Thursday 28 May 2020

Logistics Officer at Kibogate Company Limited

Position: LOGISTICS OFFICER (1 POSITION) EQUPOINT PROPERTIES LTD Job Summary Kibogate Tanzania Ltd is a main distributor of both road and building materials including granite aggregates, washed sand, Pit Sand, crushed stone , building blocks , iron steel, Pavel’s and others, The company is located in Dar es Salaam and now looking forward to extend its other branches in Coastal… Read More »

The post Logistics Officer at Kibogate Company Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job at Tanga Cement PLC, Dispatch Clerk II

Dispatch Clerk II Employment Opportunity Position: Dispatch Clerk II Reporting to: Weighbridge Supervisor Location: Tanga Key responsibilities: Responsible for Weighbridge administration ensuring compliance with procedures Principle Accountabilities: Accurate weighing and recording of truck weights Preparation of daily and monthly weighbridge reports Plan, coordinate and control plant operations Customer Care Ultimate responsible for safe working practices especially areas of… Read More »

The post Job at Tanga Cement PLC, Dispatch Clerk II appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mwanamke Aua Mwanae Na Kisha Kumzika Baada Ya Kutelekezwa Na Mwanaume Aliyempa Mimba

Na salvatory Ntandu
Mkazi wa kijiji cha Seke Ididi wilayani Kishapu mkoani shinyanga Lucia Lukenya (42) kwa tuhuma ya kumuua na kisha kumzika mwanae mwenye jinsia ya kiume mwenye umri wa siku mbili.

Akizungumza na Waandishi wa habari Leo Mei 28 mwaka huu Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Aprili 19 Mwaka huu katika kitongoji cha Wizunza wilayani humo baada ya kujifungua.

Alisema kuwa Lucia alikamatwa na jeshi la polisi Mei 26 mwaka huu majira ya saa 12 baada ya wananchi wa kitongoji hicho kubaini hana mtoto aliyejifungua salama ndipo walipoamua kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi.

"Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa Mtuhumiwa alijifungua mtoto huyo tarehe 17/4/2020 na kisha kumuua Tarehe 19/4/2020 na kuamua kumzika peke yake katika eneo la shule ya msingi Ididi majira ya saa 12 jioni wakati mvua ikiendelea kunyesha ili watu wasimuone,"alisema Magiligimba.

Kamanda Magiligimba alifafanua kuwa Mabaki ya mwili wa marehemu yalipatikana tarehe 26 mwaka huu katika kaburi alilozikwa na Mtuhumiwa huyo na kukabidhiwa kwa ndugu zake kwaajili ya taratibu za mazishi.

Ameongeza kuwa chanzo cha mauaji hayo ni ugumu wa maisha baada ya kutelekezwa na mwanaume aliyempa mimba na kutoa wito kwa wananchi mkoani humo hususani wanawake kuacha kukatisha uhai wa watoto kwa visingizio vya   kutelekezwa na badala yake wafike katika madawati ya jinsia yanayopatikana katika vituo vya polisi ili kupata ufumbuzi.

Amesema baada ya kukamilika kwa upelelezi mshitakiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Mwisho.


Share:

Mwongozo Wa Udhibiti Wa Maambukizi Ya Ugonjwa Wa Corona (Covid-19) Katika Shule, Vyuo Na Taasisi Za Elimu Nchini

Kufuatia Mlipuko wa Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19) uliripotiwa kwa mara ya kwanza hapa nchini tarehe 16 Machi, 2020, Serikali ilichukua hatua mbalimbali kwa ajili ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huu nchini. 


Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kufunga shule zote za Awali, Msingi, Sekondari, Vyuo na taasisi za elimu nchini. Kutokana na takwimu za mwenendo wa ugonjwa huu nchini kwa sasa kuonyesha kupungua kwa maambukizi ya Virusi vya Corona, mnamo tarehe 20 Mei 2020 Serikali kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ilitangaza uamuzi wa kurejesha ratiba za masomo kwa shule (Kidato cha 6), Vyuo na Taasisi za Elimu kuanzia tarehe 01 Juni 2020.  
 
Katika kuendeleza jitihada za kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vya Corona (COVID-19) nchini, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeandaa Mwongozo huu ambao unalenga kuweka mazingira wezeshi ya udhibiti wa maambukizi ya COVID-19 katika Taasisi za Elimu ikiwa ni pamoja na Vyuo, Shule za Sekondari na Shule za Msingi.  
 
Ili kufanikisha uwepo wa mazingira hayo, Mwongozo huu umezingatia maeneo makuu manne ambayo ni Maandalizi ya mazingira ya taasisi za elimu kabla ya kufunguliwa, Uchunguzi wa Afya, Usafiri wa kwenda na kurudi shuleni/Chuoni na Mazingira ya kujifunzia kama inavyoonekana hapo chini: - 

    i. Maandalizi ya Mazingira ya Taasisi za Elimu kabla ya kufunguliwa 
    a. Kutakasa (Decontamination) mazingira yote ya shule, Chuo au taasisi kwa kuzingatia miongozo ya utakasaji iliyotolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Hii inahusisha taasisi ambazo zilitumika kwa ajili ya kutunza washukiwa au wagonjwa wa Corona. Utakasajii huu ufanyike angalau masaa 72 kabla ya wanafunzi kuingia.  
 
    b. Siku ya kwanza ya kufunguliwa shule, chuo au taasisi ya Elimu ni muhimu itumike kutoa elimu kwa wanafunzi/wanachuo na wafanyakazi wote kuhusu ugonjwa wa COVID-19 pamoja na dalili zake na hatua za kuchukua ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu.  
 
    c. Kuhakikisha uwepo wa vifaa vya kunawia mikono (sabuni na maji tiririka) kwa ajili ya usafi wa mikono katika kila eneo au maeneo ya madarasa, ofisi, kila geti/lango kuu, mabweni, maktaba, bwalo la chakula, vyoo na maeneo mengine muhimu. Wizara inasisitiza matumizi ya sabuni na maji tiririka ndiyo iwe njia kuu ya usafi wa mikono. Vilevile vifaa vya kunawa mikono vizingatie mahitaji ya wanafunzi/wanavyuo wenye ulemavu. Aidha, Vitakasa Mikono (Hand sanitizer) vinaweza kutumika kama mbadala wa maji tiririka na sabuni.  
 
    d. Uongozi wa Shule/Chuo uhakikishe vitakasa mikono (hand sanitizer) vinavyotumika vina ubora unaotakiwa (iliyotengenezwa kwa ethanol yenye asilimia zaidi ya 70) kwa wanafunzi na wanavyuo. Matumizi ya vitakasa mikono ni suala la hiari kwa mwanafunzi/mwanachuo kwa sababu Wizara tunasisitiza zaidi matumizi ya maji tiririka na sabuni.  
 
    e. Spirit (Methanol) isitumike kama kitakasa mikono katika maeneo yote ya shule, Chuo na taasisi. Wanafunzi wasiagizwe kwenda na spirit shuleni na Chuoni. Uongozi wa Shule/Chuo uhakikishe wanafunzi hawaingii na spirit katika maeneo/Taasisi zao.  
 
    f. Shule, Chuo au taasisi yenye vituo vya kutolea huduma za afya, watumishi wote wanaohusika wapewe elimu juu ya kuwahudumiwa wanafunzi, walimu na wafanyakazi wote watakaoshukiwa kuwa na COVID-19 ikiwemo kuwapatia msaada wa kisaikolojia na kuondoa unyanyapaa. Aidha, Shule/Chuo/Taasisi hizi zinapaswa kuwa na dawa na vifaa kwa ajili ya dharura.  
 
    g. Uongozi wa Shule, Chuo na taasisi za Elimu zinazotoa huduma za kulaza wanafunzi (bweni) uhakikishe kadri inavyowezekana kunakuwepo na nafasi ya kutosha kati ya kitanda kimoja hadi kingine na kudhibiti uchangiaji vifaa kwa wanafunzi kama vile taulo, mashuka, vyombo vya kuogea na vifaa vya usafi wa mwili.  
 
    h. Uongozi wa Shule, Chuo na taasisi za elimu zihamasishe wanafunzi, walimu na wafanyakazi wao kuvaa barakoa za vitambaa (Cloth masks) wakati wanaporudi shuleni au vyuoni. Aidha, wazazi/walezi wahimizwe kuwapatia watoto wao barakoa za vitambaa kabla ya kwenda shuleni/Vyuoni.  
 
    i. Uongozi wa Shule, Chuo na Taasisi za elimu ziweke utaratibu mzuri wa upatikanaji wa barakoa za vitambaa  (Cloth Masks) zinazotengenezwa nchini na ambazo vinaweza kufuliwa na kupigwa pasi kila siku katika maeneo yao kwa gharama nafuu. Barakoa za vitambaa vya pamba zenye safu mbili (two layers) ndizo zinazoshauriwa kuvaliwa kwa kuwa ni bora na salama kiafya.Wazazi wanaweza kuwapa au kuwanunulia watoto wao.  
 
    j. Uongozi wa Shule, Chuo na Taasisi ya Elimu unapaswa kuhakikisha uwepo wa vifaa vya kuhifadhia taka zitokanazo na barakoa zilizotumika na kuziteketeza kama taka nyingine hatarishi ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona. 

ii. Uchunguzi wa Afya;
 a. Wanafunzi watakaohisiwa kuwa na dalili za COVID-19 wafanyiwe vipimo kabla ya kurudi shuleni/chuoni. 
 b. Wanafunzi watakaobainika kuwa na maambukizi wabaki nyumbani hadi hapo hali zao za afya zitakapoimarika. 
 c. Kwa wanafunzi ambao watabainika kuwa na dalili za ugonjwa wa Corona wakiwa Shuleni/chuoni, Uongozi wa Shule au chuo utoe taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho karibu nao kwa ajili ya uchunguzi na matibabu zaidi.


    iii. Usafiri wa kwenda na kurudi shuleni/chuoni: 
a. Wamiliki wa magari ya Shule/Chuo (School bus) waweke vitakasa mikono kwenye magari yao kwa ajili ya wanafunzi wakati wa kupanda kuelekea shuleni/Chuoni, 
b. Wamiliki wa magari ya Shule/Chuo (School bus) wahakikishe kuwa abiria na wahudumu wote wanavaa barakoa za vitambaa na kutumia vitakasa mikono kabla ya kupanda gari husika.
   
    iv. Mazingira ya kujifunzia:  
a. Uongozi wa Shule au Chuo unapaswa kuhimiza wanafunzi/wanachuo, walimu na watumishi wao kuzingatia Kanuni za Usafi binafsi ikiwemo kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni kabla ya kuingia getini/lango kuu, darasani, bwenini, maktaba, bwalo la chakula, ofisini na maeneo mengine muhimu. Wizara inasisitiza matumizi ya sabuni na maji tiririka ndiyo iwe njia kuu ya usafi wa mikono. Aidha, Vitakasa Mikono (Hand sanitizer) vinaweza kutumika kama mbadala wa maji tiririka na sabuni. Inaelekezwa walimu wa madarasa wakisaidiana na viongozi wa wanafunzi/viranja wahakikishe haya yanasimamiwa ipasavyo.  
 
 b. Uongozi wa Shule au Chuo unapaswa kuhakikisha, kadri inavyowezekana, watumishi wote na wanafunzi/wanachuo wanakaa/kusimama kwa umbali utakaokuwa ni salama kati ya mtu mmoja na mwingine wawapo sehemu yoyote wakati wa mafunzo. 
 
    c. Uongozi wa Shule, Chuo na taasisi za elimu zihakikishe wanafunzi, walimu na wafanyakazi wao wanavaa barakoa za vitambaa (Cloth masks) wakati wote wawapo shuleni na vyuoni hususani wanapokuwa katika mikusanyiko ikiwa ni pamoja na darasani au katika vikundi vya majadiliano. Watoto wenye umri chini ya miaka mitano, wanafunzi/walimu/watumishi wenye magonjwa ya moyo, selimundu (sickle cell) na wenye magonjwa ya mfumo wa hewa kama vile pumu hawapaswi kuvaa barakoa.  
 
    d. Kwa shule na vyuo vyenye wanafunzi wenye mahitaji maalumu, walimu wanapaswa kuvaa barakoa maalum zitakazoruhusu mwanafunzi mwenye matatizo ya usikivu kuwasiliana na mwalimu.  
 
    e. Wataalam wa Afya wa Mkoa na Halmashauri husika washirikiane na Uongozi wa Shule au Chuo kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya barakoa, hatua sahihi za unawaji mikono kwa maji tiririka na sabuni na utumiaji sahihi wa vitakasa mikono kwa wanafunzi, walimu na wafanyakazi wa Shule/Chuo husika.  
 
    f. Pale ambapo Shule, Chuo au Taasisi ina watumishi wenye taaluma ya afya, inashauriwa watumishi hawa watumike ipasavyo kutoa elimu ya COVID-19 na kusimamia Utekekelezaji wa Mwongozo huu kwa kushirikiana na Watalaam wa afya wa Mkoa na Halmashauri zao. 
 
    g. Ziara za mafunzo nje ya shule zifanyike kwa kuzingatia tahadhari zote za kujikinga na maambukizi  ya COVID-19. 
 
    h. Uongozi wa Shule, Chuo au Taasisi ya Elimu zinahimizwa kuzingatia Matumizi ya TEHAMA katika kufundisha na kujifunzia ili kupunguza uwezekano wa maambukizi ya COVID-19. 
 
    i. Wataalamu wa Afya wa Mikoa na Halmashauri zote nchini wafanye ukaguzi wa mara kwa mara katika shule, vyuo na taasisi za elimu zilizoko katika maeneo yao ili kuhakikisha tahadhari zote za kujikinga na maambukizi ya COVID-19 zinazingatiwa kabla ya kufunguliwa Shule/Chuo na wakati wa masomo ikiwemo kutoa taarifa kwenye mamlaka husika. 
   
Mwongozo huu utaboreshwa mara kwa mara ili kukidhi mahitaji ya wakati husika. 


Ummy A. Mwalimu (Mb) 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, 
Jinsia, Wazee na Watoto 
27 Mei, 2020


Share:

Halima Mdee Akutwa Na Kesi Ya Kujibu Katika Kesi Ya Kutoa Maneno ya Kuudhi Dhidi ya Rais

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemkuta na kesi ya kujibu, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee,  katika kesi ya uchochezi ya kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya Rais John Magufuli. 

Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 28 Mei, 2020 na Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba.

Inadaiwa Julai 3, 2017 katika ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA zilizopo mtaa wa Ufipa Wilayani Kinondoni, Mdee alitamka maneno  ya kuudhi dhidi ya Rais Magufuli


Share:

Maandamano dhidi ya kifo cha Mmarekani mweusi Aliyeuawa Kikatili na Polisi Yaendelea Marekani

Waandamanaji mjini Minneapolis nchini Marekani wamepambana na polisi wa kutuliza ghasia kwa usiku wa pili mfululizo kufuatia hasira ya umma inayotokana na kifo cha kikatili cha mmarekani mweusi aliyekuwa chini ya mikono ya polisi. 

Hasira ya umma inatokana na video iliyorekodiwa na mpita njia siku ya Jumatatu ikionesha polisi mzungu akitumia goti kumkandamiza shingoni mwanaume mmoja mweusi aliyefungwa pingu huku akiomba msaada kutokana na kukosa pumzi. 

Siku ya pili ya maandamano iliyoambatana na visa vya wizi na uharibifu wa mali ilianza saa chache tangu meya wa mji huo alipotoa wito kwa waendesha mashtaka kufungua kesi ya jinai dhidi ya polisi huyo aliyesababisha kifo cha George Floyd. 

Mauaji ya kiholela ya Wamarekani wenye asili ya Afrika ambayo yanatekelezwa na polisi wazungu nchini Marekani yameongezeka sana katika miaka ya hivi karibuni nchini humo.


Share:

Bashe: Serikali Yaokoa Tani 556.5 Ya Mbegu Za Nafaka Kwa Kudhibiti Kwelea Kwelea

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.Hussein Bashe amepokea ndege ya kunyunyizia  dawa aina ya beaver 5Y DLD kwaajili ya kudhibiti visumbufu vya mimea aina ya kweleakwelea ambao wana uwezo wa kuharibu gramu 10 za nafaka kwa ndege mmoja kila siku.

“Kwa kawaida mikoa 12 ya Tanzania bara hupatwa na milipuko ya kwelea kwelea kila mwaka kutokana na tabia ya kwelea kwelea kuwa na uwezo wa kuharibu gramu 10 za nafaka kwa ndege mmoja kila siku.,kundi dogo lenye idadi ya wastani wa ndege milioni moja lina uwezo wa kuharibu tani 10 kwa siku.” Alisema Bashe

Mhe.Bashe ameendelea kusema kwamba uvamizi wa kwelea kwelea katika mashamba husababisha wastani wa uharibifu wa asilimia 30 kwa mazao yetu kila mwaka, na pia visumbufu vya mimea hususan vya milipuko ni tishio kubwa la usalama wa chakula hapa nchini.

Hata hivyo Tanzania husumbuliwa kila mwaka na aina nne ya visumbufu , ambavyo ni ndege aina ya kwelea kwelea, Viwavijeshi,Nzige na Panya. Visumbufu hivi vina tabia ya kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine vikifuata chakula.Ili kuweza kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na kudhibiti visumbufu hivyo  Mhe. Bashe amesema Wizara inatarajia kuanzisha Kitengo cha Kilimo anga ambacho kitafanya kazi hii.

Aidha, katika msimu 2019/2020  jumla ya ndege milioni 55.65 wameuwawa na kuweza kuokoa tani   556.5 za mbegu za nafaka kwa siku. Pia kwa ajili ya udhibiti wizara imetumia jumla ya lita 1,905 za kiuatilifu (FenthionULV 60%) na lita 5,716 za mafuta JET A-1.

 Kwa musimu wa 2019/2020 ndege hawa wamedhibitiwa katika Mikoa ya Mwanza; (wilaya ya Sengerema), Mkoa wa Shinyanga; (wilaya ya Kishapu na Shinyanga DC), Tabora; (wilaya ya Igunga, Uyui na Nzega), Mkoa wa Geita;  (wilaya ya Geita DC na Chato).

Mkoa wa Dodoma; (wilaya ya Dodoma jiji,  Bahi na Kondoa), Mkoa wa Singida; (wilaya ya Singida DC, Manyoni na Ikungi).

 Mkoa wa Iringa; (wilaya ya Iringa DC) na Mkoa wa Mbeya (wilaya ya Mbarali) na   Mkoa wa Manyara (wilaya ya Hanang).

 Bashe amemalizia kwa kusema kwamba Udhibiti umefanywa na Wizara Kilimo kwa kushirikiana na shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nzige wa Jangwani (Desert Locust Control Organization for East Africa) kutoka Nairobi Kenya kwa kutumia ndege ya kunyunyizia aina ya beaver 5Y DLD ambapo ilianza kufanya kazi Dodoma na inaelekea Mvomero Morogoro kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.


Share:

MAMA ALIYEPEWA MIMBA NA KUTELEKEZWA MBARONI KWA KUMUUA NA KUMZIKA MTOTO WAKE MVUA IKINYESHA KISHAPU

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Lucia Lukenya Mahizi (42) mkazi wa Kitongoji cha Wizunza kijiji cha Seke Ididi kata ya Sekebugoro wilayani Kishapu mkoani Shinyanga anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua kisha kumzika mtoto wake mwenye umri wa siku mbili kwa madai kuwa ni ugumu wa maisha baada ya kutelekezwa na aliyempa mimba.

Akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari leo Alhamis Mei 28,2020 Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema mtuhumiwa amekamatwa Mei 26,2020 baada ya wananchi kubaini kuwa mwanamke huyo hana mtoto aliyejifungua. 

“Tunamshikilia Lucia Lukenya Mahizi (42) mkazi wa kitongoji cha Wizunza kijiji cha Seke Ididi kwa kosa la mauaji ya mtoto wake mchanga, jinsia ya kiume anayekadiriwa kuwa na umri wa siku 02 baada ya kuzaliwa kwake kisha kumzika mwenyewe pekee yake wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha ili watu wasimuone”,amesema Kamanda Magiligimba. 

Akisimulia kuhusu tukio hilo Kamanda Magiligimba amesema tarehe 26.05.2020 majira ya saa kumi na mbili jioni (12:00) katika maeneo ya kitongoji cha Wizunza kijiji cha Seke Ididi wananchi wa maeneo hayo walibaini kuwa mtuhumiwa Lucia Lukenya Mahizi hana mtoto aliyejifungua tarehe 17/04/2020. 

“Baada ya wananchi kubaini kuwa Lucia hana mtoto ndipo wananchi hao waliamua kutoa taarifa kwa jeshi la polisi na mtuhumiwa huyo alikamatwa siku hiyo ya tarehe 26/05/2020”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

Kamanda Magiligimba amesema chanzo cha mauaji hayo ni ugumu wa maisha baada ya kutelekezwa na aliyempa mimba. 

Kamanda huyo wa polisi amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa mtuhumiwa alijifungua mtoto huyo tarehe 17/04/2020 na kumuua tarehe 19/04/2020 na kumzika mwenyewe pekee yake huko maeneo ya shule ya msingi ididi majira ya saa kumi na mbili na kasoro robo (11:45) jioni wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha ili watu wasimuone. 

“Mabaki ya mwili wa marehemu yalipatikana tarehe 26/05/2020 majira saa tisa alasiri katika kaburi alilozikwa na mtuhumiwa huyo na kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi”,ameongeza Kamanda Magiligimba. 

Kamanda Magiligimba anatoa wito kwa wananchi hususani wanawake kuacha kukatisha uhai wa watoto kwa sababu tu ya kutelekezwa na wenza wao bali wafike katika madawati jinsia na watoto yaliyopo vituo vya polisi na ofisi za ustawi wa jamii ili kupata ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili.
Share:

Trump atishia kufunga mitandao ya kijamii nchini Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump anatarajia leo Alhamisi kutia saini kwenye agizo linalolenga mitandao ya kijamii, maafisa wa Ikulu ya White House wamesema, saa chahe baada ya rais huyo kutishia  kufunga makampuni ya mitandao yote ya kijamii, akiyatuhumu kujaribu kuzuia uhuru wa kujieleza.

Wawakilishi hao hawakutoa maelezo zaidi kuhusu yaliyomo kwenye agizo hilo la rais Trump. Haijulikani kwa wakati huu jinsi Donald Trump atakavyopitisha  tishio lake la kufunga kampuni binafsi, ikiwa ni pamoja na Mtandao wa Twitter.

Mzozo huo uliibuka Jumanne wakati Mtandao wa Twitter ulihakiki ukweli wa baadhi ya ujumbe wa Rais wa Marekani Donald Trump alioundika katika ukurasa wake. Ni mara ya kwanza mtandao huo ambao Trump anapendelea zaidi kuutumia unafanya hivyo.

Rais wa Marekani alighadhibishwa na jambo hilo na kushumu mtandao huo kwa kile alichokiita ‘kuingilia kati' uchaguzi wa urais wa mwezi Novemba pamoja na uhuru wa kujieleza.

Twitter ilichukua hatua hiyo ambayo haraka ilichochea mvutano kati yake na Trump, baada ya rais huyo wa Marekani kuandika Tweet mbili akidai kwamba mtindo wa kupiga kura kwa njia ya posta huwa una udanganyifu mwingi.

Ilichofanya Twitter ni kuweka kiungo kingine chini ya ujumbe wa Trump kinachosema "Pata taarifa za ukweli juu ya kura ya njia ya posta,” na baadae kiungo hicho kinampeleka mtumiaji kwenye makala ya habari inayompa taarifa za ukweli kuhusu suala hilo, na orodha ya maelezo yanayopinga madai ya Trump.

Trump mwenye wafuasi wapatao milioni 80 katika ukurasa wake wa Twitter, anasema anautumia mtandao huo wa kijamii kupinga kile anachodai kuwa ni taarifa za upendeleo zinazotolewa na vyombo vya habari.

Trump amekuwa akidai kwamba mtindo wa kupiga kura kwa njia ya posta, una viwango vya juu vya udanganyifu katika wakati ambapo majimbo mengi yanazingatia kuitumia njia hiyo ili kulinda afya ya raia dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Covid-19 wakati taifa hilo likiwa linaelekea katika uchaguzi wa rais wa mwezi Novemba.

Credit:RFI


Share:

WAGONJWA WA CORONA UGANDA WAFIKA 281 BAADA YA WENGINE 28 KUONGEZEKA


Wizara ya Afya nchini humo imetangaza ongezeko la Wagonjwa wengine 28 na kufanya jumla ya visa vya Corona nchini humo kufikia 281.

Wagonjwa 21 ni madereva wa malori walioingia Uganda kupitia mpaka wa Elegu wakitokea Sudan Kusini huku 7 ni waliokuwa Karantini baada ya kukutana na madereva waliotangazwa awali.

Kati ya madereva 21, 7 ni raia wa kigeni kutoka Tanzania (4), Congo (1), Burundi (1) na Eritrea (1). Wote wamekabidhiwa kwa nchi zao.

Aidha, Wizara hiyo pia imetangaza jumla ya Wagonjwa waliopona kuwa 69. Jumla ya sampuli zilizopimwa jana na kuleta matokeo hayo ni 2,004.


Share:

VIFO VYA CORONA MAREKANI VYAPINDUKIA 102,107


 Idadi ya wagonjwa waliofariki kutokana na virusi vya corona nchini Marekani imefika  102,107 katika kipindi cha chini ya miezi minne.

Taifa hilo limeandikisha vifo vingi zaidi ya taifa lolote lile huku watu 1,745,803  wakithibitishwa kuambukizwa virusi hivyo idadi ambayo ni asilimia 30 ya maambukizi yote duniani.

Maambukizi ya kwanza nchini Marekani yaliripotiwa mjini Washington tarehe 21 mwezi Januari.

Kufikia sasa idadi ya waliofariki nchini Marekani imefikia 102,107, kulingana na Chuo kikuu cha John Hopkins mjini Maryland ,ambacho kimekuwa kikifuatilia mlipuko huo. Waliopona 490,130


Share:

NEC yakutana vyama vya siasa kujadili na kupitisha kanuni na maadili kwa uchaguzi Mkuu 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imejizatiti na imejipanga kuhakikisha kuwa inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, Sheria, Kanuni pamoja na kuzingatia masharti ya Kanuni za Maadili ya Uchaguzi.

Hayo yamesemwa jana  Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Mhe.Jaji Semistocles Kaijage katika kikao na vyama vua Siasa na Wadau wengine wa Uchaguzi kujadili na kupitisha Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2020.

Akizungumza katika kikao hicho Jaji Kaijage alisema kuwa NEC kwa kushirikiana na vyama vya Siasa na Serikali huandaa Maadili ya Uchaguzi kwa shabaha ya kuwa na Uchaguzi ulio huru, wa haki, wa wazi na wa kuaminika.

“Maadili yatasaidia kuwa na uwanja sawa wa ushindani katika Uchaguzi.Maadili hayo huandaliwa kwa mujibu wa kifungu Cha 124A Cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 ya sheria za Tanzania kwa kuzingatia mahitaji yaliyopo”. Alisema Jaji Kaijage.

Jaji amesema kuwa ni muda mwafaka tena kwa vyama vya siasa, Tume na Serikali kama wadau wa Uchaguzi kuandaa Maadili hayo kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

“Natambua kuwa vyama na Serikali mlipewa Rasimu ya Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020 ambapo mlipata fursa ya kupitia na kutoa maoni na mapendekezo yenu ambayo yamezingatiwa katika Rasimu hii ya Maadili”. Alisema Jaji Kaijage.

Pamoja na hayo Mhe.Kaijage aliwaaomba Wadau mbalimbali wa Uchaguzi baada ya majadiliano hayo na kuridhiwa kwa Maadili,wahusika wataweka saini ya kuyakubali, kuyaheshimu na kuyatekeleza kuanzia wakati was kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu na chaguzi ndogo zitakazofuata.


Share:

Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) Chasema Corona Imepungua Sana Nchini, Champongeza Rais Magufuli

Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) kimesema kinafanya uchambuzi ili kubaini tiba mbadala ambazo zimetumika kwenye kukabiliana na virusi vya corona zina mchango gani katika kupungua kwa maradhi hayo Tanzania.

Rais wa chama hicho, Dk. Elisha Osati, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati MAT ikitoa tathmini ya kitaaluma kuhusu mwenendo wa corona.

Dk. Osati alisema tathmini waliyoifanya kuhusu mwenendo wa corona, wamebaini idadi ya wagonjwa imepungua kwa kiasi kikubwa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma wakiwamo wanaohitaji kuwekewa oksijeni.

“Tunafanya uchambuzi ambao tutautoa unaolenga kujua kitu gani kimechangia na kwa namna gani kimepunguza corona Tanzania.

“Hatuwezi kudharau njia mbadala kwa sababu Watanzania wengi wanatumia miti shamba, wengi walikuwa wanatumia limao, tangawizi ambavyo vina vitamin C kwa wingi inayosaidia kujenga kinga ya mwili ili kupambana na wadudu mbalimbali wakiwamo corona.”

Alisema inawezekana tiba mbadala imekuwa na nafasi yake, hivyo uchambuzi kuhusu hilo utakuja.

“Watanzania tumewaelekeza vitu vingi vya kufanya watu wananawa mikono, wiki tatu mfululizo watu wamevaa barakoa, tunaamini hiyo imesaidia kupunguza tatizo pia. Kila kimoja tutakifanyia uchambuzi ikiwa ni pamoja matumizi ya tangawizi na limao,” alisema.

Akizungumza ugonjwa huo, Dk. Osati alisema Aprili sampuli zilizokuwa zikipelekwa maabara takribani 90 zilikuwa na corona wakati kwa sasa ni chini ya asilimia 10.

“Idadi ndani ya jamii zimepungua, kwa kuangalia idadi ya simu zinazopigwa kwa kuuliza au kuomba msaada wa kitaalamu kuhusu wagonjwa wenye dalili za ugonjwa huu. Pia idadi ya vifo imepungua,” alisema.

Alisema MAT kimempongeza Rais John Magufuli, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu kwa kuwaongoza Watanzania katika kipindi hicho kigumu.

“Tunawapongeza madaktari na watumishi wa sekta ya afya kwa kuwa askari wa mbele kupambana na corona.

“Tunawaomba wagonjwa walioko nyumbani kwa matatizo ya corona au magonjwa mengine waje hospitali tuwahudumie, kwani corona imepungua kwa kiasi kikubwa. Madaktari tupo tayari kuwahudumia.”

Chama hicho kimewaeleza Watanzania kuwa ugonjwa huo bado upo, hivyo waendelee kuchukua tahadhari hasa wakati huu wa wanafunzi wanaporudi vyuoni.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 28,2020





















Share:

Wednesday 27 May 2020

Rais Magufuli Aongoza Kikao Cha Baraza La Mawaziri Ikulu Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Mawaziri Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri pamoja na Manaibu Mawaziri tarehe 27 Mei 2020.

Awali kabla ya kikao hicho Mhesimiwa Rais aliwaongoza wajumbe kusimama kwa dakika moja ili kumkumbuka na kumuombea aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Marehemu Balozi Dkt. Augustine Mahiga kabla ya kuanza kwa Kikao hicho.


Share:

SADC Wapendekeza Kuondolewa Kwa Vikwazo Vya Kibiashara Mipakani

Eric Msuya – MAELEZO
Katibu Mkuu Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kanali Wilbert Ibuge amewataka watanzania kuendelea kudumisha umoja na Ushirikiano wa Kibiashara katika ukanda wa Jumuiya ya maendeleo Kusini mwa Afrika SADC.
 
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kufungua Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC kwa ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika kwa njia ya Mtandao (video conference) leo jijini Dar es Salaam, amesema Mkutano huo ni mahususi kwa kujadili na kuondoa vikwazo vyote vya Kibiashara ili kuweza kuendeleza Uchumi ndani ya Jumuiya.
 
“Kikao cha makatibu wakuu cha leo, kimekubaliana kuondoa kikwazo cha bidhaa mahususi tu kupita katika mipaka yetu badala yake bidhaa zote zinazowezesha wananchi wetu kuendelea na maisha ni lazima ziruhusiwe kupita katika mipaka ya nchi wanachama wa SADC” Amesema Balozi Ibuge
 
Aidha, Katibu Mkuu ameongeza kuwa ni muhimu wa wanaSADC kujumuika katika wakati huu na kuona ni jinsi gani wanaweza kushirkikiana na kuhakikisha kuwa Uchumi wa Nchi Wanachama wa SADC unakua na kuongeza juhudi za kibiashara kuendelea kufunguka.
 
“kwa mfano halisi sisi kama Tanzania hatukufunga mipaka yetu, na katika kutokufunga mipaka yetu bado tunatambua kwamba tunaendelea kuwategemea wenzetu kama wanavyotutegemea sisi, tuna bandari inayohudumia Nchi nane za SADC na zisizokuwa za SADC na ambazo ndizo hasa tunapozungumzia utengamano na mazingiara ya kufanya biashara na kuzingataia zile tahadhari mbalimbali ambazo nchi hizo zimekuwa zikichukua” amesema Balozi Ibuge
 
Mkutano huo wa siku tatu 27 hadi 29 Mei, 2019 unajadili Hali ya kifedha ndani ya Jumuiya, Utekelezaji wa Maazimio yaliyotokana na kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC ambayo ni Menejimenti ya Maafa, utekelezaji wa kaulimbiu ya Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC isemayo "Mazingira Wezeshi kwa ajili ya Maendeleo Endelevu na Jumuishi ya Viwanda, Kukuza Biashara na Ajira ndani ya SADC" na mapitio ya hali halisi ya biashara baina ya nchi, maendeleo ya viwanda ndani ya Jumuiya na taarifa ya utekelezaji wa Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda wa Jumuiya na Mpango kazi wake.
 
Pia, Mkutano huo unahusisha wataalamu kutoka nchi 12 wanachama wa SADC kutoka sekta za Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Fedha na Mipango, Uchukuzi na Mawasiliano, Viwanda na Biashara, Maliasili na Utalii pamoja na Afya. Mkutano huo pia utatoka na maazimio ambayo nchi wanachama watatakiwa kuyatekeleza ndani ya muda utakaokubaliwa.
 
Nchi zinazoshiriki Mkutano huo ni Angola, Afrika Kusini, Comoro, Eswatini, Mauritius, Msumbiji, Madagascar, Namibia, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Zimbabwe na Mwenyekiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
MWISHO.


Share:

Ufaransa Yaipatia Serikali Mkopo Nafuu Wa Euro Milioni 70 Kujenga Mradi Wa Maji Mjini Morogoro

Na Farida Ramadhani-WFM, Dodoma
Serikali ya Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) zimetiliana saini mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Euro milioni 70, sawa na takriban shilingi za Tanzania bilioni 175.6 kwa ajili ya kugharamia Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazigira Mjini Morogoro (MORUWASA).

Mkataba wa mkopo huo umesainiwa Jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James kwa upande wa Serikali na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa, Bi. Stephanie Mouen Essombe.

Bw. James alisema mkopo huo utawezesha wakazi wa Mjini Morogoro wapatao 722,010 kupata maji safi na salama kupitia upanuzi wa mfumo wa usambazaji wa Maji kutoka Bwawa la Mindu.

Alisema kukamilika kwa mradi huo kutawezesha upatikanaji wa Maji kutoka mita za ujazo 33,000 hadi kufikia mita za ujazo 108,000 kwa siku pamoja na kuwezesha Mji wa Morogoro kupata kiwango cha mahitaji ya maji safi kinachokadiriwa kuwa mita za ujazo 126,253 kwa siku, ifikapo mwaka 2035.

“Mradi pia utaongeza upatikanaji wa huduma za majitaka kutoka kiwango cha sasa cha asilimia 5 hadi asilimia 15 kwa wakazi wa mjini Morogoro”, alifafanua.

Bw. James alisema Tanzania imekuwa ikinufaika na ufadhili wa AFD hususan katika sekta za Nishati, Maji, Usafirishaji na Kilimo kupitia idadi ya miradi  mbalimbali inayoendelea na ile inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Alisema miradi 7 inayoendelea kutekelezwa katika sekta mbalimbali hapa nchini kupitia misaada na mikopo inayotolewa wa Shirika hilo inafikia takriban Euro milioni 154.5 sawa na shilingi bilioni 387.6.



“Miradi 6 yenye thamani ya Euro milioni 141.4 kupitia ufadhili wa AFD imekamilika na kuna miradi mingine 12 yenye thamani ya Euro milioni 1,021.7 ambayo tuko kwenye mazungumzo na AFD katika sekta ya Nishati, Maji, Kilimo Usafiri wa mwendokasi Jijini Dar es Salaam, miundombinu ya viwanja vya ndege na Usafi wa mazingira Jijini Dare salaam” alisema Bw. James.



Aliishukuru Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) kwa ufadhili huo muhimu, ambao utachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya nchi na kupunguza umaskini na kuahidi kuwa Serikali itafuatilia kwa karibu utekelezaji wa mradi huo ili kuhakikisha kwamba fedha zitakazotolewa zinatumika kama ilivyokusudiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD), Bi. Stephanie Mouen Essombe aliahidi kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania ili kuhakikisha inafikia malengo yake katika kuboresha maisha ya wananchi hasa katika upatikanaji wa maji.

“Ushirikiano wa Tanzania na Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) ulioanza miaka 20 iliyopita umezidi kuimarika ambapo katika kipindi cha miaka 10 iliyopita Shirika limewekeza kiasi cha Euro milioni 258 sawa na takriban Sh. bilioni za Tanzania 655” alisema Bi. Essombe.

Alisema mradi huo umelenga kupanua Bwawa la Mindu linalochangia upatikanaji wa maji yanayotumika katika Mji wa Morogoro kwa asilimia 70 pamoja na kuboresha mfumo wa huduma ya maji taka katika mji huo.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Prof. Kitila Mkumbo alisema kuwa mkopo huo utatatua changamoto ya maji ambayo ilikuwa kilio cha muda mrefu kwa wananchi wa Morogoro.

Alisema mkopo huu unafaida nyingi nchini ikiwemo kutoa ajira pamoja na kutoa fursa kwa viwanda vya ndani kwa sababu vifaa vitakavyotumika kutekeleza mradi huo wa kihistoria vitanunuliwa ndani ya nchi.

Alisema hivi sasa Serikali inatekeleza miradi ya maji 1,423, miradi 792 imekamilika na miradi 631 inaendelea na kwamba mradi huo wa maji wa Mji wa Morogoro utakuwa mkombozi mkubwa wa wananchi wa mji huo.

Alisema upatikanaji wa fedha hizo ambazo mjadala wa kupata mkopo umechukua zaidi ya miaka minne utawezesha kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji nchini ambapo hivi sasa kiwango cha upatikanaji wa maji vijijini kimefikia asilimia 85 ya lengo la asilimia 95 iliyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM huku katika miji kiwango kimefikia asilimia 70.1 kati ya lengo la asilimia 85 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2020

Mwisho.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger