Sunday 9 August 2020

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili August 9















Share:

Saturday 8 August 2020

Assistant Lecturers at Mkwawa University College of Education (MUCE)

Mkwawa University College of Education (MUCE), a Constituent College of the University of Dar es Salaam invites job applications from suitably qualified candidates to fill the following vacant posts below… ASSISTANT LECTURERS (2 POSTS) Areas of Specialization; Geoinformatics/ Statistics/ Geology/ Survey/ Evolution and Genetics, who is willing to serve in department of Geography and area of […]

The post Assistant Lecturers at Mkwawa University College of Education (MUCE) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Accountant at ABC Capital School Nursery and Primary

Job Overview ABC PRIMARY AND NURSERY SCHOOL Is looking for the competent accountant and assistant accountant with the following qualifications: ACCOUNTANT Bachelor degree in accounting or above Certificate school in advanced level secondary Certificate school in ordinary level secondary Knowledge in tally accounting system Fluency in speaking English   SEND YOUR APPLICATION TO: DIRECTOR, ABC […]

The post Accountant at ABC Capital School Nursery and Primary appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Digital Finance Officer at Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania

Introduction: The Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania (SCCULT) is the umbrella organization for SACCOS in Tanzania mainland. It was established in 1992 under Cooperative Act No. 15 of the year 1991 and was given registration no. 5480. The Union was established to promote and encourage thriftiness of SACCO’s members, foster and promote […]

The post Digital Finance Officer at Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WAZIRI KILIMO AZINDUA MFUMO WA KUHAKIKI MBEGU NA PEMBEJEO, 'T-HAKIKI'

Share:

LIVE : Tundu Lissu Akichukua Fomu Ofisi Za NEC

LIVE : Tundu Lissu Akichukua Fomu Ofisi Za NEC


Share:

LIVE Dodoma: Uchaguzi Wa Wabunge 10 Wa UVCCM

LIVE  Dodoma: Uchaguzi Wa Wabunge 10 Wa UVCCM


Share:

Simamieni Maadili Wakati Wa Kumuhudumia Mgonjwa – Mganga Mkuu Wa Serikali

Na WAMJW- Bombo, Tanga
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi ameagiza Watumishi wa Afya kusimamia maadili na kujishusha pindi wanapotoa huduma, ili kuondoa malalamiko yanayotolewa na wananchi wanaokuja kupata huduma.

Prof. Makubi ametoa rai hiyo wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo, ikiwa ni sehemu ya maboresho ya huduma za Afya kwa wananchi.

"Nitoe wito kwa Watumishi wote katika maeneo ya kutoa huduma hapa Hospitali, turudi katika maadili yetu na kujishusha wakati wa kumuhudumia mgonjwa, huduma kwa wagonjwa ianzie  getini mgonjwa anapoingia mpaka anapotoka" alisema Prof. Makubi.

Kwa upande mwingine, Prof. Makubi ametoa wito kwa Watumishi wote wanaotoa huduma za afya kudumisha umoja na ushirikiano baina yao katika maeneo ya kazi, jambo litalosaidia kuboresha huduma za Afya kwa wananchi wenye uhitaji.

"Niwaombe sana kada zote katika maeneo ya kutoa huduma za Afya  muungane muwe kitu kimoja baina yenu, ili kuboresha utoaji huduma, wengine wakiona watafuata mfano wenu " alisema Prof. Makubi.

Aidha, Prof. Makubi kwa kiasi kikubwa ameridhishwa na hali ya utoaji huduma katika kitengo cha dharura na mapokezi, huku akisisitiza ni vyema Idara nyingine kuiga mfano mzuri ili kuboresha huduma za Afya kwa wananchi.

Mbali na hayo, Prof. Makubi ameeleza kwa Watoa huduma wote kutoa mrejesho kwa wagonjwa pindi wanapokuja kupata huduma ili kuondoa mkanganyiko unaoweza kujitokeza bila sababu ya msingi.

Prof Makubi ambaye pia alipata nafasi ya kuwaona wagonjwa waliolazwa na kushaurina na Madaktari na wauguzi katika kutoa huduma za tiba, alibaini changamoto kwa wagonjwa kuchelewa kuona wanapolazwa ambapo ameagiza muda ya wagonjwa kuonwa katika vituo afya uwe mfupi kwa kupunguza ucheleweshaji katika hatua zote anazopita mgonjwa.

Naye, Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe  ametoa wito kwa viongozi kujenga tabia ya kusikiliza na kutatua kero za Watumishi wao wanaowaongoza, jambo litalokuwa chachu ya kutoa huduma bora kwa wananchi mwenye uhitaji.

Hata hivyo, Dkt. Grace Maghembe amesisitiza kuwa, ni muhimu kwa watoa huduma za Afya kufanya kazi kwa kuzingatia taratibu na miongozo inavyoelekeza, ili kuboresha huduma kwa wagonjwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa uhakika ubora kutoka Wizara ya Afya Dkt. Eliud Eliakim, amesisitiza kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa kuzingatia ubora wa huduma na kufuata miongozo ya kujikinga wakati wa kuwahudumia wagonjwa.


Share:

Majambazi Wawili Wauawa Mkoani Pwani ,polisi Yakamata Silaha Na Risasi

Na MWAMVUA MWINYI,PWANI
JESHI la polisi mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limefanya operesheni maalum ya kudhibiti makosa ya jinai na kufanikiwa kuwaua majambazi wawili na kukamata silaha zao pump action na risasi kumi .

Jeshi la polisi lilipata taarifa za kiitelijensia kuwa kuna majambazi wamepanga kufanya tukio la unyang’anyi wa kutumia silaha katika moja ya viwanda vilivyopo eneo la Zegereni ,Mlandizi.

Agost 7 mwaka huu ,jeshi hilo liliweka mtego na kufanikiwa kuwaona majambazi hao wakiwa watatu kwenye pikipik moja wakielekea eneo la viwanda.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Pwani ,Wankyo Nyigesa ,akithibitisha juu ya tukio hilo ameeleza, askari walipowasimamisha hawakusimama na jitihada za kuwafukuza zilianza mara moja ,askari walipowakaribia watu wawili waliruka kwenye pikpik na kuanza kukimbia huku wakirusha  risasi kwa askari .

Walianza kurushiana risasi na majambazi hao ambapo walijeruhiwa na baadae walifariki wakiwa njiani wakipelekwa hospital.

Wankyo ameeleza,jambazi mmoja aliyekuwa dereva wa pikpiki amefanikiwa kukimbia na majambazi waliouawa ,miili yao imehifadhiwa hospital ya Tumbi .

Wakati huo huo jeshi hilo linawashikilia watu watatu waliohusika na wizi wa hydrolic pump ya gari mtambo wa kuchimbia mchanga yenye namba za usajili T.525 DFN aina ya Komasu yenye thamani ya milioni 15 Mali ya kampuni ya Yong Da comp.ltd ya Masaki Dar es salaam. 

Wankyo amewataja watu hao kuwa ni Hamis Zaitun Janja 40, Saimon Chache 37 na Evance Kimaro miaka 28 ambao wamekiri kuhusika na wizi huo .


Share:

Ujenzi holela unakwamisha juhudi za jeshi la zimamoto na uokoaji.

Na Samirah Yusuph
Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Simiyu limeeza kuwa shughuli za ujenzi wa makazi ya kuishi bila mpangilio mzuri unakwamisha utendaji kazi wake.

Changamoto hiyo imekuwa ikiwafanya askari wa kupambana na Moto, kushindwa kufika kwa urahisi katika eneo linalokusudiwa kutokana na mitaa mingi hasa katika maeneo ya mijini kutokuwa na mpangilio mzuri wa ujenzi.

Akiitaja changamoto hiyo kuwa Ni moja ya sababu ya wao kupewa lawama nyingi yatokeapo majanga ya moto, akiwa katika viwanja vya naenane Nyakabindi Wilayani Bariadi.

Kamishna wa utawala na fedha wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mbaraka Sultan Semwanza alisema, licha ya kuwa wamefanya mwasiliano na mamlaka hisika Bado utatuzi was changamoto hiyo Ni mgumu.

"Tunamagari mengi na ya kisasa pamoja na vifaa vya kuzima Moto na uokozi lakini changamoto Ni tunapo fika huko mtaani Shida inakuwa Ni kutafuta wapi gari lipite ili huduma ipatikane," alieleza

Alisema kuwa wamejipambanua kutoa huduma kwa wateja wenye uhitaji, na kuwataka wananchi watoe taarifa mapema waonapo majanga ya moto ili jeshi Hilo liweze kufanya kazi yake kwa usahihi.

"Sisi kazi yetu Ni kuhudumia wananchi hivyo tunahitaji ushirikiano wao lakini pia wanafurusa kupitia sisi wakijifunza namna ya kukabiliana na majanga ya moto wa awali wafikapo katika maonyesho haya" aliongeza.

Akionyesha namna ya kutumia vifaa vya kuzima Moto wa awali station sagent katika Banda la nane nane Nyakabindi Wilayani Bariadi Mohamed Mkesa alisema, Ni wajibu wa Kila mmoja kuelewa namna ya kukabiliana na Moto wa awali.

Mwisho.


Share:

Nyongo azitaka benki kushirikiana na wizara katikakukuza uchuumi wa madin

Nuru Mwasampeta na Steve Nyamiti,WM
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo azitaka Benki zilizopo nchini kushirikiana na Wizara ya Madini katika kuwawezesha kimitaji wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini ili kuwawezesha kuwekeza katika shughuli zao.

Naibu Waziri Nyongo aliyasema hayo tarehe 6 Agosti, 2020 wakati akifungua mafunzo yaliyoandaliwa hususani kwa ajili ya  wafanyakazi wa benki ya CRDB yaliyofanyika katika hoteli na NAShera jijini Dodoma.

Alisema mafunzo hayo yatawasaidia wataalamu hao wa benki  kuwa na  uelewa wa namna shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa ujumla zinavyoendeshwa.

“Biashara ya Madini ni kama biashara nyingine hivyo msisite kutoa mikopo kwa wachimbaji wadogo pindi wanapohitaji kwa ajili ya kuwekeza katika uchimbaji  na biashara ya madini”. Nyongo alikazia. 

Akizungumzia dhumuni la kutoa mafunzo hayo kwa taasisi za benki nchini, ambapo awali mafunzo kama hayo yalitolewa kwa watumishi wa benki ya NMB, Nyongo alisema hatua hiyo  ni utekelezaji wa sera ya Madini ya Mwaka 2009 inayoitaka Serikali kuwasaidia wachimbaji wadogo wa Madini katika kutatua changamoto za mitaji zinazowakabili na kuwafanya wawekeze kwa tija.

Wizara ikishirikiana na Tume ya Madini imeona njia bora ya kuwawezesha wachimbaji hao ni kuwaunganisha na taasisi muhimu za fedha ili kutoa elimu muhimu kwa taasisi hizo zitakazowasaidia wakati wa kuhakiki taarifa za wachimbaji na wafanyabiashara wa madini pindi watakapowasilisha taarifa zao benki kwa ajili ya kuomba mikopo.

Akizungumzia matarajio ya wizara mara baada ya elimu kutolewa, Nyongo alisema benki zilizopo nchini kuwawezesha kwa kuwapa mikopo na elimu ya biashara wachimbaji wa Madini hasa wachimbaji wadogo.

Vilevile Waziri Nyongo amesema, mafunzo hayo yataendelea kutolewa kwa taasisi nyingine za fedha nchini ili kuwezesha taasisi hizo kujifungamanisha kwenye  uchumi wa Madini ambayo ni sekta inayoongoza kwa ukuaji nchini.

Akihitimisha hotuba yake ya ufunguzi, Nyongo alisisitiza kuwa elimu ya biashara ya madini itaendelea kutolewa kwa wataalamu wa benki nchini ili kuwajengea uwezo wakopeshaji kutambua fursa zilizopo kwenye sekta ya madini na kuwataka kuajiri wataalamu wenye uelewa na masuala ya madini watakaoweza kuchambua michanganuo ya mikopo ya uchimbaji wa madini vile inavyostahili.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Profesa Shukrani Manya alisema, sekta ya madini ni sekta muhimu katika uchumi wa nchi ambayo inahitaji mitaji mikubwa katika uwekezaji wake hivyo ni muhimu kwa watoa huduma za mikopo kuwa na uelewa wa sheria na kanuni za madini.

“Sekta ya madini ni biashara kama biashara nyingine inahitaji mitaji mikubwa hivyo ninyi watu wa benki inabidi mjue vizuri suala la leseni za madini, uhai wa leseni hizo na sheria na kanuni zinazoongoza sekta hii muhimu”.

Pamoja na hayo, Prof. Manya alisema mafunzo hayo yataondoa kusitasita kutoa mikopo kwa wachimbaji wa madini mara baada ya wataalamu wa mikopo kuwa na uelewa mpana kuhusu mnyororo wa madini unaohusu wachimbaji, wauzaji, vifaa vya uchimbaji na uchakataji wa madini na watoa huduma wengine katika sekta hiyo.

Kwa upande wake, Meneja wa Dawati maalum kwa wateja wakubwa kutoka benki ya CRDB, Frederick Mwamyalla amekirii kuwa semina hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwao na kuwawezesha kuona fursa zilizopo kwenye sekta ya madini zitakazowasaidia kuongeza mchango wao katika kusukuma mbele ukuaji wa sekta ya madini ili iweze kuchangia vilivyo katika miradi ya maendeleo.

Alisema ni muhimu kwao kama taasisi ya kifedha kuongeza nguvu na kuboresha huduma zao ili kuhakikisha mchango wa benki hiyo unaongezeka kwa kuwawezesha wachimbaji wadogo na hivyo kuinua vipato vyao pamoja na kuongeza mchango wa sekta kwenye pato la taifa.


Share:

Waliotafuna fedha za Babati Saccos na kuingia mtini,wahitajika Takukuru Manyara Jumatatu.

Na John Walter-Babati
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Manyara inamshikilia Yuda Sendeu kwa tuhuma za kuchukua kisha kukataa kurejesha fedha za Babati Saccos kiasi cha shilingi milioni 44,726,000.

Mkuu wa Takukuru mkoa wa Manyara Holle Makungu ameeleza kuwa mwaka 2010, Sendeu alichukua shilingi milioni 35,000,000 kama mkopo ambapo alitakiwa kuzirejesha fedha hizo pamoja na riba ya shilingi milioni 44,726,000 katika kipindi cha miezi 24.

Uchunguzi uliofanywa na Takukuru mkoani hapa unaonyesha kuwa, Sendeu alifanya makubaliano ya kihalifu na baadhi ya wanachama waliochukua fedha katika Saccos hiyo kutokurejesha ili haki za wanachama waaminifu wa Saccos hiyo ziweze kupotea.

Makungu amesema, hadi wanachama waaminifu wa Saccos hiyo ya Babati wanawasilisha malalamiko ya dhuluma hiyo katika ofisi za Takukuru, Sendeu bila kustahili amekaa na fedha hizo kwa miaka kumi sasa.

Makungu ametoa rai kwa wanachama wote wa Babati Saccos ambao wamechukua mkopo na muda wa kurejesha umeshapita, kufika kwa hiari yao ofisi za Takukuru zilizopo mtaa wa Miyomboni mjini Babati siku ya Jumatatu Agosti 10,2020 ili wapewe hesabu zao waweze kurejesha na wale watakaokaidi hatua kali dhidi yao zitachukuliwa kuanzia agosti 12,2020.


Share:

SADC Ngazi Ya Makatibu Wakuu Wajadili, Kuboresha Rasimu Za Nyaraka Za Kisera Na Kimkakati

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ngazi ya Makatibu Wakuu wamekutana na kujadili rasimu ya mpango mkakati elekezi mpya wa maendeleo wa kanda (2020 - 2030) pamoja na rasimu ya dira ya SADC (2020 - 2050) kwa njia ya (Video Conference) jijini Dar es Salaam.

Akiongea mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo, Mwenyekiti wa mkutano ambae ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Brigedia Jenerali, Balozi Wilbert Ibuge amesema kuwa lengo la mkutano huo lilikuwa ni kuangalia mambo mawili makubwa ambayo ni dhima ya SADC kuanzia sasa 2020 hadi 2050 pamoja na mpango mkakati wa SADC kuanzia mwaka 2020 - 2030 kwa sababu mpango mkakati wa SADC uliokuwa unatumika tangu mwaka 1992 umeisha muda wake.  

"Nyaraka hizi mbili ni za muhimu sana kwa sababu hadi sasa hivi toka SADC ilipoanzishwa 1992 imefanya mambo makubwa lakini sasa ule mpango mkakati wake uliokuwa unatumika tangu mwaka 2010 na ambao ulihuishwa mwaka 2015 ukafika hadi 2020 umeisha muda wake hivyo ilikuwa ni muhimu kuandaa rasimu ya nyaraka hizi muhimu," Amesema Balozi Ibuge.

Ameongeza kuwa, rasimu za nyaraka hizo mbili zitawasilishwa kwenye mkutano wa 40 wa Wakuu wa nchi wanachama wa SADC na Serikali unaotegemewa kufanyika tarehe 17 Mwezi Agosti 2020 kwa njia ya mtandao.

Mpango Mkakati wa SADC ni mpango wa maendeleo ya kanda uliopitishwa na Mkutano wa wakuu wa nchi na serikali wa SADC uliofanyika mwaka 2003 jijini Dar es Salaam na ulianza kutekelezwa rasmi mwaka 2005 kwa kipindi cha miaka 15 (2005  - 2020). Aidha, mpango huo una vipaombele vinne ambavyo ni maendeleo ya viwanda na mtangamano wa soko, miundombinu bora, amani na usalama, pamoja na programu maalum.

"Dira ya SADC 2020 - 2050 inatoa taswira ya Jumuiya kwa miaka 30 ijayo ambapo msingi wake ni amani, ulinzi, utulivu na utawala bora, uchumi wa kati unaoendeshwa na sekta ya viwanda na wanajumuiya wenye hali bora ya maisha," Amesema Balozi Ibuge.

Hivyo dira ya SADC 2050 ni muhimu kwa maendeleo ya Ukanda wa Kusini mwa Afrika hususan katika kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia 2030 na ajenda ya Umoja wa Afrika ya Mwaka 2063.

Katika tukio jingine, Brigedia Jenerali, Balozi Wilbert Ibuge amekutana na kufanya amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) nchini Tanzania, Bw. Antonio Canhandula katika ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Balozi Wilbert Ibuge amesema kuwa UNHCR imekuwa na mchango mkubwa sana unaohusisha kulinda haki za wakimbizi lakini pia kuwarejesha wakimbizi nchini mwao.

Pamoja na mambo mengine, mazungumzo yalilenga kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) kwa ujumla.



Share:

Wasimamizi Wasaidizi Wa Uchaguzi Nzega Mjini Watakiwa Kuepuka Ushabiki

NA TIGANYA VINCENT
MSIMAMIZI wa Uchaguzi wa Jimbo la Nzega Mjini Philemon Magesa amewataka Wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata kuepuka ushabaki  wa aina yoyote wa kisiasa katika utekelezaji wa majukumu yao ili kutosababisha vurugu wakati zoezi la uchaguzi mkuu ujao.

Alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua mafunzo ya Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi Mkuu ujao kutoka Kata 20 za Halmashauri hiyo.

Magesa alisema  ili Wasimamizi wasaidizi wawe salama katika zoezi hilo ni vema wakazingatia Katiba , Sheria na Kanuni zinasimamia zoezi zima la uchaguzi.

Alisema hali hiyo itasaidia kuufanya uchaguzi kuwa mzuri, wenye ufanisi na hivyo kuondoa kabisa malalamiko au vurugu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.

Aidha Magesa aliongeza kuwa katika utekelezaji wa majukumu yao ni muhimu wakavishirikisha vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi katika masuala ambayo wanastahili kushirikishwa.

Naye Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Glays Barthy walioteuliwa na Ttume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) ambao ni wanachama wa vyama vya siasa kuhakikisha wanajitoa katika vyama vyao ili kuweza kusimamizia zoezi kwa umakini.

Aliwataka wasimamizi wasadizi hao kuwa makini na watu wa karibu nao kwa kujiepusha kutoa maoni ambayo yanaweza kusababisha uvunjifu wa sheria za uchaguzi na kanuni zake.

“Muwe makini na ma group mnayo socialize kwa kuepuka kutoa maoni ambayo nanaweza kusababisha kuonekana unashabikia upande fulani na kusababisha vurugu” alionya.

Alisema katika kipindi chote cha zoezi la uchaguzi wanapaswa kujizuia kupenda kujadiliana na makundi mbalimbali nyakati zote za shughuli za uchaguzi.

“Tunajua baadhi yenu mna kazi za vyama vya siasa …baada ya kiapo hiki mnatakiwa kujitoa kabisa kuzungumzia mambo ya vyama vyenu ili muweze kuwatendea haki hata wote…na wale wenye ushabiki wa ndani ni vema wakaauacha ili waweze kutekeza majukumu yao kwa mujibu Katiba, Sheria na kanuni zinazosimamia uchaguzi” alisisitiza.

MWISHO


Share:

Serikali Yabuni Mbinu Ya Kubaini Viuatilifu Feki-Waziri Hasunga

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu
Licha ya kwamba Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli kuendelea kuimarisha sekta ya kilimo kwa kuongeza upatikanaji wa mbegu na viuatilifu bado wapo wafanyabiashara wasio waaminifu wanaoingiza pembejeo hizi feki katika maduka yao na kuwabambikizia wananchi.

Ili kuhakikisha kuwa wafanyabiashara ya mbegu wasio waaminifu hawaingizi sokoni mbegu feki, taasisi za TOSCI na TTCL zimebuni mfumo wa kielektroniki utakao wawezesha wakulima kubaini mbegu feki zilizo na lebo feki.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga jana  tarehe 7 Agosti 2020 wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa huduma maalum ya kuhakiki pembejeo za kilimo inayojulikana kama T-Hakiki wakati wa sherehe za wakulima (Nanenane) katika viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Aidha, ili kudhibiti ubora wa viuatilifu, Waziri Hasunga amesema kuwa katika kipindi cha mwaka 2019/2020, Wizara kupitia TPRI imekagua wafanyabiashara 222 wakiwemo wauzaji, watengenezaji, wafukizaji na waagizaji kutoka mikoa saba nchini.

Pia TPRI imetoa mafunzo ya matumizi sahihi na salama ya viuatilifu kwa wakulima, maafisa ugani na wauzaji 765 kutoka katika mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuendeleza jitihada za kudhibiti matumizi ya viuatilifu feki.

Vivyo hivyo, Wizara kupitia TOSCI na sekta binafsi inaendelea kuimarisha upatikanaji, utumiaji na udhibiti wa mbegu ili kuongeza tija, kipato na usalama wa chakula na lishe.

Amesema kuwa kutokana na kukua kwa sekta ya mbegu nchini, matumizi ya mbegu bora zilizothibitishwa na TOSCI yameongezeka kutoka tani 10,946 (2014/2015) hadi tani 57,023 (2018/2019).

Mhe Hasunga amesema kwa katika juhudi hizo za kuongeza matumizi ya mbegu bora, Wizara kupitia TOSCI imeongeza kiasi cha mbegu bora zilizothibitishwa na TOSCI zinazozalishwa hapa nchini kutoka tani 4,337 (2014/2015) hadi tani 46, 335 ambazo ni asilimia  81 ya mbegu zote zilizothibitishwa na TOSCI.

Kadhalika, ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na udhibiti wa ubora wa mbegu, Wizara kupitia TOSCI imekuwa ikiongeza matumizi ya lebo za ubora za TOSCI. “Katika mwaka wa fedha 2019/2020, jumla ya lebo 9,000,000 zilitolewa na TOSCI kwa wazalishaji mbali mbali wa mbegu ikilinganishwa na lebo 400 zilizotolewa mwaka wa fedha 2014/2015” Amekaririwa Mhe Hasunga

Hasunga amesema kuwa mfumo wa T-hakiki, ni sawa na mkombozi kwa mkulima kwa sababu ni huduma inayomwezesha mkulima kupata taarifa ya mbegu na kiuatilifu kilichosajiliwa.

“Pia inamsaidia mkulima kufahamu matumizi sahihi ya pembejeo hizo kupitia simu ya mkononi, hakika haya ni mapinduzi bora ambayo yatazidi kumkomboa mkulima lakini pia kuisaidia Serikali kukabiliana na wafanyabiashara wasio waaminifu na kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wakulima wetu” Amesisitiza Waziri Hasunga

MWISHO


Share:

Naibu Waziri Mabula Aagiza Eneo La Maonesho Nyakabindi Kupimwa Na Kupatiwa Hati

Na Munir Shemweta, WANMM SIMIYU
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemuagiza Kamishana Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Simiyu Essau Mwakatumbula kuhakikisha unafanyika mchakato wa kupima eneo la maonesho ya Nanenane Nyakabindi wilayani Bariadi mkoani Simiyu na kumilikishwa.

Dkt Mabula alitoa kauli hiyo alipotembelea Banda la Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi tarehe 6 Agosti 2020 kwenye viwanja vya maonesho vya Nanenane  vilivyopo eneo la Nyakabindi mkoani Simiyu.

Alisema, kwa sasa viwanja vya Nyakabindi Bariadi yanakofanyika maonesho ya nanenane halijamilikishwa kutokana na eneo hilo kutopimwa jambo alilolieleza kuwa linaloikosesha serikali mapato yatokanayo na kodi ya pango la ardhi.

 ‘’ Lazima tumsaidie mhe Rais katika juhudi zake za kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati kwa kuhakikisha tunakusanya kodi ikiwemo ya pango la ardhi, sekta hii ya ardhi ikisimamiwa vizuri hakuna idara itakayoizidi kwa ukusanyaji mapato‘’ alisema Dkt mabula.

Dkt Mabula alisema baada ya maonesho ya nanenane ya mwaka huu jitihada za kumilikishwa eneo la Nyakabindi vilipo viwanja vya maonesho zifanyike ili maonesho yajayo serikali ianze kukusanya kodi ya pango la ardhi.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Simiyu Essau Mwakatumbula alisema ofisi yake ilishaanza mazungumza na wahusika kuangalia na namna ya kumilikisha eneo hilo ili serikali kupitia Wizara ya Ardhi iweze kukukusanya mapato kupitia kodi ya pango la ardhi.

Katika hatua nyingine Dkt Mabuala aliwataka maafisa wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wamaoshiriki maonesho ya Nanenane Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo kuhusiana na sheria mpya iliyopitishwa Bungeni hivi karibuni ya kutaka wananchi waliokamilisha taratibu zote za kupatiwa hati ikiwemo kupimiwa eneo kuanza kutozwa kodi ya ardhi hata kama hawajachukua hati.


Share:

Usikivu wa TBC Mikoa ya Lindi na Mtwara Waimarika

Na Shamimu Nyaki –WHUSM-Mtwara
Serikali imeendelea kuimarisha usikivu wa Shirika la Utangazaji la Taifa TBC kwa idhaa  za TBC Taifa na TBC Fm katika Mikoa ya Lindi na Mtwara  baada ya kufunga Mtambo wenye nguvu ya kilo wati moja (1KW) kwa kila idhaa hizo.

Akizungumza wakati alipotembelea kituo cha kurusha matangazo ya redio hizo cha Lilungu Mkoani Mtwara Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe amesema, kuimarika kwa usikivu wa TBC katika  mikoa ya kusini ni jitihada za Serikali kuhakiksha wananchi wake wanapata taarifa ambazo zinaelezea utekelezaji unaofanywa na Serikali kwa ajili ya wananchi wake.

“Wananchi wana haki kikatiba ya kujua Serikali imewafanyia nini,na ili wajue ni kupitia vyombo vya habari vya kuaminika kama TBC,hivyo upanuzi wa usikivu wa shirikia hili umesaidia wananchi kupata habari zinazohusu nchi yao” alisema Dkt.Mwakyembe.

Aidha Dkt.Mwakyembe amesema kuwa kuna changamoto ya miundombinu  ya kufikia maeneo mbalimbali ya mitambo ya TBC hasa barabara kutokana na Mitambo hiyo kusimikwa maeneo ya miinuko,ambapo ameahidi kuwasiliana na Mamlaka husika ziweze kushughulikia changamoto hiyo.

Kwa upande wake Mhandisi wa Shirika hilo Bibi.Upendo Mbele amesema kuwa fedha za maendeleo zilizotengwa katika kutekeleza miradi mbalimbali ya usikivu zimesaidia kuboresha mradi wa Kilwa na Ruagwa ambao utasaidia katika kuongeza nguvu ya usikivu.

“Kituo hiki cha Mtwara kimepatikana kutokana na juhudi na mipango ya shirika kutumia mafundi wa ndani na  vipuri vya vituo  vya Namanga,Rombo,Tarime,Kibondo na Mbamba Bay ambavyo vilitumika kuunda mtambo huu”alisema Bibi Upendo.

Naye Fundi Mitambo wa Shirika hilo Bw.Hamis Kalanje amesema kuwa kituo hicho kimeanza kurusha matangazo kwa mitambo ya FM kwa idhaa za TBC TAIFA kwa masafa ya 87.7Mhz na TBC FM kwa masafa ya 89.7Mhz kwa uwiano wa nguvu ya kilo wati moja kwa kila mtambo.

“Baada ya kufunga mtambo huu usikivu umeongezeka katika maeneo ya Msimbati, Mtendachi,Kilambo,Mayanga,Mikindani,Nanguruwe,Mpapura  na  Ndumbwe”alisema Bw.Kalanje.

Katika hatua nyingine Waziri huyo amezindua kituo cha redio cha Hopaje FM (Nyakati za Kusisimua) kilichopo Mtwara ambapo amewahimiza wanahabari wa kituo hicho kufanya kazi kwa weledi na kufuata miiko ya taaluma ya habari,ambapo pia amesisitiza kutoa habari zinazoelezea utekelezaji wa serikali kwa wananchi wake na kusisitiza amani katika kipindi hiki cha uchaguzi mkuu.

…MWISHO..


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger