Sunday 9 August 2020
Saturday 8 August 2020
Assistant Lecturers at Mkwawa University College of Education (MUCE)
Mkwawa University College of Education (MUCE), a Constituent College of the University of Dar es Salaam invites job applications from suitably qualified candidates to fill the following vacant posts below… ASSISTANT LECTURERS (2 POSTS) Areas of Specialization; Geoinformatics/ Statistics/ Geology/ Survey/ Evolution and Genetics, who is willing to serve in department of Geography and area of […]
The post Assistant Lecturers at Mkwawa University College of Education (MUCE) appeared first on Udahiliportal.com.
Accountant at ABC Capital School Nursery and Primary
Job Overview ABC PRIMARY AND NURSERY SCHOOL Is looking for the competent accountant and assistant accountant with the following qualifications: ACCOUNTANT Bachelor degree in accounting or above Certificate school in advanced level secondary Certificate school in ordinary level secondary Knowledge in tally accounting system Fluency in speaking English SEND YOUR APPLICATION TO: DIRECTOR, ABC […]
The post Accountant at ABC Capital School Nursery and Primary appeared first on Udahiliportal.com.
Digital Finance Officer at Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania
Introduction: The Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania (SCCULT) is the umbrella organization for SACCOS in Tanzania mainland. It was established in 1992 under Cooperative Act No. 15 of the year 1991 and was given registration no. 5480. The Union was established to promote and encourage thriftiness of SACCO’s members, foster and promote […]
The post Digital Finance Officer at Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.
Simamieni Maadili Wakati Wa Kumuhudumia Mgonjwa – Mganga Mkuu Wa Serikali
Majambazi Wawili Wauawa Mkoani Pwani ,polisi Yakamata Silaha Na Risasi
JESHI la polisi mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limefanya operesheni maalum ya kudhibiti makosa ya jinai na kufanikiwa kuwaua majambazi wawili na kukamata silaha zao pump action na risasi kumi .
Jeshi la polisi lilipata taarifa za kiitelijensia kuwa kuna majambazi wamepanga kufanya tukio la unyang’anyi wa kutumia silaha katika moja ya viwanda vilivyopo eneo la Zegereni ,Mlandizi.
Agost 7 mwaka huu ,jeshi hilo liliweka mtego na kufanikiwa kuwaona majambazi hao wakiwa watatu kwenye pikipik moja wakielekea eneo la viwanda.
Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Pwani ,Wankyo Nyigesa ,akithibitisha juu ya tukio hilo ameeleza, askari walipowasimamisha hawakusimama na jitihada za kuwafukuza zilianza mara moja ,askari walipowakaribia watu wawili waliruka kwenye pikpik na kuanza kukimbia huku wakirusha risasi kwa askari .
Walianza kurushiana risasi na majambazi hao ambapo walijeruhiwa na baadae walifariki wakiwa njiani wakipelekwa hospital.
Wankyo ameeleza,jambazi mmoja aliyekuwa dereva wa pikpiki amefanikiwa kukimbia na majambazi waliouawa ,miili yao imehifadhiwa hospital ya Tumbi .
Wakati huo huo jeshi hilo linawashikilia watu watatu waliohusika na wizi wa hydrolic pump ya gari mtambo wa kuchimbia mchanga yenye namba za usajili T.525 DFN aina ya Komasu yenye thamani ya milioni 15 Mali ya kampuni ya Yong Da comp.ltd ya Masaki Dar es salaam.
Wankyo amewataja watu hao kuwa ni Hamis Zaitun Janja 40, Saimon Chache 37 na Evance Kimaro miaka 28 ambao wamekiri kuhusika na wizi huo .
Ujenzi holela unakwamisha juhudi za jeshi la zimamoto na uokoaji.
Nyongo azitaka benki kushirikiana na wizara katikakukuza uchuumi wa madin
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo azitaka Benki zilizopo nchini kushirikiana na Wizara ya Madini katika kuwawezesha kimitaji wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini ili kuwawezesha kuwekeza katika shughuli zao.
Naibu Waziri Nyongo aliyasema hayo tarehe 6 Agosti, 2020 wakati akifungua mafunzo yaliyoandaliwa hususani kwa ajili ya wafanyakazi wa benki ya CRDB yaliyofanyika katika hoteli na NAShera jijini Dodoma.
Alisema mafunzo hayo yatawasaidia wataalamu hao wa benki kuwa na uelewa wa namna shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa ujumla zinavyoendeshwa.
“Biashara ya Madini ni kama biashara nyingine hivyo msisite kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo pindi wanapohitaji kwa ajili ya kuwekeza katika uchimbaji na biashara ya madini”. Nyongo alikazia.
Akizungumzia dhumuni la kutoa mafunzo hayo kwa taasisi za benki nchini, ambapo awali mafunzo kama hayo yalitolewa kwa watumishi wa benki ya NMB, Nyongo alisema hatua hiyo ni utekelezaji wa sera ya Madini ya Mwaka 2009 inayoitaka Serikali kuwasaidia wachimbaji wadogo wa Madini katika kutatua changamoto za mitaji zinazowakabili na kuwafanya wawekeze kwa tija.
Wizara ikishirikiana na Tume ya Madini imeona njia bora ya kuwawezesha wachimbaji hao ni kuwaunganisha na taasisi muhimu za fedha ili kutoa elimu muhimu kwa taasisi hizo zitakazowasaidia wakati wa kuhakiki taarifa za wachimbaji na wafanyabiashara wa madini pindi watakapowasilisha taarifa zao benki kwa ajili ya kuomba mikopo.
Akizungumzia matarajio ya wizara mara baada ya elimu kutolewa, Nyongo alisema benki zilizopo nchini kuwawezesha kwa kuwapa mikopo na elimu ya biashara wachimbaji wa Madini hasa wachimbaji wadogo.
Vilevile Waziri Nyongo amesema, mafunzo hayo yataendelea kutolewa kwa taasisi nyingine za fedha nchini ili kuwezesha taasisi hizo kujifungamanisha kwenye uchumi wa Madini ambayo ni sekta inayoongoza kwa ukuaji nchini.
Akihitimisha hotuba yake ya ufunguzi, Nyongo alisisitiza kuwa elimu ya biashara ya madini itaendelea kutolewa kwa wataalamu wa benki nchini ili kuwajengea uwezo wakopeshaji kutambua fursa zilizopo kwenye sekta ya madini na kuwataka kuajiri wataalamu wenye uelewa na masuala ya madini watakaoweza kuchambua michanganuo ya mikopo ya uchimbaji wa madini vile inavyostahili.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya alisema, sekta ya madini ni sekta muhimu katika uchumi wa nchi ambayo inahitaji mitaji mikubwa katika uwekezaji wake hivyo ni muhimu kwa watoa huduma za mikopo kuwa na uelewa wa sheria na kanuni za madini.
“Sekta ya madini ni biashara kama biashara nyingine inahitaji mitaji mikubwa hivyo ninyi watu wa benki inabidi mjue vizuri suala la leseni za madini, uhai wa leseni hizo na sheria na kanuni zinazoongoza sekta hii muhimu”.
Pamoja na hayo, Prof. Manya alisema mafunzo hayo yataondoa kusitasita kutoa mikopo kwa wachimbaji wa madini mara baada ya wataalamu wa mikopo kuwa na uelewa mpana kuhusu mnyororo wa madini unaohusu wachimbaji, wauzaji, vifaa vya uchimbaji na uchakataji wa madini na watoa huduma wengine katika sekta hiyo.
Kwa upande wake, Meneja wa Dawati maalum kwa wateja wakubwa kutoka benki ya CRDB, Frederick Mwamyalla amekirii kuwa semina hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwao na kuwawezesha kuona fursa zilizopo kwenye sekta ya madini zitakazowasaidia kuongeza mchango wao katika kusukuma mbele ukuaji wa sekta ya madini ili iweze kuchangia vilivyo katika miradi ya maendeleo.
Alisema ni muhimu kwao kama taasisi ya kifedha kuongeza nguvu na kuboresha huduma zao ili kuhakikisha mchango wa benki hiyo unaongezeka kwa kuwawezesha wachimbaji wadogo na hivyo kuinua vipato vyao pamoja na kuongeza mchango wa sekta kwenye pato la taifa.