Sunday 28 February 2021

Bible Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Bible Teacher   Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Accounting & Business Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Accounting & Business Teacher     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Math Teacher – Middle School at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Math Teacher – Middle School     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

ART Teacher – Primary & Secondary at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ART Teacher – Primary & Secondary     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Music Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Music Teacher     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Library and Media Specialist at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Library and Media Specialist    Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Special Needs Coordinator at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Special Needs Coordinator     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

IT Teacher / Google App Specialist at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

IT Teacher / Google App Specialist    Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior School Principal at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior School Principal    Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Geography/History Teacher at Haven of Peace Academy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Geography/History Teacher     Haven of Peace Academy is an International Christian School looking for qualified teachers to join our mission to provide an excellent, Christ-centred education fulfilling international academic standards, equipping students to live out a Biblical worldview in all areas of their life to the glory of God. The following positions are open for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

NAIBU WAZIRI MARYPRISCA ATOA SIKU 7 PAMPU YA MAJI ILIYOCHUKULIWA NA MKANDARASI IRUDISHWE GEITA

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi MaryPrisca Mahundi (Mb) amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita Mhandisi Frank Changawa kuhakikisha mkandarasi wa awali aliyekuwa anatekeleza mradi wa Nyamtukuza Petty and Company (Ltd), kurejesha pampu ya mradi huo aliyorudishiwa kwa ajili ya matengenezo madogo ili iweze kufungwa na wananchi waendee kupata huduma ya maji safi na salama.

Ametoa kauli hiyo alipokuwa anakagua utekelezaji wa mradi huo ambao umechukua muda mrefu kukamilika kutokana na wakandarasi kushindwa kukamilisha mradi kwa wakati hadi mkataba ulipovunjwa na kazi ya utekelezaji kuchukuliwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA).

“Ninawapa siku saba (GEUWASA) kuhakikisha pampu iliyochukuliwa na Mkandarasi kwa ajili ya matengenezo inarejeshwa haraka ili ije ifungwe kwenye mradi kama mchoro wa awali unavyoonesha kufunga pampu mbili ili moja ikipata hitilafu, basi nyingine iendelee kufanya kazi, wananchi waendelee kupata huduma ya maji”, amesema Mhandisi Mahundi, na kusisitiza kuwa ndani ya siku hizo saba kupatiwa ripoti ya pampu hiyo kama imerejeshwa.

Amesema wananchi wengi nchini hususani wa maeneo ya vijijini wanahitaji maji na hivyo kuwataka watekelezaji wa miradi hiyo kukamilisha kwa wakati unaotakiwa ili wananchi wapate huduma wanayostahiki.

Aidha, amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA) na watendaji wake kwa kuweza kutekeleza mradi huu ambao hapo awali ulikuwa kati ya miradi kichefuchefu kwa kutokamilika kwa wakati na sasa mradi umefikia hatua za mwisho na baadhi ya wananchi wa Nyamtukuza wameanza kupata huduma ya majisafi. salama na yenye kutosheleza.

Mradi wa Nyamtukuza kwa sasa unatekelezwa na GEUWASA kwa kutumia wataalam wa ndani (Force Account) na umegharimu shilingi bilioni 11 ambapo kwa kutumia watalaam hao wa ndani serikali imeweza kuokoa shilingi bilioni 4 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi, 2021.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 28,2021














Share:

Saturday 27 February 2021

KUTANA NA NDEGE WA AJABU MWENYE JINSI MBILI...NUSU JIKE, NUSU DUME


Ndege ambaye ameonekana kuwa nusu-jike na nusu-dume amepigwa picha jimboni Pennsylvania na mfuatiliaji ndege baada ya kumsikia rafiki yake ambaye alimuona ndege huyo.

Ndege wa namna hii mwenye maumbile mchanganyiko ni nadra kuonekana.

Ndege aina ya cardinals dume ni wekundu lakini jike huwa ni rangi ya udongo iliyofifia, ikimaanisha kuwa spishi za ndege huyu pengine ni mchanganyiko wa jinsi mbili.

