Friday 22 January 2021

Breaking : APIGWA NA WALINZI WA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SHINYANGA AKIHUDUMIA MAMA YAKE WODINI

Mlinzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga ambaye hajajulikana mara moja jina lake akimshambulia Daudi Lefi leo jioni ambapo video ya tukio hilo imesambaa mtandaoni 
Mlinzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga akimshambulia Daudi Lefi
Mlinzi wa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga akiamua ugomvi uliotokea mlinzi mwenzake akiendelea kumshambulia Daudi Lefi.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katika hali isiyotarajiwa mwanaume aliyejulikana kwa jina la Daudi Lefi (40) amejikuta katika wakati mgumu baada ya kushambuliwa na Walinzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga wanaodaiwa kumtaka aondoke wodini kwamba muda wa kusalimia wagonjwa umeisha. 

Tukio hilo lililozua gumzo la limetokea leo Ijumaa Januari 22,2020 majira ya saa 11 na dakika 45 jioni wakati kijana hiyo akiwa aktika wodi ya wanawake namba 1 ambako mama yake mzazi Victoria Lugano Mwakagari aliyelazwa hospitalini hapo jana. 

Akisimulia kuhusu tukio hilo, ndugu wa kijana huyo Lydia Lefi amesema kuwa kaka yake amekutwa na mkasa huo wakati akiwa katika harakati za kulipia dawa za mama yao ambaye amelazwa katika hospitali hiyo jana Januari 21,2021. 

“Kaka alikuwa alipie dawa, alipewa karatasi ya kwenda kulipia dawa, alipoenda kufuata Control number ili alipie, jina likawa halionekani , ikabidi aende wodini kwa mgonjwa kuangalia amesajiliwa kwa jina gani,akiwa wodini hao walinzi ndipo walipoingia wodini na kumtaka aondoke kwamba muda umekwisha. 

"Walivyomtaka aondoke wodini akawaambia amekuja kuangalia jina gani mgonjwa ameandikishwa, wale walinzi wakamwambia aondoke muda huo huo, akawaomba lakini wakamwambia huwezi kutupangia kazi. Kaka akasema nitaondokaje mama hajapata huduma ,wale walinzi wakaanza kumsukuma ndipo mlinzi mmoja akachomoa mkanda wa suruali na kuanza kumshambulia huku mwingine akimsukuma, baadae akaja mlinzi wa kike akasogea na kuwaachanisha”,ameeleza Lydia.

Daudi Lefi amesema walinzi hao hao walidhani amefika muda huo huo hospitalini wakati yeye alikuwa  amefika hospitalini hapo muda mrefu lakini Computer za Hospitali zikawa hazisomi jina la mgonjwa wake wakati anataka kununua dawa.

"Sikurusha ngumi kwa sababu ni eneo la hospitali wangesema nimeenda kufanya vurugu. walionishambulia walikuwa wawili lakini mmoja ndiyo aliyeanza kwa kunichapa na mkanda", amesema Daudi.

"Wamenifuata na mkubwa wao na kuniomba tuyamalize kwamba kijana wao amekosea nami nimeamua kuwasamehe. Katika hali ya ubinadamu nimeamua kumsamehe kijana huyo baada ya kuomba radhi",ameongeza. 

 Baadhi ya wagonjwa na watu wanaouguza wagonjwa wameeleza kusikitishwa na kitendo cha mlinzi kumpiga ngumi na mkanda na kuongeza kuwa baadhi ya walinzi katika hospitali hiyo wana lugha mbaya na wanatumia ubabe hawaangalii utu.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga, Luzila John Boshi amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa atatoa taarifa baadae na kwamba yupo kwenye kikao.

Tutawaletea taarifa zaidi hivi punde
Share:

Picha : RPC MAGILIGIMBA AZINDUA MRADI WA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO....SPC, RAFIKI SDO, YWL, TAI NA HALMASHAURI YA SHINYANGA WAUNGANA.


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akionesha Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto Mkoa wa Shinyanga wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba amezindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). 

Uzinduzi huo umefanyika leo Januari 22,2021 katika kata ya Iselamagazi halmashauri ya wilaya ya Shinyanga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa mkoa, halmashauri, maafisa maendeleo ya jamii,maafisa watendaji wa kata, waandishi wa habari na wawakilishi wa mashirika yanayotetea haki za wanawake na watoto. 

Kamanda Magiligimba amesema suala la ulinzi wa mtoto ni la kila mtu katika jamii na kusisitiza kuwa ni wajibu wa kila kiongozi kuanzia ngazi ya mkoa,halmashauri,kata na kijiji kuhakikisha wanakuwa na mipango mikakati ya kuzuia unyanyasaji wa mwanamke na mtoto katika himaya zao. 

Aidha amempongeza Mkuu wa mkoa wa Shinyanga kwa kuweka Mpango Mkakati wa Mkoa katika kukomesha vitendo vya ukatili wa kijinsia ifikapo mwaka 2025 ambao umekuwa chachu ya mabadiliko katika mkoa wa Shinyanga. 

“Nimtake Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutengeneza Sheria ndogo ambazo zitasaidia kila Mtendaji wa Kata au Kijiji kuhakikisha kwenye himaya yake hakuna mimba kwa wanafunzi wala ndoa za utotoni na kama zitatokea basi tujitahidi kumpata mtuhumiwa ili kupata hukumu ambayo itakuwa fundisho kwa jamii ili iachane na vitendo vya ukatili”,amesema Kamanda Magiligimba. 

Amelishukuru Shirika la Women Fund Tanzania kwa kufadhili mradi wa Ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambao utadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Januari 2021 hadi Machi 2021. 

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba amesema mradi huo utakuwa chachu ya mabadiliko katika jamii ili kuondokana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

Hata hivyo amesema halmashauri hiyo inaendelea na utaratibu wa kuwa na Sheria ndogo katika kila kijiji ili kuchukua hatua dhidi ya matukio ya ukatili wa kijinsia katika jamii. 

Kwa upande wake, Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia amewasihi wadau waliopata ruzuku kutekeleza mradi huo ikiwemo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Rafiki Social Development Organization, Thubutu Africa Initiatives (TAI), Young Women Leadership ( YWL) na Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club –SPC) kuzingatia taratibu za utekelezaji miradi pamoja miongozo ya serikali. 

Amesema WFT inaendelea kupokea mawazo mazuri kutoka kwa wadau yatakayoleta matokeo chanya kwani shirika hilo lipo kwa ajili ya kuhudumia jamii na kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na kufurahia nchi yao. 

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, Alphonce Kasanyi amewataka watekelezaji wa mradi huo kutoa taarifa za fedha za mradi kwa wakati bila kuchelewa hata kidogo na kuepuka kutoa takwimu za uongo huku akiwasisitiza kufanya kazi kwa ushirikiano. 

Kwa upande wao, watekelezaji wa Mradi huo,wamesema wamejipanga kikamilifu katika kuhakikisha wanatekeleza mradi wa kutokomeza ukatili wa dhidi ya wanawake na watoto katika kata 13 ambazo ni Solwa, Lyabukande, Lyamidati, Nyamalogo, Mwalukwa, Pandagichiza, Ilola, Puni, Nyida, Usule, Mwamala, Itwangi na Masengwa. 

Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia Kwesigabo aliwakumbusha watekelezaji wa mradi huo wasisahau kuyafikia makundi maalumu wakiwemo watu wenye ulemavu kwani wapo wanaofanyiwa matukio ya ukatili lakini hawapati nafasi ya kusemewa. 

Nao wadau walioshiriki uzinduzi huo wameshauri ushirikishwaji wa wazee maarufu, wa kimila wanaume wanaopendelea kwenye vijiwe vya kahawa, viongozi wa sungusungu,watoto,wasanii wa nyimbo za asili ‘marenga’ ili jamii ione kuwa huo ni mkakati halisi wa kuhamasisha kuachana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

Naye Mkaguzi Msaidizi wa Polisi kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Analyse Kaika ameshauri jamii kutoa ushahidi kwenye kesi zinazohusu matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto huku Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga Victoria Maro akiwaomba wadau kulifikia pia kundi la wanawake wanaofanya biashara ya ngono na kuangalia vyanzo vya mimba kwa wanafunzi.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). Kulia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba, Kushoto ni Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, Alphonce Kasanyi. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT). Wa kwanza kulia ni  Afisa Mradi Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akifuatiwa na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akizungumza leo Januari 22,2021 wakati akizindua rasmi Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga, Alphonce Kasanyi akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Hoja Mahiba akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mratibu wa MTAKUWWA halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Aisha Omary akielezea kuhusu utekelezaji wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na halmashauri hiyo pamoja na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).
Mratibu wa MTAKUWWA Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga , Aisha Omary akiwasilisha Mpango Kazi wa Halmashauri hiyo kuhusu namna watakavyotekeleza mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini wakifuatilia uwasilishwaji wa mipango kazi ya utekelezaji wa mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Afisa Miradi wa shirika la Young Women Leadership (YWL), Veronica Massawe akiwasilisha mpango kazi namna watakavyotekeleza Mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga
Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club -SPC), Estomine Henry akiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji wa mradi wa Nafasi ya Vyombo vya Habari katika kumaliza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club -SPC), Estomine Henry akiwasilisha mpango kazi wa utekelezaji wa mradi wa Nafasi ya Vyombo vya Habari katika kumaliza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Mratibu wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kutoka Shirika la Rafiki SDO, George Nyanda akiwasilisha mpango wa utekelezaji wa mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto walioupa jina la "Tuwalee".
Meneja Miradi kutoka Shirika la Thubutu Africa Initiatives ,Paschalia Mbugani akiwasilisha mpango kazi wao katika kutekeleza mradi wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto  wilaya ya Shinyanga, Victoria Maro akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Afisa Mradi wa Shirika la Women Fund Tanzania mkoa wa Shinyanga, Glory Mbia akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Salehe Hassan akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mkaguzi Msaidizi wa Polisi kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga Analyse Kaika akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wilaya ya Shinyanga Faustine Sengerema akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga
Mtoto Stephen Kiyenze akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Mtoto Irene Laurent akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini.
Meneja Miradi wa Shirika la ICS ,Sabrina Majikata akichangia hoja wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Kuruthum Mlolwa kutoka shirika la PWWCO akichangia hoja ukumbini.
Mdau akichangia hoja ukumbini.
Mdau kutoka Shirika la TIDO akichangia hoja ukumbini
Afisa Ustawi wa Jamii halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Agnes Ginethon akichangia hoja ukumbini.
Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Muhoja akizungumza ukumbini.
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Wadau wa haki za wanawake na watoto wakiwa ukumbini
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba akipiga picha ya pamoja na wadau wa haki za wanawake na watoto baada ya kuzindua Mradi wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Rafiki SDO,Thubutu Africa Initiatives, Young Women Leadership, Shinyanga Press Club na halmashauri hiyo kwa ufadhili wa Shirika la Women Fund Tanzania (WFT).

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Tutegemee Makubwa Kutoka Kampuni Ya Simu ya Infinix.


Kampuni ya simu Infinix Mobile LTD inasema tukae mkao wa kula. Je ni nini tutegemee kutoka Infinix?


Na kama ni simu mpya je nisimu kutoka series gani na kama ni valentine campaign basi watujuze tuanze kujichanga mapema ...nimewazatu.


Nikiwa bado najiuliza ni nini hasa Infinix kutuletea mapema mwaka huu? lakini pia tufahamu Infinix imekuwa kampuni imara na iliweza kuthibitisha hilo mwaka jana ambapo COVID-19 iliweza kusimamisha biashara nyingi lakini kwa Infinix bado walisimama imara nakuendelea kutupa simu zilizo bora kama vile Infinix NOTE 8 inayoendelea kutamba sokoni kutokana na ubora wake wa MP16 za camera ya mbele na MP64 za camera ya nyuma.


Uimara wa kampuni hii kunazidi kunipasha shauku ya kutaka kujua ni nini kipo njiani,lakini kwa taarifa zilizopo chini ya pazia ni kwamba Infinix itakuja na moja ya simu kabambe na huenda ikawa tishio kwa simu zote zenye kupatikana sokoni kwa bei isiyozidi sh. 350,000 huku baadhi ya sifa zikitajwa kupitia tovuti mbalimbali kwa kuusifu zaidi uwezo wa battery yenye mAh6000 kudumu na chaji kwa muda mrefu pamoja na ubora wa resolution yenye kukifanya kioo cha HOT 10 play kioo6.82 HD kuwa ang’avu wakati wote. 


Tembelea https://www.infinixmobility.com/tz/ ili kufahamu mengi zaidi.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger