Saturday 23 January 2021
DC MBONEKO ATINGA HOSPITALI YA MKOA WA SHINYANGA SAKATA LA MLINZI KUPIGA MTU..AITAKA KAMPUNI YA ULINZI SUMA JKT KUCHUKUA HATUA
WACHAWI WAAPA KUMROGA ALIYECHOMA MOTO KANISA LAO
MAMA AJIUA AKIWA NA UJAUZITO WA MIEZI 9 KISA WIVU WA MAPENZI
RC SINGIDA AMVUA UONGOZI MWALIMU MKUU KWA TUHUMA ZA UBADHILIFU
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akizungumza na watendaji na wananchi ambapo alimuagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Singida DC Rashid Mwandoa kumvua cheo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwachambia, Edward Ighonde pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi Charles Mtiko kwa tuhuma ya wizi wa vifaa vya ujenzi wa nyumba ya walimu .
Na Mwandishi Wetu, Singida
MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amemwagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Singida Dc Ndugu Rashid Mwandoa kumvua cheo Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mwachambia, Edward Ighonde pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi Charles Mtiko Kwa tuhuma ya wizi wa vifaa vya ujenzi wa nyumba ya walimu (Two in one).
Vifaa vinavyodaiwa kuibiwa ni mbao za kupauliwa, Saruji na nondo ambayo thamani yake bado haijafahamika.
Dkt. Nchimbi ametoa agizo hilo baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kwa lengo la kukagua miradi ya maendeleo ya ujenzi ambapo watuhumiwa wote wako Polisi.
Aidha ametoa maagizo kwa viongozi kuacha tabia ya kuwatetea watumishi wanao tuhumiwa kwa ubadhilifu na atakaye bainika atashughulikiwa vilivyo.
Nchimbi amewataka viongozi wa Serikali kusimamia miradi na kuwa waminifu katika fedha zinazoletwa na Serikali ya Rais Magufuli pia wananchi wa hakikishe wanalinda mali hizo kwani miradi hiyo ni kwa ajili ya maendeleo yao.
Various Posts at Musoma Utalii Training College
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
About the College Musoma Utalii Training College is a college registered by Ministry of Education, National Council for Technical Education (NACTE) and Vocational Education Training Authority (VETA). We are offering different courses as per society needs. The College is located near Bweri Bus Terminal in Musoma municipality. It is an oldest College in Lake Zone […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Many (Various) Hotel Jobs in Moshi (Kilimanjaro)
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
A new Hotel in Moshi (Kilimanjaro) is looking for a dynamic and experienced person to take the role of following vacancies – Apply free to these various Hotel job openings. Many (Various) Hotel Jobs in Moshi (Kilimanjaro) January, 2021 SOURCE: Mwananchi newspaper The deadline for submitting the application is 23 January, 2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Marketing & Sales Officer in Insurance at Speed Ways Limited
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Marketing & Sales Officer in Insurance SPEEDWAYS LIMITED is a privately owned Insurance Agents Under Phoenix Assurance Company Limited and established in 1978, with its offices based in Dar-Es-Salaam- TANZANIA. Our mission is to serve our customers by providing them with cost- effective solutions that continually meet and exceed our customers’ expectations and provide unquestionable […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Pastry Chef at Meliá Hotels International
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Pastry Chef Meliá Hotels International Arusha, Tanzania At Meliá Hotels International, you have the power to create your future. For us, the most important thing is your talent: We share the passion that makes you put your heart into everything you do, day after day. We are by your side to help you go […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Interns at Gwala Digital
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Interns Gwala Digital Dar es Salaam, Tanzania Gwala Digital is a digital marketing agency based in Dar Es Salaam – Tanzania. We are currently offering limited internship opportunities to passionate individuals who are willing to learn, practice and grow their skills. We are looking for people with the skills listed below: 1 – Videography 2 […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Friday 22 January 2021
BARAZA LA MCHELE TANZANIA (RCT) LAWAFUNDA WASINDIKAJI WA ZAO LA MPUNGA 100 KANDA YA ZIWA KULETA USHINDANI SOKO LA KIMATAIFA
Baraza la mchele Tanzania(RCT) kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti Tanzania (REPOA) wanaendesha mafunzo kwa wasindikaji wa mpunga 100 kutoka mikoa ya Geita,Shinyanga, na Tabora ili kuwajengea uwezo wa kusindika bidhaa hiyo kwa viwango vya kimataifa.
Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi mkuu wa baraza hilo, Winnie Bashagi katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa wasindikaji wa zao la mpunga kutoka mikoa ya kanda ya ziwa na kusema kuwa mchele wa Tanzania unakosa soko kimataifa kutokana na kutofungashwa kwa viwango vya kimataifa.
Alisema zaidi ya asilimia 80 ya mchele unaozalishwa na wakulima wadogo katika wilaya zaidi ya 64 hapa nchini unakosa sifa katika masoko ya kikanda ya jumuia ya afrika mashariki (EAC) na (SADC) kutokana kutosindikwa kwa viwango vinavyotakiwa licha ya kuwa na uzalishaji mkubwa.
“RCT na REPOA tulifanya utafiti katika wilaya zinazolima zao hili tulibaini kukosekana kwa elimu ya usindikaji,wasindikaji wengi wanachanganya madaraja,usafi,usimamizi usiridhishwa wa magahala ya kuhifadhia mpunga,matumizi yasiyosahihi ya pembejeo kwa wakulima wakati wa kuandaa mashamba,”alisema Bashagi.
Awali akifungua mafunzo hayo ya siku tatu Katibu tawala wa wilaya ya Kahama Timoth Ndanya kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack aliwataka (RCT) kufungua ofisi katika mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa lengo la kuwajengea uwezo wakulima na wasindikaji katika kuongeza thamani mazao yao.
“Kahama tunazalisha mpunga wa kutosha hakikisheni mnawajengea uwezo wasindikaji na wakulima wa zao hili la biashara ili kuwainua kiuchumi hakuna sababu ya wao kuendelea kukosa masoko ilihali wanamchele safi ambao unahitaji kupangwa katika madaraja yanayotakiwa kimataifa,”alisema Ndanya.
Naye Steven Mombela mtafiti kutoka (REPOA) alisema wao kwa kushirikiana na baraza la mchele wanatekeleza mradi huo ujulikanao kama Tradecom II kwa ufadhili wa jumuiya ya ulaya (EU) na waliandaa mafunzo hayo ili kuwajengea uwezo ili waweze kuzalisha mchele wenye viwango vinavyokidhi ushindani katika soko la ndani na nje ya nchi.
“Mradi huu ni wa miaka miwili ulianza mwaka 2020 na unatarajiwa kukamilika mwaka huu,na tukimaliza kwa kanda hii tutaelekea katika kanda nyingine inayojumuisha wasindikaji kutoka mikoa ya Morogoro,Njombe,Iringa na Mbeya,”alisema Mombela.
Asha Hassan Msangi ni mmoja wa wasindikaji wa zao mpunga kutoka Kahama ameiomba Serikali kuboresha mazingira ya biashara ya mchele ikiwa ni pamoja na kufungua masoko ya mchele na kuwazuia wafanyabiashara wa nje kununua mpunga kwa wakulima.
SERIKALI YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA WATAFITI KUBORESHA TIBA ASILI NCHINI
******************
Serikali ya Mkoa wa Morogoro, na hasa vitengo vya Uchumi na Mali Asili vimewahakikishia wadau wa tiba asili kuwa wako tayari kushirikiana nao kikamilifu ili kuona kuwa mimea dawa nchini inatumika kwa uangalifu na kwa mpango endelevu.
Wito huo umetolewa na katibu tawala Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo kwa niaba yake na Mratibu wa Tiba asili mkoa wa Morogoro Dkt. Ngalula Wille wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya siku moja ya wadau wa tiba asilina bidhaa zake yaliyofanyika mkoani Morogoro nankuandaliwa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kupitia Mradi wa GRILI.
"Hivyo tunawaahidi kuwa tutaendelea kuwa nanyi bega kwa bega kwa kusaidia jitihada za wadau wote kwenye sekta hii katika kuboresha biashara hii ya bidhaa zitokanazo na mimea dawa kwa kadri mazingira yatakavyoruhusu" Alisisitiza Dkt. Ngalula.
Mratibu huyo wa tiba asili mkoa wa Morogoro amewataka wazalishaji wa bidhaa hzo za mimea dawa kipindi hiki ambacho kuna ugonjwa wa mlipuko kama COVID-19, waone namna gani watatengeneza dawa ilikusaidia jamii kukabiliana na majanga kama haya yanayiweza kujitokeza.
"Nimefurahishwa sana na taarifa kwamba maonesho haya yamendaliwa na Chuo chetu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kupitia Kurugenzi yake ya Uzamili kitengo chake cha Uhaulishaji wa tekinolojia pamoja na mradi wa utafiti wa GRILI Hii inatokana na uzoefu na ueledi walionao kwenye masuala ya utafiti na Biashara za aina hii zikiwemo za bidhaa zinazotokana na mimea dawa hivyo ni matumaini yangu kuwa maonesho haya, yataangalia pia namna yakupunguza changamoto za uzalishaji na za kibiashara zilizopo na zinazoweza kujitokeza katika biashara nzima ya bidhaa za mimea dawa" Alisema Dkt. Ngalula.
Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua maonesho hayo Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha Prof. Amandus Mhairwa kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo Prof.Raphael Chibunda amesema kuwa ingawa kwenye kanuni zabiashara ya madawa kuna mitizamo tofautikuhusu kutangaza dawa za mimea zitokanazona mimea tiba, lakini ukweli ni kwamba bilikujitangaza, wateja hawatatambua biashara za bidhaa na soko.
“Biashara hii iko pia kwenye biashara ya huduma zinakuzwa sana na watoa huduma wenyewe hivyo hii sio tu yatatangaza biashara zao bali pia yatatangaza watoa huuma wenyewe na kauli zao kwa wateja ni muhimu sana ili waweze kupata masoko ya bidhaa na huduma zao hvyo lengo la maonesho haya nikuwakutanisha wazalishaji, wasambazaji, watengenezaji na wanunuzi wa bidhaa za mimea dawa” alifafanua Prof Mhairwa.
Aliongeza"Napenda niwahakikishie wadau hawawanaozalisha dawa zinazotokana na mimeadawa kwamba, Chuo Chetu cha SUA, kupitia kurugenzi ya Uzamili, Utafiti,Uhaulishaji waTekinolojia na Ushauri wa Kitaalaamu, kwakushirikiana na Watafiti tulionao na wamasuala ya kisayansi na tekinolojia, na wale wa masuala ya biashara, tutaendelakushirikiana bega kwa bega na wajasiriamalihawa ili kuboresha bidhaa wanazozalishatukishirikiana na wadau wengine katika sektahii kwa kadri uwezo wetu utakavyoturuhusu".
Akitoa neno la shukrani kwa mgeni rasmi Ras wa Ndaki ya Sayansi za jamii na Insia Prof. Samweli Kabote kwa niaba ya Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma Prof. Maulid Mwatawala amesema wamepokea ushauri na maelekezo yote aliyoyatoa mgeni rasmi na kuahidi kutafanyia kazi na kushirikiana nao zaidi katika kuboresha bidhaa za tiba asili kufikia viwango vya kimataifa ili kuinua uchumi wao na taifa sambamba na kuboresha afya za jamii.
Amesema maonesho hayo ni mwanzo wa maonesho ya fursa nyingi za katika tafiti za mimea dawa na tiba asili na kuwataka wataalamu wa tiba asili kuwatumia watafiti wa SUA kwenye mambo mbalimbali yanayohitaji sayansi zaidi.
Kwa pande wake Mkuu wa Mradi wa GRILI ambao ndio waandaaji wa maonesho hayo Dkt. Faith Mabiki amesema tafiti nyingi zimefanywa na watafiti wa SUA kwenye Mradi huo kwenye masuala ya miti dawa na kupata matokeo mazuri ambayo yatassidia kwenye kuongeza thamani na kuboresha tiba asili na uendelevu wake.
Dkt. Mabiki ametumia nafasi hiyo kuwakaribisha wadau wote wa Tiba asili nchini kushiriki kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Ubunifu katika tiba asili na bidhaa zake litakalofanyika kwenye Ndaki ya Solomon Mahlangu ya Sayansi na Elimu kwenye kampasi ya Mazimbu kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 7:00 Mchana.
Amesema uzinduzi wa jukwaa hilo utakuwa mwanzo mzuri wa kupata jukwaa la pamoja kati ya wadau wote wa tuba asili na wasimamaizi wa tiba asili upande wa serikali kujadiliana kwa pamoja mambo muhimu ya kuendeleza sekta hiyo ambayo imeshika kasi sana ikilinganishwa na huko nyuma kabla ya Ugonjwa wa Covid-19.