Mtaalamu wa masuala ya ndege Jamie Hill, 69, ameiambia BBC kuwa ilikuwa ni ''mara moja katika maisha, mara moja kati ya milioni''. Kukutana na ndege huyo.


Ndege wa kushangaza

Rafiki wa Bwana Hill alimwambia amemuona ''ndege asiye wa kawaida'' akifika katika malisho ya ndege katika kaunti ya Warren huko Pennsylvania.

Mara ya kwanza Bwana Hill alijiuliza ikiwa ndege huyo alikuwa na athari ya melanini kwenye manyoya yake, lakini hatakuwa nusu-jike, nusu-dume.

Lakini baada ya kuona picha kwenye simu, alishuku kuwa ndege huyo alikuwa na jinsia mbili, maana yake akiwa na ovari inayofanya kazi na korodani inayofanya kazi.

Alitembelea eneo ambalo ndege huyo alionekana.

Ndani ya saa moja aliweza kumpiga picha ndege huyo wa ajabu.

''Baada ya kupata picha, moyo wangu ulikuwa unadunda kwa saa tano mpaka nilipowasili nyumbani na kuzitengeneza picha ili kuona kile nilichonacho,'' alisema Bw.Hill.


Jamie hill amekuwa akichunguza kwa miaka 48

Ndege nusu-jike, nusu-dume ni nadra kupatikana, anaeleza profesa Brian Peer kutoka Chuo cha Illinois, ambaye amekuwa akifanya utafiti viumbe vya namna hiyo nchini Marekani.

Lakini, anaongeza kuwa hali hiyo inaweza isigundulike kwa baadhi ya spishi.
''Hali hii husababishwa na hitilafu wakati wa mgawanyo wa seli wakati wa kuumbwa kwake,'' alisema.

Ndege wa namna hii si mara ya kwanza kuonekana katika eneo hilo.

Mwaka 2019, wenza walimshuhudia ndege kama huyo, kwa mujibu wa jarida la National Geographic. Bwana Hill anashuku kuwa ndege ailiyemuona huenda akawa huyo huyo.

CHANZO - BBC SWAHILI
Share:

AJALI YA BASI,GARI NDOGO YAUA WATU WANNE WAKIWEMO WAFANYAKAZI WA MAMLAKA YA MAJI SIMIYU


Magari yaliyopata ajali na kuua watu wanne
**
Watu wanne wamefariki dunia, akiwamo Afisa Ugavi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (RUWASA) mkoa wa Simiyu, Castory Mamboleo (35), kufuatia ajali iliyohusisha magari mawili wilayani Bariadi, mkoani humo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu, ACP Richard Abwao, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kusema kuwa ajali hiyo imetokea Februari 26, 2021, saa 1:30 jioni katika eneo la Dutwa wilayani Bariadi, ambapo mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa.

Kamanda Abwao amewataja watu wengine waliopoteza maisha katika ajali hiyo ya barabarani kuwa ni Penina Naveta (38) ambaye ni Afisa Utumishi wa RUWASA mkoa wa Simiyu, Raphael Kichele (30) mfanyabiashara na Ntobi Mpalala ambaye ni mtoto mwenye umri wa miaka7, mwanafunzi na mkazi wa Dutwa.

Magari yaliyogongana na kusababisha vifo vya watu hao ni T 851 DKF Toyota Mark X na T 350 DUH, TATA BUS mali ya kampuni ya Ngalabushi, iliyokuwa ikiendeshwa na Paulin Abel (31) mkazi wa Lamadi, na kusema kuwa basi hilo lilikuwa likitokea Lamadi kuelekea Bariadi.

Share:

WATUMISHI WA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA WAASWA KUYAISHI MAISHA YA KAIZEN MAHALA PA KAZI

 

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Raslimali watu wa wizara ya viwanda na biashara Bi Veronica Nchango akizungumza wakati akifunga mafunzo ya KAIZEN kwa watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Chuo cha Biashara CBE jijini Dodoma kuanzia Februari 23 hadi 25, 2021. Mafunzo yalilenga kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa Wizara hiyo ili kuleta tija mahala pa kazi.

Mkuu wa kitengo cha KAIZEN Tanzania ambaye ni afisa Biashara Mkuu Wizara hiyo Bi Jane Lyatuu akifafanua jambo kwa wajumbe wakati ya kuhitimisha mafunzo ya KAIZEN kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara yaliyofanyika katika Chuo cha Biashara CBE jijini Dodoma kuanzia Februari 23 hadi 25, 2021. Mafunzo yaliyolenga kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa Wizara hiyo ili kuleta tija mahala za kazi.

Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Viwanda Bw. Gaitan Mrimi akitolea ufafanuzi jambo wakati ya kuhitimisha mafunzo ya KAIZEN kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara yaliyofanyika katika Chuo cha Biashara CBE jijini Dodoma kuanzia Februari 23 hadi 25, 2021. Mafunzo yaliyolenga kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa Wizara hiyo ili kuleta tija mahala za kazi.

Mkufunzi wa KAIZEN Bw. Emanuel Zakayo akitoa majumuisho mara baada ya kumalizika kwa ziara ya kutembelea viwanda wakati ya kuhitimisha mafunzo ya KAIZAN kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara yaliyofanyika katika Chuo cha Biashara CBE jijini Dodoma kuanzia Februari 23 hadi 25, 2021. Mafunzo yaliyolenga kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa Wizara hiyo ili kuleta tija mahala za kazi

Mratibu wa mafunzo ya KAIZEN ambaye ni Mhandisi wa Wizara hiyo Eng. Kamala Gombe akifafanua jambo wakati ya kuhitimisha mafunzo ya KAIZEN kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara yaliyofanyika katika Chuo cha Biashara CBE jijini Dodoma kuanzia Februari 23 hadi 25, 2021. Mafunzo yaliyolenga kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa Wizara hiyo ili kuleta tija mahala za kazi.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria mafunzo ya KAIZEN wakiangalia bidhaa aina ya wine zinazotengenezwa na kiwanda cha Dane Holding wakati walipotembelea kiwanda hicho kilichopo Mkulabi Mpunguzi Jijini Dodoma.

Meneja uzalishaji wa kiwanda cha Dane Holding Limited Bw. Meshack Yotam kulia akitoa maelezo ya namna kiwanda hicho kinavyofanyakazi au moja ya njia katika uzalishaji wa wine kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda waliohudhuria mafunzo ya KAIZEN walipotembelea kiwanda hicho kuona KAIZAN inavyotekelezwa mahala pa kazi.

Meneja uzalishaji wa kiwanda cha Glory Farm kilichopo Nane nane Jijini Dodoma kinachojihusisha na uzalishaji wa mafuta ya alizeti Bw. Denis Kokino akionesha moja ya mtambo wa kusafisha mafuta ya alizeti kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara waliohudhuria mafunzo ya KAIZEN walipotembelea kiwanda hicho kwa mafunzo.

Meneja uzalishaji wa kiwanda cha Glory Farm kilichopo Nane nane Jijini Dodoma kinachojihusisha na uzalishaji wa mafuta ya alizeti Bw. Denis Kokino akitolea ufafanuzi moja ya jambo kwa watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara waliohudhuria mafunzo ya KAIZEN walipotembelea kiwanda hicho kwa mafunzo.

Afisa Tawala mwandamizi wa Wizara hiyo. Bw. Juma Mantatakala akionesha moja ya mtambo wa kusafisha mafuta ya alizeti akitaka kujua namna unavyofanya kazi, wakati watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara waliohudhuria mafunzo ya KAIZEN walipotembelea kiwanda cha kukamua na kusafisha mafuta cha Glory Farm kilichopo Nane nane Jijini Dodoma kwa mafunzo ya vitendo.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Raslimali watu wa wizara ya viwanda na biashara Bi Veronica Nchango amewasisitiza watumishi wa Wizara hiyo kuishi maisha kwa kufuata misingi ya Falsafa ya KAIZEN inayowahimiza kuzingatia udhibiti wa mazingira ya kazi na kuboresha usimamizi wa raslimali kama vile Mda Watu na Fedha ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.

Bi Nchango ameyasema hayo alipokuwa akifunga mafunzo ya KAIZEN kwa watumishi wa Wizara hiyo yaliyofanyika katika Chuo cha Biashara CBE jijini Dodoma kuanzia Februari 23 hadi 25, 2021. Pia Amewasisitiza watumishi hao kuzingatia ubunifu, ubora na tija ili kupunguza malalamiko, upotevu na gharama zisizokuwa za lazima katika utendaji kazi.

Amewahimiza watumishi hao kuwa chanzo cha mabadiliko katika utendaji wao na wawafundishe watumishi wenzao katika wizara nyingine pamoja na familia zao wakiwemo watoto wao ili wakue katika misingi ya kufanya kazi kwa ufanisi, tija na ubora nchini.

Aidha, Mkurugenzi huyo amewashauri wakufunzi wa Falsafa ya KAIZEN kuongeza S moja inayomaanisha “Sensitization” ili kuhamasisha watu zaidi kujifunza na kutekeleza falsafa hii katika kuongeza tija na ubora. “S” nyingine (5) tano zinazotumika kama njia za utekelezaji wa KAIZEN ni Sasambua (Sort), Seti (Seti), Safisha (Shine), Sanifisha (Standardize) na Shikilia (Sustain).

Ameshauri mafunzo hayo yaliyolenga kuongeza ufahamu kuhusu falsafa KAIZEN inayolenga kuongeza thamani endelevu ya tija na ubora viwandani yaingizwe kwenye mitaala ya shule na yafundishwe nchi nzima ili kuhimili kufikia matokeo bora, makubwa na kwa haraka na kuhimili ushindani.

Aidha, Mkurugenzi huyo aliwapongeza watumishi hao kwa kuhudhuria mafunzo hayo pamoja na kutembelea Viwanda vinavyotekeleza falsafa ya KAIZEN vilivyopo jijini Dodoma kama sehemu ya mafunzo kwa vitendo. Viwanda hivyo ni Dane Holding Limited kinachotengeneza mvinyo na kiwanda cha “Groly Farm” kinachozalisha mafuta ya Alizeti.

Utekelezaji wa KAIZEN nchini unayofadhiliwa JICA unalenga kuongeza tija na ubora katika sekta ya viwanda na shughuli za maisha ya kila siku inaongozwa na misingi ambayo ipo katika ubunifu wa mawazo, maarifa na ushiriki wa kila mtu ndani ya taasisi, shirika au kampuni ili kuhimili ushindani.

KAIZEN ni neno la kijapani lenye maana ya badilika kwa ubora / uzuri linalohusu shughuli endelevu zinazofanyika ili kuboresha kazi mifumo michakato na nyanja yoyote ya kuendesha biashara. KAIZEN asili yake ni Japani lakini sasa inatekelezwa Duniani kote.

Share:

FURAHIA HUDUMA ZA KIBENKI UKIWA NA 'SIMBANKING' MZIGO ULIOBORESHWA

Benki ya CRDB imeboresha huduma yake ya SimBanking na kuipa jina la Benki ni SimBanking 'Mzigo Ulioboreshwa' . Maboresho haya makubwa yanampa uhuru mkubwa mteja kufanya miamala yote kupitia SimBanking na ndiyo maana sasa inaitwa Benki ni SimBanking.

Benki ni SimBanking inawawezesha wateja kufungua akaunti wenyewe bure popote walipo na kupata huduma za kibenki mbalimbali ili kuhakikisha Benki ya CRDB inakuwa kinara wa teknolojia katika utoaji wa huduma za kibenki.


Share:

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI MKUTANO WA EAC KWA NJIA YA MTANDAO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki mkutano wa 21 wa kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika leo tarehe 27 Februari, 2021 kwa njia ya mtandao.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger