba walifanya uamuzi sahihi”, alisema Waziri Makamba.

Ameongeza kuwa semina hiyo inalenga kutengeneza uelewa mpana kwa viongozi hao kuhusu mradi na kujadili fursa mbalimbali zitakazopatikana kwenye utekelezaji wake.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Wakili Stephen Byabato ametoa rai kwa viongozi hao kuhakikisha wanatengeneza mazingira mazuri ili fursa zitakazotokana na utekelezaji wa mradi huo zinufaishe wananchi wa mikoa husika.

Mh. Byabato amesema kuwa Bomba hilo litapita katika mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga,Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga.

Ameeleza kuwa Mkataba Hodhi wa Mradi (HGA) baina ya Serikali na Kampuni ya Bomba umeainisha baadhi ya bidhaa na huduma zitakazotolewe na Watanzania pekee (Reserved Contracts).

Naibu Waziri Byabato ameongeza kuwa, bidhaa na huduma hizo ni pamoja na usafirishaji, ulinzi, chakula na vinywaji, huduma ya malazi, mafuta kwa ajili ya magari na mitambo, shajala, bidhaa za ujenzi zinazopatikana hapa nchini, shughuli za ujenzi (civil works), huduma za mawasiliano, na ukodishaji wa mitambo ya ujenzi.

Bidhaa na huduma nyingine za manunuzi tofauti na zile zilizotengwa kwa Watanzania tu zitapatikana kwa njia ya ushindani na Watanzania wenye uwezo, vigezo na sifa stahiki wataweza kushiriki.

Ameongeza kuwa bidhaa na huduma nyingine za manunuzi tofauti na zile zilizotengwa kwa Watanzania tu zitapatikana kwa njia ya ushindani na Watanzania wenye uwezo, vigezo na sifa stahiki wataweza kushiriki.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) Dkt. James Mataragio ameeleza kuwa serikali kupitia shirika hilo inamiliki hisa asilimia 15% ya utekelezwaji wa mradi huo, huku asilimia 62% ikishikiliwa na kampuni ya Total Energies, asilimia 15% ya UNOC ya Uganda huku CNOOC ikishikilia asilimia 8%.

“Majukumu ya TPDC kwenye mradi huu ni pamoja na kuwa mbia kwenye mradi wenyewe, kushughulikia masuala ya ardhi, kusimamia mikataba yote ya EACOP, kuwa na uwakilishi wa asilimia 15% kwenye uongozi na kuwa na mjumbe kwenye Bodi ya Wakurugenzi ya EACOP pamoja na kuratibu ushirikishwaji wa wadau mbalimbali watakaofanikisha utekelezaji wa mradi huu”, aliongeza.

Semina hiyo iliyowakutanidha wakuu wa mikoa minane jijini Tanga pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali, Bunge, Wizara ya Nishati na Taasisi zake itafanyika kwa siku tatu hadi tarehe 29 Septemba, 2021.



Share:

Kesi ya Mbowe: Mshtakiwa adai hakupewa chakula kwa siku 10


Shahidi wa pili upande wa utetezi katika kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake, Mohamed Ling’wenya amedai hakula chakula siku kumi akiwa katika kituo cha polisi Mbweni.

Shahidi huyo amedai alifikishwa kituo cha polisi Mbweni Agosti 9, 2020 hadi Agosti 19, 2020 alipofikishwa mahakama ya Kisutu ndipo alikula ugali na dagaa.

Ling’wenya ametoa madai yake leo Jumanne Septemba 28, 2021 katika mahakama kuu divisheni ya makosa ya rushwa na uhujumu uchumi wakati akitoa ushahidi wake katika kesi hiyo ndogo.



Share:

Secretariat for the DPG PSDT at UNDP

Background   The development partner group for private sector development and trade (DPG PSDT) was formally established in 2007, in order to build a coordinated development partner response to the Government’s Joint Assistance Strategy for Tanzania (JAST), within the overarching framework of the MKUKUTA. It continues to exist, to support the government with the realization […]

This post Secretariat for the DPG PSDT at UNDP has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Investment Officer at UNCDF/UNDP

Background   The UN Capital Development Fund makes public and private finance work for the poor in the world’s 46 least developed countries (LDCs). UNCDF offers “last mile” finance models that unlock public and private resources, especially at the domestic level, to reduce poverty and support local economic development. UNCDF’s financing models work through three […]

This post Investment Officer at UNCDF/UNDP has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

59 Job Opportunities at TANGANYIKA District Council

59 Contract Jobs Opportunities at TANGANYIKA District Council September, 2021. Katavi Region is one of Tanzania’s 31 administrative regions with a postcode number 50000. The regional capital is Mpanda. In March 2012, shortly after the Katavi Region was created, Dr. Rajab Mtumwa Rutengwe was appointed Katavi Regional Commissioner. He was formerly the Mpanda District Commissioner. […]

This post 59 Job Opportunities at TANGANYIKA District Council has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

DRIVERS at KINONDONI Municipal Council

Kinondoni District is a district in north west of Dar es Salaam’s central business district, Tanzania, others being Temeke (to the far Southeast) and Ilala (downtown Dar es Salaam). To the east is the Indian Ocean, to the north and west the Pwani Region of Tanzania. The area of Kinondoni is 537 km2 (207 sq […]

This post DRIVERS at KINONDONI Municipal Council has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Nurses at Ifakara Health Institute (IHI)

Nurses   Work station: Help Project, Bagamoyo Ifakara Health Institute Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa, with strong track records in developing, testing and validating innovations for health. We are driven by core strategic mandate for research, training and services. The institute’s work spans across a wide spectrum of sciences […]

This post Nurses at Ifakara Health Institute (IHI) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Maintenance Planner at Tanga Cement PLC

Tanga Cement PLC believes that for employees to play their full role in the achievement of the Company’s business objectives, there should exist an on going comprehensive and effective training and development process at all levels. The company therefore invests in personal and professional development from the start of an individual’s career. The periodic People […]

This post Maintenance Planner at Tanga Cement PLC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MAFUNZO YA CHANJO KWA KAMATI ZA AFYA YA MSINGI WILAYA YA MKALAMA YAZAA MATUNDA


Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI) Idara ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe, Dinah Atinda akizungumza jana wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Wajumbe wa Kamati ya Msingi ya Afya Wilaya ya Mkalama mkoani Singida yenye mpango harakishi wa kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu chanjo ya Uviko 19 na kuchanja.

Richard Magodi kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara ya Mpango wa Taifa wa Chanjo akishiriki kutoa mafunzo hayo.
Mkuu wa wilaya hiyo Sophia Kizigo (katikati) akishiriki mafunzo hayo.
Mafunzo hayo yakiendelea. Nyuma mwenye miwani ni Mchungaji Sefine Kanga wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Usharika wa Dumanga.
Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI) Idara ya Afya Ustawi wa Jamii na Lishe, Dinah Atinda na Afisa Msanifu Patrice Makhao kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakifuatilia mafunzo hayo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Afya Wilaya ya Mkalama, Sippi Shabani akichangia jambo kwenye mafunzo hayo.
 Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama     Bosco Charles akizungumza kwenye mafunzo hayo.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Ibrahim Pazia, akipata chanjo hiyo.

     Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Mkalama Hamisi Ramadhani akizungumza kwenye mafunzoh hayo.

Mafunzo hayo yakiendelea.
Mafunzo hayo yakiendelea
Mafunzo hayo yakiendelea.
Mafunzo hayo yakiendelea.
Watoa Huduma wa Afya wilayani Mkalama wakisubiri kupata chanjo.


Na Dotto Mwaibale, Mkalama


MAFUNZO yaliyotolewa kwa Watoa Huduma wa Afya wilayani Mkalama mkoani Singida kwa ajili ya kutoa elimu  dhidi ya Uviko 19 kwa wananchi juu ya kujikinga na ugonjwa huo na kupokea chanjo yamezaa matunda baada ya baadhi ya wahudumu hao kuelewa na kuchoma chanjo hiyo hivyo kuwa mabalozi wa kwenda kutoa elimu hiyo kwa wananchi.

Mafunzo hayo yalitolewa jana wilayani hapa kutoka kwa timu ya uhamasishaji wa chanjo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Maofisa kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI)

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo ya chanjo kwa Wajumbe wa Kamati ya Afya ya Msingi Mkuu wa wilaya hiyo Sophia Kizigo alisema changamoto ya wananchi kutojitokeza kwa wingi kwenda kupata chanjo hiyo kwa idadi ya watu 10 inaweza kuwa ni moja ya sababu iliyosababisha wilaya hiyo na zingine hapa nchini kuwa na idadi ndogo ya watu walioitikia mwito wa kupata chanjo.

" Utaratibu wa kutoa chanjo hiyo ilikuwa wapatikane watu 10 ili dawa itakayotumika isiweze kuharibika hivyo watoa huduma walikuwa wakisubiri ifike idadi hiyo ndipo watoe chanjo,". alisema Kizigo.

Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (TAMISEMI) Idara ya Jamii  na Lishe, Dinah Atinda alisema uelewa na uhamasishaji mdogo kwa wananchi kuhusu umuhimu wa chanjo hiyo iliyozinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan umechangia kwa kiasi kikubwa watu kutojitokeza kwa wingi kwenda kuchanjwa.

" Serikali imetumia fedha nyingi kuagiza chanjo lakini wananchi bado hawaja kwenda kuchanjwa hivyo imetengeneza mpango mkakati harakishi wa kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu chanjo ya Uviko 19 na kuchanja" alisema Atinda.

Alisema hatua iliyofikiwa na Serikali ni kuanza kutoa mafunzo kuanzia ngazi ya Taifa hadi kuwafikia walipo wananchi.

Richard Magodi kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Mpango wa Taifa wa Chanjo alisema baada ya kutokea vifo vingi maeneo mbalimbali duniani kutokana na ugonjwa huo sasa hivi vifo hivyo vimeanza kupungua kutokana na kutumia chanjo.

" Na sisi kama nchi na pia Taifa ambalo lipo miongoni mwa mataifa mengine lilikuwa ni jukumu letu kuishauri Serikali na kuanzisha mpango huu wa chanjo," alisema Magodi.

Magodi alisema chanjo hiyo ni salama na haina madhara yoyote baada ya kuhakikiwa na wataalamu na tayari imetolewa nchi mbalimbali duniani.

Wakizungumza baada ya kupata mafunzo hayo Mchungaji Setina Kanga wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Usharika wa Dumanga alisema sasa anakwenda kuwaeleza waumini wake umuhimu wa kupata chanjo hiyo.

Kaimu Sheikh wa Wilaya ya Mkalama Hamisi Ramadhani alisema awali alikuwa alielewi zoezi hilo la chanjo kutokana na kuwa na maneno mengi ya kukanganya lakini sasa anakwenda kutoa elimu hiyo kwa wananchi.

Makamu  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bosco Charles aliwataka washiriki wote waliopata mafunzo hayo kwenda kuhamasisha wananchi katika maeneo yao ili wapate chanjo hiyo.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo waliopata chanjo hiyo ni Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Ibrahim Pazia, Afisa Elimu Taaluma Sekondari, Ernest Stephen, Kalisti Faustin ambaye ni Muuguzi, Nyandewa Zabron, Afisa Muuguzi Salum Mputa, Farida  Seleman, Aizack Zabron.

Share:

Data Officer at Youth Wings

Vacancy Title – Data Officer – Post (01)   Organization: Youth Wings (YW) – Tanzania. Duty Station: Meru DC – Arusha, Tanzania.  Reports to: Data Manager. Start Date: October 2021. Background  Youth Wings (YW) is a Youth-Led CSO based in Arusha whose purpose is to respond to the rights and needs  of young generations caught up in […]

This post Data Officer at Youth Wings has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Case Manager at Youth Wings

Vacancy Title – Case Manager – Post (01)   Organization: Youth Wings (YW) – Tanzania. Duty Station: Meru DC – Arusha, Tanzania.  Reports to: Programme Manager. Start Date: October 2021. Background  Youth Wings (YW) is a Youth-Led CSO based in Arusha whose purpose is to respond to the rights and needs  of young generations caught up in […]

This post Case Manager at Youth Wings has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Data Manager at Youth Wings

Vacancy Title – Data Manager – Post (01)   Organization: Youth Wings (YW) – Tanzania. Duty Station: Meru DC – Arusha, Tanzania.  Reports to: Programme Manager. Start Date: October 2021. Background  Youth Wings (YW) is a Youth-Led CSO based in Arusha whose purpose is to respond to the rights and needs  of young generations caught up in […]

This post Data Manager at Youth Wings has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Community Engagement Officers at Youth Wings

Vacancy Title – Community Engagement Officers – Post (02) Organization: Youth Wings (YW) – Tanzania. Duty Station: Meru DC – Arusha, Tanzania.  Reports to: Programme Manager. Start Date: October 2021. Background  Youth Wings (YW) is a Youth-Led CSO based in Arusha whose purpose is to respond to the rights and needs  of young generations caught up in […]

This post Community Engagement Officers at Youth Wings has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Biomedical Programme Officer at Youth Wings

Vacancy Title – Biomedical Programme Officer – Post (01)   Organization: Youth Wings (YW) – Tanzania. Duty Station: Meru DC – Arusha, Tanzania.  Reports to: Programme Manager. Start Date: October 2021. Background  Youth Wings (YW) is a Youth-Led CSO based in Arusha whose purpose is to respond to the rights and needs  of young generations caught up […]

This post Biomedical Programme Officer at Youth Wings has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 28,2021











Share:

SERIKALI YAOMBWA KUBORESHA MAZINGIRA YA UTOAJI TAARIFA KWA WANANCHI


Na Magrethy Katengu_Dar es salaam

Ikiwa imesalia siku moja kuelekea siku ya maadhimisho ya kupata taarifa, Umoja wa asasi zinazotetea haki ya kupata taarifa (CoRI) umeziomba  taasisi zote za kiserikali na zisizo za kiserikali kuzingatia kifungu cha sheria yakikatiba ubara ya  18 ya haki ya kupata taarifa kama ilivyotungwa na bunge miaka  iliyopita.

wito huo umetolewa leo na CORI, ikiwa ni siku moja kabla ya maadhimisho ya kimaifa ya siku ya haki ya kupata taarifa ambayo ni Septemba 28 kila mwaka ambapo kwa mwaka huu kitaifa itaadhimishwa Dar es salaam katika ukumbi wa kimataifa Mwalimu Kambarage Nyerere

Akizungumza na wanahabari Mwenyekiti wa Umoja wa asasi zinazotetea haki ya kupata taarifa (CoRI) Kajubi Mukajanga wakati akitoa tamko la pamoja kuelekea siku hiyo amesema ni nusu muongo sasa tangu kupitishwa na bunge sheria ya haki kupata taarifa lakini utekelezaji wake ni hafifu kumekuwa matukio ya Waandishi wa habari wawapo katika majukumu yao mtoa habari kuhitaji aandikwe anavyotaka yeye.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jukwaa la Tahariri Tanzania (TEF) Deodatus Balile amesema kila mtu anayo haki ya kutafuta,kupatiwa na kusambaza taarifa,katiba pia ina tamko la kimataifa la haki za binadamu kama sehemu ya maudhui yake likitamka uhuru wa maoni,kujieleza na kujumuika

"Tunataka kuteuliwa kwa maofisa watoa taarifa katika kila taasisi ya Umma wenye mamlaka na wajibu wa utoaji taarifa za mara kwa mara na zile zinazoombwa na mwananchi mmoja mmoja kama inavyotamkwa na kifungu cha 7cha sheria",alisema  Balile.

Hata hivyo amesema kuna umuhimu wa kuanzishwa mfumo wa ufuatiliaji kubaini maombi yote ya taarifa na majibu yake katika taasisi za Umma ili kuepusha malalamiko baadhi ya waandishi kuwa barua za maombi wanapohitaji taarifa kutojibiwa au kukaa muda mrefu bila majibu

Meneja utetezi kutoka twaweza Anna Rugamba amesema CoRI inaamini kuwa ipo haja ya marekebisho ya sheria ya huduma za vyombo vya habari ys mwaka 2016,kuongeza kasi ya Utekelezaji wa sheri haki ya kupata taarifa pamoja na maboresho na utekelezaji wa kanuni za sheria hizo.
Share:

SHIRIKA LA C4C LATAMBULISHA MABALOZI NA WADAU KUSHUGHULIKIA MASUALA YA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO


Na  Mapuli Misalaba, Shinyanga
Shirika la Citizens 4 Change (C4C) Jamii kwa ajili ya Mabadiliko limewatambulisha mabalozi na wadau mbalimbali zaidi ya 70  watakaoshughulikia masuala ya ukatili kwa wanawake na watoto  katika Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
 
Kikao hicho kimejumuisha  viongozi wa serikali pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya ulinzi na usalama kwa watoto pamoja na wanawake  ili kuwatambulisha na kuwapa maelekezo ya hatua ambayo wanapaswa kuanza nayo katika kukomesha ukatili kwa watoto na wanawake 

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mipango na Utaratibu Mkoa wa Shinyanga, Mkuu wa Idara ya  maendeleo ya jamii Mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale amewaomba wadau hao kushirikiana na serikali katika kukomesha ukatili kwa wanawake na watoto kwa kupata matokeo ya kumaliza ukatili unaofanyika hasa katika wilaya ya Shinyanga mjini.

“Ninyi sasa ni viongozi tunaomba mtatusaidia sana iwe ni Halmashauri ya mfano kwa masuala ya ukatili kwa watoto na wanawake kuyamaliza ili viongozi wengine waje kujifunza kutoka kwenu nawaomba mshirikiane na serikali katika kufanya kazi”,alisema

Kwa upande wake Dkt. Kate Mcalpine ambaye ni Kiongozi na Mtaalamu wa utafiti wa ukatili kwa wanawake na watoto Shirika la Citizens 4 Change (Raia kwa ajili ya mabadiliko) amesema lengo la Shirika hilo kufika Mkoa wa Shinyanga ni kumaliza ukatili na kuonesha njia nzuri ya kulinda usalama wa watoto na wanawake.

“Nia yetu ni kuonesha kwamba watu wa Shinyanga waseme sasa ukatili basi lakini tunataka tuoneshe njia ya nzuri ya kulinda usalama kwa watoto na wanawake njia hii ipo moyoni mwetu “amesema Dkt. Kate 

Dkt. Kate amesema Shirika la Citizens for Change lipo nchi ya Tanzania na Uganga ambapo linafanya kazi kwa kutumia njia ya ujumbe kuwasiliana na watu ambao wanania ya kulinda usalama wa watoto na wanawake ili kutatua ukatili kwenye jamii 

Amewaomba wananchi wote kujisajili  na shirika la Citizens 4 Change (C4C) kwa kutumia simu ya mkononi kwa kupiga *149*46*11#  ambapo amesema huduma hii ni bure kabisa ili kuwa raia anayewalinda watoto na wanawake dhidi ukatili.

Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Deus Muhoja amesema baadhi ya maeneo ukatili umepungua ambapo amesema changamoto kubwa ni mimba za utotoni pamoja na ndoa za utotoni   amewataka wananchi kuacha matendo ya ukatili .

“Kwa hali ya ukatili katika Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa sasa ukatili umepungua na ukatili mkubwa ambao upo kwa sasa hivi ni mimba za utotoni pamoja na ndoa za utotoni nitoe wito kwa wananchi tuache matendo ya ukatili kwa sababu ukatili hauna faida na wale ambapo wanaendelea kufanya majirani watoe taarifa mapema sehemu husika ili kuwashughulikia hao watu”,amesema

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger