Monday 6 July 2020

Mtandao Wa Maji Ruangwa Wamtua ‘wamtua Ndoo Mama Kichwani’

Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
SERIKALI kupitia Wizara ya Maji imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji katika maeneo ya mijini na vijijini kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002.

Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002 inaelekeza kuwapatia wananchi waishio vijijini maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao, hatua inayolenga kuwaondelea changamoto mbalimbali ikiwemo maskini na magonjwa yanayosababishwa na maji.

Wizara ya Maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi waishio vijijini kwa kujenga, kupanua na kukarabati miradi ya maji, lengo ikiwa ni kufikia asilimia 85 ya wananchi wanaopata huduma ya maji safi na salama katika maeneo ya vijijini ifikapo mwaka 2020.

Miradi ya Maji Vijijini inatekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na wananchi pamoja na sekta binafsi ambapo katika kuwapunguzia wananchi gharama, Serikali kwa kushirikiana na wadau inaandaa mifumo itakayofaa kusimamia na kuendesha miradi ya maji ikiwa ni pamoja na kuviimarisha Vyombo vya Watumiaji Maji.

Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi inatekeleza miradi mbalimbali ya maji katika vijiji mbalimbali vya Wilaya hiyo hatua inayolenga katika kutoa huduma endelevu kwa wakazi waishio mijini na pembezoni mwa miji.

Wananchi wanaendelea kupata huduma ya maji safi na salama kutoka katika vyanzo vya Visima vifupi, Visima vya kati, Visima virefu ambavyo vimefungwa pampu za mikono, miradi ya maji bomba ya maporomoko na miradi ya maji ya kusukumwa na mitambo.

Tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini imeongezeka kutoka 38.5% mwaka 2015 hadi kufikia 51.20% kufikia mwezi Novemba, 2018 ikiwa ni ongezeko la 12.7% ambapo jumla watu 64,498 waishio vijijini wanapata huduma ya maji.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Maji wa Naunambe-Mpekenyera unaosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kushirikiana na Kamati za Vijiji vya Naunambe na Mpekenyera katika kuhakikisha kuwa Serikali inamtua mama ndoo kichwani na kumuondolea changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji.

Kufuatia juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali ya Wilaya ya Ruangwa mradi huo ulikamilika mwezi Juni, 2018 na jumla wananchi 7,000 wameanza kupata maji na salama na kiasi Tsh. Milioni 828 zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, ikiwemo ununuzi wa vifaa mbalimbali ikiwemo mashine za kusafisha maji na miundombinu mbalimbali kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa maji kutoka katika vyanzo na kuwafikia wananchi.

Akizungumza na Timu ya Maafisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) waliofanya ziara Wilayani humo, hivi karibuni, Katibu wa Mradi huo, Selemani Nyamiri anasema mradi huo ulianza kuibuliwa na wananchi mwaka 2010 kwa kaya mbalimbali katika vijiji hivyo kuchangishana fedha kwa ajili ya kuhakikisha mradi huo unatoa huduma endelevu ya maji katika vijiji hivyo vyenye wakazi zaidi ya 10,000.

‘Maji yaliyokuwa yakizalishwa katika chanzo cha Mpekenyeara yalikuwa yana chumvi sana, pia yalipatikana katika vyanzo visivyo safi na salama hivyo ilitulazimu kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya kwa ajili ya kutumia mafundi na utaalamu wa ziada ili kuhakikisha kuwa maji yanarejea katika ubora wake’’

Nyamiri anasema kwa sasa kiwango cha chumvi katika maji hayo kimepungua na kufanya maji hayo kuwa na ubora wa matumizi kwa binadamu, ambapo watumiaji wanalazimika kuchangia gharama ya Tsh. 200 kwa kila ndoo, ikiwa ni fedha zinazokusanywa na kamati hiyo kwa ajili ya kufanya matengenezo na ukarabati wa miundombinu ya mradi.

Akifafanua zaidi anasema wananchi wa vijiji hivyo wataendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuboresha huduma za maendeleo ya jamii ikiwemo huduma ya maji ambapo wananchi wamekuwa na mwamko wa kusimamia uhifadhi wa maeneo ya vyanzo vya maji ili kufanya vijiji vyote vinapata maji ya uhakika.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Naunambe Bi. Amina Abdalla aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kusimamia utekelezaji wa mradi huo kwa kuwa umeondoa kero kwa akina mama wa vijiji hivyo waliokuwa wakisafiri umbali mrefu kutafuta huduma ya maji.

Bi. Rehema Mussa Mkazi wa Kijiji cha Mpekenyera alisema kwa kipindi cha nyuma hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika vijiji hivyo haikuwa ya kuridhisha, hususani wakati wa kipindi cha kiangazi na kuwalazimu wananchi wengi kutembea umbali wa kilometa 3 kufuata huduma ya maji katika vyanzo visivyo rasmi huku wakitembea na watoto migongoni.

‘Utekelezaji wa mradi huu ni mkombozi mkubwa sana kwetu wananchi wa Naunambe na Mpekenyera kwani kwa sasa shida ya maji imeisha, tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Mbunge wetu wa Ruangwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa’’ alisema Rehema.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Andrea Chezue alisema hali ya upatikanaji wa maji katika Wilaya hiyo umefikia asilimia 55  huku kukisaliwa na maeneo machache ambayo yanakosa huduma ya maji ambapo Ofisi yake imekuwa ikiendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha huduma ya maji inafikia walau asilimia 70 ifikapo mwishoni mwaka 2020.

‘Halmashauri ya Ruangwa inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya maji katika vijiji mbalimbali ikiwemo mradi wa maji wa Naunambe-Mpekenyera wananchi wanapata maji na wanafurahia huduma inayotolewa kwa mwaka 2019 pekee tulipata miradi minne ikiwemo mradi wa maji Kitandi na tayari tumeanza kufanya mawasiliano na Halmashauri ya Mtama kuhakikisha kuwa maji yanafikishwa katika vijiji jirani ikiwemo vijiji vya Nangumbu A na B’’ alisema Chezue.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maji Kata ya Mandawa Rashid Mshamu anasema mradi wa maji mandawa unahuhudumia jumla ya vijiji 5 vya Nahanga, Chikundi, Mandawa Chini, Mchichili na Mtondo unaogharimu kiasi cha Tsh. Bilioni 1.7 zilizotolewa na Serikali, ambapo mradi huo unawanufaisha jumla ya watu 13,756.

Anaongeza kuwa mradi huo ulioasisiwa mwaka 1975 ulikuwa na miundombinu  chakavu na kusababisha kero kubwa kwa wananchi hususani wazee, wanawake na watoto ambapo walikuwa wanahangaika, ambapo Serikali iliamua kuufua mradi huo katika bajeti ya mwaka 2014/15.

Anasema kuwa kwa sasa mradi huo unaendelea vyema na huduma ya maji ni ya uhakika na wananchi wa vijiji hivyo wanalazimika kuchangia kiasi cha Tsh. 50 inayopelekwa katika mfuko wa maji wa kijiji hicho na kutumika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya mradi.

Miradi mingine ya maji inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ni pamoja na mradi wa maji Nanganga, mradi wa maji Likunja, mradi wa maji Namahema, mradi wa maji Chenjele, ambapo katika maeneo yote hali ya upatikanaji wa maji ni ya kurithisha.

Miradi mingine ni pamoja na ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Mibure, Namakuku na Namahema ambao tayari umekamilika na jumla ya watu 6,133 wananufaika, ambapo kiasi cha Tsh. Milioni 631,593,444.50 zimetumika.

Serikali imewekeza katika miradi ya maji mikubwa na midogo ili kufikisha huduma ya maji kwa wananchi, ambapo uwekezaji huo umeleta mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali nchini na maisha ya wananchi kwa ujumla.

Ili kuleta matokeo tarajiwa utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maji hapa nchini unahusisha ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi na pia wadau wa maendeleo kutokana na ukweli kuwa Serikali imeweka lengo la kufakisha huduma ya maji kwa asilimia 85 kwa upande wa wananchi.

MWISHO


Share:

VIDEO: Tigo yaongeza tahadhari kwa wateja wanaotembelea Banda lao SabaSaba

USALAMA KWANZA: Jinsi ambavyo #TigoSabasaba inachukua tahadhari mbalimbali uwapo ndani ya banda Ili kujikinga na maambukizi juu ya Covid-19 Tigo imechukua tahadhari mbalimbali ili uwepo katika banda la Tigo. Ni salama! Karibu ufurahie ofa na huduma msimu huu wa Tigo Sabasaba.


Share:

Waziri Mkuu:Tutaendelea Kudhibiti Matumizi Ya Fedha Za Umma

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli itaendelea kudhibiti matumizi ya fedha za umma ili iweze kuendelea na ujenzi wa miradi ya kimkakati zikiwemo bandari kwa lengo la kuboresha maendeleo ya wananchi wake.

Pia, Waziri Mkuu amesema changamoto ya usafirishaji wa mizigo na abiria kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) itakuwa historia baada ya kuboreshwa na kujengwa kwa miundombinu ya bandari katika wa Ziwa Tanganyika ukiwemo upanuzi wa bandari ya Kasanga.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumapili, Julai 05, 2020) alipozungumza na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa upanuzi wa Bandari ya Kasanga iliyoko wilaya ya Kalambo akiwa katika ziara  ya kikazi mkoani Rukwa. Mradi huo unagharimu zaidi ya sh. bilioni 4.7.

Alisema upanuzi wa bandari hiyo utawezesha mizigo inayotoka nchini kwenda Congo kufika kwa wakati kwa sababu itasafirishwa moja kwa moja bila kupitia katika nchi nyingine kama ilivyo sasa, ambapo madereva wanalazimika kupita kwenye Mataifa mengine na kutumia muda mrefu.

“Mradi huu ukikamilika utaongeza pato la mwananchi mmoja mmoja pamoja na Taifa kwa ujumla. Rais Dkt. Magufuli amedhamiria kuboresha maendeleo ya wananchi nchi nzima ikiwemo na wilaya hii ya Kalambo. Ujenzi wa miradi hii unatoa fursa za ajira kwa wananchi, hivyo zichangamkieni.”

Vilevile, Waziri Mkuu alisema mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa bado yanaendelea nchini, hivyo mtu yeyote atakayebainika anajihusisha na masuala hayo atafutwe popote alipo akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria kwa sababu rushwa ni adui wa haki.

Pia, Waziri Mkuu aliendelea kuwakumbusha watendaji ndani ya Serikali wahakikishe wananchi wanapofika katika maeneo yao ya kazi wawapokee, wawasikilize na kuwahudumia bila ya ubaguzi. “Hatuangalii sura wala kabila yeyote atakayekanyaga kwenye maeneo yenu ahudumiwe ipasavyo.”

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe alisema Tanzania na Congo zimeungana kwa Ziwa Tanganyika, usafiri wa barabara uliokuwa unatumika awali uliyalazimu maroli ya mizigo kupitia nchini nyingine na kuchelewa kufika.

Alisema kukamilika kwa upanuzi wa bandari hiyo pamoja na ujenzi wa barabara kwa kiwago cha lami kutoka Sumbawanga hadi Kasanga kutarahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo kwa kutumia bandari hiyo kuingia nchini Congo moja kwa moja bila kupita kwenye nchi juirani.

Waziri Kamwelwe alisema kuwa awali kulikuwa na changamoto ya barabara hali iliyosababisha meli kufika kwenye Bandari ya Kasanga na kulazimika kusibiri mizigo ambayo ilikuwa ikichelewa kufika kutokana na ubovu wa barabara na sasa tayari Serikali imeitatua kwa kuijenga kwa kiwango cha lami.

Awali, akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi huo, Kaimu Katibu Mkuu wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Uchukuzi, Mhandisi Thomas Ngulima alisema mradi huo umeanzishwa ili kuongeza ushindani na tija katika shughuli za kibandari kusini mwa Ziwa Tanganyika.

Alisema mradi huo unahusisha upanuzi mkubwa wa gati ilililopo sasa lenye urefu wa mita 20 lifikie mita 120, ambazo zitawezesha kuhudumia  meli mbili hadi sita kwa wakati. Kazi nyingine ni ujenzi wa miundombinu ya bandari ikiwemo jengo la kupumzikia abiria, mgahawa na nyumba za watumishi.

Mhandisi Ngulima alisema mradi huo unaojengwa na kampuni ya Inter-Consult Limited umefikia asilimia 70 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Septemba, 2020 na kwamba utafungua na kuboresha njia ya biashara ya mazao ya chakula katika nchi za DRC, Burudi na Zambia.

Aliongeza kuwa, ujenzi wa barabara ya kimkakati inayoanzia Manispaa ya Sumbawanga hadi Kasanga (km 107), pamoja na upanuzi wa bandari unaoendelea, utawezesha mtiririko wa shehena za saruji, makaa ya mawe, chokaa na sabuni kuongezeka hivyo kukuza uchumi wa wananchi na Taifa.


Share:

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WATAKIWA KUWACHUJA WAGOMBEA, MAGUFULI AMWAGIWA SIFA



 Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uimarishaji wa Maadili na Usaidizi Katika Utumishi wa Umma na wa Binafsi (WoLaOTa) Samwel Olesaitabau akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa taasisi hiyo iliyofanyika mkoani Singida jana.
Waandishi wa habari wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa taasisi hiyo. 

Na Dotto Mwaibale, Singida

VIONGOZI wa vyama vya kisiasa wametakiwa kuhakikisha wote wanaoomba nafasi ya uongozi wanachujwa ipasavyo ili kusaidia kupunguza viongozi wala rushwa nchini.

Ombi hilo limetolewa na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uimarishaji wa Maadili na Usaidizi Katika Utumishi wa Umma na wa Binafsi (WoLaOTa) Samwel Olesaitabau wakati wa hafla ya uzinduzi wa taasisi hiyo iliyofanyika mkoani hapa jana.

Katika hatua nyingine Olesaitabau amewaomba viongozi wa dini kote nchini kutenga muda katika ibada zao hata kwa dakika tano kuiombea Nchi na Uchaguzi Mkuu wa 2020 hata kwa wale wasio na dini rasmi wanaoabudu mawe au milima nao wafanye hivyo.

"Mwaka huu kuna uchaguzi na niwaombe sana viongozi wote wa vyama vya kisiasa kikiwemo chama Tawala cha CCM kuhakikisha wote wanaoomba uongozi wamechujwa ipasavyo na wasiwe na huruma na wakifanya hivyo basi kwa vyovyote vile tutapunguza viongozi wala rushwa Serikalini" alisema Olesaitabau.

Akizungumzia kusudi la kuanzisha taasisi hiyo alisema ni kusaidia uongozi wa nchi yetu kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli kama aalivyoonesha Rais John Magufuli. 

Aidha Olesaitabau alisema dira ya taasisi hiyo ya kipekee hapa nchini ni utoaji wa elimu ya kuimarisha maadili kwa waajiri, na watumishi wa sekta za umma na binafsi Tanzania Bara ili watumie Ueledi na Taaluma zao kwa kuleta matokeo chanya.

Olesaitabau akizungumzia baadhi ya sifa kati ya 35 alizoziona za utendaji kazi wa Rais Dkt. John Magufuli alisema ni kiongozi ambaye ana uwezo wa kuamua jambo na kulisimamia kuanzia mwanzo hadi mwisho na kuwa hayumbishwi na kelele  ama za ndani ya nchi au hata nje kwa jambo ambalo amelianzisha kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Alitaja sifa nyingine kuwa anaichukia rushwa na anapenda kila mtu afanye kazi ya kujipatia kipato kwa jasho lake mwenyewe bila ya kumdhulumu mwingine na kuwa ana uwezo wa kuweka kumbukumbu/ takwimu kiusahihi katika kichwa chake kwa muda mrefu bila ya kusahau.




Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 6,2020


 




















Share:

Sunday 5 July 2020

FULL POWER, ZATI 50 NI KIBOKO YA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO

Zati 50
Full Power
Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Zati 50


⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4


⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.



Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama



Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

MGEJA : SIONI CHAMA CHA KUISHINDA CCM 2020

Khamis Mgeja
Na Paul Kayanda - Kahama 
MWENYEKITI wa taasisi ya Tanzania Mzalendo Foundation Khamis Mgeja amesema kuwa wakati Taifa likielekea katika uchaguzi mkuu 2020 ili kuwapata viongozi ngazi ya Urais Ubunge na Udiwani haoni chama cha kukishinda Chama cha Mapinduzi (CCM).


Mgeja aliyasema hayo jana alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari waliomtembelea nyumbani kwake katika kijijini cha  Nyanhembe Kata ya Kilago Halmashauri ya Mji wa Kahama Mkoani Shinyanga kwa ili kupata maoni yake binafsi na mtazamo wake kuhusu mustakabali wa nchi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020.

Mwenyekiti huyo wa taasisi ya Mzalendo Foundation inayojishughulisha na masuala ya demokrasia haki na utawala bora alisema kuwa mtazamo wake na uzoefu mkubwa wa masuala ya siasa na mahusiano ya jamii haoni chama chochote hivi sasa nchini cha kushindana na kukishinda chama cha Mapinduzi CCM.

Mgeja alisema kuwa zipo sababu nyingi za kusababisha CCM kishinde kwa kishindo na kupelekea vyama vya upinzani kuanguka kwa kishindo.

Aliendelea kuwaeleza waandishi wa habari kuwa sababu kubwa moja ni kupitia serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli ni utekelezaji wa kiwango cha hali ya juu sana kuhusu utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi katika Nyanja zote za huduma ya jamii.

Alisema kuwa pia ni uzalendo wa mheshimiwa Rais Magufuli alioufanya katika Taifa na kuongeza kuwa tatu ni uadilifu wake kuhusu kuisimamia serikali anayoiongoza kwa uadilifu wa hali ya juu sana.

Mgeja alisema kuwa sifa nyingine ni Rais kuwa mjasili na kuthubutu kuyatekeleza mambo makubwa hususani miradi iliyokuwa imeshindikana kutekelezwa katika miaka ya nyuma ikiwamo mradi mkubwa wa uzalishaji umeme katika Mto Rufiji, reli ya kati, serikali kuhamia Dodoma pamoja na mambo mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi.

Mgeja alisema kuwa kwa sababu hizo za utekelezaji wa miradi mbalimbali ndiyo sababu pekee itakayopelekea CCM kushinda kwa kishindo kikubwa sana na kupelekea kwa mafanikio hayo makubwa yanayomwekea Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli njia nyeupe ya kwenda Ikulu oktoba 2020.

Akizungumzia kuhusu upinzani alisema kuwa sababu kubwa zitakazopelekea kushindwa kwa kishindo kwa mwaka huu wa 2020 kwa vyama vyote vya upinzani sababu moja wapo ni wanaingia mwaka huu wakiwa hawana agenda yoyote ile inayogusa nchi na maisha ya watu badala yake yote yanatekelzwa na CCM.

Alisema kuwa katika kpindi cha miaka mitano iliyopita kutokea uchaguzi wa mwaka 2015 wamekosa sela nzuri mbadala dhidi ya chama tawala CCM sela ambayo wangekuwanazo wangewajengea imani wananchi na kujijenga wao.

Tatu vyama vya upinzani kukosa utayari wa kuongoza nchi ikiwemo mfano mkubwa katika tatizo hili la kukabiliana na Gonjwa la Corona COVID-19 huku akitolea mfano wa chama kikuu cha upinzani kikikimbia bungeni na kuhoji kuwa je? Kama taifa likipata misukosuko ya njaa au vita itakuwaje ikiwa na viongozi ambao hawana utayari na ujasiri.

 “Nne sioni kiongozi hivi sasa wanaosemwa semwa kutokea upinzani wenye sifa au vigezo vinavyokidhi uwezo wa kuwa Rais ili kuiongoza nchi, alisema Mgeja mwenyekiti wa taasisi ya Mzalendo Foundation.

Mgeja alisema kuwa wapinzani wakikosa sifa zote hizo maana yake wataingia katika kinyan’ganyilo cha uchaguzi mwaka huu 2020 wakiwa wamefirisika ni vyema kama vyama makini wakajitathmini.

Pia alivishauri kwa vyama vyote vya upinzani wawe wastaarabu na kukubali matokeo mapema ya kushindwa watakuwa wamejijengea heshima kubwa sana kwani si busara wakashiriki uchaguzi huku wakijua wanaenda kushindwa ni sawa na Simba, Yanga, Azam zinaingia fainali na kucheza timu za mchangani unategemea nini katika matokeo ya ubingwa.

“Pamoja na kuwa wote tunapenda na kuheshimu demokrasia lakini demokrasia inayokosa ushindani hayo ni matumizi mabaya ya demokrasia na raslimali za nchi kwani mabilioni ya fedha yatakayotumika na kuteketea bure hiizo ni kodi za wananchi na hasa wanyonge ingekuwa vyema fedha hizo kujielekeza kwenyenye huduma za jamii ikiwemo afya, elimu, barabara, umeme na miundombinu mingine ikiwemo reli,” alisema Mgeja.

Alisema kuwa japo ukweli unauma lakini ukweli utabaki palepale na kunausemi wa waswahili unaosema, heri aibu kuliko fedheha na kuwashauri wapinzani wakubali yaishe kwani katika siasa kuna wakati mnaweza kutofautiana na wakati mwingine mnaweza kukubaliana katika masuala ya msingi yanayohusu mstakabali wa Taifa.

“Ni busara na kukomaa kisiasa kukubali na kupongeza unapoona mshindani wako anapofanya vizuri  na kumuunga mkono aendelee kuongoza nchi kama TLP walivyounga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano binafsi nawapongeza TLP kupitia mwenyekiti wao mheshimiwa Augustino Lyatonga Mrema kwa kuonyesha uungwana wa kisiasa nawaomba wanasiasa na vyama vingine viige mfano huo ili tuungane pamoja katika kuleta maendeleo kwa wananchi,” alisema Khamis Mgeja.

Mgeja ambaye ni mwanasiasa mkongwe nchini ambaye ameamua kupumzika siasa na kujikita kijijini na kujishughulisha na suala la kilimo na ufugaji.
Share:

Government Job opportunity at Songea July 2020

Government Job opportunity at Songea July 2020

The post Government Job opportunity at Songea July 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MEDICAL SPECIALIST II(RE-ADVERTISED) – 2 POST at Muhimbili National Hospital (MNH)

On behalf of Muhimbili National Hospital (MNH), Public Service Recruitment Secretariat invites dynamic and suitably qualified Tanzanians to fill 2 vacant posts mentioned below; 1.0 MUHIMBILI NATIONAL HOSPITAL (MNH) Muhimbili National Hospital (MNH) is a tertiary specialised and super specialist hospital in Tanzania organized into nine directorates with bed capacity of 2,178 out of which […]

The post MEDICAL SPECIALIST II(RE-ADVERTISED) – 2 POST at Muhimbili National Hospital (MNH) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Maalim Seif achukua fomu kugombea Urais Zanzibar

Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalengo, Maalim Seif Sharif Hamad leo amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais visiwani Zanzibar kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa Viongozi utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Maalim Seif amekabidhiwa fomu hiyo leo na Katibu Mkuu wa ACT- Wazalendo, Ado Shaibu katika ofisi za Chama za Vuga Zanzibar.


Share:

BARAZA LA JUMUIYA YA WAZAZI WILAYA YA TANGA LAMPONGEZA RAIS MAGUFULI

 KATIBU wa CCM Mkoa wa Tanga Shaibu Akwilombe akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza  kuu la Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga Nassoro Makau
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga Nassoro Makau akizungumza wakati wa mkutano huo kulia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Shaibu Akwilombe
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Mkoba akizungumza kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Shaibu Akwilombe na kulia ni Katibu wa CCM wilaya ya Tanga


MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa kikao hicho

 MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu katika akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT wilaya ya Tanga Sussan Uhinga

Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiwa kwenye picha moja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga Nassoro Makau na Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Tanga Moza Shilingi
 wakiwa kwenye ;picha ya pamoja


BARAZA kuu la Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga limempongeza Rais Dkt John Magufuli kwa uongozi bora wenye uweledi na kusimamia maadili kwa watumishi wa umma huku wakieleza kwamba anastahili kuendelea kuwatumikia watanzania.



Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga Nassoro Makamu alisema kwamba Rais Magufuli amefanya kazi kubwa iliyotukuka ya kuhakikisha anawapa maendeleo watanzania hivyo wataendelea kumuunga mkono kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.



Alisema kwamba tarehe 14 ndio siku ya kuchukua fomu ua kuwania nafasi za udiwani na Ubunge na baadae uchaguzi huu lengo la chama na nia ya dhati  kwa kauli ya wazazi ni kumuhakikishia kura nyingi Rais Magufuli kwa mkoa wa Tanga kwa asilimia 98 .



Alisema kwani wao kama wazazi ni jeshi kubwa kwa sababu katika jumuiya hii vijana wapo, uwt wapo hivyo hawana sababu ya kuacha kumpa kura zote Rais Dkt Magufuli kwa wakati wa uchaguzi mkuu ambao unatarajiwa kufanyikamwezi Octoba mwaka huu.



“Ndugu zangu tunakwenda kwenye uchaguzi sisi kama wazazi tuhakikisha tunampa kura za ndio Rais Dkt Magufuli kwa asilimia 98 huku 78 zikitoka kwa wazazi na hatutashindwa kufanya hivyo kwa sababu wazazi ndio wenye kutafsiri elimu ya malezi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2020”Alisema



Awali akizungumza wakati akifungua mkutano huo Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Akwilombe aliwataka kwenda kuitafsiri dhana ya elimu ya malezi kuelekea kwenye uchaguzi mkuu maana ya moja ya mambo yanayowapa changamoto ndani ya chama ni ukosefu wa elimu ya siasa na elimu ya utambuzi.

 “Tatizo lenu kubwa ni kuitafsiri dhana ya elimu na malezi kwa mujibu wa wakati… kuna jambo ambalo linazungumzwa sana ni uchaguzi tukiwa kwenye maandalizi ya mchakato ndani ya chama hivyo niwaombe muitafsiri dhana ya elimu na malezi kuelekea kwenyue uchaguzi mkuu “Alisema



Alisema kwa maana moja ya mambo yanayowapa changamoto ndani ya chama ni ukosefu wa elimu ya siasa na elimu utambuzi kwa kuwa jumuiya ndio ina dhamana ya kusimamia masuala ya elimu na malezi naomba jumuia ya wazazi Tanga mjini muitafisiri dhana ya elimu na malezi wakati chama kikielekea kwenye uchaguzi mkuu wa nchi.



Share:

CCM Yaipongeza Serikali Kwa Kusimamia Uchumi Imara Na Jumuishi Uliopelekea Tanzania Kuingia Uchumi Wa Kati Duniani

Chama Cha Mapinduzi kimeipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Chini ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa usimamizi wa Uchumi imara, madhubuti na jumuishi ambao umewezesha kuingia katika kundi la nchi zenye uchumi wa kati miaka mitano kabla ya wakati.

Katibu wa NEC – Itikadi  na Uenezi ameyasema hayo jana tarehe 04 Julai 2020 Katika Mkutano Mkuu Maalum wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dodoma na uliyohudhuriwa na maelfu ya vijana jijini Dodoma.

Ndg. Polepole anaeleza ni kwa namna gani Sera za CCM zimeelekeza shughuli za maendeleo zilenge kuwatoa wananchi kutoka Tabaka la umaskini na kuishi katika maisha ya staha, utu na kuwezesha ushiriki wao kwenye uzalishaji, biashara na masoko pamoja na fursa jumuishi kwa vijana na wanawake wa kipato cha chini.

Maamuzi makubwa yamefanyika yaliyopelekea uchumi imara yaliyokwenda sambamba na maamuzi ya kimkakati na  sahihi kwenye sekta ya madini, usafiri na usafirishaji, viwanda na biashara na sekta nyingine nyingi.

Aidha Polepole amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa miaka mitano ya kazi kubwa ambayo mafanikio yake yanaonekana na kupelekea kuvuka kwa haraka kulekea uchumi wa kati tofauti na ilivyotarajiwa kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa iliyolenga kufika huko mwaka 2025.

Chama Cha Mapinduzi kimeridhishwa na Utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi Mkuu kwa Mwaka 2015 – 2020 na kuingia katika uchumi wa kati ikiwa ni moja ya utekelezaji wa maono ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake.


Share:

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Lafanikiwa Kuzuia Tukio La Ujambazi / Wizi Katika Bank Ya Crdb

Tukio hili limetokea usiku wa tarehe 05.07.2020 majira ya 02:00hrs katika bank ya crdb, tawi la igoma, wilaya ya nyamagana, mkoa wa mwanza, baada ya kundi la wahalifu/majambazi kuvunja kwa nyuma eneo la jengo la bank hiyo ambayo imepakana kwa karibu na majengo mengine na kufanikiwa   kukata bati la paa na dari (ceiling board) na kupata mwanya wa kuingia ndani ya benki hiyo.

Askari polisi waliokuwa lindo katika eneo hilo walibaini  kuwepo kwa  mazingira yasiyo ya kawaida, walipozungukia jengo hilo kuchunguza kwa kina walibaini kuwepo kwa mmoja wa majambazi aliyekuwa tayari ndani akijaribu  kutoka kupitia sehemu waliyovunja wakati wakiingia. Askari walimuamuru ajisalimishe lakini alikaidi amri hiyo halali na walimrushia risasi iliyomjeruhi  mkono  na  bega la kulia  akalazimika kurudi ndani ya bank na akakamatwa huku akiwa katika hali mbaya .

Mtuhumiwa alikimbizwa hospitali ya mkoa ya sekou toure kwa matibabu lakini kwa bahati mbaya alifariki  dunia akiwa bado  njiani,   mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kusubiri uchunguzi wa daktari na utambuzi.

Uchunguzi wa awali uliofanyika eneo la tukio kwa kushirikiana na maneja wa bank hiyo umebaini kuwa licha ya wahalifu hao kuingia ndani ya bank na kuvuruga droo za ofisi hizo lakini hawakuweza kufanikiwa kuiba fedha zilizokuwa zimehifadhiwa sehemu maalum. Jeshi la polisi linaendelea na ufuatiliaji mkali wa kuhakikisha watuhumiwa wengine waloshiriki  kupanga na kujaribu kutenda tukio hili  wanakamatwa.

Jeshi la polisi mkoa wa mwanza linaendelea kutoa onyo kali kwa baadhi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu kutojaribu au kufanya vitendo hivyo kwani hatua  za kisheria ikiwa ni pamoja na kukamatwa zitachukuliwa dhidi yao. Pia kitendo kilichofanywa na marehemu (muhalifu) licha ya kuwa ni kosa kisheria lakini ni dharau na kejeli kwa jeshi la polisi anbalo limeapa kutovumilia vitendo vya namna hiyo.


Share:

Waziri Mkuu: Tuongezee Bidii Ili Tufikie Uchumi Wa Juu

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka Watazania waendelee kufanya kazi kwa bidii ili nchi iendelee kukua kiuchumi na kufikia uchumi wa juu kwa kuwa tayari imekuwa ya uchumi wa kati.

“Kama ni mkulima lima kwa bidii, mtumishi wa umma fanya kazi kwa bidii, mlio viwandani fanyeni kazi na mamalishe nanyi pikeni sana ili mzunguko wa fedha uweze kuendelea kuwa mkubwa nchini.”

Alitoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Julai 04, 2020) alipozindua jengo la ofisi na biashara la Mpanda Plaza lililojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mpanda kwa gharama ya sh bilioni  2.8.

Waziri Mkuu alisema Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani pato la mwananchi kwa mwaka lilikuwa dogo na baada ya miaka mitano limeongezeka na kufikia sh, milioni mbili.

Alisema ongezeko hilo la pato la mwananchi kwa mwaka limeliwezesha Taifa kuingia katika uchumi wa kati kabla ya matarajio yaliyopendekezwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo.

Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Tanzania ililenga kuifikisha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda ifikapo mwaka 2025 lakini nchi imewezeka kufikia uchumi wa kati 2020.

Baada ya kuzindua jengo hilo, Waziri Mkuu alitembelea kijiji cha Kasekese kilichoko wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi ambapo alizindua msimu wa ununuzi wa zao la pamba kwa mwaka huu.

Waziri Mkuu alisema lengo la Serikali ni kurudisha ushirika  ili uweze kuwa na tija kwa wakulima, aliwataka viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika (AMCOS) wawasaidie wanachama wao.

Vilevile, Waziri Mkuu aliwaagiza Maafisa Kilimo nchini wawaelimishe viongozi wa vyama vya ushirika namna bora ya uendeshaji wa vyama hivyo ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Aliwahakikishia wananchi hao kwamba Serikali itaendelea kuwasaidia kwa kuhakikisha Maafisa Ugani wanawafikia katika maeneo yao na kuwapa elimu itakayowawezesha kujiongezea tija.

Mwisho.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Waziri Mkuu: Bandari Ya Karema Ijengwe Usiku Na Mchana

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiagiza Kampuni ya Xiamen Ongoing Construction Group inayojenga  Bandari ya Karema kwa gharama za zaidi ya sh. bilioni 47 ifanye kazi usiku na mchana na  kukamilisha ujenzi huo kwa wakati ili kuimarisha biashara kati ya Tanzania na Congo.

Pia, Waziri Mkuu ametoa muda wa siku 21 kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Polisi, Wizara ya Madini na wawe wameanza kutoa huduma katika eneo la Ikola ili kuhudumia wageni wanaotoka Congo.

Alitoa agizo hilo jana jioni (Jumamosi, Julai 04, 2020) baada ya kuweka jiwe la msingi la  ujenzi wa Bandari ya Karema inayojengwa kwenye ziwa Tanganyika katika kata ya Karema wilayani Tanganyika, Katavi. Alisema mkandarasi anatakiwa ahakikishe mradi huo unakamilika haraka.

Waziri Mkuu alisema mradi huo unalenga kuongeza tija katika shughuli za kibandari kwenye ukanda wa Ziwa Tanganyika ndani na nje ya nchi na kwamba utaongeza fursa za kibiashara nchini na pia utakuwa chachu ya kukuza uchumi pamoja na kuboresha huduma za usafiri kwa wananchi.

“Tumeamua kujenga bandari hii ambayo itawezesha meli zaidi ya moja kupakia na kushusha abiria na mizigo kwa wakati mmoja. Hii ni Serikali ya kuahidi na kutekeleza na ni Serikali ya kusikia na kutenda na ndio maana halisi ya falsafa ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya Hapa Kazi Tu.”

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mhandisi Dkt. Baraka Mdima alisema mradi huo unahusisha ujenzi wa gati kubwa la kufungia meli lenye urefu wa mita 150 pamoja na kingo ya kuzuia mawimbi makali, uchimbaji wa kuongeza kina cha lango la kuingilia bandarini na sehemu ya kugeuzia meli.

Alisema eneo jinguine ni ujenzi wa miundombinu ya bandari ikiwemo mgahawa, jengo la kupumzikia abiria, majengo ya ofisi, eneo la sakafu ngumu kwa ajili ya kuhifadhia makasha pamoja na miundombinu ya Zimamoto na Tehama. Mradi huo utazingatia ujumuishi wa Reli ya Kisasa (SGR).

“Mradi unajengwa kwa miezi 24 na kukamilika kwa bandari ya kisasa ya Karema, kutaboresha shughuli za kiuchumi katika mkoa wa Katavi na Tanzania kama kusafirisha watu na bidhaa katika maeneo ya mwambao wa Ziwa Tanganyika na nchi jirani za Congo, Burundi na Zambia.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera aendelee na operesheni ya kuwasaka watu wote wanaomiliki silaha kinyume cha sheria.“Watu wote wanaomiliki silaha bila ya kuwa na vibali watafuwe popote walipo na wachukuliwe hatua za kisheria.”

Awali, Waziri Mkuu alizungumzia upatikanaji wa umeme katika wilaya ya Tanganyika, alisema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kufikisha huduma ya umeme katika vijiji vyote nchini, hivyo waendelee kuwa na subira.

“Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli anataka kuona kila nyumba ya Mtanzania inawaka umeme na amepunguza gharama za kuunganisha umeme kutoka sh. 380,000 hadi sh. 27,000 ili kila mwananchi aweze kumudu gharama hizo.”

Waziri Mkuu aliongeza kuwa licha ya gharama za kuunganishiwa umeme kupunguzwa, pia wananchi hatolazimika kulipia gharama za nguzo pamoja na gharama za fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwani tayari zimeshalipiwa na Serikali.

Mwisho.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Mgumba; Serikali Imetatua Changamoto Jimbo La Morogoro Kusini Mashariki

NAIBU waziri wa Kilimo Omary Mgumba  amesema kuwa serikali imefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali maendeleo kwa  wananchi katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki tofauti na watu  baadhi ya watu  wanavyoeneza propaganda juu ya kile kilichotekelezwa katika jimbo hilo.

Mgumba ambae ni Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki ameyasema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa kamati za siasa katika Kata ya Kidugalo na Ngerengere Mkoani Mkoani Morogoro.

Alisema kuwa wanaoeneza Propaganda hizo hawana nia njema na Chama cha Mapinduzi CCM kwani hivi sasa wananchi wamefunguliwa fursa mbalimbali ikiwemo miundombinu ya Barabara,elimu huduma za afya pamoja na huduma ya maji.

Aidha alisema kuwa hivi sasa wananchi pamoja viongozi wa CCM katika Jimbo hilo wanatakiwa watembee kifua mbele kutokana na yale yalitokelezwa na serikali ya awamu ya tano chini Dr John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na yeye akiwa Mbunge wa Jimbo hilo la Morogoro Kusini Mashariki.

Akizungumzia kuhusu Barabara amesema kuwa hivi sasa barabara nyingi zinapitika amabzo zilikuwa changamoto hapo awali hali iliyaofanya wanachi kuteleza shughuli za zao za kimaendeleo licha ya kuwepo changamoto ndogongo katika baadhi ya barabara ambazo serikali imekuwa ikizitatua kwa kwa wakati.

Kuhusu Barabara ya Bigwa Kisaki amesema kuwa barabara hiyo hivi karibuni Itaanza kujengwa kwa Kiwango cha lami kwa Kilometa 60 na makandarasi ameshapatika.na hapo awali katika ilani ya CCM 2005 iliahidi kuifanyia upembuzi yanikini ili iweze kujengwa kwa lami

Sanjari na hayo alisema kuwa kwa kipindi cha uongozi wake amefanikiwa kutembelea takribani wa Vijiji na Kata Zote Kila mwaka tofauti na wasikuwa na nia njema wanaodai amekuwa Mbunge wa kata Moja ya Mkuyuni.

ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa jimbo la Morogoro kusini Mashariki kwa ushirikiano wao walioutoa katika kipindi ambacho alikuwa mbunge wa Jimbo hilo

wajumbe hao wa kamati ya Siasa wamempongeza Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki Omary Mgumba kwa kufanikwa kuteleza na kutatua changamoto mbalimbali ambazo hapo awali katika viongozi waliopita hazikuweza kutatuliwa.

Walisema kuwa hivi sasa ni faraja kwa serikali awamu ya tano chini Dr John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wanaimani nayo kutokana na miradi mikubwa ya kimkatati ambayo wameitekeleza kwa kipindi kiupi cha miaka miatano.

Waliongeza kuwa juhudi zao katika kusimamia shughuli za maendeleo ndizo zimeifanya sasa serikali hiyo kuingia katika uchumi wa kati.

Jimbo la Morogoro kusini Mashariki chini ya Mbunge wake Omary Mgumba katika kipindi cha awamu ya tano limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupokea fedha za miradi ya maendeleo kupitia mfuko wa Jimbo ambazo zimezaa matunda katika sekta mbalimbali.

Pia wamefanikiwa kudhibiti mapato ya halmsahauri ya Wilaya ya Morogoro ambayo yalikuwa yanapotea mikono mwa wachache,ujenzi wa Kiwanda cha kucahata mazao jamii ya mikunde ambacho ni pekee kwa Tanzania Nzima,pia kujengwa kwa kiwanda Kikubwa cha sukari cha Mkulazi kutafungua fursa kubwa ya ajira kwa wakazi wa jimbo hilo na maeneo mengine.
Ujenzi wa Hospital ya Wilaya,na kuhamishwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mogororo kwenda Mvua yote hayo ni moja ya mafanikio amabyo yamepatikana katika serikali ya awamu ya Tano
 


Share:

Waziri Lukuvi Ataka Wamiliki Wa Ardhi Wenye Hati Za Miaka 33 Kuzihuisha Ofisi Za Ardhi Za Mikoa

Na Munir Shemweta, WANMM MUSOMA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amewataka wamiliki wa ardhi ambao hati zao za ardhi zinaishia miaka 33 kwenda ofisi za ardhi za mikoa zilizoanzishwa hivi karibuni kuzihuisha ili kupatiwa za miaka 99.

Lukuvi ametoa kauli hiyo jana mkoani Mara wakati akizindua ofisi ya ardhi mkoa wa Mara ambayo ni ofisi ya kumi na mbili kuzinduliwa ikiwa ni mfululizo wa kuzindua ofisi za ardhi kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Alisema, kuna baadhi ya wamiliki wa ardhi kwenye mikoa mbalimbali ambao viwanja vyao vimepimwa na michoro kuidhinishwa lakini hati zao ni za miaka 33 na wamiliki hao watakapoenda kuzichukua wanatakiwa kuziangalia ili zibadilishwe na  kupatiwa hati za miaka 99.

‘’ Hati nyingi za wale wamiliki ambao hawajazichukua zimekwisha muda wake, muende kwenye ofisi za ardhi za mikoa, huko mtaelekezwa na Wasajili Wasaidzi wa ardhi katika ofisi hizo namna ya kuzibadilisha ili mpatiwe za miaka 99’’ alisema Lukuvi.

Kwa mujibu wa Lukuvi,  zaidi ya wamiliki wa ardhi 50,000 kwenye mkoa Mara hawajachukua hati za ardhi wengi muda wa hati zao unaishia miaka 33 na kutaka kufika ofisi za ardhi mkoa wa Mara kurekebishiwa na kupatiwa za miaka 99 ili iwe rahisi kupata mikopo mikubwa .

Akizungumzia uzinduzi ofisi ya ardhi mkoa wa Mara, Lukuvi alisema mkoa huo umekuwa na migogoro mingi ya ardhi na kubainisha kuwa uzinduzi wa ofisi hiyo utawawezesha wananchi wa Mara kumaliza migogoro kupitia ofisi hiyo badala ya kuipeleka migogoro kwake.

Waziri Lukuvi aliongeza kuwa, pamoja na Wizara yake hapo awali kushughulikia kero na migogoro ya ardhi lakini tatizo la kimfumo lilikuwa kubwa na kuweka wazi kuwa uzinduzi wa ofisi za mikoa unakomesha kero ambapo sasa hakutakiwa na gharama yoyote kwa mmiliki wa ardhi zaidi ya ile atakayolipia wakati wa kuomba hati.

‘’Mgogoro wa kimfumo ulikuwa mkubwa zaidi na leo hii tumekomesha kero na hakuna gharama yoyote mmiliki wa ardhi ataingia kufuatilia hati zaidi ya ile aliyolipa wakati wa kuomba hati, serikali ya awamu ya tano imeondoa kero zote kwa wananchi kwenye utawala wa ardhi’’  alisema Lukuvi.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima alisema, ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko na kero nyingi na kati ya malalamiko kumi na mbili anayopokea kwa siku sita yanahusiana na ardhi na kusisitiza kuwa, mingi ya migogoro ya wananchi lazima nguvu hutumika jambo alilolieleza kuwa linaongeza gharama za kiafya katika masuala ya matibabu  na kubainisha kuwa uwepo ofisi ya ardhi katika mkoa huo utarahisisha huduma katika sekta ya ardhi..

‘’ Kila malalamiko kumi na mbili ninayopata ofisini kwangu sita ni ya ardhi na mengi yana sura ya kijamii na hapa kuna neno la msamiati ukisikia vyesi ujue ni kesi’’ alisema Malima.

Mmoja wa wakazi wa Musoma aliyepatiwa hati katika uzinduzi ofisi ya ardhi Bi. Mara Sophia Lugera alifurahishwa na usogezwaji huduma za ardhi mkoani Mara na kubainisha kuwa aliifuatilia kwa muda mrefu hati yake iliyokuwa ofisi ya Kanda Mwanza na kusema, baada ya kuipata hati ataitumia kuchukulia mkopo benki ili aendeleze biashara yake ya ujasiriamali.

Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alitembelea na kukagua ujenzi wa mradi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mara inayojulikana kama Mawalimu Nyerere Memorial Hospital iliyopo eneo la Kwangwa Musoma mkoa wa Mara.

Akiwa katika mradi huo, Lukuvi aliagiza kukamilika kwa jengo ya Huduma ya Mama na Mtoto kufikia mwisho wa mwezi huu ili lianze kutumika kwa wananchi wa mkoa huo na Mikoa jirani.

Alisema, ujenzi wa jengo hilo umechukua muda mrefu na anataka kuona sehemu ya jengo hilo inakamilika kufikia julai 31 mwaka huu na Agosti mosi 2020  atamuagiza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kwenda kuona kama agizo lake limetekelezwa kama alivyoahidiwa.

Mhandisi na Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Hosiptarli ya Rufaa mkoa wa Mara Renald Kazyoba alisema, kimsingi sehemu ya ujenzi wa mradi huo sehemu ya Huduma ya Mama na Mtoto (Wing C) itakamilika kama alivyoagizwa kwa kuwa kazi kubwa imefanyika.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger