Tuesday 29 September 2020

Rais Magufuli ateua Mkurugenzi mpya wa TAWIRI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Eblate Ernest Mjingo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI).

Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Mjingo alikuwa Mkuu wa Kitengo cha Tiba ya Wanyamapori na Huduma za Maabara wa TAWIRI, na anachukua nafasi iliyoachwa na Dkt. Simon Mduma ambaye amestaafu.

Uteuzi wa Dkt. Mjingo unaanza leo tarehe 29 Septemba, 2020.


 


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne September 29



















Share:

WAZIRI UMMY ATOA AGIZO KWA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI NCHINI

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto akizungumza na wananchi wa Kata ya Pongwe Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akimnadi mgombea udiwani wa Kata ya Pongwe (CCM) Mbaraka Sadi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika kata ya Pongwe Jijini Tanga
MWENYEKITI wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba akimuombea kura mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati akiwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba wakitembea kwenye maeneo mbalimbali Pongwe wakati wa kampeni ya mgombea ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu
MSANII Kasim Mganga akitumbuiza wakati wa kampeni hizo
Umati Mkubwa wa wananachi wakifuatilia kampeni hizo
Katibu Mwenezi wa CCM wilaya ya Tanga Lupakisyo Kapenge kulia akiwa na wadau mbalimbali wakifuatilia mkutano huo

 

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka wakurugenzi wa Halmashauri kote nchini kuacha kuwapa wanawake mikopo kiduchu ambayo haiwezi kuwasogeza mbele kimaendeleo.

 

Badala yake amewataka wawape mikopo itakayowawezesha kuwasaidia kufanya shughuli zao ambazo zinaweza kubadilisha maisha yao na hivyo kujikwamua kiuchumi wao na jamii zao

 

Ummy ambaye pia ni Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) aliyasema hayo wakati akizungumza na wananch wa Kata ya Pongwe Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa hadhara ambapo alisema katika hili amedhamiri kuhakikisha linafanyiwa kazi.

 

“Ninajua Katika hili ninaongea kama Waziri ninayesimamia Maendeleo ya wanawake ninawataka wakurugenzi kote nchini kuacha kuwapa wanawake mikopo ya laki tano, laki mbili, milioni moja badala yake wawapeni ya milioni 5, 10 na 20 ili muweze kufanya shughuli ambazo zinaweza kubadilisha maisha yenu na sio kuwadanganya na mikopo kiduchu ambayo haiwezi kuwasogeza mbele”Alisema

 

Alisema katika ilani ya uchaguzi ya CCM wamehaidi kwamba endapo watakichagua chama cha Mapinduzi (CCM) na endapo watamchagua wataongeza idadi ya wanawake watakaopata mikopo bila riba ili waweze kufanya shughuli zao na ujasiriamali.

 

“Ninawaomba sana wanawake wa Kata ya Pongwe ninafahamu hapa kwenu kuna vikundi 7 vimepata mikopo lakini vingi havijapata mikopo ninawaomba sana katika hili mniamini nitashirikiana na Diwani tuwafikie wanawake wengi zaidi hivyo ninaomba mnichague suala hili nikalisimamie kikamilifu”Alisema Waziri Ummy.

 

Katika ilani hiyo hawajawashau wafanyabiashara na wajasiramali wadogo wadogo huku akiwaomba wakiamini chama cha Mapinduzi (CCM) wamchague Rais Joh Magufuli na yeye ili waweze kuweka mazingira mazuri zaidi ya kwa wafanyabsiuara wadogo wadogo, wajasiramali wadogo wakiwemo mama ntilie wauza ngenge na vijana wa bodaboda waweze kufanya shughuli zao bila vikwazo.

 

“Lakini pia ninatambua hapa Pongwe kuna matatizo ya upatikanaji wa maji bado maeneo ya Kakindu,Kisimatui na Kilango na hili limeanza kuonekana baada ya maji kupelekwa Muheza hapa kwetu Pongwe upatikani wa maji umekuwa changamoto niwaombe mniamini nitalifanyia kazi”Alisema

 

Ummy alisema kwamba tayari alikwisha kuanza kulifanya kazi suala hilo na Tanga Uwasa tayari wamekwisha kupata fedha za kuboresha mtandao wa maji  ili kuweza kuongeza idadi ya kaya na nyumba ambazo zinapata maji safi na salama ili kuhakikisha maji yanapatikana kwenye eneo hilo kwa muda mrefu.

 

Mwisho.

 

Share:

Monday 28 September 2020

Wakazi 60,000 Babati Kupata Majisafi Na Salama


Jumla ya wakazi 60,000 wa Mji wa Magugu Wilayani Babati Mkoani Manyara wanatarajia kunufaika na huduma ya maji pindi mradi wa maji unaotekelezwa kwa kutumia chanzo cha Mto Kou utakapokamilika.

Hayo yameelezwa Septemba 27, 2020 wakati wa ziara ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga wilayani humo ya kukagua hatua ya utekelezaji wa mradi huo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA), Mhandisi Idd Msuya.

Mara baada ya kupokea taarifa na kujionea hali halisi ya hatua iliyofikiwa ya utekelezwaji wa mradi, Mhandisi Sanga aliielekeza BAWASA kufanya mapitio ya mradi kwenye baadhi ya maeneo ili kuongeza tija.

“Hakikisheni mtandao wa maji unaongezeka ili muweze kuwafikia wananchi wengi zaidi lakini pia wananchi waweze kunufaika kwa Saa 24 kila siku,” alielekeza Mhandisi Sanga.

Aidha, Katibu Mkuu Sanga aliielekeza BAWASA kuhakikisha mradi huo wa Magugu unakamilika kwa wakati na kwamba jitihada zifanyike ili utekelezwaji wake ufanyike bila kusimama.

“Inatakiwa muongeze watendaji zaidi kwa ajili ya kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi ili ukamilike kwa muda uliopangwa; hakuna sababu ya kuchelewesha mradi,” alielekeza Mhandisi Sanga.

Katibu Mkuu Sanga alitembelea eneo la mradi ambapo alikagua ujenzi wa mitambo ya kuchuja maji pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji kwenye Mto Kou.

Mradi wa maji katika mji wa Magugu unatekelezwa na Wizara ya Maji kwa gharama ya Shilingi Milioni 575 kupitia Mamlaka ya Maji Babati kwa lengo la kuongeza hali ya upatikanaji wa maji pamoja na kuboresha ubora wa maji yanayotumika kwa sasa.

Kwa mujibu wa Mhandisi Msuya, mradi unatekelezwa na wataalam wa BAWASA na kwamba ulianza kutekelezwa rasmi Agosti 2020 na unatarajiwa kukamilika Desemba 2020.

Katibu Mkuu Sanga amekamilisha ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya maji Wilayani Babati


Share:

PICHA: Mgombea Urais kupitia CCM Dr Magufuli akizungumza na Wananchi wa IRINGA Mjini leo

 








Share:

KUTANA NA CHUCK FEENEY BILIONEA ALIYEGAWA MALI ZAKE ZOTE KWA WALIMWENGU


Chuck Feeney katikati amekuwa bilionea kwa muda wa miaka 40 iliyopita.
**
Charles "Chuck" Feeney ni bilionea ambaye alikuwa na ndoto za kumaliza mali yake yote akiwa hai, kwa kutoa fedha zake zote kwa mashirika ya hisani.

Mfanyabiashara huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 89 , hatimaye amefikia lengo lake siku chache ziliopita alipotoa dola ,milioni 8,000 kusimamia miradi ya hisani duniani.

Hivi sasa hana nyumba wala gari na ni maarufu kwa kuvalia saa iliyonunuliwa kwa dola 15 pekee.

''Nilikuwa na wazo ambalo halikuondoka katika fikra zangu , kwamba unapaswa kutumia mali yako kuwasaidia watu'', alisema mfanyabiashara huyo. Na kwa kipindi kirefu alichangisha fedha bila kujulikana.

Wakati mwandishi Gerardo Lissardy, kutoka BBC Mundo alipomuuliza 2017 kwanini alikuwa akifanya kuwa siri, alijibu, ''kwa sababu hakuna haja ya kuelezea watu kwanini unafanya hivyo''.

Kulingana na Conor O'Clery, aliyeandika kitabu kuhusu Feeney, anasema kwamba mtu huyo alipatiwa msukumo na kitabu cha 'Mali', kikijulikana, 'The Gospel of Wealth', kilichoandikwa na Andrew Carnegie.

Mishororo kama ''Kufa tajiri ni kufa kwa aibu'', iliwacha kovu katika fikra za Feeney. Alisafiri kote duniani kwa siri , akitafuta njia za kukamilisha kazi yake ndio maana aliitwa jina la Utani James Bond wa hisani.

Je Chuck Feeney ni nani? 

Charles F. Feeney alizaliwa mjini Elizabeth, New Jersey mwaka 1931. Mama yake alifanya kazi kama nesi katika hospitali huku baba yake akiwa wakala wa bima.

Akiwa kijana mdogo alionesha uwezo wake wa kufanya biashara.

Aliuza kadi za krisimamsi mlango hadi mlango akiwa na umri wa miaka 10. Akiwa kijana alisajiliwa katika jeshi na kushiriki katika vita vya Korea.
Chuck Feeney

Alitumia fursa ya mpango wa elimu wa Marekani kwa wakongwe na kuwa mtu wa kwanza wa familia yake kujiunga na chuo cha masomo.

Baada ya kuhitimu katika chuo kikuu cha Cornell University mjini New York , alianza biashara yake akiuza bidhaa kwa wanajeshi wa Marekani waliopo katika kambi barani Ulaya.

Biashara hiyo ilipiga hatua na kuwa maduka yasiotoza ushuru DFS kampuni ya mauzo isiotoza ushuru alioanzisha kwa pamoja na Robert Miller 1960.
Chuck Feeney alitoa fedha ya msaada Australia, Cuba na Ireland

''Mali inakuja na majukumu'' alikuwa akinukuliwa akisema.

''Sikufanya hivyo ili kuthibitisa chochote: Tajiri huyo aliyechangisha dola bilioni nane na kuwachwa na bila kitu.

''Watu wanapaswa kuchukua jukumu kutumia baadhi ya mali yao kuimarisha maisha ya wanadamu wenzao, la sivyo watajenga matatizo makubwa katika vizazi vya siku za baadaye''.

Kwa sasa anaishi katika nyumba ya vyumba viwili katika mji wa San Fransisco na mkewe Helga.

James Bond wa hisani
Mwaka 1982 alianzisha wakfu wa Atlantic Philanthropies Foundation , shirika la kimataifa kusambaza mali kwa miradi ya hisani duniani.

Katika kipindi cha miaka 15 ya kwanza, Feeney kisiri alichangisha fedha, na kumfanya kuitwa James Bond wa hisani, hadi alipojitokeza 1997.
Ufadhili umetajwa kubadili maisha ya wengi

Tangu alipoanzisha wakfu wa Atlatntic Phillanthropies, ametoa karibia dola bilioni nane kama misaada.

Wakfu huo umetangaza kwamba utasitisha operesheni zake siku ya mwisho ya mwaka wa 2020 baada ya lengo la Feeny kuafikiwa,

Filosofia yake ya kutoa wakati unapoishi imewapatia msukumo mabilionea wengi , ikiwemo mwanzilishi wa Microsoft Bill Gates na mwekezaji Warren Buffet.

Feeney hajulikana sana kama matajiri wengine kwasababu ya kutoa michango yake kisiri katika kipindi cha kwanza cha miaka 15 cha kazi yake.

CHANZO- BBC SWAHILI
Share:

SHIRIKA LA TANUA KUZINDUA KAMPENI YA UTALII WA NDANI TANZANIA

Share:

Project Managers (2 positions) at TAHEA

Background Tanzania Home Economics Association (TAHEA) is a national professional organization of nutritionist, home economics, agriculturists and other related social science professions. TAHEA envisions ‘A democratic society with better livingConditions’; with the Mission to improve the socio-economic conditions of the society through advocacy and capacity building on agriculture, food and nutrition, health and environment in […]

The post Project Managers (2 positions) at TAHEA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Legal Officer Job Opportunity at TAZARA, Dar es Salaam

Legal Officer Job Opportunity at TAZARA, Dar es Salaam The Tanzania Zambia Railway Authority, popularly known as TAZARA, is a bi-national railway linking the Southern Africa Regional transport network to Eastern Africa’s seaport of Dar es Salaam, offering both freight and passenger transportation services between and within Tanzania and Zambia.

The post Legal Officer Job Opportunity at TAZARA, Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Livelihood Officer/Agronomist at Umwema Group Morogoro Trust Fund

Livelihood Officer/Agronomist at Umwema Group Morogoro Trust Fund September, 2020 UMWEMA MOROGORO (Umwema Group Morogoro Trust Fund) is a registered non- governmental organization with its Head Quarter in Morogoro Municipal. It is a non-profit making organization incorporated under NGO act of Tanzania.UMWEMA has partened with Save the Children International (SCI) in Tanzania, to implement USAID […]

The post Livelihood Officer/Agronomist at Umwema Group Morogoro Trust Fund appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MUHAS-Late applicants selected for Postgraduate degree programmes 2020-2021

MUHAS-Late applicants selected for Postgraduate degree programmes 2020-2021 MUHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES DIRECTORATE OF POSTGRADUATE STUDIES LATE APPLICANTS SELECTED FOR POSTGRADUATE DEGREE PROGRAMMES 2020-2021 DIRECTOR, POSTGRADUATE STUDIES, Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS) has provided the List of Late applicants selected for Postgraduate degree programmes for the academic year 2020/2021.   […]

The post MUHAS-Late applicants selected for Postgraduate degree programmes 2020-2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Muhas: Important Announcement To All Undergraduate Degree And Diploma Applicants.

IMPORTANT ANNOUNCEMENT TO ALL UNDERGRADUATE DEGREE AND DIPLOMA APPLICANTS This is to inform all applicants for undergraduate degree and diploma programmes that the window for the first round of application is closed. Results will be announced on the 12th October, 2020 through respective students accounts (OAS), SMS and the University Website which is www.muhas.ac.tz Applicants […]

The post Muhas: Important Announcement To All Undergraduate Degree And Diploma Applicants. appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Lodge Manager at Evolve People Solutions

Position Description: Lodge Manager   Purpose of Position: Our client is looking to hire a Lodge Manager who shall be responsible for maintaining the smooth operation of their remote Lodge complex. In addition to that the successful incumbent shall provide leadership to staff, maintain lodge facilities and provide a level of hospitality which meets the […]

The post Lodge Manager at Evolve People Solutions appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Researchers at SUA

2 Job Opportunities at SUA, Researchers   Researchers (2 Posts)  Applicants are invited from qualified Tanzanians to fill vacant positions at SUA- APOPO RODENT RESEARCH PROJECT. The application letters should indicate names and addresses of THREE REFEREES, together with CERTIFIED   COPIES   OF   ACADEMIC   CERTIFICATES,   furthermore   the applicant must submit a copy of BIRTH CERTIFICATE, a signed […]

The post Researchers at SUA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tanzania Railways Corporation (TRC) Notice About 50,000 Fake Jobs Advertisement | MUST READ

  Overview The Tanzania Railways Corporation (TRC) is a state-owned enterprise that runs one of Tanzania’s two main railway networks. When the East African Railways and Harbours Corporation was dissolved in 1977 and its assets divided between Kenya, Tanzania and Uganda, TRC was formed to take over its operations in Tanzania. In 1997 the inland […]

The post Tanzania Railways Corporation (TRC) Notice About 50,000 Fake Jobs Advertisement | MUST READ appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Quality Assurance Manager at TP Label Limited

Quality Assurance Manager at TP Label Limited September, 2020 TP Label Limited is one of the fastest-growing label companies in the region in the following market segments: Beverage and Spirits. We are seeking to recruit one position of a Quality Assurance Manager to be based in Dar es Salaam. Job Overview: To manage quality systems […]

The post Quality Assurance Manager at TP Label Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MGOMBEA URAIS KUPITIA ADA TADEA JOHN SHIBUDA AZINDUA RASMI KAMPENI ZA UCHAGUZI..APEWA KAMPANI NA MAMA YAKE


John Shibuda akiteta jambo na mama yake mzazi kwenye uzinduzi wa kampeni za chama cha ADA TADEA kitaifa wilayani Maswa

Mgombea Urais kwa tiketi ya (ADA TADEA) Mh John Shibuda akihutubia wakazi wa Maswa Septemba 27 wakati akizindua kampeni zake kitaifa 

 Na Mwandishi wa Shinyanga Press Club blog
Mgombea Urais kupitia Chama cha ADA TADEA, John Shibuda amesema chama hicho hakina uadui na chama chochote cha kisiasa nchini badala yake maadui wakubwa wa chama cha ADA TADEA ni Ujinga, Umaskini na Maradhi huku vita kuu ya chama hicho ni kuhakikisha utawala bora unapatikana. 

Shibuda amebainisha hayo Septemba 27, 2020 wakati akizindua kampeni za chama hicho kitaifa wilayani Maswa Mkoa waSimiyu ambapo amesema kuwa suala la Umaskini,Ujinga na Maradhi bado ni tatizo kubwa nchini.

“Sisi kama chama cha ADA TADEA hatuna tatizo lolote na vyama vingine vya siasa bali tatizo letu kubwa ni mapambano dhidi ya madhira watatu ambao ni ujinga,maradhi na Umaskini na vita ya chama chetu ni kuhakikisha kuwa utawala bora unapatikana”

Amesema kimejipanga kuondoa maadui wakubwa wa ustawi na maendeleo ya jamii ya watanzania ambapo amewaomba watanzania kumpigia kura ili awezea kuongoza dola.

Katika hatua nyingine Shibuda ametaja vipaumbele vinnne vya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu ikiwemo suala la utawala wa sheria wakati wote kwa wananchi na watendaji wa umma sambamba na siasa safi na atawajibika kwa uwazi,ushirikishwaji, uwajibikaji, ufanisi na uadilifu.

Mgombea Ubunge Jimbo la Maswa Magharibi kupitia chama hicho, Lydia Mbuke Bendera amewaomba wakazi wa Maswa kumpigia kura ili aweze kutatua kero ,changamoto na adha mbalimbali ambazo zimeendelea kuwepo ndani ya jimbo hilo kwa kipindi cha miaka mingi .

Amesema kuwa iwapo atachaguliwa suala la kwanza kushughulikia ni changamoto ya kina mama kusafiri umbali mrefu,kero ya miundombinu pamoja na kumtua ndoo mama kichwani ikiwa ni kusogezwa huduma karibu na wananchi.
John Shibuda akiwapungia mkono wananchi baada ya kuwasili uwanjani wilayani Maswa
Shibuda akizungumza na wananchi wa wilaya ya Maswa katika uzinduzi wa kampeni za chama cha ADA TADEA
Shibuda akiendelea kuinadi sera na ilani ya chama chake kwa wananchi wa wilaya ya Maswa kwenye uwanja wa Majengo
Mama mzazi wa John Shibuda akimuombea kura mwanaye John Shibuda kwa wananchi wa mkoa wa Simiyu
Wananchi wa eneo la Majengo wilayani Maswa mkoa wa Simiyu wakifuatilia kampeni za chama cha ADA TADEA zilizozinduliwa katika eneo hilo
Wananchi wakifuatilia kampeni za chama cha ADA TADEA
Mgombea Ubunge Jimbo la Maswa Magharibi kupitia ADA TADEA, Lydia Mbuke Bendera akiomba kura kwa wananchi
Mgombea Ubunge Jimbo la Maswa Mashariki kupitia chama cha ADA TADEA, Mipawa Ndilizu akiomba kura kwa wananchi wakati wa mkutano huo wa kampeni
Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama cha ADA TADEA akiomba kura kwa wananchi waweze kukichagua chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, mwaka huu
Wananchi wa Jimbo la Maswa Magharibi wakimsikiliza mgombea ubunge wa jimbo hilo, Lydia Bendera
Wananchi wa jimbo la Maswa Magharibi mkoani Simiyu wakiendelea kufuatilia uzinduzi wa kampeni za chama cha ADA TADEA katika uwanja wa Majengo wilayani Maswa

Via Shinyanga Press Club Blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger