Tuesday 29 June 2021
RAIS SAMIA AZUNGUMZA NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA
UHAMASISHAJI WANANCHI KWENYE MIRADI YA UPANUZI IIA( DENSIFICATION IIA) YAENDELEA MKOANI TABORA
Monday 28 June 2021
Tanzania Kunufaika Soko Eneo Huru La Biashara Afrika
Na Mwandishi wetu, Dar
Serikali ya Tanzania inategemea kunufaika na soko la bidhaa zake katika masoko ya nje baada ya kusainiwa kwa Mkataba wa ushiriki katika Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA).
Akiongea na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCTA) Mhe. Wamkele Mene, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amesema kwa sasa Serikali ipo katika hatua za mwisho kusaini Mkataba wa AfCTA.
“Lengo la ziara ya Mhe. Mene hapa nchini pamoja na mambo mengine ni kukutana na viongozi na wadau wengine muhimu kujadiliana na masuala mbalimbali yanayohusu Mkataba wa AfCTA ikiwa ni pamoja na umuhimu wa Tanzania kuridhia Mkataba huo,” Amesema Balozi Mulamula
Balozi Mulamula ameongeza kuwa, uanzishwaji wa AfCTA ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa ambapo pamoja na mambo mengine, utekelezaji wake unatarajiwa kuongeza wigo wa fursa nafuu za biashara nchini kwa kuwavutia wawekezaji na kuongeza mauzo hasa ya bidhaa za kilimo.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Sekretariati ya Eneuo Huru la Biashara Afrika (AfCTA) Mhe. Wamkele Mene ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano ambao imempatia tangu wakati wa uchaguzi hadi sasa na kuahidi kuwa utekelezaji wa Mkataba huo utanufaisha kila Nchi Mwanachama.
“……….Naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwani tangu ilipoingia Madarakani imetumia muda mfupi katika kushiriki kwa ukamilifu katika majadiliano ya kusaini mkataba huu na Tanzania imeshiriki vizuri sana kwenye majadiliano haya muhimu,” Amesema Mhe. Wene
Ameongeza kuwa kwa sasa Eneo Huru la Biashara Afrika lina Nchi wanachama 38 ambazo zimekubaliana na Mkataba huo na kwamba kwa sasa Sekretariati hiyo inaendelea kuimarika katika kukuza biashara na sekta binafsi katika nchi wanachama wa AfCTA.
Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Afrika umesainiwa na Nchi 54 kati ya nchi 55 za Umoja wa Afrika ikiwemo Tanzania. mkataba huo ulipata nguvu ya Kisheria Julai, 2019 baada ya nchi 28 kuridhia Mkataba huo. Mkataba wa AfCTA unahusisha maeneno ya ushirikiano katika bishara ya bidhaa, biashara ya huduma, uwekezaji, hakimiliki na ubunifu pamoja na Sera za ushindani.
Katika tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameshiriki uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia ambapo pamoja na mambo mengine, Balozi Mulamula kongamano hili litakuwa mahsusi kuangalia masuala ya uswa wa jinsia kwa kizazi hiki na kizazi kijacho na kwamba wakuu wa Nchi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa watakuatana Ufaransa katika kongamano hilo kuanzia tarehe 30 Juni hadi 2 Julai 2021.
Balozi Mulamula ameongeza kuwa, Tanzania itashiriki katika kongamano hilo ambapo Rais wa Jamhuri ya Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan atawakilishwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango
Uzinduzi wa Kongamano la Usawa wa Kijinsia uliofanyika leo jijini Dar es Salaam umehudhuriwa na Balozi wa Ufaransa nchini Mhe. Fredric Clavie pamoja na Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Bibi Hodan Addou.
IGP Sirro Atoa Maagizo Kwa Wadau Wa Usafirishaji
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewataka wadau wa usafirishaji kuendelea kushirikiana na Jeshi hilo na kutoa mchango wao utakao saidia kupunguza ajali zinazosababisha vifo na majeruhi kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri.
IGP Sirro amesema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na wadau wa usafirishaji nchini katika kikao kazi cha kufanya tathimini, changamoto na mafanikio kwa kipindi cha mwaka mzima.
Aidha, IGP Sirro ametoa maagizo kwa Makamanda wa Polisi nchini kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa magari katika maeneo yaliyoainishwa na kuepuka kusimamisha magari mara kwa mara.
Naye mdau wa usafirisha bwana Enos Lema, ameiomba serikali pamoja na mamlaka zinazohusika kuangalia upya suala la mabasi ya abiria yanayofanya safari zake mikoani pamoja na nchi jirani kuruhusiwa kuanza safari hata nyakati za mchana hatua itakayowezesha kupunguza changamoto za usafirishaji kwa abiria.
RC Asema Watumishi Watakaonyanyasa Wazee Kukiona
NA TIGANYA VINCENT
SERIKALI imesema haitawavumilia watumishi wa afya na watendaji wote ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakiwanyanyasa wazee wanapokwenda kupata huduma kwenye maeneo yao ya kazi.
Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora dokta Batilda Buriani alipokutana na viongozi wa dini na wazee wa mkoa huo kwa nia ya kujitambulisha tangu ateuliwa kushika wadhifa huo na pia kupokea changamoto zinazowakabili ili aweze kuzitafutia ufumbuzi.
Alisema Serikali ya Mkoa chini ya uongozi wake haitawafumbia macho watumishi wanatoa lugha na kauli zisizostahili kwa wazee na watu wengine waofika kwenye maeneo yao ya kazi kupata huduma.
Mkuu huyo wa Mkoa amesema huduma za Afya ni muhimu sana kwa wazee kwani walio wengi wamekuwa wanakabiliwa na magonjwa ya mara kwa mara hivyo wanahitaji uangalizi na matunzo maalumu na ya kitaalamu.
Alisema Serikali ya Mkoa itahakikisha Wazee wanapewa kipaumbele katika kupata huduma za kiafya kwa haraka na zilizo bora ikiwa ni pamoja na kuhakikisha madirisha ya Wazee yanakiweko katika hospitali, zahanati na vituo vyote vya Afya
Halikadhalika alielekeza zikiwemo Hospitali, Benki na Tanesco na Idara nyingne kuwapa kipaumbele Wazee na Viongozi wa Dini wanapofika kupata huduma.
Mkuu wa Mkoa aliwaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kunakuwa na madirisha ya Wazee katika Hospitali Zahanati na Vituo vya Afya ilii Wazee wasikae foleni wanapoenda kupata huduma,
Katika risala ya wazee hao iliyosomwa na Willfred Mrutu walisema kuwa walilalamikia kutopata dawa kwenye vituo vya kutolea huduma pamoja na baadhi ya watumishi kuwatolea lugha mbaya,
SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).
AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).
AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.
CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1. Shinikizo la damu (B.P)
2. Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3. Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4. Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5. Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6. Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7. Uzito na unene uliozidi
8. Kutofanya mazoezi
9. Umri
10. Kurith
UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1. Kusikia njaa mara kwa mara
2. Kusikia kiu mara kwa mara
3. Kupungua uzito
4. Maono machafu
5. Uchovu mara kwa mara
6. Ukipata kidonda hakiponi
7. Kushuka kwa kinga mwili
DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo kama cha mbuzi
DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi ya gonzi kukakamaa
TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.
Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.
Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.
BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152
TGNP YAJIVUNIA SIKU 100 ZA RAIS SAMIA... LIUNDI ASEMA ' ANA MWENDO WA TOFAUTI USAWA WA KIJINSIA'
INTERNSHIPS 6 posts at TPC Ltd
TPC Limited TPC Ltd is one of the fast growing sugar producing companies in Tanzania. The company is situated at the foot of Mount Kilimanjaro, 22kms south of Moshi Municipality. Applications are invited from qualified, energetic, proactive and dynamic Tanzanians to fill internships positions below….. Intern Details: Applications are invited from suitably qualified, energetic, proactive and dynamic […]
This post INTERNSHIPS 6 posts at TPC Ltd has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Kada wa CHADEMA Mdude Nyagali Aaachiwa Huru
Monitoring, Evaluation and Learning and GIS Officer at RTI International
RTI (www.rti.org) is an independent, non-profit organization dedicated to conducting innovative, multidisciplinary research that improves the human condition. With a worldwide staff of more than 4,000 people, RTI offers innovative research and development and multidisciplinary services. USAID Tanzania Tuhifadhi Maliasili Activity Research Triangle Institute (RTI) is an independent non-profit research institute dedicated to improving the […]
This post Monitoring, Evaluation and Learning and GIS Officer at RTI International has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Accountant at RTI International
RTI (www.rti.org) is an independent, non-profit organization dedicated to conducting innovative, multidisciplinary research that improves the human condition. With a worldwide staff of more than 4,000 people, RTI offers innovative research and development and multidisciplinary services. USAID Tanzania Tuhifadhi Maliasili Activity Research Triangle Institute (RTI) is an independent non-profit research institute dedicated to improving the […]
This post Accountant at RTI International has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Grants Assistant at RTI International
RTI (www.rti.org) is an independent, non-profit organization dedicated to conducting innovative, multidisciplinary research that improves the human condition. With a worldwide staff of more than 4,000 people, RTI offers innovative research and development and multidisciplinary services. USAID Tanzania Tuhifadhi Maliasili Activity Research Triangle Institute (RTI) is an independent non-profit research institute dedicated to improving the […]
This post Grants Assistant at RTI International has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Burna Boy Ashinda Tuzo Ya BET 2021 katika kipengele cha Best International Act
Msanii Burna Boy kutokea nchini Nigeria leo Juni 28, 2021 amefanikiwa kushinda tuzo ya BET kupitia kipengele cha BEST INTERNATIONAL ACT 2021.
Ushindi wa msanii huyo kutoka Nigeria, unamfanya awabwage washindani wake waliokuwa wakichuna katika kipengele hicho akiwemo Diamond Platnumz na Wizkid kutoka nchini Nigeria.
Wengine waliokuwa katika kipengele hicho ni Aya Nakamura (Ufaransa),Emicida (Brazili), Headie One (Marekani) Young T & Bugsey (Marekani) na Youssoupha (Ufaransa)
CCM Yahimiza Watanzania Kulinda Amani Ya Nchi
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinatambua na kuthamini mchango wa dini zote katika kuimarisha na kuhuisha amani, umoja na mshikamano nchini.
Hivyo CCM imewaomba watanzania kuendelea kuitunza, kuilinda na kuidumisha amani kwa vile maendeleo hayawezi kupatikana bila amani, mambo yote mazuri ili yafanyike ikiwemo ibada lazima amani iwepo kwanza hivyo kila mmoja asikubali kwa namna yoyote kuona amani ya nchi ikichezewa na kutoweka.
Akizungumza kwa Niaba ya Katibu Mkuu wa CCM, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndugu Shaka Hamdu Shaka katika mkutano mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) mkoani hapa amesema kazi ya kulinda na kuitunza amani ya nchi ni jukumu la kila raia mwema hivyo wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuvipa taarifa juu ya uwepo wa mipango au viashiria vya kuhujumu amani au kutenda uhalifu ili hatua stahiki za kisheria zichukuliwe kwa wakati.
"Mwenyezi Mungu katika Quran Suratul al Imran (103) amesema shikamaneni katika Kamba ya Mwenyezi Mungu, wala msifarikiane kumbukueni neema ya allah iliyo juu yenu. katika Zaburi 133 (1) anasema tazama ilivyo vema na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja. CCM inaipongeza Serikali inayongozwa na Rais Samia kwa namna inavyoendelea kuwaunganisha watanzania bila kujali itikadi za kisiasa, kiimani na kikabila" Alisema Shaka
Shaka amefahamisha kuwa CCM kupitia ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 itaendeleza amani, umoja, usalama, utawala wa sheria na utulivu wa kisiasa jambo ambalo litawezesha shuhuli zote za kiimani na kimaendeleo kufanyika nchini.
"Niwaombe watanzania wote tuendelee kumuombea Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan na serikali anayoiongoza kuendelea kutuongoza kwa kuheshimu utawala wa sheria, haki na usawa ili amani yetu iendelee kudumu na nchi yetu ipige hatua zaidi kimaendeleo." Alifahamisha Shaka.
Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango
Taaluma Ya Famasi Ni Muhimu Katika Vita dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza- Dr. Gwajima
Na. Catherine Sungura,WAMJW-Mwanza
Katika vita dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza Taaluma ya Famasi ni muhimu katika kuwezesha upatikananji wa bidhaa za dawa kwa wale watakaoshindwa kuzuia kupata magonjwa yasiayoambukiza na ikawalazimu wafike vituoni kupata tiba.
Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima wakati wa Kongamano la 12 la kisayansi la Chama cha Wanafunzi wa Taaluma ya Famasi (TAPSA) lililofanyika jijini Mwanza.
Dkt. Gwajima amebainisha kwamba bidhaa hizo za dawa kwa ajili ya kundi hilo ni ghali na bahati mbaya nchini Tanzania hakuna kiwanda cha kutengeneza na badala yake wanaagiza toka nje ya nchi.“Tunapaswa kutafakari iwapo kasi ya kukua kwa maradhi haya ni inaongezeka je tunazijazititi vipi kwenye kasi ya kinga kwani bado kasi hiyo ni ndogo”.Aliongeza Dkt. Gwajima.
Alisema kuwa, katika kupambana na magonjwa yasiyoambukiza Serikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa huduma bora karibu zaidi na wananchi kwa kujenga miundombinu , kuajiri watumishi na kuweka vifaa tiba na dawa. Maboresho haya yameendelea kufanyika katika vituo vya huduma za afya ngazi zote.
Hata hivyo amesema kumekuwa na changamoto mbalimbali ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi ikiwemo changamoto ya upatikanaji wa bidhaa za dawa na vifaa tiba kwa ajili ya huduma mbalimbali zikiwemo na huduma kwa ajili ya wanaougua magonjwa hayo yasiyoambukizwa.
Aidha, Dkt. Gwajima amesema wapo baadhi ya wanataaluma wachache wasio waadilifu na wasio wazalendo ambao ni doa kubwa kwenye taaluma hiyo adimu ambayo inatarajiwa kuwa na mchango mkubwa kwenye ajenda ya afya. Hivyo iwapo itasimama kwa nafasi yake basi wanataaluma hao wanaweza kufanya mapinduzi makubwa ya afya na kiuchumi.
“hii itawezekana kwa kujikita kwenye ajenda ya jinsi gani viwanda vya ndani viweze kuzalisha bidhaa mbalimbali na kuhakikisha matumizi yasiyotia shaka ya bidhaa za afya zinazopokelewa kwenye vituo vya huduma na kuepuka upotevu na matumizi yasiyofuata miongozo na kusababisha usugu wa baadhi ya dawa na pia baadhi kuleta madhara kwa wateja kama ilivyokusudiwa”.
Dkt. Gwajima alitoa rai kwa jamii ya kitanzania kuzingatia ulaji unaofaa ambapo kila mlo uwe na makundi yote matano ya vyakula halisi, kutotumia mafuta mengi,chumvi nyingi,kufanya mazoezi ,kupata usingizi wa kutosha,kuepuka matumizi ya tumbaku na madawa ya kulevya na pia kuchunguza afya angalau mara moja kwa mwaka.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 75 ya vifo vyote duniani vinavyohusu watu wenye miaka 30 hadi 70 husababishwa na magonjwa hayo.Hapa nchini inakadiriwa kuwa magonjwa yasiyoambikiza husababisha asilimia 27 ya vifo vyote.Kauli mbiu ya Kongamano hilo mwaka huu ni “Wataalamu wa Famasi: kuongeza wigo katika kupambana na magonjwa yasiyoambukiza”.
Awali akiongea wakati wa kongamano hilo Mfamasia Mkuu wa Serikali Bw. Daudi Msasi aliwataka wafamasia na wataalum wengine wa afya nchini kuhakikisha wanatumia fomu za dawa( prescription form) kama nyenzo muhimu za kuondoa changamoto za dawa kwani dawa ni fedha za haraka hivyo wahakikishe kabla hawajatoka lazima wahakikishe dawa zinatoka kwa kujaza fomu hizo.
Aliongeza kuwa kwenye kutenda kazi za umma lazima wafuate miongozo ikiwemo muongozo wa matibabu nchini (STG) wanapokuwa sehemu za kazi hivyo ni wakati wao sasa wa kupitia na kuelewa nini wanapaswa kutekeleza kwenye kazi zao.
Hata hivyo Bw. Msasi aliwataka chama hicho kuanziasha klabu za mazoezi kwenye vyuo vyao ili kuweza kupambana na magonjwa yasiyoambukiza kwa vitendo na hiyo itasaidia jamii kuelewa umuhimu wa kufanya mazoezi.
Naye Mlezi wa wanafunzi wa Famasi na Masajili wa Baraza la Famasi nchini Bi. Elizabeth shekalaghe aliwataka wanafunzi hao kufanya kazi kwa kujitoa, kuwajibika na kuipenda taaluma yao ili kuweza kuitumikia vyema taaluma yao.
Bi. Shekalaghe alisema kama Baraza wataendelea kusimamia na kuhakikisha wanaendeleza taaluma kwa kutoa elimu ya maadili kwenye vyuo vya famasi nchini ili wanapokua chuoni wazitambua na kuzijua angali wanafunzi.
Naye Rais wa Chama cha Wafamasia Wanafunzi Tanzania(TAPSA) Bw. Hamis Msagama ameipongeza Serikali kwa uboreshaji wa dawa na vifaa tiba ambapo kazi kubwa inafanywa na wafamasia na kuonesha jinsi gani inawajali watanzania.
Pia Bw.Msagama ameipongeza Wizara ya Afya kwa kuanzisha kitengo cha Magonjwa Yasiyoambukiza (NCD) hivyo wao kama chama waliona ni vyema kongamaono lao mwaka huu kujadili kwa kina namna ya kupambana na magonjwa hayo ambayo yanaathiri watu wengi nchini na duniani.
Majaliwa: Miradi 93imesajiliwa Siku 100 Za Rais Samia
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema katika kipindi cha siku 100 za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imesajili miradi 93 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 1.6 ambayo itaingiza ajira zaidi ya 24,600 kwa vijana.
Amesema kuwa hatua hiyo inatoa alama kwa wawekezaji wa nje kwamba kwa sasa urasimu katika sekta ya uwekezaji unaendelea kupunguzwa katika maeneo ya usajili wa makampuni pindi muwekezaji anapokusudia kuja kuwekeza nchini.
Waziri Mkuu ameyasema jana (Jumapili, Juni 27,2021) alipofungua Kongamano la siku 100 za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan lililofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Ametumia fursa hiyo kutaja miradi iliyotekelezwa katika kipindi cha siku 100.
Amesema mbali na miradi hiyo, pia Mheshimiwa Rais amefanya jitihada kubwa ya kuondoa tozo 232 zilizokuwa zinawakwaza wafanyabishara. “Tozo hizi zimeondolewa ili kuwawezesha wafanyabiashara kufanya biashara zao hapa nchini.”
“…Na haya yote ni katika kuongeza mzunguko wa fedha kwa Watanzania ambao wanashiriki katika shuhguli mbalimbali za kuimarisha uchumi wao.”
Waziri Mkuu amesema katika kufanya kazi zake, Mheshimiwa Rais Samia ameendeleza mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na nchi jirani ambapo ametembelea nchi za Kenya, Uganda na Msumbiji kwa lengo la kuimarisha urafiki na Mataifa ya jirani. Pia amepokea ujumbe kutoka nchi mbalimbali ikiwa ni alama ya mshikamano.
Amesema kuwa Mheshimiwa Rais Samia ameendelea kupanga mipango ya ujenzi wa miradi mipya katika siku 100 za uongozi wake ikiwemo kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa reli ya kimataifa kipande cha kutoka Mwanza mpaka Isaka, ujenzi wa meli mpya nne na ukarabati wa meli kongwe moja.
"Meli hizi zimewekwa katika maeneo yote, ziwa Victoria tuna meli moja ambayo ina uwezo wa kubeba tani 3000 za mizigo itakayotoa huduma kati ya Tanzania, Kenya na Uganda, pia meli nyingine ya MV Umoja ambayo awali ilikuwa inakwenda Uganda nayo inakarabatiwa"
Waziri Mkuu ameongeza kuwa katika kipindi cha siku 100 za uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia ameanzisha mradi wa shule za sekondari za wasichana katika halmashauri zote nchini. Pia amesema Rais ametoa shilingi milioni 500 kwa kila jimbo kwa ajili ya kukarabati barabara ili kuboresha huduma za usafiri vijijini.
Akiongea katika Kongamano hilo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Eric Hamissi amesema kuwa katika kipindi cha siku 100 za uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia mamlaka hiyo imepokea barua za pongezi kutoka katika makampuni makubwa ya usafirishaji duniani ikiwemo ya Mediterrainian na Mesina Line kwa uboreshaji wa huduma bandarini hapo.
Amesema kuwa katika kipindi cha robo ya mwisho kuanzia Aprili hadi Juni mwaka huu wameweza kukusanya shilingi bilioni 236.8 sawa na ongezeko la asilimia 14 ukilinganisha na robo iliyopita ya kuanzia Januari hadi Machi ambayo walikusanya shilingi bilioni 203.
Naye, Kamishna wa Uhamiaji nchini Dkt. Anna Makakala amesema kuwa kwa kushirikiana na idara ya kazi wameanza kutoa vibali kwa kutumia mfumo wa kielektroniki ambapo katika kipindi cha kuanzia Mei 2021 hadi sasa wametoa vibali 3,377 vya kazi ukilinganisha na vibali 2166 vilivyotolewa katika kipindi kama hiki kwa mwaka jana.
(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU